Elton Tonny
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 396
- 2,976
- Thread starter
-
- #301
FOR YOU
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Luteni Jenerali Weisiko anaanza kufumbua macho yake taratibu, naye anatambua kwamba yuko ndani ya chumba fulani chenye giza kiasi. Anahisi kizunguzungu kichwani, naye anapojaribu kujishika kichwa, anatambua kwamba mikono yake imefungwa nyuma ya mgongo wake. Akakisawazisha vizuri zaidi kichwa chake na kuanza kuhisi vyema hali aliyokuwa ndani yake. Sasa akatambua kuwa alikuwa ameketi kwenye kiti cha chuma, mikono na miguu yake ikiwa imefungwa kwa kamba nene na ngumu sana, na chumba alichokuwemo kilikuwa ndani ya jengo kubwa lililoonekana kama "godown" au "warehouse." Alipozoesha macho yake vizuri ndani hapo, aliona mbao nyingi pembezoni mwa jengo hilo na vifaa mbalimbali vya ujenzi, naye akawa anajaribu kujivuta kwa nguvu sana lakini ikawa kazi bure.
Akaanza kupiga kelele akiita wale waliomfanyia hivi wafike kumfungulia haraka sana, naye akashtukia anapondwa na kopo dogo la bati la soda ya sprite, bila kumwona aliyemponda.
"Nani wewe? Jitokeze mpumbavu wewe! Unaogopa nini? Njoo!" Weisiko akasema.
Lakini hakujibiwa, bali kopo la namna hiyo hiyo likamponda tena kichwani.
"Mnataka kucheza mchezo na mimi washenzi nyie? Najua tayari kwamba ni nyie Mess Makers... hamna haja ya kujificha. Tena nawashangaa mmenifunga halafu bado mnajificha. Gut zenu zilibumbwa kwa kutumia roho za kuku, au?" Weisiko akauliza kwa kujiamini.
Akapondwa tena na kopo kama awali, naye akakasirika sana. Aliona alikuwa anafanyiwa mchezo wa kitoto, na angefanya yote awezayo ili kuukomesha.
"Mnajua nini? Hapa mnajisumbua tu aisee. Hamjui kama kunileta huku ni matatizo kwenu, kwa sababu hata kama mkifanya nini, bado mtavurugwa tu. Na ninawahakikishia, huko kuvurugwa kumeshaanza," Weisiko akasema.
"Nani avurugwe, malaya wewe?"
Weisiko akaisikia sauti hiyo ikiuliza. Ilikuwa ya mwanaume, na ilitokea sehemu ya mbele zaidi kutokea alipokuwa amekaa, na kwa sababu kwa huko palikuwa na giza zaidi, hakuweza kumwona.
"Unaogopa nini sasa kaka? Kama unaniona malaya kweli, nifate. Ukikaa huko utakulaje utamu?" Weisiko akasema kwa kejeli.
Sauti za hatua zikaanza kusikika zikimfata Weisiko, na hapo akaanza kumwona mwanaume fulani ambaye alimtambua kwa uharaka. Ilikuwa ni Victor. Akawa anamfata taratibu, huku mikononi akiwa ameshikilia makopo mengine mawili ya sprite, naye akasimama mbele yake huku akimtazama kwa makini. Weisiko akawa anamwangalia kwa hasira sana, naye Victor akamponda na kopo moja kichwani huku akitabasamu kwa kejeli.
"Ningetarajia mzee mtu mzima kama wewe uwe na hekima ya kutosha kutocheza michezo ya kitoto namna hii. Unajitafutia kifo chenye maumivu sana," Weisiko akasema kwa utulivu.
"Malaya wangu, si umeniita nije kula utamu? Nimekuja halafu unasema nacheza kitoto tena?" Victor akasema kwa dharau.
"Nifungulie basi nikupe huo utamu," Weisiko akamwambia.
"Hakuna haja ya kukufungulia. Nakuja tu kwa nyuma," Victor akasema.
Akazunguka mpaka sehemu ya nyuma alipoketi Weisiko na kuanza kumshika-shika sehemu ya makalio, naye Weisiko akaanza kumtukana huku akijaribu kujinasua.
"Ahahahahah.... utamu wenyewe wa kubabaiiisha..." Victor akamkejeli Weisiko na kuanza kumtekenya.
Weisiko akawa anatukana huku akijivuta huku na huku, na hii ikasababisha aangukie upande mmoja pamoja na kiti chake.
Victor akaendelea kucheka tu na kusema, "Hapo sasa ndiyo umejiweka vizuri. Yaani kama ni utamu nitaula wote."
Akasogea karibu na mwili wa Weisiko na kuanza tena kumtekenya na kumkandamiza makalioni.
"Naona unapata some fun," sauti ya Mensah ikasikika.
Victor akaacha kumchezea Weisiko na kusimama, akimwona Mensah anaingia.
"Yeah, ilikuwa kidogo tu upitwe. Karibu ujiunge nami, nimeahidiwa kupewa utamu hapa," Victor akasema.
"Well save that for later," Mensah akamwambia.
"Mbona umerudi?" Victor akauliza.
"Lexi amenipigia, kasema boss na akina Torres wameshamkamata Jacob kabla hawajafika kule, kwa hiyo wanarudi pia. Wanakuja huku," Mensah akasema.
Weisiko akashangaa kiasi.
"About time. Lakini... mbona kama vile wamefanya upesi sana?" Victor akasema.
"Inaonekana jamaa aliwahi kupita pale wakamnasa... tutajua wakifika," Mensah akamwambia.
Mensah akasaidiana na Victor kunyanyua kiti alichofungwa Weisiko na kukiweka sawa tena, naye Weisiko akawa anapumua kwa hasira sana.
"Mzee wa jeuri, imekupata fresh?" Mensah akamuuliza Luteni Jenerali Weisiko.
Weisiko akamwangalia kwa hasira sana, na ni hapa ndiyo watatu hawa wakaanza kusikia hatua za watu wengine wakija. Weisiko akatazama kwa makini sana mlangoni kule pasikoonekana vyema, na hapo akaanza kuwaona watu wawili aliowafahamu vizuri sana. Lakini alitambua kwamba kulikuwa na mtu wa tatu ambaye alibaki sehemu ile ya mlangoni, na hawa wawili hawakuwa wengine ila Lexi pamoja na Nora. Wakafika mbele yake na kusimama, wakiwa wanamtazama kwa umakini sana. Weisiko akaachia tabasamu la kiburi, lakini kihalisi alikuwa bado anastaajabishwa na ukweli wenyewe wa kuwa "mwanamke" huyo alikuwa hai muda wote huo ambao alifikiri hakuwepo tena duniani.
"Ama kweli... ukistaajabu ya Musa, utayaona ya mfiraji wake. Yaani sasa naamini kuna miujiza kwenye hii dunia," Weisiko akawaambia.
"Na bado," akasema Victor.
"Alexandra Casmir! Aah! Mama la mama. Umerudi kutoka kuzimu hata salamu tu ukashindwa kutuma?" Weisiko akasema.
Hakuna mtu aliyemjibu, bali wote wakabaki kumwangalia tu.
"Ahah... kikundi chenu mlichounda kwa kweli naweza kusema ni kizuri sana. Mmetupa shida, lakini mnapaswa kujua bado hamjashinda. Hata kama mtaamua kuniua mimi, bado hamtaweza kutoka ndani ya haya yote salama," Weisiko akaongea.
"Umekuwa ukisaidiana na Jenerali wako kuharibu maisha ya watu wengi. Miaka yako yote uliyotumiwa kama mbwa imekufikisha wapi Weisiko?" Nora akauliza.
"Sehemu nyingi ambazo haungeweza kuwazia binti. Na wewe hauna lolote. Ni mnafiki mkubwa, msaliti, usiyestahili kubeba jina la baba yako," Weisiko akamwambia.
"Ninafurahi sana kujua matendo ya huyo mwanaume, kwa sababu kuliondoa jina lake kwenye langu Imekuwa justified hata zaidi sasa," akasema Nora.
Weisiko akamtazama sana Lexi, akiona ni jinsi gani alimwangalia kwa chuki kali.
"Unaangalia nini? Nimejinyea?" Weisiko akamuuliza.
"Ni nini kilichokufanya ukamchukua mdogo wangu na kumwekea vitu vingi vya kipuuzi kwenye akili na maisha yake?" Lexi akamuuliza.
"Ahah... ahahahah... nilidhani ungenishukuru kwa kuahirisha kumuua mdogo wako lakini kumbe na hilo hujapenda? Unge-prefer kama ningekuwa nimemuua?" Weisiko akaongea.
"Nikushukuru kwa lipi? Kuwaua wazazi wangu na dada zangu kulikupa faida gani ambayo ni ya kudumu?"
"Kwani hujui? Kwa mambo mengi we si unajifanya mjuzi sana, unashindwa vipi kujua kuhusu hilo? Halafu... Mary nilimgeuza kuwa kile ambacho alitakiwa kuwa sikuzote, na akawa kamili zaidi tofauti na vile yeyote angetazamia..."
"Jina lake ni Azra... siyo Mary..."
"Yeye ni Mary! Ni mwanangu, na atabaki kuwa mwanangu tu!" Weisiko akafoka.
"Huyu jamaa mpumbavu sana," Mensah akasema.
"Mpumbavu ni wewe," Weisiko akamwambia.
Mensah akamsogelea na kumtandika ngumi mbili nzito usoni, naye Weisiko akahisi maumivu lakini akawa anacheka huku mdomo wake ukidondosha damu nzito.
"Ahahahah... ssss... yule siyo mdogo wako tena. Yule ni silaha yangu. Hata kama mngemfanya nini, hangeweza kamwe kukubali wewe ni dada yake. Hajui mtu yeyote zaidi ya mimi, na itaendelea kubaki hivyo upende usipende," Weisiko akamwambia Lexi.
"Kwa hiyo haukumwokoa kwa sababu ya hisia, ila tu kumfanya awe kama mwanasesere wako. Ulikuwa radhi kujiaminisha kwamba unamlea kama binti yako, ila yale yalikuwa ni majuto tu kwa sababu ulishindwa kumlea binti yako wa kumzaa mwenyewe," Nora akasema.
"Chunga maneno yako," Weisiko akasema.
"Au utamfanya nini? Yeye ndiyo alikutuma umuue wa kwako halafu uchukue wa mwingine kumlea baada ya kuwaua wazazi wake?" Victor akamuuliza.
"Mshenzi wewe! Nani amekwambia nilimuua? Nifungue hapa nikuonyeshe!" Weisiko akafoka huku akijivuta-vuta.
Victor akacheka.
"Mary mmemweka wapi? Niambieni!" Weisiko akauliza.
"We unafikiri tumemweka wapi?" akauliza Victor.
"Anajifanya anamjali sana," Mensah akaongea.
"Ulifanya nini mpaka ukaharibu kumbukumbu zake?" Lexi akauliza.
"Haikuhusu. Tambua kwamba yule hakufahamu tena, na wala hawezi kamwe kukukumbuka tena kwa sababu nilihakikisha chembe zozote zile zilizobaki za kumbukumbu kuwahusu nyie nimeziondoa kichwani kwake... kwa hiyo...."
Kabla Weisiko hajamaliza kuongea, yule mtu mwingine aliyekuwa amesimama kule kwenye mwingilio wa jumba hilo akawa ameanza kuelekea upande wao, na taratibu Weisiko akatambua ilikuwa ni Azra. Aliishia kumwangalia tu usoni kadiri alivyowasogelea, na wasiwasi ukamwingia kwa kuwa alijua kila kitu alichokisema, mwanadada huyu alikisikia. Azra akasimama usawa wa Lexi na kumwangalia Weisiko kwa hisia tata, huku Weisiko akijaribu kutabasamu.
"Ahah... Mary... Mary help me. These sickos want to kill me (Mary nisaidie.. hawa wagonjwa wa akili wanataka kuniua)," Weisiko akamwambia.
"You're such a sicko yourself not realizing how huge of a fool you're making yourself look (we ndiyo mgonjwa wa akili kutotambua ni jinsi gani unavyojionyesha kuwa mpuuzi mkubwa)," Mensah akamwambia.
"Mary nisikilize. Don't listen to whatever these people have told you... I'm..."
"Hatujamwambia lolote mjinga wewe. Ametoka tu kuthibitisha ukweli yeye mwenyewe kwa kila kitu ulichokisema," Victor akamwambia.
