Simba na Yanga huwa wanapataje faida?

Simba na Yanga huwa wanapataje faida?

uzio usio onekana

JF-Expert Member
Joined
Apr 21, 2019
Posts
836
Reaction score
2,658
Mimi sio shabiki wa hizi timu ila nikiziangalia kiundani ni kama zimekaa kisiasa sana. Na huwa najiuliza hizi timu mbili ni kama zinatumia pesa nyingi sana kuliko pesa wanayo ingiza nikijaribu kuwauliza wadau wanasema chanzo cha Mapato ya jezi na matangazo.

Lakini naona bado hela wanazozitumia ni nyingi kuliko Mapato.
 
MBet wanaipa Simba Bilioni 26 KWA miaka 5. Ni kama 5B KWA mwaka. Hai ni MBet tu
 
Mshahara wa chama wa Mayele kwa mwaka unaweza kuta ni zaid ya million 150. Huyo ni mchezaji mmoja tu bado wengine, bado gharama za hotels bado matibabu bado nauli za ndege na mambo mengine halaf mwisho wa siku kombe sina uhakika thamani yake kama zawad ila sidhan kama linafika 500M ..Viingilio getin kwa hiz timu kubwa za Dar kwa mechi 1 sina uhakika kama inazid milion 50 (tofaut na mech za derby). Hapa ndio kwel lazima ujiukize, how do they cover these expenses (weka mbali masuala ya kutengeneza profit).?
 
MBet wanaipa Simba Bilioni 26 KWA miaka 5. Ni kama 5B KWA mwaka. Hai ni MBet tu
Kama kwa MBet kwa mwaka anailipa simba billion 5 ina maana kwa siku simba wanalipwa million 13.5 lakini ukipiga hesabu Hela nado haitoshi kwa sababu kocha tu mshahara wake kwa siku tu ni kama million 4 hapo bado wachezaji mishahara yao na timu bado haijasafiri.
 
MBet wao wanapata faida gani ? Maana hata wasingeweka nembo zao kwenye jez za simba sion kama kungekua na tatizo lolote katika biashara zao, au hii ni namna tu ya ku channel pesa ionekane kama income halali?

Matangazo na mileage kuna watu wameijua au wamevutiwa na mbet kupitia Simba
 
MBet wao wanapata faida gani ? Maana hata wasingeweka nembo zao kwenye jez za simba sion kama kungekua na tatizo lolote katika biashara zao, au hii ni namna tu ya ku channel pesa ionekane kama income halali?
Watu wanalipwa kwenye kamali. MBet anataka awe maarufu Watu wabet kupitia MBet waliwe
 
Watu wanalipwa kwenye kamali. MBet anataka awe maarufu Watu wabet kupitia MBet waliwe
5B KWA mwaka ni kama 14 milioni kea siku. Hiyo hela ni ndogo sana kwa siku kwa kampuni la kamari. Anawezaliwa mtu mmoja tu hiyo. Kamari sio poa. Mtu alipwa 1M. Siku hiyo hiyo 800,000 inaliwa.
 
Mapato wanayopata yanaishia kwenye matumizi .. kuhusu faida wanufaika wakuu ni wafadhili, wadhamini na mashabiki huku timu inapata sifa kuwa ni tajiri lakini kwenye mkoba kunasoma Tsh. 354.43
 
Watu wanalipwa kwenye kamali. MBet anataka awe maarufu Watu wabet kupitia MBet waliwe
Je unajua matumizi ya simba kwa siku makadidilio inaweza sio chini ya million 50
Lakini hao MBet kwa siku wanaipatia simba million 13.5 sasa hiyo hela nyingine ya kujazia hapo juu wanaipata wapi?
 
5B KWA mwaka ni kama 14 milioni kea siku. Hiyo hela ni ndogo sana kwa siku kwa kampuni la kamari. Anawezaliwa mtu mmoja tu hiyo. Kamari sio poa. Mtu alipwa 1M. Siku hiyo hiyo 800,000 inaliwa.
Na kabla MBet haijaja hao simba walikuwa wanaishije na vip kuhusu yanga ukiachana na hizi timu za mikoani
 
MBet wao wanapata faida gani ? Maana hata wasingeweka nembo zao kwenye jez za simba sion kama kungekua na tatizo lolote katika biashara zao, au hii ni namna tu ya ku channel pesa ionekane kama income halali?
Ana pata spotlight. Mfano kwanza inakuwa rahisi kwa Mbet kufanya kampeni kwa uwepo tu wa jina la Simba wengi atawafikia na wengi watashiriki hivyo basi ataongeza wateja wa wapya kupitia simba. Mfano michuano ya AFL atapata pia spotlight kutoka mataifa ya nje hivyo hivyo anatanua zaidi brand yake kupitia jina la simba
 
Mimi sio shabiki wa hizi timu ila nikiziangalia kiundani ni kama zimekaa kisiasa sana. Na huwa najiuliza hizi timu mbili ni kama zinatumia pesa nyingi sana kuliko pesa wanayo ingiza nikijaribu kuwauliza wadau wanasema chanzo cha Mapato ya jezi na matangazo.

