Simba imefanya maamuzi mabovu kwenye usajili wa Asante Kwasi

Simba imefanya maamuzi mabovu kwenye usajili wa Asante Kwasi

Prince Warinko

New Member
Joined
Jan 7, 2018
Posts
2
Reaction score
1
Simba imefanya maamuzi mabovu kwenye usajili wa Asante Kwasi,imesikiliza mapendekezo ya mashabiki badala ya mwalimu

Kwasi sio mbaya ila hana uwezo wa kucheza simba kwenye kikosi cha kwanza,anaweza kwa Simba lakini sio kucheza kama mchezaji tegemeo.

Kwenye mchezo wa jana alifanya makosa zaidi ya matano lakini kosa moja kati ya hayo yaliigharimu timu.

Tulimlaumu mwalimu tunapaswa kuwalaumu viongozi na mashabiki wa Simba.

Unamsajili Asante kwa kigezo etii anafunga kwa Simba hakuna washambuliaji?.Tunahitaji kubadilika na sio kusikiliza kelele za mashabiki.

Mashabiki wengi wanapenda kuwaona wachezaji wanaowapenda na sio kwamba wanawajua "hapana" ,yani mchezaji "aki-kiki" tuu wanamtaka,akuwafunga tuu wanamtaka kama ulivyokuwa kwa Chelsea kipindi kile Mo Salah yupo Basel aliwafunga na mashabiki wakaomba asajiliwe na uongozi ukatii kelele za mashabiki na baada ya muda wakamuuza.TUBADIKIKE,TUONDOE MAAMUZI YA KIJINGA.
 
Asante kwasi ana kiwango kinachofaa kuichezea Simba.
Ni mchezaji makini na mwenye bidii mazoezini na mchezoni. Kikosi cha timu lazima kiwe kipana ili kukabiliana na matatizo ya wachezaji kama Majeruhi, dhalula na mengineyo.
 
Wameshamfukuza kocha sasa kilichobaki ni kuchapana viboko2 maana mambo yapo vilevile
 
Back
Top Bottom