"Mary... Mary... Mary please..." Weisiko akaendelea kuomba.
"No. I'm not Mary. My name is Azra," Azra akasema.
Weisiko akakunja sura kimaswali, akiwa kama mtu ambaye haamini kile alichosikia.
"Mary, I'm your father. Umesahau... have you forgotten all the time we spent together? Usiwasikilize hawa, I'm the one who raised you (mimi ndiyo niliyekulea)," Weisiko akamwambia.
"To be your weapon? To be... a killer? (Ili kuwa silaha? Kuwa.. muuaji?)" Azra akauliza.
Lexi alikuwa anamwangalia Weisiko kwa hasira kuu.
"I took care of you because I love you. You... you're my daughter... (Nilikutunza kwa kuwa nakupenda. Wewe ni binti yangu...)"
"F(...) you," Azra akamkatisha.
Mensah na Victor wakacheka.
"You know... I put up with all of your shit all that time because I really thought I had only you. You... you killed my parents, and then fed me all the lies, made me into a weapon to kill for you... and now you admit that you erased my memory. You think I care a damn about what you did to keep me alive? Ahah... it would've been better if you just killed me that night, because now I'm gonna make sure you never see tomorrow's light," Azra akaongea kwa hisia.
Weisiko akawa anamtazama kwa hasira sana. Azra akarudisha mkono wake nyuma ya kiuno chake na kutoa bastola yake, kisha akaikoki na kuendelea kuishikilia kiganjani.
"Mary... kweli... unaweza kufikiria kuniua mimi?" Weisiko akauliza.
"Just give me the word, I'll be more than happy to put a hole in his head (naomba uniruhusu tu, itakuwa ni zaidi ya furaha kwangu kukitoboa kichwa chake)," Azra akamwambia Lexi.
"Wait, we shouldn't do that yet (subiri, tusifanye hivyo kwanza)," Nora akasema.
"Kinachowafanya msubiri ni nini? Kama mnataka kuniua, niueni sasa hivi," Weisiko akasema.
"Tulia nyau wewe, utakufa tu," Mensah akasema.
"Why wait? If you want to kill me dear, go ahead, do it now," Weisiko akamwambia Azra, akimshurutisha amuue.
Lexi na Azra wakawa wanamtazama kwa hisia kali sana.
"Ahahahah... hii dynamic duo inawapendeza. Wazazi wenu wangekuwepo sasa hivi, wangekuwa proud. Too bad niliwaondoa duniani mapema sana," Weisiko akamwambia Lexi.
"Ah..."
Lexi akatoa sauti hiyo na kunyoosha kiganja chake kumwelekea Azra, naye Azra akampatia bastola yake na hapo hapo Lexi akainyoosha kuelekea kichwa cha Weisiko kwa hasira sana.
"Wait, wait, wait, wait, subiri, Lexi..." Nora akasema haraka kumzuia.
Lexi alikuwa amekasirishwa sana na maneno ya mwanaume huyo. Kila kitu kuhusu jinsi mwanaume huyu alivyowaua wazazi wake kilirudi kwenye akili yake, na tamaa kubwa ya kutaka kumuua pia ilikuwa imemlemea sana. Weisiko akawa anamwangalia kwa jeuri huku bastola ikiwa katikati ya usawa wa macho yake.
"Lexi... please, tuwasubiri wengine kwanza... then tutaamua cha kumfanya," Nora akamwomba.
Lexi akawa bado ameielekeza bastola kwa mwanaume huyo huku amekaza meno yake kwa hasira.
"Mhm... ni bora kama ungeniua sasa hivi tu mpenzi, maana mkikaa kusu...."
Kabla ya Weisiko kumaliza kuongea, Lexi akafyatua risasi mbili haraka sana, naye Nora akashtuka na kurudi nyuma!
Zilifuata kelele za maumivu kutoka kwa Weisiko, kwa kuwa sasa hakuwa na sehemu za nje za masikio yake mawili. Lexi alizifyatua zote kwa kasi sana, naye Weisiko akawa analia kwa maumivu huku damu zikiruka kutokea pande mbili za kichwa, na sikio moja lilinyofoka kabisa, huku lingine likining'inia usawa wa taya. Azra akang'ata meno yake na kushusha pumzi kwa kuhisi mridhiko kiasi baada ya Lexi kumnyamazisha kiaina mwanaume huyo, huku Mensah na Victor wakitabasamu kwa kufurahia jambo hilo.
"Omba Yesu ashuke akurudishie hayo," Victor akamwambia Weisiko.
Jamaa akawa anaugulia maumivu huku amekaza macho yake na kupiga-piga miguu chini, naye Lexi akamgeukia Nora na kumwona jinsi alivyomtazama kwa hofu kiasi. Akamgeukia tu Azra na kumrudishia bastola yake, kisha akamsogelea karibu zaidi Luteni Jenerali asiyekuwa na masikio tena.
"Unakumbuka nilichokwambia usiku ule? Nilikwambia ningekuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe. Usijali. Sijaisahau hiyo ahadi," Lexi akasema na kusogea nyuma.
Azra akasogea karibu na Weisiko na kumtemea mate usoni, kisha akamwangalia Lexi kwa hisia machoni. Lexi akakishika kiganja cha mdogo wake ili kumtuliza hisia, naye Azra akamkumbatia. Nora hakupendezwa kwa kadiri fulani na jambo lililokuwa limetokea, naye akageukia upande mwingine na kuziba mdomo wake kwa kiganja. Moyo wake ulidunda kwa kasi, kwa kuwa masuala ya ukatili yalimhofisha sana, hata ingawa aliyefanyiwa hivyo wakati huu alikuwa mkatili kupitiliza. Lexi akamwachia Azra taratibu, kisha akamfata Nora na kumshika mabegani kutokea kwa nyuma, na Nora akitambua ilikuwa ni yeye, akavishika viganja hivyo kama njia ya kuonyesha ameikubali pole hiyo isiyo ya moja kwa moja.
Wakati huu sasa Weisiko alikuwa akiguna tu kwa maumivu, huku damu zikiendelea kutiririka taratibu, na ni hapa ndipo wote wakahisi hatua zikija kutokea kule kwenye mwingilio wa jengo hilo. Upesi Mensah na Victor wakatoa bastola zao na kuzielekeza upande huo, naye Nora akatoa yake pia na kuielekeza upande huo huo. Ni Lexi na Azra pekee ndiyo waliobaki kusimama wakiwa wanatazama upande huo bila kutoa silaha zao, na hatimaye hatua hizo zikafika mwanzoni mwa mlango na mtu huyo kuingia.
Ni baada ya kuona kwamba ilikuwa ni Kevin, ndiyo wengine wakashusha silaha zao. Akasimama tu huko huko huku akiwatazama wenzake kwa umakini, na jambo hili likampa Lexi hisia fulani mbaya.
"Oya vipi? Mmepitwa na uhondo huku," Victor akamuuliza.
"Bila shaka mambo yamekwenda vizuri upande wenu. Huyo bwege mlimkamata kwenye saa ngapi? Kabla hata giza halijaingia?" Mensah akauliza huku akianza kumfata Kevin.
Lexi akamzuia Mensah kwa kuweka mkono wake usawa wa tumbo lake ili asiendelee kwenda. Azra kuona hivyo, akatoa bastola yake na kuiweka mikononi kwa utayari. Jambo hili likafanya umakini wa Nora upande pia.
"Vipi?" Mensah akamuuliza Lexi.
Kevin akawa amesimama tu pale pale huku akiwatazama kwa mkazo.
"Kevin... boss yuko wapi?" Victor akauliza, naye akiwa amehisi kuna jambo haliko sawa.
"Usijali, tuko naye..."
Sauti hiyo iliyotoa hilo jibu, ilitokea nyuma yake Kevin, nayo iliwafanya wengine pale waitikie haraka sana kwa kutoa silaha zao na kunyoosha upande wa Kevin, isipokuwa Lexi, ambaye ingawa alikuwa amebeba bastola, hakuitoa kwa sababu ya kushangazwa na jambo hili. Ijapokuwa Weisiko alikuwa amekatwa masikio yake, bado aliweza kupokea mawimbi ya sauti vyema kutambua kuwa hiyo ilikuwa ni sauti ya Jenerali Jacob.
Kutokea nyuma yake Kevin, Jenerali Jacob alifika hapo na kusimama pembeni yake, akiwa anatabasamu kwa hila sana. Wengine wote wakawa wanashangaa sana kuona jambo hilo, wakiwa hawaelewi nini kinaendelea.
"What is this Kevin? Unafanya nini hiki?" Mensah akamuuliza kwa hasira.
"Itakuwa bora mkishusha silaha zenu ikiwa mnataka kuwaona wenzenu tena," Jenerali Jacob akasema.
"Itakuwa bora kama utafunga hilo domo la sivyo nitaumwaga ubongo wako!" Mensah akafoka kwa hasira.
"Huyu ndiye ambaye huwa hakosi shabaha?" Jenerali Jacob akamuuliza Kevin.
Kevin akatikisa kichwa mara moja kukubali.
"That son of a bitch is nothing but a backstabber! (Huyo mtoto wa malaya ni msaliti mkubwa sana!)" Azra akaongea kwa hasira, akimaanisha Kevin.
Nora alikuwa akimwangalia baba yake kwa hasira kuu machoni mwake.
"Uncle Kendrick yuko wapi?"
Swali hilo likatoka kinywani mwa Lexi hatimaye. Alikuwa akimuuliza Kevin, lakini jamaa akanyanyua tu kidevu juu huku anamtazama kwa kiburi.
"Binti ya Casmir. Nimesikia mengi kukuhusu. Kiukweli unanikumbusha wakati ule ambao...."
Mensah akafyatua risasi iliyopita usawa wa bega la kulia la Jenerali Jacob na kuchana sehemu ndogo ya koti alilokuwa amevaa, akikatisha maneno yake ambayo hayakuwa na maana yoyote.
"Ahahah... show off," Jenerali Jacob akasema huku anajiangalia begani.
"Ameuliza swali, jibu swali. The next shot I swear napasua kichwa chako!" Mensah akasema kwa hisia kali.
"Kuwa makini na unachoniambia kijana. Huenda ni hicho hicho ndiyo kikakupata wewe," Jenerali Jacob akasema.
Papo hapo wote wakashtushwa sana baada ya kichwa cha Mensah kutobolewa kwa kupigwa na risasi! Hakukuwa na mlio wa risasi, lakini upande wa juu wa jengo hilo kwenye kuta za pembeni kilipasuka kioo kimoja, na ni hapo ndipo risasi hiyo iliyopigwa kwa shabaha ya mbali ilipopita. Mensah akadondoka chini huku kichwa chake kikiwa kinatoa damu nyingi, na jambo hilo liliwahofisha sana wenzake. Jenerali Jacob akawa anatabasamu kwa sifa sana, naye Victor akataka kumfyatulia risasi, lakini papo hapo naye pia akapiga kelele za maumivu baada ya kupigwa kwa risasi kifuani, kisha kichwani!
Wengine walipotaka kutoa itikio la haraka, Jenerali Jacob akasema kwa sauti, "Msijaribu kufanya action yoyote kutuelekea, kwa sababu hizo ni drone, mkijongea tu, mmekwisha!" akasema Jenerali Jacob.
Nora, Azra na Lexi ndiyo waliokuwa wamebaki kusimama, na kilichokuwa kimewapata Mensah na Victor ni kitu ambacho kiliwaumiza sana. Weisiko akawa anatabasamu kwa kiburi huku bado akisikilizia maumivu ya masikio.
"Tupeni hizo silaha chini," akasema Jenerali Jacob.
Hapo hapo wakaanza kuingia wanaume wale wa Jenerali Jacob, wakiwaelekea wanawake wote kwa kuzingira. Idadi yao ilikuwa 11, na hatimaye wakawazunguka watatu hao huku wakiwaelekezea bunduki.
"Hakuna trick zozote zilizobaki kwenu tena, kwa hiyo fuateni ninachowaambia ikiwa bado mnataka kuendelea kupumua," Jenerali Jacob akasema.
"Ni afadhali kufa lakini siyo kukuomba wewe unusuru maisha yetu," Nora akasema kwa ujasiri.
"Siyo wote wanafikiria kama wewe mwanangu," Jenerali Jacob akasema, kisha akageuka nyuma.
