Simba yamnyatia mshambuliaji wa AFC Leopards Allan Kateregga

kirerenya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2013
Posts
1,696
Reaction score
2,253
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili wa klabu ya simba SC Zacharia Hans Poppe amesema wametuma mtu kwa ajili ya kuzungumza na uongozi wa timu ya AFC Leopard, ili kumsajili mshambuliaji Allan Kateregga, aliyefanya vizuri kwenye michuano ya Sport Pesa Super Cup.

Hans Poppe, amesema tangu kumalizika kwa michuano hiyo walikuwa wakijipanga kwa ajili ya kumalizana na wachezaji wengine ambao tayari walishaanza mazungumzo na baada ya kumalizana nao sasa wameona ni muda muafaka kumfukuzia mshambuliaji huyo.

“Ni mchezaji mzuri tumemuona hapa alipokuwa na timu yake ya AFC Leopards, ni mchezaji mwenye uwezo wa kucheza hata eneo la kiungo hata kocha Joseph Omog, alivutiwa naye na ndiyo ametushauri kumsajili,”amesema Hans Poppe.

Kiongozi huyo alisema Kateregga ndiyo atakuwa mchezaji wa mwisho kumsajili msimu huu, na kazi itakayobaki ni kujazia nafasi zenye mapungufu kwa kusajili wachezaji wazawa ambao wataona wanastaili kuichezea timu yao.

Amesema wapo wachezaji ambao tayari walishawaanda kwa kufanya mazungumzo nao ya awali na hivi karibuni wataanza harakati za kukamilisha usajili wao ili kufunga rasmi zoezi la usajili kwa ajili ya msimu ujao.

Simba ilikuwa ikimfukuzi Donald Ngoma wa Yanga, lakini mshambuliaji huyo tayari amewaponyoka na baada kusaini mkataba wa miaka miwili kuendelea kuwatumikia mabingwa hao wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara.

Chanzo: Shaffih Dauda
 
Katerega hana uwezo unaohitajika Simba sc.
Anatumia kucheza na mguu wa kushoto pekee.
Kulia haendi kabisa, kukimbia na mpira, kupiga chenga au shuti anatumia kushoto.
Mpira ukikaa kulia hawezi kuumudu inavyopasika.

Simba tatizo ni washambuliaji,
Tafuteni wafungaji wazuri kama, Obrey Chirwa.
Itawasaidia.
Katerega hamna kitu.
 
Wewe kweli bure Chirwa naye mchezaji???
 
Kuna mshambuliaji gani kama chirwa pale simba? Tatizo lenu mmekariri mwisho wa ligi mkiona yanga ana magoli mengi mnakimbilia FIFA hebu angalia forward kuna Ngoma ,Tambwe ,Chirwa, Ajibu na Msuvu tutakosaje kuwa na magoli mengi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…