Siku ya kwanza kufanya kazi ya Saidia Fundi

Siku ya kwanza kufanya kazi ya Saidia Fundi

BARDIZBAH

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2017
Posts
5,259
Reaction score
10,078
Nimeiiba sehemu.....
Kuna mwanangu baada ya kuchapwa na life, akaamua kujitosa kwenye kazi za saidia fundi.

Kazi ya kwanza aliyokutana nayo kwenye ghorofa moja hapo kariakoo ilikua ni kubeba zege. Kwa jinsi alivyofika tu kazini walivyotizama umbo lake mafundi wakamuambia “Dogo utaweza kweli?” 😂👇

Mwanetu akasema “nitaweza” si unajua shauku na hasira za kuisogelea pesa kivyovyote ile! Mafundi wakasema poa.

Kwa waliofika site za kkoo za maghorofa wanaelewa, fundi yupo ghorofa ya 7 anataka tofali za block zipo floor ya kwanza. Jala la kwanza ikawa kupandisha tofali juu.

Ile kazi mwanetu aliifanya kuanzia saa 2 mpaka mida ya saa sita hivi! Na humo ndani inapigwa mixer ya kubebeshwa makarai ya zege anakimbia nayo pia. Hii sikia tu kwa jirani. Maana kazi ambayo kirahisi ingefanywa na lift inafanywa na binadamu ili kupunguza gharama Za ujenzi 😂
Kufikia saa saba Mchana mwanangu alikua kashasanda kitambo.

Kila akisogeza mguu na karai la zege lipo kichwani anaona hatembei. Hatimae akadondoka na karai chini! Sasa sehemu Za site kunakuaga na wale jamaa wa OSHA (ambao wanasimamia usalama kazini)

Ikabidi mwanangu pale awekwe pembeni kwa sababu alikua kashachoka Ila kusema anashindwa.

Kikasikika kidari kimoja ambacho kilikua kinabeba tofali kikisema “Dogo kashasanda huyu na kwenye mgao hayumo”
Kwa uchungu mkubwa mwanangu alikiri kushindwa moyoni lakini hata hivyo la zaidi zaidi ni jinsi alivyoumizwa na kazi na mwisho wa siku anarudi kapa.

Alinawa miguu kwa huzuni kubwa mno ili asepe! Mara ghafla msimamizi wa vibarua aliyekuepo pembeni akiusoma mchezo wote akasema.

“Usijali Dogo mgao wako utapata” hii ilikua kama sauti kutoka peponi kwani hakuamini na hii ni stori ambayo hatakuja kuisahau maishani mwake.

Kupiga saidia fundi ujipange! Yote kwa yote vijana tusiache kupambana na kujaribu🤝
 
Mi mara yangu ya kwanza kusaidia fundi ilikua ni gereji bus imetoka Dodoma to Arusha imefika hata haijazimwa fundi akaniambia niingize mkono kwenye exhaust(bomba la moshi) ili tupime oil kama ni safi mi sikujua kama exhaust inakuaga ya moto vile baada ya kugusa nilihisi mwili mzima unawaka moto.

Nikaokota wheel spanner nikaweka record ya kuwa nyokaa wa kwanza kumtandika fundi wake na wheel spanner
 
We yako cha mtoto kuna jamaa humu ,alisimulia aliambiwa hii kazi mpaka maji utaita mmaa na kweli aliita mma.Picha linaanza aliambiwa kuna kushusha simenti mifuko 1500.Hapo bado Zege.Itafute.
Kazi hufundishwa polepole na kwa muda fulani.Tatizo la wenyeji wa hizo kazi wamuonapo mgeni wanawaza kumfelisha tu.Ni roho mbaya na kutawaliwa na utoto mwingi.
 
Mi mara yangu ya kwanza kusaidia fundi ilikua ni gereji bus imetoka Dodoma to Arusha imefika hata haijazimwa fundi akaniambia niingize mkono kwenye exhaust(bomba la moshi) ili tupime oil kama ni safi mi sikujua kama exhaust inakuaga ya moto vile
Sasa hapo aliamua kukufanyia roho mbaya tu.

Wengine tangu wazaliwe hawajawahi kuwa karibu na vyombo vya moto kuvihudumia.

Kukueleza ushike eksozi siyo uuaji huo?

Na changamoto nyingine ni kwamba anayefanyiwa mizaha na kuumizwa mara ya kwanza anabaki na roho ya kulipa kisasi kwa wageni watakaofuata.
 
hahaha dah unanikumbusha mbali mkuu enzi natafuta mtaji kwa kila namna, kuna fundi mmoja pale external alikuwa na tenda ya kujenga mzani wa malori nikajipinda kuomba kibarua cha saidia fundi pale dah. kesho yake naambiwaa kazi yangu nikachote lami iliochemka kwenye pipa kwa ndoo ya plastick na kuipeleka umbali wa mita kama 200 ivi😁. ila saidia fundi cha mtoto.

kwa bakharesa pale godown zake za kiwanda chake cha unga dah, viroba vya kilo 25 na 50. unabeba 12hrs nonstop.

yule ndio maana litimu lake la azam halifanikiwi.
 
hahaha dah unanikumbusha mbali mkuu enzi natafuta mtaji kwa kila namna, kuna fundi mmoja pale external alikuwa na tenda ya kujenga mzani wa malori nikajipinda kuomba kibarua cha saidia fundi pale da...
Wanasema huwezi kuwa tajiri kama huna roho mbaya.
 
Kuna hiyo enzi hizo nikakutana nayo ya kushusha semi ya mbao..ikabidi niingie mitini.
 
Back
Top Bottom