Simulizi: Lisa

"Rodney, hayakuhusu." Alimpiga kitako kwa nguvu kwa mguu wake. Sehemu ya nyuma ya kiti ilikuwa na sehemu ya wazi, kwa hivyo teke lake lilitua moja kwa moja kwenye kitako cha Rodney kilichojeruhiwa.

Alishindwa kujizuia na kuruka kutoka kwenye kiti chake huku akiomboleza kwa maumivu.

Kesi ilinyamaza papo hapo. Kila mtu, pamoja na hakimu, walielekeza macho yao kwa Rodney kwa njia isiyo ya kawaida.Uso wa Rodney mwekundu kwa aibu. "Mimi...Samahani."

Hakimu alimkazia macho kama onyo. "Ikiwa utapiga kelele zaidi, sitakuwa na chaguo ila kukutupa nje."

Alvin alimtazama Rodney bila la kusema. Rodney alikuwa tayari amejeruhiwa. Hakuweza kukaa kimya?
Rodney aliketi chini kwa uchungu kabla ya kugeuka nyuma na kumtazama Pamela kwa ukali. Pamela alimpa tabasamu la kukasirisha. Aliinua hata kidole chake cha kati na kukielekeza chini.

Rodney alikosa la kusema. Alipotazama pembeni, alimuona msichana aliyekuwa pembeni ya Pamela akimtazama pia. Macho yale baridi ambayo yalikuwa wazi yalikuwa na alama za tabasamu ndani yake. Yalionekana kufahamika sana.


Eliza alikuwa amehisi macho ya Lisa pia, akageuza kichwa na kumtazama Lisa. Lisa alirudisha kichwa. Alipotaka kuendelea kutazama kesi hiyo, hakutulia.

Pamela alimpiga tena Rodney teke.
Muda huo Rodney alitetemeka mwili mzima kwa maumivu, lakini hakuthubutu kuruka juu tena.

Pamela haraka akamsogelea na kusema kwa sauti ya chini, “Samahani, samahani. Sikufanya makusudi. Miguu yangu ni mirefu sana. Nilikuwa nikisogeza tu miguu na bahatimbaya nikakugonga .”

Rodney alivumilia maumivu na kusaga meno kwa uso uliopauka. "Pamela Masanja, unafikiri mimi ni mjinga?"

“Tulia. Kwanini unawafikiria wengine vibaya hivyo?” Pamela alisema huku akimpiga teke tena bila huruma.

Rodney alitokwa na jasho baridi. Hakuthubutu tena kuketi pale, haraka akakikunja kiuno chake na kuburuza kitako chake chenye maumivu na kuketi kwenye safu ya mwisho. Alikaa nyuma ya Pamela kimakusudi.

Pamela aligeuka nyuma na kusema kwa upole, "Najua miguu yako ni mirefu pia, lakini tafadhali kuwa mwangalifu. Mimi ni tofauti na wewe. Nina mtoto tumboni mwangu. Ukinipiga teke na kuniumiza, nitamwambia hakimu.”

Rodney, ambaye alikuwa akijiandaa kujifanya kumpiga teke, alishtuka sana hadi miguu yake ikakakamaa.
Pamela alitazama hali yake ya huzuni na iliyokata tamaa na akatabasamu kwa hasira.

Lisa alimtazama kwa unyonge. “Kwanini wewe na Rodney msitoke nje, mkapigane na kuingia tena?”

"Ah, nitaacha kukusumbua usimtazame Alvin, sawa?" Ni baada tu ya ukumbusho ambapo Pamela alinyamaza. Hakuweza kusubiri kuona sura ya Sarah iliyokata tamaa kwa kumfundisha Rodney somo. Katika kesi hiyo, Alvin alikuwa katika hali ya kufanya mambo.


Sura ya: 669



Sarah aliketi kwenye kiti cha mshtakiwa. Macho yake yalikuwa ya baridi, na alijihisi mnyonge sana.


Wakili wake, Stevens, alisema bila kujali, "Wakili mkuu wa uvumi nchini Kenya sio chochote tena.”


Sarah aliuliza kwa sauti ya chini, “Tuna uhakika wa kushinda?”

“Ni zaidi ya uhakika. Hukuona macho ya hakimu ya kumdharau Alvin? Sasa ngoja nimkanyage kwa mara ya mwisho.”

Stevens alisimama na kumuuliza Alvin, “Bw. Alvin Kimaro, nilisikia kwamba ulirudiana na mwanamke aliyeolewa hivi karibuni. Ni kweli?"

Midomo ya Alvin ikasogea. "Yeye ni mke wangu wa zamani ..."

“Unachohitaji kujibu ni kama ni kweli au si kweli. Je, ulikutana na mwanamke ambaye bado hajaachika?” Stevens aliuliza.

“Ndiyo.” Alvinakaitikia kwa kichwa.

Stevens alitabasamu. Akatazama upande wa hakimu. “Mheshimiwa umesikia hivyo pia. Haijalishi ni sababu gani Alvin anayo, ukweli kwamba yuko pamoja na mwanamke aliyeolewa unasema hadharani kwamba ana maadili duni. Huu ni ushawishi mbaya hata kwa jamii. Kwa hivyo, kudanganya hisia za Sarah na kupoteza zaidi ya miaka kumi ya ujana wa mteja wangu bila shaka ni jambo la kudharauliwa. Ni mwenendo mbaya. Natumaini Heshima yako inaweza kutoa hukumu ya haki. Mtu kama yeye akitajirika, atafikiria tu kuwadhuru wasichana wasio na hatia. Machoni mwake, wanawake ni kama nguo ambazo zinaweza kuvaliwa na kuvuliwa tu.”
 
Hakimu alikuwa mwanamke. Kwa hiyo, baada ya kusikia maneno ya Stevens, hakuridhika na matendo ya Alvin pia.

Alvin akasimama. “Bi Sarah Langa Njau, acha nikuulize kwa mara ya mwisho. Nilifanya ngono na wewe hapo awali?"

Sara alimtazama kwa huzuni. "Kumbe ni nini mwanamke na mwanamu watafanya ikiwa watakaa kwa muda mrefu kama wapenzi?"

"Tafadhali jibu swali langu moja kwa moja," Alvin alisema kwa ubaridi.”


“Ndiyo.” Sarah akaitikia kwa kichwa.


Alvin alimgeukia hakimu na kusema, “Nakata rufaa kuleta shahidi wa mwisho mahakamani.”

“Shahidi ni nani?” hakimu aliuliza.

"Ni kaka wa damu wa Sarah, Thomas Njau." Baada ya Alvin kumaliza kuongea, sura ya Sarah ikabadilika.

Stevens mara moja alisema, "Pingamizi. Alvin hakuwasilisha ombi hilo hapo awali.”

Alvin alisema, “Mambo fulani yalimtokea Thomas hivi majuzi, na alikuwa amelazwa hospitalini muda wote. Sikujua kama angeweza kufika kwenye kesi hii au la, kwa hivyo sikutuma ombi. Hata hivyo, alinitumia ujumbe kabla ya kesi kuanza na kusema atakuja. Zaidi ya hayo, pande zote mbili zilitaja jina la Thomas mara nyingi wakati wa kesi ya kwanza.”

Hakimu aliangalia rekodi za zamani kabla ya kutikisa kichwa. “Mruhusu aingie.”


Uso wa awali wa Sarah ulizama. Hakuelewa kwanini Thomas angeibukia kwa Alvin baada ya kupotea kwa mwezi mmoja? Alifikiri Thomas aliogopa sana baada ya kufundishwa somo na Chester hivi kwamba aliondoka nchini kwa siri.

“Kaka yako anafahamu kiasi gani kuhusu mambo yako?” Stevens aliuliza kwa sauti nzito.

“Mengi.” Sarah hakujisikia vizuri.

Stevens alikunja ngumi kwa kufadhaika. “Kwanini hukuniambia kabla?”