Hatua zingine zikaanza kusikika zikija kutokea mlangoni, na baada ya kufika usawa wa Jenerali Jacob, Lexi akaingiwa na hofu kubwa. Ilikuwa ni Kendrick pamoja Torres, wakiwa wameshikiliwa na wanaume wawili-wawili. Walionekana kuchoka sana kwa kuwa walilegea haswa, huku sura zao zikiwa na vimbe ndogo-ndogo na michirizi ya damu, kuonyesha walikuwa wamepigwa mno. Walifungwa kwa gundi za karatasi midomoni, lakini hawakufungwa mikono wala miguu kwa sababu hawakuwa na nguvu mwilini kutokana na kupigwa sana, kutia ndani na risasi zilizokuwa zimetoboa miguu yao.
Lexi akakunja ngumi kwa nguvu akihisi hasira sana, kwa sababu aliona ni makosa yake kutotambua aina ya mtu Kevin aliyekuwa, na kuendelea kumwamini ilikuwa imewaponza wenzake, na sasa wote kwa ujumla.
"Ninatumaini... ingawa sote tunajua jinsi hii itakavyokwisha, angalau utataka kutumia muda kidogo na hawa wapendwa wako waliobaki badala ya ikiwa nitawaua tu haraka. Nadhani umeshachoka kuona watu unaowapenda wakifa mbele ya macho yako, siyo?" Jenerali Jacob akamsemesha Lexi.
Nora na Azra wakamwangalia Lexi kwa hisia, naye akatazama chini kwa huzuni.
Jenerali Jacob akatabasamu na kutoa ishara kwa vidole vyake, na wale wanaume waliowazunguka wanawake wakawafuata na kuwanyang'anya silaha zao. Walipoanza kulazimisha kuwafunga, Azra akaweka kipingamizi na kuanza kuwapiga wanaume hao kwa mitindo yake ya haraka, lakini mmoja wao akamtandika kwa chuma la bunduki nyuma ya kichwa chake, naye Azra akapoteza fahamu. Lexi alikuwa amevunjika sana moyo. Alikuwa amekazwa na wanaume wawili walioanza kumfunga, huku Nora naye wakimfanyia hivyo hivyo. Wanaume wengine wakaanza kumfungulia Luteni Jenerali Weisiko pale alipokuwa amefungwa, naye akanyanyuka hatimaye akiwa bado anahisi maumivu makali sehemu za masikio yake, lakini akajikaza kiume na kumsogelea Lexi alipokuwa ameshikiliwa. Jenerali Jacob pamoja na Kevin wakaanza kuelekea hapo pia, huku Kendrick na Torres wakikokotwa nyuma yao.
"Eti nilikwambia nitakuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe! Yako wapi?" Weisiko akamwambia Lexi kwa kejeli.
Kisha akampiga ngumi kwa nguvu sana tumboni iliyofanya Lexi ahisi maumivu makali mno. Lakini hata hakutoa sauti, bali akajikaza tu na kuendelea kutulia huku Nora akilia na kusema wamwache. Jenerali Jacob akawa amefika karibu na binti yake, naye akamtazama kwa hisia kali sana, na Nora vilevile akamwangalia kwa hasira. Jenerali Jacob akamwasha Nora kofi zito usoni, na wanaume wale wakaendelea kumshikilia kwa nguvu.
"Nimekutendea kwa fadhila toka mama yako alipoamua kujiondoa duniani na hii ndiyo shukrani yako kwangu? Haujui ni jinsi gani kila kitu ulichofanya kinavyonikumbusha maumivu aliyoacha mama yako," Jenerali Jacob akamwambia.
Nora akawa anapumua kwa hasira sana huku mdomo wake ukitiririsha damu.
"Lakini mimi bado ni baba yako. Hiyo mishipa yako bado ina damu yangu. Ni hicho tu ndiyo kinachofanya mpaka sasa uendelee kuwa hai," Jenerali Jacob akasema.
"Sihitaji unusuru maisha yangu. Nitakuwa na furaha zaidi ikiwa utaniua, kwa kuwa maumivu aliyopitia mama kwa sababu yako sijayasahau. Lakini nakuonya. Ukiendelea kuniacha mzima I swear... nitakuua mimi mwenyewe," akasema Nora.
"Ahahahah.... empty threats my love..."
Jenerali Jacob akiwa anasema hivyo, Weisiko akachukua bastola moja iliyokuwa chini na kuielekeza kwenye kichwa cha Lexi, akiwa na nia ya kukipasua haraka sana. Lexi alikuwa anamwangalia tu bila hofu.
"Weisiko... subiri," Jenerali Jacob akamzuia.
"Nimesubiri sana General. Hhh... niruhusu kusahihisha makosa niliyofanya miaka mingi iliyopita," Weisiko akamwambia.
"Usijali jembe langu. Kama ni kifo tu, atakipata. Lakini nataka kiwe kifo ambacho hakuna yeyote kati yao anaweza kutarajia," Jenerali Jacob akasema.
Akamsogelea Lexi karibu kabisa na uso wake.
"Kujisumbua huko kote kwa faida gani mwanangu? Mwisho wa siku umerudi tena kule kule ulikotoka. Ila kwa wakati huu... utatamani ingekuwa bora kama ungekufa kipindi hicho," Jenerali Jacob akamwambia.
"Hakuna kingine zaidi nitakachopoteza maishani kuliko kile ambacho ulikichukua kutoka kwangu... na unachotaka kuchukua sasa. Hata kama nitakufa, tayari nina amani moyoni, lakini hicho ni kitu ambacho kamwe wewe hautaweza kupata. Tokea mwanzo Mungu amekuwa pamoja nami, na mpaka wakati ambao pumzi yangu itakata ndiyo atakuwa amemalizana nami. Usifikiri wewe ni mkubwa kwa kila kitu. Mwisho wako unakuja. Na utakuwa mbaya kuliko unavyoweza kufikiria," Lexi akasema huku chozi likimtoka.
Jenerali Jacob akaanza kucheka sana, kisha akasema, "Umenikumbusha mambo mengi kuhusu baba yako. Alikuwa na maneno mazuri pia, lakini hayakumfikisha popote. Ninataka upate glimpse ndogo ya kile ninachoweza kufanya, na finally utambue kwamba kiburi chako hakijawaletea manufaa yoyote yale, kwa sababu sikuzote nitaendelea kuwa mkubwa... kuliko hata huyo Mungu wako."
Maneno ya mwanaume huyo yalijaa kufuru sana. Lexi alikuwa akimwangalia kwa hisia nzito, kisha Jenerali Jacob akarudi nyuma kidogo kuwapisha wanaume wengine wawili waliokuwa wameshikilia kamba, nao wakaifunga mikono na miguu ya Lexi. Kisha, wakatoa gundi ya karatasi nao wakaanza kuizungusha mwilini mwake Lexi, wakisaidizana na wale waliokuwa wamemshika ili kumfunga mwili mzima kuanzia mabegani mpaka miguuni. Akawa amebanwa kwenye mwili wake mwenyewe, asiweze kabisa kujongea kama vile sanamu, huku wanaume hao wakiendelea kumshikilia.
Kisha Jenerali Jacob akawaamuru wengine, yaani Weisiko na wale waliomshikilia Nora warudi nyuma mpaka usawa wake, nao wakatii. Bado Azra alikuwa amepoteza fahamu pale chini, na sasa wale wanaume wanne waliokuwa wamewashikilia Kendrick na Torres wakawasogeza mbele yake Lexi na kuwaachia, wakidondoka chini kwa kishindo. Wakawabandulia gundi mdomoni, nao wakawaacha hapo chini na kutoka kabisa ndani ya jengo hilo.
Lexi alikuwa anawatazama wenzake hao kwa hisia sana, huku akihisi hatia nyingi moyoni, kwa sababu alielewa walikuwa wanaandaliwa kwa ajili ya nini. Jenerali Jacob akatoa bastola kutoka kiunoni kwake na kuishikilia kiganjani.
"Unahitaji tiba mzee. Ni nani aliyekukata masikio?" Jenerali Jacob akamuuliza Weisiko.
"Huyo malaya," Weisiko akamwambia.
"Ahahah... mtoto wa moto huyu! Asingekuwa upande huo angependeza sana kuwa moja ya mikono yangu," Jenerali Jacob akasema.
"Lexi... my dear..."
Maneno hayo yskasikika kutoka kwa Kendrick, akiwa ameyasema kiuchovu sana. Lexi akamtazama chini hapo na kuendelea kudondosha machozi.
Kendrick akajitahidi kuunyanyua uso wake ili amtazame, kisha akamwambia, "Its okay. Tume... tumefika mbali pamoja. Angalau umefanikiwa kusaidia watu... wengi. I'm proud of you..."
Torres, bila kuweza kunyanyua shingo yake vizuri, akasema kwa sauti iliyokwaruza, "Lexi... I'm sorry..."
Jenerali Jacob akamkabidhi Kevin bastola hiyo, naye Kevin akamtazama kwa njia yenye maswali.
"Kill them," Jenerali Jacob akamwambia.
Kevin akatoa tabasamu lenye kuonyesha wasiwasi, naye akaipokea na kumwelekezea Torres.
"Kevin... why? Kwa nini umeamua kuwasaliti watu ambao walikuwa tayari kufa pamoja nawe kwa kupigania haki?" Nora akamuuliza kwa hasira kutokea nyuma yake.
Kevin akawa anasitasita kuvuta kifyatulio cha risasi, kwa sababu kuna sehemu fulani ya dhamiri yake ilikuwa inamsumbua kuhusiana na yote aliyokuwa amechagua kuyafanya. Akamwangalia Jenerali Jacob kwa hofu kiasi kutokana na jinsi yeye na wanaume wake walivyomtazama kwa hila. Akakikaza kiganja chake na kufyatua risasi iliyompiga Torres sehemu ya mgongo wake, naye akalegea zaidi na kulala chini kwa kutulia. Lexi alifumba macho na kuinamisha uso wake akihisi huzuni iliyoambatana na hasira kali sana, naye akafumbua macho na kumwangalia Kevin kwa hasira zaidi.
"Lexi..."
Lexi akashusha macho yake na kumwangalia Kendrick, aliyekuwa ameita hivyo huku amepiga magoti chini sasa.
"Its okay. Hii ikiwa ni mara ya mwisho kukuambia maneno haya... nataka tu ujue kuwa ninakupenda sana... sana Lexi. Hhh... ninajivunia sana kwa kutumia muda wote niliokuwa nimebakiza hapa duniani nikiwa nawe. Na ninafurahi sana, kwa sababu huu nauona kuwa ushindi. Nakupenda sana binti yangu. Ahah... nimejisahau. Nakuchukia sana binti yangu," Kendrick akamwambia kwa hisia.
Jenerali Jacob na Weisiko wakaanza kucheka kwa dharau kwa kuwa waliona maneno ya Kendrick kuwa ya kipuuzi.
Lexi akawa analia kwa kwikwi, naye akamwambia, "Nakuchukia pia uncle Kendrick."
Kendrick akatabasamu kwa kufarijika moyoni.
Jenerali Jacob akazungusha macho yake kwa dharau na kumwambia Kevin, "Well?"
Kevin akaelekeza bastola yake kwa Kendrick, na hapo hapo akafyatua risasi iliyompiga mwanaume huyo mgongoni na kumwangusha chini. Lexi akatoa sauti ya kilio mara moja na kubaki mdomo wazi tu, akilia kwa hisia sana. Nora alikuwa analia sana pia huku akimwangalia mpenzi wake, asijue la kufanya ili kumsaidia. Kwa sifa, Weisiko akaanza kuipiga risasi nyingi sana miili ya Kendrick na Torres huku akimwangalia Lexi na kucheka kwa sifa sana, naye Lexi akageukia pembeni huku akifumba macho kwa nguvu mpaka Weisiko alipomaliza risasi kwenye bastola yake.
"Unajisikia vizuri sasa?" Jenerali Jacob akamuuliza Weisiko.
"Ningefurahi zaidi kama ungeniruhusu niutie matundu mwili wa huyu malaya pia," akasema Weisiko.
"Usijali. Dawa yake inakuja," Jenerali Jacob akasema.
"Wewe ni mpumbavu! Haustahili kuitwa mwanadamu kwa ukatili huu unaofanya!" Nora akamwambia baba yake.
"Na huyu tumwiteje? Au umesahau kama na yeye aliua watu wengi pia?" Weisiko akamuuliza.
