Hakika sikio la kufa halisikii dawa,
Tanzania bado ni kichwa cha mwendawazimu.Ukweli ulio wazo viwango vya Makocha wetu wazawa ni mdogo sana kwani January mpaka Desemba tupo nao hapa hapa hawajatoka kusema wamekwenda kupata Mafunzo na mbinu mbalimbali za mpira nje ya nchi kwenye Vyuo mbalimbali.
Vilabu vyetu vimekuwa vinashiriki kwenye mashindano ya kimataifa na vilabu vyenye uwezo mkubwa wa kuajiri Makocha wenye uwezo mkubwa matokeo yake ni kutolewa mapema. Nashauri viongozi wa vilabu vyetu kuwa hawa Makocha wazawa hawawezi kutuvusha Kimataifa tafuteni Makocha wenye ujuzi na elimu ya mpira.