Simba na Yanga wanakwama wapi?

kasuhe

New Member
Joined
Jul 21, 2019
Posts
1
Reaction score
0
Nimewaza sana kuhusu vilabu vyetu vya tanzania ila jibu sijapata bado. Ukiafuatilia vizuri soka la Tanzania mara nyingi hakuna luxury kbsa zaidi tu mashabiki wanalaumu wachezaji au kocha wa kilabu husika.

Hivi natuna watanzania ambao wanaoweza kucheza mpira vizur au usajili wetu unakwama wapi mbona tukiwa away tunaonekana kama kituko wachezaji wanapoteana hadi tunaomba mechi iishe.

Naomba tujadili wana jamii tunakwama wapi?
 
sema hivi: timu yenu vyura fc wanakwama wapi. Wenzenu simba tulishalijua hillo muda mrefu sana. Sshv tumeanza kupiga hatua na ndo maana simba ikicheza inavutia wengi hata majirani wanapenda kuangalia match za Simba
 
Hamsa hamsa mnazokula ugenini..timu inacheza kama under 15...hivi mikia mmewahi kupata goli dk 90 Misri
 
sema hivi: timu yenu vyura fc wanakwama wapi. Wenzenu simba tulishalijua hillo muda mrefu sana. Sshv tumeanza kupiga hatua na ndo maana simba ikicheza inavutia wengi hata majirani wanapenda kuangalia match za Simba
Hahaha wa matopeni bana Kama ile mlo cheze na ud songo ilinivutia kweli kweli
 
sema hivi: timu yenu vyura fc wanakwama wapi. Wenzenu simba tulishalijua hillo muda mrefu sana. Sshv tumeanza kupiga hatua na ndo maana simba ikicheza inavutia wengi hata majirani wanapenda kuangalia match za Simba

Mmmmmh...jibu lako ndilo moja ya matatizo makubwa ya soka ya Tanzania...Mashabiki wa Simba na Yanga hawajitambui, wamejaa mipasho, majivuno, kupamba timu zao kwa sifa zisizostahili na ambazo kiukweli hazipo...Sifa peke waliyo nayo mashabiki wa Tanzania ni kwamba ni kweli wanapenda soka lakini hawaelewi chochote zaidi ya hapo...Kila kukicha kujisifu tu kwa misifa hewa...Simba imepiga hatua gani mpaka sasa? Hilo la kufika robo fainali kwenye michuano ya CAF?? Yanga pia iliwahi kufikia hapo kitambo...Simba na Yanga zina matatizo makubwa yanayofanana...Kwa sasa wanaSimba, baadhi yao, wanadhani wao timu yao ni tajiri jambo ambalo siyo kweli...Hata Yanga nao wakati wakiwa na Manji walidhani Yanga ni tajiri, na alipoondoka Manji ndipo wakajua kuwa kumbe timu haina utajiri wowote...Simba na Yanga zina matatizo yanayofanana...Magazeti ya Tanzania nayo yanachangia kutoa sifa za uongo kwa ajili ya kujipatia fedha kutokana na mauzo ya magazeti...siku hizi magazeti karibu yote ya michezo utayaona yakiwa na maandishi makubwa yakiwa na rangi za njano, kijani na nyekundu ambazo ni rangi za klabu hizi mbili...Yote hii ni kuvutia wasomaji wa Simba na Yanga...mara utasoma hakuna kama Shiboub, mara Sibomana ndiyo kiboko yao....Ni sifa za kitoto kabisa...Wanachama nao hawana jipya kabisa...wengi wao wanataka klabu iwasaidie wao...Yanga wana kitu kinaitwa task force lakini wasipopewa fedha wanakuja juu...Simmba nao wako sijui na mtandao wa ushindi... Yanga au Simba ziikisafiri mikoani timu zinapokelewa na maandammano ya wanachama yasiyo na tija...kwenye hoteli walizofikia wachezaji wanachama na wapenzi wa timu hizo kwa mamia kama siyo maelfu nao utawakuta hapo na kuwanyima wachezaji mmuda wa kupumzika...Simba kwa misimu ni kweli wanafanya vizuri lakini Yanga nao wanajipanga na watakuja kuifunga Simba na kama siyo msimu huu basi msimu ujao...Kutamba kwa Simba hakuwezi kudumu zaidi ya miaka mitatu na wala haitafika miaka kumi kama alivyowahi kudai mropokaji mmoja...Soka ya Tanzania ina matatizo makubwa...rushwa, wizi, sifa za uongo, hujuma, majungu, imani za uchawi ndivyo vinavyotawala
 
Hahaha wa matopeni bana Kama ile mlo cheze na ud songo ilinivutia kweli kweli
Nyie vyura hamjui style ya mpira kucheza ugenini,(subiri kitakachowakuta huko kwa makilikili) wengi wanadhani simba ilicheza chini ya kiwango kule msumbiji hakika mnajidaganya, dhamira ya simba kutoa draw ilifanikiwa kwa kiwango kikubwa: angalia TP mazembe, Ismail na Al ahal za mistri zikija bongo tunazigeuzageuza kama samaki wa kuokwa wanaonekana kucheza kawaida lkn lengo ni kutaka lango lisiguswe ili watoe draw halafu ukienda kwao chamoto utakiona.(kama itakavyokuwa kwa u do songo). hiyo ndo style ya kucheza ugenini ambazo hufanywa na timu zinazojitambua na zenye malengo kama simba.. mgekuwa vyura mgejitutumua kutaka kufunga bila kutumia akili at the end mgefuliwa malinda
.
 
Kati ya simba na Yanga iliyoshinda mechi za ugenini ni nyingi au hata droo ni ipi?
Au na saizi mnadhani mtaenda fifa kama miaka ile?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…