Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 21,967
- 32,074
Kaka Francis ahsante kwa kutukumbusha kuhusu Siku ya Vitabu.
Ilikuwa mwaka wa 1957 nina umri wa miaka 5 nimekwenda sokoni na mama yangu Bi. Mwanaidi bint Sheikh Mohamed Mvamila.
Mlango aliopita yeye ni ule wa madrasa na kwa hakika hakuwa anakwenda popote kwa kuwa baba yake ndiye alikuwa mwalimu wa hicho chuo hapo hapo nyumbani kwao.
Mama yangu hakuona mlango wa shule lakini alikuwa mpenzi wa elimu.
Siku moja tumeongozana sokoni hili soko ni soko la Mtaa wa Chini Moshi ndilo lilikuwa soko kubwa kwa miaka ile kabla halijajengwa soko kubwa zaidi Mtaa wa Juu.
Kulikuwa na muuza unga wa mhogo akichanganya na sembe ambao mama yangu akiupenda.
Jirani na muuza unga alikuwapo muuza vitabu.
Mama yangu akaninunulia kitabu cha kujifunza kusoma na mwalimu wa kunishika alif kwa kijiti alikuwa yeye.
Hapo sijaanza hata shule.
Nakikumbuka kitabu kile.
Nasomeshwa, ‘’aeiou, babebibobu,’’ nk. hadi tunafika, ‘’baba kanasa...’’
Naamini wale wa umri wangu watakumbuka haya maneno katika kujifunza kusoma.
Kitabu changu cha kwanza kikubwa kukishika mkononi ingawa nilikuwa siwezi kukisoma sawasawa kilikuwa, ‘’Machimbo ya Mfalme Suleiman’’ cha H. Rider Haggard.
Kitabu hiki kilikuwa cha dada yangu yeye akisoma Girls School shule hii ilikuwa Mtaa wa Kitchwele na Msimbazi na hadi leo shule hii ipo hapo Mtaa wa Uhuru na Msimbazi.
Picha ndani ya kitabu kile zilikamata sana fikra yangu.
Dada yangu alikuwa akija nyumbani na kila aina ya vitabu vingine vya Kiingereza na mimi nikawa nachukua naangalia picha najitahidi kusoma lakini wapi siambulii kitu.
Kitu kingine nikumuusudu dada yangu alikuwa akiimba nyimbo za Kizungu.
Nikawa naona raha kumsikiliza nikajua haya yote kwa kuwa anajua Kiingereza.
Nikawa napenda vitabu na ndiyo maana niliporudi Dar es Salaam likizo kutoka Moshi nilikokuwa nimeanza darasa la kwanza nasoma Lutheran Primary School dada yangu akanipa ‘’Mashimo ya Mfalme Suleiman.’’
Nilisoma Kinondoni Primary School mwaka wa 1963 nikitokea Moshi Majengo Middle School.
Kulikuwa na mwalimu wa Kiingereza Mr. Romenesco.
Huyu alikuja Tanganyika katika mradi wa Peace Corps.
Mr. Romenesco alivyoona bidii yangu katika somo lake akanifanya Mkutubi wa Darasa.
Vitabu vya kusoma mimi ndiyo mwangalizi wa kabati lake.
Hii ilinipa fursa ya kusoma kila kitabu kipya kilicholetwa Dar es Salaam
Tulikuwa na mwalimu wa Kiingereza kutoka Uingereza, Mrs. Grant akisomesha St. Joseph’s Convent.
Mumewe alikuwa Mwalimu Chang’ombe Teacher’s College na yeye kama mkewe akifundisha Kiingereza.
Hawa waliletwa na serikali ya Uingereza kuja kusomesha lugha yao.
Mrs. Grant pia alinipenda na nikawa vilevile Mkutubi wa Darasa.
Hapa ndipo nilipofaidi.
St. Joseph’s ilikuwa shule haina mfanowe kwa uzuri wake katika taalum, masomo na nidhamu.
Mrs. Grant alikuja na ‘’Labaratory,’’ hata sijui niieleze vipi lakini alikuwa anatufundisha kusoma kwa kasi na kuelewa.
Anasimamisha ‘’stop watch’’ yake tunafunga vitabu kisha anauliza maswali.
Nikimaliza na Mrs. Grant nakutana na Ms. Menez mwalimu wa Literature.
Hapa ni William Shakespeare, ‘’The Merchant of Venice,’’ na African Writers Series tunapambana na Chinua Achebe, ‘’Things Fall Apart,’’ na Wole Soyinka, ‘’The Trials of Brother Jero.’’
