Theb
JF-Expert Member
- Jan 25, 2019
- 3,927
- 7,276
Nimeangalia mechi ya leo ya simba akiwa ugenini pale ushirika moshi akicheza na mwenyeji wake polisi katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara. Kiuhalisia na ukweli usiofichika simba tuna tatzo la wafungaji/wamaliziaji. Mfungaji anakimbia kabla mpira haujapigwa au anashindwa kusoma position aliyopo kabla hajapiga mpira wa mwisho. Mugalu kaokoa kama 2 hivi badala ya kufunga. Aisee kiujumla tukubaliane tu mwaka huu kikombe cha ligi kuu tuwape tu utopolo aka utopwinyo au kwa jina lingine chura/bwawani fc. Tunazidi kuweka pengo la points baina yetu na utopwinyo, leo tusije kumlalamikia muamuzi yoyote yule kwa maana makosa na kukosa hizi points 3 ni yetu simba sc wachezaji na bench la ufundi hizi lawama ni zao wala wasije kutuambia eti imepanda imeshuka. Kikosi kilikua dhaifu mno angalau walivyoingia chama, Morrison na mkude walisukuma sukuma ila tayari muda ulisha sogea saana kiasi kwamba pressure ya mchezo imefikia kuleta umakini kwa wote
Uongozi wa simba msimj ujao tunawaombeni saana tusajilieni mashine za magoli waliopo wamechoka mno.
Kocha nayeye amezingua kikosi alichopanga sio cha kushinda bali cha kukamilisha ratiba tu.
Uongozi wa simba msimj ujao tunawaombeni saana tusajilieni mashine za magoli waliopo wamechoka mno.
Kocha nayeye amezingua kikosi alichopanga sio cha kushinda bali cha kukamilisha ratiba tu.