Anafanyiwa kitu gani mbona hamsemi kuhusu mlipili?Naamkubali sana Ndemla ila anachofanyiwa sio poa kabisa
Ndemla na yeye apunguze umbumbumbu
Sent using Jamii Forums mobile app
Fact [emoji1666]Soka ni ushindani na sio huruma kama ambavyo mnataka nyinyi, ni sawa na mwanao anapata mitihani 95 lakini kuna wanaopata 100 mitihani yote unataka apewe number moja kwa huruma!!
Ukiona hapati number ujue ushindani umemzidi hata kama kiwango chake ni cha juu.Kama Wewe ni Simba kweli unataka akiingia yeye atoke nani ambae kiwango chake kiko chini kuliko Ndemla??
Sent using Jamii Forums mobile app
Fact [emoji1666]Ndemla ni mchezaji mzuri sana lakini anakosa mwendelezo. Mechi hii akicheza vizuri mechi ijayo anavurunda. Achukue mfano kwa Muzamiru Yasin yeye alionekana kama kashapotea na hana namba Simba lakini alifanya mazoezi kwa nguvu sana na akaweka malengo yake siku alipopewa nafasi na Ausems hakufanya makosa mpaka leo bado anapambana na akina Chama.Hata Sven naye ameshamuamini ila hizi mechi chache kakosekana sababu ya majeruhi. Pia ajifunze kwa mwenzake Mkude waliotoka naye timu ya vijana ya Simba jinsi alivyopambana pamoja na Simba kuleta viungo wakabaji kibao ndani ya hii miaka takribani sita lakini Mkude kakomaa mpaka leo ndio mmiliki wa dimba la kati.
Kwa Ndemla anatakiwa afanye mazoezi sana na ajiandae siku akipewa nafasi aonyeshe uwezo wake wote kwa faida ya timu nzima. Mimi ni mmojawapo wa wale wananoamini kuwa Ndemla ana kiwango kizuri lakini tatizo akipewa nafasi badala ya kuisaidia timu yeye anacheza kibinafsi ili aweze kuwaonyesha mashabiki na benchi la ufundi kuwa anaweza. Kwa mfano kwenye Mapinduzi Cup alipewa nafasi alitakiwa aonyeshe namna ya kuisaidia timu lakini alishindwa kabisa ilifika mahali hata yupo mita 45 anataka apige afunge mwenyewe. Kwa Simba ya sasa hivi ukipata nafasi itumie kuisaidia timu ipate ushindi lakini ukitumia nafasi ya kucheza kibinafsi ujue umepotea.
Ushauri wa mwisho kwa Ndemla ajifunze kucheza nafasi zaidi ya moja uwanjani. Kwa sasa Simba ina viungo wengi lakini washambuliaji wa mwisho ni wachache. Mimi namuona Ndemla kama mshambuliaji mmoja mwenye kitu cha tofauti iwapo tu atapata maelekezo kidogo kutoka benchi la ufundi na yeye mwenye akiamua kwa moyo wake wote kucheza kama mshambuliaji wakati huo huo akiwa kiungo. Lakini akishindwa yote hayo bora msimu ujao atafute timu nyingine itakayompa nafasi ya kucheza ili asipoteze kipaji chake kwani umri unaenda na yeye hii miaka miwili mitattu ijayo anatakiwa awe kwenye kilele cha ubora wake.
Kagera sugar wanaweza kumlipa mshahara anaopata Simba kwa Sasa?Tatizo lipo kwa Ndemla, kwanini asiondoke akacheze timu kama KMC, MTIBWA, KAGERA SUGAR, NAMUNGO?
