mangonjoli
Senior Member
- Aug 29, 2012
- 154
- 110
Wadau wa Soka nimeangalia klabu ya Simba msimu huu nimekutana na Mapungufu ambayo yasipofanyiwa Kazi Jahazi litazama. Hapa nimejaribu kuelezea mambo saba ambayo yanaweza yakaleta maafa msimu huu.
1. Ni muda mrefu tokea Atimuliwe kocha msaidizi masoud Juma mpaka leo kocha mkuu Patrick Aussems hajatafutiwa msaidizi hili ni kosa kubwa kwa klabu kama Simba ambayo juzi tu Imeingia katika mfumo mpya wa Kisasa.
2. Tatizo lisiloisha la kipa Aishi Manula la Kufungwa Magoli ya Faulo na mashuti ya mbali asipobadilika litaigharimu sana Timu. Nakumbuka nilishawahi kumkumbusha katika page yake ya Instagram muda sana na hakuna Mabadiliko.
3. Timu kubwa kama Simba mpaka leo haina mtaalam wa kupiga Faulo au kona . wana kona zao fupi fupi ambazo hazijawahi kuwasaidia na bado wanazitumia Kiufupi Simba hata wapate faulo 50 kwenye mechi moja usitegemee maajabu. Wakati timu kubwa kama Nkana , Al Ahly , Zamalekh , Enyimba N.k wasipokuadhibu kwa Faulo watakumaliza kwa kona.
4. Simba kabla ya kufungwa Dirisha dogo walipaswa kusajili mshambuliaji mwengine wa Kimataifa atakayemsaidia John boko maana ameanza kupoteza umakini na Goli. Boko wa sasa inabidi apoteze nafasi Tatu za wazi ndio aje afunge moja . Au angalau wampe nafasi Adam Salamba baada ya kumchezesha Boko kwa dakika zote 90. Sina uhakika lakini naamini Wachezaji wanaopaswa kuongezwa ligi ya Mabingwa kama Simba watafuzu makundi iwe klabu bingwa au kombe la Shirikisho anapaswa kuwa na leseni ya Ligi kuu Tanzania ambapo Dirisha lishafungwa.
5. Mechi za Viporo Simba zitawasumbua sana. Ni kawaida Simba huwa wanashindwa kucheza mechi za Pressure kwa hili wajipange kwelikweli. Yanga akiambiwa kuna mechi Saba za Ubingwa atashinda zote hata kwa mbinde. Lakini Simba mpe mechi tatu za Ubingwa lazima moja ataharibu.
6. Simba wana tabia za kuridhika wakishapata goli mbili wanaanza Showgame na pasi ambazo hazina Tija kwa timu mwishoe wanazidiwa na kufanya mashabiki kuwa roho juu. Rejea mechi za msimu huu za African lyon, JKT Ruvu na ya juzi dhidi KMC.
7. Simba ndio timu inayotengeneza nafasi nyingi lakini magoli ni haba. Katika nafasi Tano wanaweza kupata moja. Wakati kiuhakika inatakiwa katika nafasi mbili upate moja au unaingia wavuni zote mbili . Hii ni vita!!
1. Ni muda mrefu tokea Atimuliwe kocha msaidizi masoud Juma mpaka leo kocha mkuu Patrick Aussems hajatafutiwa msaidizi hili ni kosa kubwa kwa klabu kama Simba ambayo juzi tu Imeingia katika mfumo mpya wa Kisasa.
2. Tatizo lisiloisha la kipa Aishi Manula la Kufungwa Magoli ya Faulo na mashuti ya mbali asipobadilika litaigharimu sana Timu. Nakumbuka nilishawahi kumkumbusha katika page yake ya Instagram muda sana na hakuna Mabadiliko.
3. Timu kubwa kama Simba mpaka leo haina mtaalam wa kupiga Faulo au kona . wana kona zao fupi fupi ambazo hazijawahi kuwasaidia na bado wanazitumia Kiufupi Simba hata wapate faulo 50 kwenye mechi moja usitegemee maajabu. Wakati timu kubwa kama Nkana , Al Ahly , Zamalekh , Enyimba N.k wasipokuadhibu kwa Faulo watakumaliza kwa kona.
4. Simba kabla ya kufungwa Dirisha dogo walipaswa kusajili mshambuliaji mwengine wa Kimataifa atakayemsaidia John boko maana ameanza kupoteza umakini na Goli. Boko wa sasa inabidi apoteze nafasi Tatu za wazi ndio aje afunge moja . Au angalau wampe nafasi Adam Salamba baada ya kumchezesha Boko kwa dakika zote 90. Sina uhakika lakini naamini Wachezaji wanaopaswa kuongezwa ligi ya Mabingwa kama Simba watafuzu makundi iwe klabu bingwa au kombe la Shirikisho anapaswa kuwa na leseni ya Ligi kuu Tanzania ambapo Dirisha lishafungwa.
5. Mechi za Viporo Simba zitawasumbua sana. Ni kawaida Simba huwa wanashindwa kucheza mechi za Pressure kwa hili wajipange kwelikweli. Yanga akiambiwa kuna mechi Saba za Ubingwa atashinda zote hata kwa mbinde. Lakini Simba mpe mechi tatu za Ubingwa lazima moja ataharibu.
6. Simba wana tabia za kuridhika wakishapata goli mbili wanaanza Showgame na pasi ambazo hazina Tija kwa timu mwishoe wanazidiwa na kufanya mashabiki kuwa roho juu. Rejea mechi za msimu huu za African lyon, JKT Ruvu na ya juzi dhidi KMC.
7. Simba ndio timu inayotengeneza nafasi nyingi lakini magoli ni haba. Katika nafasi Tano wanaweza kupata moja. Wakati kiuhakika inatakiwa katika nafasi mbili upate moja au unaingia wavuni zote mbili . Hii ni vita!!