sembo
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 4,350
- 3,451
Wanadai eti 'Uzalendo Kwanza'!!
Kwa soka lile, mipango ile, matokeo yale, kujituma kule kwa 'mapro' wetu n.k kuna Uzalendo kweli pale??
Kwangu mimi 'Simba SC Kwanza.. Mengine Baadae'. Kwanini hili??
1. Simba SC ndiyo timu pekee inayocheza soka maridadi na makini kwa sasa katika ukanda huu wa Africa mashariki na kati, pia ndiyo timu yenye wachezaji bora zaidi katika ukanda huu.
2. Wachezaji wa Simba SC wanajitoa na kujituma kwa zaidi ya 100% kwa ajili ya timu yao pendwa.
3. Katika siku za hivi karibuni, kila msimu Simba SC hatoki kapa. Mfano, msimu uliopita Simba SC alikua bingwa wa VPL, msimu huu kaanza na ngao ya hisani.. Yaani kwa kifupi lile kabati lao la kutunzia makombe ni heka heka tupu kila msimu.
4. Aina ya 'kabumbu' wanalosakata Simba SC ni wanaonana haswaa, wanazijua njia za mipira, wanacheza kwa kujiamini n.k. Kwa kifupi Barcelona ni "Simba SC ya Ulaya".
Sasa kwa mwendo huu.. Naachaje kuiweka Simba SC Kwanza halafu hayo mengine yakafuata??
NB: 21/10/2018 Simba SC atakua Taifa Stadium kupambana na timu anayoichezea Alex Kitenge, Stand United katika muendelezo wa TPL. Karibuni Taifa.
Kwa soka lile, mipango ile, matokeo yale, kujituma kule kwa 'mapro' wetu n.k kuna Uzalendo kweli pale??
Kwangu mimi 'Simba SC Kwanza.. Mengine Baadae'. Kwanini hili??
1. Simba SC ndiyo timu pekee inayocheza soka maridadi na makini kwa sasa katika ukanda huu wa Africa mashariki na kati, pia ndiyo timu yenye wachezaji bora zaidi katika ukanda huu.
2. Wachezaji wa Simba SC wanajitoa na kujituma kwa zaidi ya 100% kwa ajili ya timu yao pendwa.
3. Katika siku za hivi karibuni, kila msimu Simba SC hatoki kapa. Mfano, msimu uliopita Simba SC alikua bingwa wa VPL, msimu huu kaanza na ngao ya hisani.. Yaani kwa kifupi lile kabati lao la kutunzia makombe ni heka heka tupu kila msimu.
4. Aina ya 'kabumbu' wanalosakata Simba SC ni wanaonana haswaa, wanazijua njia za mipira, wanacheza kwa kujiamini n.k. Kwa kifupi Barcelona ni "Simba SC ya Ulaya".
Sasa kwa mwendo huu.. Naachaje kuiweka Simba SC Kwanza halafu hayo mengine yakafuata??
NB: 21/10/2018 Simba SC atakua Taifa Stadium kupambana na timu anayoichezea Alex Kitenge, Stand United katika muendelezo wa TPL. Karibuni Taifa.