Simba walichezea nafasi na sasa wanalia lia hovyo, nani alaumiwe?

Simba walichezea nafasi na sasa wanalia lia hovyo, nani alaumiwe?

Its Pancho

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
15,966
Reaction score
26,404
Wakuu,

Simba walichezea nafasi waliyopata na sasa wameanzisha propaganda kubwa sana

Kila timu ikifungwa na yanga basi ni udhaminj wa GSM na urafiki wa GSM. Hizi ni hoja mfu sana.

Wakati wa game yao na Namungo mgunda kocha kindakindaki wa simba alionekana wazi akifurahia wao kufungwa mpaka kufikia halftime wachezaji wa namungo wakigoma kurudi uwanjanj baadavya card ya mkombozi ambayo ilikuwa ya mchongo na kufutwa.

Lakini Mgunda akawaambia wachezaji warudi tu uwanjanj hakuna namna huku anacheka cheka what a fella!

Msimu ule team pacha ya Simba coastal union waliwaazima kocha Simba ambaye ni Mgunda lakini watu walikaa kimya tu huo ulikuwa upumbavu mkubwa sana kutokea kwa Simba

Zilifanyika figisu Tabora wachezaji wao wqkanyimwa vibali mpaka game yao na simba ipite na wakafanikiwa kwa hilo kisha ikaja kwa fountain Gate hivyo hivyo wakafanikiwa wakishiriana na TFF mume wao halali.

Bado Yanga waliomba kuchezea kwa mkapa game yao na azam lakini TFF waliwagomea wakidai uwanja upo kwenye maintenance lakini leo mke wao simba kakubaliwa acheze na azam pale, kisingizio ni eti uwanja ujae

Ni lini hivi viteam viwili simba na azam vilijaza uwanja? Pia tuwakumbushe kuwa card ya mkombozi imefutwa kwa sababu imetolewa kimakosa je refa aliyetoa amewajibishwa? Kama bado kwanini? TFF waache kupendelea mke wao simba ni aibu.

Simba wanaongoza kupewa penati. Wanaongoza kuwa maamuzi ya utata hasa card na kuongezwa madakika mengi.

La mwisho tumuombee kijana kibu Denis anatimiza miaka miwili bila goli ligi kuu

Aucho goli 1
Kibu 0 miaka miwili.

Kupanga ni kuchagua.

Its Pancho
 
Ila kiukweli hakuna timu inabebwa kwenye ligi kama Simba.
 
Back
Top Bottom