“Sikuwa na uhakika. Siku zote alinisikiliza.” Sarah naye alichanganyikiwa. Wakati huo huo, alimchukia kwa siri. Alipaswa kuachana na Thomas muda mrefu uliopita.

Punde, Thomas aliingia. Thomas alipomwona Sarah, hakuweza kujizuia lakini kutetemeka.

Sarah haraka akasema kwa macho mekundu, “Kaka, ulikuwa wapi muda wote huu? Nilikuwa na wasiwasi sana. Uliumia vipi? Je, Alvin alikutishia?”

Mara Alvin akakemea, “Sarah, tafadhali zingatia maneno yako. Ninaweza kukushtaki kwa kuchafua jina langu.”

Hakimu alimkodolea macho Sara kama onyo pia. "Shahidi anaweza kuchukua nafasi yake."
Baada ya Thomas kwa woga kuingia kwenye kizimba cha mashahidi, Alvin aliuliza, “Bw. Thomas Njau, ningependa kuuliza swali. Je, sikuisaidia New Era Advertisings mara nyingi baada ya baba yako kufariki? Sikuisaidia kwa siri kutafuta washirika wa ushirikiano mara nyingi pia?”

Thomas aliitikia kwa hofu. “Ndiyo.”


Alvin alisema, “Kama si mimi, je New Era Advertisings ingedumu hadi leo?”

Thomas akatikisa kichwa. "Hapana."

Alvin akauliza tena, “Dada yako alisema nilifanya naye mapenzi hapo awali. Je, unadhani hii ni kweli?”

Stevens alisimama. “Pingamizi. Thomas ni kaka wa mteja wangu tu. Angejuaje swali la kibinafsi kama hilo? Aidha, nijuavyo mimi, uhusiano wa Thomas na Alvin haukuwa mzuri kamwe. Kuna mashaka mengi sana kwanini Thomas angekuwa tayari kwa ghafla kuwa shahidi wa Alvin. Tunashuku kuwa Alvin alimtishia shahidi. Nyote mnaona majeraha kwenye mwili wa shahidi.”

Hakimu alikunja uso, na kila mtu akaanza kunong'ona.

Hata hivyo, Thomas alisema kwa sauti, “Hapana, hakunitishia. Mimi ndiye ninayemchukia Sarah. Yeye ni mbaya sana."

Usemi wa Sarah ulibadilika. Alisema huku machozi yakimtoka, “Kaka, unajua unachosema? Tumepitia mambo mengi sana baada ya kifo cha Mama. Kama nisingekuwa mimi, bado ungekuwa hapa katika sehemu moja?”

Alvin alicheka kwa kejeli na kusema, “Usijichukulie sifa kwa mambo yote mazuri. Mimi ndiye niliyepigania kesi kwa ajili yake enzi hizo. Kama si mimi, angeenda jela. Kwa upande mwingine, Sara, ulimdhulumu ndugu yako mara nyingi sana miaka hii. Hukuwa na hatia kwa sababu alibeba lawama zote.”
 
"Hiyo ni kweli." Thomas ghafla alikumbuka matukio ambapo Chester alimfanyia, na hasira ikajaa ndani yake. "Baada ya familia ya Kimaro kushuka, niligongana na Alvin wakati mmoja alipokuwa amelewa. Nilikupigia simu na kukuambia kuhusu hilo. Mwishowe, ulinichochea nimwambie Simon Kelly kuhusu hilo ili amfundishe Alvin somo, baadaye lawama nikabeba mimi lakini wewe ukawa safi.”

Akiwa amekabiliwa na macho yenye kutatanisha ya kila mtu, Sarah alijibu mara moja na kusema, “Unaongea upuuzi gani?”

Stevens alisema, “Hakuna haja ya kuzungumza kuhusu chuki zako za kibinafsi hapa. Hii ni mahakama, si soko.”

Thomas karibu apoteze busara kwa sababu ya hasira. Kwa bahati, Alvin mara moja alisema, "Thomas Njau, tafadhali jibu swali langu la awali."

Thomas alinyamaza kwa muda kabla ya kusema kwa haraka, “Wewe na dada yangu mngewezaje kufanya ngono? Sarah aliniambia mara nyingi kwamba hukushtuka kila alipokugusa. Siku zote alikuwa akinilalamikia faraghani, na hata alisema... Alisema wewe si ridhiki.”

Mara baada ya maneno hayo kutoka, kila mtu alishtuka. Thomas alisema, “Kuna wakati mmoja aliniambia ninunue dawa. Mwishowe, hakufanikiwa, na hata alinilaumu kwa kukosa nguvu za kutosha za dawa hiyo.”

“Upuuzi.” Stevens alisema kwa sauti nzito, “Niambie. Je, Alvin alikupa bei gani kumkandamiza dada yako?”

Sarah alilia na kusema, “Kaka, sisi ni familia.”
Alitaka kudokeza kwa Thomas kwamba pesa zake pia zilikuwa pesa zake, akitumaini Thomas atakuja kutambua hilo.

Hata hivyo, Thomas alikuwa amemdharau kwa muda mrefu. Angemwamini vipi? “Wakati yeye na Alvin walipokuwa wakichumbiana, mara nyingi alinichochea nimpe Alvin vidokezo ili ampe nyumba za kifahari na vitu vya thamani. Zaidi ya hayo, wakati Alvin na Lisa walikuwa hawajatalikiana bado, siku zote alijifanya kuumia na hata kujiumiza kwa makusudi ili aweze kumdanganya Alvin arudi nyumbani kwake na kumfanya Lisa asielewe. Alitaka kujipenyeza wakati mume na mke walipokuwa wakipigana.”

Sarah alikasirika. “Hiyo si kweli.”

Thomas alidhihaki. "Ni kweli. Majeraha yako yalikuwa mepesi sana kila mara, lakini kila mara ulinifanya nikutie chumvi mbele ya Alvin.”

Sura
ya: 670



Sarah mwili mzima ulimtetemeka kwa aibu.

Thomas aliendelea kusema, “Kwa hakika wewe ni mvunja nyumba ambaye aliharibu ndoa za watu wengine. Baada ya Alvin na Lisa kugombana, na baada ya kujijeruhi muda huo kwa makusudi, uliniambia nimwambie Alvin kuwa unataka kuishi katika jumba lake la kifahari. Sababu halisi ni kwamba ulitaka kuishi katika kiota cha mapenzi ambacho Lisa na Alvin walitumia ili kumuumiza Lisa.”

“Zaidi ya hayo,” Thomas aliendelea, “mwaka ule wakati Lisa alikuwa na ujauzito wa mapacha, uliniambia kwamba bila shaka ungewashughulikia mapacha hao baada ya Alvin kukukabidhi watoto.”

Thomas alipofichua tukio baada ya tukio, kila mtu katika chumba cha mahakama alipigwa na butwaa. Wengine hata hawakuweza kupinga kuijadili.
“Si alisema yeye ni mhanga asiye na hatia? Kwamba ni Alvin ndiye aliyemsaliti na alioa mwanamke mwingine, naye akambembeleza kwa maneno matamu tena baadaye.”

"Kwa hivyo, mwishowe, alikuwa mchepuko. Waooo.”

"Yeye ni mjanja sana, na karibu anidanganye."


"Yeye si mdanganyifu tu. Yeye ni mbaya. Alikuwa hata na nia mbaya hadi kwa watoto waliokuwa tumboni.”

"Hiyo ni sawa. Watoto ndio malaika safi zaidi ulimwenguni."

"Ukiniuliza, Alvin pia ni mnafiki. Inachukua vidole viwili kuvunja chawa. Kama angekuwa mtu mwema, asingedanganywa na Sara. Anastahili mara mbili."

"Watu wasio na hatia zaidi ni Lisa na watoto."


Rodney aliyekaa kwenye kiti cha watazamaji, aliweza kusikia majadiliano ya kila mtu kwa uwazi.

