May Day
JF-Expert Member
- May 18, 2018
- 6,311
- 9,027
Ananisimulia jamaa yangu:-
Miaka kama tisa iliyopita nilikuwa kwenye mahusiano na Mwanadada mmoja tuliyekuwa tunafanya nae kazi kwenye kampuni moja.
Ndani ya miaka mitatu mapenzi yetu yalikuwa motomoto kabla ya Mimi kuamua kujitoa ghafla bila ya hata sababu za msingi. Hali iliyomuumiza sana Mwanadada huyu mpaka kupelekea kuhitaji msaada wa kisaikolojia (niliambiwa na watu wake wa karibu).
Siku zikapita kila Mtu akiendelea na maisha yake....baadae Dada alipata Mtu mwingine na sasa ana maisha yake na wana Watoto wawili.
Baada ya kupoteana kwa muda niliamua kumtafuta kisirisiri kujua yuko wapi na anaendeleaje kwani Mimi niliacha kazi kwenye ile kampuni nae nikasikia baadae aliacha.
Baada ya sakasaka ya muda karibia miaka miwili hatimae nilimpata kwenye facebook akitumia jina tofauti kabisa...na nilimshtukia kupitia comment yake kwenye ukurasa wa Mtu.
Nilianza kwa kucomment na ku like kwenye post zake mwishowe aligundua ni mimi...kinyume na matarajio yangu Dada akaonesha amefurahi sana na tukaanza kuwasiliana. Kutoka hapo tumekuwa tunawasiliana mara kwa mara huku mimi nikiwa muoga kumtonesha kidonda cha yaliyopita kwani ni dhahiri ya kuwa nilimuumiza sana mpaka nikikumbuka najiona sifai....nakumbuka neno la mwisho alinitumia kwenye meseji wakati huo "wewe ni shetani...wewe ni muuaji"
Kwa sasa huwa tunafuatana facebook ku comment na ku like, na mara moja moja huwa anakuja inbox...mimi kama mimi sijawahi kuanza kwenda inbox ila kuna siku niki comment kwenye post yake yeye anakuja inbox na tunachati hili na lile.
Kuna wakati atapost yupo kwenye bata na Wanae au Rafiki yake/zake, niki comment tu yeye ata comment "njoo".....mimi naishia tu kusema "nipo mbali ningekuja".
Kwa sasa mambo yake ni safi kwani ni boss kwenye kampuni anayoifanyia kazi na ameanzisha kampuni yake ya utalii.
Bado sijaelewa kama ananikaribisha ki roho safi pamoja na nilichomfanyia miaka kadhaa nyuma. Ingawa nimeshawahi kumuuliza kama alishanisamehe akaniambia yaliyopita yamepita tuachane nayo.....Huo moyo ndio bado nimeuogopa.
Ningekuwa sijamtenda ningekuwa huru hata kumwambia anipige tafu maana mambo yake safi huku mimi nachechemea.
Miaka kama tisa iliyopita nilikuwa kwenye mahusiano na Mwanadada mmoja tuliyekuwa tunafanya nae kazi kwenye kampuni moja.
Ndani ya miaka mitatu mapenzi yetu yalikuwa motomoto kabla ya Mimi kuamua kujitoa ghafla bila ya hata sababu za msingi. Hali iliyomuumiza sana Mwanadada huyu mpaka kupelekea kuhitaji msaada wa kisaikolojia (niliambiwa na watu wake wa karibu).
Siku zikapita kila Mtu akiendelea na maisha yake....baadae Dada alipata Mtu mwingine na sasa ana maisha yake na wana Watoto wawili.
Baada ya kupoteana kwa muda niliamua kumtafuta kisirisiri kujua yuko wapi na anaendeleaje kwani Mimi niliacha kazi kwenye ile kampuni nae nikasikia baadae aliacha.
Baada ya sakasaka ya muda karibia miaka miwili hatimae nilimpata kwenye facebook akitumia jina tofauti kabisa...na nilimshtukia kupitia comment yake kwenye ukurasa wa Mtu.
Nilianza kwa kucomment na ku like kwenye post zake mwishowe aligundua ni mimi...kinyume na matarajio yangu Dada akaonesha amefurahi sana na tukaanza kuwasiliana. Kutoka hapo tumekuwa tunawasiliana mara kwa mara huku mimi nikiwa muoga kumtonesha kidonda cha yaliyopita kwani ni dhahiri ya kuwa nilimuumiza sana mpaka nikikumbuka najiona sifai....nakumbuka neno la mwisho alinitumia kwenye meseji wakati huo "wewe ni shetani...wewe ni muuaji"
Kwa sasa huwa tunafuatana facebook ku comment na ku like, na mara moja moja huwa anakuja inbox...mimi kama mimi sijawahi kuanza kwenda inbox ila kuna siku niki comment kwenye post yake yeye anakuja inbox na tunachati hili na lile.
Kuna wakati atapost yupo kwenye bata na Wanae au Rafiki yake/zake, niki comment tu yeye ata comment "njoo".....mimi naishia tu kusema "nipo mbali ningekuja".
Kwa sasa mambo yake ni safi kwani ni boss kwenye kampuni anayoifanyia kazi na ameanzisha kampuni yake ya utalii.
Bado sijaelewa kama ananikaribisha ki roho safi pamoja na nilichomfanyia miaka kadhaa nyuma. Ingawa nimeshawahi kumuuliza kama alishanisamehe akaniambia yaliyopita yamepita tuachane nayo.....Huo moyo ndio bado nimeuogopa.
Ningekuwa sijamtenda ningekuwa huru hata kumwambia anipige tafu maana mambo yake safi huku mimi nachechemea.