Sikupanga kuwa na mtoto...



Well kwasababu kila mtu anaruhusiwa kuwa na opinion basi naomba niache uendelee kuamini upendavyo.

Ila kama ukijaribu kuelewa post yangu ya kwanza...nia haswa ilikua kuwafahamisha wale wanaolalamika kwamba hawakupanga kuwa na watoto walipanga kwa kutokua waangalifu on the first place. Siwezi kulaumu kwa wale watakaotafsiri tofauti na lengo langu so asante kwa mchango wako.
 
Ni pale unapokuwa ndani ya ndoa na unagundua tayari una mimba na kwa sababu moja nyingine unashindwa hata kufikiria kuitoa.
Tunarudi pale pale kwenye kua mwangalifu...hicho ni kitu ambacho kiko ndani ya uwezo wetu ila tunajifanya hatujali mpaka pale inapotokea. Kama mke na mume wote wamekubaliana hawataki mtoto basi watumie kinga.
 

Hapo chini kwenye red quotation ... inatoka katika uzi wako ... kama nimekuelewa vibaya then nisamehe kwa hilo!!

Pale unapogundua kwamba una mimba na ukaamua kuiacha ili ikue...uzae na kupata mtoto basi unakua umepanga kuwa na mtoto.Huo ndio ukweli na hiyo ndio hali halisi.
Hamna mtoto anaezaliwa kwa bahati mbaya!!
 
Tunarudi pale pale kwenye kua mwangalifu...hicho ni kitu ambacho kiko ndani ya uwezo wetu ila tunajifanya hatujali mpaka pale inapotokea. Kama mke na mume wote wamekubaliana hawataki mtoto basi watumie kinga.

hUWEZI TUMIA KINGA MIAKA YAKO YOTE.
 
Tafsiri ya hapo kwenye red ni nini?
 
Hapo chini kwenye red quotation ... inatoka katika uzi wako ... kama nimekuelewa vibaya then nisamehe kwa hilo!!

Kwahiyo hayo maneno ya kwenye nyekundu yanajustify abortion?! Sikuwahi kufikiri..nwy kama ndivyo haikua nia yangu maana mimi binafsi sisupport abortion!
 
Tafsiri ya hapo kwenye red ni nini?

Tafsiri yake ni hiyo sentensi ya mwisho...hamna mtoto anaezaliwa kwa bahati mbaya maana wote tunajua matokeo ya kuhusiana kimwili na jinsia tofauti. Hivyo watu waache kulalamika na wakubali kuishi na matunda yaliyotokana na matendo yao.
 
Kwahiyo hayo maneno ya kwenye nyekundu yanajustify abortion?! Sikuwahi kufikiri..nwy kama ndivyo haikua nia yangu maana mimi binafsi sisupport abortion!

na utafanyaje ili usiendelee kuwa na mimba ambayo tayari unayo??

Pale unapogundua kwamba una mimba na ukaamua kuiacha ili ikue...uzae na kupata mtoto basi unakua umepanga kuwa na mtoto.Huo ndio ukweli na hiyo ndio hali halisi.
Hamna mtoto anaezaliwa kwa bahati mbaya!!
 
Kwahiyo hayo maneno ya kwenye nyekundu yanajustify abortion?! Sikuwahi kufikiri..nwy kama ndivyo haikua nia yangu maana mimi binafsi sisupport abortion!

Kama husupport abortion huu mjadala wako hauna basis....mtu akipata mimba (bila kupanga) anawezaje kupanga kupata mtoto au kutokupata (ikiwa abortion haikubaliki/huikubali)? Unless kama pia unasema hakuna mimba ambayo haikupangwa! Au kuna sehemu sijakuelewa?
 

na utafanyaje ili usiendelee kuwa na mimba ambayo tayari unayo??


Abortion...miscarriage....

Kwasababu tu sikubali abortion haina maana kwamba haipo au mimi naweza kuzuia mtu mwingine asifanye. The only persona i'm responsible for when it comes to such matters is MYSELF.
Alafu mada yangu iko based kwenye wale walioamua kuzaa...baada ya kuzaa na sio kipindi cha mimba.Hivyo wanaotoa sio wahusika wakuu...wahusika wakuu ni wale walioamua/lazimika kuzaa ila bado wana malalamiko na lawama kibao wanazoelekeza kwa watoto wakati wao wenyewe ndio waliohusika kwenye tendo ambalo lilizaa mtoto huku wakijua fika hilo linawezekana na kutokujali kwa wakati ule.
 

