Simba SC tukishinda leo nitafurahi, ila kiufundi nina wasiwasi na mazingira yake

Simba SC tukishinda leo nitafurahi, ila kiufundi nina wasiwasi na mazingira yake

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Tukishinda itakuwa ni furaha kubwa kwangu, ila kwa mazingira ya huu mchezo na mikakati fulani fulani naiona ni mechi ngumu kwa Simba SC, hadi kuhisi kuwa tunaweza kutoka sare, suluhu au hata kufungwa pia na Dodoma Jiji FC kama tusipojipanga vyema ndani na nje ya uwanja.

Kwanini GENTAMYCINE nina hofu?

Dodoma Jiji FC ni Yanga B na 98% ya viongozi wake waandamizi kuanzia Mbunge na Naibu Waziri Mavunde ni wana Yanga SC lia lia kabisa.

Hivyo GENTAMYCINE najua hawa waandamizi wa Dodoma Jiji FC wenye DNA ya Yanga kwa Kushirikiana na matajiri wa GSM watawatia sana ndimu (Morali) wachezaji wa Dodoma Jiji FC ili wafike, wagongane mno na hata kutuumizia wachezaji wetu muhimu na mahiri Simba SC.

Pia kutokana na mechi kubwa ya Klabu Bingwa wikiendi ijayo na Waangola, upo uwezekano wachezaji wa Simba SC wakacheza kwa tahadhari na uwoga wa kutokuumia ili wasiikose hiyo mechi, hivyo kufanya timu ikose matokeo leo dhidi ya Dodoma Jiji FC.

Ombi,
Benchi la ufundi litulie mno leo katika kupanga kikosi cha kucheza na wahakikishe wachezaji wanaimaliza mapema hii mechi kwa kufunga magoli mengi, ili kipindi cha pili wale wachezaji muhimu na tegemeo kwa michuano mikubwa na migumu ya kimataifa, akina Phiri, Inonga, Chama, Okra na Kanoute wapumzishwe.

Tusiende na matokeo yetu leo.

Cc: SN.BARRY
 
Unaanzaje kuhofia kitimu cha juzi against timu kubwa kama simba
 
Mhhhhhh.

Niliishia kuguna.

Ila jamani muwe mnaweka Akiba ya Maneno.

Mambo ya utabiri utabiri Nje ya uwanja ni kiendeleza ma Ushirikina.
 
Unaanzaje kuhofia kitimu cha juzi against timu kubwa kama simba
Wale huwa wanacheza kuumiza wachezaji kwa maelekezo ya akina Hersi.
Tuna kumbu kumbu nzuri sana mwaka jana.
Bahati nzuri safari hii hawakuumiza mchezaji wetu
 
Wale huwa wanacheza kuumiza wachezaji kwa maelekezo ya akina Hersi.
Tuna kumbu kumbu nzuri sana mwaka jana.
Bahati nzuri safari hii hawakuumiza mchezaji wetu
Wamejaribu lkn wakakuta mziki wa Simba ni mzito na ni mkubwa, wakaishia kulambwa tatu
Mahesabu ya Simba kwa macho huyaoni na unaona kama mpira siyo mtamu lkn wao Simba wanajua wanachokifanya kumhadaa timu pinzani, we chunguza mechi zote hujui mfungaji atakuwa nani
 
Wale huwa wanacheza kuumiza wachezaji kwa maelekezo ya akina Hersi.
Tuna kumbu kumbu nzuri sana mwaka jana.
Bahati nzuri safari hii hawakuumiza mchezaji wetu
Wale huwa wanacheza kuumiza wachezaji kwa maelekezo ya akina Hersi.
Tuna kumbu kumbu nzuri sana mwaka jana.
Bahati nzuri safari hii hawakuumiza mchezaji wetu
Wale huwa wanacheza kuumiza wachezaji kwa maelekezo ya akina Hersi.
Tuna kumbu kumbu nzuri sana mwaka jana.
Bahati nzuri safari hii hawakuumiza mchezaji wetu
Kikosi cha jana tulipanga wazawa watoto wa mjini,timu nzima maproo watatu au wanne tu,chama,phiri,onyango.
 
code za mayor , sporybet , nigeria
IMG_20221108_213346_246.jpg
IMG_20221108_213357_117.jpg
 
Back
Top Bottom