Simba kuachana na Morrison ni uthibitisho kuwa ni taasisi imara

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Zamani ilikuwa ni vigumu kwa Simba kumtema au kumweka mapumzikoni mchezaji tegemeo hata kama hana nidhamu, ilikuwa ikiogopa kuwaudhi wanachama na mashabiki wake kwa sasa hivi mambo hayo hamna.

Kwa namna Morrison alivyokuwa na mchango kwenye timu huku bado tuna safari ya kuusaka ubingwa na bado tuna kombe la ASFC, na bado wachezaji kibao majeruhi lakini uongozi umeona Morrison harekebishiki nidhamu yake, umeona Simba ni kubwa kuliko yeye.

Simba imemuonya vya kutosha Morrison na tukio la juzi la kumjeruhi shabiki wa Yanga ndio limewakera sana viongozi na kuamua kumweka kando, hata kama ni mchezaji mzuri kiasi gani.

Sidhani kama Yanga wanaweza kumuadhibu mchezaji muhimu kipindi hiki na kumwambia apumzike kama walivyofanya Simba.

Kila la heri Morrison.
 
Utopolo hii ninayoijua?Hata mchezaji awatukanie mama yao mzazi kama ana kipaji watamchukua tu
 
Hakuna adhabu ya mapumziko soma vizuri barua
 
Simba wameshindwana na Morrison ishu sio nidhamu labda malipo,Mbona Mkude ana matatizo ya kinidhamu na bado yupo Simba?
 
Simba wameshindwana na Morrison ishu sio nidhamu labda malipo,Mbona Mkude ana matatizo ya kinidhamu na bado yupo Simba?
Mukude ni mzawa na hajawahi kuiba gari wala kubaki na kichupi uwanjani ndo Maana anavumiliwa
 
Rafiki yangu yawezekana hujui historia,unajua kuwa yanga ilifukuza timu nzima?
 
Kuna mtu humu kasema mkude ana watu, Morrison kaiga kichwa kivhwa kwa Mkude wakati mwenzie mkude ana watu haswa
Ilibidi Simba idanganye uma "tukimpima na ikionekana anashida ya ubongo tunamfukuza'' ama kweli anawatu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…