Simba SC kwanini haijasajili Mshambuliaji mpaka sasa?

Si yupo Mshambuliaji wa kimataifa MUGALU.
Unataka nini tena.
Anashambulia na kukaba mabeki.
 
Ila Yanga wakifungwa bao la mapema huwa nawaaminia sana wataforce mpaka wasawazishe ikiwezekana na kuongeza jingine. I like that fighting spirit!
Hicho ndio kitu simba wanakosa.simba haina utulivu na mipango yakiufundi yakurekebisha makosa na kutafuta ushindi.Wao wanachojua nikujaza washambuliaji wengi mbele wakafanye gombania goli.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Si yupo Mshambuliaji wa kimataifa MUGALU.
Unataka nini tena.
Anashambulia na kukaba mabeki.
Huyo jamaa ni fundi sana, anajua kuficha mpira, anawatoka mabeki anakosa msaada kwa namba 10 wenu na winga zenu zinazo cheza kistar tu hapewi mpira sehemu sahihi.
 
Yan sijui kwann mnajipanikisha bila sababu za msingi. Gap la pointi tano kitu gan???? Daaaaah
Huu msimu umeisha tujipange kwa ujao, sioni namna ya kulipunguza hili gape la point tano.
 
Yan sijui kwann mnajipanikisha bila sababu za msingi. Gap la pointi tano kitu gan???? Daaaaah
Ishu sio gepu la Point tano.
Ishu ni namna ya uchezaji ya wachezaji wa Simba msimu huu ni kama vile wamechoka sana.
Goli linapatikana kwa taabu sana na wakati mwingine halipatikani kabisa.
Wachezaji wanashinda hata kufunga Penati.
We huoni kuna tatizo huu msimu.

Wapeni Kombe lao tu Yanga Msimu huu.
Wamejipanga vizuri sana.
 
Simba walijisahau sana. Msimu uliopita washambuliaji wao walikuwa wanapata nafasi hata zaidi ya kumi kwa mchezo mmoja wakifunga goli mbili au tatu wanaridhika kabisa na hapo utakuta mara nyingine washambuliaji wakishindwa kufunga viungo au mabeki wao walikuwa wanafunga. Kwa kuwa timu ilikuwa inapata ushindi basi wakawa hawaoni madhaifu ya washambuliaji wao kati namba tisa. Hili liliwapumbaza ndio maana dirisha kubwa na hata dogo hawakuhangaika kutafuta washambuliaji wa maana huiku waliopo wakionekana wameanza kuchoka kutokana na majeraha na umri. Yaani kwa krosi zile za akina Kapombe, Mohamed Hussein, Dilunga, Morison, Bwallya, Sakho na wengineo Simba ingekuwa na mshambuliaji namba tisa mzuri wala wasingekuwa wanapata shida kupata ushinda tena mnono hasa wanapokutana na vitimu vidogo vidogo kama Mbeya City

Mbaya zaidi watu wengi ambao wanaufahamu mpira walishaona hilo tatizo na wengine wakaenda mbali kuwatahadharisha (tena hata hapa jamvini) viongozi juu ya hatari iliyopo iwapo wasingesajili mshambuliaji mwenye uwezo zaidi ya Kagere. Mugalu na Boko. Kwa kuwa ni sikio la kufa maoni hayo yalipuuzwa kwa sababu hakuna mshambuliaji wa maana aliyesajiliwa si dirisha kubwa wala dogo. Kwa hali hii nadhani Simba kwa mwaka huu wameweka rehani ubingwa wao kwani wanapata ushindi kiduchu tena kwa taabu sana.

Hivi kweli benchi la ufundi, kamati ya usajili na viongozi hakukuwa na mtu hata mmoja ambaye aliona umuhimu wa kusajiliwa mshambuliaji namba tisa mwneye uwezo zaidi ya waliopo sasa? Au ndio Mo aligoma kutoa pesa ya usajili? Na lile wazo la kuleta wachezaji wa viungo wafanye majaribio ili wasijiliwe alilileta nani wakati timu ina viungo mpaka wa ziada na mapungufu yapo kwenye ushambuliaji? Na kazi ya "match analyst" bwana Calvin Mavuga ni kuangalia tu timu pinzani ina mapungufu gani au pia kuangalia timu yake ya Simba ina mapungufu gani na kushauri benchi la ufundi na Uongozi nafasi za kuboreshwa?

Ni mtizamo tu.
 
Ila mashabiki ni vigeu geu sana waliupenda wimbo wa Chama masikioni mwao kuliko wimbo wowote ule. Chama alivyotangazwa rasmi kurejea kwake tukaona wachambuzi wa mitandaoni walivyotengeneza vikosi vyao vya nguvu huku wakisema mpiga mabao wa Bocco na Kagere karejea ngoja waanze kufunga sasa. Kufungwa mechi moja tu malalamiko yamekuwa kila kona kwa viongozi wa Simba na kwa Pablo. Mimi nadhani kabla ya kuanza kulalamika mngejipa subira muone impact ya chama kwenye kulainisha safu ya ushambuliaji ya Simba
 
Tatizo la Simba halikuwa Kwa kiungo mchezeshaji. Chama amerejea kishabiki tu. Ni kama Ronaldo alivyorejea kishabiki Man Utd wakati tatizo la Man utd haikuwa mchezaji Kariba ya Ronaldo.
 
Ila Yanga wakifungwa bao la mapema huwa nawaaminia sana wataforce mpaka wasawazishe ikiwezekana na kuongeza jingine. I like that fighting spirit!
Tena kuna muda utajuta kuwafunga watakavyo kushambulia
 
Weakness point ya Simba...inawezekana wana share mshahara na wanaofanya maamuzi..Mugalu,Bocco,Kagere watoke wote apatikane striker mmoja
umenigusa hapo kinaumuhimu mkubwa selemani matola kufatiliwa huyu anakula kamisheni kwawachezaji hao sio bure kunakitu
 
Hata kama Chama atakuwepo hilo gap bado lipo tuseme atalipunguza kwa kuwatafunia strikers haya siku kaamka vibaya na team inahitaji matokeo kuna wakat striker huwa anabeba team akipata nafasi anaitumia ipasavyo sio hadi akose nafasi 5 aje kupata moja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…