"Alimuua nani bila kuwa na sababu? Wewe na wenzako mliua mamia ya watu kwa sababu ya tamaa..."
"Funga domo lako we mtoto! Haujui ni kiasi gani baba yako amejitoa kwenu halafu wewe uje kusema maneno hayo yasiyo na shukrani," Weisiko akamwambia.
"Nimshukuru kwa lipi huyu? Pamoja na yote ambayo mmefanya bado mnajiona kuwa sahihi kabisa? Sikuwahi kukuomba fadhila yoyote, na wala sikuzihitaji. Lakini kama ni kitu nachotaka unipe sasa hivi, basi ni kifo nikiwa pamoja na Lexi. Niue nikiwa pamoja naye, ni hapo tu ndiyo nitakuwa na shukrani kwako," Nora akaongea kwa hisia sana.
Jenerali Jacob akashusha pumzi na kufumba macho yake kwa nguvu.
"Hebu mfungeni mdomo huo," Weisiko akawaambia wanaume waliomshika Nora, nao wakatii na kuuziba mdomo wa Nora kwa gundi ya karatasi. Inaonekana walikuwa nazo nyingi.
Wanaume wale wanne waliokuwa wametoka jengoni hapo dakika chache nyuma, wakarejea pamoja na mwanaume mwingine pia, yule yule Sniper wa Jenerali Jacob. Wenyewe walikuwa wamesaidizana kubeba sanduku refu na kubwa la mbao, lililoonekana kuwa zito mno, likiwa ndiyo lile lile ambalo walimletea Jenerali Jacob kama "mzigo wake" wakati ule yuko nyumbani. Sniper wa Jenerali Jacob ndiye aliyewaua Victor na Mensah kutokea nje muda mfupi nyuma, na wala hazikuwa "drone" kama Jenerali Jacob alivyodai. Wale wanaume wanne wakaliweka sanduku hilo mbele ya Jenerali Jacob, huku Nora, na hata Weisiko na Kevin wakijiuliza kulikuwa na nini ndani yake. Jenerali Jacob akatabasamu kwa hila sana huku akimwangalia Lexi, wakati huo Lexi akiwa ameinamisha tu uso wake kwa kupoteza matumaini.
Luteni Jenerali Weisiko alikuwa wa kwanza kutambua kuwa Azra alianza kurejesha fahamu zake muda huo. Akamtazama jinsi alivyoanza kujigeuza taratibu, na baada ya Kevin kuona ameanza kujongea, yeye pamoja na wanaume wa Jenerali Jacob wakaelekeza silaha zao kwake ili wampige na risasi, lakini Weisiko akawazuia.
"Mfungeni tu huyo. Msimuue," Weisiko akawaambia.
"Lakini... lakini...." Kevin akawa haelewi.
Jenerali Jacob akamwangalia Weisiko kimaswali pia.
"General... unajua umuhimu wake. Popote tutakapoenda nitahakikisha tunaendelea kumtumia," Weisiko akamwambia.
"Lakini huyu ameshajua kila kitu... atawasaliti..."
"Kaa kimya dogo. Huyu ana umuhimu mara mia zaidi yako hapa. General... nitaziondoa tena kumbukumbu zake... nita...."
Jenerali Jacob akamkatisha kwa kunyanyua kiganja chake.
"Fanya jinsi moyo wako unavyotaka Weisiko. Hata mimi nafanya kile moyo unachotaka, siyo kichwa tu," Jenerali Jacob akasema hivyo huku amemwangalia Nora.
Wanaume watatu wakasaidizana kumfunga Azra kwa kamba, ambaye alianza kufurukuta huku akipiga kelele sana pasipo kufanikiwa kujinasua, na akihisi maumivu kichwani kwake pia. Wakamnyanyua na kumsogeza mpaka usawa wa Luteni Jenerali Weisiko, naye akamwangalia kwa ufupi, kisha akawapa ishara wanaume hao wampeleke kwa nyuma. Sasa wakawa wamebaki wanaume wawili waliokuwa wamemshikilia Lexi aliyefungwa mwilini, akiwa anamtazama Nora kwa hisia sana wakati huu.
"This is going to be incredible. You're gonna f(......) love this!" Jenerali Jacob akamwambia Weisiko kwa shauku.
Akatoa ishara kwa vidole, na wale wanaume waliokuwa wamemshikilia Lexi wakamwachia na kusababisha adondoke chini mzima mzima, akiwa wima lakini uso wake ukiangalia juu ili aone kile ambacho Jenerali Jacob alikuwa anataka kumfanyia. Jenerali Jacob akaanza kupeleka mkono wake taratibu kwenye sanduku hilo kubwa, lakini kabla hajalifungua, mmoja wa wanaume wake akamsogelea karibu na kumnong'oneza jambo fulani. Akasimama vizuri na kumwambia yeye na wengine wachache waelekee nje kuyaandaa magari upesi ili waondoke haraka. Weisiko alipouliza tatizo, Jenerali Jacob akasema kwamba wale waliokuwa wakiwasaka walikuwa karibu kuwafikia, hivyo wangetakiwa kuharakisha kuondoka hapo na kutoroka nchi haraka sana.
"Usjie kufikiri kwamba umepata tiketi ya kunusurika my dear, no, no, no... ni kwamba tu tunakuacha u-enjoy some quality time na rafiki yetu hapa," Jenerali Jacob akamwambia Lexi.
Akatoa ishara kwa wengine kwamba waanze kurudi nyuma, na kiukweli hofu iliwaingia wale wote ambao hawakuelewa alichokuwa anataka kufanya, na baada ya Weisiko, Kevin, Azra, Nora, na wanaume wengine kusogea nyuma, Jenerali Jacob akalifungua sanduku hilo na upesi kurudi nyuma pia mpaka usawa wa wengine.
Lexi alikuwa bado chini hapo akitazama kwa uzito sanduku hilo, na hangeweza kuzuia hofu yake kubwa kupanda baada ya kuona kichwa cha chatu kikitangulia kutoka nje ya sanduku hilo! Nora na Azra walishtuka sana, hata Weisiko na Kevin hawakuwa wametarajia hilo, huku Jenerali Jacob akitabasamu kikatili sana. Nora akaanza kupiga kelele za kilio zilizozibwa kwa karatasi ya gundi mdomoni mwake, huku Azra naye akilia kwa hisia ndani ya kiziba mdomo chake alichokuwa amewekewa pia.
Chatu huyo akawa anatoka taratibu kwenye sanduku hilo, na kadiri alivyozidi kutoka ndivyo wengine walivyozidi kuona jinsi alivyokuwa na mwili mnene sana uliokuwa na nguvu kubwa. Lexi akaanza kujiviringisha kwa kurudi nyuma, akijitahidi kukikimbia kifo hicho ambacho alielewa wazi kwamba hakukuwa na namna ya kukiepuka.
"Ohohooo... hapo ndiyo anamwalika vizuri zaidi. Wanapenda movement, na jamaa ana njaa kichizi," Jenerali Jacob akasema kikejeli na kuanza kucheka, lakini bila kutoa sauti.
Chatu yule akaendelea kumfata Lexi taratibu, kama hana haraka vile. Jenerali Jacob akamwangalia Nora machoni kama kumwambia kwamba kama hakuujua ukatili wake vizuri, hiyo ndiyo ingekuwa somo kwake. Kisha akaanza kuondoka hapo haraka na kutoa ishara kwa wengine waondoke pamoja naye. Nora na Azra walijitahidi kujinasua sana lakini ikawa kazi bure, nao wakakokotwa mpaka nje na kuelekea upande ambao kulikuwa na magari sita meusi na kila mmoja kuingizwa kwenye magari mawili tofauti. Nora alishangaa sana baada ya kuingizwa ndani ya gari na kumkuta mdogo wake, yaani Asteria. Akawa anataka kumuuliza nini kilimpata, lakini hawakuweza kusemeshana kutokana na wote kuwa wamezibwa midomo yao, na hivyo kubaki wanatazamana kwa huzuni sana, huku Asteria akionyesha wazi kwamba aliogopa mno kwa kulia sana.
Nora pia alilia sana, sana, sana. Alimwonea huruma sana Lexi, kumwacha akipambana na kifo kibaya sana ambacho hakuwa na hali yoyote ambayo ingemsaidia kukishinda. Lakini pia hali ambayo baba yake alikuwa amemwingiza Asteria ndani yake ilikuwa mbaya mno, kwa sababu binti huyo hakustahili kupitia mambo haya. Azra pia aliumia moyoni kupita maelezo, kwa sababu alielewa kwamba Lexi alikuwa ndiyo mtu wa mwisho kubaki kwenye familia yao, hivyo kumpoteza kulimaanisha anaachwa akiwa peke yake kwa mara nyingine tena na kwenda kuendelea kutumiwa kama silaha. Magari yote yaliondoka eneo hilo upesi na kuanza kuelekea upande mwingine kabisa.
Kule ndani ya jengo, Lexi alikuwa amejitahidi sana kujivuta-vuta na kujiburuza ili kumwepuka mnyama huyo mbaya sana, na kila mara alipotazama lilipokuwa, aliona jinsi lilivyojongea kwa njia ya umendeaji, kana kwamba lilikuwa linafurahia "kumwinda" kwa njia hiyo, ikionekana kama mchezo. Lexi alielewa wazi kwamba mbio zake kwenye sakafu hiyo zingeishia tu hatimaye kwenye ukingo, na hili likathibitika kuwa kweli baada ya kuufikia ukuta mwishoni kabisa kwenye jengo hilo. Alikuwa akihisi maumivu mengi, siyo mwilini, siyo moyoni. Alichoka sana. Akatulia tu hapo hapo, ikionekana kama vile amekubali kile kilichokuwa mbele yake, naye akaendelea kumtazama chatu huyo alipozidi kumkaribia.
Akafumba macho yake, naye akajisemea maneno haya moyoni: "Sandra... nimejitahidi kukimbia kwa muda mrefu, lakini nahisi huenda huu ndiyo utakuwa muda ambao natakiwa kusimama. Niliamua kuchukua maisha mapya ili nitimize ulichoniomba, lakini nimekuangusha pacha wangu. Nimewaangusha wote. Labda kusimama kwangu sasa itakuwa bora... ili niweze kupumzika pamoja nanyi."
Lexi aliweza kuhisi kitu fulani chenye umajimaji kikitekenya pua yake, naye akafumbua macho na kukutana uso kwa uso na chatu huyo, akiwa karibu zaidi na uso wake, huku ulimi wake ukitoka nje ya kinywa chake kilichofunga na kuilamba-lamba pua yake. Lexi aliogopa sana, na kwa kuelewa kwamba mnyama huyo alikuwa anajipa muda kujiburudisha na windo lake, yeye akaamua tu kufumba macho tena na kutulia, na labda hiyo ingesaidia kifo chake kisiwe chenye kuhofisha zaidi ya alivyodhani.
Ghafla, mlio mkali sana ukasikika kwenye ngoma za masikio yake, uliomshtua sana, lakini hakufumbua macho baada ya kuhisi vitu kama vimiminika vyenye ugumu fulani vikimwagika usoni mwake kwa njia fulani kama mtu aliyemwagiwa maji kwa nguvu. Viliambatana na sauti za vishindo kwenye sakafu ya hapo, na mapigo ya moyo wake Lexi yaliendelea kudunda kwa nguvu sana akiwa bado hajafumbua macho yake. Mwili wake uliokuwa umebanwa ulitetemeka sana, na taratibu akafumbua macho yake hatimaye.
Mbele yake sasa aliweza kuona mwili wa chatu huyo, ukiwa unajinyonga-nyonga taratibu bila mpangilio, na ilimchukua sekunde kadhaa kutambua kwamba sehemu ya kichwa cha mnyama huyo mbaya kilikuwa kimepasuka. Ilikuwa hali yenye kuhofisha sana! Hakuelewa ni nini kilikuwa kimetokea mpaka aliponyanyua macho yake na kutazama mbele zaidi, na hapo akamwona mtu akisogea upande wake taratibu huku ameelekeza bunduki upande wake.
Lexi akakaza macho yake kwa mtu huyo, na sasa sura yake ikaanza kuonekana vyema hata zaidi. Ilikuwa ni Luteni Michael!
★★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893
Story by Elton Tonny
Familia, Urafiki, Mapenzi, Tamaa, Hila, Usaliti, Unyanyasaji, Uhalifu, Mauaji, Visasi, Vita, Mambo yasiyotazamiwa
R-rated 18+
Enjoy!
