Simba hili kundi tutachukua points kwa nani?

Naona watu wamechukulia kundi kirahisi ila mziki wa Berkane Kama unafuatilia mechi zao mpira wa kasi wanaocheza ni balaa
Kocha wao si ndio alikua AS Vita , amefungwa mara 3 mfululizo na Simba
 
Katika kundi hili ASEC Mimosas ya mwaka huu inaweza kuwapa Simba changamoto zaidi, na si RS Berkane
 
Baba wa kaya analeta nini? Simba awe baba wa kaya na AL Ahly awe nani nyie mbumbumbu?
Al Ahly hachezi NBC Premier League, uwe unaelewa, Simba ni baba wa kaya NBC Premier League
 
Naamini kurudi kwa Lwanga na Fraga hapo Kati kutaituliza timu...hapo tunahitaji kiungo mshambuliaji mmoja na mshambuliaji mmoja, Basi. Mechi zenyewe zinaanza mwezi wa 2 katikati timu itakuwa imeimarika tayari
 
Naona watu wamechukulia kundi kirahisi ila mziki wa Berkane Kama unafuatilia mechi zao mpira wa kasi wanaocheza ni balaa
hawa berkane wakutoa draw na APR ndio amsumbue Simba??? unaumwa korona wewe!

kwenye Hilo kundi Simba anaongoza
 
Kumbe ndiyo maana haya majamaa yameshiriki CL nyingi ila zote yanagoma kufika makundi maana yanajua fika yatadhalilika [emoji23][emoji23]
Ukiona wanatajtaja 5-0 alizopokea Simba mwaka ule, ujue yanaogopa maana katika hayo magoli 19 waliyofungwa, kulikuwapo kipigo cha 6-0 walichopokea kutoka kwa Raja Casablanca ya Morocco
 
Timu ya kutusumbua kidogo labda Mazembe na Pyramid. Mwaka huu hiyo ndoo ya shirikisho tunaichukua asubuhi tu.
 
Baba wa kaya analeta nini? Simba awe baba wa kaya na AL Ahly awe nani nyie mbumbumbu?
Usianze kutamani mabwana wa wenzako(waarabu), wewe bwana wako ni simba mvumilie tu hâta kama hirudi na kitu kikubwa maana utafutaji sio kitu kirahisi.

Wewe hujifunzi kutoka kwa mabwana ambao umekuwa ukwapokea na kudhania kuwa wanaweza kuwa na kitu special kuliko bwana wako lakini kila siku anawabonda?? Amini katika nguvu za bwana wako.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapa simba tukatalii tu kisha turudi kujenga kiota
 
Simba a.k.a Wazee wa Influenza watapata kujiimarisha zaidi kwa kushiriki Kombe la Mapinduzi. Maana watakutana katika michuano hii na timu ambazo si za kubeza hata kidogo za Mchambawima F.C, Bububu United pamoja na Kizmkazi Rangers.

Sent from my Nokia 2.3 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…