Uso wake mzuri, ambao tayari ulikuwa umepauka, ulibadilika rangi kana kwamba alikuwa karibu kuzimia na kuvunjika wakati wowote. Alifikiri kwamba Sara alikuwa na tamaa tu, mtupu, na alipenda kucheza na watu wenye mamlaka na ushawishi. Hata hivyo, hakutarajia kwamba mwanamke huyo alikuwa mwovu na mwenye hila kuliko vile alivyofikiri.
 
Ambacho hakuweza kukikubali zaidi ni kwamba, Sarah alikusudia hata kuwaumiza watoto wa Alvin. Je! hiyo ilikuwa sawa? Je, mtu anaweza kuwa wa kutisha sana kufanya jambo kama hilo?

Upendo wake usioweza kusahaulika, mchanga usiostahiliwa wakati wa ujana wake ulikuwa wa picha bandia wakati wote.


Mahakamani, Alvin alikasirika sana hivi kwamba mishipa yake ilimdunda.


Baadhi ya mambo ambayo Thomas alisema yalitokea kabla ya Alvin kudanganywa.
Mambo mengi katika kumbukumbu zake yalikuwa yamepotoshwa. Ikawa kila mara Sarah alipopata kuumia ni kwa kujifanya yeye mwenyewe na kwamba alitaka jumba lake la kifahari ili kumchoma Lisa. Si ajabu Lisa alimchukia sana.
Hata kwa upumbavu alimpa Sara kiota chao cha upendo.


Alipofikiria miaka hiyo yeye na Sarah waliishi katika jumba hilo la kifahari, alitaka kujipiga makofi mwenyewe hapo hapo. Matendo yake yote yalikuwa yakiutesa moyo wake mwenyewe.

"Wewe b*tch." Macho ya Alvin yalikuwa yakimetameta damu.

“Hiyo si kweli,” Sarah alifoka huku akitoa kilio cha kukata tamaa na kukosa matumaini. “Sikufanya hivyo. Thomas, kwanini unanibumbia maneno? Alvin alikupa nini? Najua. Je, unamuogopa Chester? Umesahau ni nani aliyekufanya hivi?”

“Wewe. Ni wewe tu.” Thomas akawa hana akili pia. “Kwanini wewe kama dada yangu hukunizuia kila nilipokuwa na mawazo mabaya? Ilimradi inaweza kuwaumiza watu wa upande wa Lisa, ungenitia moyo kuyafanya. Isingekuwa kwa sababu ulikuwa karibu sana na Alvin na marafiki zake, nisingekuwa na kiburi. Wewe ndiye uliyenifanya hivi leo.”
Umejiletea kila kitu leo.”

“Si nimekusafisha vya kutosha miaka yote hii? Huna moyo na huna shukrani.”

“Ha, kwa hiyo umenichoka na kutuma watu kuniteka. Unataka kuniua kwa siri, sivyo? Wewe mwanamke mbaya, nitakushusha chini na mimi hata kama nitakuwa na bahati mbaya."

“Una kichaa. Nilikuteka lini? Usizungumze ujinga.”
Ndugu hao, Thomas na Sarah, walianza kuzozana hadharani katika chumba cha mahakama.

"Kimya." Hakimu alitoa sauti kali. Alisema kwa hasira, “Je, nyote mnachukua mahali hapa kama soko? Ugomvi huu ukiendelea, mtawekwa kizuizini.”

Sara alilia na kumwambia hakimu, “Sina hatia.”

Thomas akasema, “Nilichosema kilikuwa ukweli.”

Hasira za hakimu ziliwaka. Alipiga meza tena kwa hasira. “Kimya.”
Akamkazia macho Sarah.

Kwa hayo, Stevens alimshikilia Sarah kwa haraka na kumwambia asiseme chochote zaidi. Hakimu alikasirika sana. Hatimaye chumba kikatulia.

Hakimu alituliza hasira yake na kusema kwa upole, "Mshtakiwa, unaweza kuwasilisha maelezo yako."

Sarah akasimama haraka na kujikaba. “Ingawa sielewi kwanini kaka yangu amsaidie Alvin, nilichosema hapo awali kilikuwa cha kweli. Nilipokuwa na umri wa miaka 18, Alvin aliniomba nichumbiane naye. Ili kumpenda, nilifanya mambo aliyopenda na hata kuwa mwanasaikolojia wa kutibu ugonjwa wake. Kila nilichofanya ni kwa ajili yake. Sijaridhika kwamba nilimpa zaidi ya miaka kumi ya maisha yangu ili tu niishie kuwa kama mbwa. Hata mimi ninalaumiwa kimakosa kama mwanamke asiye mwaminifu. Inatia hasira. Mimi kwa kweli... sitaki kukubali hili. ”
Kufikia mwisho, alianza kulia.

Sauti ya kilio chake ilisikika katika mahakama nzima. Kila mtu alikaa kimya akimsikiliza akilia, na wote walikuwa na sura tofauti kwenye nyuso zao.

Pamela, ambaye alikuwa ameketi nyuma, hakuweza kujizuia kukemea, “Yeye ni mzuri sana katika uigizaji. F*ck, kwa nini hakuwa mwigizaji?"

Eliza alikodoa macho. "Ustadi wangu wa kuigiza sio chochote ukilinganisha na wake."
Lisa akahema. “Nasikia kichefuchefu tu.”

“Wewe pia una mimba?” Pamela aliuliza kwa furaha. "Hapana, Alvin hawezi kukupa ujauzito, sawa?"


"...Nilimaanisha kuwa nimechukizwa sana na maneno yake hadi nataka kutapika," Lisa alisema.

Pamela alitabasamu kwa unyonge. “Unadhani hakimu ataguswa na kitendo cha Sarah?”
"Angekuwa hakimu wa kiume, angeweza kuwa. Hata hivyo, kwa hakimu wa kike...” Lisa alicheka.
 
Eliza alimtazama Lisa na kuendelea na sentensi ya Lisa. "Wanaume huwa dhaifu kwa urahisi wanapoona machozi ya wanawake. Lakini, kama mwanamke, hakimu wa kike hataenda kwa moyo mpole. Badala yake, atahisi kuwchukizwa zaidi na wanawake wanaopenda kutumia kilio ili kupata huruma. Ikiwa huamini, angalia pande zote. Miongoni mwa wasikilizaji, wengi wa watu ambao wamekuwa wapole kwa maneno ya Sarah ni wanaume. Wanawake wengi wanamdharau.”

Pamela alitazama kushoto na kulia. "Ninagundua nyinyi wawili mna kemistri nzuri sana."

"Siyo kemistri. Ni logiki ya kawaida.” Lisa alitabasamu.

"Hiyo ni sawa." Eliza aliitikia kwa kichwa.

Pamela alikosa la kusema. "Inatosha. Usifanye ionekane kama siwezi kufanya maamuzi ya kawaida, sawa?”

”Hata ulisema nina mimba. Unafikiri bado unaweza kufanya maamuzi ya kawaida?" Lisa alimpa pigo.


Sarah alipokuwa karibu kumaliza kulia, hakimu alimwambia Alvin, “Mshtaki unaweza kuwasilisha kauli."
Alvin alisimama na kumtazama Sarah. Chini ya nywele zake fupi nyeusi, uso wake mzuri ulijaa huzuni na majuto. “Kama mtu angeniuliza mapenzi ya kwanza ni nini, nitafikiri ni ndoto mbaya. Ninajuta kwanini nilitaka kukufahamu wakati huo. Umekuwa nuru yangu wakati wa ujana wangu, kwa hivyo nilikutendea kama familia. Kwa zaidi ya miaka kumi, nilitoa nilichoweza. Iwe ni wewe au familia yako, niliwaruhusu ninyi nyote kuchukua na kuomba chochote kutoka kwangu. Nilioa tu baada ya wewe kutoweka kwa miaka michache.