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
SEHEMU YA HAMSINI NA MOJA
★★★★★★★★★★★★★★★★★★
Luteni Jenerali Weisiko anaanza kufumbua macho yake taratibu, naye anatambua kwamba yuko ndani ya chumba fulani chenye giza kiasi. Anahisi kizunguzungu kichwani, naye anapojaribu kujishika kichwa, anatambua kwamba mikono yake imefungwa nyuma ya mgongo wake. Akakisawazisha vizuri zaidi kichwa chake na kuanza kuhisi vyema hali aliyokuwa ndani yake. Sasa akatambua kuwa alikuwa ameketi kwenye kiti cha chuma, mikono na miguu yake ikiwa imefungwa kwa kamba nene na ngumu sana, na chumba alichokuwemo kilikuwa ndani ya jengo kubwa lililoonekana kama "godown" au "warehouse." Alipozoesha macho yake vizuri ndani hapo, aliona mbao nyingi pembezoni mwa jengo hilo na vifaa mbalimbali vya ujenzi, naye akawa anajaribu kujivuta kwa nguvu sana lakini ikawa kazi bure.
Akaanza kupiga kelele akiita wale waliomfanyia hivi wafike kumfungulia haraka sana, naye akashtukia anapondwa na kopo dogo la bati la soda ya sprite, bila kumwona aliyemponda.
"Nani wewe? Jitokeze mpumbavu wewe! Unaogopa nini? Njoo!" Weisiko akasema.
Lakini hakujibiwa, bali kopo la namna hiyo hiyo likamponda tena kichwani.
"Mnataka kucheza mchezo na mimi washenzi nyie? Najua tayari kwamba ni nyie Mess Makers... hamna haja ya kujificha. Tena nawashangaa mmenifunga halafu bado mnajificha. Gut zenu zilibumbwa kwa kutumia roho za kuku, au?" Weisiko akauliza kwa kujiamini.
Akapondwa tena na kopo kama awali, naye akakasirika sana. Aliona alikuwa anafanyiwa mchezo wa kitoto, na angefanya yote awezayo ili kuukomesha.
"Mnajua nini? Hapa mnajisumbua tu aisee. Hamjui kama kunileta huku ni matatizo kwenu, kwa sababu hata kama mkifanya nini, bado mtavurugwa tu. Na ninawahakikishia, huko kuvurugwa kumeshaanza," Weisiko akasema.
"Nani avurugwe, malaya wewe?"
Weisiko akaisikia sauti hiyo ikiuliza. Ilikuwa ya mwanaume, na ilitokea sehemu ya mbele zaidi kutokea alipokuwa amekaa, na kwa sababu kwa huko palikuwa na giza zaidi, hakuweza kumwona.
"Unaogopa nini sasa kaka? Kama unaniona malaya kweli, nifate. Ukikaa huko utakulaje utamu?" Weisiko akasema kwa kejeli.
Sauti za hatua zikaanza kusikika zikimfata Weisiko, na hapo akaanza kumwona mwanaume fulani ambaye alimtambua kwa uharaka. Ilikuwa ni Victor. Akawa anamfata taratibu, huku mikononi akiwa ameshikilia makopo mengine mawili ya sprite, naye akasimama mbele yake huku akimtazama kwa makini. Weisiko akawa anamwangalia kwa hasira sana, naye Victor akamponda na kopo moja kichwani huku akitabasamu kwa kejeli.
"Ningetarajia mzee mtu mzima kama wewe uwe na hekima ya kutosha kutocheza michezo ya kitoto namna hii. Unajitafutia kifo chenye maumivu sana," Weisiko akasema kwa utulivu.
"Malaya wangu, si umeniita nije kula utamu? Nimekuja halafu unasema nacheza kitoto tena?" Victor akasema kwa dharau.
"Nifungulie basi nikupe huo utamu," Weisiko akamwambia.
"Hakuna haja ya kukufungulia. Nakuja tu kwa nyuma," Victor akasema.
Akazunguka mpaka sehemu ya nyuma alipoketi Weisiko na kuanza kumshika-shika sehemu ya makalio, naye Weisiko akaanza kumtukana huku akijaribu kujinasua.
"Ahahahahah.... utamu wenyewe wa kubabaiiisha..." Victor akamkejeli Weisiko na kuanza kumtekenya.
Weisiko akawa anatukana huku akijivuta huku na huku, na hii ikasababisha aangukie upande mmoja pamoja na kiti chake.
Victor akaendelea kucheka tu na kusema, "Hapo sasa ndiyo umejiweka vizuri. Yaani kama ni utamu nitaula wote."
Akasogea karibu na mwili wa Weisiko na kuanza tena kumtekenya na kumkandamiza makalioni.
"Naona unapata some fun," sauti ya Mensah ikasikika.
Victor akaacha kumchezea Weisiko na kusimama, akimwona Mensah anaingia.
"Yeah, ilikuwa kidogo tu upitwe. Karibu ujiunge nami, nimeahidiwa kupewa utamu hapa," Victor akasema.
"Well save that for later," Mensah akamwambia.
"Mbona umerudi?" Victor akauliza.
"Lexi amenipigia, kasema boss na akina Torres wameshamkamata Jacob kabla hawajafika kule, kwa hiyo wanarudi pia. Wanakuja huku," Mensah akasema.
Weisiko akashangaa kiasi.
"About time. Lakini... mbona kama vile wamefanya upesi sana?" Victor akasema.
"Inaonekana jamaa aliwahi kupita pale wakamnasa... tutajua wakifika," Mensah akamwambia.
Mensah akasaidiana na Victor kunyanyua kiti alichofungwa Weisiko na kukiweka sawa tena, naye Weisiko akawa anapumua kwa hasira sana.
"Mzee wa jeuri, imekupata fresh?" Mensah akamuuliza Luteni Jenerali Weisiko.
Weisiko akamwangalia kwa hasira sana, na ni hapa ndiyo watatu hawa wakaanza kusikia hatua za watu wengine wakija. Weisiko akatazama kwa makini sana mlangoni kule pasikoonekana vyema, na hapo akaanza kuwaona watu wawili aliowafahamu vizuri sana. Lakini alitambua kwamba kulikuwa na mtu wa tatu ambaye alibaki sehemu ile ya mlangoni, na hawa wawili hawakuwa wengine ila Lexi pamoja na Nora. Wakafika mbele yake na kusimama, wakiwa wanamtazama kwa umakini sana. Weisiko akaachia tabasamu la kiburi, lakini kihalisi alikuwa bado anastaajabishwa na ukweli wenyewe wa kuwa "mwanamke" huyo alikuwa hai muda wote huo ambao alifikiri hakuwepo tena duniani.
"Ama kweli... ukistaajabu ya Musa, utayaona ya mfiraji wake. Yaani sasa naamini kuna miujiza kwenye hii dunia," Weisiko akawaambia.
"Na bado," akasema Victor.
"Alexandra Casmir! Aah! Mama la mama. Umerudi kutoka kuzimu hata salamu tu ukashindwa kutuma?" Weisiko akasema.
Hakuna mtu aliyemjibu, bali wote wakabaki kumwangalia tu.
"Ahah... kikundi chenu mlichounda kwa kweli naweza kusema ni kizuri sana. Mmetupa shida, lakini mnapaswa kujua bado hamjashinda. Hata kama mtaamua kuniua mimi, bado hamtaweza kutoka ndani ya haya yote salama," Weisiko akaongea.
"Umekuwa ukisaidiana na Jenerali wako kuharibu maisha ya watu wengi. Miaka yako yote uliyotumiwa kama mbwa imekufikisha wapi Weisiko?" Nora akauliza.
"Sehemu nyingi ambazo haungeweza kuwazia binti. Na wewe hauna lolote. Ni mnafiki mkubwa, msaliti, usiyestahili kubeba jina la baba yako," Weisiko akamwambia.
"Ninafurahi sana kujua matendo ya huyo mwanaume, kwa sababu kuliondoa jina lake kwenye langu Imekuwa justified hata zaidi sasa," akasema Nora.
Weisiko akamtazama sana Lexi, akiona ni jinsi gani alimwangalia kwa chuki kali.
"Unaangalia nini? Nimejinyea?" Weisiko akamuuliza.
"Ni nini kilichokufanya ukamchukua mdogo wangu na kumwekea vitu vingi vya kipuuzi kwenye akili na maisha yake?" Lexi akamuuliza.
"Ahah... ahahahah... nilidhani ungenishukuru kwa kuahirisha kumuua mdogo wako lakini kumbe na hilo hujapenda? Unge-prefer kama ningekuwa nimemuua?" Weisiko akaongea.
"Nikushukuru kwa lipi? Kuwaua wazazi wangu na dada zangu kulikupa faida gani ambayo ni ya kudumu?"
"Kwani hujui? Kwa mambo mengi we si unajifanya mjuzi sana, unashindwa vipi kujua kuhusu hilo? Halafu... Mary nilimgeuza kuwa kile ambacho alitakiwa kuwa sikuzote, na akawa kamili zaidi tofauti na vile yeyote angetazamia..."
"Jina lake ni Azra... siyo Mary..."
"Yeye ni Mary! Ni mwanangu, na atabaki kuwa mwanangu tu!" Weisiko akafoka.
"Huyu jamaa mpumbavu sana," Mensah akasema.
"Mpumbavu ni wewe," Weisiko akamwambia.
Mensah akamsogelea na kumtandika ngumi mbili nzito usoni, naye Weisiko akahisi maumivu lakini akawa anacheka huku mdomo wake ukidondosha damu nzito.
"Ahahahah... ssss... yule siyo mdogo wako tena. Yule ni silaha yangu. Hata kama mngemfanya nini, hangeweza kamwe kukubali wewe ni dada yake. Hajui mtu yeyote zaidi ya mimi, na itaendelea kubaki hivyo upende usipende," Weisiko akamwambia Lexi.
"Kwa hiyo haukumwokoa kwa sababu ya hisia, ila tu kumfanya awe kama mwanasesere wako. Ulikuwa radhi kujiaminisha kwamba unamlea kama binti yako, ila yale yalikuwa ni majuto tu kwa sababu ulishindwa kumlea binti yako wa kumzaa mwenyewe," Nora akasema.
"Chunga maneno yako," Weisiko akasema.
"Au utamfanya nini? Yeye ndiyo alikutuma umuue wa kwako halafu uchukue wa mwingine kumlea baada ya kuwaua wazazi wake?" Victor akamuuliza.
"Mshenzi wewe! Nani amekwambia nilimuua? Nifungue hapa nikuonyeshe!" Weisiko akafoka huku akijivuta-vuta.
Victor akacheka.
"Mary mmemweka wapi? Niambieni!" Weisiko akauliza.
"We unafikiri tumemweka wapi?" akauliza Victor.
"Anajifanya anamjali sana," Mensah akaongea.
"Ulifanya nini mpaka ukaharibu kumbukumbu zake?" Lexi akauliza.
"Haikuhusu. Tambua kwamba yule hakufahamu tena, na wala hawezi kamwe kukukumbuka tena kwa sababu nilihakikisha chembe zozote zile zilizobaki za kumbukumbu kuwahusu nyie nimeziondoa kichwani kwake... kwa hiyo...."
Kabla Weisiko hajamaliza kuongea, yule mtu mwingine aliyekuwa amesimama kule kwenye mwingilio wa jumba hilo akawa ameanza kuelekea upande wao, na taratibu Weisiko akatambua ilikuwa ni Azra. Aliishia kumwangalia tu usoni kadiri alivyowasogelea, na wasiwasi ukamwingia kwa kuwa alijua kila kitu alichokisema, mwanadada huyu alikisikia. Azra akasimama usawa wa Lexi na kumwangalia Weisiko kwa hisia tata, huku Weisiko akijaribu kutabasamu.
"Ahah... Mary... Mary help me. These sickos want to kill me (Mary nisaidie.. hawa wagonjwa wa akili wanataka kuniua)," Weisiko akamwambia.
"You're such a sicko yourself not realizing how huge of a fool you're making yourself look (we ndiyo mgonjwa wa akili kutotambua ni jinsi gani unavyojionyesha kuwa mpuuzi mkubwa)," Mensah akamwambia.
"Mary nisikilize. Don't listen to whatever these people have told you... I'm..."
"Hatujamwambia lolote mjinga wewe. Ametoka tu kuthibitisha ukweli yeye mwenyewe kwa kila kitu ulichokisema," Victor akamwambia.
