Simulizi: Lisa

SIMULIZI........LISA
KURASA.. 136-140

Sura ya 136

Alvin alikaa kwenye siti ya nyuma ya gari lake. Alikuwa ametawaliwa na maamuzi ya hasira mapema asubuhi, lakini sasa ghafla alihisi njaa sana. Tumbo lilianza kumuuma tena. Aliwasha sigara kwa hasira. Ikiwa angejua kwamba hilo lingetokea, angemaliza kula kifungua kinywa chake kwanza kabla ya kupandisha hasira zake za kijinga.

"Bwana Kimaro, ngoja nikununulie chakula." Hans alimtazama kwa wasiwasi.

“Sina njaa. Nenda uniletee Lina Jones hapa,” Alvin alisema kwa upole, “Sikuzote nilitaka Lisa ashughulike naye, lakini haina maana sana. Nitamalizana naye mwenyewe.”

Hans aliitikia kwa kichwa. Ilionekana kana kwamba ingemlazimu kumuombea Lina kwa kile ambacho alihisi kilikuwa kinaenda kumkuta.
•••
Katika kampuni ya Mawenzi Investments. Lina alifukuzwa moja kwa moja na walinzi. Hakutaka kuondoka na kuishia kupiga kelele mlangoni, “Hata kama baba yangu alikamatwa, bado ana hisa kwenye kampuni na mimi bado ni mtoto wake. Nina haki ya kurithi hisa zake na kufurahia gawio langu.”

“Potelea mbali!” Yule mlinzi alimtemea mate isivyostahili. “Kila mtu anajua kuwa wazazi wako walimuua bibi mzee ili wapate hisa za Mawenzi Investments. Walimuua Mzee Madam Masawe. Hawana utu kabisa. Mwenyekiti Jones tayari ameomba mawakili wengi kurejesha hisa za Jones Masawe. Utarithi nini? Endelea kuota!"

"Subiri. Nitakaporudi Mawenzi, nitafanya maisha yako kuwa mabaya zaidi kuliko kifo. Lina alitetemeka kwa hasira.

Hata mlinzi alithubutu kumdhalilisha sasa. Kweli dunia haikuwa ya haki. Ni wazi alikuwa ametuma picha zote za uchafu za Lisa na Kelvin kwa waandishi wa habari jana yake, lakini sio tu kwamba ilishindwa kuharibu sifa ya Lisa, bali watu walianza hata kumuoanisha na Kelvin sasa. Ilikuwa inakasirisha sana na kukatisha tamaa.

Alitembea kando ya barabara wakati gari lisilo na nambari ya leseni lilisimama ghafla mbele yake. Kisha, watu wawili wakamsukuma moja kwa moja kwenye gari.

"Unafanya nini?" Kabla Lina hajajibu, alifunikwa kwenye gunia na kupoteza fahamu. Muda si muda, ndoo ya maji baridi ilimwagiwa juu yake na akapiga kelele kutokana na baridi. Gunia lilipasuliwa.

"Baridi ilikuwa nzuri?" Hans alimtazama kutoka juu.

Lina alitazama juu na kufikiria kuwa anaonekana kuwa mzoefu kidogo. Baada ya muda, alimkumbuka. "Ni wewe. Wewe ni msaidizi wa Alvin Kimaro…”

"Ni vizuri kukumbuka." Hans aliachia tabasamu hafifu. Akageuka pembeni, akamfunua mtu aliyekaa kwenye sofa ambalo halikuwa mbali. Mwanaume huyo alivalia suti nyeusi na kushika sigara mkononi, moshi ukitanda hewani. Macho yake ya wino yaliangaza na mwanga mweusi uliokuwa mkali kama kisu. Mwanamume huyo alitoa sauti ya kutisha.

Lina alimtambua. Hofu isiyoelezeka ikapanda kutoka ndani ya moyo wake. "Bwana. Kimaro, unajishughulisha na kazi ya kisheria. Unataka kunyang'anywa leseni yako kwa kuvunja sheria? Ninakuonya, afadhali uniache mara moja, la sivyo sitakuacha kamwe.”

Hans alicheka kana kwamba amesikia mzaha.

“Unacheka nini? Huwezi kuelewa nilichosema?” Lina alicheka. “Hebu niambie, haufahamu kuwa mimi ni mwanamke wa Willie Kimaro? Unajua Bwana Kimaro ni nani? Unajua kuwa ananipenda sana? Ikiwa huniamini, unaweza kuchukua simu yangu na kuangalia picha zetu pamoja.”

Alvin alimaliza kuvuta sigara na kuitupa kwenye sinia ya majivu kabla ya kuinuka. Mwili wake mrefu ulitembea polepole kuelekea kwake. Lina alifikiri anaogopa na akacheka. “Alvin Kimaro, wewe ni mwanasheria tu. Willie Kimaro si mtu ambaye mtu kama wewe unaweza kudiriki kumuudhi—”

Kabla hajamaliza, Hans alimpiga kofi kwenye shavu na kumng'oa jino mdomoni. Lina alipiga mayowe, “Willie hatakusamehe—”

Smack! Kofi jingine likasikika. Baada ya makofi kadhaa, Lina alipoteza meno machache na hakuthubutu kuongea tena.

"Nyamaza." Hans alitabasamu. “Unafikiri Willie Kimaro ni nani? Hujaelewa kwa nini Willie alibadili mtazamo wake kwako haraka hivyo?”

Lina aliganda. Alimtazama Alvin na ghafla akakumbuka kuwa jina lake la mwisho lilikuwa Kimaro pia. “Hilo haliwezi kuwa. Sijawahi kusikia mtu anaitwa Alvin katika familia ya Kimaro."

“Unawajua watu wangapi katika familia ya Kimaro?" Hans alidhihaki. “Acha nikwambie, Alvin Kimaro ndiye kaka mkubwa katika familia ya Kimaro. Amekuwa akisimamia familia tangu akiwa na umri wa miaka 20.”

Ubongo wa Lina ulivuma kana kwamba anaota. Kila mtu alijua kwamba kaka mkubwa, wa ajabu wa familia ya Kimaro alikuwa mtoto wa Leah Kimaro. Mtu huyo alikuwa mtu wa chinichini sana, lakini mbinu zake za ukatili zilijulikana sana. Aliingia katika kampuni hiyo akiwa na umri wa miaka 20. Mjomba wake wa pili alipokaidi, alimvunja mguu wake mbele ya umati.

Baada ya kuchukua jukumu la kuongoza KIM International, alipanua biashara yake hadi ng'ambo kwa kasi ya radi na hata akaingia katika nyanja za mawasiliano, fedha, na teknolojia kwenye masoko ya nje ya nchi kwa haraka haraka. Kwa wakati huo, alikuwa ameingia kwenye orodha ya watu miamoja tajiri zaidi Afrika, akiachwa kwa karibu sana na kina Dangote, Mo Dewji, Bhakresa na wengineo. Kulingana na uvumi, alikuwa mtu wa tatu tajiri zaidi nchini Tanzania na pia wa kushangaza zaidi.

"Hiyo haiwezekani. Unasema uwongo!” Lina alikuwa akiingiwa na wivu. Lisa alimkamataje mtu kama huyo?

“Kwa nini nikudanganye? Huyo mjinga Willie Kimaro aliogopa sana hivi kwamba alikojoa kwenye suruali yake alipomwona Bwana Kimaro. Hans alifoka. “Lina Jones, Bwana Kimaro hakutaka kushughulika na wewe mara ya kwanza, lakini hukupaswa kumpa Lisa Jones dawa ya kulevya. Na kwa kweli hukupaswa kutoa picha hizo kwenye vyombo vya habari.”

Lina alishtuka. Alipiga magoti mbele ya Alvin na kutetemeka. “Bwana Kimaro, mimi ni mjinga. Nilikuwa mjinga. Tafadhali nisamehe sana.”

Alvin akampiga teke kwa kuchukia. Ujeuri wa macho yake ulidhihirisha kwamba hakutaka chochote zaidi ya kumwangamiza kabisa. “Unadhani nitakuacha ukipumua?”

"Hapana, hapana, hapana. Haikuwa mimi. Sikupiga picha.” Lina akatikisa kichwa kwa hofu. “Nilitumiwa na mtu nisiyemjua. Ni kweli nilimpa Lisa dawa usiku huo, lakini Kelvin Mushi alipokuja, kamera ya video iliyokuwa chumbani iliharibiwa.”

“Hukuwa wewe?” Uso wa Alvin ulikaza zaidi huku alama ya mshangao ikimulika machoni mwake, akiamini hadaa ya Lina.

"Naapa." Lina alikuwa amepoteza meno kadhaa na mdomo wake ulikuwa umejaa damu. “Kama ningekuwa na hizo picha ningezitumia kumtishia Lisa zamani. Ningewezaje kumruhusu kukaa katika nafasi ya mwenyekiti kwa muda mrefu hivyo na kuwaweka wazazi wangu jela?”

“Kiapo chako hakina thamani.” Uso wa Alvin ulizidi kutisha, lakini aliamini maneno ya Lina. Ikiwa hakuwa yeye, basi ni nani?

Alikuwa na wazo, na midomo yake ikachanua katika tabasamu. Usiku huo, mbali na Lisa, ilionekana kana kwamba kulikuwa na Kelvin pekee. Kwa Kelvin Mushi haikuwa rahisi hata kidogo kwa Lisa kumshuku. Lisa alijua kwamba anampenda, lakini bado alikuwa tayari kuendelea kuwa na urafiki naye. Kelvin alikuwa ameenda ng’ambo kufungua ofisi ya tawi alipokuwa kijana, kama yeye tu. Anawajua watu wenye uthubutu wa kuvuka mipaka na kwenda kufanikiwa nje ya nchi huwa wajanja wajanja sana. Alvin hakumwamini Kelvin hata kidogo.

Lina alijua kwamba alimwamini na akasema kwa haraka, “Bwana Kimaro, tafadhali niruhusu niende. Ninaahidi sitomsumbua Lisa tena. Nitaondoka Dar es Salaam.”

“Unadhani nitakuacha uondoke kwa amani?” Alvin alitabasamu kwa giza. “Nimechunguza mambo yako. Ulikulia kijijini baada ya kuibiwa ukiwa mtoto mdogo, ukatolewa usichana wako na mwanakijiji ukiwa na umri wa miaka 15. Baadaye katika shule ya sekondari, ulifumaniwa zaidi ya mara kumi na waume za watu. Uliwekwa kinyumba na tajiri mmoja na hata kutoa mimba zisizo na idadi. Ni aibu iliyoje. Hukuwa na maisha mazuri hata baada ya kurudi kwenye familia ya akina Masawe.”

Uso wa Lina ulikuwa umepauka kwa aibu. Hii ilikuwa historia yake ya giza. Alikuwa ameifunika kwa makini sana, lakini mtu huyu kwa kushangaza aliweza kujua juu yake. Alikuwa anatisha sana.

"Kwa kuwa unapenda wanaume sana, nitakuozesha mume wa kuishi naye." Alvin alisema na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Punde, mzee mfupi na mbaya mwenye umri wa miaka 50 aliingia. Alipomwona Lina, alimeza mate ya uchu. "Bwana Kimaro, unaniruhusu nimuoe?"
Lina alimtazama Hans kwa uso wa kutisha. “Usimruhusu anioe. Nitakwenda na wewe. Unaweza kufanya chochote unachotaka. Unaweza kunifanya vile Willie alinifanya pia!”

Hans alikwepa nyuma kwa kuchukizwa. “Usinishike, nachukia mambo machafu. Usimwogope sana. Anaonekana kuwa mzee, lakini ana umri wa miaka 40 tu na amekuwa peke yake kwa miaka kadhaa kwa sababu hakuweza kupata mke. Utamfuata kijijini na kumpatia mtoto.”

Kisha, Hans akaondoka, akimuacha Lina nyuma. Alilia kwa kukata tamaa, lakini hakuna mtu aliyemjali. Wakati huo, alijuta sana. Hakupaswa kumlazimisha Lisa Jones kuondoka nyumbani wakati huo. Hakupaswa kumsukuma Bibi Madam Masawe chini ya ngazi.
Lakini, hakuna na dawa ya majuto katika ulimwengu huu.

Sura ya 137

Katika mlango wa kituo cha polisi, Lisa alikuwa amemaliza tu kurekodi ushahidi wake mara ghafla akasikia mtu akiliita jina lake.

“Lisa.” Aligeuka nyuma na kumuona Kelvin akija kwake huku akiwa na tabasamu usoni mwake. Hali ya hewa ilikuwa ya baridi, na alikuwa amejifunika kitambaa shingoni.

"Ni bahati tu nimekuona. Kwa nini upo hapa?” Lisa alilazimisha tabasamu kumsalimia. Kila alipokuwa akimuona, alizikumbuka picha zile na mgogoro kati ya Alvin na yeye.

"Kuna jamaa wa nyumbani alifanya tukio la ajabu, kwa hivyo nilikuja kumdhamini." Kelvin alionekana hoi. "Nilisikia kwamba Jones Masawe na Mama Masawe walikamatwa hivi majuzi. Je wewe…”

“Ndio, polisi waliniita hapa kuchukua maelezo yangu. Kesi hiyo itafikishwa mahakama wiki ijayo kisha watasomewa hukumu.”

"Hongera, hatimaye umelipiza kisasi kwa bibi yako." Kelvin alifurahi kusikia hivyo.

“Asante.” Tabasamu la Lisa halikumfikia machoni. Alionekana kuchoka kabisa.

Kelvin alitembea pamoja naye kuelekea sehemu ya maegesho, huku akimtazama njiani. “Unaonekana umechoka. Umekuwa ukipumzika vizuri kweli? Na Alvin bado hajakuelewa tu…?!”

"Hatuwezi kuzungumza juu ya hili?" Lisa alimkatisha.

"Ni kosa langu." Kelvin alionekana kuwa na hatia.

“Kosa lako kivipi? Ulinisaidia usiku ule. Kama si wewe, ningefanyiwa ukatili mbaya na pengine ningeweza kujiua muda mrefu uliopita. Jana, hata ulishirikiana nami kufafanua hali ilivyokuwa na kuokoa sifa yangu. Ninapaswa kukushukuru,” Lisa alitikisa kichwa na kusema kweli.

Wawili hao walizungumza huku wakitembea. Lakini kijana mmoja aliibuka kando yao ghafla na hawakumjali, wakidhani ni mpita njia tu. Hata hivyo, ghafla mwanamume huyo alitoa kisu cha matunda kutoka kwenye mfuko wake wa suruali na kukichoma kuelekea kifuani kwa Lisa.

“Lisaaa!” Kelvin aliona Lisa amechelewa sana. Alipoona kile kisu kinataka kumchoma, alinyoosha mkono haraka kukizuia, na kisu hicho kikapenya kwenye mkono wake.

Wakati Lisa anajibu, mtu huyo alikuwa amechomoa kisu haraka ili kumchoma Lisa tena. Kelvin angeweza tu kutumia mwili wake kumkinga, na kisu kikapenya sehemu ndogo ya mgongo wake.

“Msaada!” Lisa alilia. Kwa msukumo aliushika mkono wa mwanaume huyo. "Wewe ni nani?!”

“Hutakiwi kunifahamu. Ni kosa lako kuwa mwanamke wa Alvin Kimaro. Nimekuwa nikikufuatilia kwa muda mrefu sasa.” Mwanaume huyo alifichua uso wake wa kutisha huku akiendelea kudunga kisu kwenye mwili wa Kelvin kana kwamba alikuwa na wazimu.

Kwa bahati nzuri, walikuwa karibu na kituo cha polisi. Polisi mmoja alisikia kilio cha kuomba msaada na haraka akakimbia ili kumshika mhalifu.

Punde, ambulensi ilifika na upesi ikampeleka Kelvin hospitalini. Hata hivyo, tayari alikuwa amepoteza damu nyingi njiani na kupoteza fahamu. Lisa alipiga simu kwa haraka kwa Ethan, ambaye alikimbia mara baada ya Ambulance kufika hospitali.

Mlango wa Emeregence Room ulisukumwa, na daktari akatoka na fomu mkononi. “Kisu kilichomwa kwenye figo ya kushoto ya mgonjwa na inabidi itolewe mara moja ili kuokoa maisha yake. Familia ya mgonjwa iko wapi? Tafadhali saini mara moja.”

Lisa alipigwa na butwaa. Ethan pia aliona ni vigumu kukubali. "Daktari, lazima ni lazima figo iondolewe? Kwani hakuna namna nyingine?"

"Necrosis tayari imeingia kwenye figo ya kushoto, kwa hivyo haina maana sasa," daktari alisema bila msaada, "Kama tungeweza kuiokoa, bila shaka tungeiokoa."

Ethan hakuwa na la kufanya zaidi ya kuvumilia maumivu na kusaini zile karatasi. Lisa alitoa machozi ya uchungu. “Yote ni makosa yangu. Mtu huyo alitaka kuniua. Mjomba wako ndiye aliyetumia mwili wake kunisaidia kuzuia kisu."

Ethan alikuwa na hisia tofauti. Hakutarajia Kelvin angekuwa na hisia za kina namna hiyo kwake. Sasa, pia alikuwa na wasiwasi sana kuhusu usalama wa Kelvin. Angeweza tu kusema, “Usifikirie juu yake. Daktari alisema kuwa kuondoa figo yake kutaokoa maisha yake. Mwili wa mwanadamu bado unaweza kufanya kazi na figo moja tu. Anapaswa kuwa mwangalifu zaidi katika siku zijazo."

Lisa alitabasamu kwa uchungu. Kelvin alikuwa anaenda kupoteza figo. Angewezaje kuwa mzima kama hapo awali? "Umewajulisha babu yako?"

“Hapana, babu na bibi wamezeeka na sitaki kuwapandisha presha. Tusubiri hadi upasuaji wa Mjomba umalizike.” Ethan alimtazama na kuhema moyoni mwake. Aliogopa hasa kwamba babu na bibi yake wangezimia ikiwa wangejua ukweli.

Kwa bahati nzuri, saa tatu baadaye, Kelvin aliokolewa. Operesheni ilikuwa imekwisha, lakini bado hakuweza kufumbua macho.

Muda si muda, polisi walifika hospitalini. Walipomwona Lisa walimwambia. “Bi. Jones, tumemhoji mhalifu. Mtu aliyetaka kukuua anaitwa Zigi Kabwe. Yeye si mwenyeji wa hapa Dar.”

Lisa alikasirika. “Hata simfahamu mtu huyu.”

Afisa huyo alitikisa kichwa. “Kulingana na maelezo yake, alikuwa na dada yake pacha anayeitwa Lily Kabwe. Miaka mitano iliyopita, Lily Kabwe alikuwa na umri wa miaka 17 tu, lakini alivutia macho ya Thomas Njau kutoka kwa familia ya Njau huko Nairobi. Thomas alimbaka Lily kwa nguvu baada ya kukataa kulala naye na akaamua kujirusha hadi kufa kutoka kwenye jengo kutokana na fedheha. Familia ya Kabwe ilimshtaki Thomas. Wakati huo, kulikuwa na karibu ushahidi kamili, lakini familia ya Njau ilimwajiri Alvin Kimaro kutetea kesi yao. Alvin Kimaro alidai kuwa Lily alimtongoza Thomas lakini Thomas alimdharau, hivyo akaamua kujiua kwa sababu ya unyonge wake. Mahakama haikushindwa tu kumwadhibu Thomas, lakini hata ilimfanya Lily aonekane kama mtu duni asiye na maana. Mama yake hakuweza kuvumilia na na akapata presha. Amefariki hivi karibuni…”

Lisa alishtuka. Alijua tu kwamba Alvin hawezi kushindwa mahakamani, lakini hakujua kwamba alikuwa amechukua kesi nyingi zisizo na moyo wa utu. "Kwa hivyo, alitaka kuniua ili kulipiza kisasi kwa Alvin Kimaro?"

“Ndiyo. Alitoweka miaka mitano iliyopita baada ya kesi hiyo, na tuligundua tu kwamba alirudi Dar es salaam mwaka huu. Alitaka Alvin Kimaro ajue uchungu wa kufiwa na mpendwa wake, lakini… Alvin Kimaro amezungukwa na walinzi na ni mwangalifu sana, kwa hivyo Zigi Kabwe ameshindwa kutimiza lengo lake licha ya kujaribu kwa miaka kadhaa.”

Afisa huyo alimwambia, “Amekuwa akikufuata kwa muda, lakini umekuwa ukilindwa na mlinzi siku hizi za karibuni. Ni leo tu ndipo alipata nafasi hiyo kwa sababu hukuwa na mlinzi.”

Ghafla, Lisa alionekana kugundua kitu. Siku chache zilizopita, Alvin alikuwa amepanga ghafla Shani afuatane naye kama mlinzi wake. Haikuwa kumlinda dhidi ya Jones na binti yake bali kumtazama Zigi Kabwe. Hata hivyo, hakumwambia chochote.

Haukuwa ulinzi wake hata kidogo. Kama Kelvin asingetokea siku hiyo, angekufa. Hofu isiyo na kipimo ikaufunika moyo wake. Lisa ghafla alifikiri kwamba hakumfahamu kabisa Alvin kama alivyodhani.

"Kwa nini kulipiza kisasi kwako kwa kile Alvin Kimaro alichofanya kwa mtu mwingine?" Ethan alikasirika. “Lisa, nakushauri ukae mbali na Alvin Kimaro. Nani anajua ni maadui wangapi amewachokoza kwa miaka mingi? Nilisikia huwa anaenda mahakamani kuwatetea matajiri tu, madhalimu na mafisadi, je ni haki za wangapi amedhulumu? Lazima atakuwa amepata pesa nyingi kwa njia isiyo halali."

Lisa alinyamaza, akiinamisha kichwa chini na uso wa huzuni. Moyo wa Ethan uliumia. Ikiwa asingefanya chaguo baya hapo kwanza, Lisa asingeangukia kwa Alvin

Sura ya 138

Saa nne usiku, Alvin aliingia kutoka nje akiwa na uso jeuri na mkali. Alipanda juu ndani ya dakika mbili kabla ya kushuka tena kwa haraka. "Lisa bado hajarudi?"

"Hapana." Shangazi Linda aliogopa kidogo sura yake.

“Mbona bado hajarudi?”

"Sijui. Yeye hapokei simu pia.” Aunty Linda alipomaliza kuongea, hali ya joto ndani ya jumba hilo ilionekana kushuka na kumfanya ashtuke.

Alvin akatabasamu kwa ujeuri. Vizuri. Hata baada ya kumsaliti na Kelvin, bado hakujua jinsi ya kuishi. Ilikuwa tayari saa nne usiku lakini hakuwa amefika nyumbani bado. Hata hakupiga simu nyumbani. Mwanamke huyo hakubadilika kamwe.

“Bwana Kimaro,” wakati huo, Hans alikimbia kutoka nje. “Nimepata habari. Zigi Kabwe alimvamia Miss Jones nje ya kituo cha polisi leo, lakini Kelvin Mushi alimzuia na kuchomwa visu vingi mwilini. Lisa yuko salama, lakini Kelvin amejeruhiwa vibaya na sasa anatibiwa hospitalini.”

Mwili wa Alvin uliganda pale pale huku macho yake meusi yakiwa yamemtoka ghafla. “Shani yuko wapi? Amechoka kazi? Si nilimwambia amlinde Lisa?”

Hans alipumua na kukumbusha kwa upole, “Bwana Kimaro, ulisahau? Ulipoona picha za Lisa na Kelvin kwenye vyombo vya habari siku moja kabla ya jana, ulishindwa na kumwambia Shani aache kumlinda Miss Jones. Ulimwambia Shani amwache Bibi Jones kwa hiari yake mwenyewe.”

'Nilimwambia asimlinde Lisa na kweli aliacha kumlinda Lisa? Ana akili timamu?" Alvin alishindwa kujizuia tena. Hans alikuwa kimya. Shani alifuata tu maneno ya Alvin kwa utii.

“Twende hospitali.” Alvin akatoka nje.

Baada ya kufika hospitalini, alivamia moja kwa moja hadi kwenye wodi ya watu mashuhuri. Kelvin bado alikuwa katika hali ya kukosa fahamu. Mrija wa oksijeni ulikuwa umefungwa kwenye pua yake, na Lisa alikuwa akifuta uso wake kwa kitambaa.

Tukio hilo lilimchoma macho Alvin bila huruma. Hapo zamani alipokuwa amelazwa hospitali, alikuwa amemtunza vile vile. Sasa, alikuwa akimtunza mwanamume mwingine.

"Njoo hapa," alimtazama na kusema polepole, "Tuondoke haraka."
Lisa aliacha harakati zake na kutikisa kichwa. “Bado hajaamka. siwezi kuondoka.”

"Lisa Jones, huelewi nilichosema?" Mwali wa hasira kweny moyo wa Alvin ukawashwa papo hapo. Sauti yake ilikuwa ya kikatili sana. "Ninakupa nafasi ya mwisho."

Sauti yake iliufanya moyo wa Lisa kusinzia. Alikaribia kuchomwa kisu hadi afe siku hiyo. Hakuona kuwa alikuwa ametapakaa damu? Je, aliwahi kumjali? "Alvin Kimaro, kuwa mwenye busara. Kama si Kelvin, ningekuwa maiti kufikia sasa. Alimlinda mpenzi wako. Ni sawa ikiwa huna shukrani yoyote, lakini mtazamo wako unawafanya watu wahisi kwamba wewe ni mnyama mwenye damu baridi.”

“Mimi ni mnyama mwenye damu baridi?” Alvin akapiga hatua kuelekea kwake. Alikuwa amemfanyia mengi, akimlinda mara kwa mara, hata kumpenda. Hata hivyo, alikuwa akimshutumu kwa kuwa na damu baridi? Maneno hayo mawili yaliupiga moyo wake kama kisu, na kusababisha maumivu yasiyovumilika.

"Unapaswa kuwa tayari umejua kwa nini Zigi Kabwe alitaka kuniua," Lisa alidhihaki, "Hivi kweli familia maarufu ya Kimaro ina ukata wa pesa kiasi kwamba unalazimika kupigania kesi isiyo ya haki kwa pesa hizo kidogo? Au ilikuwa kwa ajili ya umaarufu? Ulifika kileleni na kupata sifa uliyonayo sasa katika ulimwengu wa wanasheria kwa kuwakanyaga watu wengine?”

Alvin alikunja ngumi. Mishipa ya nyuma ya mkono wake ilitoka nje. "Lisa Jones, elewa hili. Mimi ni mwanasheria. Wanasheria hushinda au kushindwa tu. Mimi si mjumbe fulani wa haki.”

"Lakini mtu hawezi kuishi bila dhamiri." Lisa akatikisa kichwa. Ghafla aligundua kuwa yeye na Alvin walionekana kutoka dunia mbili tofauti kabisa.

“Nimekufanyia mambo mengi, lakini leo hii unasema sina dhamiri?”
Alvin alimtazama kwa hasira. Hajawahi kumtendea mwanamke kinyume sana hapo awali, lakini alipinga kila kitu katika sentensi moja. “Kwa sababu Kelvin alitoa maisha yake ili kukuokoa, kwa hiyo unataka kuwa pamoja naye? Ni kweli, siku zote amekuwa akikufuata.”

"Acha kuongea ujinga." Lisa alikasirika. "Amepoteza figo kwa sababu yangu. Siwezi hata kukaa na kumtunza? Hiki ndicho kitu kidogo zaidi ninachoweza kumfanyia baada ya kuokoa maisha yangu.”

“Sijali. Njoo tuondoke mara moja. Kelvin Mushi sio mtu mzuri kama unavyofikiria wewe. Kelvin ndiye aliyetuma picha hizo kwa siri kwa Lina. Alijifanya kama mtu mzuri juu ya uso lakini alicheza hila za siri gizani. Alikuwa ni mnafiki tu.” Alvin hakujali hata kidogo kuhusu hali ya Kelvin.

"Nadhani wewe ndiye ambaye sio mzuri." Lisa alikasirika.

Muda huo Ethan aliingia kutoka nje akiwa na nguo. “Lisa, nimekuletea nguo. Unapaswa kubadilisha haraka…” Kabla hajamaliza, akamuona Alvin na uso wake ukiwa mweusi mara moja. “Nani alikuruhusu kuingia humu? Ondoka haraka..."

Alvin alimtazama kisha akamtazama Lisa kabla ya kucheka ghafla. “Si ajabu hutaki kuondoka. Mpenzi wako wa zamani yuko pamoja nawe, na mpenzi wako mpya amelala kitandani. Una jozi hii ya mjomba na mpwa wake iliyozunguka moyoni mwako. Lazima uwe na furaha tele.”

"Nimekuozea, siku zote nimekuwa mtu kama huyo moyoni mwako." Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku mwili ukimtetemeka bila kuvumilika.

“Alvin Kimaro, umeenda mbali sana. Je, hilo ni jambo ambalo mwanadamu anaweza kusema?” Ethan hakuweza kuvumilia. Akatupa zile nguo pembeni na kumpiga ngumi Alvin. Alvin aliinua mkono wake kwa urahisi ili kuizuia, na Ethan akanguruma kwa hasira. “Hapana, wewe si binadamu hata kidogo. Lisa na mjomba wangu wamebeba tu matokeo ya matendo yako maovu. Walikaribia kupoteza maisha kwa sababu yako, lakini huna ubinadamu. Ondoka mbele yangu!”

"Nitaondoka, lakini sitaondoka peke yangu, lazima nimchukue mwanamke wangu." Alvin alinyoosha mkono kumnyanyua Lisa begani. Ethan alikimbia kumzuia, lakini Hans alimzuia haraka.

“Alvin Kimaro, niache! Usifanye hivi! nitakuchukia.” Lisa alianza kumpiga mgongoni, lakini Alvin alipuuza.

“Huchukii kuwa mimi ni mchafu? Je, huogopi kwamba nitakuchafua?” Lisa alipiga kelele.

Alvin akamshusha na kumtupa kwenye gari. Hans akawasha gari na kufunga milango. Lisa alijua kwamba asingeweza kushinda dhidi yake na akachagua kukaa mbali naye iwezekanavyo, bila kumwangalia hata kidogo.

Moyo wa Alvin uliudhika sana, akawasha sigara ili avute katika safari nzima. Lisa alikohoa mfululizo. Alijua kuwa hapendi kuvuta sigara hata kidogo kabla ya hii, lakini sasa, alikuwa akivuta sigara mara kwa mara. Hakupenda wanaume wanaovuta sigara, na hakupenda wanaume wasio na akili kama yeye hata kidogo.

Baada ya kufika nyumbani, Alvin alimbeba tena na kumtupa kitandani. Lisa alipanda na kusema kwa ujeuri, “Utanifunga tena? Alvin Kimaro, mimi ni mwenyekiti wa kampuni sasa. Kuna watu wengi nyuma yangu wananitegemea. Siamini kwamba utaweza kunifunga maisha yangu yote.”
“Kila saa ni ampuni, kampunii! kampuni, ni upuuzi tu kwangu.” Alvin alimuigiza kwa kubana pua. “Je, utaniamini nikisema nitaifunga kesho?” Alvin alifoka na kumpa jicho la pembeni. "Si tayari kabisa unajua utambulisho wa jina langu?"

Macho meusi ya Lisa yalitetemeka. Ilibadilika kuwa tayari alijua. Je, Willie Kimaro alimwambia? Yule mwongo aliyelaaniwa. Yeye ndiye alisema atamficha Alvin. Ingawa hakuwa wazi kuhusu utambulisho halisi wa Alvin katika familia ya Kimaro, pamoja na ujuzi wake, angeweza kweli kufanya hivyo. Familia ya Kimaro ilimiliki 25% ya hisa za kampuni hiyo, ukichanganya na ujuzi wake wa sheria, kufumba na kufumbua tu alikuwa anaukosa uenyekiti wake!

"Alvin Kimaro, ungekuwa na furaha zaidi ikiwa ningeuawa na Zigi Kabwe leo?" Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku machozi yakimtoka. "Ninamtunza Kelvin si kwa sababu ninampenda, lakini kwa sababu ninamshukuru."

“Sitakuruhusu umkaribie tena.” Macho ya Alvin yalikuwa yamepoa sana. Alikuwa na hisia kwamba ikiwa angemruhusu Lisa abaki na Kelvin kwa muda mrefu, angempoteza milele. Japo alikuwa amepoa kwake, bado hakutaka kutengana naye baada ya kujua kuwa alikuwa amenyweshwa dawa na Lina. Hata hivyo, hakuweza kuondoa fundo lililokuwa moyoni mwake. Bado alihitaji muda.

Sura ya 139

“Lisa Jones, kama kweli unanipenda, usiende kwa Kelvin Mushi tena. Hii ni nafasi ya mwisho ninayokupa.” Alvin alimtazama kwa kina, sauti yake ikisikika kwa ukali na kishindo.

Lisa alipigwa na butwaa. Ingawa alimchukia na kumkasirikia, bado moyo wake ulimpenda. "Na wewe je? Unanipenda?" Ikiwa alimpenda, kwa nini aliita jina la mwanamke mwingine wakati alikuwa amelewa?

"Naweza kukupenda, na ninaweza kuacha kukupenda wakati wowote." Alvin alisema bila kujali kabla ya kugeuka kuondoka.

Lisa alikaa kitandani huku akishangaa kidogo. Alvinaliweka wazi kuwa upendo wake unaweza kubadilika wakati wowote. Je, ni kwa sababu hakumpenda vya kutosha?

Katika chumba chake cha maktaba, Alvin alisimama mbele ya dirisha akiwa na glasi ya divai nyekundu, akitazama nje ya dirisha matone ya mvua yakishuka chini taratibu. Alitumaini kwamba Lisa alimuelewa. Ndio, ingawa alimpenda, ikiwa angetaka kuendelea kujihusisha na Kelvin Mushi, basi angeweza tu kuachana na upendo huo. Ingawa Kelvin alikuwa ameokoa maisha yake, Alvin alikuwa ameokoa maisha yake mara nyingi zaidi. Asingeweza kuvumilia kumuona mwanamke wake akimlipa fadhila kwa kumhudumia hospitali. Alvin alikunywa divai nyekundu kwa machungu.

Hans alisimama nyuma yake kimya. “Bwana Kimaro, kwa nini hukumwambia Bi Jones kuhusu picha hizo?”

“Kuna faida gani kumwambia? Je, angeniamini? Kelvin Mushi ndiye mwokozi wake sasa. Atafikiri kwamba ninamsingizia kwa makusudi kwa sababu simpendi,” Alvin alidhihaki.

Hans alikuwa kimya. Ilibidi akubali kwamba Kelvin Mushi alikuwa amedhamiria sana. Ili kumlinda Lisa, hata alitoa sadaka maisha yake. Ikiwa hata yeye angelikuwa mwanamke, angeliguswa pia.

Usiku sana, Lisa alioga na kukaa kitandani huku akiwa ameduwaa. Mwishowe, alichukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Pamela, akimwomba aende hospitali kumuona Kelvin kwa niaba yake.

Pamela : [[emoji2297]Usiniambie! Kelvin Mushi alipoteza figo kwa ajili yako? [emoji24][emoji22]Nini unadhani; unafikiria nini? Usichanganyikiwe tu, sawa?]

Lisa: [[emoji26]Sikuwahi kufikiria kwamba angefanya hivyo. Nina deni kubwa kwake. Sitaweza kumlipa maisha yangu yote.]

Pamela : [[emoji22]Hapana, usifikirie sana juu yake. Chukulia tu ni ajali ya kawaida. Ninapanga kumleta Patrick nyumbani kwa Krismasi. Kisha nitaandamana naye hadi kwa familia ya Jackson katika Mkesha wa Mwaka Mpya.]
Lisa: [[emoji39]Nyinyi watu mmesuluhisha matatizo yenu?]

Pamela : [Nilimchunia kwa nusu mwezi, na aliniahidi kukutana na Linda haraka iwezekanavyo katika siku zijazo. Nitamtambulisha mpenzi kwa Linda pia. Nataka kumpa Patrick nafasi moja zaidi. Ninampenda kupita kiasi.[emoji849][emoji849][emoji849]]

Lisa: [[emoji122][emoji122]Hongera kwa kumpata tena Bwana wako.]

Alipotuma tu ujumbe huo, mlango wa chumba cha kulala ulifunguliwa. Mkono wake ulitetemeka, na akazima skrini bila fahamu kabla ya kuweka simu chini.

“Unachat na nani?” Alvin alitoa harufu ya mvinyo mwekundu, na uso wake wote uliwaka kwa hasira. “Nionyeshe simu yako.”

Lisa hakuamini. Alvin hakuwahi kuangalia simu yake hapo awali, lakini alikataa kumpa kabisa. "Alvin, usiende mbali sana."

