TAI DUME
JF-Expert Member
- Feb 20, 2014
- 9,748
- 26,238
Wakuu nimezaliwa na kukulia mwambao wa ziwa nyasa.
Leo nimetafakari sana mstakabali wa profesheno niliyonayo, hakika haitasaidia taifa langu hata kidogo. Hapa ninawaza, kwa kuwa shuguli kuu ya wakazi wa mwambao wa ziwa nyasa ni uvuvi mdogo mdogo usio na tija,
Leo nimetafakari sana mstakabali wa profesheno niliyonayo, hakika haitasaidia taifa langu hata kidogo. Hapa ninawaza, kwa kuwa shuguli kuu ya wakazi wa mwambao wa ziwa nyasa ni uvuvi mdogo mdogo usio na tija,
- vipi kama serikali ingetuwekea shule au chuo cha uvuvi,
- ingetupa maarifa kuhusu uvuvi wenye manufaa,
- ingetuwekea mitaala mizuri ya jinsi ya ufugaji wa samaki ktk mabwawa ili kuendeleza uzalishaji,
- ingetujengea viwanda au kutufundisha utaalamu jinsi ya kusindika samaki kwa ajili ya soko la ndani na la nje,
- Ingetuwekea masharti nafuu katika kununua au kukodi vyombo bora vya uvuv. Naona kabisa leo hii watu wa mwambao tungekuwa exporters wakubwa wa samaki nje ya nchi na pia tungekuwa walipa kodi wazuri kwa serikali yetu. Anywei labda mwanangu atayakuta mazingira haya ambayo mimi niliyakosa. Rasilimali tunazo ila raia wanazidi kuwa masikini. Naipenda nchi yangu