adden
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 7,033
- 15,638
Simba ndiyo mnyama mkubwa kuliko wote katika jamii ya paka. Simba hupatikana Afrika na Asia, idadi yao ikitizamiwa kufikia 23000(elfu 23), huku Tanzania ikiongoza kwa kuwa na idadi ya zaidi kuliko nchi zote. Simba wako katika hatua ya kutoweka (vulnurable).
Ndiye mnyama pekee jamii ya paka anaeishi kifamilia, hii inapelekea kuwa ndiye mnyama anayeweza kufanikiwa zaidi kulingana na umoja wao. Kufanikiwa huku ni pamoja na mawindo yao au ulinzi kwa familia kiujumla.
Simba dume wakifika miaka 3 hufukuzwa na baba zake ili wakajitafutie maisha yao, sababu nyingine wasipate muda wa kutoka na dada zao au shangazi zao, pia wasije kupindua nyumba na kurithi utajiri wa familia.
Simba akishafukuzwa kwenye familia huunda genge lao (coalition), iwe ni ndugu au rafiki atakayekutana naye huko porini. Baada ya hapo huwinda pamoja na wakikuta familia ina simba dume dhaifu basi humpiga au kumuua kisha kuirithi ile familia, na wakati mwingine wakikosa hurudi alipotoka kwa baba yake kumfanyia uharamia huo!
Wakisharithi wanaanza kufagia kizazi cha dume aliepita, kama mtoto ana chini ya mwaka 1 huua. Sababu hii hufanya jike aache kunyonyesha na kuingia kwenye kipindi cha hedhi (heat), sababu nyingine ya kuua ni kutaka kuwe na kizazi chake tu, siyo watoto wa baba mwingine.
Kufanya mapenzi kwa binadam au jamii ya nyani kunaweza kuwa ni starehe sana. Lakini kwa simba ni mateso makubwa sana. Baada ya jike kuingia kipindi cha kupata mimba, basi wale madume au dume hujitenga na familia.
Hufanya mapenzi kila baada dakika 20 kwa siku 5, ambako siku ya 3 dume huwa amechoka sana hivyo kumuachia dume mwingine amalizie siku zilobaki. Kama yuko mwenyewe itabidi apambane siku 5 ziishe. Simba jike mayai yake huchavushwa taratibu sana (low rate of fertility), hivyo kila muda wa tendo dume hutumia uume wake wenye miiba (barbed penis) ili kumpa hamu.
Sababu ya kupiga mtungo jike mmoja madume wawili ina sababu zake, hasa ili dume wote wajue mtoto atakayeezaliwa ni wao (confuse partenity). Simba hubeba mimba kwa muda wa miezi mitatu na nusu (siku 100).
Mtoto huzaliwa akiwa haoni na humtegemea mama kwa kila kitu (atricial), tofauti na nyumbu au nyati hubeba mimba zaidi ya miezi 8 na mtoto akizaliwa huweza kuona na kutembea na mama yake kwa wakati huo (precocial), sababu mtoto hukua tumboni kwa muda mrefu tofauti na paka.
Mtoto simba akifikisha mwaka 1(mmoja)mamaake anakuwa amefanya mapenz mara elfu 3.
Turudi kwa simba, baada ya wiki 4 kutoka mafichoni vitoto vya simba hupelekwa kutambulishwa kwenye familia. Ikiwa kuna simba jike mwingine ana watoto wakubwa (miezi 3 au 4), basi yule simba mzazi huacha ipite wiki 7 ndiyo hupeleka kutambulisha wale watoto.
Sababu kubwa ni kuwa simba watoto wote hunyonya kwa mama yoyote (cross milking), hii ni lazima kwa simba mtoto kunyonya kwa mama tofauti, hii huchangia ukuaji haraka.
Simba jike ndiye mwindaji sababu ni mwepesi na anaweza kujificha kirahisi. Jike wakishapata windo hawali hadi dume aje kuanza kula. Muda mwingine dume anaweza kumaliza msosi wote mama na watoto wakakosa na jike hawezi kufanya chochote sababu dume ana nguvu na ndiye mlinzi wa familia.
Ulimi wa simba ni kama msasa, kwa kulamba tuu huweza kutenganisha mfupa na nyama. Dume hula hadi kilo 8 za nyama.
Jike huishi maisha marefu kuliko dume, ambapo dume hazidi miaka 15 hufariki. Nywele za simba dume zikiwa nyeusi ndiyo anakuwa na testorone nyingi (handsome) na nywele humsaidia simba dume asiumie shingoni wakati wa mapigano.