Lakini naona bado hela wanazozitumia ni nyingi kuliko Mapato.
Ni kweli ila kwa hii miaka ya karibuni, kuna unafuu katika matumizi kuliko miaka ya nyuma kwa vile wadhamini hawakuwepo wengi tofauti na sasa na pia thamani ya hivi vilabu viwili ni vikubwa kwa sasa.

Mapato yanayoweza kupatikana ni kama Gate collection, wadhamini, kadi za wanachama, haki za matangazo, michuano mbalimbali (ligi kuu+kombe la ligi, klabu bingwa/shirikisho), mauzo ya wachezaji, mauzo yenye nembo ya klabu (merchandise-jezi, kofia, skafu, etc), mauzo ya kidijitali(club youtube channels + apps)

Matumizi yanaweza kuwa mishahara, usajili, malazi, usafiri
Kikubwa ni klabu wawe wabunifu hili wakuze fans engagement ndio hela na itawavutia zaidi wawekezaji. Kwa hiyo pesa ipo tena nyingi sana kwa hivi vilabu viwili tofauti na miaka ya nyuma na sisi mashabiki ndio mtaji wao
 
MBet wao wanapata faida gani ? Maana hata wasingeweka nembo zao kwenye jez za simba sion kama kungekua na tatizo lolote katika biashara zao, au hii ni namna tu ya ku channel pesa ionekane kama income halali?
unaposikia biashara matangazo ndio maana yake hyo.
Kutangaza bidhaa zako.
usipotangaza hauwezi kupata wateja.azam na camera zake anapommulika chama pale kifuani kuna maandishi yanaonekana.yule asiyejua akiona atataka kujua nini.mwisho wa siku na yeye anaanza kumchangia mzungu ada za watoto wake
 
Mimi sio shabiki wa hizi timu ila nikiziangalia kiundani ni kama zimekaa kisiasa sana. Na huwa najiuliza hizi timu mbili ni kama zinatumia pesa nyingi sana kuliko pesa wanayo ingiza nikijaribu kuwauliza wadau wanasema chanzo cha Mapato ya jezi na matangazo.

Lakini naona bado hela wanazozitumia ni nyingi kuliko Mapato.
Ukianza kuangalia ivo bas dunian kote vilabu kama Madrid au bayern nao wanatoaa sana ela lakin kama unakumbuka rais wa yanga alipokuwa anatoa ripot ya msimu ulopita yanga ilipataa faida zaid ya million 500 kwaiyo utaangalia apoo vilabu ivi vipnapata sana elaa kusingekuwa na elaa wasingekuwa wanagombanag kweny mauchaguz
 
Hizo timu hazina hasara ni faida tu ,ila huwezi kuziona hizo faida ukiwa nje .
 
Ni kweli ila kwa hii miaka ya karibuni, kuna unafuu katika matumizi kuliko miaka ya nyuma kwa vile wadhamini hawakuwepo wengi tofauti na sasa na pia thamani ya hivi vilabu viwili ni vikubwa kwa sasa.

Mapato yanayoweza kupatikana ni kama Gate collection, wadhamini, kadi za wanachama, haki za matangazo, michuano mbalimbali (ligi kuu+kombe la ligi, klabu bingwa/shirikisho), mauzo ya wachezaji, mauzo yenye nembo ya klabu (merchandise-jezi, kofia, skafu, etc), mauzo ya kidijitali(club youtube channels + apps)

Matumizi yanaweza kuwa mishahara, usajili, malazi, usafiri
Kikubwa ni klabu wawe wabunifu hili wakuze fans engagement ndio hela na itawavutia zaidi wawekezaji. Kwa hiyo pesa ipo tena nyingi sana kwa hivi vilabu viwili tofauti na miaka ya nyuma na sisi mashabiki ndio mtaji wao

Umemaliza yote mkuu.
Unafanana sana na GJ.

Hadi Maandiko.
 
Mshahara wa chama wa Mayele kwa mwaka unaweza kuta ni zaid ya million 150. Huyo ni mchezaji mmoja tu bado wengine, bado gharama za hotels bado matibabu bado nauli za ndege na mambo mengine halaf mwisho wa siku kombe sina uhakika thamani yake kama zawad ila sidhan kama linafika 500M ..Viingilio getin kwa hiz timu kubwa za Dar kwa mechi 1 sina uhakika kama inazid milion 50 (tofaut na mech za derby). Hapa ndio kwel lazima ujiukize, how do they cover these expenses (weka mbali masuala ya kutengeneza profit).?
Kapitie taarifa ya mapato na matumizi ya hizi club.


Kwa taarifa yako mwaka wa fedha 2022/23 yanga ilipata faida.

Sent from my Pixel 5 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom