Kwanza niwahongere wana Simba kwa kutupa raha! Wachezaji na wapenzi wa Simba mmefanya wandaz!
Sipati picha kama leo tungefungwa 5 tena! Sijui tungelalaje leo, maana vyura majike wangepiga makelele ya kuita machura dume mpaka tungeomba poo!!
Naomba, Jumamos pale kwa Mchina tumuadhibu huyu mtani asiye na adabu walau goli nne akajifie na kiu jangwani!! Simba mkacheze mpira wa kuua mtu! Full ufundi, magoli na kukomoa hawa Ndala FC aka Yeboyebo!!
Dawa ya mtoto asiye na adabu ni kumchakaza bakora za kutosha!!!
Viva Simba, viva wanasimba! Viva mfalme wa nyika!!
mwiny zahera analalamikia washabiki wa yanga hawataki kuchangia ila wamekuwa msitari wa mbele kulipia mechi za simba ingawa ukweli kinachowavuta mashabiki wa vyura ni maufundi ya wachezaji wa simba kina Okwi, Chama na wengineo