Ndugu yangu walimu hawa Allah atawalipa kwa hisani waliyonifanyia.
Wanapenda kusomesha na wanasikia raha kusomesha.
Unadhani kumsomesha mtoto wa Kariakoo Kiingereza hadi apate First Class Cambridge Examination ni jambo rahisi?
Ana ulimi mzito kama nanga hicho Kiingereza chenyewe anakiogopa kukisema mbele ya wajuzi wa lugha hiyo katika darasa ambalo kuna wanafunzi Wazungu na Magoa na Waafrika ambao walisoma ‘’special schools,’’ za wakati ule unadhani wewe wa Kinondoni Primary School utafua dafu hapo?
Mrs. Grant ndiye aliyenifanya nijiunge na Tanganyika Library wakati huo ipo Mtaa wa Mkwepu, baadae hii maktaba ikawa ofisi ya Takwimu baada ya kujengwa Maktaba ya Taifa, Titi Street.
Hii Maktaba ilisheheni vitabu.
Hapa ndipo nilipopata wazimu wa vitabu kabisa ambao kwa hakika ulihitaji mganga aniague.
Siku ya Jumatano ni ni nusu siku shule hadi saa saba mwisho.
Nyumbani kwetu ni Libya Street jumba la Posta ya Kisutu.
Nikishakula nabadili nguo nakuja Maktaba hapo Mkwepu.
Vitabu viliyokuwa navipenda ni vile vya ‘’adventure,’’ Spaniards wanakwenda Amerika ya Kusini ndani ya majahazi wanavuka Atlantic Ocean kutokea Spain.
Basi huwezi kuamini akili yangu inahama Dar es Salaam kwa muda naingia katika jahazi na mimi na kuwa baharia na nashiriki katika mikasa yote ambayo mabaharia hawa wanakumbananayo kuanzia dhoruba za baharini hadi kuingia katika visiwa na kufanya vita na wenyeji.
Spaniards wanaingia Aztec na mimi mmoja wa hao askari.
Nikiinua kichwa naangalia nje taa zinawaka Maghrib imeshaingia na mimi niko Dar es Salaam.
Naondoka na vitabu vya kuazima kwenda kusoma nyumbani.
Sent using Jamii Forums mobile app
Ilikuwa mwaka wa 1957 nina umri wa miaka 5 nimekwenda sokoni na mama yangu Bi. Mwanaidi bint Sheikh Mohamed Mvamila.
Mlango aliopita yeye ni ule wa madrasa na kwa hakika hakuwa anakwenda popote kwa kuwa baba yake ndiye alikuwa mwalimu wa hicho chuo hapo hapo nyumbani kwao.
Mama yangu hakuona mlango wa shule lakini alikuwa mpenzi wa elimu.
Siku moja tumeongozana sokoni hili soko ni soko la Mtaa wa Chini Moshi ndilo lilikuwa soko kubwa kwa miaka ile kabla halijajengwa soko kubwa zaidi Mtaa wa Juu.
Kulikuwa na muuza unga wa mhogo akichanganya na sembe ambao mama yangu akiupenda.
Jirani na muuza unga alikuwapo muuza vitabu.
Mama yangu akaninunulia kitabu cha kujifunza kusoma na mwalimu wa kunishika alif kwa kijiti alikuwa yeye.
Hapo sijaanza hata shule.
Nakikumbuka kitabu kile.
Nasomeshwa, ‘’aeiou, babebibobu,’’ nk. hadi tunafika, ‘’baba kanasa...’’
Naamini wale wa umri wangu watakumbuka haya maneno katika kujifunza kusoma.
Kitabu changu cha kwanza kikubwa kukishika mkononi ingawa nilikuwa siwezi kukisoma sawasawa kilikuwa, ‘’Machimbo ya Mfalme Suleiman’’ cha H. Rider Haggard.
Kitabu hiki kilikuwa cha dada yangu yeye akisoma Girls School shule hii ilikuwa Mtaa wa Kitchwele na Msimbazi na hadi leo shule hii ipo hapo Mtaa wa Uhuru na Msimbazi.
Picha ndani ya kitabu kile zilikamata sana fikra yangu.
Dada yangu alikuwa akija nyumbani na kila aina ya vitabu vingine vya Kiingereza na mimi nikawa nachukua naangalia picha najitahidi kusoma lakini wapi siambulii kitu.
Kitu kingine nikumuusudu dada yangu alikuwa akiimba nyimbo za Kizungu.
