SIMULIZI......LISA
KURASA.....91-95
Sura ya 91
Lisa aliishia kuguna tu. Alitaka kulia. Bilioni moja? Hakuwa na uwezo wa kumlipa hiyo pesa.
Sam naye aliligundua hilo na kumpa sura ya huruma. “Lisa, hutaweza kamwe kuepuka makucha ya Alvin kwa maisha yako yote.”
Lisa alikohoa na kusema. “Nilikosea."
Sam aliongeza kwa upole. “Hata hivyo, Mawenzi Investiments wanathubutu vipi kukuumiza bila kutoa maelezo?! Hakika nitavuruga mradi wao wa uendelezaji mali.”
"Nilisikia kwamba Mawenzi Investiments imegeuka kutoka kuwa biashara ndogo na kuwa moja ya biashara 100 bora Tanzania ndani ya muongo mmoja tu. Imekuwa ikifanya vyema kwa miaka hii yote kwa sababu kuna nguvu ya ajabu inayoiunga mkono," Hans ghafla alisema.
Kauli hiyo ilimshtua Sam. Alvin alifungua mdomo wake na kuongea “Ndio. Yuko sawa. Nenda kachunguze kama kilichotokea leo ni mpango wa makusudi au makosa ya kibinadamu, Hans."
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. "Labda ilikuwa ajali kwani sikumkosea mtu yeyote hapo Mawenzi Investiments. Kando na familia ya akina Jones Masawe, Janet, na Cindy, sidhani kama nina tatizo na mtu yeyote hapa Dar!”
"Shemeji, umewaudhi watu wengi, huh?" Sam aliongea kwa kejeli kidogo.
Alvin alimtazama na kusema kwa jeuri, “Haijalishi. Mradi tu uko chini ya mbawa zangu, nitakulinda hata kama ungemkosea kila mtu hapa Tanzania.”
Hans na Sam walikosa la kusema. Wakiwa kama mabachela, waliona kwamba uwepo wao haukuwa wa lazima.
"Hans, afadhali tuondoke.” Sam alikohoa huku akikunja ngumi mdomoni. “Kwa kuwa Alvin aliumia wakati akimwokoa Lisa, Lisa atalazimika kumhudumia Alvin. Niko sawa, Lisa"
"Ndio ndio. Hamna shida.” Lisa aliitikia kwa haraka.
Hans na Sam walipoondoka tu ndipo Lisa alipogundua kwamba haikuwa rahisi kwa mwanamke kama yeye kumwangalia Alvin. Hata hivyo, kwa kuzingatia kwamba alikuwa amekubali mbele yao, hangeweza kuvunja ahadi yake. Kwa bahati nzuri, ilikuwa wodi maalum yenye vifaa kamili ambapo angeweza hata kupika. Ilikuwa kama ghorofa kubwa.
"Una njaa? naenda kukununua…”
"lam. Nataka nyama ya nguruwe iliyochomwa.” Akiwa amelala kitandani kwa unyonge, Alvin alimtupia jicho.
Lisa alishindwa cha kusema. “Umesahau ushauri wa daktari kuwa huwezi kula chakula chenye mafuta? Vinginevyo, hutapona vizuri.”
“Haijalishi. Hakuna kitu kibaya sana na mwili wangu. Sijambo.”
"Hapana. Sitakupikia. Nitasimamia menyu yako wakati ukiwa hospitalini." Lisa alionyesha sura ya msimamo. Alvin aliinua uso wake lakini hakuwa na hasira.
“Lala tu upumzike hapa. Nitaenda kutafuta mboga.” Baada ya kumkumbusha Alvin, Lisa alishuka haraka haraka kwani aliogopa kumuacha peke yake kwa muda mrefu. Alirudi baada ya kununua nyama na mboga kwa haraka.
Alvin aliitazama mboga iliyokuwa mikononi mwake kwa sura isiyoelezeka. “Unapanga kunipikia chakula cha kawaida na viungo hivi?”
“Nimebaki sina jinsi. Hivi ndivyo viungo pekee vilivyouzwa nje ya hospitali, na wewe ndiye ulitaka nikupikie.” Kisha Lisa akasema kwa uchungu, “Usijali, hakika nitatayarisha chakula kitamu.”
Alipoelekea jikoni kuanza kupika, Hans alikuja tena.
“Umekuja kwa wakati ufaao. Nenda ukalete viungo vizuri vya chakula hapa,” Alvin alisema, “Jaza viungo kwenye friji.”
“Sawa.” Ndani kabisa, Hans aliendelea kunung'unika. 'Utakaa hapa kwa siku chache tu. Pia hutabaki hapa kabisa.' Lakini hakusema hivyo na badala yake akasema kilichompeleka. "Aah bosi, nilirudi baada ya kumaliza kuchunguza tukio la ajali yenu kule Mawenzi Investiments. Tofali lilianguka kwa sababu mfanyakazi alishindwa kulishikilia vizuri alipojaribu kuliweka kwenye ukuta wa nje.”
Alvin alikunja paji la uso wake kwa hasira. “Hakuna chochote cha kutilia shaka kuhusu hilo. Vipi kuhusu yule mtu aliyemuongoza Lisa pale? Alionekana kuwa salama wakati huo.”
"Alidai kwamba alikuwa na jukumu la kumwongoza Miss Jones kuchukua vipimo. Wakiwa njiani, wawili hao walikuwa wamezama sana katika mazungumzo kiasi kwamba alisahau kumpa Miss Jones kofia ya chuma ya usalama.”
"Hata hivyo, anahitaji kubebeshwa lawama za ajali hii," Alvin alisema kwa upole, "Tuma barua ya mwanasheria wa Mawenzi Investiments. Ikiwa fidia ambayo Mawenzi Investiments itatoa si ya kuridhisha, sitawaacha salama.”
“Sawa.”
Wakati huo, Lisa alileta chakula kwenye meza. Alipogundua uwepo wa Hans, alipigwa na butwaa. "Samahani, nimeandaa chakula cha watu wawili tu."
'Ni sawa. Tayari nimekula. Hata hivyo, nitaondoka baada ya muda mfupi.” Macho ya Hans yalizama kwenye chakula kilichokuwa mezani, jambo lililomshtua. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Bw. Kimaro akiwa na mlo wa kawaida hospitalini. Kwa kweli, milo ya Alvin ilijumuisha zaidi ya aina kumi za vyakula. Kilichomshtua zaidi Hans ni kwamba Alvin hakuongea chochote kuhusu hilo.
Baada ya Lisa kuweka vyakula vyote, aliutupia macho mkono wa Alvin wa kushoto ambao bado angeweza kuutumia. “Unataka nikulishe? Au bado unaweza kula peke yako?"
