Simba ifanye nini kuishinda USG

bulabo

JF-Expert Member
Joined
Aug 20, 2015
Posts
628
Reaction score
780
Kwa kuangalia analysis na game plan ya mchezo kati ya Asec vs Simba Coach Pablo alifeli sana katika mipango. Alijisahau kuitizama asec wakiwa na mpira wanakuwa na kasi ya ajabu huku sisi wachezaj wetu ni wazito sana. Kwanza ilibidi aanze na Viungo wa kukaba wawili LWANGA+MZAMIRU ili kuipa nguvu beki laini ya SIMBA. Kwa kosa hili kumeigarimu timu ya simba.

Mchezo wa SIMBA vs USG

Hii mechi ngumu sana kwa Simba kwa sababu hawa USG ni kama ASEC tu huyu Adebayor ni hatari zaidi ya kanate wa ASEC. Ili SImba ifanikiwe wajipange kukaba sana hasa hasa katika kwenye mechi hiyo KANOUTE + LWANGA Waanze ili kuwadhbiti ukimbiaji wa viungo wao. Kufanya hivi kutaipa nguvu simba kucheza mpira wake ingawa inavyoonekana benchi la ufundi la SIMBA wana poor analysis ya michezo hili ni janga kwa Simba na ndio limetufikisha hapa kwenda kukosa ubingwa wa Ligi kuu kutozisoma vzr mechi za wapinzani wetu hata hii mechi ya juzi na berkane tushukuru.

Mwisho wa ligi

Simba ilete maingizo mapya sio lazima congo tuchukue hata huko ( asec usg )vijana wenye damu changa na coach wa fitness wa zamani wa simba arudishwe waangalie wachezaj wengi wa Simba wamenenepa mnoo LWANGA MZAMIRU KIBU n.k Pia Kibu sio mchezaji wa kariba ya SIMBA kwa sababu hana uwezo wa kupiga pass, kupunguza hata mchezaj mmoja yeye ni mbio tu kitu ambacho mpira wa sasa unahitaji akili nyingi.

MWISHO SIMBA KIPA TUNAYE, INONGA good Banda good Mugalu angalau anauwezo wa kukaa na mpira hata dk chache MKUDE ana game zake hili ni tatizo(sio wa kutegemea kutupeleka fainal), Tshabalala is good ila anahtaji backup akienda mbele hapo jana alikosa hiyo huduma hili ni tatizo la kocha(Pablo abadilishwe mwisho wa msimu ikiwezekana). Kapombe is good ila umri umeanza kumuacha(ISRAEL anatakiwa kustep up).

Kagere ameisha, Bocco ameisha, Mzamiru bad passer(Anapiga pasi kwa maadui sana) na unene hana mbio, Onyango ameisha, WAWA ameisha, Bwalya sijajua tatizo lake ni mfumo au nini hana nguvu, Chama very slow ndio maana amefeli berkane hana speed, Haya mambo SImba wayaangalie kama tunataka kufika fainali ya CAFCC. Ukiangalia mechi za CAF mpira unapigwa balaa nimeangalia mechi ya Orando, al altihd, TP Mazembe, Pyramids wanaubonda sana kitu ambacho SImba kucheza away ni tatizo kwetu kuvuka kwenda mbele.

CHINI YA MO DEWJI NA ANAUJUA MPIRA SIMBA ITAFANYA MABADILIKO SAFI ( Transition isiyoathiri timu iliyopo)

NAWAKILISHA, MKULIMA WA NANASI IRINGA

NGUVU MOJA.
 
Wafanye kama wanavyofanyaga tu wanapocheza kwa Mkapa
 
Hapo kwa ISRAEL , wamrudishe DUCHU, yule kijana waliyempeleka kwa mkopo Geita Gold FC yupo vizuri sana. Mechi iliyopita na Yanga aliwasumbua sana.
 
Huyu kocha si mzuri , kwa malengo ya Simba yalivyo huyu hafit .Kocha anayetakiwa Simba anatakiwa awe full tacts na awe na mfumo unaoeleweka wa kucheza sasa kocha hujui anaamkaje yaani kama game ya jana Mkude na Mzamiru hii ni comb gani? Mchezaji hata kupiga accuracy pass hawezi eti akawekwa eti mido wa kuchezesha timu.

Na usajili walifeli wenyewe maana kila kijana wa ndani walimtupia virago kila siku kusajili ,akina Ame wana kitu ila tumewatupia virago tumebaki na madingi tupu
 
Ibenge aliwapa bichwa kua watafika fainali😂😂
 
Iroge / Turoge sana hata kwa Kukufuru.
 
Hapo kinachotakiwa ni kupulizia tu dawa kwenye chumba cha kubadilishia nguo cha wageni, wiki moja kabla ya mchezo. Maana hakuna namna..
 
Simba ni Lipuli fc iliyochangamka.... Alisikika mlevi mmoja.
 
Inatakiwa kufunga magoli tu na kutoruhusu goli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…