Simba na Yanga hazitegemei makocha kushinda mechi ndio maana hata leo Fahdu anaweza kufukuzwa na timu ikashinda

Mwishokambi

JF-Expert Member
Joined
Nov 23, 2020
Posts
390
Reaction score
1,425
Kusema kuwa Gusa Achia Twende Kwao imeiva kiasi kwamba kila anayekanyaga anakula 4 au 5 sio kweli, uongo, uongo, uongo.

Kitendo cha jamaa kuhamia KMC na kujifanya wanafanya mazoezi maana yake yale mambo waliyokuwa wakoyafanya pale Chamazi yamehamia kule Kinondoni.

Simba watapata wakati mgumu sana raundi ya pili kwenye uwanja huo kama watakosa wataalamu wazuri wa kudetect ndumba za jangwani.

siku hizi wamehamia kabisa pale Kinondoni kufanya mazoezi, sio kwa bahati mbaya, Gusa achia twende kwao imechanganyika na uswahili na wala sio ufundi wa kocha.

Raundi ya 2 watashinda mechi zote pamoja na kutufunga sisi Simba, believe me or not
 
Majungu FC!
 
Mbona mnaanza kutoka kwenye mashimo yenu mapema sana? Moto wa petroli imeanza kuwachoma uko mliko na bado mpaka mtaimba mapambio ya kusifu na kuabudu!
 
🤣Twende pamoja Camara kadaka mech zoote aumie leo utaona pengo ....


Namba 7-Yanga vs Simba-Max vS Mutale
Sub:Mzize vs Chasambi

No 11-Pacome Vs Kibu
Sub:Farid Vs Mpanzu

No 10:Aziz ki vs Ahou
Sub:Chama vs Awesu awesu

Najarib kutengeneza kikosi uchwara nikufikirishe tuachane na mambo ya nyuma ya pazia kwa NBC yanga kamzidi Simba vitu vingi asee bila ushabiki ..Simba anasema kafungwa goli chache ambazo ni 5 katika mech 3 ,yanga kafungwa goli 6 katika mech 3 hizo hizo....Simba bado sana sana asee
 
Hakuna uchawi ni mbinu tu inatumika,Yanga wana mpira wa speed kubwa na pass nyingi hazipotei wana ball control,ukiwaiga wanakutandika vizuri. Mechi yao na Al Hilal ya Sudan walikuja kwa speed hivo hivo wakawa hawapenyi maana majamaa hawana presha na hawabadili mfumo wao wa kucheza mwisho wa siku counter 2 magoli mawili ,hao ukiwaachia wacheze mpira wanachoka.
 
Usiitaje Yanga kwenye ujinga kama huu, bado German machine anajitafuta akifungulia booster ni nane nane
 
Yaani unempangia kocha kikosi cha kwanza ili upate cha kukosoa? Eti Mutale anaanza na Mpanzu anaanzia benchi. Utaona vipi pengo la Camara wakati kuna kipa namba moja wa timu ya taifa ya Tanzania Manula yuko benchi? Kwa kuwa kuna pengo la Diarra unataka kubalance mzani.

Simba ilipoanza msimu tulisema wachezaji wakijiamini timu imepatikana. Wachezaji sasa wanajiamini hasa baada ya kushinda mechi ngumu ngumu na kupata matokeo katika mazingira magumu, ambacho bado kinajengwa ni chemistry kuanzia kati hadi mbele. Siyo kiwango, ni maelewano kati ya wachezaji na kucheza kitimu. Hili linachukua muda ila linakuja taratibu.

Hakuna pia asiyejua kuwa wachezaji wa Yanga wana experience zaidi ila hiyo haiondoi ubora wa wachezaji wa Simba. Experience inakuja na muda.
 
Nimekupa challenge Tu maana angalia mfano farid Vs mpanzu ataanza mpanzu Tu...Manula ni huyu aliekula 5,inshu sio experience Tu pia exercises za kutafuta hio experience ni muhimu ndio mana timu karibia zote duniani zinazosumbua akiumia flani unajipangia kikosi ww mwenyewe au niseme mchezaji Fulani kachoka flani akiingia chaap kikosi kinatiki tukiangalia Simba kapombe Tu akiumia Kijiri bado kama vile anaingia Leo .....au tuseme mpanzu akichoka nan upande wake ataleta ladha inayokaribiana nae Mutale???,Chasambi????....
 
Hakuna timu, au niseme ni timu chache sana zinatokeaga ambazo mchezaji aliye first 11 na aliye benchi wote wanalingana uwezo. Acheni kudanganyana. Ingekuwa hivyo wachezaji wangekuwa wanalipwa mishahara sawa. Hao kina Kibabage hamtaki hata kuwasikia. Mzize mwenyewe mlishamkataa. Musonda naye mnampendaga kwa vipindi. Captain wenu hamumuamini. Hakuna asiyejua Yanga bila Bacca na Aucho hamna timu.

Hakuna challenge yoyote ya maana uliyotoa hapo. Kwa hiyo Manula kula 5 mechi moja maana yake nini? Diarra kafungwa magoli mangapi msimu huu tu hadi mkaamua kumpumzisha. Mkamjaribu yule mwingine mkaona majanga. Umetafuta mifano ya kusapoti hoja yako lakini ukweli unaujua. Yanga haina benchi lolote la kutosha. Huyo Farid kacheza mechi ngapi, si alikuwa anaozea benchi?
 

Management iliyopo umeidharau sana,ubora wake hujauona hata kidogo,wachezaji wanavyoandaliwa pia hujaona.


Unamaanisha ndumba bila management bora inafua dafu?


Be positive
 
Eti unautaka ubingwa unaongoza kwa pointi moja dhidi ya Yanga.

Hii point moja mtaitapika mtake msitake na siku hiyo mtawata GSM, bahasha, Kayoko, tunahamia Burundi..
 
Huu nao ni ushabiki tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…