Mgononi
Member
- Dec 1, 2020
- 6
- 3
KWANINI LWANGA HAKUWA NA TIMUBrother mbona maelezo marefu sana wew ni upande wa pili au, mana kuna wenzako wakisikia jina okwi wanapatwa na homa ya kuendesha, mim najua gap lililokuepo ni la kiungo mkabaji na kushambulia apo apo achukue mikoba ya Gerson Fragha so kumtaja okwi nilikuwa nasababu zangu kuna viumbe nawatafuta, pili kuhusu kwamba ni mim na nan tunamtaka inakusaidia nin? Kwani kama ni mim na mke wangu ndo tunataka wew unapata nini? Tatu, kuhusu kwamba mim ni mshabiki au mwanachama what do you want ni unafanya sensa au research???
Anaandika @exaud_msaka_habari
Ni kweli Lwanga mpaka anajiunga na Simba leo alikuwa free yani hakuwa na timu yoyote.
Ni hivi Kiungo huyo mkabaji alisaini mkataba wa miaka mitatu na Tanta Sports ya Misri ikiwa ni baada ya kufanya vizuri sana kwenye AFCON lakini mwaka huu kiungo huyo aliomba kuvunja mkataba wake kwa sababu mbalimbali ikiwemo kumaliza miezi saba bila kulipwa kitu ambacho kwa mujibu wa sheria za FIFA ana haki ya kuvunja mkataba huo
Uongozi unaomsimamia ambao ni kampuni ya YELO MANAGMENT waliandika barua kwenda kwa uongozi wa timu yake kuomba kuvunja mkataba huo pamoja na kulipwa stahiki zake ambazo waliahidiwa kulipwa mwezi january mwaka huu
Mwezi July mwaka huu Kiungo huyo pamoja na Nyota wa Gabon Mario Bernad waliachwa rasmi na timu hiyo na Lwanga kurejea kwao Uganda kama mchezaji huru
Vyombo vya habari vya Misri vilieleza kuwa chanzo cha Nyota hao kuvunjiwa mikataba yao ni pamoja na barua zao za kuomba hilo wakionyeshwa kutoridhishwa na maisha ndani ya club hiyo.
Uongozi wa Lwanga walieleza kuwa Mambo waliyoahidiwa na Timu hiyo hayakutimizwa ikiwemo mishahara, pamoja na huduma za kawaida za mchezaji kitu ambacho Lwanga aliomba kuondoka Misri.
Baada ya Kurejea Uganda Lwanga alipata ofa zaidi ya tatu za nje ya africa ila sababu ya Covid 19 alishindwa kujiunga nazo (vyombo vya habari vya uganda vimeandika)