Simba yafanya mazoezi bila kocha Mkuu Aussems ambae amesimamishwa na Uongozi

ZionGate

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
6,362
Reaction score
2,991
Baada ya mapumziko ya siku tatu, kikosi cha Simba leo kimerejea mazoezini kuendelea na maandalizi ya michezo ya ligi inayofuata

Simba imejifua bila ya kocha wake Mkuu Patrick Aussems ambaye amesimamishwa akisubiri maamuzi ya kikao cha Kamati ya Nidhamu na Maadili ambacho kitakaa keshokutwa Alhamisi

Kocha Msaidizi Denis Kitambi pamoja na maafisa wengine wa benchi la ufundi walisimamia mazoezi hayo yaliyofanyika uwanja wa Gymkhana jijini Dar es salaam
 
Kwahiyo wamemwadhibu kabla ya kutoa maamuzi?
 
Hakuma mafanikio bila nidhamu, pale ambapo nidhamu inapwaya viongozi kazeni buti hilo swala la chama na mkude lisimamiwe.
Chezea pesa sio kazi.
 
Hakuma mafanikio bila nidhamu, pale ambapo nidhamu inapwaya viongozi kazeni buti hilo swala la chama na mkude lisimamiwe.
Chezea pesa sio kazi.
Nidhamu ya nini tena?? Manara kasema kocha Alienda Tottenham Hotspurs kucheki nafasi. Sasa wanamuadhibu wa nini
 
Si nimesikia auseums alienda kwenye usaili wa timu ya totenham spurs? Wabongo bana!
 
Aliondoka bila kuaga aliporudi anaulizwa anajibu kwani lazima kuaga
Nidhamu ya nini tena?? Manara kasema kocha Alienda Tottenham Hotspurs kucheki nafasi. Sasa wanamuadhibu wa nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…