Hapo Simba kuna vipaji vinapotea sana:
1.Mlipili
2. Rashid Juma
3. Ndemla
4. Gadiel
Sent using Jamii Forums mobile app
Kwa mchezaji mwenye malengo, mwenye kipaji, mpambanaji na anayejiamini hawezi kukaa tu benchi kwenye timu eti kwa sababu analipwa mshahara mkubwa. Kwa vyovyote vile lazima atatafuta jukwaa sahihi kwenye hizi timu za kati kama Mtibwa, kagera, Ruvu, n.k. aonyeshe uwezo wake halafu hizi timu kubwa zitamfuata kwa mshahara mkubwa zaidi ya huo wanaompa sasa. Mfano mmoja Hasani Dilunga alikuwa Yanga yakatokea yaliyotokea lakini kwa kuwa alikuwa anajiamini aliachana na Yanga na kama sikosei akaenda Ruvu na baadae akaibukia Mtibwa na sasa yupo Simba tena akiwa na kiwango cha hali ya juu. Hata Kelvin Yondani Simba walianza kumpiga benchi kiajabu ajabu lakini kwa kuwa alikuwa anajiamini aliamua kuondoka na kujiunga na Yanga ili kuokoa kipaji chake vinginevyo angeng'ang'ania mshahara tu Simba Yondani angepotea mazima katika ramani ya soka.Kagera sugar wanaweza kumlipa mshahara anaopata Simba kwa Sasa?
Ni mtaalamu wa kucheza BAO KAMA WEWE!
Beki wa zamani wa Toto African ya Mwanza. Beki mmoja hivi fundi, ng'ado kwa ng'ado, mbishi mbishi fulani awapo kazini uwanjani, kwa mbali ana umbo kama la George Magere Masatu na hata uchezaji wake kidogo umefanana kama wa Masatu. Beki ambaye ndiye alikuwa muhimili wa ukuta wa Simba kwenye ligi ya ndani na michezo ya kimataifa miaka michache hivi iliyopita na ili kuujua ubora wake nenda "youtube" ukaangalie Simba VS Al Masry.Kwa sasa Mlipili yupo anaozea benchi pale Simba Sport Club na hakuna anayejua sababu hasa ni nini kwani alianza Ausems kumpiga benchi na hata Sven naye hajampa nafasi kabisa kuonyesha uwezo wake.Mlipili ndo nani?
Kwaiyo awekwe benchi Mkude, Kahata,Louis,Dilunga au Chama ili acheze huyo mchezaji wako?
Soka ni ushindani na sio huruma kama ambavyo mnataka nyinyi, ni sawa na mwanao anapata mitihani 95 lakini kuna wanaopata 100 mitihani yote unataka apewe number moja kwa huruma!!
Ukiona hapati number ujue ushindani umemzidi hata kama kiwango chake ni cha juu.Kama Wewe ni Simba kweli unataka akiingia yeye atoke nani ambae kiwango chake kiko chini kuliko Ndemla??
Sent using Jamii Forums mobile app
Labda lakini hana lolote kwa sasa, abadiliki amekariri kupiga mashuti tu.
Gadiel wacha yamkute nilimwambia ila hakunisikia sasa pesa imeisha na mwakani wana mtemaTatizo lipo kwa Ndemla, kwanini asiondoke akacheze timu kama KMC, MTIBWA, KAGERA SUGAR, NAMUNGO?
Hapo Simba kuna vipaji vinapotea sana:
1.Mlipili
2. Rashid Juma
3. Ndemla
4. Gadiel
Sent using Jamii Forums mobile app
Wacha hizo Fraga Yuko juu yake, Fraga anakaba na kushambulia na kufunga.Kinachoniuma zaidi ni yule Mbrasil Fraga anacheza alafu huyu dogo hachezi hata benchi hakai hii sio fair kabisa
Sent using Jamii Forums mobile app
Gadiel hawezi kutemwa hakuna timu isiyokuwa na mchezaji subGadiel wacha yamkute nilimwambia ila hakunisikia sasa pesa imeisha na mwakani wana mtema
Sent using Jamii Forums mobile app
Swali atoke nani yaani nani asicheze ili yeye acheze. Kwa hiyo hapa unamaanisha Mkude asianze? Kwamba Ndemla aanze akimuweka benchi Mkude? Ndio changamoto Ilipo kakaAkianza Chama,au Shibobo amalizie Ndemla, or viseversa.