Simba sc itarudisha makombe iliyoyapoteza

Simba sc itarudisha makombe iliyoyapoteza

K2S7J3

JF-Expert Member
Joined
Apr 9, 2013
Posts
449
Reaction score
332
Wasalaam wana jf

Kwanza nianze kwa kuwapongeza wanafainali wote wa ngao ya jamii 2023 kwa kufanikiwa kucheza fainali.

Pili niwapongezea tena simba sc kwa kufanikiwa kushinda ngao ya jamii mwaka 2023 tena mbele ya mtani.

Tatu nijielekeze kwenye nada;

Nimeangalia mechi tatu za simba kwa makini na kugundua kuwa;

1. Timu hii bado inajitafuta kwenye safu ya umaliziaji japo ilishinda dhidi ya power dynamos

2. Kocha hajapata kikosi cha kwanza wala sub kitu kinacholeta changamoto kubwa katika uchezaji wa kitimu

3. Eneo pekee ambalo simba iko imara hata kabla ya muungamiko wa timu ni "backline"

4. Katika mechi hizi tatu, yaani dhidi ya dynamos, singida na yanga, sijaona golikipa wa simba akipata makashikashi.

Hivyo,

Kwa hoja za 3 na 4, ni dhahiri simba wanaukuta imara sana ambao timu zinazosemekana kuwa ni timu bora zimeshindwa sio tu kushinda dhidi ya simba bali hata kumsumbua kipa kwa michomo kwani mashambulizi yote yamemezwa na ukuta imara unaosemekana kuwa wa yeriko.

Kwahyo;

Kwa kuzingatia principle ya "safu bora ya ushambuliaji huleta ushindi na safu bora ya ulinzi huleta ubingwa, naitabiria simba kurejesha mataji iliyoyapoteza kwaisimu miwili iliyopita.

Ndimi mdau wa moira (sio mchambuzi)
 
Baada ya kunyakua ngao ya Jamii kwa kuifunga Yanga kwa mikwaju ya penati 3 kwa 1 sasa wana kitu kabatini.

Mwanzo nzuri pamoja na kuzidiwa kwa procession kwa 54% dhidi ya 46%.
 
Simba Ina shida Sana Katikati ya Uwanja.

HASA kwenye KIUNGO Cha chini
Wangekuwa na Aina ya kiungo kama Bangala wangecheza Fainali 3 MSIMU Huu.

Mzamiru na Kanute ni CDM.
1. HAWAWEZI KUCHUKUA timu.
2. WANAPOTEZA mno MIPIRA
3. HAWAWEZI passing.
4. Wanakuwa off position
5. Technicality Yao IPO CHINI sana.


Wamsacrifice mchezaji mmoja.
Phili, kramo au Moquesson kwa MKOPO watafute kiungo WA MAANA WA kucheza na NGOMA.
 
Back
Top Bottom