Sikujua kama miscarriage nayo inapangwa! Naweza kukubaliana na wewe kwamba sio sawa kuelekeza lawama kwa mtoto....lakini hilo haliondoi ukweli kwamba muhusika hakupanga kumpata huyo mtoto (isipokuwa alilazimika kwa sababu asingeweza kufanya abortion kwani kwa kufanya hivyo ni kinyume na sheria).

Keyword katika mada yako ni kupanga, kama una specific definition ya hilo neno katika muktadha wa mada yako ingalikuwa vema unge share na sisi ili tujue tunajadili kitu gani. Inawezekana mjadala wote huu unarevolve around tofauti tulizonazo juu ya defintion ya 'kupanga'. Lakini kama ni kupanga kama tunavyolitumia katika matumizi ya kawaida...then yes mtu anaweza kupata mtoto/kuzaa bila kupanga!
 
kuna miscarriage fake mtu anatoa mimba lkn unaambiwa imetoka yenyewe ...
 
Hi lizzy! Ni kweli hakuna mtoto anazaliwa kwa bahati mbaya ila vile vile hakuna anayependa kuzaa wakati hajawa na utayari au uwezo wa kufanya hivyo.
Kuna mdada mmoja alizaa kwasababu alikuwa anashambuliwa na dada zake ambao walikuwa na watoto.
Hakupanga kupata mtoto kwa kipindi hicho, hakumpenda hata huyo mwanaume aliyezaa nae ila mazingira yalisababisha afanye hivyo.
Mambo yanapoenda tofauti na matarajio, kauli kama hizo huwa hazikosekani.
Ila kwa yoyote anayefanya yale mambo atarajie suala la mtoto, yaani ajiandae kwa lolote asije sema hakupanga.
 
Kwani mwanamke katika mzunguko wake wa mwezi ana siku ngapi ambazo anaweza kupata mimba na ana siku ngapi ambazo kamwe mimba haiwezi kuingia? mkipata jibu la swali hili ndio mtajuwa kwamba hakuna mimba ya bahati mbaya bali ni uzembe wa wanawake. PERIOD.
Mwanamume hausiki na maswala ya mimba hapa ni lazima ieleweke, mwenye uwezo wa kupokea au kutokupata mimba ni mwanamke, huu ndio ukweli wenyewe.
 

hii mada ina sarakasi nyingi sana ... Matola ningekushauri usome tena substance ya uzi wa Lizzy na halafu upime kama ulicho comment bado kina hold! unless, huu uzi una maana 2 tofauti, kitu ambacho sikubahatika kukiona!
 

Kujua mzunguko tu hakutoshi mkuu....waulize waliopo kwenye ndoa na hawana watoto watakwambia vizuri! Hili suala la mzunguko lipo complicated na peke yake tu lina several assumptions. Kwamba mwaume hausiki sio kweli hasa.
 

What I meant was ..mtu anaweza akapata miscarriage....japo sio yeye anaefanya iwe hivyo bado inafanyika.

Kuhusu kupanga tunarudi pale pale kwenye knowledge. Wengi wetu tunajua sana matokeo ya sex...mtu anapoamua kufanya mapenzi bila kuwa mwangalifu tayari anajua kwamba anaweza akapata mimba na bado anaendelea kufanya vile. Kitendo hicho ni kielelezo tosha kwamba alipanga (japo anajifanya hataki kuwa na mtoto/hakutaka kupata mimba!
 
hii mada ina sarakasi nyingi sana ... Matola ningekushauri usome tena substance ya uzi wa Lizzy na halafu upime kama ulicho comment bado kina hold! unless, huu uzi una maana 2 tofauti, kitu ambacho sikubahatika kukiona!
Madabwada inawezeka mimi na Lizzy tukawa tumeongea kitu kimoja lakini katika Lugha tofauti,.....nakushauri na wewe usome upya uzi wa Lizzy uone maudhui ya lugha yake, ndio maana mimi nimeamuwa kutoa ufafanuzi katika lugha nyepesi lakini ikiwa imebeba mantiki mbadala kwamba kupata mimba zisizotarajiwa ni uzembe wa mwanamke,.........nilitalajia kama ni chalenge ungechalenge hapo.

Narudia tena kusema, mimba zisizotaljiwa ni uzembe wa mwanamke kwa sababu anazijuwa siku zake vyema, na kondomu kazi yake sio kuzuia maambukizi ya ukimwi bali kazi kuu ya kondomu ni kuzuia hizi mimba zisizotalajiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…