“Upuuzi gani unaongea. Nitakulaje kwa mkono wangu wa kushoto tu?” Ndita usoni kwa Alvin zilikunjamana.
Mdomo wa Hans ulitetemeka. “Tafadhali, Bw. Kimaro. Mkono wako wa kushoto una nguvu zaidi kuliko mkono wako wa kulia. Na ndiyo unaotumia mara kwa mara”
“Ondoka sasa hivi.” Alvin alimtimua Hans bila huruma.
"Ndiyo ndiyo, bosi, natoka sasa hivi.” Hans alikimbia.
“Mbona unakuwa mkali sana kwa Hans? Nadhani yeye ni mzuri sana." Lisa hakuweza kujizuia kumuonea huruma Hans.
“Yeye ni mzuri?” Macho ya Alvin yalimtoka kwa huzuni. "Je, yeye ni mzuri kuliko mimi?"
Lisa alikuwa ameduwaa kwa muda. Ghafla, macho yake yakawa ya kushangaza. "Inaonekana ... una wivu."
“Mwenye wivu?” Uso wa kuvutia wa Alvin ulianguka kwa sekunde. Sentensi hiyo ilionekana kama mzaha kwake. “Naweza hata kupata wivu kwa sababu yako? Hivi ndivyo ambavyo huwa unajidanganya? Najaribu kukukumbusha tu, wewe usiye na shukrani. Usisahau ni nani ambaye amekuokoa mara nyingi."
"Ni wewe. Nakumbuka ni wewe. Haraka basi uanze kula. Usife njaa, la sivyo nitakosa mtu wa kunikoa siku nyingine.” Kwa vile Lisa hakutaka tena kusikiliza mihadhara yake, alimshawishi haraka kula huku akimlisha.
Hizi zilikuwa aina za vyakula vya kawaida ambavyo Alvin hakupenda kula wakati huo. Hata hivyo, mara tu Lisa alipomlisha chakula hicho, alikiona kitamu sana hivi kwamba akaomba zaidi.
Baada ya kula, Alvin alifumbua macho kwa uvivu. “Niinue. Nataka kwenda chooni.”
Lisa alijaribu kumuinua. Kwa mawazo ya mgongo wake uliojeruhiwa, alisita kabla ya kuweka mkono wake kiunoni mwake. Kiuno chake kilikuwa chembamba sana. Aliweza hata kuhisi misuli yake kupitia gauni jembamba la hospitali. Alvin akaketi. Vidonda na mshono kwenye bega lake vilimuuma sana hivi kwamba alitokwa na jasho baridi mara moja. Uso wake ulikuwa umepauka sana.
Kwa mshtuko, Lisa akasema mara moja, “Usishuke. Nitakuletea beseni.”
Mara moja akapata beseni mpya kutoka kwenye kabati kando yake. Alvin alivuta mdomo kwa kuhisi maumivu. Muda mfupi baadaye, alinong'ona, "Ninahitaji msaada wako."
Lisa alikosa la kusema. "Je! huna mkono mwingine?" Aliuliza kinyonge.
“Huoni jinsi maumivu yanavyokuwa yanavyoongezeka nikijisogeza?” Alvin alijaribu kusogeza mkono wake, na akasaga meno yake kwa ghafla. "Harakisha. Vinginevyo, nitajikojolea.”
Sura ya 92
Akiwa amejawa na aibu, Lisa alisogea mbele na kuingiza mkono wake ndani ya shuka aliliokuwa kajitanda Alvin. Hatimaye Alvin alishindwa kukojoa kwani Lisa alihangaika tu akiogopa kushika nanihii yake!
“Utachukua muda gani?” Alvin alimtazama kwa haya.
Akiwa amedhamiria moyoni, Lisa akataka kuishika na kuitoa nje….Muda huo huo daktari akaingia. "Bwana. Kimaro, ngoja niangalie…” Kwa kuona hali hiyo, daktari aliona haya huku akiwa amesimama palepale akiwa ameganda. “Samahani. Samahani. Nilikuja kwa wakati mbaya? Ninaondoka sasa hivi… Sasa hivi…”
Lisa alitoka haraka kwa Alvin. Alikuwa katika butwaa. Daktari aliwaelewa vibaya?
“Hapana, Dokta. Nilikuwa tu - "
"Usijali, na sikuona chochote. Nitakuja tena baada ya muda mfupi. Mnaweza kuendelea.” Akiwa na uso wenye haya, daktari alikwepa macho yake. Kisha mara moja akatembea hadi mlangoni.
Alipoufikia mlangoni, hakuweza kujizuia kugeuka. “Najua nyinyi wawili bado ni vijana, lakini afadhali muwe waangalifu. Kwani, ametoka tu kufanyiwa upasuaji.”
“Sikuwa…” Kabla Lisa hajamaliza sentensi yake, daktari aliondoka kwa haraka.
Lisa alibaki hoi. Jinsi alivyotamani kuruka kutoka kwenye jengo hilo na kukatisha maisha yake kwa aibu. Kwa hasira, akamtazama yule mchochezi Alvin pale kitandani. "Yote ni kazi yako."
“Imekuwa mimi ndiyo sababu siyo?” Alvin aliongea huku akivumilia maumivu. “Pengine. Sikupaswa kukuokoa wakati huo. Labda ungekuwa umelala kwenye chumba cha kuhifadhia maiti chenye barafu kufikia sasa. Basi nisingehitaji kuomba msaada wakati wa kutumia choo…”
“Inatosha. Acha mada zako za kijinga!” Lisa alifadhaika. "Sitakulaumu kwa kuwa wewe ni mkombokozi wangu."
“Vizuri.” Alvin alifumbua macho. "Unaweza kunisaidia sasa."
Lisa akashusha pumzi. Aligeuka huku akionyesha mkanganyiko kwenye uso wake mdogo mzuri. “Je, nimuombe Hans aje? Sitaweza kufanya hivyo. Tangu nilipoona mwili wako mzuri, siwezi kuacha kufikiria juu yake. Naogopa nita…”
“Midomo myembamba ya Alvin ilipinda na kuwa tabasamu la kuvutia. Akamwambia kwa tabasamu la utani. "Hata hivyo, ni nusu ya juu tu ya mwili wangu ndiyo imejeruhiwa."
Lisa alikaribia kuuma ulimi wake. Wakati huo, alifunga mlango na kukaa macho.
Ingawa aliuona mwili wake mara moja siku za nyuma, ilikuwa ni mtazamo wa haraka tu. Hakuwahi kuona kama alivyokuwa anafanya wakati huo. Alikuwa na umbo zuri sana, lililofanana na sanamu ya David, aliyejengeka vizuri.
