Simba Sport Club: Taarifa kwa umma

Mwandiko wa Haji Manala naujua kabisa maana aliwahi kuleta barua ya maombi ya kuchumbia kwetu na mimi ndo nilikuwa msomaji wa barua ile...nina uhakika ndo yeye maana si unaona mwandiko ulivyocharangwa ...
 
kwa mtu anayejua mpira hawezi reply ujinga
taalifa imejieleza vizuri tu msilete mambo ya jerry muro humu kujifanya mmesoma sana alafu kwenye mambo ya mpira zero
 
Yote semeni lakini ni aibu ya mwaka imefanya na mashabiki wa SSC.

Barua ndefu ya kusingizia refa ni kuhalisha kitendo hicho na kuruhusu viendelee.

Pia kumtetea Nahodha kwa utovu wa nidhamu ni dhahiri uongozi wa Simba hubariki vitendo hivyo.

Uongozi uombe tu radhi na kuitisha Mkutano Mkuu kuzungumzia vitendo hivyo vya aibu.
 
viti tutalipa ..ila hii taarifa nani kaiandika? aandike jina lake basi nina wasi wasi na hili tamko.
 
Hv kwann TFF ndio inamamlaka ya kuchagua mwamuz badala ya frat?
 
Eti waziri kushangilia goli ka ovyo la mwajiri wake?kwahio nyie simba mlitaka tambwe alipofunga waziri aanze kulia badala ya kushangilia? Nyie lipeni viti kwanza bhana
 
Kisaikolojia mchezaji aliyefunga hilo.goli ataathirika sana ktk michezo ijayo, maana anajua kosa alilofanya lilivyosababisha msururu wa matukio kuanzia lile la kumdanganya refa mpaka la kufanya watu waumize vichwa kujadili bila kupata jibu
 
Labda kama tunajadili gori tulilopigwa na maamuzi ya refa sawa, lakin yawezekana si taarifa ya klabu mtu tu amejiandikia lakn hii haiwezi kuwa official, pili suala la kuvunja viti hata Mimi binafsi sijalifurahia hata kama refa hakuchezesha mpira kama inavyotakiwa kuvunja viti si solution ona sasa vilabu nimekosa mapato hii itaathir hata utendaj wa timu next time mashabiki tuwe wavumilivu
 
Nyie Simba mbona Sarungi na Kapuya walikuwa mawaziri wamichezo na ni manazi wa simba wa Serengeti watu walikaa kimya!
 
Mwigluu aache kiherehere nae ni kwl kbisa huwez kutumia rasilimali za gvt hasa hii inayobana matumizi kwa aajili ya mambo binafs maana huko yanga hata uongozi hana
Umesahau Kapuya na Sarungi?
 
Simba wahuni tu lipeni gharama za uwanja wetu wa Taifa kisha mjenge wenu Bunju muwe mnang'oa viti vyenu wenyewe, Yanga ilifungwa 5-1 na red card mbili haikung'oa kiti hata kimoja
sasa kama ilikuwa halali mlitaka kungoa kwasababu IPI...
 
hii taarifa mbona haieleweki
Watanzania hatuko makini kwa mambo mengi iwe kwa mtu mmoja mmoja, vikundi na hata viongozi wa ngazi mbalimbali.
Ni wepesi kuridhika na majibu mepesi kwa mambo mazito yanayoweza kuleta matokeo mbaya siku za baadaye. "Usipoziba ufa utajenga ukuta". Uongozi mbovu wa mpira nchini umevumiliwa vya kutosha. Mahaba kwa vilabu yanaua mpira. Rushwa ikiachiwa itawale itakuwa kaburi la soka. Waamuzi wasio weledi na wavivu viwanjani husababisha vurugu na hasara.
Baadhi ya viongozi wa tff wako pale kupigania maslahi ya timu walizo na mapenzi nazo. Hilo limedhihirishwa na maamuzi yanafanywa na mashauri mengine yanayofikishwa kwenye kamati husika hayahitimishwi. Tunaona namna viongozi walivyo bize kuandaa mazingira ya kubaki madarakani.
Tukatae mahaba yaliyopitiliza ya viongozi wa kitaifa kwa timu za mpira. Kiongozi mmoja wa kisiasa alikuwa maarufu kwa fitna. Hakuona taabu kuwafitini wapinzani kwa viwango vya mateso yenye madhara makubwa kwa binadamu.
 
Ushindi ni mtamu zaidi ukipatikana kihalali. Ukijengeka utamaduni wa kushinda vinginevyo soka la Tanzania litaenda ICU. Lengo liwe ni kukuza mpira nchini kwa ushindani viwanjani ili kupata wachezaji wazuri wa kimataifa km Samatha.
Tumesikia vurugu kubwa viwanjani zilizosababisha vifo sehemu mbalimbali duniani. Vurugu za aina hiyo mara nyingi huchochewa na waamuzi waliokosa weledi na maadili kwa ushawishi wa rushwa. Tusifike huko.
Michezo huleta umoja na amani.
 
hapana mkuu arsenal wamefunga kwa mkono sekunde ya mwisho hakuna alieng'oa kiti wakat tambwe amefunga kwa mguu.
Wasingeweza kung'oa viti kwa sababu sio vya kichina. Halafu kuna vitu vinafanana kati ya Yanga na CCM.
1. Uniforms zinafanana-Kijani na Njano
2. Wote wanapenda kushinda kwa ujanja ujanja, hasa kwa kutumia waamuzi au wasimamizi wa chaguzi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…