Sikubaliani na ujumbe huu wa Sugu unaoleta taharuki na sintofahamu

Kwani majambazi huwa hayaingii na silaha za kivita yakitaka kuteka mahali fulani?
SIlaha walizotumia Ni silaha zitumikazo na Vyombo vya Dola!

Na kingine ni Polisi Aliyekuwa ndani ya Gari kama wangekuwa Majambazi nadhani angetoa taarifa hata baada ya kuondoka kwamba Gari limevamiwa na majambazi..

Na hata Tashriff wenyewe wangetoa taarifa Kwamba majambazi wamevamia basi..

Ila ulisikia Taarifa ya Majambazi kuvamia Basi?

Kuna jambazi gani anapata ujasiri wa kuvamia Basi na Kumchukua Mtu bila kufunika Nyuso zao?
Tena mbele ya Polisi? Na kibaya Zaidi ni Mjini kati kati Kwenye watu wengi na nyumba nyingi za watu na sehemu iliyochangamka? Tegeta??

Huyo jambazi atakuwa na intelligence kali sana!
Na kingine kwanini Polisi ndani ya Basi hakureport uhalifu??

Umesoma Maswala ya Intelligence na criminology Lucas??

Mimi nilisoma Kozi Kuhusu Criminology kidogo..
Kwa tukio hili kwa maelezo ya Wadau Ni tukio hatari sana..

Sisemi kwamba Polisi ndo wamefanya au Serikali wamefanya..

Ila ninachossma ni kwamba Aliyefanya ana Nguvu zaidi ya Polisi au Polisi wamemshindwa au kwa sasa Haogopi tena Polisi Au Kwa sasa ana kibuli sana!

Sitaki kusema mengi ila Vyombo vya Uchunguzi kwa kuwa vimeanza kulifanyia kazi vitatusaidia Sana kujua Hii "Tragedy"..

Umeona Katuni ya MASUDI KIPANYA LEO LUCA..


Unajua inamaanisha nini?
Watu ambao mama kawashikilia Watamuangusha mama akatechain Mapema kabla hajapotoshwa..

Shukrani Mwanangu Lucas
 
Basi alilotekwa Mzee Kibao limetoa taarifa rasmi kwa umma? Hata pole? Watu binafsi wanatoa taarifa wenyewe wamekausha tu? Hii inafikirisha sana.
Wanapata ajali na kuua binadamu wengi na hawatoki kusema chochote kwa hili itawezekana kweli?
 
Wanapata ajali na kuua binadamu wengi na hawatoki kusema chochote kwa hili itawezekana kweli?

Walishatoa fuatilia mitandano yao. It was just a matter of time.
 
Mara nyingi nikiangalia unaachoandika huku kwenye jukwaa huwa napuuza sababu kwa kiasi kikubwa huw aunaandika ngonjera za kufikirika na dhanania ambazo sio halisi ni zina kila namna ya kujikomba kwa wenye mamlaka ili kukidhi tamaa zako binafsi za kujulikana (umaarufu) au kupewa cheo kwa sababu mifumo iliyojengwa hivi karibuni ikianzia na JIWE inaruhusu hayo kufanyika kwa gharama za kutweza utu wa watu na wakati mwingine gharama za damu za watu.

Baada ya kupita humu jukwaani hasa kipindi hiki cha msiba mzito ambapo Mtanzania mwenzetu ameuawa kikatili baada ya kutekwa na baadaye mwili wake kutelekezwa Ununio, Ni matarajio yangu kwamba ungeingiwa na hofu na kuwakumbusha watu hasa wenye mamlaka ambayo wameitwaa kwa nguvu kukumbuka kuthamini uhai ambao ni zawadi tunayopewa na Mungu na sio kiumbe mwingine yoyote.

Nilitaraji ungeficha ujinga wako na ulikumbushe jeshi la polisi na idara ya usalama wa taifa ambayo Rais hivi karibuni ameitungia sheria ya kuruhusu kufanya ukamataji na kuwakinga watumishi wake dhidi ya mashtaka ya jinai ambayo ni kama haya yanayotokea. Nilitarajia ungetoa wito kufanyike reforms kwenye idara ya polisi hasa kwa namna inavyoshughulikia mambo kama haya na jinsi yanavyotokea katika jamii.

Kwanini Jongwe kaka yako kutoka Mwanjelwa amekua na uthubutu kwa kuandika ukweli huo aliouandika hapo:
1. Taarifa na malalamiko ya kuwa kuna watu wanapotea na kutekwa katika mazingira ya kutatanisha zilienea sana kwa kipindi hiki na majibu ya Mama yako ilikua kwamna ni drama na watu wanajiteka na sio kweli. Leo hii watu hawaonekani na mtu amekutwa amekufa.

