Simba SC kuondoka nchini Jumatano kwenda Algeria kwa mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya CS Constantine

Simba SC kuondoka nchini Jumatano kwenda Algeria kwa mechi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya CS Constantine

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Kikosi cha timu ya Simba SC kinatarajiwa kuondoka nchini Jumatano alfajiri (Disemba 4) kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wao wa pili wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika. Akizungumza kuhusu safari hiyo, Afisa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba SC, Ahmed Ally, amesema kuwa wachezaji na viongozi wa timu hiyo wataelekea Algeria kwa ajili ya kukutana na wapinzani wao, CS Constantine, katika mechi ya kuwania hatua ya juu ya mashindano hayo.

Simba SC inajiandaa kwa mchezo muhimu ambapo wanatarajiwa kupigania pointi tatu muhimu dhidi ya timu ya CS Constantine, wakilenga kuimarisha nafasi yao katika kundi A la Kombe la Shirikisho Afrika.
 
Kuondoka Jumatano,Sasa walishindwa nn kucheza mechi ya ligi na Singida Black star,hizi siku tatu? Kweli ligi ya bongo safari bado ndefu kufikia level ya ligi zenye akili,japokuwa hujidanganya ni ligi ya 6 kwa ubora Afrika
 
Hawa CS Constantine ni ndugu zetu kabisa. Mashabiki wa soka safi la Afrika Kaskazini tukutane jukwaa kubwa.
 
Baada ya kupitia furaha ya muda mfupi, sasa ni wakati wa kusikilizia maumivu.
 
Kuondoka Jumatano,Sasa walishindwa nn kucheza mechi ya ligi na Singida Black star,hizi siku tatu? Kweli ligi ya bongo safari bado ndefu kufikia level ya ligi zenye akili,japokuwa hujidanganya ni ligi ya 6 kwa ubora Afrika
Wangeumizwa. Si unaona Dickson Job ameumia kule Ruangwa?
 
Kikosi cha timu ya Simba SC kinatarajiwa kuondoka nchini Jumatano alfajiri (Disemba 4) kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wao wa pili wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika. Akizungumza kuhusu safari hiyo, Afisa Habari na Mawasiliano wa klabu ya Simba SC, Ahmed Ally, amesema kuwa wachezaji na viongozi wa timu hiyo wataelekea Algeria kwa ajili ya kukutana na wapinzani wao, CS Constantine, katika mechi ya kuwania hatua ya juu ya mashindano hayo.

Simba SC inajiandaa kwa mchezo muhimu ambapo wanatarajiwa kupigania pointi tatu muhimu dhidi ya timu ya CS Constantine, wakilenga kuimarisha nafasi yao katika kundi A la Kombe la Shirikisho Afrika.
ff8b8b68-d20d-4ffe-a2f1-f50e16f1ff97.jpeg
 
Back
Top Bottom