“Hapo awali, ilikuwa ni ndoa ya kimkataba tu na mke wangu. Lakini, polepole nilimpenda kadiri tulivyotumia wakati pamoja. Baada ya hapo, ulirudi, na nilihisi hatia kuelekea kwako. Ili kukushukuru, siku zote nilikuwa wa kwanza kukupa mkono wakati wowote ulipokuwa na shida. Lakini sikujua matendo yangu yalikuwa yamemuumiza mke wangu na kumfukuza yeye na watoto wangu kutoka kwangu kwa miaka mitatu.

“Najuta, hasa siku hizi nilipogundua ukweli. Najuta sana kwamba nimekuwa nikilewa kila siku na kutamani sana kujichoma na kisu hadi kufa. Kwa sababu ninajuta, nilikata kidole changu hiki ili kulipia dhambi zangu.” Akainua kidole chake ambacho bado kilikuwa kimefungwa bandeji. Kila mtu aliogopa.
 
Sura ya: 671



Alvin aliendelea kusema, “Kwa kweli, nimepata tu kujifunza kuhusu mambo ambayo Thomas alisema hapo awali. Sidhani nina deni lolote kwa Sarah. Namuonea huruma mke wangu wa zamani. Nilikuwa nikimchukulia kama mwanamke asiye na adabu ambaye alikuwa tamaa kutokana na hadhi yangu, lakini sikumwelewa. Nina deni kwake kupita kiasi.
"Mimi ni mfano wa damu, hai. Iwapo wanaume wengine walipata hali kama yangu, nataka kuwaambia hili. Exes ni ex. Ikiwa umeoa, basi unapaswa kukatisha uhusiano wako nao. Usimdhuru mkeo.”

"Sababu ya kutaka kurudisha bilioni 1o zangu sio kwamba ninahitaji pesa, lakini kwa sababu nadhani hastahili. Mwanamke mwenye tamaa kama yeye hastahili kuwa na kiasi hicho kikubwa cha pesa. Ikiwa sivyo, itawafanya baadhi ya watu wabaya katika jamii na hata kundi la vijana kufikiri wanaweza kuchukua njia za mkato na kupata mafanikio kwa kudanganya hisia za watu wengine.” Macho makali ya Alvin yalimtazama Sarah. "Natumai utaweza kupata pesa kupitia uwezo wako mwenyewe."


Baada ya kusema sentensi yake ya mwisho, uso wa Sarah ulikuwa umepauka kama karatasi. Alvin alikuwa wa ajabu. Aliweka toba ndefu kama hiyo ya kibinafsi ya hisia zake mwanzoni na kumalizia kwa onyo kwa jamii kuelekea mwisho.

Kesi hiyo ilikuwa imekua kubwa sana, hivyo hakimu angesisitiza kuleta ushawishi chanya kwa jamii. Hakika, hakimu akawa mpole. Baada ya kuwasiliana na majaji wawili kwa muda, alisema, “Baada ya kusikilizwa mara mbili, mahakama imesikiliza maelezo ya pande zote mbili. Ifuatayo ni hukumu ya mahakama kwa kesi hii:

"Mahakama inaona kwamba Sarah anafaa kurejesha hizo bilioni 10 na jumba la kifahari kwa Alvin mara moja. Pesa hizi si zako tangu mwanzo. Kuhusu gharama zote ambazo Alvin alitumia kwa Sarah kwa zaidi ya miaka kumi, hakuna haja ya kuzirejesha. Hii ni adhabu kwa Alvin. Kama mwanaume, ulimsaliti mke wako na watoto wako. Umejiletea mwenyewe hili. Hili ni funzo kwako.”

Hakimu alinyamaza kwa muda kabla ya kumtazama Sarah. “Watu hawawezi kupata faida kwa kudanganya hisia za watu wengine. Ulichonacho tayari ni kitu ambacho wengine wengi hawawezi kuwa nacho hata baada ya kufanya kazi kwa bidii maisha yao yote. Usiwe mtu wa tamaa sana. Kesi hii imeisha. Mahakama inaahirishwa.”

Baada ya hakimu kutoka nje ya mahakama, Sarah alikaa kwenye kiti huku akiwa amehuzunika. Bilioni 10 zake zilitoweka hivi hivi. Hata aliamriwa na hakimu katika chumba cha mahakama kuzirejesha mara moja. Kwa Sara, hilo lilikuwa likimtia jeraha.

Stevens alimtazama bila kujali, kisha akatembea kuelekea kwa Alvin. "Kwa kweli unastahili jina la wakili mkuu nchini. Ulijiweka katika hali mbaya kimakusudi wakati wa kusikilizwa kwa mara ya kwanza, sivyo? Ulitaka kufanya kesi hii kuwa kubwa na kuruhusu hakimu atambue athari mbaya ambazo kesi hii huleta. Bilioni 1o zinaweza kuwajaribu watu wengi. Kama hakimu hakuhukumu kurudishwa pesa hizo kwako, watu wengi wangeiga kutoka kwa Sarah, na kutumia udhaifu wa hisia za wengine kwa faida yao.”

"Ni kweli, lakini umegundua kuwa umechelewa sana." Alvin akatabasamu. “Hata kama nisingemwita Thomas katika kesi ya pili, matokeo yangekuwa sawa. Hata kama hakimu alihisi kwamba nilikosea, bado angelazimika kusema kwamba nilishinda ili kuleta uvutano mzuri kwa jamii.”

"Wewe ni wa kushangaza." Stevens aliitikia kwa kichwa. Alichukua kamari na kukubali hasara. "Natumai kutakuwa na nafasi ya kupingana nawe tena katika siku zijazo." Kisha, akageuka ili kuondoka, hakujali tena kuhusu Sarah.

Sarah pia alijaribu kutoroka, lakini Alvin alimwona. “Nirudishieni pesa hizo ndani ya siku tatu, au nitalazimika kuwataka polisi wasimamie sheria. Vilevile, ondoka nje ya jumba langu la kifahari mara moja. Ninataka nyumba yangu kabla ya giza kuingia."

"Alvin Kimaro, usiende mbali sana." Sarah alitaka kumuua kwa macho yake.


“Umechukua nafasi ambayo si yako kwa muda wa kutosha. Ni wakati wa wewe kutoka nje.” Baada ya hapo, Alvin alitembea moja kwa moja kuelekea kwa Lisa.

Kesi hiyo ilimfanya ahisi hatia zaidi dhidi ya Lisa. Lisa alisimama taratibu na kufungwa mikononi mwake kwa nguvu kabla ya kuongea.
 
"Lisa, samahani." Alvin aliomba msamaha kwa huzuni. "Nilikuwa mjinga sana hapo awali. Sasa naelewa kuwa ulikuwa sahihi kwa kutonisamehe.”

"Basi ... Je! nirudishe maneno yangu ya msamaha?" Lisa aliinua uso wake kwa uchochezi.

Akiwa na hofu, Alvin akasema kwa haraka, “Nimemaliza.”


Lisa akaangua kicheko. "Sahau. Baadhi ya mambo yanaweza kuwa yasiyopendeza zaidi wewe kufikiri juu yake.”

“Ndiyo.” Pamela pia alisema. “Mwanamke yeyote atakufa kwa hasira ikiwa angegundua kuwa kiota chake cha mapenzi na mumewe kilitolewa kwa hawara. Je, unajua Lisa alihamia kwenye jumba la kifahari la kando ya bahari ili kukuhudumia ugonjwa wako uliporudi tena? Ninyi wawili kimsingi mlistawisha mapenzi yenu hapo. Na hata mimba ya watoto wenu ilitokea hapohapo.”

Uso wa Alvin ulikuwa mwekundu. “Sikujua. Sikumbuki...”


“Inatosha, Pamela. Hakuna haja ya kuzungumza juu ya hilo." Lisa alimkatisha tamaa.


Pamela akacheka. "Hakika wewe ni mvumilivu."


Lisa alikasirika. "Ningepata kutokwa na damu kwenye ubongo kwa hasira kama nitakanyaga kwenye jumba hilo.”

