Sikubaliani na suala la kufuta sherehe za Nanenane mwaka huu 2021

Sikubaliani na suala la kufuta sherehe za Nanenane mwaka huu 2021

Wakusoma 12

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
4,035
Reaction score
11,462
Wakuu amani iwe nanyi.

Hivi Jana tarehe 10 Februari waziri wa kilimo prof Mkenda alitoa msimamo wa Serikali juu ya sharehe za maonesho ya kilimo ya wakulima Nanenane, ambapo alisema kuwa serikali imeamua kufutilia mbali sherehe hizo.

Moja ya sababu kuu aliyotoa kiongozi huyo ni pamoja na kuelekeza pesa zilizotengwa katika uandaaji na ufanikishaji wa maonesho hayo katika shughuri zingine. Mimi binafsi napinga kufutwa kwa sherehe hizo kwa sababu zifuatazo.

1. Nanenane huadhimishwa kama sehemu ya kuutambua mchango wa kilimo na wakulima kwa ujumla katika ukuaji wa uchumi wa taifa letu, hivyo kufuta sherehe hizi ni kupuuza suala mhimu sana ambalo ndilo linapaswa kusisitizwa katika kipindi hiki cha ukosefu wa ajira kwa vijana wengi.

2. Maonesho ya Nanenane yanaenda sanjari na maonesho mbalimbali ya teknolojia za kilimo hivyo kuyafuta ni sawa na kudidimiza sekta ya viwanda kupitia sekta zake ndogondogo kama SIDO.

3. Maonesho ya Nanenane huenda pia na matangazo ya biashara mbalimbali za mazao hivyo kuzifuta ni kuwanyima wakulima haki ya kutangaza bidhaa zao za kilimo.

Hivyo naiomba Wizara husika ijaribu kukifikiria suala hili kwa uwazi zaidi ili kukinusuru kilimo chetu na biashara zetu.

# kilimo ni biashara.
 
Mambo ni tight sana kibajeti, hakuna fedha serikalini.

Otherwise, nakubaliana na wewe kabisa kuhusu kuinuliwa kwa sekta ya kilimo na sekta mwambata zake ikiwemo sekta ya viwanda.

Maonesho haya ya WAKULIMA - NANENANE ni motivation na push factor ya sekta nzima ya kilimo na wakulima + viwanda.

Kufuta ni sawa na kuamua kuipa kisogo sekta ya kilimo na kuwapuuza wakulima.

Yapo mambo mengi ya kipuuzi na yasiyo na tija ya kuyatupilia mbali na kuokoa fedha ili zitumike ktk maeneo mengine yenye tija.

Mfano idadi ya wabunge karibu 400 ni wengi mno na wanatumia fedha nyingi sana bila ya tija yoyote.

Ni vyema tukawa na wabunge wasiozidi 60 kwa kila mkoa kuwa na mbunge mmoja tu. Huyu anatosha sana kusimama na kuwakilisha wananchi wote wa mkoa husika.
 
Heh... hii ndo naisikia kwako

Hatahivyo, sherehe ambazo zilitakiwa kufutwa tangu zamani ni hizi
1.za kiserikali (kitaifa)
A.mwenge
B.mapinduzi
C.sabasaba
2.za kidini (japo ni universal religious)
A.mawlid
B.christmass
 
Jiongeze na wewe, humuoni mgeni wetu kutoka China kuwa yupo hapa nchini? hata kama hujui kusoma hata picha huwezi kuona mkuu?.
 
Jiongeze na wewe, humuoni mgeni wetu kutoka China kuwa yupo hapa nchini? hata kama hujui kusoma hata picha huwezi kuona mkuu?
Mkuu siyo kweli, sabasaba hawajafuta, mashabiki uwanjani hawajazuiliwa sasa hapo huonu kama kuna namna?.
 
Atakuja Raisi amtukane waziri kufuta Nanenane na bado MATAGA watapiga makofi wakidhani Waziri alitoa tamko lile bila amri kutoka juu
 
Jf ni makumeri tuu siku hizi. Comment yangu mmeifuta ina shida gani? Kumeri nyie ngoja nirudi zangu Twita.
 
88 SIYO sherehe, ni maonesho - wakulima hufundishwa mbinu bora za kilimo
Unajua maana ya sherehe? Basi na Xmas siyo sherehe ni kumbukumbu ya kuzaliwa Yesu Kristu! Watu wanafundishwa namnavya kuyaishi matendo ya kristo. Umeridhika sasa.
 
Wakuu amani iwe nanyi.

Hivi Jana tarehe 10 Februari waziri wa kilimo prof Mkenda alitoa msimamo wa Serikali juu ya sharehe za maonesho ya kilimo ya wakulima Nanenane, ambapo alisema kuwa serikali imeamua kufutilia mbali sherehe hizo.

Moja ya sababu kuu aliyotoa kiongozi huyo ni pamoja na kuelekeza pesa zilizotengwa katika uandaaji na ufanikishaji wa maonesho hayo katika shughuri zingine. Mimi binafsi napinga kufutwa kwa sherehe hizo kwa sababu zifuatazo.

1. Nanenane huadhimishwa kama sehemu ya kuutambua mchango wa kilimo na wakulima kwa ujumla katika ukuaji wa uchumi wa taifa letu, hivyo kufuta sherehe hizi ni kupuuza suala mhimu sana ambalo ndilo linapaswa kusisitizwa katika kipindi hiki cha ukosefu wa ajira kwa vijana wengi.

2.Maonesho ya Nanenane yanaenda sanjari na maonesho mbalimbali ya teknolojia za kilimo hivyo kuyafuta ni sawa na kudidimiza sekta ya viwanda kupitia sekta zake ndogondogo kama SIDO.

3.Maonesho ya Nanenane huenda pia na matangazo ya biashara mbalimbali za mazao hivyo kuzifuta ni kuwanyima wakulima haki ya kutangaza bidhaa zao za kilimo.

Hivyo naiomba Wizara husika ijaribu kukifikiria suala hili kwa uwazi zaidi ili kukinusuru kilimo chetu na biashara zetu.

# kilimo ni biashara.
5+2 tena
 
Back
Top Bottom