Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,307
- 25,932
Kwa huu mpira wa fainali ya AFL mkondo wa kwanza ninaoushuhudia hapa, nathubutu kusema Simba walibahatika kupangwa na Al Ahly.
Simba na wenzao wote wanacheza mpira wa taratibu. Wote wana wachezaji wazito. Hakika, kama Simba angepangwa na Wydad au Mamelodi hii, tungepata aibu ya kitaifa.
Wababe hawa Wydad na Mamelodi wanaupiga mwingi sana. Pamoja na hadi sasa Mamelodi kuwa nyuma kwa 2-1 ugenini, unapigwa mpira mzito sana.
Kama Yanga ya akina Aucho na Max imewapoteza hivi leo, ingekuwaje kama wangepambana na Mamelodi au Wydad hii. Walibahatika sana kupangwa na Al Ahly.
Simba walistahili kupata sare mbili. Ila level hii wangefika tungeshazima tv zetu muda huu. Wanalunyasi huwa wana bahati sana mashindano ya kimataifa.
FT: 2-1
Marudiano ni tarehe 12 pale kwa Madiba
Simba na wenzao wote wanacheza mpira wa taratibu. Wote wana wachezaji wazito. Hakika, kama Simba angepangwa na Wydad au Mamelodi hii, tungepata aibu ya kitaifa.
Wababe hawa Wydad na Mamelodi wanaupiga mwingi sana. Pamoja na hadi sasa Mamelodi kuwa nyuma kwa 2-1 ugenini, unapigwa mpira mzito sana.
Kama Yanga ya akina Aucho na Max imewapoteza hivi leo, ingekuwaje kama wangepambana na Mamelodi au Wydad hii. Walibahatika sana kupangwa na Al Ahly.
Simba walistahili kupata sare mbili. Ila level hii wangefika tungeshazima tv zetu muda huu. Wanalunyasi huwa wana bahati sana mashindano ya kimataifa.
FT: 2-1
Marudiano ni tarehe 12 pale kwa Madiba