“Lisa, usijali. Nikirudisha jumba hilo, nitalichoma moto." Alvin alisema mara moja, “kisha tujenge mpya."

"Hakuna haja. Sitaki kuona tena hata kipande hicho cha ardhi. Iuze tu. ” Lisa alibadili mada. "Ulipigania kesi hii kwa uzuri kabisa."

"Nimefanya vizuri tu kwa sababu uko hapa." Alvin alimbembeleza kwa makini.

Kisha, akamuona Rodney akielekea mlangoni akiwa ameduwaa.
Akamshika na kumpigapiga Rodney begani. “Uliruhusiwa?”

“Ndiyo.” Rodney bado alikuwa hajielewi, na hata macho yake yalikuwa mekundu. "Alvin, Thomas alisema ukweli?"

Sauti ya huzuni ya Pamela ilisikika. "Lo, inaonekana kama mtu fulani bado hawezi kukubali ukweli huu. Lisa, huoni kwamba yeye ni mjinga?”

Lisa alitabasamu. “Kwa kweli, sidhani kama kuna haja ya kujisumbua kuhusu tabia ya Sarah. Je, humpendi? Katika kesi hiyo, unapaswa kuvumilia pande zake zote mbaya na nzuri. Upendo wa hali ya juu kabisa ni kumpenda mtu jinsi alivyo.”

"Hiyo ni kweli. Haya, fanya haraka na umfuate Sarah. Lazima atakuwa na huzuni sana na hana msaada sasa. Unapaswa kumfariji.” Pamela alitoa dole gumba.

Kama inavyotarajiwa kwa dada yake mzuri. Uwezo wa Pamela wa kuchoma majeraha ya watu haukuwa na kifani. Rodney awali alikuwa na huzuni sana, lakini uso wake mzuri uligeuka mwekundu kwa aibu kwa maneno yao.

"Pamela Masanja, inatosha." Rodney alionekana kuchoka.

“Inatosha.” Pamela akageuka pembeni na kumvuta Eliza. “Si uliahidi kula chakula cha jioni na mimi? Twende zetu. Lisa, unataka kujiunga…?!”

“Hakika.” Lisa alimpenda sana Eliza na akakaribia kutikisa kichwa alipoona macho ya Alvin ya uchungu. Alipepesa macho na kusema kwa haraka, “Kwanini tusimfanye Alvin atuhudumie usiku wa leo? Tunaweza kusherehekea ushindi wake katika kesi hiyo.”

“Lisa...” Alvin hakuwa na furaha. Alitaka kuwa peke yake na Lisa.

“Kuna faida gani ya kuwa pamoja kila wakati? Inapendeza kujichanganya na watu wengi zaidi wakati mwingine.” Lisa alimkatisha.

Alvin alihisi kushambuliwa. Walikuwa wamerudiana pamoja, lakini tayari alifikiri kwamba hakuna maana kwao kuwa na wakati wa pamoja peke yao?

“Hutaki?” Lisa alimuona akinyamaza na kuinua uso wake.


"Hapana, nilikuwa nikifikiria mahali pa kula." Alvin alitoa tabasamu kwa haraka. Alimradi alikuwa na furaha, angefanya chochote.

“Umefikiria kitu?” Lisaaliuliza huku akitabasamu.

“Ndio, nakumbuka Rodney alitupeleka kwenye mkahawa wa Kaiseki mara ya mwisho. Mazingira ni ya kifahari, na ni mazuri kabisa,” Alvin alisema mara moja.

"Kaiseki inasikika vizuri. Hiyo ni sawa, Bi Robbins?"
Lisa aligeuka kumuuliza Eliza maoni yake.


Eliza alimtazama Alvinkimya kimya. Hakutaka kwenda baada ya kujua kuwa Alvin angeennda pia.

Sura ya: 672


Hata hivyo, alipowaona Pamela na Lisa wakimtazama, aliitikia kwa kichwa mwishowe.
“Basi twende.” Alvin akauzungusha mkono kiunoni mwa Lisa na kutoka nje.
 
Hatimaye ni weekend, lakini haitaenda poa bila kushushia kisa chetu pendwa cha LISA hivyo mwandishi kwa unyenyekevu tunaomba tuianze asubuhi kwa vipande kadhaa kama hutajali[emoji39][emoji39][emoji39]
 
Pamela na Eliza walifuata kwa nyuma. Wakati wale wanne walipoingia kwenye lifti, mtu mmoja ghafla aliingia nao. Isipokuwa Alvin, kila mtu alimtazama Rodney kwa sura ya kuchukia machoni mwake. Mtazamo wa Pamela ulikuwa, haswa, umejaa dharau.

"Huna mpango wa kuja nasi, sivyo?"

“Ahem. Alvin ni kaka yangu. Ni kawaida kusherehekea ushindi wake.” Rodney aliweka uso wa ujasiri na kumtazama Alvin. "Alvin, hutanifukuza, sivyo?"

Alvin hakujua jinsi ya kujibu. Hakuwa na la kusema kidogo kwenye uso wa Rodney usio na aibu. Alimuelewa Rodney. Rodney labda alikubali ukweli na alikuwa akijaribu kujiweka karibu na Pamela sasa ili kurudi kwenye familia ya Shangwe.

Pamela alitema mate, “Bado una shavu la kumsherehekea? Ulisimama na Sarah katika kesi iliyotangulia. Je, hukutaka Sarah ashinde? Sasa kwa kuwa umeachwa, unarudi mbio kwa kaka yako. Sijawahi kuona mtu asiye na aibu kama wewe.”

Uso wa Rodney uliwaka kutokana na ukosoaji huo. "Pamela, mbona una ulimi mkali sana?"

“Samahani, huku hakuitwi kuwa na ulimi mkali. Ninasema ukweli tu.” Pamela alijibu. “Unajua nini maana ya rafiki? Ni kama mimi na Lisa. Sisi kamwe hatukatiani tamaa juu ya kila mmoja, na tunaheshimu mapenzi ya kila mmoja wetu na kusaidiana maamuzi. Kufanya unavyotaka na kusisitiza mambo yafanywe kwa njia yako inaitwa tu ubinafsi.”

Alvin aliridhika kabisa na jibu hilo. Ingawa maneno ya Pamela yalikuwa makali kidogo, yote yalikuwa hadharani, na hakukuwa na uchochezi uliojificha. Isitoshe, kama si yeye, Lisa na yeye wasingekutana na kupendana.
Mhadhara wa Pamela ulimfanya mtu kama Rodney awe na rangi nyekundu usoni na shingoni. Ikiwa ingekuwa zamani, angebishana kwa sauti kubwa. Lakini sasa, alihisi kwamba kwa kweli alikuwa mbinafsi sana kwa rafiki yake.

“Sawa, najua uko sahihi, lakini hiyo ni kati yangu na Alvin,” Rodney alisema kwa huzuni.

Pamela akaitikia kwa kichwa. "Umesema kweli, lakini siwezi kuvumilia jinsi ulivyo na ngozi nene."

Rodney mwenye ngozi nene alikosa la kusema.
Kama angekuwa yeye huko nyuma, angekuwa amegombana na Pamela tayari. Lakini sasa, midomo yake myembamba iliishia tu kusogea, lakini alifunga mdomo wake kimya kimya.

Lifti ilipofika, Rodney alifuatana na Alvin na Lisa kuingia kwenye gari la Alvin. Pamela alikaa kwenye gari la Eliza. Gari la Lisa likarudishwa na Logan. Kwa hayo wakaelekea mgahawani.

Wakiwa njiani Alvin alimshika Lisamkono kwa mkono mmoja huku akiushika usukani kwa mkono mwingine. "Lisa, wakati bilioni 1o zitakapofika, nitakuhamishia kwenye akaunti yako."

“Hakika.” Lisaaliitikia kwa kichwa.

Macho ya Alvinyalimtoka kwa mshangao. "Nilidhani itachukua muda kukushawishi kuipokea."

