Tetesi: Simba kupata Captain mpya hivi karibuni

Tetesi: Simba kupata Captain mpya hivi karibuni

Nani anastahili kuwa nahodha mpya wa Simba?

  • Henock Inonga

    Votes: 11 16.7%
  • Shomari Kapombe

    Votes: 7 10.6%
  • Clatous Chama

    Votes: 12 18.2%
  • Che Malone

    Votes: 3 4.5%
  • Fabrice Ngoma

    Votes: 4 6.1%
  • Mzamiru Yassin

    Votes: 4 6.1%
  • Moses Phiri

    Votes: 2 3.0%
  • Denis Kibu

    Votes: 16 24.2%
  • Essomba Onana

    Votes: 5 7.6%
  • Kennedy Juma

    Votes: 2 3.0%

  • Total voters
    66
  • Poll closed .

SAYVILLE

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2010
Posts
7,895
Reaction score
12,975
Simba imeondoka leo kuelekea Morocco katika mtanange wa kufa na kupona dhidi ya Wydad AC. Katika safari hiyo, Captain wa Simba John Bocco ameachwa nyumbani. Hii ni safari ya pili mfululizo ambapo Bocco ameachwa katika safari wakati katika uwanja wa mazoezi anaonekana. Safari ya kwanza ilikuwa ile ya Botswana kucheza dhidi ya Jwaneng Galaxy.

Kuna dalili zote kuwa Benchikha hakubaliani na uwepo au uongozi wa Bocco katika timu maana hizi ni mechi muhimu sana na kuachwa kwa Bocco katika safari nzima kuna tafsiri iliyo wazi.

Nani unadhani anastahili kuchukua unahodha wa Simba?

Kwa mtazamo wangu, Simba inahitaji nahodha mwenye ufahamu mzuri wa lugha ya kigeni, hii itasaidia kuwakabili marefa katiks mechi za kimataifa. Pia inabidi kuwa anaweza kuisimamia timu na kuhakikisha nidhamu na ari ya kushindana kupo kwa hali ya juu ndani na nje ya uwanja wa mazoezi na mechi.
 
Mbona haujamweka Mohamed Hussein? Mm naona anajituma sana na ana moyo na Simba...
He is Simba's Icon....
Nimejaribu kumuongeza imeshindikana. Inaonyesha wakishaanza kuvote hairuhusu tena kuedit machaguo. Ila siyo mbaya, wanaomtaka waendelee kumtaja tutajumlisha kura zake mwishoni.
 
Kuwa specific bro nanii???? Acha kuzunguka zunguka na wakati wachezaji wanajulikana.....inonga au Nani????
Piga kura yako bro. Kama kuna unayemtaka awe nahodha ila hajaorodheshwa hapo, mtaje tu
 
Simba kwenye mech hyo anakufa, wydad kapoteza mech 2, hatakubali kupoteza ya 3 kabisa.
Hii sio sababu.
Mechi ya 1 na ya 2 alikubali kupoteza? Tuambie Simba itafungwa kwa sababu zipi za kimpira sio suala la kukubali au kukataa.
Labda useme kikosi cha Wydad kipo nyumbani, kina uzoefu na ni bora kuliko Simba.
 
Tunakujua wewe ni Yanga lia lia kwa hiyo kwenye hili mtuache familia. Mawazo yenu hayawezi kuwa na nia nzuri kwa Simba
Mbona nyie mliingilia suala la Feisal na hata majuzi hapo mkamuunga mkono Gamondi kwenye kukataa mechi kupewa jina la mchezaji?

Tanzania ni yetu sote kabla ya timu, na maendeleo hayana timu Mkuu.
 
Back
Top Bottom