Simba yafanya mauaji Geita, yatuma salamu Mbao FC

brave one

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2013
Posts
4,879
Reaction score
7,386
Wekundu wa Msimbazi na mabingwa watarajiwa wa msimu wa 2016/17 Simba wameitafuta timu ya Geita gold mining inayoshiriki ligi daraja la kwanza kwa jumla ya 7 katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Leo.

Hizi ni salamu kwa Mbao FC wanaotarajiwa kucheza nao weekend hii kwenye mchezo muhimu wa ligi kuu

Simba inaitaji ushindi namba yoyote ili kusafisha safari ya ubigwa

 
Ni kujifariji ambako hakuna maana yoyote na mechi kama hizo sidhani kama zinaiongezea chochote Simba SC

Tumepoteza mechi muhimu sana dhidi ya Kagera Sugar, timu inakuwa ya Media tuu, ovyo sana..!
 
Sawa....kirumba itatupa majawabu
 

Hatuhitaji huu ' upuuzi ' wao na wakae wakijua kuwa wametuudhi na kutusononesha mno sisi Wana Simba kwa kipigo kile kutoka kwa akina ' Nshomile ' Jumapili iliyopita. Hivi inaingia akilini kweli Timu inacheza kitimu na vizuri kabisa halafu katika mechi muhimu ya Ligi ina ' mbwela mbwela ' tu? Simba wakae wakijua kuwa tarehe 8 tukitoka tu sare au kufungwa na Mbao FC basi tayari Yanga FC watakuwa wana 99.99% ya kuwa Mabingwa kwa mara ya tatu mfululizo. Timu yetu iache mno kuwekeza katika ' Ushirikina ' na badala yake tuwajenge tu Kisaikolojia Wachezaji wetu. Tumefungwa Kagera kwa imani zetu za Kipumbavu kabisa za Kishirikina huku tukiwalazimisha baadhi ya Wachezaji waliokuwepo Taifa Stars kucheza wakati baadhi yao wakiwa na maumivu na wamechoka.

Na mkifungwa huko Mwanza nyie Wachezaji wa Simba tafuteni kwa kwenda kuishi kwani kiukweli hapa Dar mtatusamehe tu. Tumechoka na huu upuuzi wenu!
 
Pole mkuu umeongea kwa uchungu sana.. Ila kwenye soka lolote hutokea
 
Yanga wana wanamechi ngumu kuliko unavyofikiria
 
Ukiona mtu yeyote anaiye jiita mwana michezo akaropoka kwamba
"hakuna timu itakayo tufunga tena"
ZIMA REDIO AU TV ENDELEA NA SHUGHULI ZAKO ASIKUPOTEZEE MUDA
kwani hajitambui na hana akili
 
Pamoja mkuu

Ujinga uliofanyika Kagera haupaswi kuona kama jambo la kawaida tu hasa ukizingatia kipindi hiki cha kugombea ubingwa.. Timu imekuwa ya ajabu sana miaka hii, mzuka wa ubingwa haionekani kabisa.. Wajitathimini bhana wache upuuzi
 

Kweli kabisa mkuu,,,me ndio itakuwa mwisho wa kuishabikia simba
 
Kweli nimeamini mashabiki wa Simba ni Mambumbumbu ya kufa mtu,yaani wakina Aveva wanawachezea akili watakavyo. Embu anza na swala la nyasi then njoo kwenye ubingwa halafu malizia na hizi match zisizonampango wachezazo na kushinda kapu la magoli. Ubingwa mtauona kwenye T.V
 
Kweli kabisa mkuu,,,me ndio itakuwa mwisho wa kuishabikia simba

Michezaji yetu Mipumbavu mno Mkuu halafu kinachotuudhi wengi ni kwamba kila kitu wanakipata na hawana njaa yoyote ile na wanaangaliwa na kujaliwa kuliko kipindi chochote lakini wao hata hawajali na hawathamini. Bahati yao sikuwepo Kagera ila kama ningekuwepo ule upuuzi ambao aliufanya mdogo wangu Abdi Banda jr kwa kucheza rafu ya Kipumbavu kabisa kwa kumpiga Ngumi ya makusudi George Kavila ningekuwa nae karibu ningempa bonge la ' Ndoo ' kwani kama yule Mwamuzi asingetumia busara nakuhakikishia siku ile angekula ' umeme ' yaani angeonyeshwa Kadi nyekundu na angeigharimu mno Timu hasa ukizingatia Kagera Sugar ndiyo walikuwa wanakuja utadhani wamewekewa ' mota ' matakoni. Ole wao mechi ya Mbao FC na Toto Africa ' wachemshe ' ndipo watatujua mashabiki wa Simba Sports Club kuwa ' tumeshadata ' na ' kuchoka ' kitambo sana. Mkuu kile Kipigo cha kutoka kwa Kagera Sugar kimeniuma kupita maelezo kwani ni bora uzidiwe points 15 na Ndanda FC lakini siyo uzidiwe point 1 tu na Yanga FC kwani kuwakuta hapo au kuwaondoa inatubidi wenye uchungu na Simba yetu tufanye Kazi ya ziada tena nje ya Uwanja na tujitoe mhanga vinginevyo Yanga analichukuwa tena Kombe.
 
Pole bro.... Simba hawajui wanahitaji nini.... Hizi mechi za kirafiki wakati ligi inaendelea imewacost na itaendeleea kuwacost
 
bro rekebisha mwandiko wako kiukweli huwa una hoja sana ila mwandiko wako huwa hauvutii na unaumiza macho kwa sisi wengine. tumia tu mwandiko wa jf
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…