“Unawaza sana. Ninawawekea Suzie na Lucas. Nani anajua nini kitatokea baadaye? Ni bora niwaachie pesa zaidi kwa ajili ya ulinzi wao,” Lisa alisema kwa unyonge.

“Jambo pekee litakalotokea wakati ujao ni kwamba siku zote nitakupenda zaidi na zaidi,” Alvin alikiri kwa upole.

Lisa aliona haya. “Tafadhali. Kuna mtu mwingine ndani ya gari.”


Alvin hata hakutazama nyuma huku akitabasamu vibaya. “Kweli? Kwa nini sioni chochote? Nina wewe tu machoni mwangu."


"Acha ujinga." Lisa alijifanya kuwa na hasira. "Mimi nakuchukia tu."

Rodney, ambaye alichukuliwa kama hewa, aliringishiwa kwa mapenzi yao ya hadharani njia nzima. Alipata uzoefu wa jinsi alivyohisi kuwa mtu wa tatu. Ikiwa angejua, angeenda na Pamela. Angependelea kulengwa naye kuliko kutazama mapenzi yao ya hadharani baada ya kutengana kwake.

Wakiwa katikati ya safari, Alvin alipokea simu kutoka kwa Chester. “Nimesikia umeshinda. Hongera sana. Chakula cha jioni kinapaswa kuwa kitamu kwako."

“Hicho ndicho ninachopanga kufanya. Kwanini usijiunge nasi?” Alvin alimkumbusha, “Lakini huruhusiwi kumleta Cindy.”

“Hakika.”

Baada ya kukata simu, Alvin alimtazama Lisa kwa wasiwasi. “Lisa, ni sawa nikimwalika Chester? Ikiwa hupendi, nitamwambia asije mara moja.”

“Ni sawa. Nilikubali hata yule aliyekuwa kwenye siti ya nyuma aingie kwenye gari.” Lisa alitabasamu. "Mbali na hilo, alinisaidia kushughulika na Kelvin mara ya mwisho, kwa hivyo nina deni kwake."
 
“Asante, Lisa.” Alvin alitabasamu kwa upendo.
Muonekano huo ulimfanya Rodney kukosa la kusema kabisa.

Mara walipokuwa kwenye mgahawa, Lisa na wanawake wawili walitembea mbele, na hatimaye Rodney alipata nafasi ya kumshika Alvin. “Alvin, umezidi sana. Tangu umerudiana pamoja na Lisa, Chester na mimi tumekuwa hatuna maana kwako.”
"Ni vizuri unajua. Ukitaka urafiki wetu uendelee, usimuudhi mke wangu.” Alvin alisema kwa umakini, "Ikiwa ataniambia nisikukaribie sana, hakika nitamsikiliza." Alvin akampiga begani kwa huzuni. "Baada ya kufikisha miaka thelathini, ninagundua kuwa ninachotaka zaidi ni nyumba bora. Kurudi nyumbani kwa watoto wangu wa kupendeza na mke mzuri baada ya kazi kila siku ni jambo zuri zaidi maishani.”

Rodney aliganda kwa maneno hayo. Alikuwa akifikiria juu ya maisha kama hayo na Sarah, lakini bila huruma alitupwa kama blanketi lenye maji.

“Huwezi kuelewa hisia hii,” Baada ya hapo, Alvin alisonga mbele ili kumpata Lisa.

Rodney alikasirika sana. Alvin alijivunia watoto, na yeye si alikuwa na mtoto pia? Kisha, akatazama nyuma ya Pamela lakini akamuona akitangulia mbele huku akimshika mkono Eliza. Hakuacha hata kumtazama.

Mhudumu alikiongoza kikundi hicho cha watu kwenye chumba bora zaidi cha kibinafsi katika mgahawa huo. Ilikuwa mtindo wa Kijapani, kwa hiyo iliwahitaji kuvua viatu vyao.

Meza ndani ya chumba ilikuwa ya mstatili, na upande mmoja unaweza kukaa watu watatu. Alvin na Lisakawaida walikaa upande mmoja na kuacha kiti tupu karibu nao.

Wakati huo huo, Pamela na Eliza walikaa upande mwingine. Rodney alitazama kushoto na kulia kabla ya kuchagua kuketi kwenye kiti kilichokuwa wazi karibu na Pamela.

“Nani amekuruhusu kukaa hapa? Nenda ukaketi karibu na Alvin.” Pamela alimtazama kwa hasira.

Rodney hakuwa na furaha. Lakini, alijua kwamba ikiwa uhusiano wake na Pamela hautaboreka, mtoto wake hatamkubali katika siku zijazo. Kisha, kurudi kwa familia ya Shangwe itakuwa nje ya equation. "Pamela, najua nilikosea. Ninakuomba msamaha, sawa? Wacha yaliyopita yawe yamepita. ”

Kama ilivyotarajiwa, uso mzuri wa Pamela ulijaa hasira. “Unaweza kuruhusu yaliyopita yapite kwa maneno machache tu, lakini wewe ndiye uliyegeuza maisha yangu kuwa chini. Isingekuwa mtoto huyu, ningeweza kutafuta mchumba na kuendelea na mahusiano sasa. Kama usingeniburuza ili kutoa mimba, nisingeanguka kutoka kwenye ngazi. Ikiwa ningempoteza mtoto, nisingeweza kupata ujauzito tena maishani mwangu. Watu kama wewe ni wabinafsi sana."

Uso wa Rodney uliwaka moto kwa kukemewa mbele ya kila mtu. “L-lakini isingekuwa kwa sababu ya huyo mtoto, usingekuwa binti wa familia ya Shangwe. Baba mdogo wangu hivi karibuni atakuwa Rais wa nchi, na wewe utakuwa binti wa Rais…”

“Hah. Nyamaza tu kama hujui kuongea. ” Pamela alikasirika. "Familia ya Masanja pia ni familia ya wasomi. Sijawahi kukosa pesa tangu nizaliwe. Unafikiri nataka kuwa binti wa Rais? Mbali na hilo, kuwa binti wa Rais si rahisi kama unavyoweza kuwa. Siwezi kuwa huru kama nilivyokuwa zamani, na lazima nijuane na kila aina ya waheshimiwa. Watu watanitendea kwa fadhili kijuujuu, lakini nyuma ya migongo yangu, wananidharau na kusema kila aina ya mambo mabaya.”

Rodney aliganda na kuinamisha kichwa chake kimya kimya. Kadri Pamela alivyozidi kuongea ndivyo alivyozidi kukasirika. Hata macho yake yalikuwa mekundu. “Nilikuwa nikifikiria kuwa na upendo wa kawaida, kuoa, na kuwa na watoto. Hata hivyo, nina mimba kabla sijaolewa. Tumbo langu halionekani sasa, lakini linapokuwa kubwa, itabidi nijitokeze nje ya nchi ili kujifungua mtoto wangu. Umeharibu maisha yangu.”

Kama asingejizuia, angemwaga maji ya moto usoni mwa Rodney. Kwa maneno yake, Rodney alihisi huzuni sana, na haikuwa hisia nzuri. Alihisi uchungu kana kwamba amekula kibuyu kichungu.
Ilibidi akubali kwamba alikuwa amemuumiza Pamela. Ikiwa si karamu hiyo ya uzinduzi wa bidhaa na yeye kuwaalika Sarah na kaka yake, Pamela asingetiliwa dawa kwenye kinywaji na Thomas na kupata mimba baadaye kwa sababu Jessica aliwapanga kimakusudi. Alikuwa mwathirika tangu mwanzo hadi mwisho.

Sura ya: 673
 
Kama... Laiti angekubali mpango wa familia ya Shangwe na kumuoa wakati huo, mtoto angekuwa na familia kamili, na Pamela asingekuwa mjamzito kabla ya ndoa. Kwa bahati mbaya, hapakuwa na dawa ya majuto katika ulimwengu huu.

