Hapo mwanzo Simba haikuonekana timu tishio. Kila mshabiki wa Simba hakuwa na tumaini na timu yake. Ndipo Mo akasema, anarudi kwenye uenyekiti wa bodi ya wakurugenzi. Ikiwa jioni, ikawa asubuhi siku ya kwanza.
Mo akamleta Camara akasaidiane na Manula, Salim na Abel. Mo akamwambia Camara, kwa muda mrefu tulihitaji kipa anayeweza kucheza ili tuanze kujenga mashambulizi kuanzia nyuma. Camara akasimama kwenye milingoti 3.
Akaenda kuifanya kazi vyema kama alivyoagizwa. Mpira aliucheza na kudaka alidaka. Ubora mkubwa wa Diara kwa misimu kadhaa. Umepata mshindani wa kweli. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.
Mo akamuita Chemalone, akamwambia nikuletee nani? Chemalone akasema , niletee Karabou. Mo akamuongezea na Hamza. Kisha akawaambia.
Simba ni timu inayopenda kucheza mpira. Nendeni mkatuletee burudani uwanjani. Mzuie lakini pia mcheze, mburudishe washabiki na kuelimisha mabeki wengine wa Tanzania. Nao wakafanya kama walivyoagizwa. Ikawa jioni, ikiwa asubuhi siku ya tatu.
Mo akawasikiliza watanzania, washabiki wa Simba kwa wachambuzi, Kuwa Mohammed Hussein na Kapombe wamechoka, Watafutiwe mbadala. Duchu akarudishwa kundini, Kijili na Valentino Nouma wakaletwa ili kuwapumzisha wakongwe.
Ujio wa Kijili ukawa catalyst kwa Kapombe, na timu ya taifa akarudi. Kule kwa Zimbwe kazi ipo. Akicheza yeyote hakuna tatizo. Ikiwa jioni, ikawa asubuhi siku ya nne.
Mo akamleta Mavambo na Okejepha, wakatawale kiungo. Dimba la juu na la chini likawekwa himayani kwao, kisha akawaongezea Kagoma, Akamwambia, nenda katukumbushe kile kiungo cha Kotei.
Mzamiru akaambiwa, atulie awape wenzake uzoefu, Ngoma akapewa jukumu la kuwa nahodha msaidizi, akaambiwa apige pasi elekezi, na urefu wake akasaidie kufunga mipira ya adhabu na kona.
Nao wakatingisha kichwa kuonesha wameelewa maelekezo, wakaenda kuitenda kazi kama walivyoagizwa.
Ikawa jioni, ikawa asubuhi siku ya tano.
Mo akamleta Barua, Chasambi na Mutale, Ahoua na Awesu. Wakaongeza machachali pembeni ya uwanja na katikati. Magoli yakapatikana. Ikiwa anaelekea kupumzika akawaletea Fadlu kuwa Mwalimu.
Fadlu akasema 'timu inajengwa' sio ya 'kuchukua ubingwa'. Watu wakawa hawamuelewi kwa kauli zake maana timu inayojengwa ndiyo ikaongoza msimamo wa ligi.
Timu inayojengwa inapata matokeo kwenye mashindano ya kimataifa. Ikaacha maswali , Ikiwa timu bado inajengwa ndio matokeo haya? Je! baada ya ujenzi itakuwaje?
Ikawa jioni, Ikawa asubuhi siku ya sita.
Siku ya Saba Mo akiwa amepumzika. Ndipo akakutana na andiko, Je ni nani atakayeacha kondoo wake asinywe maji siku ya sabato?
Mo akainuka na kumuuliza Fadlu, Mwalimu nikuongezee nani? Fadlu akasema sio vyema Mukwala awe peke yake. Mo akamleta Valentino Mashaka na Ateba kuwa wasaidizi. Kisha wakamuongeza na Mpanzu.
Point tatu zinapatikana na timu inacheza. Kocha anasema bado anaijenga timu, boss anauliza nimlete nani?