"Mary... Mary... Mary please..." Weisiko akaendelea kuomba.
"No. I'm not Mary. My name is Azra," Azra akasema.
Weisiko akakunja sura kimaswali, akiwa kama mtu ambaye haamini kile alichosikia.
"Mary, I'm your father. Umesahau... have you forgotten all the time we spent together? Usiwasikilize hawa, I'm the one who raised you (mimi ndiyo niliyekulea)," Weisiko akamwambia.
"To be your weapon? To be... a killer? (Ili kuwa silaha? Kuwa.. muuaji?)" Azra akauliza.
Lexi alikuwa anamwangalia Weisiko kwa hasira kuu.
"I took care of you because I love you. You... you're my daughter... (Nilikutunza kwa kuwa nakupenda. Wewe ni binti yangu...)"
"F(...) you," Azra akamkatisha.
Mensah na Victor wakacheka.
"You know... I put up with all of your shit all that time because I really thought I had only you. You... you killed my parents, and then fed me all the lies, made me into a weapon to kill for you... and now you admit that you erased my memory. You think I care a damn about what you did to keep me alive? Ahah... it would've been better if you just killed me that night, because now I'm gonna make sure you never see tomorrow's light," Azra akaongea kwa hisia.
Weisiko akawa anamtazama kwa hasira sana. Azra akarudisha mkono wake nyuma ya kiuno chake na kutoa bastola yake, kisha akaikoki na kuendelea kuishikilia kiganjani.
"Mary... kweli... unaweza kufikiria kuniua mimi?" Weisiko akauliza.
"Just give me the word, I'll be more than happy to put a hole in his head (naomba uniruhusu tu, itakuwa ni zaidi ya furaha kwangu kukitoboa kichwa chake)," Azra akamwambia Lexi.
"Wait, we shouldn't do that yet (subiri, tusifanye hivyo kwanza)," Nora akasema.
"Kinachowafanya msubiri ni nini? Kama mnataka kuniua, niueni sasa hivi," Weisiko akasema.
"Tulia nyau wewe, utakufa tu," Mensah akasema.
"Why wait? If you want to kill me dear, go ahead, do it now," Weisiko akamwambia Azra, akimshurutisha amuue.
Lexi na Azra wakawa wanamtazama kwa hisia kali sana.
"Ahahahah... hii dynamic duo inawapendeza. Wazazi wenu wangekuwepo sasa hivi, wangekuwa proud. Too bad niliwaondoa duniani mapema sana," Weisiko akamwambia Lexi.
"Ah..."
Lexi akatoa sauti hiyo na kunyoosha kiganja chake kumwelekea Azra, naye Azra akampatia bastola yake na hapo hapo Lexi akainyoosha kuelekea kichwa cha Weisiko kwa hasira sana.
"Wait, wait, wait, wait, subiri, Lexi..." Nora akasema haraka kumzuia.
Lexi alikuwa amekasirishwa sana na maneno ya mwanaume huyo. Kila kitu kuhusu jinsi mwanaume huyu alivyowaua wazazi wake kilirudi kwenye akili yake, na tamaa kubwa ya kutaka kumuua pia ilikuwa imemlemea sana. Weisiko akawa anamwangalia kwa jeuri huku bastola ikiwa katikati ya usawa wa macho yake.
"Lexi... please, tuwasubiri wengine kwanza... then tutaamua cha kumfanya," Nora akamwomba.
Lexi akawa bado ameielekeza bastola kwa mwanaume huyo huku amekaza meno yake kwa hasira.
"Mhm... ni bora kama ungeniua sasa hivi tu mpenzi, maana mkikaa kusu...."
Kabla ya Weisiko kumaliza kuongea, Lexi akafyatua risasi mbili haraka sana, naye Nora akashtuka na kurudi nyuma!
Zilifuata kelele za maumivu kutoka kwa Weisiko, kwa kuwa sasa hakuwa na sehemu za nje za masikio yake mawili. Lexi alizifyatua zote kwa kasi sana, naye Weisiko akawa analia kwa maumivu huku damu zikiruka kutokea pande mbili za kichwa, na sikio moja lilinyofoka kabisa, huku lingine likining'inia usawa wa taya. Azra akang'ata meno yake na kushusha pumzi kwa kuhisi mridhiko kiasi baada ya Lexi kumnyamazisha kiaina mwanaume huyo, huku Mensah na Victor wakitabasamu kwa kufurahia jambo hilo.
"Omba Yesu ashuke akurudishie hayo," Victor akamwambia Weisiko.
Jamaa akawa anaugulia maumivu huku amekaza macho yake na kupiga-piga miguu chini, naye Lexi akamgeukia Nora na kumwona jinsi alivyomtazama kwa hofu kiasi. Akamgeukia tu Azra na kumrudishia bastola yake, kisha akamsogelea karibu zaidi Luteni Jenerali asiyekuwa na masikio tena.
"Unakumbuka nilichokwambia usiku ule? Nilikwambia ningekuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe. Usijali. Sijaisahau hiyo ahadi," Lexi akasema na kusogea nyuma.
Azra akasogea karibu na Weisiko na kumtemea mate usoni, kisha akamwangalia Lexi kwa hisia machoni. Lexi akakishika kiganja cha mdogo wake ili kumtuliza hisia, naye Azra akamkumbatia. Nora hakupendezwa kwa kadiri fulani na jambo lililokuwa limetokea, naye akageukia upande mwingine na kuziba mdomo wake kwa kiganja. Moyo wake ulidunda kwa kasi, kwa kuwa masuala ya ukatili yalimhofisha sana, hata ingawa aliyefanyiwa hivyo wakati huu alikuwa mkatili kupitiliza. Lexi akamwachia Azra taratibu, kisha akamfata Nora na kumshika mabegani kutokea kwa nyuma, na Nora akitambua ilikuwa ni yeye, akavishika viganja hivyo kama njia ya kuonyesha ameikubali pole hiyo isiyo ya moja kwa moja.
Wakati huu sasa Weisiko alikuwa akiguna tu kwa maumivu, huku damu zikiendelea kutiririka taratibu, na ni hapa ndipo wote wakahisi hatua zikija kutokea kule kwenye mwingilio wa jengo hilo. Upesi Mensah na Victor wakatoa bastola zao na kuzielekeza upande huo, naye Nora akatoa yake pia na kuielekeza upande huo huo. Ni Lexi na Azra pekee ndiyo waliobaki kusimama wakiwa wanatazama upande huo bila kutoa silaha zao, na hatimaye hatua hizo zikafika mwanzoni mwa mlango na mtu huyo kuingia.
Ni baada ya kuona kwamba ilikuwa ni Kevin, ndiyo wengine wakashusha silaha zao. Akasimama tu huko huko huku akiwatazama wenzake kwa umakini, na jambo hili likampa Lexi hisia fulani mbaya.
"Oya vipi? Mmepitwa na uhondo huku," Victor akamuuliza.
"Bila shaka mambo yamekwenda vizuri upande wenu. Huyo bwege mlimkamata kwenye saa ngapi? Kabla hata giza halijaingia?" Mensah akauliza huku akianza kumfata Kevin.
Lexi akamzuia Mensah kwa kuweka mkono wake usawa wa tumbo lake ili asiendelee kwenda. Azra kuona hivyo, akatoa bastola yake na kuiweka mikononi kwa utayari. Jambo hili likafanya umakini wa Nora upande pia.
"Vipi?" Mensah akamuuliza Lexi.
Kevin akawa amesimama tu pale pale huku akiwatazama kwa mkazo.
"Kevin... boss yuko wapi?" Victor akauliza, naye akiwa amehisi kuna jambo haliko sawa.
"Usijali, tuko naye..."
Sauti hiyo iliyotoa hilo jibu, ilitokea nyuma yake Kevin, nayo iliwafanya wengine pale waitikie haraka sana kwa kutoa silaha zao na kunyoosha upande wa Kevin, isipokuwa Lexi, ambaye ingawa alikuwa amebeba bastola, hakuitoa kwa sababu ya kushangazwa na jambo hili. Ijapokuwa Weisiko alikuwa amekatwa masikio yake, bado aliweza kupokea mawimbi ya sauti vyema kutambua kuwa hiyo ilikuwa ni sauti ya Jenerali Jacob.
Kutokea nyuma yake Kevin, Jenerali Jacob alifika hapo na kusimama pembeni yake, akiwa anatabasamu kwa hila sana. Wengine wote wakawa wanashangaa sana kuona jambo hilo, wakiwa hawaelewi nini kinaendelea.
"What is this Kevin? Unafanya nini hiki?" Mensah akamuuliza kwa hasira.
"Itakuwa bora mkishusha silaha zenu ikiwa mnataka kuwaona wenzenu tena," Jenerali Jacob akasema.
"Itakuwa bora kama utafunga hilo domo la sivyo nitaumwaga ubongo wako!" Mensah akafoka kwa hasira.
"Huyu ndiye ambaye huwa hakosi shabaha?" Jenerali Jacob akamuuliza Kevin.
Kevin akatikisa kichwa mara moja kukubali.
"That son of a bitch is nothing but a backstabber! (Huyo mtoto wa malaya ni msaliti mkubwa sana!)" Azra akaongea kwa hasira, akimaanisha Kevin.
Nora alikuwa akimwangalia baba yake kwa hasira kuu machoni mwake.
"Uncle Kendrick yuko wapi?"
Swali hilo likatoka kinywani mwa Lexi hatimaye. Alikuwa akimuuliza Kevin, lakini jamaa akanyanyua tu kidevu juu huku anamtazama kwa kiburi.
"Binti ya Casmir. Nimesikia mengi kukuhusu. Kiukweli unanikumbusha wakati ule ambao...."
Mensah akafyatua risasi iliyopita usawa wa bega la kulia la Jenerali Jacob na kuchana sehemu ndogo ya koti alilokuwa amevaa, akikatisha maneno yake ambayo hayakuwa na maana yoyote.
"Ahahah... show off," Jenerali Jacob akasema huku anajiangalia begani.
"Ameuliza swali, jibu swali. The next shot I swear napasua kichwa chako!" Mensah akasema kwa hisia kali.
"Kuwa makini na unachoniambia kijana. Huenda ni hicho hicho ndiyo kikakupata wewe," Jenerali Jacob akasema.
Papo hapo wote wakashtushwa sana baada ya kichwa cha Mensah kutobolewa kwa kupigwa na risasi! Hakukuwa na mlio wa risasi, lakini upande wa juu wa jengo hilo kwenye kuta za pembeni kilipasuka kioo kimoja, na ni hapo ndipo risasi hiyo iliyopigwa kwa shabaha ya mbali ilipopita. Mensah akadondoka chini huku kichwa chake kikiwa kinatoa damu nyingi, na jambo hilo liliwahofisha sana wenzake. Jenerali Jacob akawa anatabasamu kwa sifa sana, naye Victor akataka kumfyatulia risasi, lakini papo hapo naye pia akapiga kelele za maumivu baada ya kupigwa kwa risasi kifuani, kisha kichwani!
Wengine walipotaka kutoa itikio la haraka, Jenerali Jacob akasema kwa sauti, "Msijaribu kufanya action yoyote kutuelekea, kwa sababu hizo ni drone, mkijongea tu, mmekwisha!" akasema Jenerali Jacob.
Nora, Azra na Lexi ndiyo waliokuwa wamebaki kusimama, na kilichokuwa kimewapata Mensah na Victor ni kitu ambacho kiliwaumiza sana. Weisiko akawa anatabasamu kwa kiburi huku bado akisikilizia maumivu ya masikio.
"Tupeni hizo silaha chini," akasema Jenerali Jacob.
Hapo hapo wakaanza kuingia wanaume wale wa Jenerali Jacob, wakiwaelekea wanawake wote kwa kuzingira. Idadi yao ilikuwa 11, na hatimaye wakawazunguka watatu hao huku wakiwaelekezea bunduki.
"Hakuna trick zozote zilizobaki kwenu tena, kwa hiyo fuateni ninachowaambia ikiwa bado mnataka kuendelea kupumua," Jenerali Jacob akasema.
"Ni afadhali kufa lakini siyo kukuomba wewe unusuru maisha yetu," Nora akasema kwa ujasiri.
"Siyo wote wanafikiria kama wewe mwanangu," Jenerali Jacob akasema, kisha akageuka nyuma.