Hah. Wakati ule hakupendezwa naye hata kidogo, na ilionekana kuwa alikuwa akijaribu kumnyanyasa kila alipoutazama mwili wake. Sasa ilikuwa ni nafasi yake kwa macho yake. Hmmph.
Alvin aliona sura yake. Alijua kwamba kwa muda mrefu macho ya Lisa yalikuwa yamelala juu ya mwili wake. "Harakisha. Utaendelea kujivuta hadi lini?" Alvin alimharakisha.
Kwa aibu, Lisa alifumba macho. Haraka akamalizia kumtolea ‘chululu’ yake na Alvin akakojoa.
Baada ya hapo alimuogesha kwa kumfuta na kitambaa palepale kwa sababu hakuweza kwena bafuni. Baada ya kuoga alijilaza nae kwa pembeni kwenye kitanda huku taa zikiwa zimezimwa.
Alvin hakumruhusu kulala naye. Mwanamke huyo alikuwa hajui kutumia nafasi ya kitanda na alikuwa akibiringita hovyo kitandani. Sasa kwa kuwa alikuwa amejeruhiwa, hakuweza kumudu kulala naye vinginevyo angetoneshwa majeraha yake yote.
Lisa hakuthubutu kulala fofofo. Katikati ya usiku, alimsikia mtu huyo akijirusharusha na kugeuka. Aliinuka na kuuliza kwa wasiwasi, "Je, unajisikia vibaya?" Alvin alifumbua macho.
Mwale wa mbalamwezi uliangaza kwenye mabega ya Lisa kupitia dirishani. Usiku huo, hakufanikiwa kurudi nyumbani kuchukua nguo zake, hivyo alikuwa amevaa tu nguo nyepesi ya ndani. Huku nywele zake ndefu na laini zikianguka juu ya mabega yake, alionekana mrembo na mzuri mithili ya video-vixen.
Maumivu bado yalikuwa yanavumilika kwake. Hata hivyo, kitu kingine kilitoka kinywani mwake. "Ndio, naumia."
“Nfanye nini?” Lisa alishikwa na hatia. “Ngoja nimpigie simu daktari.”
“Kuna umuhimu gani wa kumwita daktari? Hawezi kusaidia kupunguza maumivu yangu pia." Alvin alifumba macho, na macho yake yalionyesha kuchanganyikiwa. Akaachia mguno kwa unyonge. Alijifanya kana kwamba anajitahidi sana kuvumilia maumivu hayo. Usemi huo, pamoja na uso wake wa kuvutia, ulimfanya Lisa aushike mkono wake bila kujua. “Je, kuna chochote ninachoweza kukufanyia?”
“Utanisaidia?” Akafungua macho yake meusi.
“Ndiyo.” Lisa aliitikia kwa umakini.
“Uh…” Alvin alikunja uso kana kwamba anafikiria. Kisha, akasema, “Kwa nini usinipe busu ili niyasahau maumivu?”
Lisa alikodoa macho huku akijiuliza ni suluhisho gani hilo. Kama isingekuwa hali yake dhaifu, angetilia shaka sana kama hiyo ndiyo ilikuwa nia yake.
"Ikiwa hauko tayari kufanya, ni sawa basi." Alvin aligeuza uso wake pembeni na kuendelea kuugulia.
“Hapana, hapana. niko tayari kufanya hivyo.” Baada ya yote, alikuwa mwokozi wake.
Lisa alijipa ujasiri wa kumsogelea. Aliinamisha kichwa chake na kumbusu midomo yake myembamba.
Pengine ilikuwa ni kwa sababu alikuwa ametumia muda mwingi kupata sindano za dripu kwamba ladha hafifu ya dawa iliendelea kutawala kwenye midomo yake. Lakini ladha hiyo ilififia baada ya kumpiga busu lingine. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumbusu kwa hiari yake mwenyewe, na uso wake wote uliwaka furaha. Kwa bahati nzuri, taa hazikuwa zimewashwa.
Mwili wa Alvin ukawa mgumu, mapigo ya moyo yakaanza kwenda mbio.
Kabla hajapata fahamu zake, Lisa akarudi nyuma. Aliuliza kwa sauti nyororo iliyofanana na mlio wa mbu, “Umeridhika?”
"Ndiyo, nimefurahia sana na maumivu yalikuwa yanatoweka, lakini yamenza kurudi tena wakati ulipoacha," Alvin alijibu kwa sauti dhaifu ya kudeka.
“Lakini ninaogopa kwamba utakuwa na maumivu nikikubusu kwa muda mrefu,” Lisa alisema kwa unyonge.
"Njoo hapa." Alvin alitikisa kichwa kuashiria nafasi tupu upande wake wa kushoto.
Lisa alisita kwa muda kabla hajalala pale. Kisha, akambusu midomo yake tena.
Hapo awali, alionekana akimbusu kwa aibu. Baadaye, aibu zilianza kumwisha bila yeye kutambua. Huku akiwa ameduwaa, alimzungushia mikono yake kiunoni.
Hakujua ni muda gani walikuwa wamezama kwenye busu. Hatimaye Lisa taratibu alianza kuhisi uchovu. Alimuegemea Alvin na kulala baadae. Alvin akarudi nyuma, kisha akamtazama kwa jicho la giza. Baada ya hapo, alimbusu kwa upole kwenye paji la uso kabla ya kufumba macho na kulala. Maumivu aliyokuwa akiyasikia yalipungua baada ya huduma hiyo.
Kesho yake asubuhi, Lisa aliamka kabla ya Alvin. Bado alikuwa amelala wakati huo. Akiwa anatazama sura yake ya kupendeza kwenye uso wake mzuri kando ya mto, alikumbuka kila kitu kilichotokea usiku wa jana yake. Wazo hilo lilimfanya ajisikie haya. Lakini hakuonekana kuchukia.
Alishtushwa na mawazo yake hayo wakati mlango ulipogongwana sauti ikasikika. "Daktari anakuja kwa raundi."
Lisa alijitupia upande wa kanga aliyokuwa amenunua kwa haraka na kukimbilia kwa daktari. Ni Dokta Kane yuleyule aliyekuja usiku na kuwakuta kwenye pozi la utata, na kulikuwa na wahudumu wachache waliokuwa wakimfuata nyuma muda huo. Wote walipigwa na butwaa walipomwona Lisa. Macho yao yalikuwa yakimtazama kwa namna ya ajabu.
Uso wa Lisa ulishtuka. Alidhani kwamba wanafunzi wa mafunzo walikuwa wamegundua kutoka kwa Dk. Kane kuhusu kile alichokiona jana usiku.