Lisa akahema. “Pamela yuko sahihi. Hakutaka kumuweka mtoto mwanzoni pia. Dada yako ndiye aliyemtisha, akisema kwamba familia ya Masanja ingekandamizwa ikiwa angetoa mimba mtoto huyo.”

"Samahani ... samahani sana." Rodney alijuta. “Vipi... nikuoe? Nitachukua jukumu kwa hilo. Hakika nitakuwa mwema kwako na kwa mtoto katika siku zijazo." Ingawa hakumpenda Pamela, alikuwa tayari kuchukua jukumu.

"Katika ndoto zako." Pamela alikasirika. “Je, unanistahili? Wewe ni kipande tu cha sh*t ambacho Sarah alichoka kucheza nacho. Mimi si pipa la kukusanya takataka ambazo watu hutupa.”

Kwa kuguswa na maneno ya Pamela, Rodney alibadilika rangi na kufadhaika. "Inatosha, Pamela. Maneno yako ni makali mno. Kila mtu amepata mshtuko kwa wakati mmoja katika maisha yake. Hata Alvin…”

"Usinivute katika hili." Hapo hapo Alvin aliushika mkono wa Lisa kwa woga na kumkazia macho Rodney kama onyo.

Akiwa amehuzunika, Rodney alikuwa na kidonda cha ubongo, na akasema bila fahamu, “Je, wewe pia hukuachwa hapo awali? Wewe pia ni takataka. Sisi sote ni takataka, kwa hivyo tumesafiri katika mashua moja.”

Kwa maneno hayo, sura nzuri ya Pamela ilibadilika kuwa nyeusi kwa hasira, na kila mtu akanyamaza pia.

Lisa na wengine wakashusha nyuso zao. Hawakuwahi kuona mtu yeyote mwenye akili duni ya kihisia kama Rodney. Alikuwa mtaalamu wa kupaka chumvi kwenye vidonda vya watu.

Alvin akammiminia kikombe cha chai. “Rodney, kama hujui kuongea, basi kunywa chai yako kimya kimya. Usiharibu hali ya hewa.”

Rodney alipepesa macho na kugundua kuwa hali ya hewa ilikuwa imezimwa. Kwa hivyo, alisema haraka, "Nilichomaanisha ni ... Sote wawili tumepitia masaibu sawa na tuna uhusiano..."

“Rodney Shangwe, tafadhali funga mdomo wako. Afadhali kupata kipande kingine cha taka kuliko kukubali takataka ya Sarah. Mbali na hilo, kwanini usijiangalie kwenye kioo? Je, unanistahili? Mimi ni tajiri na nina nguvu, ninaungwa mkono na Rais wa baadaye, na mimi ni mrembo. Na wewe je? Una nini? Una matako tu yasiyo na maana ambayo yamepigwa bakora.”

Alvin alitema chai yake. Eliza na Lisanao wakacheka. Uso wa Rodney ukageuka mwekundu kwa aibu. Alijiuliza sana ikiwa mdomo wa Pamela ulikuwa na memory card ya maneno ya shombo.

“Mnacheka nini jamani?” Mlango ukafunguliwa ghafla, Chester akaingia ndani akiwa amevalia mavazi ya kawaida. Alibeba sura ya utulivu na ya kifahari na tabasamu la upole kwenye midomo yake ya kupendeza.

"Chester, uko hapa." Rodney alimtazama kama kaona mwokozi.


Macho ya Eliza pekee yaliangaza. Aliinamisha kichwa chake na
kunywa kutoka kikombe chake cha chai.


"Nini kimetokea?" Chester alitazama pande zote. Kiti pekee cha kando ya Alvin kilikuwa tupu. Akavua viatu vyake na kwenda kuketi. Kinyume chake aliketi mwanamke mwenye ngozi nyeupe kama theluji.

Eliza alikuwa amevaa suti nyeusi huku nywele zake ndefu zikiwa zimelala mabegani mwake. Ikiwa angekuwa mwanamke wa kawaida, angeonekana kuwa mwepesi. Lakini, sura yake ilikuwa laini na nzuri, na ngozi yake ilikuwa safi. Kwa tofauti ya nyeusi na nyeupe, alionekana kuwa kama mwanamitindo. Hata hivyo, alifyonza chai yake huku akitazama simu yake. Hakumtazama hata moja kwa moja.

Chester aliinua uso wake. Ili kumlinda, Pamela alisema mara moja, “Bwana Choka, huyu ni rafiki yangu Eliza. Yeye ni staa mkubwa wa filamu, lakini tafadhali usiwe na mawazo yoyote machafu kumhusu. Unafunga ndoa hivi karibuni.”

Chester alicheka kwa sauti ya chini. “Bi Masanja, usinifanye nionekane kama mtu anayepata mawazo juu ya wanawake wakati wowote na mahali popote.”

Pamela alipepesa macho na kusema bila hatia, “Sikufanya hivyo. Nilisikia tu kwamba Bwana Choka ana sifa ya kutopitwa na pisi kali, kwa hivyo nilikuwa na wasiwasi kidogo.”
 
"Basi umenielewa vibaya." Chester alimtazama Eliza na kutabasamu. "Mara nyingi, wanawake hunitazama kama paka anayetazama samaki. Wanataka kuwasaliti wenza wao na mimi, haswa... mastaa wa kike.”

Kwa maneno hayo, Pamela na Lisa wote walikosa furaha kidogo.
Baada ya yote, walikuwa wamemwalika Eliza. Uvumi wa Chester ulikuwa mwingi sana.

Alvin na Rodney pia waliona ni ajabu kidogo. Baada ya yote, ingawa Chester alikuwa mhuni, mara chache alimdhihaki mwanamke kimakusudi.

“Bwana Choka...” Lisa alikunja uso.
Lakini, Eliza alizungumza kwanza. “Naweza kuelewa. Nilisikia mke mtarajiwa wa Bwana Choka pia ni staa wa kike. Alipokuona kwa mara ya kwanza, lazima alikuwa kama mbwa anayeona mfupa.”

Lisa na Pamela karibu wapige makofi. Hii ilikuwa inaashiria kwamba Cindy alikuwa mbwa. Jinsi ya kushangaza.

Chester alicheza na kikombe cha chai. “Eliza, mara ya mwisho nilikuhurumia sana? Watu wanapaswa kuwa na akili wazi baada ya kupoteza, na haijalishi ni nini, kupoteza ni kupoteza."

“Huruma?” Eliza alionekana kama anasikia mzaha."
Labda huelewi maana ya neno hilo."


Midomo myembamba ya Chester ikacheza kwa jazba.


Alipohisi kwamba hali haikuwa sawa kabisa, Alvin alikatiza mara moja, “Chester, wewe na Bi Robbins mnajuana?”


"Ndio, yeye ni staa mdogo tu kutoka kwa uwekezaji wangu, Felix Media," Chester alisema kwa unyogovu.

"Ndio, mimi ni staa mdogo sana. Mwaka huu, niliingiza mamia ya mamilioni kwa Felix Media, "Eliza alisema bila kujali.

“Hiyo ni nyingi?” Chester akacheka.

Eliza akatabasamu. “Bwana Choka, hupaswi kusema mambo kama hayo hadharani. Utashutumiwa hadi kufa.”

“Nani angethubutu?” Chester aligonga meza tena na tena.

Chumba kilikaa kimya tena.
Alvin na Lisa walitazamana na kuona maumivu ya kichwa machoni mwa kila mmoja. Mlo huu ulikuwa wa machafuko sana.

Hapo awali, ilikuwa Pamela na Rodney wakipigana. Chester alipofika sasa ikawa Chester na Eliza wanarushiana visu.



“Kwa nini hatuna kinywaji?” Alvin alibadilisha mada.

“Hakika.” Eliza na Chester walisema kwa wakati mmoja.

Kisha, macho baridi na safi ya Eliza yakamsogelea Chester, ambaye alitabasamu. "Kweli tuna kemistri nzuri."

