Simba SC tunakwama wapi?

Sven ni kocha mzuri apewe muda, kutumia mshambuliaji mmoja ndio mpira wa kisasa huko ulaya
 
Kotei na Okwi hawakuuzwa, mikataba yao iliisha na Simba hawakuwa na uwezo wa kufikia dau.

Vv

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sven ni kocha mzuri apewe muda, kutumia mshambuliaji mmoja ndio mpira wa kisasa huko ulaya
Sio Ulaya tu hata hapa Afrika zipo timu nyingi sana zinafanikiwa na mfumo huo. Mfumo wa mshambuliaji mmoja inahitajika uwe na mshambuliaji mnyumbulifu mwenye nguvu, uwezo wa kuhama kushoto kulia katikati muda wote wa mchezo, pumzi ya kutosha, kasi sana, akili, chenga na uwezo mkubwa wa kumiliki mpira peke yake akiwa na mabeki wawili au zaidi. Kwa Simba hatuna fowadi aliyekamilika mwenye vigezo vyote hivyo na mbaya zaidi umri umeanza kuwatupa mkono Boko na Kagere. Kwa sasa aachane na huo mfumo atumie mfumo wa washambuliaji wawili ili apunguze presha kwa viungo na mabeki wake timu ipate ushindi ichukue ubingwa ili msimu ujao yeye mwenyewe asajili wachezaji kulingana na mfumo unaoutaka yeye kama bado atakuwepo. Tujiulize mabeki na viungo wakabaji wa Simba walikuwa hawa hawa wakati ligi inaanza lakini kwa nini sasa hivi wanaonekana ni wabovu; jibu ni kuwa mwanzoni mwa ligi presha kwao ilikuwa ndogo kwa sababu timu zilibaki nyuma kuwahofia Kagere na Boko. Na timu nyingi zenye washambuliaji wakali sasa hivi zinatumia mfumo wa kukaba kwa kushambulia timu pinzani muda wote wa mchezo kwa hiyo timu pinzani inakuwa kazi yake kuokoa tu mpaka inashindwa kupangilia mashambulizi zaidi ya kutegemea "counter attack"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…