Kwa bahati nzuri, Alvin alikuwa tayari ameamka wakati huo. Dokta Kane mara moja akamfanyia uchunguzi. Dakika kumi baada ya kufanyiwa uchunguzi, Dk. Kane alikuwa tayari kuondoka.
Alikunja ngumi na kukohoa kidogo. "Ingawa unapata ahueni ya haraka, bado lazima ujitunze."
Lisa alikosa la kusema. Alihuzunika sana hivi kwamba hakutaka kusema lolote lingine.
Ni baada tu ya kwenda kunawa uso ndipo aliona midomo yake ikiwa imevimba kwenye kioo. Alishtuka sana hata akakaribia kuangukia kwenye sinki la choo.
Hatimaye Lisa alitambua kwanini kila mtu alikuwa amemtazama kwa namna ya ajabu muda ule.
Sura ya 93
Muda mfupi baadaye, alitoka mle bafuni akiwa amechoka. “Yote ni makosa yako. Tazama jinsi midomo yangu ilivyovimba baada ya kunibusu. Nitaishi vipi hapa wodini?”
Baada ya kumwangalia, Alvin aliridhika moyoni na alichokifanya. Kwa uso uliopauka, alilalama kwa unyonge. “Samahani. Hiyo ilikuwa kwa sababu ya kunogewa sana kwangu. Mwili wangu uliuma sana jana usiku, na ilikuwa ni kosa langu. Usiku wa leo, nitajaribu kuvumilia maumivu na sitakusumbua.”
Kwa kuzingatia jinsi mwanaume huyo mzuri alivyokuwa dhaifu, Lisa hakuweza kujizuia kumkosoa wakati huo.
Hans na Sam walipofika saa tatu asubuhi, walishtuka kumuona Lisa akiwa amevaa barakoa. "Lisa, mbona umevaa barakoa?"
“Hospitali kuna watu wengi, kwa hiyo nadhani ni salama kuvaa barakoa, ukizingatia na hii hali ya korona” Lisa alijibu kwa sura ya ukali. "Nilisikia watu wengi wameambukizwa na homa hivi karibuni."
“Oh. Nipe na mimi barakoa basi, Shemeji. Nataka kuivaa ili kuepuka kuambukizwa pia.” Sam mara moja akataka kuvaa barakoa pia.
Alvin aliyekuwa amejilaza kitandani alikosa la kusema.
….
Ndani ya ofisi ya Mawenzi Investments, Jones Masawe alipopokea barua ya wakili, alimwomba Lina aje na baadaye akampa kipande cha mawazo yake.
“Umefanya nini? Nilihangaika sana kupata mradi mpya wa ukuzaji mali kutoka kwao ili tupate pesa lakini mlisababisha fujo mbaya muda mfupi baada ya kuchaguliwa. Nagombea nafasi ya mwenyekiti mwisho wa mwaka. Je, huwezi kuharibu mipango yangu?”
“Samahani, Baba. Kumwona Lisa kulifanya damu yangu ichemke, na nilitaka kumfundisha somo.” Akiwa na huzuni, Lina alipiga kelele. "Lakini sikutarajia kwamba Alvin angefanya hivyo kwa wakati ili kumuokoa."
“Alvin tena!” Masawe aliuma meno. “Lisa alimfahamuje mtu wa aina hii?”
"Lazima alilala naye." Lina akahema. "Nimemchunguza Alvin na kugundua kuwa hata wale ambao wako tayari kutumia mamia ya mamilioni ya pesa wanaweza kukosa kumwajiri, sembuse Lisa ambaye hana uwezo?"
Masawe aliposikia hivyo alionyesha sura ya kuchukia. "Anajidharirisha sana huyu binti."
“Baba, Alvin anaendelea kuharibu mipango yetu na sasa anaomba hata malipo ya fidia ya juu kutoka kwetu. Hebu tumfundishe somo.” Lina alisaga meno yake. “Hata hivyo, yeye ni mwanasheria tu. Zaidi ya hayo, yeye pia ni mgeni.”
"Usifanye haraka." Jones Masawe alimkazia macho. "Alvin ni wa kushangaza sana."
Lina alijibu kwa kutoridhika, “Ajabu, ili iweje? Kama mwanasheria, lazima atakuwa amewaudhi watu wengi kwa miaka mingi. Haitashangaza kama kuna watu wanataka kulipiza kisasi kwake…”
Jones alishawishika na wazo hilo. Baada ya muda, alipiga picha ngumu kwa binti yake.
“Nendeni mkachunguze kesi zote alizoshughulikia awali. Na je, umesuluhisha suala hilo na mradi wa usimamizi wa mali?"
“Usijali. Nimemhonga muuzaji na mfanyakazi pesa. Kilichotokea kwenye saiti ya ujenzi ilikuwa ajali tu, lakini fidia…”
“Lipa tu. Tunapaswa kulipa. Hatupaswi kumuacha Alvin afanye jambo kubwa juu yake.” Masawe aliongeza kwa kutoridhika, “Unapaswa kuacha kuendelea kurumbana juu ya suala hilo na Lisa. Kwa kuwa sasa umeachana na Ethan, unapaswa kuangalia familia nyingine tajiri na zinazojulikana.”
“Sawa.” Lina alitazama kwa aibu, kisha akasema, “Hivi majuzi, nimekuwa nikichangamana na Janet Kileo usiku, na kaka yake, Stephen Kileo, huja kila mara. Anaonekana kunipenda.”
Macho ya Jones Masawe yakaangaza. Stephen Kileo alikuwa mrithi wa familia tajiri ya Kileo, ambaye alikuwa kijana mzuri sana. Hata Ethan alikuwa hawezi kufananishwa naye.
Kwa kuongezea, familia ya Kileo ilikuwa imepanda juu zaidi ya miaka michache iliyopita. Ingekuwa nzuri ikiwa familia ya Jones Masawe ingeweza kuunganishwa nao kwa ndoa.
“Sawa. Wewe bado ni bikira katika familia yetu. Ni lazima uuteke moyo wa Steve.” Jones aliangua kicheko.
Siku iliyofuata, katika wodi ya watu mashuhuri kule hospitalini, naibu meneja mkuu wa Mawenzi Investiments alifika ana kwa ana akiwa na hundi mbili.
“Samahani sana, Bw. Kimaro. Lilikuwa kosa la mfanyakazi wetu. Hapa kuna fidia ya Bi Jones na wewe.
Lisa alipepesa macho baada ya kuona hundi yenye thamani ya shilingi milioni 30 mkononi mwake. Kisha akaitazama ile hundi yenye thamani ya shilingi milioni 100 aliyokuwa nayo Alvin.
Damn, kuna pengo gani kubwa katika matibabu kati yao wote wawili. Ingawa hakuumia, alipatwa na kiwewe kikali na karibu kupoteza maisha yake. Alikuwa amekata tamaa kabisa.
Kilichozidi kumhuzunisha ni kwamba Alvin aliitupa tu hundi kwenye meza ya kitanda. “Sawa. Mnaweza kuondoka sasa hivi.”
"Bw. Kimaro, una nia ya kubadilishana kadi za biashara na mimi?" Naibu meneja mkuu alijaribu kuchukua fursa hiyo kufahamiana na wakili huyo mkubwa.
"Nimechoka, unaweza kwenda tu." Alvin alifumba macho bila subira.
Naibu meneja mkuu, ambaye aliheshimiwa sana kazini kwake alihisi uchungu. Mara akatoka nje akiwa na uso uliosinyaa.
Lisa alimfuata alipokuwa ametoka mlangoni. "Samahani. Majeraha ya Bw. Kimaro yamekuwa yakimuumiza sana siku hizi chache. Naomba kujua kuhusu mradi wa usanifu wa nyumba…”
“Mimi sihusiki na jukumu hilo. Unaweza kuwasiliana na mtu katika idara husika.” Naibu meneja mkuu aliondoka mara baada ya kumaliza kuzungumza. Hakuweza kujisumbua kuwasiliana na mbunifu yule masikini.
Lisa alikuwa mnyonge. Laiti isingekuwa kwa lengo la kupata pesa zaidi, asingeenda hatua ya ziada kwake. Aliporudi wodini, macho ya Alvin yakafumbuliwa na ndita zake usoni zilikuwa zimekunjamana. “Umerukwa na akili? Kwa nini bado unafikiria kuchukua mradi huo chini ya Mawenzi Investiments?"
'Ikiwa nitachukua mradi huo, nitapokea kamisheni yenye thamani ya shilingi milioni kumi kutoka kwa Mawenzi Investiments. Ninaweza kupata angalau milioni 20 kutokana na ukarabati huo baadaye.”
Lisa alitazama hundi yake na kusema kwa huzuni, "Milioni 20 zinaweza kuonekana kuwa si kitu kwako, lakini ni kitu ambacho mtu wa kawaida hawezi kutengeneza maishani mwake."
"Je, umefungwa kwa pesa?" Alvin aliuliza kwa ujeuri. Kwa mshangao alimkabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 100 kutoka mezani. "Unaweza kuitumia."
Miguu ya Lisa karibu ikageuka kuwa laini kama mrenda. Ilikuwa imepita muda tangu alipoona pesa nyingi namna hiyo. Lakini hakuweza kuichukua. Akatikisa kichwa. “Ni pesa zako. Siwezi kuchukua.”
“Lisa.” Macho ya Alvin yalitiwa giza. Alionekana kukasirika. "Wewe ni mwanamke wangu, na ninakuruhusu kutumia pesa zangu."
"Nataka kupata pesa kwa uwezo wangu. Sitaki kuwa mwanamke ninayemtegemea mpenzi wangu.” Lisa aliendelea kushikamana na kanuni alizojiwekea. "Ikiwa ningetaka kupata pesa kupitia njia rahisi, ningeweza kupata mtu tajiri zaidi kuliko wewe kwa uzuri wangu, lakini mimi sio mtu wa aina hii. Ninaweza kuzeeka na uzuri ukapotea. Uwezo wa kweli pekee ndiyo utabaki.”
Baada ya kumaliza kuongea, aliguswa na maneno yake mwenyewe.
Bila shaka, Alvin angemwona kuwa mwanamke mwenye busara na heshima kubwa ambaye hakuchochewa na faida za kibinafsi. Mwanamke wa aina hii alitokea mara chache sana. Hakika ilikuwa ni nadra kumpata mwanamke yeyote mwenye tabia kama hiyo.
Lisa alinyanyua kichwa, ndipo alipogundua kuwa macho ya Alvin ya kejeli yalikuwa yakimtazama. "Unaweza kupata mwanaume tajiri kuliko mimi? Umeshiba sana. Ni nini kinakufanya ujiamini hivyo?” Maneno yake yalionekana kama kofi usoni kwa Lisa, jambo ambalo lilimfanya awe na hasira sana. Ilibidi akubali kwamba labda alikuwa mwanasheria mwenye uwezo zaidi linapokuja suala la kupata pesa. Baada ya kusema hivyo, daima kutakuwa na mtu bora zaidi yake huko nje. Kelvin alikuwa na uwezekano wa kuwa na makali juu yake katika suala hilo.
"Bw.Kimaro, usiwe na hila."
Alvin alikoroma. "Ni heshima kubwa kwako kukutana nami."
“Ndio, nina bahati kukutana nawe. Wewe ni nyota yangu ya bahati, mwokozi wangu.” Lisa hakutaka kubishana na mgonjwa.
Sura ya 94
Alipomaliza tu kuzungumza, Kelvin alimtumia ujumbe wa WhatsApp. [Nilisikia kutoka kwa Joseph kwamba kuna kitu kilikutokea ulipokuwa ukifanya kazi. Uko salama? Je, ninaweza kuja kukutembelea? Nina wasiwasi sana.]
Lisa alihema sana. Hakika, Kelvin alimtendea vyema kabisa. Ila cha kusikitisha, tayari hakukuwa na haja ya kulipiza kisasi kwa Ethan. Hivyo hakukuwa na haja ya yeye kuolewa na mjomba wa Ethan pia.
Akajibu, [Asante kwa wasiwasi wako. Niko sawa. Maendeleo ya ukarabati wa jumba lako hayataathiriwa.]
Kelvin: [Mradi wa jumba langu sio wa dharura. Kilicho muhimu zaidi ni kwamba uko salama.]
“Unachat na nani?” Alvin aliuliza kwa hasira.
“Pamela.” Lisa mara moja akaweka simu yake chini. Aliposema uwongo, hakuona haya, wala moyo wake haukuenda mbio.
“Nilifikiri ulikuwa unazungumza na Kelvin, Ethan, na kundi hilo la watu. Afadhali usiniruhusu kujua kuwa unawasiliana nao kupitia Whatsapp,” Alvin alionya.
"... Unawaza kupita kiasi."
Lisa alipata mshtuko, akishangaa kuona Alvin alikuwa na macho kama ya X-ray.
“Aha, njoo hapa. Majeraha yangu yanaanza kuuma tena.” Alvin alimtazama kwa hasira.
