Simba ijiandae, Wana Nkurukumbi hawajaja kushangaa mataa Dar es Salaam

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Simba inashuka dimbani jumatano kupepetana na Kagera Sugar ambao raundi ya kwanza waliwadhalilisha ugenini kwa bao la mchezaji wao wa zamani Hamis Kiiza Diego.

Kagera Sugar ni miongoni mwa timu zinazoisumbua sana Simba, walishawahi kuwadhalilisha mbele ya Hayati Magufuli, wana mafundi hasa sio masihara, wameweka kambi Morogoro kuepuka hujuma za mnyama, Simba wajipange otherwise itakuwa kama Yanga na Prisons vile.

Link imekuwa tamu sana.
 
Sasa hiyo jumatano ufike uwanjani uone maana halisi ya kudhalilishwa hao mafundi wao.
 
Tunaham nao tena wajiandae si chini ya bao mbili
 
Reactions: BRN
Wewe umechanganyikiwa

Dakika 10 umeweka thread 8

Nakuhakikishia mpaka mwisho wa msimu lazima uwe na faili Mirembe
πŸ€£πŸ€£πŸ€£β˜οΈβ˜οΈβ˜οΈπŸ˜‚πŸ˜‡πŸ˜πŸ€Έβ€β™‚οΈπŸ€Έβ€β™€οΈπŸ˜„
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…