Pamela aligonga meza. "Bwana Choka tafadhali kumbuka unafunga ndoa na Cindy Tambwe."

Chester alikosa la kusema. Kipindi Cindy alipotajwa, alihisi kuchukizwa.
Pamela alijua jinsi ya kugusa sehemu ya kidonda.

Chester alimtazama Rodney. “Mtunze mama wa mtoto wako. Kuna vitu vingi ambavyo mjamzito hawezi kula, hasa chakula kibichi.”

Pamela, ambaye alikuwa karibu kuchukua kipande cha sashimi, alikasirika. Huyo Chester! Alimlaani kwamba mtoto wake azaliwe kilema.

"Chester ni daktari. Msikilize.” Rodney mara moja akaivuta sashimi iliokuwa mbele yake.

Pamela akashusha pumzi nyingi sana, na Lisa akasema kwa haraka, "Acha ajaribu moja. Kipande kimoja ni sawa."

“Sawa. Kimoja tu." Rodney alimpa kipande kidogo zaidi.


"Siyo kazi yako. ” Pamela alitaka kulipuka sana.

“Bila shaka ni kazi yangu. Namjali mtoto wangu.” Rodney alisema kwa makini, “Ingawa hunitambui, huwezi kunizuia kumtunza mtoto.”

Pamela hakuweza kuhangaika naye akaosha tu sashimi aliyompa kwa maji baridi tena.
Uso wa Rodney ulitiwa giza. “Mimi si mgonjwa.”

“Sijui kuhusu hilo. Umekaa na Sarah kwa muda mrefu sana. Labda umeambukizwa na kitu."

Uso wa Rodney ukawa mwekundu kwa hasira. Baada ya muda mrefu, sauti ikatoka kwenye koo lake. "Sijafanya chochote na Sarah, sawa?"

“Ahem.” Alvin na wengine wakakohoa.

Chester alimpa sura isiyo ya kawaida. “Wewe pia huwezi kufanya hivyo?”

“Bila shaka naweza.” Rodney alitabasamu. “Mimi si mtu wa kufanya fujo na wanawake wengine. Ninaamini katika ngono baada ya ndoa.”


Sura ya: 674




Baada ya pause, akamgeukia Pamela. "Kilichotokea kwetu ni ajali."


Pamela, ambaye alitajwa ghafla, aliingiwa na aibu.


"Unamaanisha mimi na Alvin tunachafuana na wanawake wengine?" Chester ghafla alisema.

"...Hapana." Rodney aliinamisha kichwa kwa haraka na kula kimya kimya. Alijuta. Ikiwa angejua mapema, asingeenda kwa chakula hicho. Ilikuwa inachosha.
 
“Tuache mambo ya nyuma. Hongera.” Lisa aliinua glasi yake kutoa toast, ishara ya kuwakaribisha watu kwenye kinywaji.

Rodney akaichukua, akaifikiria na kuiweka chini tena. "Bado sijaruhusiwa kunywa pombe."

“Ninaendesha gari,” Eliza alisema.

Alvin naye akasema "Mimi pia ninaendesha gari."

Lisa alikosa la kusema. Mwishowe, pekee walioweza kunywa walikuwa Chester na yeye.

"Bwana Choka, hongera kwa harusi yako." Lisa aliinua glasi yake. "Natumai utapata mtoto hivi karibuni."

Chester alishindwa cha kusema. Hakuweza kunywa toast hiyo. Hakutaka baraka hiyo.

Kisha, akiogopa kwamba watu hawa wangebishana tena, Alvin alibadili mada na kuzungumzia mambo fulani katika ulimwengu wa biashara.

Lisa alikula kwa muda na ghafla akamtazama Eliza. "Oh, unapenda sill pia? nilikuwa na rafiki ambaye alipenda hii." Lisa alikuwa akirejerea Charity, bila kujua Eliza ndiye Charity.

“Ndio, Ch…” Pamela alisema herufi mbili kabla hajasongwa mara moja.
Hata hivyo, wanaume hao watatu walijua alikuwa akizungumza kuhusu nani, Charity.

Chester aliganda na kupoteza mawazo kwa sekunde mbili. Mkono wa Eliza kwenye vijiti vyake ukatulia vilevile, kisha akatabasamu. "Nadhani sill ni nzuri. salmoni nyingi hunifanya niwe mgonjwa.”

"Ndio, lakini nadhani ... sill nyingi pia zitanifanya niwe mgonjwa." Chester alichukua kipande cha sill na kuinua uso wake.

Eliza aliinua macho na kukutana na macho ya kina ya mtu huyo. Angeweza kupata ladha ya uhasama katika macho yake, na yeye akahamaki. "Bwana Choka anaweza hata kuugua kwa kuwa na wanawake wengi, achilia mbali samaki."

“Hakika unanifahamu vizuri.” Chester alitabasamu kwa kupendeza.
Watu ambao hawakujua wangefikiri kwamba walikuwa wakitaniana.


“Siwezi kujizuia. Nimeona watu wengi kama wewe kwenye mduara wa burudani. ” Eliza alimpuuza.

"Pia nimeona wanawake wengi kama wewe… " Chester akazungusha glasi yake. "Wakijaribu kuvutia umakini wangu, kama vile ..." Macho yake yakawa giza, na ghafla akanyamaza.

Macho ya Eliza yalikuwa yamejaa hali ya kumpuuza. Baada ya kumsubiri kwa utulivu kwa muda na kuona kwamba hakuendelea na kauli yake, aliendelea kula.

Tabia yake ya kupuuza ilifanya macho ya Chester kuwa baridi. “Mbona hausemi chochote?”

“Sijui niseme nini.” Eliza alikula kipande cha samaki, akakitafuna kwa uangalifu, na akakimeza kabla ya kusema, “Kwa hiyo ngoja ninyamaze, usije ukatishia kuni’blacklist tena.”

Chester alitazama harakati zake za polepole, na mikondo ya chini kwenye kilindi cha macho yake iliongezeka.

Pamela alitaka kumtetea Eliza mwanzoni. Hata hivyo aliangua kicheko baada ya kusikia maneno ya Eliza. "Hiyo ni kweli. Wanaume hawana akili wakati mwingine. Hebu tule.”

Katikati, Chester aliinuka na kwenda uani. Wakati ananawa mikono, Alvin alitokea kwa nyuma. “Haya, umenitia aibu sana usiku huu. Lisa ndiye aliyemwalika Eliza. Sijali ni malalamiko gani uliwahi kuwa naye hapo awali, lakini hukuhitaji kumlenga mara nyingi wakati wa chakula."

“Kwani ni mimi?” Chester hakukubali jambo hilo hata kidogo.

“Unakataa kuwa si wewe?” Alvin alimtazama pembeni. "Hebu ona jinsi unavyoonekana sasa. Unaonekana unataka kulala naye, lakini amekukataa, kwa hiyo hamjapatana na unataka kuharibu furaha yake ili kuweka sawa hisia zako.”

"Wewe una wazimu." Chester alimkaripia.

"Hujawahi kuwa hivi." Alvin akavuta tishu na kuifuta mikono yake.


Chester alikunja uso na kuivuta sigara yake. “Kwanini Eliza yupo hapa? Pamela na Lisa wanamfahamu?”

“Hata mimi sina uhakika sana. Nilimuona akiwa amekaa na Lisa na wengine nilipomaliza kesi. Rodney alisema wamekutana leo tu.”

“Eliza alikuja kukuona mahakamani?” Chester aliinua nyuso zake.

“Ndiyo.” Alvin kisha akaingia katika choo.


Waliporudi chumbani walikuta kiti cha Eliza hakina mtu.

"Eliza alisema kuna kitu kilitokea, kwa hivyo akaondoka." Pamela alimtazama Chester kwa huzuni. “Bwana Choka, najua Eliza ni mwigizaji tu machoni pako. Unaweza kumdharau, lakini huwezi kwenda mbali na maneno yako.”
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…