Simama kwa miguu yako

Emc2

JF-Expert Member
Joined
Sep 26, 2011
Posts
16,808
Reaction score
16,887
I HAVE A DREAM: "ONE DAY I WILL HAVE A BIG TECHNOLOGY COMPANY IN OUR COUNTRY AND THE WHOLE WORLD"



Watakutumia kama muwa na kukutupa kule usiwe na faida. Baada ya kupata wanachohitaji kwako watakutupa kuleeee. Usione wanakuchekea ni wanafiki hao lengo lao ni kupata wanachohitaji kutoka kwako. Wanakupa maisha ya muda mfupi siyo ya kudumu.

Basi simama kwa miguu yako unauwezo wa kufanya chochote kikubwa. Unanguvu zaidi yao na wanakuhiaji sana kwa sasa. Jitambue sasa na uanze kuzifanyia kazi ndoto zako. Tumia mda wako vizuri kupangilia mambo yako.

Halafu kumbuka kunawatu lazima uachane nao iliuweze kufanikiwa. Si kila mtu wa karibu na wewe anafaa kuwa na wewe. Vile vile kumbuka kunawatu lazima ukutane nao ili mambo yako yaweze kwenda.

Simama kwa miguu yako maana hao ulio nao ni mabepari, hawana huruma, wamepanga mipango yao. Sasa basi usibweteke na hivyo vitu vya mda wanavyokupa. Hawana huruma hao watakutupa kama takataka. Wamejaa udhalimu wa kila namna, wanajua mambo yao tu.

Bado unanguvu sasa jitahidi kufanya mambo yako na kupangilia vizuri mambo yako kabla ya taa kuanza kufifia. Mda huu ndio mwafaka wa kupangilia maisha yako vizuri.


Simama kwa miguu yako.
 
kuna gazeti la jitambue sijui limefia wapi, anyway ujumbe mzuri kwa asubuhi hii:clap2::clap2::clap2::clap2:
 
Wakati mwingine unaweza ukawa na mipango yako mizuri sana. Kumbuka kuwa kuna watu wengine hawatakiwi kabisa uwe nao kwenye maisha yako. Endapo utakuwa nao tu hizo ndoto zako zote zinaanza kufifia.

The dreamers never die. Mpaka ndoto zao zitakapo timia.
Nelson Mandela alipata kufaliki pale ndoto zake zilipotimia.
Wale wasomaji wa vitabu vya dini hususani biblia mtakuwa pamoja na mimi kuhusu histori ya Yusuph. Aliota kuwa ndugu zake watamsujudia. Ndivyo ilivyo tokea.

Kama mtu huna ndoto hakika utakuwa unaishi tu duniani bila dira na mwisho wa siku unaweza ukaondolewa tu ki ajabu ajabu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…