Simba hii.. Jeuri Tupu: Yasajili Kipindi Ligi Inaendelea.

Simba hii.. Jeuri Tupu: Yasajili Kipindi Ligi Inaendelea.

sembo

JF-Expert Member
Joined
May 25, 2011
Posts
4,350
Reaction score
3,451
"Mnyama afanya usajili katikati ya ligi".. ndivyo pia waweza kusema.. Na hii ni baada ya ITC ya yule kiungo bora kabisa toka "kwa wanaojua" nchini Kongo.. Mussa Ndusha kupata baraka zote toka TFF kuanza kuitumikia Simba S.C.

Hii inamfanya kiungo huyo mwenye sifa za "kupiga pasi rula", "pita wewe mpira uuache", "uwezo mkubwa wa kumiliki mpira", "uwezo mkubwa wa kufunga" kua huru kucheza mechi zozote zile zinazotambulika na;
1. TFF [ambazo ni ligi kuu na kombe la FA]
2. CAF [ambazo ni kombe la klabu bingwa barani Africa, mwaka 2018]
3. FIFA [za michuano ya mabingwa wa mabara kwa levo ya vilabu, mwaka 2018].

Usajili huu unafanya dimba la kati la Simba S.C liwe na mafundi hawa;
1. Jonas Mkude 'Le Captain'
2. Mzamiru Yassin
3. Mohamed Ibrahim 'Mo'
4. Said Ndemla
5. Mwinyi Kazimoto 'Ball Dancer'
6. Awadh Juma 'Mtani Jembe'
7. Mussa Ndusha

Kwa upinzani huu uliopo katika nafasi hii ya kiungo... wapinzani wetu wakuu msimu huu [Stand United, Mtibwa na Prisons] mjipange kisawasawa, maana la sivyo tutawaacha hata gepu la pointi 10.

1477127633861.jpg
 
Mavuge tumekula hasara
Mkuu tumpe muda.. Kama kocha wetu anavyotutaka.
Nalinukuu gazeti moja la michezo.. "... Omog ambaye amewataka mashabiki wasimbeze Laudit Mavugo kwavile yeye ndiye anayeshinda naye mazoezini na anajua nini kinakuja, wawe na subira."
 
Mavugo mchezaji mzuri, na kizuri hakikosi kasoro. Akiendelea kufanyia kazi uchoyo, na timing ya kutoa pasi atakuwa shujaa ghafla
 
Back
Top Bottom