Simiyu: Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya milioni 5 kwa kosa la kuwapa majibu wanafunzi

Simiyu: Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi ahukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya milioni 5 kwa kosa la kuwapa majibu wanafunzi

Mkalukungone mwamba

JF-Expert Member
Joined
Aug 29, 2022
Posts
862
Reaction score
1,755
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Sunzula B, Wilaya ya Itilima Mkoa wa Simiyu, Bahati Suguti amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh5 milioni kwa kosa la kufanya udanganyifu katika mtihani la darasa la nne mwaka 2023.

Katika kesi hiyo iliyotolewa hukumu leo Februari 2, 2025 na Mahakama ya Wilaya ya Itilima, mahakama imewaachia huru washitakiwa wenzake watano ambao ni walimu baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.

Hii ni baada ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Robert Kaanwa, kueleza kuwa ushahidi uliotolewa unaonyesha washitakiwa hao watano ambao walikuwa ni wasimamizi wa mitihani, hawakuhusika kutenda kosa hilo.

Source: Mwananchi
 
Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Sunzula B, Wilaya ya Itilima Mkoa wa Simiyu, Bahati Suguti amehukumiwa kifungo cha miaka mitatu jela au kulipa faini ya Sh5 milioni kwa kosa la kufanya udanganyifu katika mtihani la darasa la nne mwaka 2023.

Katika kesi hiyo iliyotolewa hukumu leo Februari 2, 2025 na Mahakama ya Wilaya ya Itilima, mahakama imewaachia huru washitakiwa wenzake watano ambao ni walimu baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha mashitaka dhidi yao.

Hii ni baada ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa mahakama hiyo, Robert Kaanwa, kueleza kuwa ushahidi uliotolewa unaonyesha washitakiwa hao watano ambao walikuwa ni wasimamizi wa mitihani, hawakuhusika kutenda kosa hilo.

Source: Mwananchi
Hizo millions 5 atachukua nani?
 
Hawa mahakimu sijui huwa wanawaza nini? Mtu dhamira yake ilikuwa kuwasaidia wanafunzi wake hata kama alitenda kosa na pia ni kinyume cha sheria lakini adhabu ni kubwa mno. Wezi wa mabilioni ya kodi za wananchi wanadunda tu mtaani na hakuna la kuwafanya. Hii nchi ni ngumu sana aisee. Anyway, hakuna marefu yasiyo na ncha. Pole sana Mwalimu.
 
Hawa mahakimu sijui huwa wanawaza nini? Mtu dhamira yake ilikuwa kuwasaidia wanafunzi wake hata kama alitenda kosa na pia ni kinyume cha sheria lakini adhabu ni kubwa mno. Wezi wa mabilioni ya kodi za wananchi wanadunda tu mtaani na hakuna la kuwafanya. Hii nchi ni ngumu sana aisee. Anyway, hakuna marefu yasiyo na ncha. Pole sana Mwalimu.
Kosa alilofanya huyu mkuu wa shule ni zaidi ya kuiba mamilioni ya pesa.Hao watoto wakija kuwa madaktari kwa mfano unajua itakuwaje?
 
Walimu wana vihelehele sana tena wakiwa na zile kadi pendwa baadhi yao huwa wanajiona ndio wameyashinda maisha kabisa
 
Mkuu wa mkoa"Mwalimu mkuu ambaye hatafaulisha wanafunzi atashushwa cheo"
Waalimu wanaamua kujiongeza
 
Wazazi wa hao wanafunzi waliokuwa wanasaidiwa si wangemchangia huyo mwalimu ili kulipa faini na hivyo kumwepusha na kifungo.
 
Ndo maana sitaki mwanangu awe Mwalimu.Nilikosana na mzee wangu alitaka nikasomee ualimu nikagoma.Saiv ananipongeza kwa kusoma hitaji la moyo wangu.
 
M/Mkuu msaidizi atakua kamchoma. Adui wa mwalimu ni mwalimu mwenzie.
 
Back
Top Bottom