Lisa alikosa la kusema. Je, Alvin alikuwa anataka kumbusu tena.
***
Alvin aliruhusiwa kutoka hospitali baada ya wiki moja. Lisa alikuwa akimuhudumia Alvin muda wote huo.
Joseph Ruta, bosi wake kazini, hakumlaumu. Baada ya yote, alikuwa karibu kupoteza maisha yake kwa sababu ya kazi. Aliuliza kwa upole, “Je, bado unapanga kuchukua mradi chini ya Mawenzi Investiments? Vinginevyo, nitateua mtu mwingine wa kuifanya."
“Ningependa kujaribu tena. Ikiwa nitashindwa, unaweza kuamuru mtu mwingine kuifanya."
Lisa hakuweza kuvumilia kuachia kamisheni hiyo nzito.
Wakati akiwa anafikiria namna ya kulishughulikia jambo hilo, ghafla bwana Frank akampigia simu. “Bi Jones, samahani kwa kilichotokea mapema. Nimejaribu kuwauliza wasimamizi kuhusu hilo katika siku chache zilizopita na wameomba radhi kuhusu hilo. Kwa hivyo, wameamua kupitisha mradi kuhusu muundo wa nyumba kwa Ruta Buildind Design & Construction.
Lisa alikuwa alihisi kana kwamba amesikia vibaya. Bila kujali, alihisi kwamba hatimaye angeweza kuona mwanga mwishoni mwa handaki.
"Lakini hatujazungumza juu yake ..." Lisa alisema.
"Ruta Buildind Design & Construction iko kila wakati. Kweli, ninahitaji uje na mpango wa kina wa muundo na ni wa haraka sana. Uongozi wa juu ungependa kuliangalia kesho yake.”
Lisa alichanganyikiwa. Mradi huo wa Mawenzi Investiments ulihitaji miundo kumi tofauti ya nyumba, ambayo alihitaji kuwasilisha kesho yake. Angewezaje kufanikisha? Baada ya kusitasita kwa muda, alitikisa kichwa kwa njia ya moja kwa moja. "Sawa, lakini tunahitaji kusaini mkataba kwanza."
"Njoo ofisini mchana na tutasaini basi."
Mchana wa siku hiyo, Lisa alielekea kwenye kituo cha mauzo tena. Alipaswa kusaini mkataba na Mawenzi Investiments bila kusubiri kwa muda mrefu. Aliporudi nyumbani usiku, aliandaa chakula cha jioni kwa ajili ya Alvin. Baada ya kumsaidia kuoga, alisema kwa wasiwasi, “Ninahitaji kutengeneza michoro ya kazi yangu usiku kwenye maktaba yako baadaye. Nenda kalale mapema uniache.”
Alvin alikunja uso. Ijapokuwa alifahamu umuhimu wa dhamira ya msichana huyo ya kujitutumua, lakini hakuipenda. Hata hivyo, alikuwa kimya kuhusu hilo. Hata hivyo, alipoendelea kukesha na asilale tena siku iliyofuata, alipandwa na hasira. “Lisa, una wazimu? Hukulala vizuri wakati ulilazimika kunihudumia hospitalini kabla ya hii. Sasa kwa kuwa uko nyumbani, hutalala tena. Unapanga kufa kwa mshtuko wa moyo?"
“Kazi itakamilika baada ya usiku wa leo, usiwaze.” Lisa alikunywa kahawa. Ndani kabisa, aliguswa kidogo na huruma ya Alvin.
Alvin alimuamuru kwa uthabiti, “Sijali. Rudi chumbani kwako na ulale sasa. Sio jambo kubwa ikiwa utakufa kwa kwa presha ya moyo. Jambo kuu ni kwamba hakuna mtu atakayenipikia. Ninakataa kutumia juhudi zangu kuchukua kesi yako bure."
Lisa alisikitika baadaya kugundua wasiwasi wake kwake ulikuwa ni udanganyifu tu.
Lisa aliuma mdomo wake kisha akasema kwa uchungu, “Usijali. Kwa kuwa nimekuahidi kukupikia, nitahakikisha sitakufa.”
“Je, huelewi? Ninautawala mwili na maisha yako. Huna nguvu tena juu ya maisha yako."
Bila kusita zaidi, Alvin akautumia ule mkono ambao haukujeruhiwa kumbeba kutoka kwenye kiti.
“Alvin…”
“Ikiwa unapanga kupinga, ni bora ufunge mdomo wako,” Alvin alimwonya kwa kukunja uso.
"Hapana. Nilitaka kukwambia uniweke chini. Naweza kurudi chumbani kwangu mwenyewe. Majeraha yako yatakuwa mabaya zaidi ikiwa utatumia mkono wako mwingine kunibeba hivi,” Lisa alijibu. Alipumua na kujisalimisha kwa hatima yake. Alvin aliridhika na jinsi Lisa alivyokuwa mtiifu na kumuelewa. Baada ya kumuacha, akaenda naye chumbani kwa ushirikiano.
Awali alipanga kuendelea na kazi yake baada ya Alvin kusinzia. Hata hivyo, mara tu alipokuwa kitandani, alizidiwa na usingizi sana hivi kwamba alilala fofofo.
Alfajiri na mapema, Alvin akiwa anatoka bafuni baada ya kupiga mswaki, alimuona mwanamke huyo akiwa amelala kama gogo kitandani. Alikuwa amepitiwa na usingizi mzito kiasi kwamba hata mate ya pembeni ya mdomo yalidondoka kwenye mto.
Alvin akampiga picha kwa siri. Angemuonyesha picha hiyo baadaye na kumfanya aaibike.
Aliweka picha kwa kuridhika. Baada ya hapo, aligeuka na kuelekea sebuleni karibu na chumba cha kulala. Kwa mkono mmoja tu, alifanikiwa kupekua neno la siri kwenye kompyuta ya Lisa ya mkononi kwa muda mfupi. Alibofya programu ya kubunia mchoro na kuona michoro kadhaa migumu ndani yake.
Akakodoa macho. Alitakiwa kuwasilisha michoro mingi ndani ya siku moja na nusu. Mawenzi Investiments alikuwa anajaribu kumpa wakati mgumu kwa makusudi?
Lisa alipoamka saa tatu asubuhi, alitazama muda na kupigwa na butwaa kabisa. Alikuwa tayari kachelewa sana. Mara moja akainuka na kukimbilia maktaba. Akawasha laptop yake kuendelea na michoro yake.Mara tu alipobofya kwenye programu, alipigwa na butwaa. Hapo awali, bado alikuwa na nyumba nne zaidi za kubuni rasimu. Jambo la kushangaza ni kwamba michoro yote ilikuwa imemalizika.