"Mbali sana? Nitajuaje kama unawasiliana na Ethan Lowe au Kelvin Mushi nyuma yangu?” Alvin hakuwahi kuwapenda wanaume ambao walisisitiza kuangalia simu za wanamke wao, lakini alipoona tabasamu kwenye midomo ya Lisa mapema, moyo wake ulikosa raha ghafla. Alipaswa kuwa na uhakika Lisa alikuwa anachat na nani!

Lisa hakuwahi kufikiria kwamba uaminifu kati yao ulikuwa umeshuka sana. Hata hivyo, huenda asingemuelewa tena ikiwa angeona yaliyomo kwenye simu yake, kwa hiyo alisema tu waziwazi, “Nilikuwa niachat na Pamela . Alikuwa akizungumza kuhusu mpenzi wake. Pia… ataenda hospitali kumwona Kelvin. Siwezi kwenda mwenyewe, lakini marafiki zangu wanaweza kwenda kwa niaba yangu.” Alitazama kinyonge jinsi sura nzuri ya Alvin ikibadilika na kuwa mbaya kwa hasira iliyoonekana waziwazi kwa macho. Moyo wake ulihisi kuchoka ghafla.

“Lisa Jones, wewe ndiye uliyekuwa unachat na Kelvin Mushi? Ni kitanda changu unacholala sasa ujue.” Alvin alichukua simu yake na kuivunjavunja ukutani. Kelele kubwa ilimfanya Lisa kuziba masikio yake kwa hofu.

Alvin aliinua mikono yake na kumkandamiza kitandani, akimbusu kwa nguvu kwenye mdomo. "Niambie, busu langu linakupendeza zaidi, au busu la Kelvin Mushi ndilo tamu zaidi?" Akambusu kana kwamba ana wazimu. Lisa alikuwa akiumia tu kutokana na busu hilo na kumsukumia mbali, lakini hakuweza kumzuia hata kidogo.

Alvin alikuwa amekunywa nusu chupa ya divai nyekundu katika chumba chake cha maktaba. Ubabe wake ulionekana kuongezeka mara moja. Alipokumbuka busu lake na Kelvin, macho yake yakawa mekundu huku akimbusu zaidi.

"Alvin unaniumiza bwana." Lisa alikwepa kwa maumivu.

“Kwanini unakwepa busu langu? Unatamani ningekuwa Kelvin badala yake?” Alvin alikuwa tayari amezidiwa na moto wa wivu. Akararua nguo yake ya kulalia kwa nguvu. "Au aliufanya usiku huo kuwa usiosahaulika sana, ndio maana umeenda naye kituo cha polisi leo? Huwezi kumwacha kabisa?”

Lisa aliogopa sana. Haraka haraka akamshika mkono na kutikisa kichwa bila msaada. “Hapana, nimechoka. Ninaogopa leo sitaki…”

“Hutaki kwa sababu ni mimi, sivyo?” Alvin alicheka ghafla. “Akili yako imejaa Kelvin Mushi sasa. Ungekuwa tayari kama angekuwa yeye, si ndiyo?"

“Mbona unaendelea mbali sana Alvin, hutaki kunielewa kwanini?” Lisa alijisikia kuchoka sana na kukata tamaa. Alikaribia kufa siku hiyo, lakini hakumjali hata kidogo. Alijua tu jinsi ya kumtilia shaka.

Alitabasamu kwa huzuni na hakuhangaika tena, akamwacha afanye anavyotaka. “Sawa, fanya tu kama unataka. Fanya chochote unachotaka.” Machozi yake yalimtoka kwenye pembe za macho yake na kutiririka kwenye nywele zake. Macho yake yalikuwa hafifu.
Siku zote alikuwa akitiliwa shaka, kukanyagwa, na kudhalilishwa naye, lakini bado alikuwa binadamu.

Mwili wa Alvin ukakakamaa kana kwamba alipigwa ghafla kichwani.
Kwanini amekuwa hivi? Ilikuwa ni kama amekuwa pepo. Hakuweza kujizuia kwa mwanamke? Kweli alipoteza busara kwa sababu ya mwanamke? Aligeuka na kukimbilia bafuni. Maji baridi yakamwagika juu ya mwili wake, na ghafla akajichukia. Alipotoka kuoga, Lisa alikuwa amelala chali pembeni ya kitanda, mtupu kabisa hana chochote baada ya nguo zake kularuliwa na Alvin. Kama kware mdogo, alijikunyata, hana msaada wowote, tayari kukwakupaliwa na mwenye mwenye njaa kali!

Alvin hakufanya chochote tena, alilala upande wa pili wa kitanda kimya! Wawili hao walitenganishwa kwa umbali, lakini hakuna aliyemkaribia mwenzake. Hakujua kuwa Lisa ambaye alikuwa amemrudisha nyuma kimawazo machozi yalikuwa yakimtoka. Hakupata usingizi mpaka ilipofika usiku sana.

Kulipopambazuka, Alvin aliamka, lakini Lisa hakuwapo tena kitandani. Haraka akainuka na kushuka chini. Lisa alikuwa amekaa kwenye meza ya chakula akinywa uji wake wa ulezi. Macho ya Alvin yalilegea kidogo, na akashuka haraka. Aliketi kando yake na kuuliza kwa ukali, "Kiamsha kinywa changu kiko wapi?"

Sura ya 140

“Bwana Kimaro, kifungua kinywa chako kimefika.” Shangazi Linda alitoka na kifungua kinywa alichotengeneza.

Alvin akakitazama, na uso wake ukachukizwa mara moja. "Lisa Jones, kwanini hukuniandalia kiamsha kinywa?"

"Wewe ndio ulisema chakula changu ni kichafu kama mimi." Lisa alimtazama kwa utulivu. Siku zote alikuwa hivi. Alipomuelewa vibaya, alimdhalilisha kwa kumwambia chakula chake ni kichafu na asimpikie tena, lakini sasa alitaka apike tena. Je, hakuchoka kumnyanyasa?

"Nitengenezee sasa hivi." Uso wa Alvin ulikuwa mbaya kwa hasira.

"Hapana. Mimi siyo yaya wako.” Lisa alisimama baada ya kumaliza uji wake. "Naenda kazini."

Alvin aligeuka na kuongea na Shani aliyekuwa amesimama mlangoni. “Mfuate kwa karibu. Akithubutu kwenda hospitali, mpige na umrudishe hapa.”

"Mimi sio mtumwa wako." Macho ya Lisa yalikua mekundu kwa hasira. Tayari alikuwa ameamua kutokwenda hospitali, lakini bado alisisitiza kumlazimisha kumwekea mlinzi wa kumchunga. "Alvin Kimaro, usiende mbali sana."

“Kwa kuwa ulinichanganya, unapaswa kuwa tayari kuwa mtumwa wangu. Hakuna anayeweza kwenda kinyume na mimi.” Alvin hakujieleza sana, lakini maneno yake yalitosha kudhihirisha hasira zake.

Lisa alichukua mkoba wake na kuondoka huku Shani akimfuata.
Njiani kuelekea ofisini kwake, haijalishi Lisa aliendesha gari kwa haraka vipi, Shani alikuwa makini naye muda wote. Kwenye maegesho, Lisa alishuka kwenye gari na Shani akamfuata kwa nyuma kwa kasi.

“Shani, unaweza kuacha kunifuata? Sitaenda hospitalini.” Lisa alitmwambia Shani kwa upole. Kwa kweli, hakuwa na shida yoyote na mlinzi yule.

"Samahani, hili ni agizo la Bwana Kimaro, bosi wangu."

“Agizo ni la Alvin, lakini usalama ni wa kwangu. Najua namna ya kujilinda mwenyewe!” Lisa mwishowe alikasirika. “ Sawa, Alvin alikuajiri? Anakulipa kiasi gani? Mimi nitakupa mara mbili." Lisa akatoa kadi kwenye begi lake.

Shani hakujali. “Bi Jones, haijalishi unanipa kiasi gani. Nilifunzwa na familia ya Kimaro. Ninafanya kazi kwa ajili yao tu.” Lisa alipigwa na butwaa. Je, familia ya Kimaro ilikuwa na watu wengi kama Shani? Familia ya Kimaro ilionekana kuwa na mambo mengi zaidi kuliko vile alivyofikiria. “Kwa hiyo lazima umekuwa na Alvin kwa muda mrefu. Kwa maana hiyo unamjua mtu anayeitwa Sarah?”

Hali ya wasiwasi ikaangaza kwenye macho tulivu ya Shani. Ingawa lilitoweka hapo hapo, Lisa bado aliliona vizuri. “Nilimsikia Alvin akimzungumzia siku moja akiwa amelewa. Lazima awe mpenzi wake wa zamani. Walikuwa wanapendana sana?"

“Bi Jones, hayo yote ni ya zamani. Bwana Kimaro ana wewe tu moyoni mwake sasa,” Shani alisema haraka.

"Ndio hivyo?" Lisa alitabasamu kwa kujidharau. Alikuwa akimpima tu Shani, lakini jibu la Shani lilimhakikishia kwamba kweli Alvin alikuwa na mpenzi wa zamani anayeitwa Sarah. Alimwita jina lake wakati alikuwa amelewa. Je, iliwezekanaje kuwa Lisa ndiye pekee moyoni mwake sasa?

“Shani, asante kwa kuniambia hivi.” Aligeuka na kwenda juu ofisini.
Shani alimfuata kinyonge.
•••
Siku iliyofuata, saa kumi na nusu jioni, Pamela alitoka hospitali baada ya kumtembelea Kelvin, akihisi huruma moyoni mwake.
Kama asingekuwa amekosea na kumchanganya Alvin na Kelvin hapo mwanzo, huenda Lisa na Kelvin wangekuwa tayari wameoana. Hapo Kelvin asingepoteza figo pia. Hata hivyo, haikufaa kujutia juu ya maziwa yaliyokwishamwagika sasa.

Akatoa simu yake na kumpigia Patrick. “Patrick, unakwenda kuwachukua wazazi wangu, au unaenda moja kwa moja kwenye Mgahawa tuliokubaliana kukutana?”

“Niko na mkutano ofisini ambao unaweza kuendelea hadi saa kumi na moja na nusu. Nitaenda huko moja kwa moja baadaye. Nisaidie kuomba radhi kwa wazazi wako kwa ajili yangu,” Patrick alisema kwa sauti ya upole.

“Ni sawa, lakini usichelewe. Baba yangu anachukia watu ambao hawatimizi ahadi zao.” Pamela alimuonya kwa upole.

“Usijali, ni suala la maisha yangu. Hakika sitachelewa. Tayari nimekuandalia zawadi ambayo wazazi wako watapenda. Tutafunga ndoa mapema, nami nitakuwa mumeo.” Patrick akatabasamu kwa dhati. Moyo wa Pamela ulikuwa mtamu alipokuwa akimsikiliza.

Baada ya kukata simu, Pamela aliendesha gari kuwachukua wazazi wake kisha akaenda Mambo Garden Restaurant. Ilikuwa saakumi na moja kamili jioni alipofika. Baada ya kuagiza chakula, kaka yake Forrest alifika. Saa kumi na mbili jioni bado Patrick alikuwa hajafika. Babake Pamela alikosa subira, akasema, “Kwa nini bado hajafika? Si sawa kutufanya wazee tungojee.”

Pamela alisema, “Baba, ni saa za jioni sasa. Pengine kuna msongamano mkubwa wa magari barabarani.”

Mama yake aliitikia kwa kichwa na kukubali. “Wafanyabiashara wana mambo mengi ya kushughulikiwa mwishoni mwa mwaka, hiyo inaeleweka. Kuwa na subira zaidi.”

Pamela alimpigia simu Patrick, lakini hakupokea, akajifariji. "Lazima asipokee kwa sababu yuko barabarani, atakuwa karibu tu hapa."

Baada ya nusu saa nyingine, Patrick hakutokea tu. Baba yake alikasirika. “Ni mara yake ya kwanza kukutana nasi lakini anatuletea dharau namna hii. Hata ukimpigia simu ni bure. Sidhani kama yeye ni mkweli hata kidogo. Sitakubali kukuruhusu uolewe naye.”

Wakati huu, mama yake hakusema chochote, na Forrest pia alikuwa na uso wa kukata tamaa. “Achana naye. Sio kama hakuna wanaume wengine ulimwenguni."

Pamela alihudhunika. Mbele ya shutuma za familia yake, alijilazimisha kutotoa machozi. Yeye tu alijisikia kukata tamaa sana kwa aibu. Zamani, alimuahidi mara nyingi, lakini sasa, hata alikosa mkutano wa kwanza pamoja na wazazi wake. Je, alimpenda kweli?

Mama yake akasema. “Pamela, jambo la muhimu zaidi katika maisha ya mwanamke ni kupata mwanaume ambaye ni mzuri kwako kwa moyo wote. Bado wewe ni mdogo, kwa hivyo usikimbilie kuolewa. Sasa, tule. Chakula kinakuwa baridi.” Wakati wote wa chakula, ilikuwa kama anatafuna nta. Mpaka mwisho, Patrick hakutokea, wala hakupiga simu hata mara moja kuelezea shida ni nini.

Baada ya kuachana na familia yake, Pamela aliendesha gari hadi ofisini kwa Patrick. Ofisi yake ilikuwa tayari imefungwa. Alianza kuhisi wasiwasi kidogo. Alikuwa na wasiwasi kwamba huenda Patrick alikuwa amepata ajali ya gari au kitu kibaya. Hata hivyo, hakujua namba za wazazi wa Patrick. Baada ya kusita kwa muda, alimpigia simu Linda. Hakutarajia kuwa mtu aliyemjibu angekuwa ni mwanamume ambaye sauti yake aliifahamu vizuri. “Habari, Pamela…”

Pamela alitazama sura yake iliyokuwa na ukungu kwenye dirisha la kioo mbele yake na ghafla akacheka peke yake. Je, alionekana kama mjinga? “Kwa nini hukupokea nilipokupigia simu? Na mbona unapokea simu ya Linda?”

“Pamela, samahani. Linda alipata ajali ya gari jioni. Niko hospitalini sasa. Nilisahau kabisa hata kuchukua simu yangu ofisini,” Patrick alisema kwa hatia, “Oh, nimechelewa sana? Mmemaliza kula? Tafadhali mwambie baba na mama smahani kwa kushindwa kuja.
Nitawaalika kwenye chakula cha jioni wakati mwingine.”

"Hakuna haja tena," Pamela alisema kwa sauti isiyo na maana.

"Pamela, ilikuwa ni dharura wakati huu ..."

“Ndiyo, kila kitu kuhusu Linda ni dharura. Kwani amekufa? Kilema? Kwani hana wazazi tena, ana wewe tu?"

Moyo wa Patrick ukasisimka. "Pamela, unawezaje kusema maneno kama haya? Kwani Linda alitaka kupata ajali? Hata kama humpendi, unapaswa angalau umuonee huruma.”

Pamela alidhihaki. “Sawa, nimekuuliza swali. Kwani amekufa? Amepooza? Mlemavu?”

TUKUTANE KURASA 141-145

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..........LISA
KURASA.... 141-145

Sura ya 141

“Umemaliza?” Patrick alikasirika.

"Yuko sawa kabisa, sivyo?" Pamela alielewa kila kitu sasa. “Patrick, niko serious. Usirudi kwangu tena baadaye. Tunaachana.”

"Inatosha. Unapaswa kujua ni mistari gani hupaswi kupita.”

“Imekwisha. Utakuwa na Linda tu machoni pako. Ndio, unaweza kwenda upande wa Linda ikiwa amepata ajali, lakini huwezi kuonana kabisa na familia yangu. Hukunipigia hata simu. Leo ilikuwa siku muhimu kwetu, lakini haujali hata kidogo. Katika siku zijazo, sitakuwa na matarajio zaidi kwako, na sitatumaini chochote pia. Natumai hatutakutana tena.” Pamela akakata simu na kuuzika uso wake mikononi huku akilia kwa uchungu.

Baada ya kulia alifuta kabisa mawasiliano ya Patrick na Linda. Alikuwa amechoka sana kuteswa na watu hao wawili. Ilikuwa ni bora asingekuwa na matarajio, matumaini, na asingekuwa na maumivu. Wakati huo, alitaka kutafuta mtu wa kunywa na kuzungumza naye. Alitaka kumpigia simu Lisa, lakini akakumbuka kuwa Lisa hakuwa huru sasa. Kwa hivyo, aliendesha gari hadi baa mwenyewe. Baa zote za Masaki zilikuwa katika barabara moja. Kulikuwa na baa chache tu ambazo watoto matajiri wangetembelea.
•••
Saa tano usiku, Sam na Alvin walishuka kutoka kwenye chumba cha juu cha jumba lake. Baada ya kula chakula cha jioni usiku huo, Alvin hakutaka kurudi nyumbani kwake, kwa hivyo Sam aliongozana naye kwenye baa tena. Lakini, Alvin hakunywa sana siku hiyo, labda kwa sababu alikuwa amechoka kwa kulewa jana yake.

"Alvin, unarudi Nairobi kwa ajili ya mwaka mpya? Kama utakuwepo, babu yangu alikuomba uje kwetu,” Sam alisema huku akitembea. Alipotazama pembeni, mara akamuona mwanamke ameketi kando ya baa hiyo. Alivaa koti la pamba la rangi ya manjano lililofifia lililosaidiana na ngozi yake nzuri, na nywele zake ndefu za mawimbi zilining'inia kwenye mabega yake. Hata hivyo, alionekana kulewa kabisa. Wanaume wawili waliokuwa kando yake waliendelea kumvutavuta na kumsumbua.

“Siyo Pamela Masanja yule? Mbona anakunywa peke yake hapa?” Sam na Pamela walikuwa wamekutana mara kadhaa hapo awali, na alikuwa na mtazamo mzuri juu yake. Alikuwa msichana mchangamfu na anayejitambua na hakuharibiwa na mambo ya kupita. Alvin alimtazama na kumtambua kuwa ni rafiki mkubwa wa Lisa. Akasugua macho yake. Ikiwa kitu kingetokea kwa rafiki yake, bila shaka Lisa angekuwa na wasiwasi. "Nenda ukawaondoe hao watu wawili."

Sam mara moja akasogea na kuwashika wale watu waliokuwa wakipepea mgongoni mwa Pamela.

“Wewe sh*t... Bwana Harrison…” Mwanaume huyo aliuona uso wa Sam waziwazi na kumkoromea.

“Ondoka machoni mwangu mara moja. Huyu ni rafiki yangu. Nitamuua yeyote atakayethubutu kumgusa siku yoyote,” Sam alionya na kumpiga teke. Wanaume hao wawili wakakimbia mara moja. Kila mtu alijua kuwa neno la Sam Harrison lilikuwa sheria kwenye baa za eneo hilo. Kumkasirisha ilikuwa ni sawa na kujitakia kifo.

“Pamela, njoo, twende. nitakupeleka nyumbani.” Sam alimsaidia Pamela kuinuka. Pamela alimuegemea huku akiyumbayumba kwani alikuwa amelewa sana asiweze kutembea kwa usawa. Mdomo wake bado ulikuwa ukipiga kelele, “Siendi nyumbani! Bado nataka kunywa! Siku njema ya kutengana! Ni kwa kuagana na wabaya tu ndipo utakutana na walio sahihi…”

Sam alimsaidia kumkokota hadi kwenye gari, akionekana kuwa na huzuni. “Mwanamke huyu ameachwa na mpenzi wake, sijui amekunywa kiasi gani?'

"Unakaa nyuma." Alvin alikwenda kwenye kiti cha mbele cha abiria, hivyo Sam aliweza kukaa tu nyuma na Pamela. Hans akaendesha.
Mara baada ya Sam kuingia kwenye gari, Pamela alimshika kola na kumkaripia.

“Patrick Jackson, wewe b*stard, wewe *sshole! Nilikupenda kwa miaka minane, lakini una Linda tu machoni pako. Wewe ni kipofu?”

Mara Pamela akacheua kwa nguvu kama anataka kutapika, lakini hakutapika. Akaendelea tu kuongea kilevi. "Nakulaani kuwa utasalitiwa na kila mwanamke katika maisha yako yote."

Sam alipigwa butwaa. "Pamela Masanja, angalia kwa karibu. Mimi ni Sam Harrison.”

"Nani Sam Harrison?" Pamela aliinamisha kichwa chake. “Sijawahi kusikia habari zako. Unajaribu kuniteka nyara kwa sababu mimi ni mrembo sana?”

Sam alikosa la kusema na akamwelekeza mbele. “Unamfahamu Alvin Kimaro? Ni mpenzi wa rafiki yako mkubwa, Lisa Jones.”

Pamela alimtazama kwa butwaa, na macho yake yakaangaza ghafla. “Oh, ni mjomba. Habari, Mjomba.”

Alvin akasugua macho yake. Pamela alikuwa akimuita kwa jina hilo la kipuuzi kila alipokuwa amelewa .

Lakini, Sam alicheka. “Umekosea. Yeye si mjomba wako.”

“Sijakosea. Yeye ni Mjomba.” Pamela alitikisa mkono wake. “Sijakosea kamwe. Ni yule mpuuzi mjomba wa Ethan Lowe. Mimi na Lisa tulikuona mara ya kwanza tukiwa kwenye baa.”

Alvin alikunja uso na kuuliza kwa sauti ya chini, "Mbona umenikazia macho?"

"Lisa alitaka kuolewa na wewe kulipiza kisasi bila shaka. Ikiwa Lisa angeweza kuwa shangazi ya Ethan, hakika hilo lingemkasirisha hadi kufa. Inaweza pia kusababisha ghasia katika familia ya Lowe, haha.” Pamela alikuwa amelewa kabisa akiropoka hovyo. “Oh, ngoja, wewe si mjomba wa Ethan. Sorry! Nilikosea. Nimekuchanganya tena kama nilivyochanganya kumwelekeza Lisa. Yaani nikinywa pombe tu nakuonaga kama mjomba wake Ethan sijui kwanini, hahahaaa…nisamehe sana mjomba!”

Macho ya Alvin yalizidi kuwa meusi huku akisikiliza, Sam akameza mate akihisi amepata siri kubwa.

“Vipi uliishia kunifananisha?” Alvin alijaribu kulainisha sauti yake. “Ninafanana na mjomba wako?”

"Sina mjomba." Pamela alionekana mjinga. Baada ya muda, alijichanganya tena, "Mjomba, unapaswa kuwa mzuri kwa Lisa. Usiwe na hasira naye. Ni mimi niliyemtia moyo kukutumia dawa za kulevya. Kwa kweli haikuwa na uhusiano wowote na Lisa… ” Kisha, aliegemea mlango kwa butwaa na kulala.

Ndani ya gari, iwe Hans aliyekuwa akiendesha gari au Sam aliyekuwa amekaa nyuma, wote wawili walihisi joto la mle ndani lilikuwa limeshuka hadi kufikia kiwango cha baridi. Baada ya kuendesha gari kwa dakika tano, Alvin ghafla alisema, "Simamisha gari."

“Alvin.” Sam alikuwa na wasiwasi kidogo. “Umechelewa sana, twende nyumbani kaka.”

"Ninahitaji kufikiria juu ya kitu pekee yangu. Nyie mrudisheni kwanza.” Sauti ya Alvin ilikuwa ya nguvu.

Hans aliweza tu kusimamisha gari. Alvin akatoka nje, akafunga mlango na kutembea peke yake kando ya barabara. Sam akahema. Ingawa kile Pamela alisema hapo awali hakikuwa wazi, alikuwa na dhana isiyo wazi juu ya kile kilichotokea.
Aliweza tu kupata picha kwamba kutokuelewana kati ya Alvin na Lisa kulisababishwa na mkanyiko huo wa awali. Maskini Alvin!

Sura ya 142

Katika jumba la kifaharila Alvin, Lisa alitazama tena wakati. Ilikuwa saa sita na nusu usiku, lakini Alvin alikuwa bado hajarudi. Je, alienda kunywa nje tena? Kwa kweli hakutaka kumjali na alitaka kumpuuza tu, lakin alishindwa kuudhibiti moyo wake. Bila yeye, hakuweza kulala hata kidogo.

Ghafla, sauti ya mlango kufunguliwa ikasikika kutoka chini. Haraka akajilaza na kujifanya amesinzia. Dakika chache baadaye, mlango ulifunguliwa, na hatua za miguu zikakaribia kitanda. Aligundua kuwa Alvin alisimama kando yake. Moyo wake ukasisimka.

Ghafla, taa ikawaka. Kisha, blanketi juu ya mwili wake lilitolewa. Sauti ya mwanaume huyo ilisikika kutoka juu yake. "Simama."

"Alvin, unafanya nini sasa?" Lisa aliketi kwa uchovu na kumtazama. Macho ya mwanamume huyo yalikuwa mekundu kama damu na kumfanya aonekane mwenye sura ya kutisha.

Alvin alimtazama usoni Lisa aliyeonekana kutokuwa na hatia. Bado alikumbuka waziwazi mara ya kwanza alipokutana naye, pamoja na kila neno na kila usemi wa hila aliosema. “Ngoja nikuulize. Kwanini ulinitongoza kule kwenye baa?”

“Mbona unauliza hivyo ghafla?” Lisa alikwepa macho yake, hakutaka kujibu swali hilo.

Hata hivyo, Alvin hakumruhusu kujificha na kumshika kidevu chake. Macho yake malegevu yalifungwa kabisa na macho makali ya Alvin. "Ilikuwa ni kwa sababu ulinidhania kuwa mimi ni mjomba wa Ethan Lowe?"

Sauti ya Alvin ilionekana kusikika katika ubongo wa Lisa kana kwamba alikuwa amepigwa na radi. Akili ya Lisa ilikuwa imepotea. Alvin alijuaje kuhusu hilo?

Alvin alimtazama na kuona wazi mabadiliko yote katika sura yake. Uso wake ulibadilika rangi. Kulikuwa na hofu, mshtuko, na wasiwasi mkubwa machoni pake. Moyo wake pia uliongezeka mapigo inchi kwa inchi.

Alvin alijihisi kana kwamba alikuwa mpumbavu tu. Aliamini kwamba Lisa alimpenda mara ya kwanza tu alipomuona. Alifikiri kwamba alikuwa na uwezo mkubwa katika uhusiano huo, lakini alikuwa akichezewa naye tangu mwanzo. Mapenzi yake yote yalikuwa ya uwongo. Utamu wake wote ulikuwa bandia. Kila kitu kizuri kilikuwa bandia. Hata hivyo, moyo wake uliguswa sana na mwanamke huyo mnafiki.

“Hapana… Hiyo si…” Lisa alishikwa na butwaa na hakujua la kusema.

"Mipango yako inanifanya niwe mgonjwa sana." Alvin akamtikisa na kuufuta mkono wake kwa kitambaa kana kwamba amegusa kitu kichafu.

Lisa alichomwa sana na matendo yake. “Sawa, nakubali. Ilikuwa kweli mwanzoni, lakini baadaye - "

"Kisha ulikutana na Kelvin Mushi kwenye sherehe ya uchumba ya Ethan Lowe na ukagundua kuwa mtu huyo ndiye mjomba halisi wa Ethan, kwa hivyo ndiyo maana mara moja ukaanza kudai talaka, sivyo?"

Alvin alikuwa tayari ameshafahamu kila kitu. Hakutambua hapo awali, lakini sasa aligundua kwamba kulikuwa na kila aina ya mambo ambayo yalikuwa ya kutiliwa shaka. "Kwa bahati mbaya, baadaye ulifanyiwa njama na familia ya Jones Masawe na ulikuwa karibu kwenda jela. Hakuna mtu ambaye angeweza kukuokoa, hivyo rafiki yako wa karibu angeweza tu kuja kuniomba na kuendelea kunidanganya, akiniacha nifikiri kwamba ulinipenda kweli.”

Midomo ya Lisa ilikuwa imepauka. Kwa kweli alikuwa na akili sana. Kila kitu kilikuwa kama alivyokisia. “Ndiyo, lakini uliponiokoa kwenye eneo la ujenzi, niliguswa moyo sana nawe.”

"Funga mdomo wako. Hakuna ukweli katika chochote kinachotoka kinywani mwako wala rafiki yako wa karibu."

Alvin alizidi kupandwa na hasira huku akiongea. Alishindwa kujizuia na kumkandamiza kitandani huku akiikaba shingo yake kwa nguvu.

“Hata kama hukuleweshwa na Lina Jones kwenye hoteli usiku ule, ungetaka kulala na Kelvin Mushi hata hivyo, kwa hiari yako mwenyewe. Yaani mimi unanipetipeti tu kisha unaenda kulala na Kelvin, si ndiyo?”

"Kweli mimi ni mtu wa namna hiyo moyoni mwako?" Alipokuwa akibanwa, hakuweza kupumua. Upande huu wa Alvin ulimtisha sana.
“Si wewe? Nilitaka kulala nawe hapo awali, lakini uliendelea kunikatalia. Baadaye, ulipogundua kuhusu utambulisho wangu wa kweli, mara moja ulitaka kulala na mimi. Inasikitisha kwamba picha hizo zilinifanya nitambue kabisa sura yako halisi. Unajua kwamba mtu wa mwisho aliyeniudhi tayari amekwisha kwenda kuzimu?”

Alvin alikuwa kama mnyama mwenye hasira. Nguvu za mikono yake ziliongezeka.

Uso wa Lisa ulikuwa mwekundu, machozi yaliendelea kumtoka. Nuru ya macho yake ikawa nyeusi, naye akafikiri ya kwamba alikuwa karibu kukosa hewa na kufa. Alvin akamsukuma na kuupiga mto uliokuwa kando yake kwa nguvu.

Macho yake yaliyokuwa na damudamu yalimtazama. "Sitakuua kwa sababu sitaki kuchafua mikono yangu." Kisha, akafunga mlango kwa nguvu na kutoka chumbani.

Lisa alikumbatia magoti yake na kuzika kichwa chake ndani yake. Moyo wake ulijihisi mtupu. Pengine, yote yalikuwa ni bahati mbaya tangu mwanzo. Lisa alikuwa amemwendea Alvin kwa nia chafu. Baada ya hapo, alimdanganya tena na tena ili atoke jela. Sasa kwa kuwa uwongo wake ulikuwa wazi, uhusiano wao ulikuwa kama povu ambalo lingepasuka kwa kuguswa kwake.

Lisa hakupata usingizi usiku mzima. Aliamka mapema na kumuandalia Alvin kifungua kinywa. Pengine kingekuwa kifungua kinywa cha mwisho alichomtengenezea Alvin.

“Mbona umeamka mapema sana? Ni saa kumi na mbili na nusu tu” Aunty Linda aliingia jikoni huku akipiga miayo. Alipouona uso wa Lisa uliopauka, alipigwa na butwaa. “Jana usiku hukulala? Huonekani vizuri sana.”

"Anti Linda, haya ndio mapishi niliyoandika jana usiku." Lisa hakujali kile Aunty Linda aliuliza bali alimwambia yake na kumkabidhi kijitabu. "Haya ndiyo baadhi ya mapishi anayopenda sana Alvin. Yeye ni mbaguzi sana, kwa hivyo ninaweza kuhitaji kukusumbua ili kumpikia katika siku zijazo.”

"Unamaanisha nini?" Shangazi Linda alishtuka. Alijua kuwa wote wawili walikuwa kwenye mzozo mkali muda huo lakini migogoro ilikuwa ya kawaida kati ya wanandoa. “Haraka weka mbali hayo mawazo. Bwana Kimaro anapenda upishi wako. Hata nikipika vizuri hataki kula chakula changu.”

"Hakuna jinsi… sioni namna nnyingine tena." Lisa alitoa kicheko cha kujidharau. Kwa mtazamo wa mambo wakati huu, hakuthubutu kutarajia kwamba angeweza kuendelea kukaa ndani ya nyumba hiyo.
Hata kama yeye mwenyewe alimwambia Alvin kwamba alikuwa akimpenda, asingeamini pia. Angefikiri tu kwamba anapendezwa naye yote kwa sababu tu ya utajiri wake alioufahamu. Isitoshe, walikuwa wamepoteza imani katika kila mmoja wao. Ikiwa wangebaki pamoja, huenda wasingeweza kuishi kwa furaha.

“Usiongee ujinga.” Shangazi Linda alikataa kupokea kijitabu hicho. Kwa hayo, aligeuka na kuondoka. Lisa hakuwa na la kufanya zaidi ya kukiweka kwenye kabati la jikoni huku akiamini kuwa Aunty Linda angekiona.

Asubuhi hiyo, aliweka juhudi nyingi katika kuandaa kifungua kinywa. Kifungua kinywa cha siku hiyo kilikuwa sawa na kifungua kinywa cha kwanza walichopata walipoanza kuishi pamoja.

Saa mbili kamili asubuhi, Alvin alishuka akiwa amevalia sweta jeusi na suruali nyeusi. Kwa umbo lake refu, hakuwahi kushindwa kufanana na mtu mashuhuri aliyependeza na kung’ara bila kujali alivaa nini. Lakini, uso wake tu ndiyo ulitisha zaidi. Macho yake meusi yalikuwa makali kama ncha ya mkuki, na kumfanya Lisa kutetemeka.

Shangazi Linda alitaka wapatane, hivyo akatabasamu na kusema, “Bwana Kimaro, Bi Kimaro aliamka mapema sana saa kumi na mbili asubuhi ili kukuandalia kifungua kinywa. Hata hakuniruhusu nimsaidie. Angalia kupikia kwake - "

“Anti Linda, endelea na unachohitaji kufanya kwanza,” Alvin akakatisha sentensi yake.

Aunty Linda akahema. Hakuwa na budi ila kuondoka. Sebule ya nyumba ilibaki na wao wawili tu. Charlie na wanae watatu walikuwa wakicheza kwenye kochi. Alipowaona wakicheza kwa furaha, Lisa alijawa na wivu wenye huzuni. Alitamani bora kuwa paka mwenye furaha muda wote kuliko mwanadamu aliyeandamwa na matatizo tu, kwa kuzingatia maisha yasiyo na presha ya paka wale.

"Tia saini hii." Alvin akatupa hati kwenye meza ya chakula. Maneno yaliyoandikwa ‘Divorce Agreement’ (Makubaliano ya Talaka) yalimtoboa macho Lisa. Alivuta pumzi kwa upole, lakini bado aliweza kuhisi maumivu. Kwa kweli, bado alikuwa akimpenda. Wakati picha za Kelvin na yeye zilipofichuliwa kabla ya hilo jingine kuzuka, hakuwa ametaja nia yake ya kutengana naye au kumtaliki.

“Isaini. Nitamwomba mtu ashughulikie suala la talaka yetu.” Alvin akatazama pembeni. Kadiri alivyokuwa akiutazama uso wake wa kinafiki, ndivyo ilivyozidi kumkumbusha jinsi alivyomdanganya kama mjinga.

Jana yake usiku, alikuwa ametumia usiku kucha akifikiria mbinu nyingi, kulingana na uzoefu wake, kulipiza kisasi kwake.
Ghafla, aliona haina maana tena baada ya mbinu hizo za kikatili kumpita kichwani moja baada ya nyingine. Hakujisikia tena kuishi maisha ya namna hiyo. Kwa kuwa lilikuwa ni kosa tu, alitaka kurudisha kila kitu jinsi ilivyokuwa kabla ya hilo. Baada ya yote, alikuwa mpita njia tu ambaye hakuona kuwa wa kuthaminiwa.

Lisa aliinyanyua ile hati taratibu na kuipitia. Alvin alipomsikia akiipekua ile hati, alikunja uso kwa kejeli. “Tulipooana, nilikuahidi kuwa nitakulipa baada ya kuachana, na nilikusudia. Lakini sasa sijisikii kukulipa hata senti moja. Unapaswa kujisikia bahati kwamba ninakuacha oundoke na roho yako, vinginevyo... Ni bora nisiende mbali sana.”

“Sijawahi kuwaza pesa zako…” Lisa alicheka kwa uchungu. Alibaini kuwa mawazo ya Alvin yalikuwa kwenye pesa zake, kwamba Lisa alikuwa akiziwinda.

Sura ya 143

“Unafikiri bado nitaamini maneno yako?” Alvin hakujisumbua kumtazama Lisa machoni.

Lisa aliinamisha macho yake kimya kimya. Kwa mtazamo wa mambo, ilionekana kuwa hakuna kitu ambacho angeweza kuelezea zaidi akaeleweka. Alichukua kalamu na kusaini karatasi. Moyo wake haujawahi kuwa mzito hivi alipokuwa akisaini 'Lisa Jones'.

"Nimemaliza. Naenda ghorofani kufunga vitu vyangu, nitaondoka mara baada ya hapo.” Aligeuka na kuelekea juu. Alvin hakuwa na mpango wa kugeuza kichwa chake. Lakini, mwishowe alitazama nyuma na kujikuta anamtazama licha ya yeye mwenyewe kutaka.
Alikuwa amevaa nguo za kulalia za waridi, na nywele zake zilianguka juu ya mabega yake kama maporomoko ya maji. Harufu kama ya mwerezi ilitanda mahali alipotoka.

Alvin alikunja ngumi. Kadri alivyozidi kukunja ngumi ndivyo alivyokuwa akikosa hewa kifuani. Hapo awali alifikiria alikuwa anamtisha tu na asingesaini karatasi. Bila kutarajia, alisaini bila kusita zaidi. Pengine hakungoja kukutana na Kelvin tena. Hah…
Alidhihaki kwa kejeli. Kwa kuwa alikuwa amepitia vikwazo vingi, hakika asingekufa kwa sababu tu ya kuondoka kwake.

Nusu saa baadaye, Lisa aliburuta masanduku yake chini. Kwa wakati huo, hakuna mtu aliyekuwa sebuleni, na kifungua kinywa kizuri alichotayarisha hapo awali kilikuwa kimeishia kwenye pipa la takataka. Alikunja midomo yake kwa huzuni, akajifuta machozi kwenye kona za macho yake, akaondoka.

Alipotazama jumba hilo likiwa mbali zaidi kupitia kioo cha nyuma cha gari, alinung'unika ndani kwa ndani, 'kwaheri, Alvin.' Alikuwa akipaona mahali hapo kama nyumba yake pekee na Alvin kama mwanafamilia wake pekee. Lakini sasa, hatimaye alikuwa peke yake tena.

Kwa kuwa hakuwa na pa kwenda kwa wakati huo, Lisa alielekea kwenye nyumba ya Pamela. Baada ya Lisa kubonyeza kengele ya mlango kwa muda, Pamela alifungua mlango. Nywele zake zilikuwa chafu na kulikuwa na harufu kali ya pombe juu yake.

“Kwa nini umekuja na masanduku yako?” Akiwa amechanganyikiwa na kustaajabu, Pamela alitazama masanduku mawili yaliyokuwa kando ya miguu ya Lisa.

“Nimepewa talaka, na nimefukuzwa nyumbani kwa Alvin. Kwa vile sijanunua nyumba, sina pa kukaa isipokuwa mahali pako.” Lisa akaburuta masanduku yake ndani ya nyumba. Alijilaza kwenye kochi kama kikaragosi asiye na roho.

"Nini?" Pamela alipandwa na hasira. "Ni kwa sababu ya picha? Kama mpenzi wako, asingewezaje kukuamini? Mimi naenda kumfanya alipe. Ameenda mbali sana…”

“Usiende kwake.” Lisa alimsimamisha Pamela. “Tayari anafahamu kuwa mwanzoni nilimwendea kwa sababu nilimdhania kuwa ni mjomba wa Ethan. Pia amegundua kuwa ulimdanganya kabla ya hili kwa ajili ya kunitoa jela.”

"Nini? Aliwezaje kujua?” Pamela alipigwa na butwaa.

"Sina uhakika. Ni mimi na wewe tu ndo tulikuwa tunajua kuhusu suala hili." Lisa alimtazama kwa sura ya kinyonge. “Sikumwambia chochote. Kwa kuzingatia harufu kali ya pombe juu yako, labda ulikunywa sana jana usiku. Una tabia ya kuzungumza upuuzi baada ya kulewa.”

“Usinituhumu…” Pamela alishikwa na wazo alipokuwa akizungumza. Alishika nywele zake. “Sasa nakumbuka. Nadhani Sam ndiye aliyenirudisha nyumbani jana usiku, na nilikuwa nimelewa sana wakati huo. Kulikuwa na mwanamume mwingine ndani ya gari, na alidai kuwa mpenzi wako."

Lisa alikosa la kusema. Alikuwa kishajua tangu aliposikia akinuka pombe. Bila shaka, Pamela alikuwa ameropoka bila kujijua. Pamela aligonga kichwa chake kwa nguvu. Alitamani angepasua kabisa ubongo wake.

“Samahani, Lisa.” Akiwa amehuzunika, Pamela alipiga magoti mara moja mbele ya Lisa. “Nimekuingiza kwenye matatizo tena. Sijui jinsi ninavyoweza kukusaidia wakati wa maisha yangu. Naona aibu sana kukukabili. Vipi kuhusu kukutolea ndugu yangu kama fidia ya kosa langu? Ninaahidi kwamba atakupenda kikweli na atabaki mwaminifu kwako.”

"Acha kuongea ujinga." Lisa alipunga mkono wake akimaanisha kuwa alikuwa amechoka sana asiweze kumkaripia. “Hata hivyo, bado ingekuwa vigumu kwetu kuendelea na uhusiano wetu hata kama hukusababisha tatizo. Kuna suala kuhusiana na Kelvin na... mpenzi wake wa zamani ambaye hawezi tu kumshau. Kila mara hutaja jina lake anapokuwa amelewa.”

"Nini? Kwa nini wanaume huwa na macho ya kupepesuka?” Pamela alisaga meno kwa kufikiria kile kilichomkuta yeye mwenyewe.

“Vipi, ulimpeleka Patrick pamoja na familia yako kula chakula cha jioni jana usiku, sivyo? Kwa nini uliishia kunywa pombe?” Lisa alianza kushangaa ghafla. “Inaweza kuwa hivyo… Patrick alikutosa tena?”

Pamela alisema kwa uchungu, “Linda alipata ajali, Patrick akaenda kumwangalia. Hakunipigia hata simu. Nimeachana naye moja kwa moja safari hii.”

“Jamani. Ni balaa gani hili?” Lisa alitukana kwa hasira. Ghafla, akahema. “Sawa. Ulinifanya niishie kuachwa, na wewe uko single sasa hivi pia. Ngoma droo. Nitakuchukulia tu kama kampani yangu. Hata Patrick akikuomba urudiane naye wakati huu, usikubali kukutana naye tena.”

“Ndiyo, bila shaka. Mimi ndiye niliyekuumiza. Maadamu haujaolewa, sitathubutu kuolewa. Ikiwa hutapata hata mwanamume mzuri wa kukuoa, tunaweza kushiriki katika uhusiano wa jinsia moja. Kwani wanawake wangapi wanasagana?”

“Potelea mbali. sina hamu na wewe.” Lisa, ambaye mwanzoni alikuwa amekasirika, hakujua kulia au kucheka wakati huo.

•••
Chini ya dakika 20 baada ya kuondoka, gari la Sam lilionekana kwenye jumba la Alvin. Alikimbia kwa kasi hadi ghorofani, akamkuta Alvin akiwa amesimama kwenye kibaraza huku macho yake yakiwa barabarani. Alikuwa ameshika sigara, na sinia ya majivu iliyokuwa kando yake ilikuwa imejaa virungu vya sigara.

"Alvin, kweli utarudi Nairobi?" Sam alisema kwa hisia, "Nitaku’miss sana, na itakuwa tofauti kutokuwa na wewe karibu."

"Utani’miss kama rafiki au utakosa kuwa nami kama chanzo cha mapato cha kampuni yako?" Alvin aliacha majivu ya sigara yadondoke bila kujali.

Kwa aibu, Sam alitoa kikohozi chepesi. "Angalia, ingawa umekuwa hapa kwa muda mfupi tu, umeipatia zaidi ya shilingi bilioni moja kampuni yangu ya sheria mwaka huu."

Alvin akaingiza mikono yake mfukoni. Macho yake meusi, mazito yalionyesha hali ya ujeuri.

Sam akahema. “Sawa. Kama ningelijua hili mapema, nisingekualika Dar es Salaam. Kwa hiyo unaondoka lini?”

“Kesho. Tafuta mtu wa kuuza nyumba hii." Baada ya kuongea kwa sauti ya kupuuza, Alvin aligeuka na kuingia ndani ya nyumba.
•••

Asubuhi iliyofuata. Kitu cha kwanza alichofanya Lisa baada ya kuinuka kitandani ni kumuandalia Alvin kifungua kinywa. Dakika akitoka chumbani, alipigwa na butwaa baada ya kuiona sebule hiyo asiyoifahamu. Alisahau kuwa Alvin alikuwa ameachana naye. Hakuhitaji kuamka mapema ili kumpikia tena. Isitoshe, kusingekuwa tena na mlinzi wa kumuangalia. Kwa kweli, alikuwa ameachwa kama jongoo na mti wake.

Kama mwenyekiti wa kampuni yenye thamani ya zaidi ya dola milioni 500, alipaswa kuishi maisha kwa uhuru mkubwa zaidi. Alipaswa kufurahishwa na jambo hilo, lakini hakuweza kuhisi furaha hiyo hata kidogo. Baada ya kifungua kinywa, Lisa aliendesha gari hadi hospitali kumtembelea Kelvin. Hakuwa amemtembelea tangu siku alipopoteza fahamu.

Sura ya 144

Lisa alikuwa akijisikia hatia kwa jinsi alivyomtendea Kelvin.
Alisimama mbele ya wodi akiwa na maua na matunda. Wakati anakaribia kugonga mlango, mara akasikia mwanamke akilia kwa sauti ya chini ndani ya chumba hicho.

“Usilie mama.” Kelvin alimfariji mama yake.

“Siwezi kulia vipi? Wewe ndiye mwana pekee wa kiume katika familia ya Mushi. Nilitarajia uendeleze ukoo wa familia ya Mushi, lakini angalia nini kimetokea. Najiuliza ni nani aliyefichua suala hilo kuhusu figo yako? Wanawake wote ambao mwanzoni walitaka kuolewa na wewe sasa watakukwepa. Hakuna atakayetaka kuolewa wewe.”

Kelvin alijibu, “Haijalishi, Mama. Hata hivyo, sijisikii kuoa bado.”

“Mimi ndiye niliyekuzaa. Unafikiri nitajisikiaje? Huwezi kuacha kumfikiria Lisa? Hata ulihatarisha maisha yako kwa sababu yake.”
Akiwa ameshikilia kikapu cha matunda kwa nguvu, Lisa alisikiliza kile ambacho Mama Mushi alisema mwishoni. “Hata hajali kuhusu wewe. Umelazwa hospitalini kwa siku nyingi, lakini hajakutembelea hata kidogo.”

“Inatosha mama. Ni chaguo langu. Kumpenda mtu haimaanishi kuwa lazima uwe naye. Kumlinda na kumwangalia akiishi kwa furaha ni zaidi ya kutosha.” Kelvin alieleza.

Lisa alihisi uvimbe kwenye koo lake. Kuna kitu kilionekana kukwama kwenye koo lake, jambo ambalo lilimfanya akose raha. Kamwe hakutarajia kwamba Kelvin angempenda sana.

“Mbona umesimama hapa?” Mzee Mushi alikoroma kwa hasira nyuma ya Lisa nje ya wodi.

Lisa alishtuka, na wale waliokuwa chumbani wakamtazama.
Kwa hayo, aliingia chumbani kwa kusitasita. Kelvin aliguswa kuwa huenda Lisa alikuwa amesikia alichokisema. Kwa hiyo, uso wake mzuri ulianza kuona haya usoni. “Lisa, kwa nini umenitembelea leo, Alvin hatachukia?”

“Nimefika hivi punde. Mimi na yeye tayari tumeshaachana.” Lisa aliinua kichwa na kumtazama. Alionekana kuwa mwembamba sana ndani ya siku chache tu. Gauni alilovaa lilionekana kumlegea huku uso wake wa kifahari na mrembo ukionyesha kama mgonjwa anayesumbuliwa na utapiamlo.

"Mbona mmeachana ghafla?" Kelvin alipigwa na butwaa. "Ilikuwa kwa sababu yangu?"

"Hapana. Kuna matatizo mengi sana kati yetu.” Lisa alibadilisha mada. “Unaendeleaje sasa?”

"Anaendelea vizuri?" Mama Mushi aliinuka akiwa na uso mchangamfu. “Alipoteza figo, sasa figo moja si sehemu ya nyama yake tena. Hawezi hata kurejesha kimetaboliki chake bado. Kwa kuwa mikono yake inakabiliwa na uharibifu wa neva, anahitaji kupitia miezi michache zaidi ya matibabu. Mbaya zaidi, maisha yake ya baadaye yataathiriwa. Daktari alisema kuwa hatakiwi kufanya kazi ama mazoezi magumu, na anapaswa kuwa mwangalifu katika lishe yake. Vinginevyo, atapoteza maisha yake. Kwa kuzingatia kwamba kwa kawaida anahitaji kusimamia kampuni kubwa kama hiyo, nadhani hawezi kuishi maisha marefu.”

Mzee Mushi alimkemea, “Unaongea upuuzi gani? Zingatia maneno yako."

“Nimekosea? Tayari tuko katika miaka ya mwisho ya uzee wetu, kwa sababu tulikuwa na mtoto wetu mmoja tu wa kiume, pengine tunapaswa kumtunza milele.” Mama Mushi alijifuta machozi usoni mwake. “Unafikiri kuna mwanamke yeyote kutoka katika familia yenye heshima ambaye yuko tayari kuolewa naye? Maskini mwanangu, nina wasiwasi na maisha yako ya baadaye.”

Akiwa ameshikwa na hatia, Lisa alihuzunika sana. Alikuwa mwishoni kabisa mwa akili zake.

“Acha, Mama.” Kelvin alimsimamisha katikati ya maumivu ya kichwa chake.

“Nimekosea? Ulijeruhiwa kwa sababu yake. Alikutunza hata siku moja? Ingekuwa afadhali ungeokoa mtu usiyemjua kuliko yeye,” Mama Mushi aliongeza kwa uchungu, “Kwa maoni yangu, yeye ndiye anapaswa kuwa mwangalizi wako milele ili akusaidie. Hata hivyo, huwezi kupata mke kwa sasa, basi yeye awe fidia yake.”

“Mama…” Kelvin alishindwa kujizuia, na uso wake mzuri ukageuka kuwa wa kustaajabisha ghafla. Maumivu yalikuwa makali sana hadi akatoka jasho la baridi. Wakati huo huo, shinikizo lake la damu lilionekana kupanda juu ya kiwango.

Kila mtu aliingiwa na hofu na kumpigia simu daktari haraka.
Daktari alifika haraka na kuwakemea, “Mgonjwa amefanyiwa upasuaji mkubwa, badala ya kumfariji, mnampandisha presha. Mnataka afe?”

Kila mtu alinyamaza mara moja. Hata Mama Mushi alifunga mdomo kwa aibu. Kelvin alichoka sana hata akapitiwa na usingizi muda si mrefu.

Tena, Mama Mushi alimtazama Lisa kwa hasira. Lisa aliinamisha macho kwa hofu. “Acha kulalamika mama. Nitalipa fadhila kwake. Kuanzia leo na kuendelea, nitamtunza. Hata baada ya kupona, nitashughulikia lishe na maisha yake hadi apate mke.”

"Lakini vipi ikiwa hawezi kupata mke?"

"Hilo halitawezekana." Lisa alimtoa wasiwasi.

Mama Mushi alidhihaki. “Nani yuko tayari kuolewa na mwanaume aliyekosa kiungo? Ikiwa kuna matatizo na figo nyingine, labda atakufa kwanza. Isitoshe, sidhani kama kuna mtu mwingine yeyote ulimwenguni angekuwa tayari kuhatarisha maisha yake ili kukuokoa.”

Lisa alikaa kimya kwa muda wa nusu dakika kisha akaongea taratibu kwa sauti ya ukali, “Sawa. Ninaahidi atanioa.”

•••
Katika mgahawa, Pamela alipopata habari hizo, karibu amwage kahawa. “Umerukwa na akili? Unapanga kurudisha fadhila kwa kutoa maisha yako, huh?"

"Sina la kufanya tena." Lisa aliinywa kahawa iliyokuwa na ladha chungu sana. "Zaidi ya hayo, picha yetu imesambazwa kila mahali. Kila mtu ana hisia kwamba tuna uhusiano wa karibu. Hata hivyo ni sawa tu, alitoa figo yake moja kwa sababu ya kuniokoa…”

Pamela alishtuka baada ya kusikia hivyo. “Kelvin anakupenda sana. Siku zote amekuwa akikulinda kwa siri, lakini wewe na
Alvin…”

"Hatutarudiana kamwe." Lisa alionyesha sura ya uchungu. Hakumwambia Pamela kwamba Alvin alikuwa mtoto wa familia ya Kimaro. Lisa na Alvin walitenganishwa na bahari, na wote wawili walikuwa katika ulimwengu tofauti. Kwa kuongezea, mawazo yao yalikuwa tofauti kabisa.

“Sawa basi. Kwa kweli, wakati mwingine ni bora kwa mwanamke kutafuta mwanaume anayempenda zaidi kuliko yeye. Kwa njia hii, mwanamke hatahisi kuchoka.” Akikumbushwa kuhusu uzoefu wake wa mapenzi, Pamela aliugua. "Kwa upande wangu ninapanga kufanya kazi huko Nairobi mara tu baada ya mwaka mpya."

Lisa aliinua kichwa chake kwa mshangao. "Kwanini unaenda huko ghafla?"

“Si ghafla. Mwaka jana, kampuni ya Osher kutoka Kenya lilinipa nafasi ya mkemia mkuu wa vipodozi. Sikuweza kuvumilia kuachana na Patrick, kwa hiyo nilikataa kazi hiyo. Kampuni hiyo ilinipa kazi hiyo tena mwezi uliopita, na niliikubali jana.”

Pamela alitazama nje ya dirisha kwa huzuni. "Nimekuwa nikifikiria juu ya Patrick katika wakati wangu wote nikiwa hapa Dar. Natamani kuona ulimwengu mpya, na ninaamini nitasahau kuhusu uhusiano huo polepole baada ya muda."

"Inaonekana kama wazo zuri." Ghafla, hali hiyo iliacha pengo kwa Lisa kwani rafiki yake wa pekee naye angemuacha. "Ninaweza kuelekea Nairobi pia na kukuza biashara ya Mawenzi Investments huko mwaka ujao. Kuhusu kifo cha mama yangu… nataka kuja kuchunguza pia.”

“Uko sahihi. Baba yako anatoka Nairobi pia. Nitakusubiri uje.”

Usiku, Lisa alipakua masanduku yake. Alipofungua moja, ghafla akakuta Mkufu wa Malkia ndani yake. Wakati anahama kwa Alvin alikuwa amepakia vitu vyake haraka na kusahau kuviangalia kwa uangalifu. Kwa kushangaza, alikuwa amebeba na Mkufu pamoja. Kwa kuzingatia kwamba kitu hicho kilikuwa cha gharama kubwa, asingeweza kubaki nacho.

Siku iliyofuata, aliendesha gari hadi kwa Alvin tena. Alitumia muda mwingi akibonyeza kengele ya mlango, lakini hakuna aliyefungua mlango.

“Huna haja ya kuibonyeza tena. Mmiliki ameondoka Dar es Salaam.” Mwanaume aliyevalia suti nyeusi akatokea nyuma yake.

"Wewe ni…" Lisa aliuliza.

“Mimi ni dalali wa nyumba. Nilikuja kuchukua picha chache za jumba hilo ili kuisambaza kwa wateja na kuiuza,” mwanamume huyo alitabasamu na kusema, “Mmiliki alisema anataka kuiuza kwa bei nafuu. Kwa kuzingatia eneo na muundo wake, ninaamini itauzika hivi karibuni.

Sura ya 145

Mara tu dalali yule alipomaliza kuzungumza, ghafla aligundua kuwa uso mzuri wa mwanamke yule ulionekana kupauka. Alikaribia kukosa mwelekeo wake. "Uko sawa, mwanamke mzuri?"

“Mimi… nipo sawa.” Lisa akamkabidhi kadi yake ya biashara. "Ningependa kununua nyumba hii ya kifahari, lakini natumai hutafichua utambulisho wangu kwa mmiliki wa awali. Nitakulipa kamisheni pia.”

“Oh, sawa, hakika.” yule dalali alifurahi. Hakutarajia kwamba angeweza kuuza jumba lile kwa kutembea tu hadi mlangoni. Ni kazi rahisi iliyoje.

Baada ya kuingia ndani ya gari, Lisa alitawaliwa na hali ya kuchanganyikiwa. Ghafla, alihisi kana kwamba moyo wake ulikuwa umetoweka. Ingawa alikuwa ametia saini hati za talaka, hakutarajia Alvin angeondoka Dar es Salaam mapema namna ile. Hiyo ilimaanisha kwamba wote wawili wangeweza wasikutane tena kwa vile walikuwa katika miji tofauti. Alikuwa amejitoa katika maisha ya Alvin, lakini kwa nini moyo wake ulikuwa bado unauma kiasi cha kushindwa kupumua? Aliushika Mkufu wa Malkia huku akilia kwa jazba.

Dakika 40 baadaye, alijitokeza kwenye ukumbi wa kampuni ya mawakili ya Jeninnings akiwa na miwani ya jua usoni. Mhudumu wa mapokezi pale mlangoni akamtambua mara moja. Baada ya kumuona mhudumu wa mapokezi alihema kwa huzuni kwani asingeweza tena kuiona sura nzuri ya Mr. Kimaro kila siku. “Unamtafuta Bwana Kimaro? Ameondoka.”

"Namtafuta Sam." Lisa alimsahihisha.

Mhudumu wa mapokezi aliwasiliana na msaidizi wa Sam mara moja. Muda si muda, aliagiza Lisa apande ofisini kwake. Ofisini, Lisa alipitisha boksi la velvet kwa Sam. “Mkufu wa Malkia uko kwenye boksi. Tafadhali mpe.”

"Alvin hataitaka" Sam alisema kwa uhakika, "Itunze tu. Nadhani ataitupa mara atakapoiona.”

“Hebu atupe basi. Bidhaa hii ina thamani ya shilingi bilioni tatu, ambayo ni gharama sana. Sitaki anidai.” Kwa hayo, Lisa aliinuka na kuondoka.

Lisa alipokea simu kutoka kituo cha mahabusu mchana. Ilitajwa kuwa Jones Masawe alikuwa na hamu ya kumuona kwa mara ya mwisho. Hukumu za Jones Masawe na mkewe zilikuwa zimetolewa. Kwa kuwa mama Masawe ndiye aliyekuwa muuaji, alihukumiwa kifungo cha miaka 20. Kwa upande wa Jones Masawe, alihukumiwa miaka kumi tu kwa kuwa msaidizi. Ukizingatia uzee wao, maisha yao yalikuwa yamekwisha. Baada ya kufikiria kidogo, aliamua kuwatembelea.

Alipomwona Jones Masawe tena baada ya siku kadhaa, tayari alikuwa na mvi kana kwamba alikuwa amekua kwa miaka kumi.

“Kwa nini ulinitaka nije?” Lisa aliuliza bila kujali. Tayari hakuwa na hisia naye hata kidogo.

Jones Masawe alijibu kwa huzuni, “Najuta, na nimejisalimisha kwa hatima yangu. Nimehamisha hisa zote za Mawenzi Investments kwako. Ninachotumai ni kwamba utamruhusu Lina atoke kwenye ndoano. Baada ya yote, yeye ni binamu yako, ambaye pia ndiye mwanafamilia wako pekee.”

"Amefanya mambo mengi maovu." Lisa alikunja uso kwa kejeli. "Aliponiumiza, hata alinifikiria kama mimi ni binamu yake?"

Jones Masawe aliuma midomo yake. “Ulimtumia pia mtu kumdhuru? Tangu mimi na mama yake tufungwe jela, hajatutembelea hata kidogo.”

Lisa akabaki ameduwaa. “Pamoja na mambo mengi yanayoendelea kwa sasa, sikupata hata muda wa kumfanyia chochote. Haishangazi kwamba hajaja kukutembelea. Umemlea kwa muda gani? Kwa mtu katili kama yeye ambaye atafanya chochote kufikia malengo yake, bado unatarajia atakuwa na mawazo na wewe? Nina hakika sasa atakukwepa kadri awezavyo.”

Jones Masawe aliyatoa macho yake kwa butwaa. Alichosema Lisa kilionekana kuwa pigo kubwa kwake. Jones Masawe na mkewe walipofikiria, waligundua kuwa Lina ndiye mtu ambaye alikuwa mbinafsi zaidi yao. Wangewezaje kuweka matumaini yao kwa binti huyo? Alikuwa binti yao wa kuzaa, lakini vipi hakwenda kuwaona?

Jones Masawe alilazimisha tabasamu. Kwa kweli, Lisa alikuwa binti mzuri. Hata hivyo, Jones Masawe na mkewe hawakuwahi kumjali kwa sababu tu hakuwa mtoto wao wa kumzaa. “Uko sahihi. Ni kosa langu, Lisa."

"Natumai utajuta gerezani kwa yale uliyofanya." Lisa alisimama na kuondoka kwenye kituo hicho cha mahabusu.

Baada ya kurudi ofisini, alimwomba msaidizi wake amtazame Lina.
Msaidizi haraka alimletea habari kuhusu Lina. "Amepotea kwa siku kadhaa. Hata hakuchukua vitu vya nyumbani kwake. Hakujawa na miamala yoyote katika akaunti yake ya benki pia. Anaonekana kutoweka kimaajabu sana.

Lisa alipigwa na butwaa. Hakutarajia kwamba Lina angetoweka vile vile baada ya kupigana naye kwa muda mrefu. Kwa mwonekano wa mambo, hakukimbia kweli. Labda maisha yake yalikuwa hatarini.

Kwa wakati huo Lisa alifanya kazi huku akimhudumia Kelvin. Kimsingi, mtu angeweza kusema kwamba walikuwa wakiishi pamoja. Alitumia mkesha wa Mwaka Mpya katika jumba la kifahari la Kelvin. Usiku, nyumba ya familia ya Mushi ilikuwa na mwanga mzuri. Lisa alipomsukuma Kelvin aliyekuwa amekaa kwenye kiti cha magurudumu kutoka chumbani, akakutana na Ethan, Tracy na Sonya waliokuja kula chakula cha jioni. Wote watatu walipigwa na butwaa kumwona. Uso wa Sonya ukawa mgumu mara moja.

"Lisa, huna aibu kama nini kuonekana nyumbani kwetu -

"Nyamaza. Mwite wifi wakati mwingine." Mama Mushi alimsogelea Sonya na kumwambia aondoke. “Atachumbiwa na Kelvin baada ya Mwaka Mpya. Acha kuongea chochote kilichotokea huko nyuma." Alinyamaza kisha akamwambia Ethan, “Lazima umuite ‘Shangazi’.” Wakati huo, Sonya na Ethan walivaa sura ya kustaajabisha.

Lisa alihisi kutokwa na machozi kutokana na hali hiyo kuwa mbaya.
Hili ndilo tukio aliloliota miezi kadhaa iliyopita. Ingawa tukio kubwa lilikuwa limefanyika hatimaye, hakufurahishwa nalo kwa sababu mambo mengi yalikuwa yamebadilika.

"Baba, unatania?" Sonya karibu aingie kichaa. Hapo awali, Lisa alikaribia kuwa ‘binti-mkwe’ wake, lakini Sonya alilazimika kumwita 'wifi' sasa. Je, Mungu alikuwa akimdanganya?

Mzee Mushi alimkodolea macho Sonya. "Sasa ndiye mtu anayesimamia Mawenzi Investments. Hadhi yake ni kubwa kuliko yako. Je, ni vigumu kwako kumwita ‘wifi’?” Sonya alinyamaza mara moja.

Hakuwa mjinga. Ikiwa Kelvin na Lisa wangefunga ndoa, ingefaidisha familia ya Mushi. Zaidi ya hayo, kwa hali ile ya Kelvin, mwanamke yeyote kutoka katika familia mashuhuri bila shaka angekataa kuolewa naye.

Jikoni, Lisa alivaa apron na kuandaa vyakula vya kiasili zaidi. Kwa kuzingatia kwamba mwili wa Kelvin ulikuwa dhaifu, alikuwa amechukua usimamizi kamili wa lishe yake. Ethan alipoingia ndani alihisi kubanwa kifuani kwa kuuona mgongo wa Lisa. Alikuwa anajua upishi wake mkubwa. Mara nyingi alipika vyakula mbalimbali kwa ajili yake wakati ule pia. Hata hivyo, asingepata tena upendeleo huo.

"Lisa, upo tayari kuolewa na mjomba wangu?" Ethan alimsogelea na kutazama umbo lake zuri na la kuvutia chini ya taa.

Lisa aliinamisha kichwa chake, akaweka viungo kwenye sufuria na kusema. "Anahitaji mimi nimtunze."

Ethan alitoa kicheko cha uchungu. “Natamani ningekuwepo siku hiyo. Ningekuwa tayari kukuokoa kutokana na kuchomwa kisu pia…”

"Kama nisingekuwa mwenyekiti wa Mawenzi, usingeniokoa." Lisa aliinua kichwa chake na kumtazama kwa kutokubali.

Uso mzuri wa Ethan ukawa mgumu. “Acha kusema mambo ya namna hii. Mpenzi wako yuko nje anakusubiri.” Lisa alitoka jikoni huku akiongea.

TUKUTANE KURASA 146-150

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..........LISA
KURASA......146-150

Sura ya 146

Saa sita kamili usiku, fataki ziliangaza anga la usiku. Lisa alimshika Kelvin mkono na kumpeleka kitandani. Alipomlaza kitandani, Kelvin alimshika mkono. Huku fataki zikionekana katika macho yake yenye giza, alionekana kuangaza macho yake vizuri. “Lisa upo tayari kuolewa na mimi kweli? Usijute.”

"Ninaogopa kuwa wewe ndiye utajuta badala yake." Lisa alikunja uso na kusema kwa mawazo, “Ninapanga kuhamisha makao makuu ya Mawenzi Investments hadi Nairobi mwaka ujao. Nataka kujua sababu ya kifo cha mama yangu. Sijui adui zangu wa baadaye watakuwa na nguvu kiasi gani—”

“Nitakusindikiza. Nitaenda hadi miisho ya dunia ili kukusaidia wakati wa maisha yangu,” Kelvin alikatiza sentensi yake kwa sauti ya kudhamiria.

Lisa alibaki kimya kwa muda. Kwa kuzingatia tabia ya Kelvin, hakuweza kuvumilia kumkataza na kumuumiza. "Asante."

Baada ya mwaka mpya, Lisa alielekeza akili yake kwenye kazi.
Mali mpya za Mawenzi Investments ziliuzwa haraka, na kurahisisha mtiririko wa pesa wa kampuni.

Alipokuwa akipakia vitu vyake ili aondoke jioni hiyo, mhudumu wa mapokezi akampigia simu ghafla. “Mkurugenzi Maganga yuko hapa. Alikuja na mtu ambaye anadai kwamba anataka kukutana nawe."
Lisa alipigwa na butwaa. Chris Maganga alikuwa amerudi Mwanza baada ya kumsaidia katika kuimarisha cheo chake kama mwenyekiti, kwa hiyo kwa nini alikuwa amerudi kwa ghafla?

Dakika tano baadaye, mlango wa ofisi ukasukumwa. Chris alitokeza mlangoni na kunyoosha mkono wake kwa heshima. Baadaye, mtu mrefu ambaye alitoa mwonekano wa utulivu na heshima aliingia.
Mwanamume huyo alikuwa na sifa za kuvutia, lakini aliweza kutambua kwamba alikuwa na umri wa makamo kutokana na mikunjo ya macho yake. Wanaume walikuwa watu wazima zaidi katika umri huu.

Chris pia alikuwa na umri wa makamo, lakini mwonekano na sifa zake hazikuweza kulinganishwa na za mwanamume huyo. Mwanaume huyo alipoingia tu ofisini, alimkazia macho Lisa. Macho yake yalionekana kuwasilisha kila aina ya hisia ikiwa ni pamoja na furaha, huzuni, na taabu.

“Mjomba Chris, huyu…” Lisa alijawa na mshangao.

Chris akajibu, "Yeye ni baba yako, Joel Ngosha."

Kichwa cha Lisa kikamlipuka. Alikuwa amemfikiria baba yake mzazi hapo awali. Hata hivyo, kwa kuonekana kwake ghafla sasa, hakuweza kujizuia kuhisi amepigwa na butwaa. Zaidi ya hayo, jina la 'Joel Ngosha' liligonga kengele akilini mwake! Alikuwa mmoja wa wafanyabiashara watanzania kumi mashuhuri zaidi waliofanikiwa nje ya nchi kwa mwaka uliopita. Hapo awali alikuwa amekutana na habari zinazoelezea kwamba Joel alitoka kwenye familia ya kisukuma huko Mwanza na alianza na baishara akiwa Mwanza hadi akafanikiwa kukuza na kuvuka mipaka hadi Kenya. Alikuwa mmoja wa watu wema zaidi huko Nairobi, na zaidi ya hayo, alikuwa mtu mashuhuri mwenyewe.

Iliaminika kuwa familia ya Ngosha haikuwa na nguvu sana mwanzoni. Chini ya uongozi wa Joel katika miaka michache, hata hivyo, waligeuka kuwa moja ya familia tajiri zaidi katika jiji la Nairobi. Mwanaume huyu kwa kweli alikuwa baba yake mzazi. Hakuweza kuamini kabisa.

"Wewe ni picha ya mama yako." Joel aliendelea kumtazama Lisa huku machozi yakimtoka. “Sikutarajia kuwa Sherly angenificha. Hakika alijifungua binti yetu.”

"Sherly alikuwa na matumaini kwamba Lisa angeweza kukua salama," Chris alisema kwa sauti ya chini.

“Uko sahihi. Sikuwa na uwezo wakati huo.” Joel alikunja ngumi akionekana kukumbushia jambo la uchungu. "Kama nisingesikia kuhusu kuteuliwa hivi majuzi kwa mwanamke mchanga, ambaye alikuwa binti ya Sheryl, kama mwenyekiti wa Mawenzi Investments, nisingejua uwepo wako."

Mambo mengi sana yalikuwa yamemtokea Lisa ndani ya kipindi kifupi. Licha ya kukumbwa na wimbi la hisia ndani yake, alijituliza baada ya muda mfupi. "Kwa hivyo, kwa nini unataka kukutana nami?" Aliuliza bila kujali na bila kujadili.

Joel alipigwa na butwaa lakini punde si punde alionyesha hali ya kusikitisha. “Tabia yako inafanana na ya Sherry enzi hizo, Lisa. Ningependa kukurudisha kwa familia ya Ngosha ili kufidia malezi yote ambayo umekuwa ukistahili kutoka kwangu kama baba yako kwa miaka mingi.”

“Sidhani kama hilo ni wazo zuri. Tayari una familia yako mwenyewe na una watoto. Mimi si mtoto tena, sitarudi nyuma.” Akiwa amechoshwa na migogoro ya kifamilia, Lisa alikataa.

“Lisa…” sura ya wasiwasi ilivuka uso wa Joel. “Lazima uende nami. Nahitaji kukutazama ili niweze kukulinda. Utambulisho wako utafichuliwa hivi karibuni. Wengi wao kutoka kwa ukoo wa Ngosha wamegundua uhusiano wangu na mama yako wakati huo.”
Lisa alipigwa na butwaa.

Chris kisha akaeleza, “Familia ya Ngosha ina mali nyingi ambazo vijana wengine katika familia wanatazamia. Kwa kuwa wewe ni binti wa Bwana Ngosha, utaingia katika urithi wake siku zijazo. Baadhi ya watu watahatarisha maisha yao kwa ajili ya madaraka.”

Lisa alikasirika na kukosa kusema, lakini hakupendezwa na utajiri wake hata kidogo. Kwa kweli, kuonekana kwa ghafla kwa baba yake kulikuwa kumeweka mzigo juu yake.

“Usiogope bwana Ngosha. Nitamshawishi. Tumtembelee Sheryl sasa.” Chris alibadilisha mada.

Lisa alikubali kuungana nao. Wakati wa safari, Joel alimsimulia hadithi nyingi kuhusu jinsi alivyokutana na Sheryl. Hata hivyo, hakuguswa hata kidogo. Aliuliza, “Kwa nini uliachana na mama yangu wakati huo?”

'Miaka 20 iliyopita, sikuwa na uwezo kiuchumi. Katika uhangaikaji wangu kwa bahati mbaya nikakutana na kulala na mke wangu wa sasa, Nina Mahewa. Baada ya mama yako kujua, aliamuua kuondoka akiwa na mimba yako. Muda si mrefu, nilisikia kwamba amefariki.”

Sura ya uchungu iliosha uso wa Joel. "Kisha, nilianza kuishi maisha yangu katika hali ya mshangao. Nina alipopata ujauzito, nilikubali kumuoa ili niwajibike kwa mtoto.”

Lisa alipokuwa akimsikiliza, alijawa na chuki. Ilikuwa hadithi ya kuudhi iliyoje. Alimuonea huruma mama yake kwa kuwa mwathiriwa. Baada ya kutembelea makaburi, aliondoka kwa kisingizio cha kuwa na kitu cha kuhudumia.

Joel alipomtazama akiondoka, alishusha pumzi ndefu. “Oh, Chris. Inaonekana binti yangu hataki kunitambua.”

"Lisa ameteseka sana katika familia ya Jones mwaka jana," Chris alieleza.
“Ndiyo. Ni kosa langu kwamba nilikuja kujua kwa kuchelewa sana. Lazima nimrudishe kwa familia ya Ngosha. Ninataka kumfanyia kazi na kumtunza vizuri,” Joel alisema kwa hatia.

Asubuhi iliyofuata, Lisa alikuwa na mkutano. Baada ya hapo, alirudi ofisini na tayari Chris alikuwa akimsubiri pale.

"Mjomba Chris, ulishajua mapema kuwa yeye ni baba yangu?" Lisa aliuliza moja kwa moja, "Je, unatarajia kwamba nitarudi kwa familia ya Ngosha pia?"

Chris alikuwa mkweli naye. "Lisa, unaweza tu kujua ni nani aliyemuua mama yako wakati huo ikiwa utarudi kwa familia ya Ngosha. Nimekuwa nikishuku kwamba huenda alikuwa Nina.”

Lisa kichwa kilimuuma. Ilimbidi ahusishwe katika mzozo mwingine wa kifamilia wakati alikuwa amemaliza tu mgogoro mmoja. Uchovu wake ulikuwa hauelezeki.

“Kwa hiyo, wakati huo alikuwa akimwonea wivu mama yangu hivyo akaamua kumuua?”

"Nina ni mtu katili sana. Yeye pia ni binti mkubwa wa familia ya Mahewa. Chris alipumua na kusema kwa unyoofu, “Ni sawa ikiwa hujisikii kuchunguza suala hilo. Kwa kweli, ni miaka mingi imepita tangu mama yako afariki. Zamani zimepita kwa muda mrefu na upepo. Kwa sasa, Joel na Nina wako kwenye uhusiano mzuri. Hata hivyo haitakuwa rahisi kwako kushughulika naye.”

Lisa alinyamaza kimya.

Chris kisha akasimama na kusema. “Nimekuja hapa kukujulisha kuhusu jambo hili. Baada ya kusema hivyo, kumbuka kwamba ikiwa Nina atapata habari kuhusu kuwepo kwako, hakika atakuwa mtu wa kwanza kushughulika nawe. Badala ya kuachwa juu na kuti kavu, afadhali ukae karibu na Joel.”

“Joel ana mke na binti ambaye ameishi nao kwa zaidi ya miaka 20. Mbali na ukweli kwamba nina uhusiano naye wa damu, nitaweza kweli kuwashinda? Lisa alitoa kicheko cha uchungu.

Chris alijibu kwa uzito, “Joel alikuwa akimpenda sana mama yako wakati huo. Amekuwa akimfikiria kwa miaka hii yote. Atakulinda.” Lisa aliposikia hivyo alikaa kimya kwa muda mrefu.

Sura ya 147

Usiku, katika ua wa jumba la familia ya Mushi, Kelvin alichukua dawa kutoka kwenye kiganja cha Lisa. Macho yake meusi yalibeba huzuni ambayo ilikuwa ngumu kidogo. “Kweli wewe ni binti Joel. Hiyo ina maana… siko na wewe kwenye level moja tena na wewe. Wewe ni wa hadhi ya juu zaidi kwa sasa.”

“Hapana. Sijawahi kuwa na nia ya kupata chochote kutoka kwa familia ya Ngosha.” Sauti ya Lisa ilijawa na uchovu. "Hata hivyo, lazima nielekee Nairobi wakati huu. Mimi…”

"Endelea." Kelvin aliweka mkono wake kwa upole juu ya nyuma ya mkono wake. “Usijali kuhusu mimi. Mlezi atanitunza.”

"Asante." Kwa kweli, Lisa aliguswa sana. Kelvin na Alvin walikuwa tofauti sana. Kelvin daima alikuwa mpole na mvumilivu kwake. Kinyume chake, Alvin alikuwa jabari na mwenye kiburi. Mara nyingi alilazimika kuvumilia tabia yake. Kila alipotaka kufanya jambo, ilimbidi ajidhatiti kumshawishi ili apate kibali chake. Aliona ni ngumu kuelewana na Alvin kwa tabia hiyo. Pia hakupendezwa na ukweli kwamba alikuwa amemwekea mlinzi wa kumtazama kwa kila hatua.
Lakini, kwa njia fulani alikuwa na ugumu wa kuzoea maisha baada ya Alvin.

"Unafikiria nini?" Macho ya Kelvin yaliangaza kwa utusitusi, na akaushika mkono wake kwa nguvu.

Lisa alirejewa na akili muda huo huku akijiuliza ni kitu gani kilimkumbusha Alvin tena. "Nilikuwa nikifikiria kuwa huenda familia ya Ngosha ni kubwa, na labda ni mahali pa hatari kuwapo huko."

Kelvin alitabasamu kwa uchangamvu sana. “Usiogope. Nitakutambulisha kwa marafiki zangu wa Nairobi baadaye. Hutakuwa peke yako katika kesi hiyo. Kwa kweli, nimerejea kutoka ng'ambo mwaka jana na nimekuwa nikipanga kuendeleza biashara yangu huko Nairobi pia. Eneo jipya la kiuchumi lilipoanzishwa huko miaka miwili iliyopita, nilikuwa tayari nimenunua kipande cha ardhi ili kupanua kiwanda.”

Lisa alipigwa na butwaa na kumshangaa sana. "Sikutarajia kuwa wewe ni mtu anayefikiria mbele."

“Bora zaidi ni kuwa na mtizamo wa mbele wa kukuangukia wewe.” Kelvin alicheka huku akibana ncha ya pua yake.

Lisa aliganda. Alvin alikuwa akimbana kwa njia hiyohiyo, lakini kubanwa na Kelvin kulimfanya akose raha na hata kustahimili kidogo.

“Tayari ni usiku sana Nitarudi chumbani kwangu kwanza.” Tabasamu kidogo liliruka usoni mwake. "Pumzika mapema baada ya kuchukua dawa." Aligeuka, na kugundua kuwa Kelvin alikuwa bado hajaachia mkono wake.

Alitazama nyuma na kukutana na macho ya Kelvin yenye upendo na upole. “Lisa, unaweza kukaa hapa usiku huu? Usijali, sitakufanya lolote kwani bado sijapona majeraha yangu.”

“…Samahani, Kelvin. Nimetoka tu kwenye uhusiano na mtu mwingine, kwa hiyo bado sijazoea. Nipe muda.” Lisa alimkataa bila kujua.

Ilikuwa rahisi sana kuwa kwenye mahusiano na Kelvin. Hata hivyo, kwa mawazo ya kulala kitanda kimoja na yeye, hakuweza kufanya hivyo. Macho ya Kelvin yalitiwa giza, lakini alilazimisha tabasamu. “Sawa.”

Siku tatu baadaye. Lisa na Joel walielekea uwanja wa ndege wa kimataitaifa wa Julius Nyerere. Kelvin binafsi aliwapeleka kwenye uwanja wa ndege. “Nisubiri Lisa. Nitakuja kukutana nawe huko mara nitakapopona.”

“Sawa. Tuendelee kuwasiliana kwa simu.” Baada ya kupunga mkono, Lisa alipanda ndege pamoja na Joel.

Joel alikuwa akimtazama Kelvin alipokuwa akielekea uwanja wa ndege. Alimpata Kelvin akimfahamu sana, lakini hakumvutia sana baada ya kufikiria kwa makini. Kwa macho ya Joel, ilikuwa ni huzuni kwamba binti yake tayari alikuwa na mchumba katika umri mdogo. Hakika, Kelvin alikuwa wa kushangaza ukizingatia jinsi alivyokuwa kijana na mwenye mafanikio. Ikilinganishwa na familia ya Ngosha, hata hivyo, hadhi yake ilizingatiwa kuwa ya chini kidogo.

"Ni kweli alipoteza figo kwa sababu ya kukuokoa?" Joel aliuliza.

“Ndiyo. Bila yeye, ningeweza kufa. Ikiwa huniamini, nenda ukachunguze jambo hilo,” Lisa alinong’ona, “Usinipangie siku ya kutoonana naye wakati tunapokuwa Nairobi. Sitafurahia.”

Joel aliposikia maneno yake aliangua kicheko. Kisha, akapumua.

“Sitaingilia masuala ya mahusiano yako. Wakati huo, wazazi wangu walinilazimisha kuoana na mtu ambaye sikumtaka. Kwa hilo, nilianza kuishi miaka ya maisha yenye huzuni. Kilicho muhimu zaidi ni furaha yako. Hali ya wastani ya Kelvin sio suala kwani ninaweza kumpa mkono kila wakati. Uwezo wake pamoja na usaidizi wangu utamfanya kuwa mzuri kama wale vijana kutoka familia tajiri huko Nairobi.

Lisa alishikwa na butwaa. Alibadili sana mtazamo wake kuelekea baba yake. "Haitakuwa ... shida sana?"

‘Ni jambo dogo tu.” Joeli bila kujali alimgusa nywele zake ndefu. "Hata kama utapanga talaka siku zijazo, hutahisi kwamba una deni la Kelvin."

“Baba...” Lisa alishtuka kwamba neno hilo lilimtoka kinywani mwake bila yeye kutambua.

Joel alifurahi sana. "Sema hivyo tena." Badala yake, Lisa aliinamisha kichwa na kukaa kimya.

Joel alitabasamu. "Nimepata msisimko wa kwanza wa upendo pia. Nilipoagana kwa muda mfupi na mama yako wakati huo, nilichanganyikiwa sana hivi kwamba sikuweza kuacha kumfikiria, jambo ambalo ni tofauti na jinsi nyinyi mnavyochukuliana sasa hivi. Ninaona kuwa anakupenda. Lakini mara tu ulipoingia kwenye ndege, nadhani ulifarijika badala yake.”

Lisa hakuongea neno lolote. Akilinganishwa na Jones Masawe, Joel alikuwa bora zaidi kwa kuwa alikuwa mwangalifu na alimjali sana. Labda angeweza kuhisi uchangamfu wa kibaba uliopotea kwa muda mrefu wakati wa safari yake kwenda Nairobi wakati huo.

Baada ya kushuka kwenye ndege, Joel alimpeleka kwenye jumba la kifahari lililopo Sherman Mountain. Hiki ni kitongoji maarufu ambacho kiko nje kidogo ya jiji la Nairobi, ambako matajiri wengi wa Kitanzania waliowekeza nchini Kenya wamejenga na kuishi huko. Kulikuwa na idadi kubwa ya majengo ya kifahari na majumba kwenye Mlima wa Sherman, yote yakiwa ya watu matajiri na wenye nguvu huko Nairobi bila kujali ukubwa wao.

Lisa aliona majengo mengi ya kifahari njiani. Moja ya jumba kubwa zaidi lililokuwa katikati ya mlima lilisimama kutoka kwa wengine
Joel alipoona kwamba alikuwa akiitazama nyumba hiyo kwa udadisi, alimjulisha. "Hekalu hilo ni la familia ya Kimaro."

Familia ya Kimaro…Moyo wa Lisa ulirukaruka. Hapo awali, alifikiria kwamba asingeweza kuwasiliana na Alvin tena. Hakutarajia kwamba siku moja angeishi karibu sana na nyumba ya familia ya Kimaro. Je, Alvin alikuwa akiishi huko pia? Utambulisho wake ulikuwa ni nani katika familia ya Kimaro? Je, wangekutana tena? Lakini, aliacha kufikiria juu yake kwani yote yalikuwa yamepita.

Joel na Lisa walifika kwenye jumba la kifahari la Joel Ngosha. Mara tu gari lilipoegeshwa, mwanamke mrembo na mwenye utulivu akatoka.

“Umerudi, mume. Lazima atakuwa Lisa. Sikujua kwamba angekuwa mrembo sana.”

“Huyu ni Aunty Nina,” Joel alisema kwa upole.

“Habari, Aunty Nina.” Tabia ya Nina ilimshangaza Lisa. Alikuwa na hisia kwamba Nina angemkaribisha kwa uso jeuri. Hata hivyo, hakuamini kwamba mwanamke yule angemtendea kwa dhati mtoto wa nje wa mumewe. Mwanamke huyo lazima angekuwa mgumu kukabiliana naye.

"Ah, una heshima gani." Nina alitabasamu. Aligeuza kichwa chake na kukimbilia ndani ya jumba ghafla. Kisha akapiga kelele,
“Acha kuchati, Melanie. Njoo ukutane na dada yako."

"Mama, hata hukuzaa binti kabla sijazaliwa."

Binti huyo mdogo ambaye alikuwa karibu umri sawa na Lisa alitoka nje ya jumba. Uso wake ulikuwa na umbo la embe dodo huku mashavu yakivimba kidogo kama mimba ya paka. Ngozi yake ilionekana kuwa nzuri ya kung’aa, ikiwa kati ya weupe na weusi wa kiafrika. Melanie Ngosha alipokutana na Lisa, alionekana kutokuwa na furaha mara tu baada ya kumtazama Lisa vizuri.

Lisa alijua Melanie alikuwa anatoka wapi. Alifanana na Joel, wakati Melanie alikuwa na mfanano mkubwa naye. Katika kesi hiyo, wote wawili walionekana sawa kabisa. Hata hivyo, midomo na meno ya Melanie hayakuwa mazuri kama ya Lisa. Meno yake yalikuwa yameungua kama kashata, sawa na mabinti wengi wa Arusha.

Basi, mwanadada tajiri ambaye amekuwa na tabia ya kiburi tangu utotoni angewezaje kumkubali binti mwingine aliyefanana naye lakini hata mrembo kuliko yeye? Melanie alisema kwa mzaha, “Hata hafanani na Baba. Unawezaje kusema ni binti yako?”

“Vipi hatufanani? Ikiwa hujui la kusema, funga tu mdomo wako. Kuanzia sasa, yeye ndiye binti wa kwanza wa familia ya Ngosha. Wewe ni binti wa pili,” Joel aliamuru kwa sura ya kiume.

"Baba, mimi ndiye binti wa kwanza." Melanie alikasirika na kukanyaga miguu yake kwa kutoridhika.

'Ni sawa, baba. Ikiwa mimi ndiye binti wa kwanza au la, haijalishi. Sisi ni binti zako hata hivyo,” Lisa aligeuza kichwa chake na kumwambia Joel, “Ninaelewa jinsi Melanie anavyohisi. Kama ningekuwa katika viatu vyake, nisingejisikia vizuri pia.”

“Huo ni uelewa wako wa kipekee sana.” Hali ya utulivu ilivuka uso wa Joel.

Sura ya 148

Baada ya kuona Melanie amekasirika, Lisa aliona ni bora kutumia njia ya chinichini. Hakutarajia kwamba siku moja angeweza kutumia mbinu za kinafiki kama za Lina. Hata hivyo, unafiki ulikuwa mkakati madhubuti.

“Baba, pamoja na kwamba umenileta nyumbani, huwezi kuwa upande wangu kila wakati na kunisifu tu kwa sababu unanionea huruma. Itamkasirisha Melanie na kuharibu udada wetu pamoja na amani ya familia. Ingawa nimeamua kurudi nyumbani, sitaki kuathiri familia yako.”

Joel aliguswa sana. Ikilinganishwa na Melanie mcheshi na mwenye majivuno ambaye alimlea, Lisa alielewa zaidi. “Njoo nikuonyeshe chumba chako. Usisite kunijulisha ikiwa haujaridhika nacho.”

Alipowaona wawili hao wakiingia ndani ya nyumba hiyo, Melanie alipandwa na hasira. "Mama, mwanamke huyu ni mjanja sana!"

Nina alikunja uso kwa hasira. Alidhani kwamba ingekuwa rahisi kushughulika na Lisa kwa kuwa alikulia katika familia isiyo na uwezo. Lakini, mambo hayakuwa rahisi kama alivyofikiria. Lisa hakuwa mtu wa kuchukuliwa kirahisi, kama mama yake wakati huo.
Baada ya kusema hivyo, Nina aliamini kwamba angeweza kukabiliana na Lisa kwa vile aliweza pia kumshinda mama yake wakati huo.

“Sio tatizo. We tulia. Kwa kuwa nimekutana na kila aina ya watu maishani mwangu, hatanipa shida.” Nina alimshika Melanie. "Umejiandaaje kwa karamu iliyoandaliwa na familia ya Kimaro usiku wa leo?"

Wakati wa kutajwa kwa tukio hilo, macho ya Melanie yaling'aa kwa msisimko. “Nimechukua gauni la waridi pamoja na mkufu. Pia nimemwajiri Kayya kunipaka vipodozi. Usiku wa leo, hakika nitakuwa msichana mrembo zaidi kwenye ukumbi na Bwana Kimaro, bila shaka atavutiwa sana na mimi.”

Nina aliitikia kwa kichwa kwa kuridhika. "Kutokana na nilivyosikia, Bibi Kimaro alisema kuwa karamu hiyo inafanyika usiku wa leo kwani hakujawa na shughuli nyingi katika jumba hilo. Kwa hakika, anajaribu kumtafutia Bwana Kimaro mwenzi wa ndoa. Wanawake wote ambao hawajaolewa ambao amewaalika wanatoka katika familia zenye ushawishi hapa jijini. Nilisikia kwamba Bwana Kimaro alienda likizo huko Tanzania mapema mwaka jana na hatimaye akarudi mwishoni mwa mwaka. Huko Tanzania hakupata mke wa kuoa. Bibi Kimaro alisema lazima aoe mwaka huu.”

“Mama, nampenda Bwana Kimaro,” Melanie alisema kwa haya, “Yeye ndiye mwanamume mzuri zaidi ambaye nimewahi kumuona. Hakuna anayeweza kumzidi.”

“Kazana sasa. Nina imani na wewe. Ukiingia kwenye familia ya Kimaro, Lisa atachukuliwa kuwa si chochote.” Sura ya dharau ilimjia Nina usoni.

Jioni, Lisa aliendelea kuongea na Joel pale sebuleni. Ghafla Joel alimwona Melanie akishuka akiwa amevalia gauni la pinki. Alikunja uso na kuuliza, "Unaenda wapi?"

“Atahudhuria sherehe aliyoalikwa na rafiki,” Nina alijibu kwa upole.

“Usichelewe sana kurudi.” Joel hakutoa maoni zaidi.

Hata hivyo, Lisa aliona sura ya Melanie yenye furaha usoni mwake na pia furaha iliyokuwa machoni mwa Nina. Alihisi kwamba kulikuwa na jambo la kutia moyo lililokuwa likiendelea kwao.

Usiku. Karamu kuu ilikuwa ikifanywa katika nyumba ya familia ya Kimaro. Vijana wazuri na mabinti warembo walikuwa wamevalia nakupendeza kupita kiasi na kucheza kwenye sakafu ya dansi.

Usiku huo, familia maarufu na tajiri zaidi huko Nairobi zilikusanyika hapo. Kila mmoja wa wasichana matajiri alikuwa akienda kuonyesha kipaji chake usiku huo. Kila mtu alijua kwamba ilikuwa hafla ya juu juu, lakini ilikuwa na nia ya msingi ya kumtafuta mwanamke ambaye angekuwa mwenzi wa ndoa wa Bwana Kimaro.

Yeyote aliyemwangukia angeanza njia rahisi ya mafanikio. Cha kusikitisha ni kwamba Bwana Kimaro mwenye sura nzuri kabisa hakuwa amefika hadi wakati huo.

Katika chumba cha maktaba kilicho kwenye ghorofa ya tatu. Alvin alishika sigara kwa mkono wake huku akiipekua hati fulani kwa mkono mwingine. Mwanga mkali juu ya dawati uliangaza uso wake mzuri, ambao ulifunua uso wa huzuni. Ni kana kwamba zogo zote zilizoendela huko chini hazikuwa na uhusiano wowote naye.

Mlango ulisukumwa kwa kishindo. Bibi Kimaro aliingia na kusema kwa uchungu, “Umejificha humu ndani! Ninakufanyia hafla hii makusudi ili uweze kumchagua mke wako mtarajiwa, lakini hapa umejificha kimya kimya. Huna mpango wa kupata mke?"

"Hapana," Alvin alijibu bila kujali.

Bibi Kimaro alizidiwa na hasira. “Lazima utoke nje sasa hata kama hujisikii kufanya hivyo. Kwa kuwa wewe ni mjukuu mkubwa katika ukoo wa moja kwa moja wa familia ya Kimaro, lazima uoe. Sarah tayari amekufa. Utaacha lini kuahirisha hili?"

Alvin aliyekuwa akiipekua ile hati kwa vidole vyake vyembamba akanyamaza kwa muda.
Bibi Kimaro aliichana ile hati na kuitupilia mbali. “Unaweza kufanya kazi wakati wowote lakini si leo. Nenda ukamchague mwanamke usiku wa leo, la sivyo nitapiga kichwa changu mbele yako hadi nife.”

“Bibi…” Alvin alipapasa paji la uso wake. Hii ndiyo sababu hasa hakutaka kurudi. Kama mwanamume ambaye angetimiza miaka 30 hivi karibuni, alikuwa akilazimishwa kwenda kuchagua wanawake ambao hata hakuwafahamu. Hapo awali, alimuoa Lisa kwa makusudi ili kukabiliana na hali kama hiyo kwa wakati huo. Hata hivyo mpango wake ulikwenda kombo.

Kwa mawazo ya bibi huyo, macho ya Alvin yalitiwa giza. Kwa kuwa ilibidi aoe mapema au baadaye, ilionekana kwamba kuoa mapema au baadaye hakungeleta tofauti. Labda amsikilize bibi yake ili ajisikie raha zaidi.

“Sawa.” Aliinuka na kutoka nje na Bibi Kimaro.

Kwa furaha kubwa, Bibi Kimaro alimpeleka kwenye ghorofa ya pili ili kuwatazama mabinti waliokuwa chini. Hali ilikuwa sawa na jinsi mfalme alivyomchagua mke wake zamani za kale. "Angalia mabinti walio hapa chini na uchague anayekuvutia."

Muda huo macho ya Alvin yalipita juu yao, kichwa kilimuuma. mabinti wote walikuwa wamepambwa sana, na labda walionekana tofauti na nyuso zao zilizo wazi mara tu mapambo yao yalipoondolewa. Badala yake, uso wa Lisa ulikuwa safi kila wakati na mzuri hata na vipodozi nyepesi. Macho yake ghafla yakahamia kwenye uso wa binti mmoja. Alvin aliganda.

Bibi Kimaro akahamishia macho yake kwa binti aliyekuwa akimwangalia na kutabasamu. "Yeye ni Melanie Ngosha, binti wa familia ya Ngosha. Baba yake ni Joel Ngosha na mama yake ni Nina kutoka familia ya Mahewa. Anatoka katika malezi tajiri pia. Kuhusu sura yake, anachukuliwa kuwa mmoja wa mabinti wenye sura nzuri kati ya wengine hapa usiku wa leo.”

Alvin alikaa kimya kwa muda. Uso wa binti huyo ulimkumbusha yule mwanamke aliyekuwa mbali huko Dar es Salaam. Kwa kweli, alimchukia sana alipomwacha. Hata hivyo, alipomwona yule binti aliyefanana naye, hakuweza kujizuia kumfikiria Lisa. Alimroga kwa mtishamba gani?

“Kwa hiyo… yeye ndiye?” Bibi Kimaro aliuliza kwa mshangao.

“…Aha, basi sawa.” Alvin alipomaliza kuongea tu akashuka ngazi taratibu.


Sura ya 149

Usiku sana, akiwa amesimama kwenye kibaraza, Lisa aliweza kuona nyumba ya familia ya Kimaro kutoka mahali alipokuwa. Usiku huo, taa zote zilimulika. Aliweza kuhisi kwamba ndani ya jumba hilo kulikuwa na shughuli nyingi. Alishangaa pale kwa muda, akashusha pumzi taratibu kisha akarejea kujilaza tena kitandani. Hata hivyo, alikuwa na shida ya kupata usingizi.

Asubuhi, Lisa alishuka chini mapema sana baada ya kukosa usingizi usiku. Mazingira ya pale sebuleni yalikuwa tofauti kabisa.
Joel alitulia tuli kwenye kochi huku Melanie akikumbatia mkono wake na kusema kwa furaha, “Baba, hujui jinsi Bwana Kimaro alinitendea kwa shauku jana usiku. Miongoni mwa mabinti wote, alivutiwa na mimi kwa mtazamo wa kwanza na hata akanialika nicheze naye. Bibi Kimaro pia alikuwa na mazungumzo ya muda mrefu nami, akiniomba niwe mpenzi wake.”

Nina alitabasamu kutoka sikio hadi sikio. "Mungu ndiye mtoaji wa bahati nzuri. Nilijua Melanie angeweza kumpata mpenzi sahihi kwa uzuri na kipaji chake, lakini sikutarajia angeweza kuolewa na Bwana Kimaro. Familia ya Kimaro ni miongoni mwa familia tajiri zaidi hapa Nairobi. Mali zote za familia ya Kimaro zitakuwa zako katika siku zijazo.”

"Usisahau kuna Jack Kimaro pia katika familia." Akiwa amekunja uso, Joel aliwakumbusha Nina na Melanie baada ya kusikia maneno yao ya tamaa.

"Kwa hiyo?” Nina aliuliza kwa nyodo. “Ingawa kila mtu anajua kwamba Bwana Kimaro ameondoka KIM International wakati fulani, Jack hana uwezo wa kusimamia kampuni vizuri.”

Melanie alisema kwa kiburi, “Hata kama Bwana Kimaro hatapata kuchukua uongozi wa KIM International, utambulisho wake kama kaka mkubwa wa familia bado ni bora. Hakuna mtu mwingine ambaye ningependa kuolewa naye maishani mwangu isipokuwa yeye.”

Nina alijawa na tabasamu. "Wote wawili mlipendana mara ya kwanza na mmeundwa kwa ajili ya kila mmoja."

Joel alifichua chembe ya kero. "Kwa hivyo ulihudhuria hafla ya familia ya Kimaro kwa ajili hiyo. Kwanini mlinificha? Mliogopa kwamba ningemwomba Lisa ajiunge pia, huh? Kwanini mna mawazo mabaya kama hayo?"

Melanie alipiga kelele. “Kuna maana gani ya kumtaka ajiunge nayo? Kwa kuzingatia kwamba hajawahi kuona tukio kubwa kama hilo, nilikuwa na wasiwasi kwamba angeiletea aibu familia yetu. Zaidi ya hayo, si tayari ana mchumba? Ikiwa atakutana na watu wengi matajiri hapa Nairobi, anaweza kuamua kumwacha mchumba wake ambaye ni masikini kama yeye mwenyewe.”

“Wewe…” Joel alikasirika sana hadi akapiga meza na kusimama. Hata hivyo, dakika tu alipomwona Lisa akiwa amesimama kwenye ngazi, aliganda ghafla. “Lisa…”

“Lo, Lisa, usimchukie Melanie.” Nina alivaa tabasamu. “Kwa kweli, Melanie alikuwa na wasiwasi kwamba hujazoea kuhudhuria karamu kama hizo, ikizingatiwa kwamba wewe bado ni mgeni hapa. Zaidi ya hayo, hafla za familia ya Kimaro huwa za ajabu kila wakati.”

Lisa aliinua macho yake kwa siri. Mama yake wa kambo alikuwa mbunifu sana katika kutamka maneno yake. Mwisho wa siku, walitaka tu kumdhihaki kwa sababu eti hajatembelea sehemu kubwa ya ulimwengu. Hawakujua kwamba Lisa alikuwa ametembea sana na hata kusoma Chuo Kikuu Marekani. Na huyo Alvin Kimaro waliyekuwa wakimshobokea kwake alikuwa zilipendwa!

“Haijalishi. Kuweza kuwa binti wa familia ya Ngosha ni heshima kwangu. Sina nia ya kujipandisha hadhi kwa kudandia wanaume matajiri hata kidogo.” Lisa alitoa tabasamu hafifu na la upole.

Nina na Melanie walipigwa na butwaa. Je, Lisa alikuwa akijaribu kuwakejeli kwa kuwa na pupa ya kutamani familia za hadhi ya juu licha ya asili yao yenye nguvu tayari? Hakika Joel alionekana kukasirika zaidi huku akiwatazama Nina na Melanie.

Nina alisema, “Hubby, ninafanya hivi kwa ajili yako. Ikiwa binti yetu anaweza kuolewa na Bwana Kimaro, hali yako itakuwa tofauti.”

"Baba, mimi sasa ni rafiki wa kike wa Bwana Kimaro," Melanie akaongeza kwa kufoka, "Bwana Kimaro alisema atakuja usiku wa leo kula chakula cha jioni."

"Nini? Bwana Kimaro anakuja?" Nina alitetemeka kwa fadhaa. “Hubby, umesikia hivyo? Inaonekana Melanie ataolewa na Bwana Kimaro hivi karibuni."

Joel pia alishangaa sana. Hata hivyo, ikiwa Bwana Kimaro alikuwa anakuja kweli, ilimbidi amtendee kwa uangalifu. "Sawa, nitamwomba mtumishi wa jikoni aandae chakula kizuri zaidi na divai nzuri usiku wa leo."

Akiwa na furaha kupita kiasi, Melanie alisema upesi, “Baba, nadhani nina kabati ndogo. Nahitaji kuvaa vizuri kwani Bwana Kimaro anakuja usiku wa leo!”

"Sawa, nenda kachukue nguo na mama yako." Joel akatupa kadi. “Usiendelee kumnunulia Melanie nguo pekee. Lisa amekuja na ana nguo chache sana, kwa hivyo mpe seti 20 hadi 30 za nguo pia. Agiza maduka yakuletee hapa mara moja."

Tabasamu za Nina na binti yake zikawa ngumu. Melanie alipokuwa karibu kudhihirisha kufadhaika kwake, Nina alimkazia macho. Baada ya hapo, wawili hao walienda kufanya manunuzi.

Joel alihema huku akiwatazama wakiondoka. “Lisa, natumai huna shida. Dada yako ni mpenda mali na amedekezwa sana na mama yake.”

“Baba, ni sawa. Usijali.” Lisa akatikisa kichwa kwa tabasamu mwanana. Macho yake meusi yalikuwa angavu na ya kupendeza. Hakuwa amepaka kitu chochote usoni mwake, na alionekana aking’aa kama theluji.

Joel alipigwa na butwaa kidogo. Moyoni alimuonea huruma. Kwa mrembo kama Lisa, kwa kweli alikuwa anamfaa kabisa Bwana Kimaro. Kwa bahati mbaya, hatima ilikuwa ya kikatili. Alitamani angemleta nyumbani mapema.

"Twende, nitakupeleka kwenye ofisi za Ngosha Corporation kwa ziara fupi."

Lisa hakupendezwa na Ngosha Corporation. Hata hivyo, alitembelea ofisi hiyo kwa kuwa hakuweza kukataa ombi la fadhili la baba yake. Alirudi tu kutoka ofisini na baba yake saa moja jioni. Taa zilizokuwa zimewashwa katika nyumba ya Ngosha zilimulika sana. Mimea na maua mengi ya bei ghali pia yaliongezwa kwenye ua uliokuwa umesafishwa vizuri.

Walipoingia ndani ya nyumba hiyo, Nina alikuwa akiwaamuru watumishi wafanye usafi katika eneo jirani. Melanie alikuwa amebadilika na kuvaa vazi la juu la sufu ambalo lilikuwa la gharama kubwa zaidi msimu huo. Alivaa sketi ambayo ilikuwa imeunganishwa na jozi ya tight. Pia kulikuwa na kitambaa cha manyoya kikiwa kimezungushiwa mabegani mwake. Alitengeneza nywele zake ndefu kimakusudi pia. Sehemu ya mbele ya nywele zake ilikuwa imejikunja na nyuma yake ilikuwa imesukwa. Alionekana kama binti wa kifalme.

“Hubby, nilisikia umempeleka Lisa ofisini leo, sivyo?” Nina alimsogelea Joel na kumuuliza huku akijua kila kitu.

“Kuna ubaya wowote kumpeleka binti yangu ofisini?” Joel alikunja uso.

"Bila shaka hapana." Huku akizuia chuki yake ndani kabisa, Nina alisema huku akitabasamu, “Lisa, nimekununulia nguo nyingi za chapa maarufu leo. Nguo hizi pengine hazipatikani Dar es Salaam. Nenda ukajaribu nguo sasa. Huwezi kuvaa vibaya wakati Bwana Kimaro atakapokuja baadaye.”

Lisa alipopanda ghorofani na kufungua kabati lake, alitabasamu baada ya kuona nguo zile mle ndani. Hakika zote zilikuwa nguo zenye chapa maarufu, lakini, zote zilikuwa aimepitwa wakati miaka kadhaa iliyopita na hazikuweza kuuzika kwa sababu ya rangi zake za kizamani. Ikiwa angekutana na kina Janet huko Dar es Salaam akiwa amevaa mojawapo ya nguo hizo, bila shaka angechekwa hadi azimie. Lakini, haikuwa muhimu kwake kwani alijiamini juu ya uzuri wake.

Dakika 20 baadaye, alishuka ngazi. Nina na Melanie, ambao walikuwa wakimtarajia aonekane wa kizamani katika mavazi yale, walipigwa na butwaa mara moja. Lisa alivaa koti refu la kijivu ambalo Nina alinunua. Jacket ilikuwa kubwa sana ilionekana kama blanketi juu yake. Bila shaka, mtu yeyote wa kawaida aliyevaa koti hilo angeonekana kuwa kituko, lakini, Lisa hakufunga zipu ya koti hilo, akaliacha wazi. Aliiunganisha na kitop cheupe cha rangi ya cream na suruali nyeupe ya kawaida. Hakuwa amepaka chochote usoni mwake, isipokuwa ndomoni aliweka lipstick nyekundu. Alionekana kama binti safi na mrembo mwenye umri wa miaka 17 au 18. Ikilinganishwa na Lisa kando yake, Melanie alionekana mwenye urembo mwingi zaidi na uso uliopambwa sana hadi ukapitiliza.

Lisa kwa makusudi alisema huku akitabasamu, “Asante kwa nguo, Aunty Nina. Zinanipa joto sana na hili baridi la Nairobi. Nimezipenda sana.”

"Nimefurahi kwa kuwa umezipenda." Nina alikuwa akihema kwa hasira. Wakati huo, aligundua kuwa Joel alikuwa akimwangalia sana.

Ijapokuwa Joel hakuwa mzoefu wa nguo, aliona wazi nia ya mkewe. Kwa bahati nzuri, Lisa alikuwa na mwili wa kuvutia na mwonekano bora zaidi, kwa hivyo angeonekana mzuri katika nguo yoyote.

Wakati huo, mtumishi aliingia na kusema, “Bwana Kimaro yuko hapa.”

Wale wanne wakatoka mara moja kwenda kumpokea. Gari aina ya Rolls-Royce lilisonga taratibu kuelekea kwenye jumba la kifahari. Baada ya gari kusimama, dereva alitoka na kufungua mlango wa nyuma. Mtu mtukufu, mashuhuri alitoka nje. Alivaa koti la kijivu na suti ya kijivu. Kwa kuzingatia mavazi yake, ilikuwa ni lazima kabisa kuzingatia sura ya mtu huyo. Kwa kushangaza, mavazi hayo yalimfaa vizuri. Miguu yake mirefu ilifanana na ya mwanamitindo wa hali ya juu, ilhali uso wake ulikuwa mzuri sana hivi kwamba hakuweza kupatikana hata kasoro ndogo.

Kipindi Lisa alipomtazama vizuri mtu huyo usoni, kichwa cha Lisa kilianza kuunguruma bila kukoma. Inawezaje kuwa yeye?!
Alijua kwamba Willie alikuwa anamuogopa Alvin, hivyo aliamini kabisa kwamba Alvin alikuwa na hadhi ya juu kabisa katika familia ya Kimaro. Hata hivyo, asingeweza kamwe kutarajia kwamba alikuwa akitetemekewa kiasi kile na familia tajiri za kitongoji kile maarufu, mtu tajiri zaidi katika eneo lote lile lililokaliwa na matajiri wa Kitanzania waliowekeza nchini Kenya, na pengine kitongoji tajiri kuliko vyote jijini Nairobi!

Pamela alikuwa amemuelekezea kwa bahati mbaya wakati huo, na kumfanya ahusishwe na mtu maarufu kama huyo. Sasa ujio wake pale ulimaanisha kwamba alikuwa mpenzi wa Melanie. Alikuwa na uwezekano mkubwa wa kuwa shemeji yake katika siku zijazo.

Sura ya 150

Uso wa Lisa ulibadilika polepole. Alipata hisia kali kwenye kifua chake, ambayo ilimsababishia maumivu. Ikiwezekana, alitamani asingemwona tena maishani mwake.

“Umefika Bwana Kimaro!” Melanie alimsogelea Alvin kwa unyonge na kumshika mkono wake kana kwamba walikuwa wanandoa kwenye mvuto wa kwanza wa mapenzi.

“Ndiyo.” Alvin alikunja uso kwa namna isiyoonekana, akijiuliza ni nini kinamsibu binti huyo. Walikuwa wamecheza pamoja tu jana yake usiku, lakini alijifanya kuwa karibu kwake kana kwamba walikuwa kwenye uhusiano kwa muda mrefu. Wakati tu alipokaribia kuachana naye, Joel na Nina walimkaribia.

"Habari, Bwana Kimaro." Joel alimpa mkono Alvin taratibu.

“Habari, Mr. Joel. Ni mara yangu ya kwanza kukutembelea. Pole kwa kukusumbua." Iilipokuja suala la kutangamana na Joel, Alvin alimtendea kwa adabu na heshima.

"Bila shaka, hakuna tatizo. Ni heshima yetu kuwa na wewe hapa,” Nina alijibu kwa pupa huku akiwa amejawa na tabasamu.

Joel alimtazama mkewe akiwa hoi. Kisha, akasema kwa upole, “Ingia ndani ukaketi. Nje kuna baridi.” Joel na Nina walimtengenezea njia.

Kabla Lisa hajasogea, Alvin alifika kwake na macho yao yakagongana. Mara ya pili alipokutana na macho yake, haraka akatazama pembeni. Alikuwa na wasiwasi kwamba kadiri alivyomtazama kwa muda mrefu, ndivyo angehisi maumivu zaidi. Zaidi ya hayo, akili yake ilikuwa katika hali ya mkanganyiko muda huo.

Macho meusi ya Alvin yalimkazia mara baada ya kumwona. Hapo hapo, hisia kali zilimtawala kutoka chini kabisa, lakini, alificha vizuri sana hivi kwamba hakuna mtu aliyetambua. Kila mtu alimuona tu akimtazama Lisa kwa makini huku akiwa ameganda palepale.

Alipoona hivyo, Melanie aliingiwa na wivu ndani kabisa. Mara moja alishika mkono wa Alvin na kusema kwa sauti, “Bwana Kimaro, unatazama nini? Huyu ni binti wa nje wa baba yangu ambaye amefika hapa jana tu, lakini hatushiriki mama mmoja.” Maneno yake yalikuwa mazito ya dharau.

Alvin alielewa kila kitu sasa. Kwa muda mrefu alikuwa akijua kuwa Lisa ni binti wa Sheryl, lakini hakutarajia kuwa Joel ndiye mwanaume ambaye Sheryl alikutana naye hapo awali. Alifikiri kwamba asingemwona Lisa tena. Bila kutarajia alikuwa ametokea mbele yake tena wakati huo. Alikuwa hata binti wa familia mashuhuri ya Ngosha.

Hatimaye Alvin alipata utulivu, lakini akapata hisia nyingine nyingi. Wakati huu, alijawa na uchungu.

"Bwana Kimaro, huyu ni binti yangu mkubwa, Lisa." Joel alimtambulisha Lisa kwake huku akionekana kutoridhika na utambulisho ambao Melanie alitoa.

“Oh, binti yako mkubwa? Si binti yako tu wa haramu?” Kauli ya kikatili ilitoka kwenye midomo mizuri ya Alvin.

Lisa alikodoa macho. Hakutarajia kwamba Alvin angekubaliana na maelezo ambayo Melanie alisema. Kauli hiyo ilionekana kumpeleka kwenye dimbwi la kukata tamaa. Hakika, hii ndiyo ilikuwa asili ya kweli ya Alvin. Alikuwa mkatili na mwenye dharau. Nina na Melanie walishangilia kwa furaha. Hawakuwa wametarajia Alvin kuchukua upande wao.

Joel alikuwa na shida kidogo. Alvin alimtupia jicho kisha akasema kwa upole, “Kuwa na mtoto wa nje kumezingatiwa kuwa ni jambo lisilofaa katika familia ya Kimaro. Ulikuwa mzembe sana, Mr. Joel."

Joel aliipokea kauli ya Alvin kwa machungu, lakini hakuwa na ujasiri wa kujibu. Baada ya yote, familia ya Kimaro ilikuwa na hadhi ya juu sana, hivyo hakuweza kudiriki kumkosea Alvin vinginevyo angeharibu biashara zake.

Akishindwa kuvumilia tabia yake, Lisa alimwendea Alvin na kumwangalia machoni kwa namna isiyo ya jeuri wala kujidharau. "Hata kama Baba yangu alikuwa mzembe au la, haina uhusiano wowote na wewe. Baada ya yote, yeye ndiye mwenyeji wako, unatakiwa uwe na heshima kwake."

Macho ya Alvin yaligeuka kuwa mabaya, na Nina akamwambia Lisa kwa ukali. “We mwanaharamu, unawezaje kuthubutu kuongea na Bwana Kimaro kwa njia hii? Omba msamaha haraka.”

“Hasa. Bwana Kimaro alitushauri tu kwa wema. Wewe ni mkorofi sana.” Kwa hayo, Melanie aliinua kichwa chake na kumwambia Alvin, “Usikasirike, Bwana Kimaro. Lisa alikulia katika familia isiyo na uwezo na hajaona sehemu kubwa ya ulimwengu.”

Alvin alikunja midomo yake mizuri na kutoa tabasamu dogo. “Inaonekana sijakaribishwa hapa. basi nitaondoka tu…”
Dakika alipogeuka, kila mtu alianza kuingiwa na hofu. Melanie alishika mkono wake kwa nguvu na kunguruma. "Baba, mwambie Lisa aombe msamaha sasa!"
Joel alikunja ngumi. Ikiwa Alvin angetoka nje ya nyumba ya familia yake muda mfupi baada ya kuingia, watu wote wenye nguvu huko Nairobi wangejua kwamba alikuwa amewaudhi familia ya Kimaro. Katika hali hiyo, familia ya Ngosha ingetengwa huko Nairobi. “Lisa, omba msamaha."
Alipomaliza tu sentensi hiyo, alitoa tabasamu la uchungu na kuhema. Lisa akiwa ameduwaa akakunja ngumi. Hakuwahi kuchukizwa sana na sura nzuri ya Alvin hapo awali. Alishusha pumzi nzito na ndefu na kusema. “Samahani, Bwana Kimaro. Sijaona mengi ya ulimwengu na sijui jinsi ya kuishi kwa heshima katika jiji. Ninatoka mashambani, kwa hivyo natumai hautakwazika na mapungufu yangu.”
Kutoka mashambani? Alvin alicheka.
"Ingia, Bwana Kimaro." Joel alibadili mada huku akitumai Alvin angesahau tukio lile.
Alvin alipoingia ndani ya nyumba hiyo, Melanie bado alikuwa amemshikilia mkono. Hapo awali alipanga kujinasua kutoka mikononi mwake, lakini alipambana na tamaa hiyo baada ya kuona sura ya Lisa iliyochanganyikiwa. Baada ya kukaa kwenye kochi, Melanie alienda mpaka kumuegemea begani.
Lisa alisikitishwa na tukio hilo. Sehemu hiyo ilikuwa ya kipekee kwake, lakini sasa ilikuwa ya mtu mwingine. Je, mwanamume huyo alikuwa akimpenda kweli wakati huo? Angewezaje kubadilika hivyo?
“Mungu wangu, mbona umeleta zawadi nyingi za gharama? Uwepo wako unatosha, Bwana Kimaro. ” Nina alipiga kelele ghafla na kutazama mbele. Alimwona dereva wa familia ya Kimaro akibeba zawadi nyingi kuingiza ndani ya nyumba, ambazo zote zilikuwa adimu na za gharama kubwa.
Alvin akageuza kichwa chake karibu na kushangaa ghafla. Alijua uikuwa ni mpango wa Bibi Kimaro. Alitaka kumfanya aonekane kana kwamba alikuwa akitoa zawadi za harusi kwa familia ya Ngosha. Alikaa kimya kwa muda kabla ya ghafla kusema kwa tabasamu, “Ni wajibu wangu. Kwani, umemlea binti mzuri kama Melanie.”

“Bwana Kimaro…” Melanie aliguswa sana hivi kwamba macho yake yakawa mekundu. Alihisi kusukumwa, aliukandamiza mwili wake kwa nguvu kifuani mwa Alvin. Mwili wa Alvin ukawa mgumu. Hakuwa na la kusema. Je, mabinti wa familia ya Ngosha walikuwa wazi na wasio na aibu? Ilikuwa Lisa zamani na Melanie baadaye. Lisa alitazama pembeni. Hakutaka kulifikiria wala kulitazama.
“Baba, mimi ni binti wa nje ya ndoa. Nitapanda ghorofani kwani uwepo wangu humfanya Bwana Kimaro kukosa furaha.” Aligeuka na kumtaarifu Joel.
Joel alielewa kuwa ilikuwa inamkera kukaa pale. Alipokaribia kuitikia kwa kichwa, ghafla Alvin alizungumza kwa sauti ya kejeli, “Nadhani unahisi kutaka kuondoka kwa sababu huna furaha kwamba nilikulazimisha kuomba msamaha.”
“Hapana…” Lisa alifadhaika. Sasa kwa kuwa wawili hao walikuwa wameachana, kwanini alilazimika kumsemesha?
Alvin alikoroma. Baada ya hapo, aliashiria sahani ya matunda na karanga kwenye meza kwa kutumia kidevu chake. “Kwa kuwa unatoka mashambani, nina hakika unajua kazi za hali ya chini. Nenda kanimenyee matunda na karanga uniletee kwenye sahani. Melanie nami tungependa kula.”
Moyo wa Melanie ulijawa na furaha. Hakufikiri kwamba Bwana Kimaro angemjali sana. Alikuwa akimtesa Lisa kwa niaba yake, akijua kwamba anamchukia Lisa. “Lete matunda haraka. Bwana Kimaro anataka kula.”
*Sawa.” Lisa alilazimisha tabasamu. Kwa vile alitaka kumtesa, basi angemruhusu tu.
Aliinama na kuchuchumaa kuanza kumenya zabibu. Baada ya hapo, alianza kumenya karanga. Hakuwa amezowe na ilisababisha vidole vyake kuuma. Alipomenya za kutosha, aliweka kwenye sahani na kwenda kuwatengea wale wapendanao!
Kwa upande wa Melanie alimuegemea Alvin na kumlisha matunda na karanga ambazo Lisa alikuwa ametoka kumenya na kuwatengea. Lisa hakujishughulisha kutazama tukio hilo kwani aliliona kuwa la kuchukiza.


Bila shaka unaendelea kufurahia mfululizo wa hadithi hii ya kusisimua.[emoji7]

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..............LISA
KURASA.........161-165

Sura ya:161

Macho ya Melanie yakaangaza. Alihisi Alvin kwa kweli alimpenda zaidi! “Asante, Bwana Kimaro. Mimi… nakupenda.”

Baada ya kusema maneno hayo matatu, aliinamisha kichwa chini kwa aibu bila kuona dalili ya dhihaka machoni pa Alvin. Upendo?
Alikuwa amekutana naye mara chache tu, lakini tayari alikuwa anazungumza juu ya mapenzi.
•••
Ofisini, Meneja wa Mawenzi Investments Bwana Freddie Ngololo aliripoti kwa Lisa kwa uso wa huzuni alipofanya naye mkutano kwa njia ya video. "Mwenyekiti Jones, ardhi ya shamba ambayo tumekuwa tukiifuatilia huko Nairobi imepewa kampuni ya Cosmos."
Lisa alipigwa na butwaa. "Si ulisema jana kwamba taratibu zote zinashughulikiwa?"
"Ndiyo, wakati nashughulikia niilisikia kwamba Bwana Kimaro ameingilia kati na kuagizwa ardhi hiyo ipewe Cosmos.” Meneja alifafanua. “Cosmos Limited ni kampuni ambayo ipo chini ya familia ya Mahewa. Nilisikia kwamba familia ya Mahewa iko pamoja na familia ya Kimaro kwa sasa.” Meneja Mkuu Ngololo alieleza kwa sauti yenye uchungu. "Tulitumia pesa nyingi katika shamba hili, lakini sasa limepotea."
Lisa alikuwa kimya na hakuzungumza kwa muda mrefu. Alijua vizuri jinsi familia ya Mahewa ilivyopatana na familia ya Kimaro. Kwa kweli hakutarajia kwamba Alvin angeisaidia familia ya Mahewa bila kusita. Alifikiri kwamba angalau angefikiria mapenzi ambayo walikuwa wameshiriki hapo awali…Hapana, hakukuwa na mapenzi hata kidogo!
"Tunaweza kubadilisha ardhi?" Lisa aliuliza.
"Makampuni mengi yanapigania kupata ardhi huko. Bado kuna ardhi, lakini ni ghali sana. Kulingana na bajeti ya kampuni, hatutaweza kupata faida yoyote.” Meneja Mkuu Ngololo alisema kwa huzuni, “Mwenyekiti Jones, labda hatuko tayari kwa sasa kujipanua huko Nairobi. Hatuna ushawishi huko Kenya, kwa hivyo ni vigumu sana kuingia kwenye mduara wa biashara huko.”
"Kama hatuwezi kupambana kupata hiyo ardhi, basi badilisha mbinu. Ninavyojua ni kwamba Mawenzi inaweza kujipanua katika nyanja nyingi tofauti. Matibabu, fedha, utalii… Mji huu una sifa ya kimataifa. Kuna fursa za kupata pesa kila mahali,” Lisa alisema kwa upole, “Ni kwa kukujipanua katika nyanja mbalimbali tu ndipo hatutaohofia ushindani katika siku zijazo.”
Meneja Mkuu Ngololo alikubaliana. “Uko sahihi. Nitaitisha kikao kujadili hili mara moja.”
Saa nne usiku, Lisa aliuburuta mwili wake uliochoka hadi ndani ya jumba la kifahari la baba yake na kumuona Melanie akiwa amejiegemeza kwenye sofa. Macho yake yalijaa dhihaka.
“Mambo yaliendaje? Vipi, baba yako alikusaidia kupata lile shamba?” Melanie alidhihaki. “Kwa neno moja tu kutoka kwangu, Bwana Kimaro akanisaidia bila masharti. Hakuna anayeweza kushindana na Bwana Kimaro.”
Lisa hakujishughulisha hata kumtilia maanani na moja kwa moja akaelekea chumbani kwake. Baada ya kuufunga mlango, aliuegemea kwa muda. Kifua chake kilimbana, na kilikuwa kikimuuma. Alvin kweli alikuwa ni mshenzi! Haijalishi kama alikuwa wakili hapo awali au kijana tajiri wa familia ya Kimaro sasa, alikuwa anaweza kumshawishi mtu yoyote kufanya anachotaka. Alimpa saluti!
Lisa alikuwa kamaliza tu kuoga na kuwa tayari kwenda kulala na mara simu yake ikaita ghafla. Ilitoka kwa nambari isiyojulikana. Alibonyeza kitufe cha kujibu na sauti ya kijeuri ikasikika. "Njoo. Chumba changu ni kichafu na kinahitaji kusafishwa.”
Lisa akashusha pumzi ndefu. Baada ya kuisikia tu sauti hiyo ilimtosha kupasuka kwa hasira. Alitaka akafanye usafi chumbani kwake katikati ya usiku, alikuwa na wazimu? Au alikuwa na ajenda gani?
“Samahani, umepiga nambari isiyo sahihi. Nadhani ni sahihi zaidi kwako kuita kampuni ya usafi wa nyumba,” Lisa alijibu kijeuri.
Alikuwa karibu kukata simu ambapo Alvin alicheka tena kwa dharau. “Hakika, nitatuma tu video hiyo nzuri ya binti wa thamani wa familia ya Ngosha akiwa amejifunga mtandio akinengua ndembendembe mbele ya kundi la wanaume. Aidha uje au uandae majibu ya kuridhisha kumpa Bwana Ngosha." Alvin kisha akakata simu.

Lisa alishika kichwa chake kwa maumivu na kumlaani yeye na mababu zake wote kabla ya kuendesha gari hadi mtaa wa Oasis ambako Alvin alikaa.
Mtaa wa Oasis ulikuwa katika eneo lenye ustawi zaidi katikati mwa jiji. Bei ya futi moja ya mraba ya ardhi inaweza kuuzwa kwa mamia ya maelfu ya dola, na Alvin alikuwa na upenu wa futi za mraba 400 katika eneo hilo.
Alifungua mlango kwa ufunguo aliopewa jana yake na Alvin na kuingia ndani, katika sebule hiyo yenye kung'aa, Alvin alikuwa amekaa kwenye sofa la ngozi huku mguu mmoja ukiwa juu ya mwingine katika mtindo wa kukunja nne, mikono yake ikiwa juu ya kisigino. Mikono na miguu yake iliyoinuliwa ilimfanya atoe haiba ya kifalme. Alitoa sauti ya uvivu lakini ya kifahari.


Bila hata kumwangalia, Lisa alienda moja kwa moja jikoni kutafuta zana za kufanyia usafi. Hata baada ya kutafuta kwa muda mrefu, hakuweza kupata japo fagio tu. Alikwenda kwenye kibaraza.
Alvin alikuwa ameketi kimya kwenye sofa kwa muda sasa, na uso wake ulikuwa ukizidi kuwa jeuri. Nini kilikuwa kikiendelea? Kwa nini hakumuuliza wala kumkaripia kwa kumpa Farres Mahewa shamba alilikuwa akilipambania mara tu alipomwona? Kwa nini hakuwa akimbembeleza ampatie yeye badala yake? Maandishi yalikuwa tofauti na vile alivyofikiria, na akainuka kwa jeuri kumfuata hadi kibarazani.
Lisa hatimaye alipata ufagio kwenye kibaraza. Alipogeuka, aligongana naye kwa nguvu na kujibamiza katika kifua chake. Pua yake iliuma kana kwamba imevunjika. "Alvin, unafanya nini?"
“Umechukua maneno yangu mdomoni.” Alvin alihisi kama amewekewa sumu na Lisa. Alikasirika zaidi wakati akimwona yeye hajakasirika.
“Si uliniambia nije nikusafishie nyumba yako? Nimechelewa sana sasa, kwa hiyo nataka tu kumaliza harakaharaka nikalale. Tafadhali nipishe nipite.” Lisa alimzunguka na kuanza kufanya usafi sebuleni kwa umakini.
Alvin alimtazama akifagia sakafu kwa makini na akatamani sana kumnyang’anya na kuutupa ule ufagio. Mwanamke mjinga huyo! Ina maana, kweli alifikiri kwamba alimuita hapo kusafisha nyumba?
"Lisa Jones, huna la kuniambia?" Alvin alijikuta akifoka bila kujua. Ikiwa angeweza kumwomba na kumbembeleza kwa uradhi wake, angefikiria kurudia ahadi yake kwa Melanie na kumrudishia shamba hilo.
Lisa alinyamaza na kutikisa kichwa. "Hapana."
Alvin alimtazama kwa muda na kuamuru kwa sauti ya kijeuri, “Nenda kasafishe bafuni kwanza kabla ya sebuleni na chumbani. Safisha sinki la kuogea na ujaze maji. Nataka kuoga.”
Lisa alijisalimisha akaweka ufagio pembeni na kupanda juu. Bafu ilikuwa kubwa, karibu mita mbili kwa upana, na lililojengwa kifahari. Sinki la kuogea lilikuwa kwa chini, angeweza tu kuchukua kitambaa na kuinama ili kulifuta kabla ya kujaza maji.
Alvin alipoingia ndani, alimuona Lisa akiwa ameimana katika hali ya kutatanisha sana. Kiuno chake kilikuwa kimejipinda juujuu na suruali yake ilikuwa imeshuka chini kidogo, ikifichua sehemu kubwa ya kiuno chake chenye ngozi iliyofanana na satin huku iking'aa sana. Mgongo wote pia ulikuwa wazi.

Sura ya: 162

Macho ya Alvin yalitiwa giza, na alikuwa karibu kumfuata kwa nyuma na kumshika kiuno, lakini mara simu ya Lisa iliita na akasimama ghafla.
Lisa hakumuona Alvin akiwa amesimama nyuma yake akatoa simu yake ili kuipokea. Jina la Kelvin Mushi liliangaza kwenye skrini. Alikuwa akisitasita kujibu simu. Baada ya yote, hii ilikuwa nyumba ya Alvin, ambayo ilimfanya ahisi hatia.
Aliinyamazisha na kuamua kuipuuza, lakini mkono uliokuwa nyuma yake ghafla ukaipokonya simu yake. Lisa aliruka kwa mshtuko na kutazama nyuma. Alvin alicheza na simu yake huku akilitazama jina kwenye skrini. Tabasamu la dhihaka lilienea kwenye midomo yake. “Kwanini hutaki kujibu simu ya mchumba wako?”
"Alvin, nirudishie simu yangu!" Kwa haraka Lisa alinyoosha mkono kuikamata, lakini Alvin alikuwa ameinyanyua juu kiasi kwamba hakuweza kuifikia.
“Una wasiwasi?” Macho ya Alvin yalikuwa kama barafu huku dharau yake ikizidi kuongezeka. “Unaogopa kwamba mchumba wako atagundua kuwa uko nami usiku huu?”
“Umemaliza?” Lisa alikasirika sana sasa.
"Una mjali sana eeh?" Macho ya Alvin yalimkazia, moja kwa moja akabonyeza kitufe cha kujibu. Sauti ya joto ya Kelvin ilisikika kutoka upande mwingine.
“Lisa, unafanya nini? Imekuchukua muda mrefu kujibu simu.” Lisa aliogopa sana hivi kwamba moyo wake ulikuwa karibu kusimama. Alimtazama sana Alvin asije akaongea.
Hata hivyo, Alivin alikaa kimya na kuweka simu kwenye kipaza sauti. Kisha, akaegemea sikio lake na kusema kwa sauti ya sumaku, “Usipomjibu, basi nitamjibu.”
Lisa hakujua alichokuwa akipanga na aliweza tu kumjibu Kelvin kwa pumzi ya shwari. "Oh, nilikuwa naoga na sikusikia simu."

“Hujanipigia simu siku nzima ya leo, kwa hiyo nimekumiss kidogo,” Kelvin alisema kwa upole. “Unaendeleaje lakini?”

Hali ya hewa katika bafu ilishuka ghafla hadi kiwango cha kuganda. Lisa alimtazama Alvin kwa macho makali na nusura apige kelele kwa maumivu. Mwanaume huyo alimng'ata sikio kweli!

Aligeuka na kuutazama uso wa Alvin wenye chuki. Alikuwa akitabasamu vibaya na kumshika mikononi mwake, akiuzika uso wake shingoni mwake na kumbusu shingo yake bila ya kujali.

Kelvin aliendelea kuuliza, “Mbona huongei? Je, hukunimiss?”

"Mimi ... Pve nimekuwa na shughuli nyingi sana siku hizi chache zilizopita." Lisa alijitahidi kujizuia.

“Umechukua hilo shamba?”

"Hapana." Lisa aliuma meno huku akiachia sauti ya msisimko. Alvin alikuja mbele yake na kumbusu kwenye midomo yake. Alihamia mbali, lakini bado Alvin alimfuata na kuendelea kumsumbua.

Kelvin alisikika akiwa na huzuni. “Ni bahati mbaya kwamba sipo na wewe na siwezi kukusaidia kwa lolote.” Mdomo wa Lisa ulizibwa na Alvin hivyo hakuweza kusema lolote. Kelvin aliendelea, “Nitakuja Nairobi hivi karibuni, kisha tutakuwa pamoja, sawa?---Lisa, mbona huongei chochote?”

Lisa alibanwa kabisa na busu la Alvin na aliweza kutoa sauti laini tu. Kwa haraka akainyakua simu kutoka mkononi mwa Alvin na kusema, “Bado nina mambo ya kufanya hapa. nitakata simu sasa hivi.” Kwa haraka akabonyeza kitufe cha mwisho na kumsukuma Alvin kwa nguvu. Macho yake mazuri yalijawa na aibu na hasira.

"Alvin, umezidi sana sasa!"

“Nimezidi?” Alvin alicheka. "Je, ulikuwa na uhusiano wa karibu sana nilipokuacha naye kwa siku hizi chache eeh?"

"Hapana! Huwezi kuamini hata hivyo, haina maana.” Lisa alisema kwa kukata tamaa. “Bafu lipo tayari. Nenda kaoge!” Alimsukuma na kuondoka. Moyo wake ungesimama ikiwa angemwacha Alvin aendelee kumbusu.

“Nenda uniletee nguo za kubadilisha” Alvin aliamuru kwa jeuri nyuma yake.

“Siendi…” Kabla hajamaliza aliona tayari Alvin ameshavua shati lake huku akiudhihirisha mwili wake wenye nguvu.
Aligeuka na kumtazama kwa tabasamu baya. “Usipoenda, nitamtumia baba yako kipande hicho cha video—”

“Basi sawa, nitakwenda.” Lisa adabu ikamrudia, aliinamisha kichwa haraka na kutoka nje. Alipoelekea mlangoni, alitazama nyuma na kumwona Alvin akitupa suruali yake kando. Macho yake yalimuuma, akageukia kabati la nguo.

Baada ya kuchukua muda wake mtamu wa kumtafutia seti ya nguo za kulalia, alisogea tena bafuni na kumuona Alvin akiwa amejilaza ndani ya sinki la kuogea huku akiwa amefumba macho. Kope zake zilikuwa kama kipepeo aliyetulia, na kifua chake chenye misuli kilikuwa kimefunikwa na matone ya maji ya mpovu.

Lisa alikuwa akimshangaa huku moyo wake ukirukaruka kifuani mwake, na hakuona maji ya sabuni yaliyomwagika kutoka kwenye sinki la kuogea chini ya hatua zake mbele yake. Aliteleza, na kwa kwa bahati alikuwa karibu na sinki la kuogea, akaanguka ndani juu ya kifua cha Alvin.

Alvin alifumbua macho ghafla. Lisa aliyekuwa mikononi mwake alijitahidi sana kufurukuta ili anyanyuke, nguo zake, kuanzia tisheti suruali, na nywele zilikuwa zimelowa kabisa. Matone ya maji yaliteleza chini ya mashavu yake, na kumfanya aonekane mwenye kupendeza sana.

Macho ya Lisa yalimtoka, na uso wake ukawa na aibu huku akitoka nje kwa haraka. “Samahani, sikukusudia. nitaondoka mara moja.”

“Ninawezaje kuamini hivyo?” Alvin akamsogeza karibu na kifua chake na kumkumbatia kwa nyuma. Uso wake mzuri ulitulia begani mwake huku akihema sana. "Unataka kutumia ujanja kama huo kunifanya nikupe shamba hilo, huh?"

Kwa muda, Lisa alishangaa kwanini Alvin afikiria hivyo. “Hapana, mimi si…”

“Wewe mwanamke mwongo. Kumbuka, wewe ndiye uliyeyataka haya!” Alvin alisema na kumbusu kwa ukali.

Akiwa amekumbana na busu kali la mwanaume huyo, Lisa alijaribu kumsukuma lakini hakufanikiwa. Alijua ikiwa angeendelea hivyo, Je, angekabiliana vipi na Kelvin katika siku zijazo? Alimuuma kwa nguvu kwenye mdomo wake, akatoa damu. Alvin alifoka kwa maumivu.

Lisa alichukua nafasi hiyo kumsukuma. Uso wake ulikuwa umejaa udhaifu na unyonge. "Alvin, ukinilazimisha hivi, nitavunja kichwa changu kwenye sinki la kuogea!"

"Sawa, endelea!" Macho ya Alvin hayakuwa na huruma yoyote. "Nitapiga simu kwa Bwana Joel kesho na kumwambia kuwa binti yake alijaribu kunitongoza lakini alijiua kwa aibu kwa sababu nilimkataa."

Lisa akaguna tu kwa hasira, “mpuuzi wewe!” Macho yake yakawa mekundu kwa hasira. Kwanini matukio ya ajabu yalikuwa yanamlazimisha kuwa na mtu huyo? Kwa kweli hakutaka kuwa na uhusiano wowote naye, lakini kwanini dunia haikutaka kuwatenga? Kila alipojitahidi kumwacha lingetokea tukio ambalo lingemlazimu tu amrudie tena, kwanini iilikuwa hivyo? Kutokana na hasira kali, machozi yalimtoka.

"Alvin, nakuchukia!" Lisa alimfokea, akampiga begani bila kujizuia.
Alvin alishusha macho na kumtazama. Paji la uso wa Lisa lilikuwa limekunjamana kwa hasira, lakini hakuwa na namna. Alvin alikuwa amemzidi kwa kila kitu, nguvu, maarifa, ujanja, ilibidi tu amwangalie na kumwacha afanye anachotaka.

“Sawa, nyamaza!” Alvin aliendelea kumbusu. Baada ya zaidi ya dakika kumi, Lisa akatoka bafuni. Alvin alimtazama mgongoni akitoka huku pembe za mdomo wake zikiwa zimejikunja kwa kuridhika.

Sura ya: 163

Dakika kumi baadaye, akiwa amejifunga vazi lake na kushuka chini, alimuona Lisa akiwa amesimama kando ya mashine ya kufulia nguo.
Nguo zake zenye maji zilikuwa zikifuliwa na kukaushwa, na alikuwa amevaa shati lake kubwa lililofika hadi katikati ya mapaja juu kidogo ya magoti. Hakuwa amevaa suruali kwa sababu suruali za Alvin zilikuwa kubwa sana. Koo la Alvin lilimtoka!

"Nataka ufue na nguo zangu pia." Alvin aliamuru nyuma yake.

Kusikia sauti yake tena, sura ya kupendeza ya Lisa ilibadilika mara moja. Ingawa alijiambia atulie, bado hakuweza kumkabili kwa utulivu. "Mbona wewe ni mkorofi sana?"

Alvin alimtazama uso wake uliochukia na kusema kwa upole, “Unataka nikupige picha sasa hivi na nimtumie Kelvin Mushi, sivyo?” Uso wa Lisa ulisinyaa kabisa. Daima alikuwa na mawazo ya kumsononesha tu.

Alvin alipanda tena juu na macho yake yakiwa chini, na muda mfupi baadaye alionekana tena akiwa na nguo zake. "Nguo zangu lazima zifuliwe kwa mikono," Alvin alisema bila kujali, "Sitavaa nguo zilizofuliwa kwa mashine."

Lisa alishindwa cha kusema, “we Alvin mbona unakuwa mkorofi sana, lengo lako unione nikihangaika tu?” Alimlaani vikali moyoni na kuelekea bafuni huku akiwa amebeba nguo mikononi mwake.

Kwa kweli, Lisa hakuwa mzuri katika kufua nguo. Alifua nguo zake ndogondogo tu, kwa hivyo ilikuwa mara ya kwanza kufua nguo za wanaume.

Alvin alielekea kuendelea na kazi zake sebuleni huku akimfikiria Lisa. Moyo wake jeuri ukaangaziwa na chembe ya huruma. Usiku wa namna ile, mwanamke yule alionekana kama mke wake ambaye alikuwa akijishughulisha na maisha yake ya kila siku. Nyumba iliyopooza ilionekana kufanana na nyumba sasa!

Alvin alifikiri juu yake kabla ya kuchukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Hans. [Hakuna haja ya kuisaidia familia ya Mahewa kupata lile shamba kando ya barabara. Mpe Lisa badala yake.]

Hans, ambaye alikuwa akijiandaa kulala usiku huo, alishangaa tu kwa jinsi Alvin alivyobadilisha mawazo yake kila siku. Alimchosha sana.

Baada ya kufua nguo, Lisa alitoka na kumuona Alvin akiwa amekaa kwenye sofa. Alikuwa amevalia miwani yenye mipini ya dhahabu na alikuwa akisoma nyaraka. Meza ilikuwa imejaa makaratasi. Alikuwa anaonekana kupendeza sana wakati anafanya kazi, lakini alikuwa amevaa pajama sasa na kifua chake kilikuwa nusu wazi na kumfanya avutie zaidi.

Hata hivyo, ilikuwa karibu saa nane usiku lakini bado alikuwa akifanya kazi. Kwa jinsi alivyofanya kazi kwa bidii, inaweza kusemwa kwamba ilikuwa sahihi kutawala KIM International kwa mkono wa chuma. Alikuwa bado hajalala, kwa hivyo Lisa asingeweza kuondoka pia. Aliendelea kudeki sakafu.

Macho yakiwa yanauma na mgongo ukimuuma, sauti ya kijeuri ya mwanaume huyo ilisikika. "Nenda kanipashie joto kitanda, nataka kulala."

“Nini?” Lisa alimtazama kwa uchungu huku akijiuliza kama alimsikia vibaya.

"Blangeti lina baridi sana. Fanya haraka,” Alvin aliamuru.

"Mimi siwezi kufanya kitu kama hicho." Lisa alipata shida kukubali. “Huoni kuwa mimi ni mchafu?”

Alvin aliinuka bila kujieleza. Akatoa kichupa kidogo cha dawa kwenye kabati na kumnyunyizia. Lisa aliweza kunusa harufu ya dawa ya kuua viini, na sura yake nzuri ikabadilika kana kwamba amekanyaga kaa la moto.

“Umesafishwa na dawa sasa, basi nenda. Huna sababu ya kukataa.” Alvin akarudi kazini.

Lisa alihangaika kinyonge kwa muda na hatimaye akaingia chumba cha kulala cha Alvin. Kitanda chake na matandiko vilikuwa vizuri sana, na alikuwa amechoka sana hivi kwamba alipitiwa na usingizi chini ya nusu dakika baada ya kujilaza.

Alvin alipoweka chini zile nyaraka, alikuta tayari ilikuwa saa kumi na mbili asubuhi. Akavua miwani yake na kupanda juu. Alikutana na picha nzuri ya mwanamke mdogo aliyelala kwenye kitanda kikubwa, kama usiku uliopita. Alilala kwa kujibinua kiuno kiasi kwamba moyo wa Alvin ulimlipuka kwa mhemuko wa hatari.

Akajilaza kidogo kwenye kitanda chenye joto. Lisa alionekana kuwa na mazoea ya kuhisi harufu yake ya kawaida na akageuka na kujichimbia mikononi mwake. Alimtazama kwa macho yake laini na yaliyozidiwa usingizi.

Ilikuwa ni kishawishi kuendelea kujilaza kitandani asubuhi ile, lakini alikuwa bosi wa kampuni ya KIM International. Kulikuwa na mambo mengi katika kampuni ambayo bado alipaswa kukabiliana nayo baada tu ya kurudi kwake KIM International. Hakuwa na ujanja zaidi ya kutoka kitandani kwa upole.

Lisa aliamshwa naye. Akiwa ameduwaa, aliona anga bado halijang'aa. Alvin aliona sura yake iliyolegea na akamwambia kwa tabasamu. "Naenda kwenye kampuni. Rudi ukalale.” Kisha, alibadilisha nguo zake na kuondoka.

Lisa alitazama wakati. Ilikuwa saa kumi na mbili tu asubuhi. Alikumbuka kwamba alikuwa amelala saa nane usiku wa jana yake na kumwacha Alvin akifanya kazi. Alishangaa sana, je, siku zote alifanya kazi kwa bidii hivyo alipokuwa katika jiji la Nairobi? Haishangazi kuwa mtu tajiri namna ile. Lakini hiyo haikuwa nzuri kwa mwili wake, sivyo?

Lisa aliachana na habari zake. Hakutaka kuwa na wasiwasi juu yake, lakini hakuweza kujizuia.

Saa mbili asubuhi, Lisa aliingia ndani ya jumba la Joel huku akipiga miayo. Melanie, ambaye alikuwa akila kiamsha kinywa, mara moja alimvaa na kusema, “Baba, tazama. Nilikuambia alitoka jana usiku na hakurudi usiku kucha. Ni aina gani ya mwanamke anayediriki kukaa nje usiku kucha? Nadhani anaweza kuwa anadanga huko nje."

Lisa alimtazama na kumdharau moyoni. Ikiwa Melanie angemshughulikia mpenzi wake ipasavyo, yeye bado angehitajika kwenda huko katikati ya usiku ili kumhudumia?

“Kwanini unanikunjia sura, kwani nimesema jambo lolote baya?” Melanie aliuliza kwa dhihaka.

“Hapana, uko sahihi. Ni kwa sababu mimi si mwanamke sahihi. Wewe ndiye uliyeniita mshamba wa kijijini na binti haramu.” Lisa alitabasamu na kumpuuza. Aliketi mezani ili kupata kifungua kinywa kwa utulivu na amani.

"Baba, umesikia alichosema?" Melanie bado alimkalia kooni.

“Acheni malumbano yenu. Ninamwamini Lisa. yeye tayari ana mchumba,” Joel alimkatisha na uso wa kikauzu. “Isitoshe, si ulikuwa unatoroka nyumbani kila mara usiku pia? Una ujasiri gani wa kuzungumza juu yake?"

Melanie alishtuka kwa aibu na kukanyaga mguu wake kwa hasira. "Baba, unampendelea sana ..."

Pembeni, mara simu ya Nina ikaita. Aliitikia wito na kusimama kwa hasira. "Nini? Shamba lilikabidhiwa kwa Mawenzi… Nini kilifanyika? Si ulisema kwamba Bwana Kimaro alizungumza nao?”

Lisa aliganda na kidogo apaliwe na sandwich yake. Nina alikuwa tayari amekata simu na alikuwa akimuelekezea kidole. "Lisa Jones, umefanya nini jamani? Kwanini shamba la kando ya barabara ya Nakuru limechukuliwa na Mawenzi?"

"Hiyo haiwezi kuwa." Melanie naye alishtuka. “Inawezekana kwamba kuna mtu mwingine ambaye anathubutu kwenda kinyume na Bwana Kimaro?"

"Mjomba wako alinipigia simu na kusema kwamba jamaa wa upande mwingine wamebadilisha mawazo yao ghafla." Nina alimkazia macho Lisa na kusema, “Lisa, wewe ni msichana ambaye umefika hapa juzi tu na huna uhusiano na mtu yoyote zaidi ya baba yako. Umelala nje usiku kucha kufanya jambo lisilofaa, sivyo? Ardhi haijalishi, lakini huwezi kuiaibisha familia ya Ngosha.”

Kusikia hivyo Joel naye akakunja uso akimwangalia Lisa. Hakutaka kuamini, lakini ni kwa kuzingatia kuwa ni binti alyeweza kujiongoza mwenyewe hadi kufikia umri ule akiwa na mafanikio makubwa, wasiwasi wake ulimshuka.

Lisa aliinua uso wake kwa utulivu na kusema, “mama, unamaanisha nililala nje jana usiku ili nipate shamba? Katika hali hiyo, ulifikiri nitakuwa nimelala na nani?”

Ngosha ghafla alicheka. “Nani ana uwezo wa kwenda kinyume na Bwana Kimaro? Nafikiri badala ya kumshutumu Lisa kwa kukosa adabu, unapaswa kujiuliza ikiwa Melanie amemkosea Bwana Kimaro, au labda aliamua kutomsaidia kwa sababu hampendi.”

Lisa alipomaliza kula, akajifuta mikono na kwenda juu kubadilisha nguo zake. Joel naye alipoteza hamu ya kula na kuinuka. "Nyinyi wawili kila wakati mnasababisha shida, lazima mjiangalie vizuri." Kisha, akageuka na kuondoka.

Nina alimsogelea Melanie na kumuuliza. "Ni nini kilifanyika kwa Bwana Kimaro?"

“Hata mimi sijui. Yeye hupokea simu zangu mara chache sana.” Melanie alifikiri kwa muda kabla ya kusema, “Nitaenda kumtafuta.”

Juu, Lisa alisimama kwenye kibaraza na kutazama gari la Joel likiondoka. Alisita kwa muda kabla ya kumtumia Alvin ujumbe. [Kuhusu ardhi, ni wewe ndiye uliyevuta kamba?]

Alvin: [Ndiyo.]

Lisa: [Hausaidii tena familia ya Mahewa?]

Baada ya kuuliza, ghafla akawa na wasiwasi. Kusema kweli, hakuwa amefikiria kumsihi kabla, sembuse kufikiria kwamba asingemsaidia Melanie. Hata hivyo, kwa kuwa sasa alipata shamba hilo tena, alisisimka sana.

Dakika tano baadaye, Alvin alijibu: [Ndio.]

Lisa: [Asante.]

Alvin: [Ikiwa kweli unataka kunishukuru, unapaswa kunihudumia kila ninapokuhitaji.]

Uso mdogo wa Lisa ulihisi joto sana hivi kwamba ulikaribia kuwaka moto. Alvin alikuwa anapanga nini kwenye kichwa chake?

Alishusha pumzi ndefu na kujibu kwa kuudhika: [Hapo awali ardhi ingeangukia mikononi mwangu hadi ulipoichukua. Shukuru mungu tu sijakutukana, bwege wewe!] Kisha, akatupa simu yake na kupuuza.

Sura ya:164

Ndani ya KIM International. Katika chumba cha mikutano mapema asubuhi, Alvin aliitazama simu yake, macho yake yakiwa yamewashwa na tabasamu.

“Kwa nini bosi Mkubwa Kimaro anafurahia sana simu yake leo?” Watendaji na wafanyakazi wa KIM walishtuka walipomuona kwenye simu yake wakati wa mkutano huo. Alvin alikuwa akitabasamu sana.

Katika kiti cha kwanza kwenye safu ya kulia, macho ya Jack Kimaro yaliangaza kwa mshangao sana. Alvin katika kumbukumbu zake alikuwa jeuri na katili, lakini Alvin huyo mbele yake alionekana tofauti. Ilikuwa ni kwa sababu ya mwanamke?

Jack alitabasamu kwa wasiwasi. “Kaka unachati na Melanie? Nimesikia kwamba mnafunga ndoa hivi karibuni.”

Ufahamu uliwajia watendaji wale wa KIM. Hivyo ndivyo ilivyokuwa! Hawakutarajia kama Melanie angependelewa naye kiasi hicho. Ilionekana kana kwamba wangelazimika kumnyenyekea katika siku zijazo.

"Anzisha mkutano." Alvin aliweka simu yake chini na kuendelea kuongoza mkutano huo akiwa amenyooka usoni.

Saa moja baadaye, alirudi ofisini kwake. Hans aliingia na kusema, “Bwana Kimaro, Melanie yuko chini na anasema anataka kukutana nawe. Pengine ni kuzungumzia ardhi.”

“Niko busy. Mwambie aondoke,” Alvin aliamuru bila hata kuinua kichwa chake.

Hans alikosa la kusema. Bila shaka, asingeweza kumwambia hivyo bila kuficha. Angeweza tu kumwambia kwa busara kwamba Bwana Kimaro alikuwa na shughuli nyingi, kwa hivyo anapaswa kurudi baadaye.

Melanie, ambaye alishindwa kukutana na Alvin, alihisi kukata tamaa. Hakuwahi kufikiria kwamba angempuuza kwa urahisi hivyo.
Ina maana Alvin hakumsaidia kwa sababu hakuridhika naye? Au ni kwa sababu hakutaka achukue nafasi ya Bibi Kimaro? Hapana. Kila mtu alijua kwamba Alvin alikuwa amemchagua kucheza naye kwenye karamu. Ikiwa asingeolewa naye, angechekwa hadi kufa.

Akiwa ameshikwa na fahamu, alimpigia simu Bibi Kimaro, na ghafla akafurahishwa na habari alizokutana nazo. “Melanie, leo ni Siku ya Wanawake. Njoo pamoja na familia yako kwa chakula cha jioni. Pia ni wakati wa wazazi wa familia zote mbili kukutana rasmi. Nilitaka kutuma ujumbe sasa hivi lakini nashukuru kwa kuwa umewahi kupiga simu”

Bahati nzuri ilikuja haraka sana, na Melanie alifurahi sana. "Ndio, hakika nitakuja."

Alifikiri kuwa Alvin amekataa kumruhusu aingie kwenye kampuni hiyo kwa sababu hakumpenda, lakini hakutarajia kwamba tayari alikuwa ameshapanga familia zao kukutana. Ilionekana kana kwamba alikuwa akimuwazia kwa fikra mbovu.

Katika nyumba ya familia ya Kimaro, Bibi Kimaro alikata simu kwa kuridhika. Mzee Kimaro alitikisa gazeti lake na kukoroma. “Unafanya mipango peke yako tena. Alvin atakufundisha tena baadaye.”

"Nataka tu anipe kitukuu katika maisha haya." Bibi Kimaro alifoka. “Nikimsubiri achukue hatua, nadhani nitasubiri maishani mwangu bila kumuona akioa. Hebu angalia ni mara ngapi ametuahidi kwamba ataoa, na miaka inazidi kukatika?”

“Sio mbaya.” Mzee Kimaro hakukubali. "Alvin ni mtu mwenye upendo wa kudumu. Alipenda mara moja tu na mapenzi yake yote yamezikwa pamoja na Sarah."

“Ndiyo nakubali kuwa hajamsahau kabisa Sarah, lakini hawezi kuwa naye tena.” Bibi Kimaro alieleza kwa masikitiko. “Lakini Familia ya Ngosha pia sio mbaya." Baada ya kusema hayo, Bibi kimaro aliuru wapishi jikoni waanze maandalizi.

Kwa upande mwingine, Melanie alimwambia mama yake mara moja kuhusu mwaliko wa chakula cha jioni kwa familia ya Kimaro baada ya kurudi nyumbani.

"Inaonekana kwamba Mungu bado anatupendelea." Nina pia alifurahi sana, lakini haikuchukua muda akatulia. “Mpigie Lisa na mwambie ajiunge pia.”

Melanie alikasirika. “Mama una kichaa. Tunawezaje kumwita…” Melanie alisita kwa wasiwasi.

“Huelewi. Hii ni fursa nzuri ya kumwangamiza.” Nina alimtazama. "Tutamharibu mbele ya familia ya Kimaro na kuharibu maisha yake ya baadaye. Umesahau kuwa mimi na Valeria ni marafiki?”

Macho ya Melanie yaliangaza kwa utambuzi. “Mama nitakuunga mkono. Hatuwezi kumwacha aendelee kuwa Nairobi tena.”

Ndani ya Kampuni ya Mawenzi.
Baada ya Lisa kumaliza mkutano wake na Meneja Mkuu Ngololo alipokea simu kutoka kwa Joel akimtaarifu kuhusu mwaliko wa chakula cha jioni kwenye makazi ya familia ya Kimaro. Mara tu aliposikia kwamba familia ya Kimaro ilikuwa imewaalika familia ya Ngosha kwa chakula cha jioni, uso wake ulibadilika ghafla.

Akiwa njiani kuelekea ofisini asubuhi hiyo, Lisa alifikiri na kufikiri kuwa Alvin hakumjali wala kumpenda kabisa Melanie. Hata hivyo, mabadiliko ya matukio yalionekana kwenda kinyume na fikra zake. Familia hizo mbili zilikuwa karibu kukutana. Ina maana wangekuwa wanajadili ndoa? Lakini alikuwa akifanya nini jana usiku nyumbani kwa Alvin? Alvin alikuwa akimchukuliaje, kumchezea yeye huku akiweka mipango ya ndoa kwa Melanie?

"Lisa, umenisikia?" Joel aliuliza tena baada ya Lisa kutomjibu kwa muda mrefu.

"Baba, siendi." Lisa alikataa kwa sauti ya chini. "Hadhi yangu haifai, na familia ya Kimaro haitanitaka huko."

"Melanie alisema kwamba Bibi Kimaro tayari anakujua wewe ni nani, ameshasikia habari zako na anataka akuone pia. kwa hivyo itakuwa mbaya ikiwa hautaenda." Joel akahema. “Nenda tu. Wewe ni mfanyabiashara. Ni nafasi nzuri pia ya kujitambulisha kwa familia ya Kimaro na kisha kupanua mtandao wako kwenye tabaka la watu wa juu hapa Nairobi. Mbali na hilo, Bibi Kimaro pia ni tofauti na wengine. Yeye ni mkarimu sana.”

“Sawa.” Lisa alitabasamu kwa jazba lakini pia aliona ajabu moyoni mwake. Melanie na Nina wasingefurahi yeye aende usiku huo. Ilionekana kana kwamba safari ya usiku huo kwa familia ya Kimaro isingekuwa rahisi kwake.

Mara tu Lisa alipoingia nyumbani mwendo wa saa kumi na nusu jioni, Nina alimsalimia kwa uchangamfu, “Tutakula chakula cha jioni na familia ya Kimaro usiku wa leo. Nguo zako za kawaida hazitafaa sana kwa tukio hili muhimu, kwa hivyo nimekununulia seti mbili za nguo wewe na Melanie kwenye maduka leo. Niliiacha juu ya kitanda chako, kwa hivyo nenda kabadilishe."

Paji la uso la Lisa liliinuka kwa mshangao baada ya kupanda ghorofani. Hakutarajia Nina angemnunulia seti ya nguo za gharama za toleo jipya kabisa la hivi punde. Shingoni ilikuwa na mapambo ya lulu na dhahabu, na alipoangalia kwa kawaida kwenye simu yake, aliona kuwa seti hii ya nguo iligharimu karibu shilingi milioni saba sa Kitanzania.

Hakuelewa Nina alikuwa anawaza nini mwanzoni, lakini alipomwona Melanie ambaye alikuwa amevaa nguo za kawaida sana ambazo kwa gharama ya kawaida zilikuwa hazizidi hata shilingi laki moja, alipata wazo. Lengo lilikuwa ni kumfanya Nina aonekane kuwa ana roho nzuri, kwamba ameweza kumjali mtoto wa nje zaidi kuliko mwanaye wa kumzaa. Bibi Kimaro angempenda sana kwa moyo wake usio na upendeleo.

“Twendeni, twendeni. Tutachelewa.” Nina alimshika Joel mkono na kuelekea kwenye maegesho ya magari.

Sura ya: 165

Jumba la kifahari la familia ya Kimaro lilikuwa katikati ya mlima na pia lilikuwa na mandhari bora katika eneo lote la Mlima wa Sherman.

Shamba kubwa lapata hekali hamsini au zaidi lilikuwa na uwanja wa mbio za farasi, uwanja wa gofu, uwanja wa mpira wa kikapu, uwanja mdogo wa ndege, mabwawa ya samaki, zizi kubwa la ng’ombe, majumba ya farasi….na…Hata Lisa, ambaye alikuwa ameona nyanja mbalimbali za jamii, alihisi kuelemewa na mazingira yale.

Baada ya kuegesha gari, kijakazi mkuu aliwaongoza wale watu wanne hadi kwenye jengo kuu. Katika sebule ya kifahari, Bibi Kimaro na binti yake wa tatu, Queen, waliketi upande mmoja. Mzee Kimaro na wanaume kadhaa walizungumza kwenye sebule nyingine ya kifahari upande mwingine.

Wale wanne walipoingia, kila mtu alitazama. Lisa, ambaye alikuwa amevaa mavazi ya gharama ya zaidi ya milioni saba mwilini mwake, ndiye aliyevutia zaidi. Midomo yake ilikuwa imepakwa lipstick nyekundu na nywele zake ndefu nyeusi zilikuwa zimejikunja kwenye mabega yake. Alikuwa na mwonekano maridadi, na urembo wake ulikuwa wa kifahari na wa kuvutia.

Karibu naye, Melanie alivaa tu kama anayekwenda matembezi ya kawaida. Kila mtu alijua kwamba alikuwa mhusika mkuu usiku huo, lakini alikuwa kama nyota iliyofunikwa na mwezi angani.

Bibi Kimaro alikuwa amesikia Melanie akimtaja Lisa hapo awali na hakumpenda tayari kutokana na mtazamo wa chuki aliomjaza. Lakini alipomuona kwa mara kwanza tena akiwa kapendeza kuliko Melanie, moyo wake ukavutiwa naye zaidi. Alitamani kama yeye ndiye angekuwa mjukuu-mkwe wake.

"Bwana Ngosha, baba yangu na kaka zangu wako huko. Unaweza kwenda kuzungumza na wanaume wenzako ikiwa hujazoea kukaa na sisi wanawake hapa.” Queen Kimaro alitabasamu na kumuondoa Joel kiakili.

"Basi nitaenda huko." Hakika Joel alikuwa anajisikia vibaya kwenye kundi la wanawake wale. Baada ya kuwasalimia huku akitabasamu, alimtazama Lisa na kuelekea kwenye sebule ya wanaume.

Mara tu Joel alipoondoka, Queen Kimaro alikunja midomo yake kwa dhihaka. “Melanie, huyu ni dada yako wa nje? Yeye ni mrembo kweli. Angalia vito vyote na dhahabu iliyopambwa kwenye nguo zake. Nakumbuka niliona hili nilipoenda Paris kwa Wiki ya Mitindo siku chache zilizopita. Seti moja inagharimu milioni sita hadi saba. Sikuweza kuvumilia kuinunua.”

Nina alitabasamu kwa heshima. “Lisa aliteseka sana siku za nyuma na haikuwa rahisi kumrudisha hapa. Nilitaka kumnunulia kitu kizuri ili kumsaidia ajisikie vizuri.”

“Kweli wewe una huruma sana. Yaani unamchukulia Lisa kama mwanao wakumzaa. Angalia ulichofanya, suala la ndoa ya Melanie na Alvin huenda likatatuliwa leo, kwa hiyo ulipaswa kumvisha Melanie vizuri badala ya kuruhusu mtu mwingine amfunike.” Valeria alisema kwa sauti ya uvivu. Valeria alikuwa ni rafiki mkubwa wa Nina na kwenye familia ya Kimaro alikuwa ni mtu wa nje kabisa. Yeye alikuwa ni mdogo wake na Iveta ambaye ni binti-mkwe wa familia ya Kimaro.

Melanie alitabasamu. “Ni sawa tu, mama yangu hana upendeleo na anatuchukulia wote sawa. Yeye anampenda sana Lisa kwa sababu ameteseka sana huko kijijini. Mimi nimekulia kwenye familia ya kitajiri kwa hiyo hivi vitu ni vya kawaida sana kwangu, ninajihisi kupendeza tu hata kwenye mavazi ya kawaida kama haya.”

Baada ya kusikiliza, Lisa alitoa tabasamu la unyenyekevu. “Kumbe nguo zangu ni ghali sana? Sikujua hilo. Leo ndo mara yangu ya kwanza ninavaa hivi. Sijawahi kuvaa nguo za kupindukia kama hizi maishani mwangu, nilikuwa sijui hata kama inagharimu pesa nyingi kiasi hicho. Asante, Aunty Nina.” Alipomaliza kuongea, aligusa kwa uangalifu lulu kwenye nguo zake, na kumfanya aonekane kama mshamba aliyeshtuka baada ya kusikia kuwa alikuwa amevaa nguo za bei ghali.

Kila mtu alibadilisha mtazamo wake. Kulikuwa na mengi ya siri kati ya mistari ya maneno ya Lisa. Kwanza, hakuwa amevaa nguo za bei ghali kabla ya siku hiyo. Pili, hakuwa na habari kama nguo alizovaa zilikuwa na thamani kiasi kile. Nani angehangaika tena na mtumshamba kama huyo?

Nina akawa na wasiwasi na kujilazimisha kucheka. “Lisa, unamaanisha nini kusema hivyo? Je, sikukununulia nguo nyingi za kifahari hapo awali? Zimejaa tele kwenye kabati lako.”

"Ndo hivyo, mimi sikujua kama zina thamani kiasi hicho. Hata hivyo ulininunulia ili watu wakusifu wewe, siyo mimi. Kwa hiyo ulinunua kwa faida yako. Ikiwa kweli unanijali mimi kama mwanao Melania basi ungeniruhusu na mimi nihudhurie karamu ya Bwana Kimaro alipokuwa anachagua mchumba. Lakini mlinificha mimi na Melanie akaja kwa sirisiri. Hapo utasema unajali kweli?”

Kila mtu alielewa sasa lengo la Nina.


Nina alichukia sana. Hakuwahi kufikiria kwamba Lisa angekuwa mjanja kiasi hicho kuharibu sura ambayo alikuwa ameijenga kwa uchungu kwa miaka mingi.

Bibi Kimaro alikunywa chai taratibu. Alikuwa amehisi kwamba Nina hakuwa mbaya sana hapo awali, lakini kwa mtazamo ule ilionekana kwamba kwa kweli alikuwa hafai. Kwa bahati nzuri, Joel Ngosha alikuwa muungwana wa kweli kwa hivyo haikuwa mbaya kwa Alvin kumuoa Melanie.

“Inatosha, sielewi haya yote yanayozungumza kuhusu mavazi ya kifahari yananiumiza kichwa tu. Nataka tu kusuluhisha suala la ndoa ya Alvin haraka.” Bibi Kimaro alisafisha hali ya hewa mara moja.

Melanie aliona haya. Nina kwa haraka alisema, “Bwana Kimaro ni jitu miongoni mwa wanaume. Ikiwa Melanie angeweza kuolewa naye, itakuwa heshima kwa familia ya Ngosha.”

Valerie alicheka na kuachia vigerere kwa furaha. "Kwa kuwa kila mtu yuko hapa leo, kwanini tusiflimalize hilo?"

"Nilikuwa nikifikiria kitu kimoja." Bibi Kimaro akamgeukia kijakazi mkuu. “Nenda uniletee ile bangili ya urithi.”

Mkwewe, Iveta, aliuliza kwa wivu, “Unamaanisha ile bangili ya urithi kutoka kwa mababu?”

"Ndiyo,” Bibi Kimaro alijibu huku akitabasamu. “Alvin ndiye mrithi wa familia ya Kimaro, kwa hivyo bangili hiyo inapaswa kupitishwa kwa mke wake mtarajiwa,"

Lisa aliinamisha macho yake huku sura ya uchungu ikimulika ndani yake. Pembeni, Melanie na mama yake tayari walikuwa wameshusha pumzi nyingi za msisimko.

Muda si muda, bangili ile ililetwa, na Bibi Kimaro akamwita Melanie. Alipotaka kuunyanyua mkono wa Melanie na kumvika, mara kishindo cha miguu kikasikika kutoka nje. Kila mtu alitazama wakati Alvin akiingia ndani. Alikuwa amevalia suti ya kijivu yenye tai ya hariri. Kulikuwa na saa ya kifahari imefungwa kwenye mkono wake. Mwili wake mzima ulionekana kama sanamu linalotembea- alionekana mtukufu, wa kifahari, na wa ajabu.

"Mnafanya nini?" Alvin aliwatazama wanawake wote pale sebuleni na hata baadhi ya wanafamilia wa Ngosha. Macho yake yalitulia kwa sekunde mbili kwa Lisa bila kusogea kabla ya kuiona bangili ya urithi mkononi mwa Bibi kimaro.

Valeria alieleza kwa tabasamu, “Bibi yako anataka kumpa mke wako mtarajiwa bangili ya urithi wa familia.”

Paji la uso wa Alvin liliinuka huku akitembea na miguu yake mirefu. Alinyoosha mkono kuinyakua bangili ya thamani kutoka mkononi mwa Bibi Kimaro na kuanza kuichezeachezea.

"Kuwa mwangalifu. Usiidondoshe,” Bibi Kimaro alimuonya.

Queen Kimaro alitabasamu. "Bibi, Alvin anataka kumvika Melanie bangili yeye mwenyewe."

"Hiyo ni kweli. Ina maana zaidi ikiwa mpenzi ndiye anayefanya hivyo,” Valeria alichombeza.

Melanie aliingiwa na woga na kuning'iniza kichwa chake kwa aibu, uso wake tayari ulikuwa na furaha ya wasiwasi. Lisa akatazama pembeni na kuinamisha kichwa chini huku akijifanya anatazama simu yake.

Alvin alimtazama Melanie na ghafla akatabasamu kabla ya kurudisha bangili ndani ya boksi. “Kwa kuwa ni urithi wa familia, ni afadhali kuuthamini na kungoja siku ya harusi yangu kabla ya kuutoa. Hata hivyo… Ni nani anayejua harusi yangu itakuwa lini, au… ikiwa bibi-harusi atabadilika au la?”

Sauti yake ya sumaku kama zumari ilikuwa ya kuvutia, lakini baada ya kuongea, ukumbi mzima ukawa na kimya cha kutisha. Nyuso za tabasamu za Nina na Melanie zilionekana kuganda, na hawakuweza kuzungumza hata baada ya muda mrefu.

Macho ya Melanie yalikuwa mekundu huku machozi yakimtoka. Bibi Kimaro alimshika mkono kwa sura ya huzuni na kumtazama Alvin. “Kubadili mchumba? Kwa hiyo ungependa kubadilisha awe nani? Wewe ndiye uliyemchagua Melanie, na kila mtu nje tayari anajua kwamba yeye ni mpenzi wako. Ulifikiri kuhusu hisia za msichana huyu uliposema hivyo? Nakwambia nimeshaamua mjukuu wangu. Ni yeye.”

Alvin alionekana kutosikia na kuokota chungwa bila kujali kabla ya kulimenya. Kila mtu aliangalia harakati zake isipokuwa Lisa, ambaye alikuwa akicheza na simu yake tangu mwanzo.

"Alvin, umesikia alichosema bibi?" Valeria alimkumbusha, “Melanie ni msichana mzuri. Usimwangushe.”

Nina aliuma meno yake na kusema, “Bwana Kimaro, ikiwa humpendi Melanie, basi sema tu moja kwa moja badala ya kumchezea kama mpumbavu. Melanie ni mboni ya jicho la familia ya Ngosha.”

"Nini? Je, ni lazima nikubali kumuoa leo?” Alvin alitupa maganda ya machungwa kwenye meza. Macho yake meusi hayakuwa na mwisho. “Inachukua angalau nusu mwaka hadi mwaka wa kuchumbiana ili wengine waanze kuzungumzia ndoa, lakini unanilazimisha kumuoa siku chache tu baada ya kukutana naye. Je, binti wa familia ya Ngosha ni wa kipekee kiasi hicho? Nisingethubutu kukusumbua kama ningelijua hili kabla.”

TUKUTANE KURASA 166-170

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.............LISA
KURASA........166-170

Sura ya:166

Baada ya kumaliza chungwa, Alvin hakushiriki mazungumzo mengine na wanawake wale na akageuka kuondoka. Muda si mrefu baada ya kuondoka, vijana wengine wawili waliingia. Mmoja alikuwa Willie Kimaro, ambaye Lisa alikutana naye huko Dar es Salaam, na mwingine ni Jack Kimaro. Lisa aliigundua bila kuambiwa na mtu kuwa huyo alikuwa ni mdogo wa Alvin kutoka kwa baba tofauti.

Bibi Kimaro akawapungia mkono wajiunge nao. Jack aliunga nao mara moja lakini Willie aliondoka na kuelekea kwenye bwawa la kuogelea nyuma ya nyumba.

Saa kumi na mbili jioni, chakula cha jioni cha familia kilianza kuseviwa. Zaidi ya watu 20 walikuwa wameketi kwenye meza ndefu ya pamoja ya chakula. Mpishi alisambaza sahanai za mbele ya kila mtu. Hata hivyo, hakujua ikiwa ni makusudi au la, lakini ilipofika zamu ya Lisa, chakula cha maana chote kilikuwa tayari kimekwisha.

Mpishi akatabasamu akiomba msamaha. “Samahani, nyama nzuri imeisha, imebaki mifupamifupa tu. Hutajali, sawa, Bi Jones?"

Queen alifoka kwa hasira. “Mpakulie chakula kilichopo maneno mengi ya nini? Pengine hajawahi hata kuona chakula kama hiki hapo awali. Hata hicho kilichobaki kinamtosha kabisa.”

Uso wa Lisa ulikuwa umetulia. Haikuwa rahisi kwa kwa familia ile kubwa ya kifahari kuwa na uhaba wa chakula. Tayari alikuwa ametarajia mambo fulani yatokee, kwa hiyo hakukuwa na jambo la kumkasirisha.

Hata hivyo, sura ya Joel ilionyesha hali ya kutoridhika. “Bi. Kimaro, Lisa ni binti yangu. Tafadhali angalia sauti yako."

Sauti ya Joel haikuwa ya kawaida, na Mzee Kimaro mara moja alichukizwa na Queen. "Funga mdomo wako ikiwa hujui kuchagua maneno yako."

“Lisa, unaweza kula sehemu yangu…” Joel alijaribu kumsukumia sahani yake.

Alvin aliyekuwa amekaa mbele akichezea simu yake ghafla akaingilia kati na kusema. "Tumbo langu halijisikii vizuri tangu majuzi, kwa hivyo siwezi kula. Lisa , unaweza kuchukua sehemu yangu. Uncle Joel anaweza kuendelea kula shea yake mwenyewe.”

Kila mtu alipigwa na butwaa na kugeuka kumwangalia Melanie.
Valeria alitabasamu. "Melanie, Alvin anakupenda sana. Afadhali kuacha sehemu yake kuliko kumtendea vibaya baba mkwe wake wa baadaye.” Melanie alifurahi kwa siri. Alikuwa na wasiwasi kidogo hapo awali, lakini ilionekana kama Alvin bado anamjali.

Alvin alipuuza mazungumzo yao na kumgeukia mpishi huku akisema kwa tabasamu hafifu, “hatujawahi kuwa uhaba wa chakula kwenye meza. Kwa hili lililotokea leo limeidhalilisha sana familia hii. Kwa uzembe huu hupaswi kufanya kazi tena kwenye familia hii, ondoka mara moja!”

Mpishi aliingiwa na hofu. "Bwana Kimaro, mimi ..."

“Hukunisikia? Chukua vitu vyako na utoke nje." Alvin taratibu akavifuta vidole vyembamba kwa kitambaa, lakini maneno aliyoyatema yalikuwa kama upanga uliowafanya watu wasithubutu kukaidi.

Punde, jamaa mmoja aliingia na kumchukua mpishi. Mpishi mpya aliingia kutoka jikoni. Mpishi aliyefuata alikuwa mwangalifu asitumikie vibaya asije akamkasirisha Alvin.

Lisa aliinamisha kichwa na kula chakula chake kwa umakini. Sehemu yake ilikuwa ya Alvin, na ingawa kila mtu alisema kwamba Alvin alifanya vile kwa ajili ya Melanie na Joel, yeye alihisi tofauti moyoni mwake. Ghafla alikuwa na maumivu makali moyoni mwake. Alikuwa anawaza nini? Alikuwa na mchumba sasa, na Alvin pia alikuwa na Melanie.

Baada ya chakula cha jioni, familia ya Kimaro ilimtazama Melanie kwa heshima zaidi. Willie tu ndiye aliyekuwa anajua kilichokuwa kikiendelea kati ya Alvin na Lisa na wengine wote walikuwa gizani. Hawakuweza hata kugundua kwamba Alvin alikasirika kwa sababu ya Lisa, Melanie alikuwa nani kwake?

Wakati huo, Bibi Kimaro alisema, "Alvin, fuatana na Melanie chumbani kwako mkatazame sinema kukuza hisia zenu kwa kila mmoja.”

Alvin alitazama ukumbini na kumuona Lisa ameinamisha kichwa chini. Alikuwa fasta kwenye simu yake tena. Moyo wake ulimpanda kwa hasira akiamini alikuwa akichati na Kelvin, akainuka na kutembea. Melanie alimfuata kwa furaha.

Kisha, Nina aliongozana na wanawake wengine wa familia ya Kimaro kuangalia tamthilia. Joel naye alivutwa na wanaume wenzake ili acheze poker, Lisa pekee ndiye aliyekaa kimya kwenye sofa akicheza na simu yake. Hakuna aliyemjali wala hata kupiga naye stori.

Willie alikimbia na sinia la matunda ili kumriwadha. Haijalishi ni nani aliyeolewa na Alvin katika familia yao, chakula cha jioni cha familia hapo awali kilimfanya aone kwamba Alvin bado anamjali Lisa. Hakika lilikuwa ni wazo zuri kwake kujipendekeza kwake sasa.

“Bi. Jones, hujazoea mazingira ya hapa na unaonekana mpweke sana, tunaweza kupiga stori kidogo?"

"Hakuna haja, nitakaa tu hapa kimya mtu yeyote asije akashuku kuwa nina kitu kuhusu wewe." Lisa alikataa kwa heshima.

"Hiyo ni sawa. Sina sifa nzuri katika familia hata hivyo, kwa hiyo ni bora nisikuharibie.” Willie alitabasamu na kuondoka zake.

Alipofika tu kwenye ngazi, Jack Kimaro alishuka kutoka juu na kuinua uso wake kwake. “Unampenda?”

"Hapana." Willie akatikisa kichwa kwa haraka.

"Ninaelewa, yeye ni mrembo sana, ni mrembo zaidi kuliko hata Melanie.” Jack alibofya ulimi wake. "Ikiwa si kwa ukweli kwamba yeye ni binti haramu, ningeweza hata kumfuata."

Willie alishtuka na kusema kwa aibu, "Ndio, hastahili hadhi yetu."

“Najua.” Jack aliinua macho yake kwa sura isiyoeleweka.

Willie alihisi kukosa uvumilivu ikambidi tu amwage umbea wake “Unahisi nini? Unaelewa kuwa yeye ni mwanamke wa Alvin Kimaro?"
Jack akashangaa, “nilikuwa sijui hilo.” Na papo hapo macho yake yakadhihirisha dhamira isiyo njema dhidi ya Lisa.
•••
Lisa alikaa kwenye sofa akicheza michezo ya kwenye simu kwa zaidi ya dakika 40 wakati kijakazi mmoja alimwendea ghafla.

“Bi. Jones, tafadhali fuatana nami. Bibi Kimaro anasema anataka kukuona."

“Anataka kuniona kwa ajili ya nini?” Lisa alibumbuwaa.

“Sina uhakika kabisa. Nafuata tu maagizo yake.” Kijakazi alionekana mwenye hofu.

Bibi Kimaro aliishi katika makazi ya nyuma, na Lisa akamfuata kijakazi huyo kwa wasiwasi kidogo. Alichokifanya mpishi kwenye meza ya chakula kilimfanya Lisa asiwe na imani na mtu yoyote ndani ya jumba lile. Hakuwa akifahamu mazingira ya jumba lile la kifahari. Alipokaribia ua, chemchemi ndogo ya maji moto ilionekana kati ya mianzi ya kijani kibichi.

“Bibi Kimaro…” Kabla Lisa hajamalizia usemi wake, nguvu kubwa nyuma yake ilimsukuma kwenye chemchemi ile ya maji moto.

Sura ya:167

Kufikia wakati anatoka majini, kijakazi alikuwa ametoweka. Lisa aligundua kitu. Kijakazi hapo awali alikuwa amemtumia Bibi Kimaro kama kisingizio cha kumvuta hadi eneo hilo hivyo alijua alikuwa ameingia kwenye mtego. Hakujua mbaya wake alikuwa ni nani, kwa hiyo ilimbidi kuondoka haraka. Alitoa simu yake ili ampigie baba yake, lakini ilikuwa imezama ndani ya maji hivyo ilikuwa haifai tena.

“Nani wewe?” Nyuma ya msitu wa mianzi, mwanamume mmoja alitembea kwa ghafla akiwa kifua wazi. Sehemu ya chini ya mwili wake ilikuwa imefungwa kwa taulo ya kuogea, na uso wakehau kuwa mgeni kwake… Alikuwa Willie Kimaro!

Wakati huo, Lisa alielewa picha iliyokuwa ikiendelea. Alipumua kwa nguvu na kucheka.

"Lisa, unafanya nini hapa?" Willie alishtuka na kujifunika kifua kwa haraka. “Ondoka haraka. Alvin ataniua kama ataniona na wewe hapa.”

"Nimedanganywa na mtu hapa." Lisa akatoka kwenye maji. Nywele zake zilikuwa zimelowa, na nguo zake ziling’ang’ania umbo lake lenye utata. Ikiwa ni mtu mwingine yeyote, Willie bila shaka angegeuka kuwa mnyama, lakini hakuwa na ujasiri huo kwa Lisa Jones.

“Nguo zako zimelowa. Kwanza—” Kabla hajamaliza kusema, sauti za hatua zilisikika kutoka nje ya ua.

Lisa aliogopa sana. Ikiwa watu wangemwona kajiloweka kwenye chemchemi ya maji moto ambayo Willie alikuwa akiogelea ndani yake, asingeweza kujieleza akaeleweka.

Willie alimvuta pembeni haraka na kumwambia, “fanya haraka, kimbilia ndani kupitia upande huu. Chumba cha kwanza kwenye ghorofa ya pili ni cha Alvin. Nitamjulisha baadaye.”

Baada ya Lisa kukimbia, Willie alirudi haraka kwenye chemchem ya maji moto na kukutana na Valeria, Nina, Queen, na wengine wengi waliokuwa wakitembea haraka. Hata mama yake, Iveta, alikuwepo pia.

