Simba itadhalilishwa hadi lini?

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Ni kweli kwamba kapuku hana thamani, lakini wakati mwingine umasikini tunajitakia tu , kwa umati wa wanachama na wapenzi wa simba nchi nzima timu hii haistahili kuitwa masikini, kama tutapata oganaiza mzuri mwenye ujuzi na mfia Simba, basi timu hii itaweza kujikimu na hivyo kuondokana na dhiki inayolazimika timu yetu kutumika hata kwenye mambo yasiyostahili kwa vile tu anayeitwa mwenye Simba yake anatumika.

Simba si timu ya kucheza bure , ambapo pamoja na kutangaza bure bado ikakosa watazamaji, hili ililofanyiwa timu ya simba ni aibu inayotufanya sisi wanasimba wengine tuinamishe vichwa chini kwa aibu, mara kadhaa nimejipambanua humu kupinga magumashi kwenye uendeshaji wa timu lakini nimeishia kubezwa na kutukanwa, bali sasa uvumilivu umefika kikomo, Simba irudishwe kwa wenyewe.

 
Wewe unataka jina liheshimiwe wakati wenzako wanataka rekodi ya kushinda mechi nyingi kabla ya ligi. Kesho watacheza mechi ya kirafiki na bodaboda wa kwa mama john mwakangale.

This is another level
Aiseeeee !!!
 
Ivooo kumbe ndo venyewe ilikuwa?
Walioitumia Simba kwa manufaa yao wanajisikiaje sasa?
Na wakome kuingiza siasa zao kwenye michezo
 
Naunga mkono hoja....this is too much ,hii sio Simba!
Hapa mguu utaota tende.
 
Endelea kusubiri hapo hapo simba kurudishwa kwa wenyewe, kichwa chako kibovu una relate kila kitu na siasa, siasa imekuharibu kichwa jitathimini na jitafakari
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…