FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
Je, una malengo?
Kama unayo, basi jaribu kurahisisha maisha yako.
Kivipi?
Jaribu kupunguza mambo ambayo yataathiri hayo malengo yako.
Mambo ambayo kwa namna moja ama nyingine hayana mchango wowote ule katika malengo uliyojiwekea.
Mambo kadha wa kadha ambayo uwepo wake katika mwenendo wa maisha ya mtu ya kila siku ni kichocheo cha kuyaharibu malengo yake.
Mambo ambayo uwepo wake katika maisha ya mtu ni kisiki cha kujikwaa na hatimaye 'kuanguka' kimaisha.
Mambo hayo ni 'mzigo mkubwa' na 'mzito sana' tena kupindukia kwa sababu muda wote yanapambana na kuhakikisha kwamba unashindwa kuyatimiza malengo yako.
Bila shaka kila mmoja anajua na anayafahamu, ni mambo gani yanayojaribu kuyawinda "kwa udi na uvumba" malengo yake.
Kama unafahamu hilo basi rahisisha maisha yako.
Always THE GREAT
Kama unayo, basi jaribu kurahisisha maisha yako.
Kivipi?
Jaribu kupunguza mambo ambayo yataathiri hayo malengo yako.
Mambo ambayo kwa namna moja ama nyingine hayana mchango wowote ule katika malengo uliyojiwekea.
Mambo kadha wa kadha ambayo uwepo wake katika mwenendo wa maisha ya mtu ya kila siku ni kichocheo cha kuyaharibu malengo yake.
Mambo ambayo uwepo wake katika maisha ya mtu ni kisiki cha kujikwaa na hatimaye 'kuanguka' kimaisha.
Mambo hayo ni 'mzigo mkubwa' na 'mzito sana' tena kupindukia kwa sababu muda wote yanapambana na kuhakikisha kwamba unashindwa kuyatimiza malengo yako.
Bila shaka kila mmoja anajua na anayafahamu, ni mambo gani yanayojaribu kuyawinda "kwa udi na uvumba" malengo yake.
Kama unafahamu hilo basi rahisisha maisha yako.
Always THE GREAT