Hatua zingine zikaanza kusikika zikija kutokea mlangoni, na baada ya kufika usawa wa Jenerali Jacob, Lexi akaingiwa na hofu kubwa. Ilikuwa ni Kendrick pamoja Torres, wakiwa wameshikiliwa na wanaume wawili-wawili. Walionekana kuchoka sana kwa kuwa walilegea haswa, huku sura zao zikiwa na vimbe ndogo-ndogo na michirizi ya damu, kuonyesha walikuwa wamepigwa mno. Walifungwa kwa gundi za karatasi midomoni, lakini hawakufungwa mikono wala miguu kwa sababu hawakuwa na nguvu mwilini kutokana na kupigwa sana, kutia ndani na risasi zilizokuwa zimetoboa miguu yao.
Lexi akakunja ngumi kwa nguvu akihisi hasira sana, kwa sababu aliona ni makosa yake kutotambua aina ya mtu Kevin aliyekuwa, na kuendelea kumwamini ilikuwa imewaponza wenzake, na sasa wote kwa ujumla.
"Ninatumaini... ingawa sote tunajua jinsi hii itakavyokwisha, angalau utataka kutumia muda kidogo na hawa wapendwa wako waliobaki badala ya ikiwa nitawaua tu haraka. Nadhani umeshachoka kuona watu unaowapenda wakifa mbele ya macho yako, siyo?" Jenerali Jacob akamsemesha Lexi.
Nora na Azra wakamwangalia Lexi kwa hisia, naye akatazama chini kwa huzuni.
Jenerali Jacob akatabasamu na kutoa ishara kwa vidole vyake, na wale wanaume waliowazunguka wanawake wakawafuata na kuwanyang'anya silaha zao. Walipoanza kulazimisha kuwafunga, Azra akaweka kipingamizi na kuanza kuwapiga wanaume hao kwa mitindo yake ya haraka, lakini mmoja wao akamtandika kwa chuma la bunduki nyuma ya kichwa chake, naye Azra akapoteza fahamu. Lexi alikuwa amevunjika sana moyo. Alikuwa amekazwa na wanaume wawili walioanza kumfunga, huku Nora naye wakimfanyia hivyo hivyo. Wanaume wengine wakaanza kumfungulia Luteni Jenerali Weisiko pale alipokuwa amefungwa, naye akanyanyuka hatimaye akiwa bado anahisi maumivu makali sehemu za masikio yake, lakini akajikaza kiume na kumsogelea Lexi alipokuwa ameshikiliwa. Jenerali Jacob pamoja na Kevin wakaanza kuelekea hapo pia, huku Kendrick na Torres wakikokotwa nyuma yao.
"Eti nilikwambia nitakuua kwa mikono yangu mimi mwenyewe! Yako wapi?" Weisiko akamwambia Lexi kwa kejeli.
Kisha akampiga ngumi kwa nguvu sana tumboni iliyofanya Lexi ahisi maumivu makali mno. Lakini hata hakutoa sauti, bali akajikaza tu na kuendelea kutulia huku Nora akilia na kusema wamwache. Jenerali Jacob akawa amefika karibu na binti yake, naye akamtazama kwa hisia kali sana, na Nora vilevile akamwangalia kwa hasira. Jenerali Jacob akamwasha Nora kofi zito usoni, na wanaume wale wakaendelea kumshikilia kwa nguvu.
"Nimekutendea kwa fadhila toka mama yako alipoamua kujiondoa duniani na hii ndiyo shukrani yako kwangu? Haujui ni jinsi gani kila kitu ulichofanya kinavyonikumbusha maumivu aliyoacha mama yako," Jenerali Jacob akamwambia.
Nora akawa anapumua kwa hasira sana huku mdomo wake ukitiririsha damu.
"Lakini mimi bado ni baba yako. Hiyo mishipa yako bado ina damu yangu. Ni hicho tu ndiyo kinachofanya mpaka sasa uendelee kuwa hai," Jenerali Jacob akasema.
"Sihitaji unusuru maisha yangu. Nitakuwa na furaha zaidi ikiwa utaniua, kwa kuwa maumivu aliyopitia mama kwa sababu yako sijayasahau. Lakini nakuonya. Ukiendelea kuniacha mzima I swear... nitakuua mimi mwenyewe," akasema Nora.
"Ahahahah.... empty threats my love..."
Jenerali Jacob akiwa anasema hivyo, Weisiko akachukua bastola moja iliyokuwa chini na kuielekeza kwenye kichwa cha Lexi, akiwa na nia ya kukipasua haraka sana. Lexi alikuwa anamwangalia tu bila hofu.
"Weisiko... subiri," Jenerali Jacob akamzuia.
"Nimesubiri sana General. Hhh... niruhusu kusahihisha makosa niliyofanya miaka mingi iliyopita," Weisiko akamwambia.
"Usijali jembe langu. Kama ni kifo tu, atakipata. Lakini nataka kiwe kifo ambacho hakuna yeyote kati yao anaweza kutarajia," Jenerali Jacob akasema.
Akamsogelea Lexi karibu kabisa na uso wake.
"Kujisumbua huko kote kwa faida gani mwanangu? Mwisho wa siku umerudi tena kule kule ulikotoka. Ila kwa wakati huu... utatamani ingekuwa bora kama ungekufa kipindi hicho," Jenerali Jacob akamwambia.
"Hakuna kingine zaidi nitakachopoteza maishani kuliko kile ambacho ulikichukua kutoka kwangu... na unachotaka kuchukua sasa. Hata kama nitakufa, tayari nina amani moyoni, lakini hicho ni kitu ambacho kamwe wewe hautaweza kupata. Tokea mwanzo Mungu amekuwa pamoja nami, na mpaka wakati ambao pumzi yangu itakata ndiyo atakuwa amemalizana nami. Usifikiri wewe ni mkubwa kwa kila kitu. Mwisho wako unakuja. Na utakuwa mbaya kuliko unavyoweza kufikiria," Lexi akasema huku chozi likimtoka.
Jenerali Jacob akaanza kucheka sana, kisha akasema, "Umenikumbusha mambo mengi kuhusu baba yako. Alikuwa na maneno mazuri pia, lakini hayakumfikisha popote. Ninataka upate glimpse ndogo ya kile ninachoweza kufanya, na finally utambue kwamba kiburi chako hakijawaletea manufaa yoyote yale, kwa sababu sikuzote nitaendelea kuwa mkubwa... kuliko hata huyo Mungu wako."
Maneno ya mwanaume huyo yalijaa kufuru sana. Lexi alikuwa akimwangalia kwa hisia nzito, kisha Jenerali Jacob akarudi nyuma kidogo kuwapisha wanaume wengine wawili waliokuwa wameshikilia kamba, nao wakaifunga mikono na miguu ya Lexi. Kisha, wakatoa gundi ya karatasi nao wakaanza kuizungusha mwilini mwake Lexi, wakisaidizana na wale waliokuwa wamemshika ili kumfunga mwili mzima kuanzia mabegani mpaka miguuni. Akawa amebanwa kwenye mwili wake mwenyewe, asiweze kabisa kujongea kama vile sanamu, huku wanaume hao wakiendelea kumshikilia.
Kisha Jenerali Jacob akawaamuru wengine, yaani Weisiko na wale waliomshikilia Nora warudi nyuma mpaka usawa wake, nao wakatii. Bado Azra alikuwa amepoteza fahamu pale chini, na sasa wale wanaume wanne waliokuwa wamewashikilia Kendrick na Torres wakawasogeza mbele yake Lexi na kuwaachia, wakidondoka chini kwa kishindo. Wakawabandulia gundi mdomoni, nao wakawaacha hapo chini na kutoka kabisa ndani ya jengo hilo.
Lexi alikuwa anawatazama wenzake hao kwa hisia sana, huku akihisi hatia nyingi moyoni, kwa sababu alielewa walikuwa wanaandaliwa kwa ajili ya nini. Jenerali Jacob akatoa bastola kutoka kiunoni kwake na kuishikilia kiganjani.
"Unahitaji tiba mzee. Ni nani aliyekukata masikio?" Jenerali Jacob akamuuliza Weisiko.
"Huyo malaya," Weisiko akamwambia.
"Ahahah... mtoto wa moto huyu! Asingekuwa upande huo angependeza sana kuwa moja ya mikono yangu," Jenerali Jacob akasema.
"Lexi... my dear..."
Maneno hayo yskasikika kutoka kwa Kendrick, akiwa ameyasema kiuchovu sana. Lexi akamtazama chini hapo na kuendelea kudondosha machozi.
Kendrick akajitahidi kuunyanyua uso wake ili amtazame, kisha akamwambia, "Its okay. Tume... tumefika mbali pamoja. Angalau umefanikiwa kusaidia watu... wengi. I'm proud of you..."
Torres, bila kuweza kunyanyua shingo yake vizuri, akasema kwa sauti iliyokwaruza, "Lexi... I'm sorry..."
Jenerali Jacob akamkabidhi Kevin bastola hiyo, naye Kevin akamtazama kwa njia yenye maswali.
"Kill them," Jenerali Jacob akamwambia.
Kevin akatoa tabasamu lenye kuonyesha wasiwasi, naye akaipokea na kumwelekezea Torres.
"Kevin... why? Kwa nini umeamua kuwasaliti watu ambao walikuwa tayari kufa pamoja nawe kwa kupigania haki?" Nora akamuuliza kwa hasira kutokea nyuma yake.
Kevin akawa anasitasita kuvuta kifyatulio cha risasi, kwa sababu kuna sehemu fulani ya dhamiri yake ilikuwa inamsumbua kuhusiana na yote aliyokuwa amechagua kuyafanya. Akamwangalia Jenerali Jacob kwa hofu kiasi kutokana na jinsi yeye na wanaume wake walivyomtazama kwa hila. Akakikaza kiganja chake na kufyatua risasi iliyompiga Torres sehemu ya mgongo wake, naye akalegea zaidi na kulala chini kwa kutulia. Lexi alifumba macho na kuinamisha uso wake akihisi huzuni iliyoambatana na hasira kali sana, naye akafumbua macho na kumwangalia Kevin kwa hasira zaidi.
"Lexi..."
Lexi akashusha macho yake na kumwangalia Kendrick, aliyekuwa ameita hivyo huku amepiga magoti chini sasa.
"Its okay. Hii ikiwa ni mara ya mwisho kukuambia maneno haya... nataka tu ujue kuwa ninakupenda sana... sana Lexi. Hhh... ninajivunia sana kwa kutumia muda wote niliokuwa nimebakiza hapa duniani nikiwa nawe. Na ninafurahi sana, kwa sababu huu nauona kuwa ushindi. Nakupenda sana binti yangu. Ahah... nimejisahau. Nakuchukia sana binti yangu," Kendrick akamwambia kwa hisia.
Jenerali Jacob na Weisiko wakaanza kucheka kwa dharau kwa kuwa waliona maneno ya Kendrick kuwa ya kipuuzi.
Lexi akawa analia kwa kwikwi, naye akamwambia, "Nakuchukia pia uncle Kendrick."
Kendrick akatabasamu kwa kufarijika moyoni.
Jenerali Jacob akazungusha macho yake kwa dharau na kumwambia Kevin, "Well?"
Kevin akaelekeza bastola yake kwa Kendrick, na hapo hapo akafyatua risasi iliyompiga mwanaume huyo mgongoni na kumwangusha chini. Lexi akatoa sauti ya kilio mara moja na kubaki mdomo wazi tu, akilia kwa hisia sana. Nora alikuwa analia sana pia huku akimwangalia mpenzi wake, asijue la kufanya ili kumsaidia. Kwa sifa, Weisiko akaanza kuipiga risasi nyingi sana miili ya Kendrick na Torres huku akimwangalia Lexi na kucheka kwa sifa sana, naye Lexi akageukia pembeni huku akifumba macho kwa nguvu mpaka Weisiko alipomaliza risasi kwenye bastola yake.
"Unajisikia vizuri sasa?" Jenerali Jacob akamuuliza Weisiko.
"Ningefurahi zaidi kama ungeniruhusu niutie matundu mwili wa huyu malaya pia," akasema Weisiko.
"Usijali. Dawa yake inakuja," Jenerali Jacob akasema.
"Wewe ni mpumbavu! Haustahili kuitwa mwanadamu kwa ukatili huu unaofanya!" Nora akamwambia baba yake.
"Na huyu tumwiteje? Au umesahau kama na yeye aliua watu wengi pia?" Weisiko akamuuliza.