“Nyie wote mnafanya nini hapa? Mmekuja kunitazama nikioga?” Willie alitabasamu na kuwazuia.

“Toka!” Iveta alimkazia macho. "Nilisikia mtu akisema kwamba Lisa Jones yuko pamoja nawe huku. Alikuwa anafanya nini? Hujamfanya chochote?” Iveta alijua mwenendo wa mwanawe na aliogopa kwamba alikuwa amefanya jambo la kipuuzi tena. Hakutaka kumuudhi Joel Ngosha na pia alimdharau binti wa nje kama Lisa. Hakutaka kabisa kusikia mwanaye anajihusisha kimapenzi na Lisa.
"Unasema nini?" Willie alichanganyikiwa. "Nilikuwa najiloweka tu kwenye chemchemi ya maji moto."

“Willie, kijakazi aliona kwa macho yake kwamba hapo mapema ulimpelekea matunda Lisa kisha baadaye akakufuata kwenye chemchem ya maji mtoto. Tunajua wewe ni mtu wa aina gani. Usiniambie umemfanyia kitu.” Valeria hakuamini kabisa kama Willie katoweka kimaajabu.

“Mam’dogo Valeria, kwanini uniheshimu hata kidogo? Ina maana mimi ni mnyama kiasi hicho?” Willie alikasirika sana.

"Inatosha. Niondokee!" Iveta alimsukuma mbali kwa haraka.

Kundi la watu liliingia kwa kasi na kukagua kwenye chemchem ya maji moto kwa muda mrefu lakini hawakupata mtu yeyote.
Nina alipigwa na butwaa. Hii haikuwa jinsi mchongo wao ulivyotakiwa kwenda. Aliamini mtu kama Willie bila shaka asingekuwa na uvumilivu wa mhemuko alipomuona msichana mzuri kama Lisa, lakini, sio tu kwamba hapakuwa na dalili yoyote ya Willie kumbaka Lisa, lakini pia Lisa alikuwa ametoweka kimaajabu.

“Mmemaliza?” Willie aliuliza kwa sauti ya hasira. “Nilwaambia mimi sijamuona hapa. Nyie mnakera sana. Mimi nimekuja peke yangu kuogelea hapa,”

“Ameenda wapi? Hawezi kutoweka hewani tu!” Nina alibadilisha mbinu zake kwa haraka. “Ni mtoto wa Joel. Jambo baya likitokea kwake, nitakuwa nimekwisha.”

Valeria pia alisema, “Usijali, nitatuma watu wamtafute. Kwa kuwa mlikuja kwenye makazi ya Kimaro kama wageni, kwa hakika hatutaruhusu baya lolote litokee kwake.”

Alipoona kundi hilo la wanawake wakifanya kitendo cha ajabu kwa Lisa, Willie alituma ujumbe kwa Alvin kwa siri.
•••
Katika jumba la sinema la faragha, Alvin, ambaye alikuwa na uso uliojaa kero, aliusoma ujumbe ule na mara akasimama na kumwambia Melanie. “Nina kazi ya dharura ya kushughulikia. Unapaswa kuendelea kutazama bila mimi." Kisha, aliondoka kabla ya kumngoja Melanie ajibu.

Alvin akaelekea chumbani kwake haraka. Hakukuwa na taa hata moja, na mwanga hafifu wa mbalamwezi ukaangaza ndani kupitia madirishani. Chumba kilikuwa tupu. Alienda moja kwa moja kwenye kabati la nguo na kuwasha taa. Mwanamke aliyekuwa akivaa nguo zake alitoa sauti ya tahadhari na kuufunika mwili wake kwa mlango wa kabati la nguo. Macho yake meusi yalimfanya aonekane kama kulungu anayeogopa, na uso wake ulikuwa mweupe kwa aibu.

Midomo ya Alvin ilijikunja vibaya. “Vipi, tena. Mwizi anaingia chumbani kwangu na kuniibia nguo bado anathubutu kunikodolea macho?”

“Sina mood ya kubishana na wewe, Alvin. Watu huko nje lazima wawe wananitafuta kila mahali.” Lisa alikuwa na wasiwasi, lakini nguo zake zilikuwa zimelowa na nywele zake zilikuwa zimelowa. Hakuweza kwenda nje akiwa vile. Angeshtukiwa.

“Kwa hiyo… hilo linanihusu nini?” Alvin aliegemea mlango bila kujali, akionekana kutotilia maanani kabisa hali ya Lisa.

“Alvin…” Uso wa Lisa ulikuwa umepauka. Hakutaka kuharibu sifa ya familia ya Ngosha kwa kuhusishwa na kashfa na bwana mdogo maarufu kama Willie na kumfanya Nina asherehekee kwa hilo.

"Unajua kwamba mimi kamwe huwa siwasaidii watu bure?" Macho ya Alvin yaligeuka.

Lisa aliuma midomo, uso wake ukiwa mweupe kwa sababu ya aibu. “Alvin, usinifanyie hivyo. Mpenzi wako yuko nje."

“Kwa hiyo?” Alvin hakujali, akamsogelea hatua kwa hatua, mkono wake wa kulia ukiwa umeshikilia rafu pembeni ya sikio lake. Macho yake meusi yalionekana kuwa na uga wa sumaku ambao ungeweza kuwavuta watu ndani.

Mapigo ya moyo ya Lisa yalimwenda mbio huku akiitazama sura ya Alvin iliyokuwa karibu sana na uso wake, midomo yao ikaumana.
Alvin akambusu kwa shauku sana, na hakuonekana kuwa na mpango wa kumwachia mapema.

"Inatosha. Uliahidi kunisaidia.” Lisa hatimaye alimkurupua na kugeuzia kichwa chake pembeni.


Macho ya Alvin yaliyokuwa yanawaka yalitazama midomo yake. Alitaka kumbusu hadi mwisho wa wakati, lakini, mlango uligongwa na Valeria akamwita, "Alvin, umemuona Lisa?"

Alishika nguo zake kwa hofu. Akampapasa kwa upole sehemu ya nyuma ya mkono na kumvuta na kumfungia kabatini. Akaweka sawa nguo zake kabla ya kuuendea mlango na kuufungua. Valeria, Nina, na Melanie walikuwa wamesimama pale.

Aliwatazama kwa macho makali na kujibu. "Nimekuwa kwenye chumba cha sinema muda wote na Melanie. Ningewezaje kumuona?”

“Lakini… alitoweka…” Melanie alitazama chumba chake kwa wasiwasi. "Tulikuwa na wasiwasi kuwa amejificha kwenye chumba chako ..."

“Chumba changu? Kwanini ajifiche kwangu?" Sauti ya Alvin ilikuwa kali. Wanawake hao walijikaza, na Melanie akagundua kuwa alikuwa ameteleza ulimi.

Alvin akafoka taratibu, “Ni bora usngeachana na mbinu chafu unazozitumia kwa Ngosha hapa katika familia ya Kimaro. Aunty Nina, unaijua hasira yangu, kwa hiyo usinitie hasira.” Akaufunga mlango kwa nguvu na kwa kishindo.

Muda si muda, akapiga namba ya simu ya mtumishi. Mtumishi mzee katika miaka yake ya 50 hivi alikuja na nguo mpya. Lisa akabadili nguo haraka haraka. Alipotoka nje, alimuona Alvin akiwa amekaa kwenye sofa huku akibana sigara katikati ya vidole vyake.

“Shangazi Yasmini, tafadhali mtoe nje.”

“Hakika. Bi Jones, nifuate.” Aunty Yasmini alitabasamu kwa upole na kumtoa Lisa nje ya chumba kile.

Sura ya:168

Wawili hao hawakugundua, lakini Jack Kimaro, ambaye alikuwa akirudi chumbani kwake, alimwona Lisa akitoka nje ya chumba cha Alvin kutoka pembeni. Alitabasamu na ghafla akaelewa kila kitu.

Shangazi Yasmini alimpeleka kwenye mlango mdogo wa makao makuu. Kutoweka kwa Lisa kulizikusanya pamoja familia za Ngosha na Kimaro—hata Mzee Kimaro na Bibi Kimaro walikuwa wamejumuka nao kumtafuta kila mahali.

Alipomwona akirudi, mara moja Nina alimkimbilia kwa wasiwasi. "Lisa, ulienda wapi bila taarifa? Ulizima hata na simu yako. Tulikuwa tunakutafuta kote. Ulitutia wasiwasi hadi kufa.”

“Huh? Mbona umevaa nguo tofauti sasa?” Valeria aliuliza ghafla.

Lisa alipepesa macho na kusema huku akihisi huzuni, “Sikuwa makini, nilipotoka kwenda matembezi nikaanguka kwenye bwawa.
Shangazi Yasmini aliniona nimelowa kabisa na kunichukua. Alinipa nguo za kubadili kuzifuta nywele zangu. Simu yangu pia ilidondoka kwenye bwawa na haiwezi kutumika tena.” Alinyamaza na kuomba msamaha, “Samahani sana. Sikutaka kuwasumbua kwa sababu mlikuwa mnatazama tamthilia”

"Ni kweli?" Bibi Kimaro alimtazama Aunty Yasmini. Shangazi Yasmini alikuwa amefanya kazi kwa familia ya Kimaro kwa zaidi ya miaka 30, kwa hiyo alimwamini.

“Ndiyo, ndivyo,” Shangazi Yasmini alisema huku akitabasamu.

"Sawa, ni vizuri kwamba yuko sawa. Hebu tutawanyike.” Bibi Kimaro alisugua macho yake, akihisi kukasirishwa na usumbufu huo.

Joel pia hakutaka kubaki tena. “Tumesababisha usumbufu mwingi kwa kila mtu usiku wa leo. Tuondokeni sasa hivi.”

Baada ya familia ya Ngosha kuondoka, Valeria aliona ni ajabu. Ni wazi alikuwa amepanga mtu amsukume Lisa kwenye chemchemi ya maji moto, kwa nini Aunty Yasmini alisema kwamba Lisa alianguka kwenye bwawa? Nani alimwambia Aunty Yasmini kusema hivyo? Nani alikuwa akimsaidia Lisa?

Wakati huo, Willie alimsogelea huku akitabasamu. "Ma’mdogo Valeria, unapaswa kuachana na biashara ya familia ya Ngosha. Babu au Bibi akigundua kwamba ulishirikiana na watu wa nje kuzusha matatizo katika familia, huenda wasikuruhusu uishi hpapa.”

Valeria alishtuka na kumtazama Willie. “Wewe ndiye ulimsaidia?”

Willie alishtuka, hakukubali wala kukataa. “Unafikiri nini kingetokea ikiwa nitawaambia wazazi wangu kuhusu ulichokifanya usiku wa leo?”

Valeria kakosa la kujibu, Ikiwa dada yake Iveta na shemeji yake Paxton Kimaro wangejua kwamba alikuwa amepanga njama dhidi ya Willie mtoto wao, wangepigana na kuzozana. Valerie alitetemeka na akajuta kumsikiliza Nina.
•••
Gari lilirudi kwenye jumba la familia ya Ngosha. Ndani ya gari, Melanie alikuwa bado analalamika, “Tafadhali toa taarifa kwa mtu wakati mwingine unapotoka badala ya kunyata kimya kimya. Hukuona kwamba Bibi Kimaro na Mzee Kimaro hawakuwa na furaha wakati tunaondoka?”

Lisa hakusema neno hata moja hadi alipofika sebuleni. Alimgeukia Joel na kusema, “Baba, kwa kweli niliitwa na mtumishi katika familia ya Kimaro hapo awali. Alisema kuwa Bibi Kimaro alitaka kuniona, lakini alinipeleka kwenye chemchemi ya maji moto na kunisukuma ndani nilipokuwa nimejisahau. Willie Kimaro alikuwa akijiloweka kwenye maji wakati huo, lakini kwa bahati nzuri, tunafahamiana, kwa hiyo hakunifanyia chochote na kunisaidia kujificha.”

"Nini?" Joel alishtuka. “Mbona hukuniambia mapema?”

Melanie aliziba mdomo wake kwa haraka. “Haiwezekani! Willie Kimaro alikusaidia? Yeye ni mbakaji maarufu na hupitia kila mwanamke anayemwona. Baba, Lisa atakuwa tayari…”

Joel mara moja akawa na wasiwasi na maneno yake. "Lisa, wewe"

“Baba usijali. Nilikuwa sawa kwa sababu hata dakika moja haikupita baada ya kuangukia kwenye chemchemi ya maji joto, Aunty Nina aliwaleta kwa makusudi Valerie na Queen kunitafuta.” Lisa alitoa tabasamu lisilo wazi kwa Nina. "Baada ya kutonipata kwenye chemchemi ya maji ya joto, walidhani kuwa nimepotea na kuwatahadharisha familia nzima ya Kimaro na kuanza kunitafuta kila mahali."

Joel hakuwa mpumbavu. Alipogundua kilichotokea, alimkodolea macho Nina.

Nina alishtuka. “Unamaanisha nini Lisa? Nilisikia kwa masikio yangu mtumishi wa familia ya Kimaro akidai kwamba ulienda kwa siri kwenye chemchemi ya maji moto. Nilidhani ulikuwa unapanga kumtongoza Willie. Kutokana na uovu wa Willie, nilikuwa na wasiwasi juu yako hivyo nikaamua kwenda huko kukuokoa…”

“Ndio, uliharakisha kuja huko. Lakini haikuwa kwa nia ya kuniokoa bali kuja kushuhudia akinifanyia vitendo vya ajabu kisha utangaze na sifa yangu iharibike. Familia ya Kimaro bila shaka wangeniona kama mtu nisiyefaa, kwa hiyo wangekubalije kumruhusu Willie anioe?”

Lisa alipumua katika hali nyepesi. “Anti Nina, kama ulikuwa na wasiwasi na mimi, ungeenda kwenye chemchemi ya maji moto peke yako kwa siri bila kupeleka familia nzima huko. Ungehisi umefarijika zaidi kwamba hukunipata badala ya kufichua jambo hilo kwa kila mtu na kuanzisha msako.”

Alieleza kila sentensi kwa njia iliyo wazi na yenye utaratibu. Hata kama Joel angekuwa mpumbavu, asingeshindwa kung’amua kuwa Nina alihusika na njama hizo.

"Nina, wewe ni mbaya sana." Joel alitetemeka kwa hasira. “Kwa nini unamchukia msichana mdogo kama huyu? Sio tu kwamba wewe na Melanie huwa mnamlenga nyumbani, lakini pia mlikuwa na wazo la kumwangamiza katika familia ya Kimaro.”

Lisa alikunja uso. “Baba, hukujua kwamba hata mpishi alikuwa amenilenga kimakusudi wakati wa chakula cha jioni?”

"Oh, karibu nisahau kuhusu hilo." Joel alipokumbuka tukio hilo, chuki yake dhidi ya Nina ilikaribia kufikia kilele. “Nakumbuka uliniambia kuwa mna uhusiano wa kirafiki na Valeria, sivyo? Nimewaona nyinyi wawili mkiwa pamoja siku nzima ya leo.”

“Baba, Lisa anajaribu kututenganisha. Usidanganywe naye,” Melanie alisema kwa wasiwasi.

“Fumba mdomo wako,” Joel alinguruma, “Angalia jinsi mama yako alivyokulea! Wewe na mama yako nyote nhamna maana kabisa.”

Melanie alipigwa na butwaa, huku Nina akipandwa na hasira. “Joel, unaendelea kumtetea Lisa tangu arudi. Nadhani bado una hisia kwa Sheryl, huyo b*tch—”

Kabla Nina hajamalizia sentensi yake, Joel alimpiga kofi la uso moja kwa moja. “Nina, hata huonyeshi kujutia makosa yako. Kukuoa ndio majuto yangu makubwa maishani.”

“Unathubutuje kunipiga kofi Joel?!” Uso wa Nina ulionyesha kutokuamini huku akiwa amefunika sehemu ya uso wake iliyokuwa na maumivu. Machozi yalitiririka mashavuni mwake. “Njoo, Melanie. Twende nyumbani kwa bibi yako.” Mara baada ya Nina kumaliza kuongea, alimkokota Melanie na kutoka nje.

“Baba, una upendeleo. Tangu Lisa aje, hutujali tena.” Melanie alilia huku akitoka na Nina.

Joel alikaa kwenye kochi na uso uliopauka sana. Lisa kisha akanong’ona, “Pole, Baba. Kwa kweli sikutaka kukuambia, lakini usiku wa leo wao—”

“Sio kosa lako. Ni mimi ndiye nimeshindwa kukulinda.” Joel alionekana kukumbuka kitu. Kwa sura ya uchungu, alifanya uamuzi.
“Nitatafuta njia ya kumtaliki.”

Lisa alishangaa kwa muda, lakini alinyamaza. Kulikuwa na mzozo mkali wa kibiashara kati ya familia ya Ngosha na familia ya Mahewa. Aliona kuwa hakuna mtu katika familia ya Ngosha ambaye angekubali wazo hilo.
•••
Akiwa na kilio, Nina alirudi nyumbani kwa Mahewa pamoja na Melanie. Kaka yake, Farres Mahewa, alishindwa kujizuia mara tu alipoona jeraha kwenye uso wa Nina. “Dada nitashughulika na Lisa. Nimekuwa nikiweka chuki dhidi yake kwa sababu ya ardhi aliyonipikonya hata hivyo.”

Aliposikia maneno yake, Nina alifarijika. Kaka yake siku zote alikuwa mtu katili na mkorofi. Alikuwa na uhusiano na watu wengi wasio na huruma. Ingekuwa rahisi sana kwake kushughulika na Lisa.

Sura ya:169

Siku mbili baada ya Nina na Melanie kuondoka, Lisa alianza kuishi maisha ya starehe. Baada ya kumaliza kifungua kinywa, aliendesha gari lake kuelekea ofisini. Gari hilo lilipokuwa likisafiri kwenye barabara inayozunguka milimani, ghafla alikumbana na zahama kali. Alijaribu kupiga breki, na kugundua kuwa breki hazifanyi kazi.

Alipojitambua, Lisa aligeuza usukani haraka. Gari hilo lilikimbia kwa mwendo wa kasi katika barabara hiyo kutokana na hitilafu ya breki.
Gari jingine aina ya VW lilionekana mbele yake ghafla. Harakaharaka Lisa aliamua kupenyeza gari kutoka kando ya barabara nyembamba na kuingia kwenye kolongo.

Dereva wa VW iliyokuwa imemchukua Bwana Jack Kimaro, alipata mshtuko. “Huyu mtu amerukwa na akili, anaendesha gari kwa mwendo wa maili 150 hadi 160 kwa saa utadhani yupo kwenye mbio za magari?”

Jack aliinua kichwa chake na kushangaa kuona gari jeupe aina Mercedes Benz likisafiri kama upepo kwenye barabara ya makolongoni. Ilionekana kuwa dereva hakuwa akipiga breki hata wakati wa kupita kwenye kona mbaya Hata yeye hakuwa na ujasiri wa kuendesha gari kwa kasi kama hiyo.

"Kutakuwa na kitu hakiko sawa kwenye gari. Lifuate.” Dereva wa Jack alianza kulifukuzia gari la Lisa kwa nyuma. Gari la Lisa sasa lilikuwa likikimbia kwa kasi kubwa ya karibu maili 200 kwa saa. Wakati gari lilipokaribia kupinduka, Lisa aliendesha mara moja hadi kwenye njia yenye matope iliyokuwa ikijengwa. Mshindo mkubwa ulisikika wakati upande wa kulia wa gari ulipogonga mti mkubwa.

Jack alitoka nje kwa haraka na kufungua mlango wa gari lile. Puto la hewa ndilo lilimuokoa Lisa asifyatuke kutoka kwenye siti yake. Alikuwa amepoteza fahamu, lakini hakukuwa na dalili zozote za majeraha.

“Lisa…” Jack alistaajabu baada ya kuutazama vizuri uso wa binti aliyekuwa kwenye gari hilo. Haraka akambeba kutoka ndani ya gari pamoja na dereva na kumpeleka hospitali ya karibu baadaye.

Muda si mrefu Joel alifika hospitali huku akiwa na sura ya wasiwasi. Jack alimfariji, “Usijali, Uncle Joel. Binti yako ana akili na jasiri. Niliona kwamba gari lake lilikuwa halina udhibiti kwa muda, hata hivyo alitulia huku akilishika gari kwenye barabara inayozunguka-zunguka. Baadaye, aliendesha gari hadi kwenye njia yenye matope iliyokuwa ikijengwa ili kupunguza mwendo wake. Wakati gari lilipoanguka, hakukuwa na mtu aliyeketi upande wa kulia wa gari. Ingawa alipoteza fahamu, hakuna majeraha yoyote ya kimwili juu yake. Labda alizimia kwa sababu ya mshtuko wa moyo."

"Asante Mungu." Hatimaye Joel alishusha pumzi. Alimwambia Jack kwa shukrani, “Asante sana, Bwana Jack. Nitakumbuka wema wako daima.”

"Hapana usijali. Ndicho nilichopaswa kufanya.” Jack alijibu kwa dhati.

Karibu nusu saa baadaye, wafanyakazi wa hospitali walitoka. Sawa na kile alichokitaja Jack, kugongwa kwa mwili na kichwa cha Lisa
ilimsababishia mshtuko wa ubongo, ambao ulieleza kwanini alizimia. Lakini hakuwa na majeraha katika sehemu zingine za mwili wake.

Baada ya kujua kuwa Lisa yuko sawa, Jack alielekea ofisini kwani alikuwa na jambo la kushughulikia asubuhi hiyo, Njiani dereva aliuliza, "Bwana Jack, unafikiri gari lake litakuwa limechezewa?"

Jack alicheka. Sababu ya kushindwa kwa breki ya gari lile la kijerumani lenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni mia moja ilikuwa dhahiri ni kutokana na kuchezewa.

Dereva akahema. "Ni mara yangu ya kwanza kuona mtu akiishia kupata majeraha mepesi baada ya kukutana na ajali mbaya kama hii. Mwanamke yeyote wa kawaida angechanganyikiwa kutoka kwa akili zake, na gari labda lingeanguka kutoka kwenye mwamba. Bi Jones anaweza kuwa binti mdogo, lakini ustadi wake wa kuendesha gari hakika ni mzuri sana. Ingawa mimi ni dereva mzoefu, ni aibu kwamba siwezi kuwa mtulivu na jasiri kama yeye.”

“Ndiyo.” Jack aligonga vidole vyake kwenye magoti yake. Alikuwa amekutana naye katika familia ya Kimaro siku chache zilizopita, akidhani kwamba alikuwa ni mrembo tu mwenye uso mzuri bila kina, lakini alishangazwa kabisa na ujasiri aliomuona nao siku hiyo.

Hapo awali, alifikiria kwamba Alvin alivutiwa tu na uzuri wake, lakini kumbe kulikuwa na hazina nzurizaidi ndani yake. Alvin angefanyaje baada ya kugundua kuwa amepata ajali?



•••
Saa sita mchana Jack alielekea kwenye ukumbi wa chakula wa kampuni hiyo. Majumba ya kulia chakula kwa wasimamizi wakuu na wafanyikazi wa kawaida yalikuwa kwenye sakafu tofauti.

Alipokuwa akielekea kwenye chumba cha chakula cha mabosi wa kampuni, alimuona Alvin ambaye alikuwa amevalia suti nnyeusi akitoka kwenye korido. Uso wake mzuri ulionekana katika hali mbaya. Watendaji wachache walikuwa wakifuatilia kwa karibu nyuma yake kuripoti utendaji wa kampuni.

Midomo ya Jack ilitetemeka kishetani. “Kaka.”

Alvin alimpa macho ya makali ya onyo. “Nilikuwa napanga kukutafuta. Kwanini hukuhudhuria mkutano asubuhi ya leo?”

“Kaka, sikukusudia kukosekana,” Jack akajibu kwa unyonge, “Nilipokuwa nakuja kutoka Sherman Mountain asubuhi ya leo, niliona ajali. Ilinibidi kumpeleka mwathirika hospitalini.”

"Wakati ujao, unahitaji kuifahamisha kampuni hata kama umepata udhuru." Alvin akanyanyua miguu yake mirefu na kuingia kwenye chumba cha chakula.

“Sawa, Kaka. Hata hivyo, unahitaji kumtembelea mwathirika? Yeye ni binti kutoka kwa familia ya Ngosha. Ni yule aliyekuja majuzi, si Melanie.”

Alvin aliganda baada ya Jack kumaliza kuzungumza. Alitazama nyuma, na macho yake meusi yakatua kwa Jack. Macho yake yalionekana kuwasilisha msukosuko wa hisia. “Lisa?”

"Ndio." Uso wa Jack ulionyesha huruma.

Alvin akaingiza mkono wake wa kulia kwenye mfuko wa suruali yake na kuuma mdomo wake mwembamba. "Amejeruhiwa vibaya?"

“Sina uhakika na hili. Nilikuja ofisini baada ya kumpeleka hospitali.” Jack akamtazama Alvin aliyekuwa amekunja uso. “Lakini nilisikia kwamba breki zilifeli. Ilikuwa hatari sana kaka. Nilipoenda kumuokoa, tayari alikuwa amepoteza fahamu.

Alvin akaufungua mlango wa chumba cha chakula. “Twende ndani.”

Baada ya kuketi kwenye chumba cha chakula, alimpa Hans jicho la kumaanisha. Hans alielewa maana ya jicho hilo kwake ndani ya sekunde moja na akaenda kutafuta ukweli juu ya jambo hilo mara moja.

Alvin alikaa kwenye kiti cha heshima, huku kundi la watendaji waliokuwa pembeni yake wakiendelea kupiga soga. Hata hivyo, hakujali walichokuwa wakisema. Fikra zake zote zilikua kwa Lisa. Siku mbili zilizopita, hata alikuwa amesimama mbele yake akiwa na uso uliokunjamana, akimruhusu kumbusu apendavyo. Sasa, alikuwa amepata ajali, na haikuwa hakika kama alikuwa hai! Moyo wa Alvin ulimuuma sana.

Ghafla, alisimama na kusema. “Sitakula kwani kuna kitu kimetokea. Nyie endeleeni tu na mlo wenu.” Watendaji hao walitazamana huku wakimtupi macho ya mshangao wakati akiondoka kwa kasi.


Jack siku zote alihisi kwamba hakukuwa na kitu kinachoweza kumdhoofisha Alvin, kutokana na ukweli kwamba alianza kuwaweka wanawake mbali tangu kifo cha Sarah. Kwa kushangaza, sehemu yake dhaifu ilikuwa imefichuliwa.

Alvin alikuwa akiendesha gari kwa kasi katika safari yake yote kuelekea hospitali. Akaongeza mwendo hadi kwenye wodi ya watu mashuhuri. Alipokaribia kuingia tu, ghafla akamuona Kelvin Mushi akiwa amekaa mbele ya kitanda na kumshika Lisa mkono. Mara moja akaacha kutembea na kujificha nyuma ya ukuta badala yake.

Alimsikia Kelvin akiuliza kwa upole, “Je, bado unahisi kizunguzungu?”

"Ndio, kidogo. Najisikia kutapika.”

"Daktari alisema kuwa ni kawaida kwa mtu aliye na mtikiso wa ubongo kupata hii. Umenitisha sana akili. Hapo awali nilipanga kusawazisha mambo kadhaa huko Dar es Salaam kabla sijaja hapa, lakini sikuweza kumudu kusubiri baada ya kusikia umepata ajali. Sitarudi nyuma. Nahitaji kubaki hapa ili kukuweka salama ili nisiwe na wasiwasi na wewe.” Kelvin alimshika Lisa mkono akauweka karibu na uso wake.

Lisa alitazama chini kwa uchungu. “Hata haujapona majeraha yako—”

“Ninaimarika zaidi. Sitaki kabisa kukupoteza, Lisa,” Kelvin alisema kwa upendo, “Tufunge ndoa mwaka huu. Nitakuwa kando yako siku zote.”

Sura ya: 170

Ghafla, Alvin alijiona mjinga kwa kumhangaikia Lisa na kukimbia kwa mwendo wa kasi hadi hospitalini. Sawa na yale yaliyokuwa yametokea huko Dar es salaam hapo awali, alidanganywa naye tena na tena.

Kila mara alijifanya kuwa msafi na mwenye haya mbele yake, hata hivyo alimtendea Kelvin kwa mapenzi mazito nyuma ya mgongo wake. Alimchukuliaje? Macho yake yalionyesha sura ya huzuni. Alvin alishindwa kuvumilia tena kusikiliza mazungumzo kati ya Lisa na Kelvin. Akageuka na kuiendea lifti.

Joel aliyetoka tu kwenye lifti alishangaa kugongana na Alvin. "Bwana Kimaro, ni nini kinakuleta hapa?"

"Rafiki yangu alilazwa hapa, kwa hivyo nilikuja kumtembelea." Kwa hali ya huzuni, Alvin alijibu bila mpangilio kabla hajaingia kwenye lifti. Upweke wake ulimfanya Joeli ashindwe la kusema.

Joel alipoingia wodini, Kelvin alikuwa akimpa maji Lisa. Joel alipumua na kusema kwa msisimko, “Kelvin anakutendea vizuri sana. Alinipigia simu asubuhi ya leo baada ya kukukosa hewani usiku mzima. Alipojua kuwa kuna jambo limekutokea, mara moja akaruka hapa. Alikuwa tayari amefika hapa kabla hata wewe haujaamka.”

Lisa hakujua la kusema, lakini alikuwa na tabasamu hafifu likienea katika uso wake uliopauka. Joel alivuta kiti na kuketi juu yake. Akashusha pumzi. “Ikilinganishwa na mtu kama Kelvin, Bwana Kimaro niligongana naye kwenye lifti sasa hivi. Alikuja kumtembelea rafiki yake. Baada ya yote, mimi bado ni baba ya Melanie mchumba wake na wewe ni shemeji yake mtarajiwa, lakini hakujali na hakuweza kuhangaika kujua kwa nini niko hapa.”

“Bwana Kimaro?” Kelvin alishikwa na butwaa. "Unamzungumzia Alvin Kimaro?"

“Ndiyo. Yuko kwenye uhusiano na Melanie,” Joel aliongeza, “Lakini sidhani kama atamuoa Melanie. Melanie amechanganyikiwa tu. Kwa kile nilichoona, yeye pia hayuko ndani yake. Hivyo sivyo anapaswa kufanya ikiwa anampenda kikweli.”

Lisa hakusema neno, lakini kichwa chake kiliendelea kumuuma.
Kwa nini Alvin alikuja hospitali? Je, alikuwa ameenda kumtembelea? Je, alikuwa nje ya wodi muda ule na kuamua kutoingia baada ya kumuona Kelvin? Ilikuwa ni dhana yake tu. Hata hivyo, ilikuwa vigumu kuelewa ni nini kilikuwa kikiendelea kichwani mwa Alvin.

“Bado hujapeleka gari kwa uchunguzi, baba?” Lisa aliuliza swali huku akilini mwake akiwa na mawazo. “Hilo ndilo gari jipya uliloninunulia. Kwa nini breki zifeli?”

Joel alionekana kukosa raha. “Nilipiga simu polisi, lakini hadi polisi wanafika, gari lilikuwa limeteketea kabisa. Kutokana na uchunguzi wa awali wa polisi, mafuta ya injini yalivuja kutokana na ajali hiyo na kusababisha mlipuko wa moto.”

Lisa aliuma mdomo. “Nina hakika gari liligonga upande wa kulia nakuangukia upande wa kushoto. Haiwezi kuwa uvujaji wa mafuta uliosababisha mlipuko huo.”
“Nitamwomba mtu achunguze jambo hilo kwa kina,” Joel alisema kwa hasira, “hakika nitamuua mtu ambaye alijaribu kumuua binti yangu baada ya kujua ni nani.”

Lisa alifikiria kidogo na kusema, “Baba unaweza kuwaomba polisi wasambaze habari kwa umma kuwa mtu aliyehujumu gari langu amepatikana? Kisha funga nyumba ya familia ya yako na usiruhusu mtu yeyote kuingia kwa wakati huu.”

Joel alipigwa na butwaa. "Lisa, unashuku kuwa kuna mtu kutoka kwa familia yetu alihujumu gari lako? Hili haliwezekani kabisa. Watumishi wote katika nyumba yangu wametumikia familia yetu kwa zaidi ya miaka kumi. Wao ni waaminifu na wa kutegemewa—”

“Baba siku hizi mbili nimetembelea ofisini na nyumbani tu, kwa hiyo hizi sehemu mbili ndizo sehemu ninazozishuku. Mtu aliyefanya hivi lazima awe mtu ambaye hatoki mbali. Akisikia hivyo hakika atashtuka,” Lisa alisema kwa uzito, “Shirikiana nami tu. Nisipomjua mtu huyo ni nani, huenda nikapoteza maisha yangu wakati ujao.” Joel aliitikia kwa kichwa baada ya kusikiliza ushauri wake.
•••
Baada ya kuingia ndani ya gari, Alvin aliufunga mlango kwa nguvu. Kisha akawasha sigara na kuanza kuivuta. Hans alipoingia ndani ya gari, tayari moshi ulikuwa umetapakaa ndani ya gari. “Bwana Kimaro, nimechunguza ajali…”

Alvin akawasha gari na kuondoka kwa kasi. Huku gari likisafiri kama roketi barabarani, Hans aliogopa sana hivi kwamba alishika mpini juu ya kichwa chake. Mara Alvin alipofika ofisini, alipanda ghorofani moja kwa moja.

Hans akammiminia kikombe cha kahawa. Alipogeuka tu kuondoka, ghafla Alvin akamuita, “Simama. Umegundua nini? Ni mtu gani aliyefanya hujuma hiyo?”
.
Hans alitazama nyuma na kuripoti kwake kwa umakini, "Gari lilichezewa na mtu kutoka familia ya Ngosha, na ilikuwa kazi ya mtunza bustani. Alipokea kiasi cha pesa kutoka kwa Beka Pongo, Nijuavyo, Beka na Farres hujumuika mara kwa mara. Baada ya kuchunguza suala hili, hata hivyo, inaonekana kwamba Farres anahusika nalo moja kwa moja.”

“Hilo halishangazi. Ikizingatiwa kwamba Farres amefanya mambo mengi mabaya, ana uzoefu wa mambo kama hayo.” Alvin aliinua yake kikombe cha kahawa na kupuliza juu yake. “Joel amegundua nini kuhusu jambo hili?”

"Amefanya uchunguzi wa gari, lakini gari tayari limeteketea. Zaidi ya hayo, hakukuwa na kamera zozote za uchunguzi kwenye eneo la tukio. Nadhani hataweza kujua chochote," Hans alisema, "labda hakutarajia familia ya Mahewa kuwa katili sana."

"Joel ni mtu mzuri, lakini kwa bahati mbaya, watu kama yeye hudanganywa kwa urahisi sana." Alvin alicheka.

“Bwana Kimaro, nimfahamishe Lisa—”

“Kuna faida gani kumwambia?” Alvin ghafla akatupa kikombe cha kahawa juu ya meza. “Si yeye anayekulipa, achana naye.” Alvin alipandwa na hasira.

•••
Siku ya pili baada ya Lisa kulazwa hospitalini. Saa sita mchana, Kelvin alikuwa akimlisha Lisa. Jack alienda kumtembelea. Jack Kimaro alikuwa amevalia sweta ya kahawa na suruali ya kijivu, ambayo ilikuwa imekunjwa ili kuonyesha vifundo vyake vya mikono vilivyopendeza. Vijana wote wa familia ya Kimaro walivutia sana hivi kwamba wangeweza kuwa waigizaji mashuhuri katika tasnia ya burudani.

"Ni nini kimekuleta hapa, Bwana mdogo wa familia ya Kimaro?" Hali ya mshangao ikapita usoni mwa Lisa. Alikuwa amekutana naye mara moja tu katika jumba la familia ya Kimaro, na hawakuzungumza hata kidogo wakati huo.

"Hata hivyo, mimi ndiye niliyekuokoa, kwa hiyo nilikuja kukuona unaendeleaje." Macho ya Jack yalimwelekea Kelvin.

Kelvin alisimama na kujitambulisha, “Hi, mimi ni mchumba wa Lisa. Asante kwa kumuokoa usiku huo, Bwana Kimaro.” Kelvin alionekana mpole na mnyenyekevu, lakini mwenendo wake haukuwa wa kujikweza wala kujidharau.

TUKUTANE KURASA 171-175

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.............LISA
KURASA.........171-175

Sura ya 171

Jack alipigwa na butwaa kwa sekunde kadhaa. "Sikujua kuwa tayari una mchumba, Bi Jones."