2. Kule kanda ya ziwa kuna kiongozi mkubwa wa chama chako amenukuliwa na vyombo vya habari katika moja ya mikutano yake kwmaba wakosoaji wa ccm wakipotezwa polisi wasipoteze muda kuwatafuta (SIO POLISI HAO WALIOWAHI KUMUITA KUMHOJI AU CHAMA KUMCHUKULIA HATUA)
3. Sativa alitekwa na akaeleza mfululizo mzima akihusisha kituo cha Polisi Oysterbay, kupigwa risasi na hatimaye kutelekezwa katika pori huko katavi. Sio jalada la uchunguzi wala askari yoyote aliyewajibishwa isipokua serikali ilimpelekeafedha kugharimia matibabu what a shame! Ni kwa namna gani polisi wasihusike na matukio haya ya utekaji na mauaji?
4. Kijana Soka , ambaye alikua ni mkosoaji mashuhuru wa serikali anayeishi tabata akifcanya biashara ya Magari. Mpaka hivi sasa hakuna whereabouts zake na alikamatwa na watu waliojitambulisha kuwa askari wa jeshi la polisi na walimfunga pingu huku wakimchukua na gari yenye namba za usajili la serikali. Polisi haijwahi kutoka kukanusha au kumshikilia mtu yeyote kwa ajili ya uchunguzi wa tukio hilo linalojusu uhai wa Mtanzania ambaye hajafanya kosa la jinai je wasihusishwe na uharamia huo?

5. Mara kadhaa Masauni amenukuliwa na vyombo vya habari akikanusha juu ya utekaji na watu kupotea kwamba jambo hilo halipo na amekua akimtuma David Misime aongee kwa niaba yake na kufanya spining. Unachotakiwa kujua ni kwamba kuwa kwenye nafasi ya uongozi sio kwamba unajua au una ufahamu mkubwa sana kuliko wale unaowaongoza. Ni katiba yetu hii mbovu ndiyo inatruhusu wajinga kuongoza.
6. Bwana Mnyika aliarifu umma juu ya madhila ya kutoonekana kwa Mzee kibao, siku chache Misime anasema anasema polisi wanalifanyia kazi. Cha kusikitisha hakusema amefungua jalada la uchunguzi kituo gani, namba ya jalada au RB hakuna isipokua alitoa taarifa ya kuhadaa umma akijua wazikabisa anadanganya na umauti lazima utamfika mhusika. Je Jeshi la polisi lisihusike?

7. Mazingira ya kutekwa Mzee Kibao yanahusisha moja kwa moja jeshi la Polisi. Kama wewe hujawahi kufika Tegeta nearby Kibo Complex area ni sehemuambayo iko busy muda wote. Katika mazingira hayo alikuwepo Traffic police akiongoza magari, magari yakzuia basi mbele yake, watekaji wakapanda ndani ya basi wakiwa na silaha na kumkamata Mhusika huku wakiendelea kujitambulisha kama askari polisi. Wakashuka na mhusika na kuondoka nae kueleka wanakojua. Kama sio askari polisi traffic lazima angewataarifu watu watu wa patrol na wangefanya intervention ili kumnusurui Marehemu lakini hakuna chochote kilichofanyika. Je tuwatenge polisi na mfululizo wa mauaji hayo na utekaji?
8. Ndugu yenu huko aliyechoma picha inayosadikika ni ya Rais alikamatwa kwa ultimatum akapandishwa kizimbani na kuhukumiwa kwa muda mfupi. Baada ya kulipa faini ameachiwa huru lakini uhuru wake umepokwa na hajulikani alipo mpaka sasa. Jeshi la polisi licha ya kutuhumiwa lipo kimya hata kutoka kujisafisha .
9. Sijui i unafiki au ni utashi wa kweli, kikao cha chama kule Dodoma ambacho mnakiita bunge kilipoketi hivi karibuni. Mooja wa wajumbe aliomba kujadiliwe kwa hali hii lakini dada yako amabaye nae amewahi kuja na kauli "pita nae" akimaanisha kuwaua wakosoaji wa Kiongozi mwenzie akalitupilia mbali aksema sio wakati wake, labda ilikua ni drama.

nimalize: Ikiwa jeshi la polisi halihusiki, kwanini lisianzishe operesheni maalumu ya kukitafuta hiki kikundi cha kigaidi kinachotejka wananchi mfululizo na kuwaua? Kama jeshi la polisi halihusiki kwanini Hata Pale mwananyamala lilitaka kuzuia mwili wa Mzee unapofanyiwa postmetrm wanshaeria wa chama husika wasiwepo?
Lucas tetea ujinga wote wa Chama chako lakini sio kumwaga damu ya Mtu. Jongwe is right and will be right
 
Nilitegemea uwe wa kwanza kulaani vikali kauli ya mwenyekiti wa uvccm taifa ile ndo ilikaa vibaya sana. Yaani mtu amekufa nchi nzima ipo kimyaaaa alafu yeye anasema hizo ni drama!!
Hili jitu ni kwamba ameshaamua kushirikiana na waovu kwahiyo lazima atakaa upande wao. Ambacho hajui ni kwamba damu ya mtu haiendi bure hata siku moja.
Kile kitabu cha Mwanzo: 4: 10-26Mwenyezi-Mungu akasema, “Umefanya nini? Damu ya ndugu yako yanililia kutoka udongoni. Sasa wewe umelaaniwa! Hutailima tena ardhi yenye rutuba ambayo kama kinywa imeipokea damu ya nduguyo uliyemuua. Ukiilima ardhi haitakupatia tena mazao yake. Utakuwa mtu wa kutangatanga, asiye na makao maalumu duniani.” na zaburi ya 26: 5 Nachukia mikutano ya wabaya; wala sitajumuika na waovu.
 
Unatafuta kiki jamii forum au umeshalawitiwa maana Kila siku unapost pumba tu humu maana watu mliolawitiwa hua mnakua na mawazo tofauti na wenzenu
 
Nini kigen kwako hapo?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…