"Alimuua nani bila kuwa na sababu? Wewe na wenzako mliua mamia ya watu kwa sababu ya tamaa..."
"Funga domo lako we mtoto! Haujui ni kiasi gani baba yako amejitoa kwenu halafu wewe uje kusema maneno hayo yasiyo na shukrani," Weisiko akamwambia.
"Nimshukuru kwa lipi huyu? Pamoja na yote ambayo mmefanya bado mnajiona kuwa sahihi kabisa? Sikuwahi kukuomba fadhila yoyote, na wala sikuzihitaji. Lakini kama ni kitu nachotaka unipe sasa hivi, basi ni kifo nikiwa pamoja na Lexi. Niue nikiwa pamoja naye, ni hapo tu ndiyo nitakuwa na shukrani kwako," Nora akaongea kwa hisia sana.
Jenerali Jacob akashusha pumzi na kufumba macho yake kwa nguvu.
"Hebu mfungeni mdomo huo," Weisiko akawaambia wanaume waliomshika Nora, nao wakatii na kuuziba mdomo wa Nora kwa gundi ya karatasi. Inaonekana walikuwa nazo nyingi.
Wanaume wale wanne waliokuwa wametoka jengoni hapo dakika chache nyuma, wakarejea pamoja na mwanaume mwingine pia, yule yule Sniper wa Jenerali Jacob. Wenyewe walikuwa wamesaidizana kubeba sanduku refu na kubwa la mbao, lililoonekana kuwa zito mno, likiwa ndiyo lile lile ambalo walimletea Jenerali Jacob kama "mzigo wake" wakati ule yuko nyumbani. Sniper wa Jenerali Jacob ndiye aliyewaua Victor na Mensah kutokea nje muda mfupi nyuma, na wala hazikuwa "drone" kama Jenerali Jacob alivyodai. Wale wanaume wanne wakaliweka sanduku hilo mbele ya Jenerali Jacob, huku Nora, na hata Weisiko na Kevin wakijiuliza kulikuwa na nini ndani yake. Jenerali Jacob akatabasamu kwa hila sana huku akimwangalia Lexi, wakati huo Lexi akiwa ameinamisha tu uso wake kwa kupoteza matumaini.
Luteni Jenerali Weisiko alikuwa wa kwanza kutambua kuwa Azra alianza kurejesha fahamu zake muda huo. Akamtazama jinsi alivyoanza kujigeuza taratibu, na baada ya Kevin kuona ameanza kujongea, yeye pamoja na wanaume wa Jenerali Jacob wakaelekeza silaha zao kwake ili wampige na risasi, lakini Weisiko akawazuia.
"Mfungeni tu huyo. Msimuue," Weisiko akawaambia.
"Lakini... lakini...." Kevin akawa haelewi.
Jenerali Jacob akamwangalia Weisiko kimaswali pia.
"General... unajua umuhimu wake. Popote tutakapoenda nitahakikisha tunaendelea kumtumia," Weisiko akamwambia.
"Lakini huyu ameshajua kila kitu... atawasaliti..."
"Kaa kimya dogo. Huyu ana umuhimu mara mia zaidi yako hapa. General... nitaziondoa tena kumbukumbu zake... nita...."
Jenerali Jacob akamkatisha kwa kunyanyua kiganja chake.
"Fanya jinsi moyo wako unavyotaka Weisiko. Hata mimi nafanya kile moyo unachotaka, siyo kichwa tu," Jenerali Jacob akasema hivyo huku amemwangalia Nora.
Wanaume watatu wakasaidizana kumfunga Azra kwa kamba, ambaye alianza kufurukuta huku akipiga kelele sana pasipo kufanikiwa kujinasua, na akihisi maumivu kichwani kwake pia. Wakamnyanyua na kumsogeza mpaka usawa wa Luteni Jenerali Weisiko, naye akamwangalia kwa ufupi, kisha akawapa ishara wanaume hao wampeleke kwa nyuma. Sasa wakawa wamebaki wanaume wawili waliokuwa wamemshikilia Lexi aliyefungwa mwilini, akiwa anamtazama Nora kwa hisia sana wakati huu.
"This is going to be incredible. You're gonna f(......) love this!" Jenerali Jacob akamwambia Weisiko kwa shauku.
Akatoa ishara kwa vidole, na wale wanaume waliokuwa wamemshikilia Lexi wakamwachia na kusababisha adondoke chini mzima mzima, akiwa wima lakini uso wake ukiangalia juu ili aone kile ambacho Jenerali Jacob alikuwa anataka kumfanyia. Jenerali Jacob akaanza kupeleka mkono wake taratibu kwenye sanduku hilo kubwa, lakini kabla hajalifungua, mmoja wa wanaume wake akamsogelea karibu na kumnong'oneza jambo fulani. Akasimama vizuri na kumwambia yeye na wengine wachache waelekee nje kuyaandaa magari upesi ili waondoke haraka. Weisiko alipouliza tatizo, Jenerali Jacob akasema kwamba wale waliokuwa wakiwasaka walikuwa karibu kuwafikia, hivyo wangetakiwa kuharakisha kuondoka hapo na kutoroka nchi haraka sana.
"Usjie kufikiri kwamba umepata tiketi ya kunusurika my dear, no, no, no... ni kwamba tu tunakuacha u-enjoy some quality time na rafiki yetu hapa," Jenerali Jacob akamwambia Lexi.
Akatoa ishara kwa wengine kwamba waanze kurudi nyuma, na kiukweli hofu iliwaingia wale wote ambao hawakuelewa alichokuwa anataka kufanya, na baada ya Weisiko, Kevin, Azra, Nora, na wanaume wengine kusogea nyuma, Jenerali Jacob akalifungua sanduku hilo na upesi kurudi nyuma pia mpaka usawa wa wengine.
Lexi alikuwa bado chini hapo akitazama kwa uzito sanduku hilo, na hangeweza kuzuia hofu yake kubwa kupanda baada ya kuona kichwa cha chatu kikitangulia kutoka nje ya sanduku hilo! Nora na Azra walishtuka sana, hata Weisiko na Kevin hawakuwa wametarajia hilo, huku Jenerali Jacob akitabasamu kikatili sana. Nora akaanza kupiga kelele za kilio zilizozibwa kwa karatasi ya gundi mdomoni mwake, huku Azra naye akilia kwa hisia ndani ya kiziba mdomo chake alichokuwa amewekewa pia.
Chatu huyo akawa anatoka taratibu kwenye sanduku hilo, na kadiri alivyozidi kutoka ndivyo wengine walivyozidi kuona jinsi alivyokuwa na mwili mnene sana uliokuwa na nguvu kubwa. Lexi akaanza kujiviringisha kwa kurudi nyuma, akijitahidi kukikimbia kifo hicho ambacho alielewa wazi kwamba hakukuwa na namna ya kukiepuka.
"Ohohooo... hapo ndiyo anamwalika vizuri zaidi. Wanapenda movement, na jamaa ana njaa kichizi," Jenerali Jacob akasema kikejeli na kuanza kucheka, lakini bila kutoa sauti.
Chatu yule akaendelea kumfata Lexi taratibu, kama hana haraka vile. Jenerali Jacob akamwangalia Nora machoni kama kumwambia kwamba kama hakuujua ukatili wake vizuri, hiyo ndiyo ingekuwa somo kwake. Kisha akaanza kuondoka hapo haraka na kutoa ishara kwa wengine waondoke pamoja naye. Nora na Azra walijitahidi kujinasua sana lakini ikawa kazi bure, nao wakakokotwa mpaka nje na kuelekea upande ambao kulikuwa na magari sita meusi na kila mmoja kuingizwa kwenye magari mawili tofauti. Nora alishangaa sana baada ya kuingizwa ndani ya gari na kumkuta mdogo wake, yaani Asteria. Akawa anataka kumuuliza nini kilimpata, lakini hawakuweza kusemeshana kutokana na wote kuwa wamezibwa midomo yao, na hivyo kubaki wanatazamana kwa huzuni sana, huku Asteria akionyesha wazi kwamba aliogopa mno kwa kulia sana.
Nora pia alilia sana, sana, sana. Alimwonea huruma sana Lexi, kumwacha akipambana na kifo kibaya sana ambacho hakuwa na hali yoyote ambayo ingemsaidia kukishinda. Lakini pia hali ambayo baba yake alikuwa amemwingiza Asteria ndani yake ilikuwa mbaya mno, kwa sababu binti huyo hakustahili kupitia mambo haya. Azra pia aliumia moyoni kupita maelezo, kwa sababu alielewa kwamba Lexi alikuwa ndiyo mtu wa mwisho kubaki kwenye familia yao, hivyo kumpoteza kulimaanisha anaachwa akiwa peke yake kwa mara nyingine tena na kwenda kuendelea kutumiwa kama silaha. Magari yote yaliondoka eneo hilo upesi na kuanza kuelekea upande mwingine kabisa.
Kule ndani ya jengo, Lexi alikuwa amejitahidi sana kujivuta-vuta na kujiburuza ili kumwepuka mnyama huyo mbaya sana, na kila mara alipotazama lilipokuwa, aliona jinsi lilivyojongea kwa njia ya umendeaji, kana kwamba lilikuwa linafurahia "kumwinda" kwa njia hiyo, ikionekana kama mchezo. Lexi alielewa wazi kwamba mbio zake kwenye sakafu hiyo zingeishia tu hatimaye kwenye ukingo, na hili likathibitika kuwa kweli baada ya kuufikia ukuta mwishoni kabisa kwenye jengo hilo. Alikuwa akihisi maumivu mengi, siyo mwilini, siyo moyoni. Alichoka sana. Akatulia tu hapo hapo, ikionekana kama vile amekubali kile kilichokuwa mbele yake, naye akaendelea kumtazama chatu huyo alipozidi kumkaribia.
Akafumba macho yake, naye akajisemea maneno haya moyoni: "Sandra... nimejitahidi kukimbia kwa muda mrefu, lakini nahisi huenda huu ndiyo utakuwa muda ambao natakiwa kusimama. Niliamua kuchukua maisha mapya ili nitimize ulichoniomba, lakini nimekuangusha pacha wangu. Nimewaangusha wote. Labda kusimama kwangu sasa itakuwa bora... ili niweze kupumzika pamoja nanyi."
Lexi aliweza kuhisi kitu fulani chenye umajimaji kikitekenya pua yake, naye akafumbua macho na kukutana uso kwa uso na chatu huyo, akiwa karibu zaidi na uso wake, huku ulimi wake ukitoka nje ya kinywa chake kilichofunga na kuilamba-lamba pua yake. Lexi aliogopa sana, na kwa kuelewa kwamba mnyama huyo alikuwa anajipa muda kujiburudisha na windo lake, yeye akaamua tu kufumba macho tena na kutulia, na labda hiyo ingesaidia kifo chake kisiwe chenye kuhofisha zaidi ya alivyodhani.
Ghafla, mlio mkali sana ukasikika kwenye ngoma za masikio yake, uliomshtua sana, lakini hakufumbua macho baada ya kuhisi vitu kama vimiminika vyenye ugumu fulani vikimwagika usoni mwake kwa njia fulani kama mtu aliyemwagiwa maji kwa nguvu. Viliambatana na sauti za vishindo kwenye sakafu ya hapo, na mapigo ya moyo wake Lexi yaliendelea kudunda kwa nguvu sana akiwa bado hajafumbua macho yake. Mwili wake uliokuwa umebanwa ulitetemeka sana, na taratibu akafumbua macho yake hatimaye.
Mbele yake sasa aliweza kuona mwili wa chatu huyo, ukiwa unajinyonga-nyonga taratibu bila mpangilio, na ilimchukua sekunde kadhaa kutambua kwamba sehemu ya kichwa cha mnyama huyo mbaya kilikuwa kimepasuka. Ilikuwa hali yenye kuhofisha sana! Hakuelewa ni nini kilikuwa kimetokea mpaka aliponyanyua macho yake na kutazama mbele zaidi, na hapo akamwona mtu akisogea upande wake taratibu huku ameelekeza bunduki upande wake.
Lexi akakaza macho yake kwa mtu huyo, na sasa sura yake ikaanza kuonekana vyema hata zaidi. Ilikuwa ni Luteni Michael!
★★★★★★★★★★★★★
ITAENDELEA
★★★★★★★★★★★★★
WHATSAPP +255 787 604 893