Simba akipoteza pointi 3 kupewa mkono wa buriani

Simba akipoteza pointi 3 kupewa mkono wa buriani

hamis77

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2013
Posts
13,628
Reaction score
20,992
Kwa taarifa zilizopo Ni Kwamba Simba akipoteza point 3 tu, au akidroo mechi 2 na kupoteza points 4, Basi rasmi atapewa mkono wa burihani.

Kwa Sasa kiuhalisia Yanga anamuacha Simba point 5 ,hiyo mechi ya kiporo ,Kamati ya ushindi ya Yanga haiwezi kukubali wapoteze au wasare.

Mkakati uliopo Ni kuhakikisha Simba akipoteza point 3 au 4 , Litengenezwe gepu la points 8 had 9, Kisha Simba aambiwe ukweli ajipange msimu ujao.

Points 8-9 ukiachwa na Yanga hii ,shughuli inakuwa imeishia hapo

Azam Hana ubavu wakukimbizana na Yanga ,maana yeye kimahesabu kaachwa points 6 , bado hajavutwa mechi 2 au 3 .


Target ya Sasa Ni Simba apigwe mechi 1 au sare mechi 2 , Kwanza kutatokea fujo ya kutukuzana na migogoro maana Hadi Sasa Simba hawajafanya uchaguzi pia Kuna mahitaji ya mabadiriko ya Katiba.

Kupoteza points 3 au 4 automatically wale wanaotaka uongozi Simba watatumia huo mwanya kuleta migogoro ,maana Ni dhahiri Yanga hatakamatika Tena .
 
Kwahiyo mmekaa na kamati yenu iwe isiwe simba ifungwe mechi moja sio
Ngoja tuone huu upangaji wa matokeo
Kingine suala la uchaguzi haliwezi kuteteresha klabu maana wakina mangungu hawatoi pesa zao mfukoni kuendesha timu nadhan mnajua timu iko kwenye mikono ya nani
 
Sisi mashabiki wa simba tuna imani na mwekezaji wetu. Hata tukifungwa, tutajipanga tena kwa msimu ujao.

Yaani sisi kazi yetu itakuwa ni kujipanga tu kila msimu.
Utopolo iliwatumia miaka minne kujipanga, sisi wala hatuna shida.
 
Sisi mashabiki wa simba tuna imani na mwekezaji wetu. Hata tukifungwa, tutajipanga tena kwa msimu ujao.

Yaani sisi kazi yetu itakuwa ni kujipanga tu kila msimu.
Kama sisi wa yanga tulikaa misimu minne bila kombe
 
Back
Top Bottom