LGE2024 Simiyu: Watumishi NMB wahimizwa kujiandikisha orodha ya Wapiga Kura Uchaguzi Serikali za Mitaa

LGE2024 Simiyu: Watumishi NMB wahimizwa kujiandikisha orodha ya Wapiga Kura Uchaguzi Serikali za Mitaa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
IMG-20241017-WA0004.jpg
Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu, Prisca Joseph Kayombo amewahimiza watumishi wa Benki ya NMB na watumishi wengine wa Sekta binafsi Mkoani Simiyu kwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili wapate haki yao ya msingi ya kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Ametoa rai hiyo alipozungumza na watumishi hao katika Mtaa wa Benki Wilayani Bariadi katika muendelezo wa zoezi la kuhamasisha Watumishi wa Taasisi za Serikali na Binafsi Mkoani Simiyu kujitokeza kujiandikisha.

Amewataka watumishi hao kutochanganya zoezi la maboresho ya Daftari la kudumu la Wapiga kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu na Daftari la wapiga kura za viongozi wa Serikali za Mitaa.
IMG-20241017-WA0005.jpg

Snapinsta.app_463632125_1272533063941955_1120128741137927277_n_1080.jpg

Amewataka pia kuwa mabalozi wa kuhamasisha Wananchi kujitokeza katika vituo vya kujindikisha ili waweze kuwa na sifa ya kupiga kura kuwachagua Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Rais -TAMISEMI uchaguzi wa Serikali za Mitaa Nchini utafanyika Tarehe 27 Novemba 2024.
 
2015 watu walikuwa wanaamka saa kumi alfajiri kwenda kujiandisha. Ila tangu wagundue huu ni usanii ndio haya tunayoona saizi.
 
IMG-20241017-WA0004.jpg

Katibu Tawala Mkoa wa Simiyu Bi.Prisca Joseph Kayombo amewahimiza watumishi wa Benki ya NMB na watumishi wengine wa Sekta binafsi Mkoani Simiyu kwenda kujiandikisha katika orodha ya wapiga kura ili wapate haki yao ya msingi ya kushiriki uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Ametoa rai hiyo alipozungumza na watumishi hao katika Mtaa wa Benki Wilayani Bariadi katika muendelezo wa zoezi la kuhamasisha Watumishi wa Taasisi za Serikali na Binafsi Mkoani Simiyu kujitokeza kujiandikisha.
IMG-20241017-WA0005.jpg


Amewataka watumishi hao kutochanganya zoezi la maboresho ya Daftari la kudumu la Wapiga kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu na Daftari la wapiga kura za viongozi wa Serikali za Mitaa.

Amewataka pia kuwa mabalozi wa kuhamasisha Wananchi kujitokeza katika vituo vya kujindikisha ili waweze kuwa na sifa ya kupiga kura kuwachagua Viongozi wa Serikali za Mitaa.


Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Ofisi ya Rais -TAMISEMI uchaguzi wa Serikali za Mitaa Nchini utafanyika Tarehe 27 Novemba 2024.
 

Attachments

  • IMG-20241017-WA0003.jpg
    IMG-20241017-WA0003.jpg
    140.3 KB · Views: 4
Back
Top Bottom