Michoro yake ilikuwa imekamilika?
Zaidi ya hayo, michoro ilifanyika vizuri sana. Dhana hizo zilikuwa za ajabu, na zililinganishwa na zake. Nini kimetokea? Je, alilala jana usiku? Au aliamka na kumalizia akiwa usingizini?
Je, alizimaliza lakini akapoteza kumbukumbu? Alijaribu awezavyo kukumbuka, lakini alikuwa na hakika kwamba hakumaliza michoro hiyo. Nani alimfanyia? Alishuka chini huku akionekana kupigwa na butwaa.
Katika chumba cha chakula, Alvin alikuwa amevaa nguo za kawaida za kijivu na akizungumza kwenye simu ambayo aliishika kwa mkono wake wa kushoto.
“Ndio. Agiza safari ya ndege ya mchana. Naenda Mbeya…”
Hadi simu inakatika, tayari Lisa alikuwa amekaa kwenye kiti kilichokuwa pembeni yake. sura ya mshangao kupita uso wake. "Bado unaendelea na safari ya kikazi katika hali hii?"
“Ndio kuna dharura imejitokeza." Kulikuwa na suala la mradi huko Mbeya ambao aliwekeza, kwa hivyo alipanga kwenda huko kutazama. “Nitakuwa huko kwa siku mbili. Afadhali uwe na tabia njema ndani ya nyumba ... "
“Najua, najua. Hakika sitakutana na Kelvin wala Ethan,” Lisa aliendelea na hotuba yake huku akiwa hana la kufanya.
“Unaweza kusema kitu tofauti? Nimechoshwa na maneno yako.” Kwa kuona aibu, Alvin alimkazia macho. Mwanamke huyo alizidi kupata ujasiri. Anathubutu vipi kumdhihaki.
Lisa aliuliza kwa udadisi, “Macho yako yana damu. Jana usiku hukulala vizuri? Ilikuwa ni kwa sababu….” Ghafla akabanwa na kikohozi.
Alvin alikasirika sana. Je, alikuwa akishuku kuwa aliamka alfajiri kumalizia michoro yake jana usiku? Hakutaka agundue kwamba alimfanyia hivyo.
Kwa usemi wa kupotezea, alisema haraka, "usielewe vibaya ...Samahani, nilipaliwa na mate. Najua labda ni kwa sababu majeraha yako yalikuwa yanauma jana usiku na hukuweza kulala tena. Ilikuwa ni kosa langu kwamba nililala kama gogo. Mbona hukuniamsha?” Lisa alijisikia hatia sana.
Sura ya 95
Uso wa Alvin uliganda bila kuonekana akizungumza kwa muda.
"Ulisema nini?" Lisa aliuliza.
Alvin alikoroma kwa namna ya kutania. "Nilitaka kukuuliza kwa nini hukupaliwa hadi kufa."
Lisa alishindwa cha kuongea huku akijiuliza kwanini mwanaume huyo aliongea kinyama namna ile. Kilichomtia shauku zaidi ni kile kilichotokea jana yake usiku. Kwa kuwa nyumba ilikuwa yake, alikuwa na uhakika wa kujua. “Jana usiku… Je, unajua ni nani aliingia kwenye chumba cha maktaba na kutumia kompyuta yangu? Kuna mtu alinimalizia michoro yangu.”
“Oh. Nilipata rafiki wa kukukamilishia jana usiku ili usife kwa mshtuko wa moyo. Vinginevyo, ningehitaji kutafuta mpishi mpya.” Alvin aliikunywa glasi ya maziwa aliyokuwa ameshika.
Lisa alipigwa na butwaa kabisa. Alikumbuka kwamba ilikuwa karibu saa sita usiku alipoenda kulala jana yake usiku. Hivi kweli aliweza kumpigia simu mtu wa kumsaidia usiku wote huo?
Ingawa siku zote alisema kwamba ni kwa sababu alitaka aendelee kumpikia chakula, je, ni kweli kwa kweli kwamba alimtendea hivyo kwasababu yeye ni mpishi tu?
Isitoshe, hata alijeruhiwa alipomwokoa kwenye eneo la ujenzi mara ya mwisho. Kichwa chake kilikaribia kupigwa na tofali, na karibu kupoteza maisha yake.
Moyo wake ulianza kudunda. Muda huo, alikasirishwa na maneno yake makali, lakini hisia tayari zilikuwa zimefutwa kwa muda mfupi.
Pengine alikuwa mtu ambaye alikuwa mgumu kwa nje lakini kwa ndani alikuwa laini.
Baada ya muda fulani, alisema, “Asante. Rafiki yako ni mzuri sana. Anafanya kazi wapi? Nikipokea kamisheni hiyo, nitagawana naye nusu yake.”
Sauti yake ya kiume iliyotoa dokezo la kejeli ilisikika, “Sahau kuhusu hilo. Yeye hajali kuhusu pesa.”
Lisa hakujali. "Sawa, nitampikia chakula kitamu kama ishara ya shukrani yangu basi ..."
“Huna sifa,” Alvin alikatiza sentensi yake huku akiwa amekunja uso. "Unaweza kunilaza tu ikiwa unataka."
“Sawa.” Lisa alijibu na kukaa kimya, hakuwa na la kusema zaidi.
Alvin alikodoa macho yake na kukunja midomo yake kwa utulivu. "Ngoja nikuonyeshe kitu." Alvin akabonyeza kufungua picha ya simu iliyokuwa kando yake na kumuonyesha. Lisa aliitazama. Papo hapo, mcho yake yakamtoka kana kwamba yanataka kufyatuka. Kweli alimpiga picha akiwa amezama usingizini? Ni mzaha ulioje!
Hakuweza kujisogeza kuitazama ile picha, akanyoosha mkono wake kwa lengo la kumpokonya simu. Alvin aliikwepesha simu yake mara moja kabla hajaipokonya. Lisa akakosa balance na baadaye akaanguka mikononi mwake. Kwa bahati mbaya, mkono wake wa kushoto ulitua kwenye sehemu isiyo ya kawaida ya mguu wake. Lisa alimsikia Alvin huku akihema kwa mshtuko. Kwa aibu kabisa, aligeuka na kutaka kukimbia lakini hakuweza. Mkono wa kulia wa Alvin ulikuwa umefungwa kiunoni mwake. Sauti ya kupumua kwake ilidumu masikioni mwake kimahaba. Sauti yake ya kiume ilikuwa ya kupendeza kama sauti iliyotolewa na zeze.
“Unajaribu kunitega asubuhi na mapema hii?”
