Simshauri mtu yeyote kuweka fedha benki kwa Tanzania ya sasa, ni hasara sana!


Mbona nilishakwambia mara kadhaa kwamba kama una cash invest kwenye real assets kama dhahabu tanzanite, nyumba, mashamba, viwanja nk? Hivi ni vitu ambavyo mara nyingi vina appreciate badala ya ku-depreciate. Na pia kuna baadhi ya vitu hapo unaweza uvibadii kuwa cash haraka sana bila matatizo.

Kanuni ya fair interest rate ni kwamba ni lazima iwe juu ya average inflation rate, la sivyo ukilipwa faida chini ya hapo ujue unatiwa hasara tu, hasa ukitia ndani na bank administration fees na charges!
 
Hakupata elimu tosha ya akaunti gani afungue.
Kuna akaunti za watoto huwa hazina charges acheni kudanganyana huko mtaani.

Hata kama mkuu. Tatizo ni kwamba iweje mtu aweke hela zake kwa kipindi chote hicho halafu akute zimepungua badala ya kuongezeka japo kidogo. Hii ina maana faida ya mwaka wanayojifanya kuwawekea wateja ni ndogo kuliko charges zao. Otherwise pesa isingepungua na badala yake ingeongezeka japo kidogo coz benki wanazifanyia biashara.

Mi kwa kweli nimeishakoma kuweka hela benki, inaingia na kutoka hapo hapo. Bora nikaitunze kwenye assets kama viwanja kuliko kuliwa na benki kiwizi wizi hivyo.
 

Tatizo ni kwamba wengi wetu hutukuwahi kuliangalia hili jambo kwa undani. Bado tuna mentality ya zile enzi za zamani kuwa ukiweka fedha benki ni faida tu kia mwaka!
 
Ndugu kuna vitu hapo nadhani inafaa tuvitazame upya. Umetaja dhahabu. Hii ni commodity na bei yake inategemea hasa na soko la dunia. Angalia kwenye chart ya price yake utaona ilikuwa juu saana 2011 then ikaenda chini. Performance yake inategemeana na hali ya uchumi wa dunia. Pia vitu kama nyumba, investment yake ni kubwa kuliko hizi normal savings za watanzania wakawaida. Lakini fair interest si lazima iwe above inflation. Unaset agreement ya interest bila kujua inflation itakuwaje. Ndio maana watu walioweka pesa zako kwenye pension funds wakati wa economic crisis, thamani ya zile investment zilipotea. Na kama savers watademand haya interest rate above inflation rate, lending rate itapanda. vivyo hivyo sector nyingine za uchumi zitakosa wawekezaji.
 

Nikajua hutumii kabisa bank:sly:
 

Nakuelewa Mkuu. Lakini risk ya kushukana kupanda kwa bei ya dhahabu bado ni nafuu sana ukilinganisha na kuweka fedha benki. Mfano hapa juzi bei ya dhahabu imeongezeka sana, tofauti na trend ya shilingi ambapo siku zote inaporomoka. Pia sio lazima iwe dhahabu tu. Mfano tanzanite iko stable sana.
 
hujaweka usumbufu na kuibiwa fedha zako yaani nawapa wanitunzie pesa wazifanyie biashara halafu mwisho wananikata umeongea ukweli mtupu
 

Kuna mahali nilisoma kwamba kwamba hisa zinapoporomoka bei ni wakati mzuri kwa smart investors kufanya move sababu lnvestors ambao ni layman watakimbilia kuuza hisa zao. Sababu kuna point tu kampuni itarudi juu kama kushuka kwake tu kumesababishwa na tukio la muda mfupi.
 
mkuu kwa hiyo hujatoa muongozo tufanyeje. Umeishia kusema tu kuweka hela benki ni hasara. Mimi naona pamoja na kupata hasara lakini ndo njia pekee naweza kudunduliza kiasi kikubwa cha fedha kufanya kama mtaji wa biashara. Njia nyingine ni kwenye soko la hisa nadhani hii ina consider na inflation na ndo njia bora zaidi ila iko more risky sababu markets zipo volatile
 

He! Hivi Mkuu umesoma post au kichwa cha post? Nakushauri usome na post zilizochangia.
 
He! Hivi Mkuu umesoma post au kichwa cha post? Nakushauri usome na post zilizochangia.

