Simba ipeleke wachezaji wa akiba Singida, 11 bora waisubiri Sevilla

Simba ipeleke wachezaji wa akiba Singida, 11 bora waisubiri Sevilla

HPAUL

JF-Expert Member
Joined
Jan 18, 2011
Posts
410
Reaction score
567
Leo tarehe 19 Simba anacheza na Ndanda, keshokutwa tarehe 21 Simba anacheza na Singida United na tarehe 23 Simba anacheza na Sevilla. Tukumbuke hakuna shirika la ndege linaloenda Singida, wala hakuna uwanja wa ndege mkubwa ambapo Simba ingeweza kukodi Ndege, hivyo usafiri pekee ni basi ambapo Dar hadi Singida ni km 718. Usafiri wa basi ukizingatia torch na speed limit ya 80 km kwa saa pamoja na chakula njiani na kuchimba dawa ni masaa 11. Hivyo kama Simba wataondoka kesho alfajiri saa 10 watafika Singida kesho alasiri saa 9. Hivyo watapumzika tu bila kufanya mazoezi kusubiri mechi ya keshokutwa na baadaye usiku kuanza safari ya kurejea Dar ambapo watafika mchana wa tarehe 22 siku ya Jumatano na Alhamisi watacheza na Sevilla.
Ni dhahiri wachezaji watakuwa wamechoka kupindukia na hawatakuwa katika kiwango cha kupambana na timu kubwa ya Hispania, itakuwa aibu.

Nashauri Simba kikosi cha wachezaji wa akiba kule Singida, na 11 bora wabaki kuisubiri Sevilla. Kama ni ubingwa Simba ataupata tu kwa msimamo ulivyo. Ubaya zaidi Simba sasa hivi imepungukiwa na wachezaji kwani kuna majeruhi hasa mabeki kama Juuko, Bukaba na Kapombe. Ingawaje taarifa nzuri ni kurejea kwa Wawa.
11 bora wa kubaki na Aussems 1. Manulla 2. Gyan 3. Tshabalala 4. Nyoni 5. Mpilipili 6. Mkude 7. Niyonzima 8. Chama 9. Bocco 10. Kagere 11. Okwi
11 wa akiba kwenda na kocha msaidizi Singida 1. Dida 2. Zana 3. Kwasi 4. Kotei 5.Wawa 6. Ndemla 7. Abdul Hamisi 8. Muzamiru 9. Salamba 10. Mo 11. Dilunga Reserves Ally Salim, Vincent Costa na wengine under 20
 
Wakitokea Mwanza au Dodoma airport haitafaa? Zingatia kuwa mechi na Singida ni muhimu kuliko ya Sevilla.

Mki lose kwa singida mnajipunguzia mbio za ubingwa, bora waende tu kozi mechi na Sevilla mmesha lose hata kabla ya game cha kufanya labda kubuni mbinu za kupunguza idadi ya magori. (Zingatia Mimi ni shabiki wa Yanga.)
 
Duh wachezaji 11 bila hata wa akiba hata mmoja..so mchezaji akiumia na akashindwa kuendelea hiyo mnakuwa mmejipa kadi nyekundu
 
Wakitokea Mwanza au Dodoma airport haitafaa? Zingatia kuwa mechi na Singida ni muhimu kuliko ya Sevilla.

Mki lose kwa singida mnajipunguzia mbio za ubingwa, bora waende tu kozi mechi na Sevilla mmesha lose hata kabla ya game cha kufanya labda kubuni mbinu za kupunguza idadi ya magori. (Zingatia Mimi ni shabiki wa Yanga.)
Labda Dodoma ambapo ni km 234 hadi Singida masaa matatu ya basi lakini kumbuka Airport Dar wataspend kama saa 2 na angani Dar to Dodoma kama saa 1 hivyo jumla kama masaa 6, watakuwa wamepunguza uchovu kidogo tu. Hicho kikosi kinachoenda Singida kinaweza lazimisha sare, na leo tunapata ushindi dhidi ya Ndanda, hivyo ubingwa tayari. Mechi za Biashara na Mtibwa ni bonasi tu.
 
Wakitokea Mwanza au Dodoma airport haitafaa? Zingatia kuwa mechi na Singida ni muhimu kuliko ya Sevilla.

Mki lose kwa singida mnajipunguzia mbio za ubingwa, bora waende tu kozi mechi na Sevilla mmesha lose hata kabla ya game cha kufanya labda kubuni mbinu za kupunguza idadi ya magori. (Zingatia Mimi ni shabiki wa Yanga.)
Dodoma angalau watakuwa wamepunguza masaa. Kama wanaweza waondoke leo wakalale Singapore. Majembe ya kuiua Sevila yawe bench,kina Zana na Salamba wakizidiwa fasta Gyan na Kagere wachome ndani
 
Duh wachezaji 11 bila hata wa akiba hata mmoja..so mchezaji akiumia na akashindwa kuendelea hiyo mnakuwa mmejipa kadi nyekundu
Timu inayoenda singida itakuwa na wachezaji wa akiba Ally Salim na Vincent Costa, lakini vile vile kanuni zinaruhusu kuchezesha under 20 watano. Timu A inayoisubiri Sevilla reserves wake ni hao wanaoenda Singida kwani watakuwa wamerudi.
 
Back
Top Bottom