Sikubaliani na shambulizi la kimaudhui dhidi ya Dejan

Shida tuliowengi tunafuataga mkumbo fulani kasema nini nami napita humohumo.
 
Ulitegemea nini kama hadi msemaji wenu wa Simba anamu-adress kwa jina la mzungu?


Mletee mzunguu, mletee mzunguu!
 
Nikusaidie kidogo mleta uzi. Utani wa Simba na Yanga siku zote ni kufurahia mabaya ya mwenzake. Kwa hiyo ukiuchukulia "serious" ndugu yangu utakufa mapema sana. Siku chahce zilizopata Bigirimana alipata mashambulizi tena mabaya zaidi kuliko haya ya anayopata Dejan.

Kikubwa kinachotakiwa kwa Dejan ni kukomaa na kuwaziba midomo wale wote wanaomzodoa kwa kufanya kazi yake vizuri uwanjani. Ni kazi yake ni rahisi sana kuliko wachezaji wananocheza kiungo, beki au golikipa. Yeye kuwaziba midomo watu ni kufunga tu kila mechi basi. Mayele alikumbana na kadhia hiyo mwanzoni anaanza kucheza Yanga kidogo apotee kabisa lakini sasa amekuwa shujaa wa Yanga na nuksi kwa mashabiki wa Simba.

Ila kwa haraka nikimtazama Dejan kwenye mikimbio yake, namna anavyojipanga, anavyotuliza mpira na utulivu wake sio mchezaji mbaya kihivyo. Ila ninachokiona ni kocha kutaka kumuingiza kwenye mfumo wa Simba haraka na huku viungo wa Simba hawajajua namna gani ya kumchezesha. Na kosa kubwa la kocha wa Simba ni kutaka kumpoteza Phiri ambaye ameshakaa na wenzake zaidi ya mwezi mzima ili huyu mshambuliaji aliyemleta ambaye ana siku mbili awe mfalme pale Simba. Na hilo limetokea hata kwa Onyango dhidi ya Outara.

Ni mtizamo tu.
 
Hii nchi haina ujinga tu,bali kuna wapumbavu kibao pamoja na kuvaa suti zao
 
Tuna wachambuzi wenye upeo mdogo kabisa wanakaa na kujadili vitu visivyohusiana na mpira
 
Ndio maana kasa Hana tatizo na washabiki wa kawaida ila Hawa wanaojiita wachambuzi
 
Natamani dhihaka hizi afanyiwe aliyemsajili maana ni tapeli mkubwa.

Hata alibaguliwa ,huyu kocha mzungu ni mshenzi hafai hata kudogo,waliomleta ni matapeli wenzie washughulikiwe
 
Simba sio timu ya majaribio
 
Naunga mkono hoja. Ubaguzi wa rangi haukubaliki! Na haukubaliki zaidi kwa mtu asiye na hatia yoyote ile kama huyo Dejan.

Lakini pia wakati mwingine simba itafute mshereheshaji wa kueleweka kwenye matamasha yao.

Kwangu mimi naona chanzo cha haya yote ni siku ya tamasha la simba day ambapo Ahemed Ali alitumia neno "Mzungu", huku akiwa hana sababu yoyote ile ya msingi ya kutumia neno hilo. Na badala yake angemtaja tu kwa jina lake, uraia wake, timu alizocheza, nk.

Haikuwa na tofauti na mchezaji wa Kiafrika aende kucheza sika Ulaya, halafu kwenye utambulisho wake yatumike maneno kama "Black man, Negro/Nigger" nk.
 
simba tumedanganywa na hiyo rangi, hakuna mchezaj hapo... Anazurula tu uwanjani
 
Kama kuna watu wabaguzi, basi waafrika watakuwa wanaongoza halafu hawaoni hilo kama ni tatizo.
Sio haki wala sahihi kumkosoa kwa kukejeli asili ya rangi ya ngozi yake.
mugabe aliwanyang'anya mashamba wazungu waafrica wote hawakulaani ila waliunga mkono ila mmarekani mweusi alipouwawa na polisi africa nzima ililaani! leo hii huyu mzungu kila kona anakejeriwa ila samata akifanyiwa hivyo utasikia magazeti yanavyouza habari za kulaani!!!!!
 
Kwa nini alikaa huo mkao kama dume la nyani...
 
Kuitwa nyani au
Na wengine
Kuitwa kitimoto hapo ubaguzi kuitwa mweusi au mzungu hapana bhana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…