Nikawa naona raha kumsikiliza nikajua haya yote kwa kuwa anajua Kiingereza.
Nikawa napenda vitabu na ndiyo maana niliporudi Dar es Salaam likizo kutoka Moshi nilikokuwa nimeanza darasa la kwanza nasoma Lutheran Primary School dada yangu akanipa ‘’Mashimo ya Mfalme Suleiman.’’
Nilisoma Kinondoni Primary School mwaka wa 1963 nikitokea Moshi Majengo Middle School.
Kulikuwa na mwalimu wa Kiingereza Mr. Romenesco.
Huyu alikuja Tanganyika katika mradi wa Peace Corps.
Mr. Romenesco alivyoona bidii yangu katika somo lake akanifanya Mkutubi wa Darasa.
Vitabu vya kusoma mimi ndiyo mwangalizi wa kabati lake.
Hii ilinipa fursa ya kusoma kila kitabu kipya kilicholetwa Dar es Salaam
Tulikuwa na mwalimu wa Kiingereza kutoka Uingereza, Mrs. Grant akisomesha St. Joseph’s Convent.
Mumewe alikuwa Mwalimu Chang’ombe Teacher’s College na yeye kama mkewe akifundisha Kiingereza.
Hawa waliletwa na serikali ya Uingereza kuja kusomesha lugha yao.
Mrs. Grant pia alinipenda na nikawa vilevile Mkutubi wa Darasa.
Hapa ndipo nilipofaidi.
St. Joseph’s ilikuwa shule haina mfanowe kwa uzuri wake katika taalum, masomo na nidhamu.
Mrs. Grant alikuja na ‘’Labaratory,’’ hata sijui niieleze vipi lakini alikuwa anatufundisha kusoma kwa kasi na kuelewa.
Anasimamisha ‘’stop watch’’ yake tunafunga vitabu kisha anauliza maswali.
Nikimaliza na Mrs. Grant nakutana na Ms. Menez mwalimu wa Literature.
Hapa ni William Shakespeare, ‘’The Merchant of Venice,’’ na African Writers Series tunapambana na Chinua Achebe, ‘’Things Fall Apart,’’ na Wole Soyinka, ‘’The Trials of Brother Jero.’’
Ndugu yangu walimu hawa Allah atawalipa kwa hisani waliyonifanyia.
Wanapenda kusomesha na wanasikia raha kusomesha.
Unadhani kumsomesha mtoto wa Kariakoo Kiingereza hadi apate First Class Cambridge Examination ni jambo rahisi?
Ana ulimi mzito kama nanga hicho Kiingereza chenyewe anakiogopa kukisema mbele ya wajuzi wa lugha hiyo katika darasa ambalo kuna wanafunzi Wazungu na Magoa na Waafrika ambao walisoma ‘’special schools,’’ za wakati ule unadhani wewe wa Kinondoni Primary School utafua dafu hapo?
Mrs. Grant ndiye aliyenifanya nijiunge na Tanganyika Library wakati huo ipo Mtaa wa Mkwepu, baadae hii maktaba ikawa ofisi ya Takwimu baada ya kujengwa Maktaba ya Taifa, Titi Street.
Hii Maktaba ilisheheni vitabu.
Hapa ndipo nilipopata wazimu wa vitabu kabisa ambao kwa hakika ulihitaji mganga aniague.
Siku ya Jumatano ni ni nusu siku shule hadi saa saba mwisho.
Nyumbani kwetu ni Libya Street jumba la Posta ya Kisutu.
Nikishakula nabadili nguo nakuja Maktaba hapo Mkwepu.
Vitabu viliyokuwa navipenda ni vile vya ‘’adventure,’’ Spaniards wanakwenda Amerika ya Kusini ndani ya majahazi wanavuka Atlantic Ocean kutokea Spain.
Basi huwezi kuamini akili yangu inahama Dar es Salaam kwa muda naingia katika jahazi na mimi na kuwa baharia na nashiriki katika mikasa yote ambayo mabaharia hawa wanakumbananayo kuanzia dhoruba za baharini hadi kuingia katika visiwa na kufanya vita na wenyeji.
Spaniards wanaingia Aztec na mimi mmoja wa hao askari.
Nikiinua kichwa naangalia nje taa zinawaka Maghrib imeshaingia na mimi niko Dar es Salaam.
Naondoka na vitabu vya kuazima kwenda kusoma nyumbani.
Sent using Jamii Forums mobile app