“Umenielewa vibaya tu…” Kwa kuona haya, Lisa alipata shida kuinua kichwa chake. Macho yao yalipokutana, macho yake yalikuwa meusi kama sumaku. Hakuweza kuangalia pembeni.
Alvin alimtazama Lisa mikononi mwake ambaye uso wake wa aibu ulikuwa kama ua linalochipuka. Alihisi hamu ya kumbusu.
Kwa kweli alifanya hivyo.Alvin alikuwa akitumia kisingizio cha kupunguza maumivu kama njia ya kumpiga denda Lisa kila siku. Mara nyingi alimbusu usiku kama njia ya kumzuia kuhisi maumivu.
Kitendo hicho kilikuwa kimezoeleka kwa Lisa. Hata mwili wake ulionekana kuzoeana na busu hilo. Lakini alihisi moyo wake ukimwenda wazimu zaidi kuliko hapo awali. Busu lla muda huo ilikuja na ladha ya utamu pia.
Huko nyuma, mara nyingi alikasirishwa na jinsi Alvin alivyozungumza kwa ukali. Hata hivyo, alikuwa amemsaidia sana. Busu lilikatishwa kwa muungurumo wa tumbo lake.
Baada ya kuishiwa nguvu, Lisa kwa aibu alielekea jikoni kupata chakula. Alvin alitoa tabasamu alipokuwa akimtazama kwa nyuma.
Baada ya kifungua kinywa, Lisa aliwasiliana na Bwana Frank kumjulisha kuwa alikuwa amemaliza kuandaa michoro. Bwana Frank alijibu kwamba alikuwa ametoka kazini wakati wa mchana na akamwomba wakutane kwenye hoteli ya SleepWay alikokwenda kupata lunch. Kiongozi wake alikuwepo pia, ili waweze kujadili miundo hiyo pamoja. Lisa alikuwa akihudhuria aina hiyo ya mialiko mara nyingi wakati akikutana na wateja wake. Ingawa hakutaka kwenda, hatimaye alikubali kufanya hivyo.
Saa nane mchana, Lisa aligonga mlango wa chumba cha faragha kwenye hoteli hiyo ya nyota tano kabla ya kuusukuma. Chumba kilikuwa cha kifahari na kikubwa, kilicho na mapambo ya Magharibi.
Aliyemshangaza Lisa ni Lina. Alikuwa amevaa koti la manyoya na kuketi katikati ya kochi. Bwana Frank alisimama kando ya Lina na kummiminia mvinyo kwa uangalifu. Hapo hapo, Lisa alihisi kuwa kuna jambo haliko sawa. Aligeuka, akijaribu kuondoka. Hata hivyo, wanaume wawili wazito waliingia ndani na kumshika moja kwa moja. Michoro aliyokuwa ameshikilia ilianguka chini.
"Bwana. Frank, umekuwa ukinidanganya muda wote huu.” Lisa alionekana kufahamu kila kitu kwa wakati huo. Aliwatazama kwa hasira. “Nimeelewa sasa. Tukio la eneo la ujenzi lilikuwa ni mipango yenu nyote wawili, sivyo?
Bwana Frank alimtazama Lina kwa woga. Aligundua tu juu ya tukio hilo baadaye. Yeye alikuwa mwajiriwa tu, na kupata nafasi yake ya juu ndani ya kampuni ya Mawenzi Investiments alipata shida kubwa. Kwa hivyo, hakutaka kumuudhi Lina kwa ajili ya Lisa na kampuni ya yake, ambayo inaweza kutishia maisha yake ya baadaye.
“Una hisia za haraka, lakini kwa bahati mbaya…” Lina alimwendea kwa uzuri huku akiwa ameshikilia glasi ya mvinyo. Hakuwa tena maridadi na mwenye kujidai kama zamani. Badala yake, alikuwa amekuwa mtu wa hali ya juu na mwovu.
Lisa alijua kwamba hii ndiyo asili ya kweli ya Lina. Hata hivyo, Kibo Group ilikuwa imeuzwa, na sifa ya familia ya Jones Masawe ilikuwa imeharibiwa. Familia ya Masawe haikuzingatiwa kuwa familia tajiri tena. Kwa nini Lina bado alionekana ameridhika?
"Unashangaa kwa nini Bwana Frank angenisikiliza?" Lina alikibana kidevu cha Lisa huku akitabasamu. "Je, ulikuwa na hisia kwamba kesi hiyo ingeharibu hadhi ya familia ya Masawe? Kweli, umekosea. Ninaweza kufikia mambo makubwa zaidi bila Kibo Group.
"Unamaanisha nini?" Lisa alichanganyikiwa kabisa.
Bw. Frank alisema kwa uungwana, “Bi. Lina sasa ndiye meneja mkuu mpya wa majengo kwenye kampuni Mawenzi Investiments. Jones Masawe ndiye mwenyehisa nyingi zaidi katika Mawenzi Investiments, na pengine atakuwa mwenyekiti mpya wa bodi mwishoni mwa mwaka. Mawenzi Investiments inaweza kuwa ya Miss Lina katika siku zijazo."
“Hili haliwezekani. Lisa alishtuka sana. “Sijawahi kusikia kutoka kwa Baba na Mama kwamba tuna hisa nyingi sana Mawenzi Investiments.”
“Kwa nini baba na mama wakuambie hayo? Hata hawakupendi. Wewe ni mgeni tu.” Lina alimwambia, na kwa sauti nzito, Lina aliongeza kwa kejeli, “Hujawahi kushuku sababu ya kwanini Baba na Mama hawakupendi? Hata wanatamani kukuua?”
Macho ya Lisa yalimtoka. Aliinua kichwa chake na kumkazia macho Lina.
Kwa hali ya huruma, Lina alibofya ulimi wake. “Ni kwa sababu wewe si binti wa kuzaa wa Baba na Mama. Nilipochukuliwa kimakosa wakati huo, Baba alitambua kwamba Mama alikuwa ameshuka moyo. Kwa kuhofia kuwa angekufa kwa presha, akakuchukua wewe kutoka katika kituo cha watoto yatima. Kimsingi, wewe ni mtu ambaye wazazi wako wa kibiolojia walikutupa wakati wa kuzaliwa! Usingefanikiwa kile ulichonacho leo bila familia ya Jones Masawe. Lakini sio shukrani kwako kuwa na nia ya kulipiza kisasi kwetu. Ulisababisha hata James kuishia jela. Siku zote Baba na Mama husema kwamba kama wangelijua hili mapema, wasingethubutu kukuchukua wakati huo!”
TUKUTANE KURASA 96-100
Sent from my Infinix X657 using
JamiiForums mobile app