Simba hunywa maji lakini pia kiu yake hupoozwa na damu ya windo wakati wanakula (blood meat). Dume huwa na uzito wa kg 180 huku jike akiwa na 130. Simba hukimbia (top speed) 60kph.
Ni hayo machache, kama yupo anaweza kuongezea, karibuni.
Ndiye mnyama pekee jamii ya paka anaeishi kifamilia, hii inapelekea kuwa ndiye mnyama anayeweza kufanikiwa zaidi kulingana na umoja wao. Kufanikiwa huku ni pamoja na mawindo yao au ulinzi kwa familia kiujumla.
Simba dume wakifika miaka 3 hufukuzwa na baba zake ili wakajitafutie maisha yao, sababu nyingine wasipate muda wa kutoka na dada zao au shangazi zao, pia wasije kupindua nyumba na kurithi utajiri wa familia.
Simba akishafukuzwa kwenye familia huunda genge lao (coalition), iwe ni ndugu au rafiki atakayekutana naye huko porini. Baada ya hapo huwinda pamoja na wakikuta familia ina simba dume dhaifu basi humpiga au kumuua kisha kuirithi ile familia, na wakati mwingine wakikosa hurudi alipotoka kwa baba yake kumfanyia uharamia huo!
Wakisharithi wanaanza kufagia kizazi cha dume aliepita, kama mtoto ana chini ya mwaka 1 huua. Sababu hii hufanya jike aache kunyonyesha na kuingia kwenye kipindi cha hedhi (heat), sababu nyingine ya kuua ni kutaka kuwe na kizazi chake tu, siyo watoto wa baba mwingine.
Kufanya mapenzi kwa binadam au jamii ya nyani kunaweza kuwa ni starehe sana. Lakini kwa simba ni mateso makubwa sana. Baada ya jike kuingia kipindi cha kupata mimba, basi wale madume au dume hujitenga na familia.
Hufanya mapenzi kila baada dakika 20 kwa siku 5, ambako siku ya 3 dume huwa amechoka sana hivyo kumuachia dume mwingine amalizie siku zilobaki. Kama yuko mwenyewe itabidi apambane siku 5 ziishe. Simba jike mayai yake huchavushwa taratibu sana (low rate of fertility), hivyo kila muda wa tendo dume hutumia uume wake wenye miiba (barbed penis) ili kumpa hamu.
Sababu ya kupiga mtungo jike mmoja madume wawili ina sababu zake, hasa ili dume wote wajue mtoto atakayeezaliwa ni wao (confuse partenity). Simba hubeba mimba kwa muda wa miezi mitatu na nusu (siku 100).
Mtoto huzaliwa akiwa haoni na humtegemea mama kwa kila kitu (atricial), tofauti na nyumbu au nyati hubeba mimba zaidi ya miezi 8 na mtoto akizaliwa huweza kuona na kutembea na mama yake kwa wakati huo (precocial), sababu mtoto hukua tumboni kwa muda mrefu tofauti na paka.
Mtoto simba akifikisha mwaka 1(mmoja)mamaake anakuwa amefanya mapenz mara elfu 3.
Turudi kwa simba, baada ya wiki 4 kutoka mafichoni vitoto vya simba hupelekwa kutambulishwa kwenye familia. Ikiwa kuna simba jike mwingine ana watoto wakubwa (miezi 3 au 4), basi yule simba mzazi huacha ipite wiki 7 ndiyo hupeleka kutambulisha wale watoto.
Sababu kubwa ni kuwa simba watoto wote hunyonya kwa mama yoyote (cross milking), hii ni lazima kwa simba mtoto kunyonya kwa mama tofauti, hii huchangia ukuaji haraka.
Simba jike ndiye mwindaji sababu ni mwepesi na anaweza kujificha kirahisi. Jike wakishapata windo hawali hadi dume aje kuanza kula. Muda mwingine dume anaweza kumaliza msosi wote mama na watoto wakakosa na jike hawezi kufanya chochote sababu dume ana nguvu na ndiye mlinzi wa familia.
Ulimi wa simba ni kama msasa, kwa kulamba tuu huweza kutenganisha mfupa na nyama. Dume hula hadi kilo 8 za nyama.
Jike huishi maisha marefu kuliko dume, ambapo dume hazidi miaka 15 hufariki. Nywele za simba dume zikiwa nyeusi ndiyo anakuwa na testorone nyingi (handsome) na nywele humsaidia simba dume asiumie shingoni wakati wa mapigano.
Simba hunywa maji lakini pia kiu yake hupoozwa na damu ya windo wakati wanakula (blood meat). Dume huwa na uzito wa kg 180 huku jike akiwa na 130. Simba hukimbia (top speed) 60kph.
Ni hayo machache, kama yupo anaweza kuongezea, karibuni.