Kwa maelezo ya Fadlu bado timu ipo kwenye uumbaji. Ijapokuwa timu inakusanya point 3. Baada y uumbaji. Tutegemee makubwa zaidi.
Mo akamleta Camara akasaidiane na Manula, Salim na Abel. Mo akamwambia Camara, kwa muda mrefu tulihitaji kipa anayeweza kucheza ili tuanze kujenga mashambulizi kuanzia nyuma. Camara akasimama kwenye milingoti 3.
Akaenda kuifanya kazi vyema kama alivyoagizwa. Mpira aliucheza na kudaka alidaka. Ubora mkubwa wa Diara kwa misimu kadhaa. Umepata mshindani wa kweli. Ikawa jioni, ikawa asubuhi, siku ya pili.
Mo akamuita Chemalone, akamwambia nikuletee nani? Chemalone akasema , niletee Karabou. Mo akamuongezea na Hamza. Kisha akawaambia.
Simba ni timu inayopenda kucheza mpira. Nendeni mkatuletee burudani uwanjani. Mzuie lakini pia mcheze, mburudishe washabiki na kuelimisha mabeki wengine wa Tanzania. Nao wakafanya kama walivyoagizwa. Ikawa jioni, ikiwa asubuhi siku ya tatu.
Mo akawasikiliza watanzania, washabiki wa Simba kwa wachambuzi, Kuwa Mohammed Hussein na Kapombe wamechoka, Watafutiwe mbadala. Duchu akarudishwa kundini, Kijili na Valentino Nouma wakaletwa ili kuwapumzisha wakongwe.
Ujio wa Kijili ukawa catalyst kwa Kapombe, na timu ya taifa akarudi. Kule kwa Zimbwe kazi ipo. Akicheza yeyote hakuna tatizo. Ikiwa jioni, ikawa asubuhi siku ya nne.
Mo akamleta Mavambo na Okejepha, wakatawale kiungo. Dimba la juu na la chini likawekwa himayani kwao, kisha akawaongezea Kagoma, Akamwambia, nenda katukumbushe kile kiungo cha Kotei.
Mzamiru akaambiwa, atulie awape wenzake uzoefu, Ngoma akapewa jukumu la kuwa nahodha msaidizi, akaambiwa apige pasi elekezi, na urefu wake akasaidie kufunga mipira ya adhabu na kona.
Nao wakatingisha kichwa kuonesha wameelewa maelekezo, wakaenda kuitenda kazi kama walivyoagizwa.
Ikawa jioni, ikawa asubuhi siku ya tano.
Mo akamleta Barua, Chasambi na Mutale, Ahoua na Awesu. Wakaongeza machachali pembeni ya uwanja na katikati. Magoli yakapatikana. Ikiwa anaelekea kupumzika akawaletea Fadlu kuwa Mwalimu.
Fadlu akasema 'timu inajengwa' sio ya 'kuchukua ubingwa'. Watu wakawa hawamuelewi kwa kauli zake maana timu inayojengwa ndiyo ikaongoza msimamo wa ligi.
Timu inayojengwa inapata matokeo kwenye mashindano ya kimataifa. Ikaacha maswali , Ikiwa timu bado inajengwa ndio matokeo haya? Je! baada ya ujenzi itakuwaje?
Ikawa jioni, Ikawa asubuhi siku ya sita.
Siku ya Saba Mo akiwa amepumzika. Ndipo akakutana na andiko, Je ni nani atakayeacha kondoo wake asinywe maji siku ya sabato?
Mo akainuka na kumuuliza Fadlu, Mwalimu nikuongezee nani? Fadlu akasema sio vyema Mukwala awe peke yake. Mo akamleta Valentino Mashaka na Ateba kuwa wasaidizi. Kisha wakamuongeza na Mpanzu.
Point tatu zinapatikana na timu inacheza. Kocha anasema bado anaijenga timu, boss anauliza nimlete nani?
Kwa maelezo ya Fadlu bado timu ipo kwenye uumbaji. Ijapokuwa timu inakusanya point 3. Baada y uumbaji. Tutegemee makubwa zaidi.