Ok part ya mwisho sikuiona. Samahani kwa oversight,. Niliconcentrate zaidi sehemu ya benki na makto ila mstari wa mwisho wa conclusion sikuuangalia sababu ulikuwa hujaupa uzito sana kama point za mwanzoni. Next time ni vizuri paragraph ya kwanza ikasummarize point zote unataka kuziraise...Ili msomaji ajue mtiriko wa hoja nzima. Mimi huwa siosmi word to word huwa nafanya scanning kwanza. Sifa moja ya uandishi mzuri wa mada ni kuonyesha point nzima unayotaka kujenga. Nafikiri kichawa cha habari kingekuwa Ni bora kuwekeza kwenye low risky kuliko kuweka fedha benki kupata hasara. Hii inabeba content nzima ya unachotaka kukizungumzia. Ili real life the tunaposoma the first few paragraph ni kwa ajili ya kumu engage reader kwenye discussion uliyoanzisha ili apase kusoma mada yote kwa undani na scanning tu mkuu. Kwa nhiyo nimekuelewa point yako baada ya kwenda kuusoma mstari w amwisho lakini ilikuwa haipo obvious kwamba utakuja conclude mwishoni na hizo suggestion kwa hiyo mimi niliscan niakjua mada nzima inahusu tu makato hakuna suggestions.
 
Hebu tuoneshe hiyo faida kupitia hizo account.
Halafu linganisha na riba ya 20% wanayokutoza ukienda kukopa kwao.

Hii riba ya 20% ipo katika benki chache tena baada ya consideration nyingi- benki nyingine huenda mpaka 25% achilia mbali Microfinance ambazo ziko juu ya 25%

Mkuu nami ningependa kujua huko ambako fixed deposit, short term deposit au saving account ya kawaida inatoa faida nzuri
 


Wekeza fedha zako kwenye fixed assets.
Achana na mambo ya benki.
 
ndugu
nyumba, mashamba na viwanja sawa vinaappreciate ila dhahabu na tizanite au niseme madini kwa ujumla kuna kipindi na yenyewe huwa yanashuka bei kutokana na soko la dunia. hiii iliwahi kuwakuta wadau huko geita, hata nyumba kama ni muda mrefu inabidi uwe unaikarabati, so kuna risk flani ipo but at least kuna kafaida kataonekana. pia nyumba na viwanja ulenge sehemu sio bora kununua tu.
 

Nakubali kabisa, hasa kwa upande wa dhahabu, huwa bei inaweza kushka na kupanda. Hata hivyo si kwa kiwango kikubwa ukilinganisha na thamani ya shilingi. In fact, unaweza pia ukafungua account ya foreign currency. Currency kama Dola, Euro na Pound ziko stable kiasi cha kutosha ukilinganisha na Tshs. Hivyo huwezi kupoteza thamani ya fedha yako kama vile ambavyo ukiweka benki Tshs
 

Nakuunga mkono 100%; Ukizingatia na risk ya kuuwawa wakati ukienda kuchukua pesa benki kutokana na "inside job" ya watumishi wa benki! Imagine janga la Access Bank Mbagala majuzi na raia wasio na hatia waliouwawa wakitoka benki kuchukua vijisenti vyao kidogo!
Hata hivyo Banks are a neccessary evil; zinaepukika at your own peril!
 
mii kinachonisikitisha kwa mabenki ni ile kutotuamini sisi wateja wao tu, yaani wao pen tu wanaifunga kamba, wakati sisi tumewaamini na mihela yetu, bila hiyana!
 
Kuweka hela nyumbani nako ni challenge kubwa hasa kwa hawa wajomba wenye pikipiki aina ya Boxer, afadhali wanasiasa wenzetu wanaenda kuweka pesa za Swiss tena wanapoenda kuzihifadhi gharamq zote za safari zinalipwa na serikali


We mkuu..umefikiria mbali sana. wanapeleka ulaya pesa kwa gharama za umma!!!!!
 
Kuweka hela nyumbani nako ni challenge kubwa hasa kwa hawa wajomba wenye pikipiki aina ya Boxer, afadhali wanasiasa wenzetu wanaenda kuweka pesa za Swiss tena wanapoenda kuzihifadhi gharamq zote za safari zinalipwa na serikali
Just missing you. .....πŸ™‚πŸ™‚πŸ™‚πŸ˜‰
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…