Lisa akajibu, “Mm. Ninashukuru sana kwa msaada wako siku hiyo, Bwana Kimaro.”

"Usijali, ni furaha yangu kwamba nilikusaidia.” Jack alimkonyeza. “Nimeona ustadi wako wa kuendesha gari ni wa ajabu sana.Nitajifunza kutoka kwako siku moja."

"Ujuzi wake wa kuendesha gari ni wa ajabu?" Kelvin alishangaa kidogo.

"Hmm… Ustadi wangu ulikuwa bora kuliko kawaida labda kwa sababu nilikuwa nikijaribu kuokoa maisha yangu." Lisa alishtuka huku akilazimisha tabasamu.

Wote watatu walikuwa na mazungumzo mafupi. Baada ya hapo, Jack aliwaaga na kuondoka.

Kimya kikatanda wodini. Uso wa Kelvin ulimulika kwa hisia tata. "Lisa, unajuta kunichumbia huko Dar es Salaam??"

"Nini tatizo?" Lisa alishangaa.

Kelvin alimtazama kwa uchungu. “Nimekuwa nikifanya vyema tangu nikiwa mdogo. Ni wakati tu nilipofika Nairobi ndipo nilitambua jinsi nilivyo duni baada ya kukutana na wababe wa hapa. Vijana wa familia ya Kimaro ni wasomi miongoni mwa wasomi. Ghafla, ninahisi kwamba sistahili kuwa pamoja nawe.”

Lisa alitabasamu kwa upole. “Unaniwazia sana. Hata baada ya kurudi kwenye familia ya Ngosha, mimi ni binti wa nje ya ndoa. Hakuna mtu kutoka kwa familia tajiri ambaye atakubali kumruhusu mtoto wao anioe.”

"Wao ni wa kina sana. Hawajui sifa nzuri ndani yako?” Kelvin alishikilia ncha ya nywele zake na kuziweka nyuma ya sikio lake.
Lisa alihisi kama kumkwepa, lakini bado alivumilia.
•••
Siku ya tatu, Nina na Melanie walifika hospitalini wakiwa na hasira.
“Joel, kwa nini unafanya hivi? Kwa nini unatuzuia kuingia nyumbani kwetu?” Nina alizua ghasia mara tu alipoingia ndani ya wodi. "Hata binti yako wa kumzaa haruhusiwi kuingia. Unachojali kwa sasa ni Lisa tu, sivyo?"

“Baba una mpango wa kunitelekeza kweli?” Melanie alianza kulia kwa uchungu.

Joel alihisi uchungu ndani kabisa. “Baada ya—”

“Baba…” Lisa alimzuia. Joel alinyamaza mara moja.

“Lisa, wewe ndiye uliyemlazimisha baba atuzuie kurudi nyumbani, si ndiyo?” Melanie alitoa hasira zake kwa Lisa. “Hapo ni nyumbani kwangu. Nimekuwa nikiishi hapo kwa miaka 20!”

"Ni kosa langu, Lisa." Nina alipiga magoti ghafla sakafuni. “Sitafanya hivyo tena. Tafadhali mwambie baba yako asitufukuze.
Melanie nami hatuwezi kuishi bila baba yako.”

Ilikuwa ni mara ya kwanza kwa Joel kuona Nina akitenda kwa unyenyekevu. Mchanganyiko wa hisia ulimjaa wakati huo. Baada ya yote, walikuwa wameoana kwa zaidi ya miaka ishirini. Zaidi ya hayo, alikuwa mama wa binti yake. Wakati anakaribia kumvuta Nina, simu yake ikaita.

Dakika alipoona taarifa ya simu inayoingia, aliijibu huku akitembea. Baada ya kujua habari hiyo, kifua chake kilianza kumuuma kwa maumivu makali.

Baada ya kukata simu, alimfuata Nina na kumpiga teke akaanguka chini. “Wewe mwanamke katili, niliweza kuvumilia nia yako ya kuharibu sifa ya Lisa hapo awali, lakini kwanini mnataka kumuangamiza pia?”

Baada ya kuangushwa chini, Nina alipigwa na butwaa. “Joel, umenipiga teke? Umenipiga teke kweli?” Macho ya Nina yakawa mekundu, na karibu aingiwe na wazimu.

Melanie aliogopa sana hivi kwamba hakuthubutu kusogea hata kidogo. “Baba una kichaa. Kwanini ulimpiga teke mama?”

"Sio tu nimekupiga teke, lakini pia nitakupa talaka," Joel alisema kwa hasira, "mtunza bustani ambaye alifanya kazi kwa familia yetu amekiri kwamba ni Beka ndiye aliyemlipa ili kuharibu breki za gari la Lisa kwa nia ya kumuua Lisa. Beka yuko karibu na Farres. Nani mwingine angefanya jambo kama hilo isipokuwa familia ya Mahewa?"

“Sikufanya hivyo.” Nina alimshika Joel mkono na kuanza kulia bila hatia. “Kwa sababu ya Beka, unaharibu uhusiano wetu ambao tumeuendeleza kwa zaidi ya miaka ishirini? Nani anajua ni nani Lisa amemkosea huko nje?"

“Inatosha. Acha kujifanya. Umechukizwa naye tangu alipokuja Nairobi, na umewahi kufikiria njia nyingi tu za kumdhalilisha. Hakika nitakupa talaka.” Joel alimsukuma Nina kisha akamwita afisa usalama na kumtoa nje. Kwa upande wa Melanie alimtaka dereva wake amrudishe nyumbani moja kwa moja.

Joel alifanikiwa kutoa tabasamu dogo wodini. “Hatimaye niligundua ni aina gani ya mwanamke katili ambaye nimekuwa nikiishi naye. Anatisha sana.”

Lisa alinyamaza. Moyoni alifikiri kwamba kwa kuwa Nina angeweza kumfanya Farres amuue kirahisi, basi angeweza kufanya hivyo kwa mama yake pia hapo nyuma. Ni hadi siku hiyo ndipo Joel alipofahamu msururu huo mbaya wa matendo ya Nina. Pengine hakuwahi kumshuku Nina kuwa na uhusiano fulani na kifo cha mama yake.

“Usijali Lisa. Nimetamani sana kumpa talaka wakati huu.” Baada ya kuongea na Lisa kwa umakini, Joel alienda nyumbani na kuanza kushughulikia masuala ya talaka yake.

Baada ya Joel kuondoka, Kelvin alisema kwa wasiwasi, “Baba yako hataweza kumtaliki Nina.”

“Ndiyo.” Lisa alihisi vivyo hivyo. “Ukweli ni kwamba familia ya Ngosha na familia ya Mahewa wamefanya kazi pamoja kwa miaka mingi, Melanie sasa ni mpenzi wa Alvin Kimaro. Familia ya Kimaro haitakubali mwanamke kutoka kwa familia iliyovunjika. Kwa sababu tu ya hili pekee, babu na bibi yangu na watu wengine wote katika familia ya Ngosha hakika hawatakubali talaka yao.”

Mwonekano wa huruma ulivuka uso wa Kelvin. “Basi wakati huu…”

"Haiwezekani kuwashinda maadui mara moja tu." Lisa alikodoa macho yake. “Uwezekano pekee wa familia ya Ngosha kuidhinisha talaka ya Joel na Nina ni pale ambapo Melanie hatakuwa tena mchumba wa Alvin.”
•••

Usiku sana, Katika kijiji cha ukiwa, Lina alikuwa akikimbia kuokoa maisha yake, akijaribu kuondoka kijijini humo. Siku hizo, alikuwa akiteswa na yule mzee mwenye karaha usiku na mchana, karibu aingie kichaa.

“Acha kukimbia, malaya wewe!” Nyuma yake kulikuwa na mzee mmoja mkali ambaye aliendelea kumkimbiza kwa fimbo. Mwanamume huyo alipokaribia kumshika, gari moja lilisimama ghafla mbele ya Lina. Mtu mmoja kutoka kwenye gari alimwingiza ndani mara moja.

Gari lilisafiri mbali zaidi na mtu huyo na hatimaye akaachwa. Lina alihisi kuwa kila kitu kilikuwa kama ndoto. Hatimaye alikuwa amekimbia. Hakuhitaji tena kufua nguo na kupika, wala hangelazimika kuvumilia njaa na baridi, wala asingebakwa tena.Ni Lisa na Alvin ndio waliosababisha aishie katika hali hiyo!

“Wewe ni Lina?” Mwanaume aliyekuwa ndani ya gari alimwangalia ghafla kwa kuchukia.

"Unanijua?" Lina alipata mshtuko mbaya sana.

"Kuna mtu anataka kukuona."

Saa tano baadaye, Lina alipelekwa mahali pa ajabu huku akiwa amefumba macho.

“Huku ni wapi? Na nyie ni akina nani?”

“Si lazima ujue mimi ni nani. Unachohitaji kujua ni kwamba ninaweza kukusaidia katika kulipiza kisasi kwa Lisa na Alvin.” Sauti ya kupendeza ya mwanamume ilisikika kando yake.

Lina alipigwa na butwaa kwa muda. Alianza kuingiwa na kinyongo. “Kweli? Lakini hadhi ya Alvin si ya kawaida.”

“Usiwe na wasiwasi, niaelewa kila kitu. Unachotakiwa kufanya ni kushirikiana na mimi.”

“Sawa.” Lina alikubali bila kusita. Alikuwa na hasira sana na Alvin na Lisa. Kwa kuzingatia kwamba alikuwa ameteseka sana, alitaka kulipiza kisasi na kuwalipa kwa yale yote waliyomfanyia.
.
Sura ya:172

Saa tatu na nusu usiku ndani jumba la familia ya Kimaro, Alvin aliingia sebuleni. Alivua suti yake bila mpangilio na kumpa mtumishi aliyekuwa kando yake. Macho yake yalitua kwa Bibi Kimaro, ambaye alikuwa akimsubiri kwenye kochi.

“Hujafika nyumbani kwa siku chache. Inaonekana ni vigumu kukuona sasa,” Bibi Kimaro alimlalamikia Alvin.

“Melanie anakuja kukushtakia si ndiyo?” Alvin alimtania Bibi Kimaro na kukaa pembeni yake. Alikuwa amevalia fulana ya bluu iliyokoza na pensi.

“Ni vizuri kwamba unajua. Haji hapa kwa nia moja tu ya kunisalimia. Anataka kukuona pia” Bibi Kimaro alisema kwa hasira, “Anatia huruma sana. Familia yake imekuwa na amani wakati wote huu, lakini Joel sasa anasisitiza kumpa talaka mkewe baada ya binti yake wa nje kurudi. Anawezaje kumtaliki mke wake namna hiyo?”

Alvin akamgusa kidevu bibi yake. "Inaonekana kama Melanie amekufanyia hila kwa kukushawishi kuchukua upande wake."

“Anahitaji kunishawishi? Nimeona mbinu nyingi chafu zinazotumiwa na familia tajiri.” Bibi Kimaro alihema. “Kama vile talaka ya baba na mama yako, sikuikubali kabisa.”

Alvin alichukua sigara. Hakuwasha mara moja lakini alicheza nayo kwanza. Paji la uso wake liliinama sana, likitoa hisia ya huzuni.

Bibi Kimaro akashusha pumzi na kusema “Leo, Melanie aliniambia kuwa siku ya kuzaliwa ya Mzee Ngosha ni wiki ijayo. Anapanga kuwaalika baadhi ya jamaa na marafiki kula chakula pamoja. Matumaini yake sasa yapo kwako. Kama utampenda Melanie basi wazazi wake watalazimika kuwa pamoja ili ndoa yenu itimie. Ikiwa utakataa uhusiano wako na yeye kwa wakati huu, mama yake labda atalazimika kupitia talaka.”

Alvin alijifanya kuziba sikio. Akatoa kiberiti na kuwasha sigara yake.

“Una mpango wa kufanya nini? Utahudhuria sherehe hiyo?” Bibi Kimaro akapaza sauti yake kutokana na kuudhika.”

“Simpendi Melanie”

“Ikiwa hupendezwi na Melanie, tafuta mchumba mwingine. lakini, lazima uoe mwaka huu."

“Nitahudhuria. Kwa kuwa umeliweka wazi, sina budi kwenda.”
Alvin alitabasamu kwa unyonge na kuinuka. “Tayari usiku umeenda. Lala usingizi mnono.”

"Hayo ndiyo maneno niliyotaka kuyasiki." Bibi Kimaro hatimaye aliridhika na jibu lake. Kisha akarudi chumbani kwake kupumzika.
•••
Punde, siku ya kuzaliwa kwa Mzee Ngosha ilifika. Alikuwa amefikisha miaka 68, lakini hakutaka kusherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kiwango kikubwa. Aliajiri tu mpishi mashuhuri kutoka ng'ambo na kuweka meza kadhaa katika hoteli. Wale walioalikwa kwenye sherehe hiyo walikuwa ni washirika wa kibiashara ambao alikuwa amefanya nao kazi kwa miaka mingi na pia baadhi ya marafiki na watu wa ukoo.

Saa tano kamili asubuhi, Joel alikutana na Lisa na Kelvin. Kisha akatoa utangulizi sahihi. “Huyu ni mchumba wa binti yangu.
Yeye pia ni CEO na mwenyekiti wa Golden Corporation.”

"Golden Corporation? Kampuni gani hiyo? Sijawahi kusikia,” Aunty Irene wa familia ya Ngosha aliongea kwa sauti ya chini ya dharau.

Kelvin alitabasamu kwa utulivu na kusema, “Golden Corporation ni kampuni ambayo ilianzishwa kutoa huduma za usafirishaji, lakini kwa sasa tunahusika na sayansi, viwanda na teknolojia. Pia tuna matawi ya nje. Tumeanzisha biashara yetu hapa Nairobi na tumejenga kiwanda kipya cha futi za mraba 5,000 katika eneo la kiuchumi hivi karibuni. Kufikia sasa, tumefanikiwa kupata hazina ya dola bilioni 50 ili kupanua rasmi biashara yetu nchini Kenya”

Kila mtu alipigwa na butwaa. Ukanda wa kiuchumi huko Nairobi ulikuwa unaendelea kwa kasi muda huo. Kwa kuzingatia kwamba angeweza kupanua mradi mapema na kuutekeleza kwa mafanikio, ilimaanisha kijana huyu alikuwa na akili.

Baadhi ya watu wazito waliosikia wasifu huo walianza kumpongeza Kelvin. Pongezi hizo ziliinua hali ya Mzee Ngosha. Hapo awali, Mzee Ngosha alikuwa amemdharau Kelvin aliposikia alikuwa akitokea Dar es Salaam. Lakini baadaye alikuwa na furaha sana. “Haha, ndio. Mjukuu wangu, fanyeni haraka mfunge ndoa. Ningependa kusherehekea ndoa yenu kabla sijafa.” Kelvin alionekana kukubalika kwenye ukoo moja kwa moja.

Lisa alikosa la kusema. Babu yake alikuwa mkorofi kwelikweli.
Hata hivyo, hakutarajia kwamba uhusiano wake na Kelvin ungekua haraka hivyo. Alikuwa amepata nafasi huko Nairobi hata haraka zaidi kuliko yeye.

“Kumbe, Mzee Ngosha, nilisikia kuwa una mjukuu mwingine ambaye ni mpenzi wa Bwana Kimaro. Mbona simuoni hapa?” Mzee mmoja aliuliza kwa shauku. "Bwana Kimaro atakuja hapa leo, sivyo?" Uso wa Mzee Ngosha uligeuka kuwa mgumu. Kwa kweli, hakuwa na uhakika kuhusu hilo pia.

Wakati huo, kulikuwa na vurugu za ghafla nje. Kila mtu akageuza macho yake upande ule. Alvin mwenye urefu wake na uzuri wake aliingia ndani. Alikuwa amevalia suti ya kijani kibichi yenye milia ambayo ilitengenezwa maalum na mbunifu mahiri wa kimataifa. Alionyesha uzuri wa hali ya juu ambao ulikuwa wa mtu wa hali ya juu kama yeye. Alikuwa ameambatana na Melanie.

Akiwa amevalia gauni jekundu, Melanie alishika mkono wake kupitia kwa Alvin kwa sura ya kupendeza.

Wawili hao waliendana vyema. Ilionekana kana kwamba walikuwa wakitembea kwenye zulia jekundu. Nyuma yao walikuwa Nina na Farres ambao walikuwa wakitabasamu kutoka sikio hadi sikio.

Nina na Farres walikuwa wameridhika sana. Mwanzoni, Alvin hakuwa na wasiwasi hata kidogo kuhusu Melanie. Hata hivyo, Melanie alitembelea familia ya Kimaro kila siku, na hatimaye kumshawishi kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa kwa Mzee Ngosha.

Hii ilimaanisha nini? IIlimaanisha kwamba Alvin alikuwa radhi kuuweka uhusiano wake na Melanie hadharani. Melanie angeolewa na Alvin mapema au baadaye. Kwa maana hiyo, familia ya Mahewa ingepanda hadhi kwa kiwango cha juu.

"Halo, Melanie. Kwa nini hukunifahamisha kwamba Bwan Kimaro amerejea?” Mzee Ngosha alimwendea Melanie kwa haraka haraka.

Alvin na Melanie walichangiwa na kutafutwa na wageni wote waliokuwepo. Wageni pia walijaribu kuwapa maneno yao ya heri.

"Bwana Kimaro, wewe na Melanie hakika mnaendana kikamilifu."

"Bwana Kimaro, ni heshima yangu kuweza kukutana nawe."

"Bibi Ngosha, umebarikiwa sana kuwa na binti mzuri kama huyo."

Kinyume chake, hakuna hata mmoja wa wageni aliyekwenda kuzungumza na Lisa na Kelvin. Sura ya mshangao iliosha uso wa Kelvin. “Lisa, yeye…”

“Ndiyo.” Lisa alijua anachofikiria. Aliitikia kwa kichwa na kukunja uso kwa kina. Hakutarajia kwamba Alvin angeandamana na Melanie kuhudhuria sherehe ya kuzaliwa kwa babu yake.

Joel na Nina walipokuwa wakielekea kupeana talaka, Alvin alionekana na mtu kutoka kwa familia ya Mahewa, akionyesha wazi msaada wake kwa Melanie. Farres alikuwa karibu kumuua Lisa mara ya mwisho. Hata hivyo, Alvin bado alihudhuria sherehe kwa ajili ya familia ya Mahewa.

Ghafla, Lisa alijawa na huzuni. Moyo wake ulikuwa ukitetemeka kwa baridi, lakini alijitahidi kadiri alivyoweza kuzuia hasira yake.
Kuanzia siku hiyo na kuendelea, angekuwa kinyume naye. Hata hivyo, angewezaje kuwa kinyume na Alvin?

Baada ya kuona sura ya Lisa inazidi kupwaya kwa huzuni, ghafla Kelvin alinyoosha mkono wake na kumshika kiuno. Alisema bila kufikiri, “Hata kama Alvin ana nguvu kiasi gani, sitakuachilia. Umechelewa sana kujuta, Lisa.”

Lisa alipigwa na butwaa akauma mdomo. “Unawaza kupita kiasi. Ilinijia akilini kwamba itakuwa ngumu zaidi kushughulika na Nina kwa kuwa anachukua upande wa familia ya Mahewa.”

Kelvin alisita. “Usiwe na haraka. Ndo kwanza umefika Nairobi, kuwa na subira."

“Sawa.” Lisa alikuwa hayupo. Alitamani angemsambaratisha Nina kwa haraka kwa sababu mara baada Alvin kumwoa Melanie, ingekuwa ngumu zaidi kudili na Nina.

Alvin, ambaye alifuatwa na umati wa watu, alielekeza macho yake kwa Lisa. Alipomwona Kelvin akiwa ameshika kiuno chake, na Lisa amejiachia mikononi mwa Kelvin, hali hiyo ilisababisha maumivu makali moyoni mwake.

Alvin aliendelea kuvaa tabasamu la kujilazimisha, lakini macho yake yalikuwa yamepoa sana kiasi cha kuonekana kama yameganda. Hata wageni walio karibu naye waliweza kuhisi uchangamfu wake ulikuwa ukiporomoka kwa kasi.

Mzee Ngosha alihisi kwamba Alvin alikuwa amekerwa na umati mkubwa wa watu waliomvamia, hivyo mara moja akasema, “Bwana Kimaro, njoo ukae kwenye kiti cha heshima. Chakula kitatolewa hivi karibuni."

Alvin alipiga hatua kuelekea kwenye kiti cha heshima na kuketi. Melanie alikuwa ameketi kando yake. Mzee Ngosha alimsukuma moja kwa moja Joel kuelekea kwa Nina na kumfanya aketi pembeni yake. Pia alimwonya Joel kwa sauti ya chini, “Bwana Kimaro yupo hapa. Inamaanisha kwamba anamjali Melanie. Ukithubutu kutoa talaka, nitajiua mbele yako.”

Akiwa na hasira, Joel alihisi kifua kinamuuma sana hata akashindwa kusema neno lolote.

"Lisa, njoo hapa na Kelvin." Bibi Ngosha alimpungia mkono Lisa nakumwelekeza aketi pia kwenye meza ya heshima.

Sura ya:173

Lisa na Kelvin walipokuwa wakielekea upande huo, Alvin alimtazama Kelvin kwa hasira.

"Wewe ni…?" Alvin aliuliza kwa kejeli utadhani hamfahamu kabisa.

“Yeye ni mchumba wa Lisa kutoka Golden Corporation.” Joel Ngosha aliwahi kutoa utambulisho haraka haraka.

"Sijawahi kumsikia." Alvin alitazama pembeni na kuongeza maneno ya kejeli kwa sauti ya dharau. “Kwa hiyo, mtu yeyote anaruhusiwa kuketi kwenye meza ya heshima ya familia ya Ngosha, sivyo?”

Kwa hayo, uso wa kifahari na mzuri wa Kelvin ulibadilika na kufunikwa na hasira. Lisa alihisi kana kwamba amepigwa kofi usoni. Alibaki katika hali ya aibu huku Melanie alicheka kwa dharau.

“Hasa. Angalia tu Bwana Kimaro ni nani. Sio kila mtu anaweza kukaa naye." Mzee Ngosha alionekana kutofurahishwa pia.

Bibi Ngosha aliona aibu sana kwa sababu yeye ndiye aliyemwomba Lisa aketi pale na Kelvin.

Nitaenda kwenye meza nyingine." Kelvin alimpiga Lisa nyuma ya mkono wake. Kisha, akageuka na kuelekea kwenye meza nyingine ya kawaida.

“Subiri. Tutaenda wote. Hata hivyo mimi ni mtoto wa nje, sistahili kuketi na Bwana Kimaro pia.” Lisa alimfuata Kelvin. Wote wawili hatimaye waliketi kwenye meza nyingine ndogo tu ya kawaida.

Alvin aliuma mdomo wake na kulazimisha tabasamu la kuridhika huku akijiachia kwenye kiti cha heshima.

Mzee Ngosha aliibuka na kumbembeleza Alvin. “Pole sana, Bwana Kimaro. Huo ulikuwa utoto tu wa Lisa. Usizame kwenye kiwango chake. Yeye ni binti haramu ambaye alitoka kijijini, kwa hiyo hana ustaarabu kabisa.” Baada ya hapo, alijifanya kutabasamu.

“Baba…” Uso wa Joel ulijawa na aibu. Hakuweza tena kuvumilia.

"Nyamaza." Mzee Ngosha alimkazia macho Joel. Kisha, akatoa ishara kwa Melanie kwa macho yake.

Melanie aliukumbatia mkono wa Alvin mara moja na kuongea kwa kujishaua. "Bwana Kimaro, ninaahidi kwamba hutawaona wawili hao tena utakapotembelea familia ya Ngosha wakati ujao."

"Ndio ndio. Bila kujali ni tukio gani, hawatakaribishwa tena hapa.” Mzee Ngosha alijitahidi sana kumbembeleza Alvin.

Alvin aliuma mdomo wake kidogo, jambo ambalo lilionekana kumaanisha kuridhika. Kwa kweli, wale waliomfahamu walijua kwamba alikuwa akiudhika zaidi moyoni mwake.

Lisa, ambaye alikuwa kwenye meza nyingine, kwa kawaida alisikia mazungumzo kati ya watu hao. Alijua kwamba kila mtu pale mezani alikuwa akimtazama kwa namna ya nderemo bila hata kumuonea huruma. Uso wake uligeuka kwa hasira kidogo kidogo. Kelvin alishikilia mkono wake kwa nguvu chini ya meza. Ilikuwa ni mara ya kwanza kujihisi mnyonge sana. Kwa unyonge aliopata siku hiyo, aliapa kwamba alipaswa kuwa na nguvu ili kuwalipa kwa faida.

Baada ya chakula cha mchana, Lisa alipotoka sebuleni, alikutana na Farres ambaye alikuwa akitoka nje ya choo cha kiume.
Mwanamume huyo mwenye umri wa miaka 40 hivi alikuwa amejengeka kwa misuli yenye nguvu na hakuwa amenyoa nywele. Alionekana mbaya na hatari.

Walipokabiliana bila kupishana, Farres alimpa tabasamu baya. "Una ustadi mkubwa wa kuendesha gari, msichana mdogo. Hongera kwa kunusurika kwenye ajali. Siku nyingine hutakuwa na bahati kama hiyo.”

Uso wa Lisa ukaingia giza. Alithubutu vipi kujitapa mbele yake kuhusika na ajali ile?! "Jitape sana lakini mwisho wako haupo mbali." Lisa naye alimtishia.

“Haha. Wakati Melanie anakuwa Madam Kimaro, nitakuua na hakuna mtu atakayesema chochote kuhusu hilo.” Farres aliinua mkono wake na kufanya kitendo cha kukata shingo yake. Kisha, akaangua kicheko kisicho na adabu.

Macho ya Lisa yalidhihirisha mshtuko. Huku akitetemeka, alisema, “Kwa kuzingatia sauti yako ya kiburi, lazima uwe umefanya ukatili mwingi. Kifo cha mama yangu nina uhakika kinahusiana na familia yako.”

Farres alipigwa na butwaa kwa muda. "Mama yako alikufa katika kimbunga huko Kigoma. Ina uhusiano gani na mimi? Sheryl alikuwa na bahati mbaya sana kufa akiwa bado binti mdogo, lakini afadhali uangalie," Farres alimuonya na kisha akaondoka akiwa ameduwaa.

Lisa alimkazia macho katika hali ya kuchanganyikiwa. Ikiwa haikuwa familia ya Mahewa iliyomuua Sheryl, basi nani?

Karamu iliisha. Lisa na Kelvin walipokuwa wakielekea kwenye maegesho ya magari, alipokea ujumbe kutoka kwa Alvin. [Nakungoja nje ya hoteli. Njoo hapa.] Lisa alishindwa tu kulia. Jinsi Alvin alivyokuwa na aibu kumtafuta! Aliufuta ujumbe huo mara moja.

Muda mfupi baadaye, hata hivyo, Alvin alimtumia video ya kucheza kwake akiwa amevalia mavazi ya aibu. Lisa alisaga meno yake. Aligeuka na kumwambia Kelvin, “Nakumbuka tu kwamba ninahitaji kukutana na bibi yangu ili kushughulika na jambo fulani. Si lazima unirudishe nyumbani.”

“Sawa. Nipigie mara tu utakaporudi." Baada ya kumkumbusha, Kelvin alimtazama akiondoka. Uso wake mzuri ulibadilika ghafla.

Dakika kumi baadaye, Lisa alilikuta gari la rangi nyeusi la Alvin kando ya barabara. Alipoingia ndani ya gari, alitazama huku na huko kama mwizi.

“Kwanini una wasiwasi, unaogopa kwamba Kelvin atatuona?” Alvin alishika sigara katikati ya vidole huku mkono wake ukiwekwa kwenye usukani. Katikati ya moshi huo uso wake mzuri ulionyesha hali ya kejeli.

Kwa wakati huu, Lisa alimchukia sana. “Bwana Kimaro, si unakumbuka uliingia ukumbini na mpenzi wako na mama mkwe mtarajiwa sasa hivi? Sasa kila mtu anajua kuwa wewe ni mtu wa Melanie. Mtu akiniona nikiingia kwenye gari lako, anaweza kudhani kwamba ninakutongoza.”

“Una wivu?” Macho makali ya Alvin yalikuwa yakimtazama.

“Siwezi kuwa na wivu kuhusu hilo.” Lisa alidhihaki na kujibu kwa sauti ya kuchafukwa. “Kwa nini unataka kukutana nami? Ikiwa hakuna kitu kikubwa, niache niondoke sasa.” Alifanya kana kwamba alilazimishwa kuwa hapo.

Alvin alikuwa na msongo wa mawazo sana wakati huo kuhusu Kelvin. Aliamua kupasua kero iliyokuwa ndani yake moja kwa moja. Alimshika mkono na kumdhihaki, akisema, “Sasa Kelvin amerudi, hujisikii kuniona tena, sih? Lisa, ukiendelea kuwa na tabia ya kipuuzi mbele yangu, nitakufukuza wewe na Kelvin kutoka Nairobi.”

“Inatosha.” Lisa alichoka kabisa na maneno yake. Macho yake yalikuwa mekundu kwa hasira. “Ulinidhalilisha sana wakati wa sherehe sasa hivi, labda utaniacha tu baada ya mimi kujiua."

“Utajiua kweli? Kwa mwanamke kama wewe, uko tayari kujiua?" Alvin alibana shavu lake kwa mkono wake wa kushoto. Maneno yaliyotoka kwenye mdomo wake yalikuwa ya kikatili kuliko hapo awali.

Macho ya Lisa yalijawa na chuki. “Nakuchukia, Alvin. Wewe ndiye mwanaume mpumbavu zaidi niliyewahi kukutana naye.”

“Thubutu kusema tena.” Alvin kweli alipoteza utulivu sasa. Alimshika koo, uso wake ukionyesha sura ya ukatili.

“Nimekosea kusema hivyo? Unavutiwa na mwanamke kama Melanie. Wewe ni kipofu, sivyo?” Lisa akapiga kelele, "Familia ya Mahewa ina nia mbaya, lakini unaendelea kuwatetea. Unawasaidia tu na kuwaunga mkono. Wakati wowote ninapokumbuka jinsi nilivyopenda mtu kama wewe wakati huo, ninachukizwa sana.”

“Ha! Ulikuwa unanipenda?” Alvin alijifanya kana kwamba anasikia mzaha. "Usipotoshe neno 'upendo'."

Lisa alijidharau kutamka hivyo na kutoa tabasamu la uchungu.

“Lisa, usijaribu kunichokoza. Najua vizuri kile kilicho mawazoni mwako.” Macho ya Alvin yalikuwa makali. “Kadiri ninavyoishi, hutaweza kuishinda familia ya Mahewa. Nina na Joel hawataweza kutalikiana.”

Lisa alimpa macho ya kifo. Kutokana na hasira kali, kifua chake kilihisi uzito asioweza kuubeba.

Alvin akaisogeza sigara kwenye midomo yake na kuutoa ule moshi taratibu. Moshi huo ulifunika uso wake ambao ulitoa hisia ngumu. "Isipokuwa, nimpatie mwanamke mwingine mimba, sitafikiria kumwacha Melanie." Alipomaliza kusema tu, alifungua vifungo vya shati lake chini ya kola. Kisha akatazama nje ya dirisha. Hiki kilikuwa tayari kidokezo kikubwa cha uvumilivu ambao angeweza kumpa. Ilikuwa pia nafasi yake ya mwisho kwake.

Lisa alipigwa na butwaa. Aliona kidogo inamchanganya. Alimaanisha nini? Je, alikuwa akimaanisha kwamba alitaka atafute mwanamke wa kumpa mimba, au yeye ndiyo achukue mimba yake?Hata hivyo, Lisa alihisi maumivu makali sana kufikiria kitu ambacho Alvin alipanga kufanya na mwanamke mwingine.

“Nimekuelewa. Naweza kuondoka sasa hivi?” Baada ya mapambano ya kukata tamaa, hatimaye Lisa alikata tamaa.

Sura ya: 174

“Umeelewa nini?” Aliuliza kwa dharau Alvin.
"Naelewa. Unataka kusema kwamba huwezi kuachana na Melanie, sivyo? Tabasamu la uchungu liliruka usoni mwa Lisa. “Ikiwa ndivyo ilivyo, hupaswi kuwa pamoja nami pia.”

Alvin alishindwa cha kusema. Mwanamke huyo kwa kawaida alikuwa na akili sana. Nini kilikuwa kimetokea kwenye ubongo wake sasa? Hakuweza kuwa na wasiwasi juu yake. Hapo hapo akanyoosha mguu na kukanya moto hadi mwisho, akaondoka kwa kasi kama yote.

"Unafanya nini? Acha nishuke.” Haijalishi Lisa alipiga vipi kelele, Alvin aliendelea kumpuuza.

Gari ilisafiri moja kwa moja hadi kitongoji cha Oasis. Alvin alimburuta Lisa hadi juu ya ghorofa na kumsukuma kuelekea kwenye kochi. Akiwa amechemka kwa hasira, alisema, “Lisa, unataka niweke mambo wazi zaidi, sivyo? Nataka uachane na Kelvin mara moja. Unaruhusiwa kuwa na mimba ya mtoto wangu tu. Ikiwa utabeba mimba, nitaachana na Melanie.”

Lisa alikodoa macho. Alijifanya kana kwamba amepigwa na radi. Kwa muda mrefu, alibakia ameganda kama kaota mizizi mahali hapo.

Alvin akavua suti yake na kuitupa chini. Aliiweka mikono yake nyuma ya kichwa chake na kumweka juu ya kifua chake. “Lisa, wewe ni jeuri. Hiki ni kikomo cha uvumilivu wangu na pia nafasi yako pekee.”

Lisa alishikwa na mshangao, na akili yake ilikuwa imefika mwisho wa kufikiri. Hakuweza kuelewa nia yake, kwa kuzingatia kwamba alimchukia sana na hata alimuona mchafu wakati huo, sasa angeachana na Melanie maadamu angebeba mimba ya mtoto wake? Je! ni kwa sababu bado alikuwa na hisia kwake…?

Moyo wake ulianza kudunda. Wakati huo, alihisi kushawishika. Tayari alikuwa akijua kwamba kifo cha Sheryl kilihusishwa na familia ya Mahewa. Zaidi ya hayo, kwa kuwa Farres alikuwa amejaribu kumuua mara moja, ilikuwa inawezekana kwamba angejaribu kufanya hivyo tena. Njia pekee ya mkato ya kuzuia hilo lisitokee ilikuwa ni kumtegemea Alvin.

Baada ya kuona hali yake ya kushtuka, Alvin alimbeba na kuelekea chumbani. Baada ya kumuweka juu ya kitanda, alimkandamiza kwa kasi na kumbusu.
Muda si muda Lisa alijitambua na kumsukuma. "Hapana. Siwezi kufanya hivi.”

Alvin alimtazama kwa macho mekundu. “Kwa nini?”

Moyo wa Lisa ulimuuma, akakwepa macho yake. “Mimi ni mchumba wa Kelvin. Ikizingatiwa kuwa amejinyima mengi kwa ajili yangu, siwezi kumuumiza. Ingawa nataka kulipiza kisasi, sitaki kutumiwa kama chombo ili kulipiza kisasi.”

Damu ya Alvin taratibu ikawa barafu. Alimtazama kwa huzuni kwa kile kilichoonekana kama mshangao wa kukata tamaa. Ghafla, alitoa kicheko dhaifu. “Potelea mbali.” Ghafla alimsukuma hadi sakafuni huku hewa ya uadui ikitoka kwenye uso wake. Lisa huku akiyazuia machozi yake, alivaa nguo zake haraka na kutoka nje ya chumba hicho.

“Lisa, hii ndiyo nafasi ya mwisho ninayokupa. Utajuta.” Alvin alimtazama kama shetani. Baada ya kutetemeka, Lisa aliondoka Oasis bila kugeuza kichwa chake.

Alirudi nyumbani kwa Ngosha akiwa na wasiwasi, akagundua kuwa vitu vyote vya chumbani kwake vilikuwa vimetupwa nje na vimetawanyika kwenye nyasi. Nina na Melanie walisimama mlangoni kwa kuridhika. “Toa vitu vyako na upotee. Haukaribishwi hapa.”

Lisa alikunja ngumi. “Hii ni nyumba ya baba yangu. Huna haki ya kunifukuza.”

“Utani ulioje. Mimi ni mke halali wa Joel. Nyumba hii kwa kiasi fulani ni mali yangu. Huwezi kuendelea kukaa hapa bila kibali changu.”

Nina alionyesha mtazamo wa kiburi. “Ulifikiri unaweza kumfanya Joel anitaliki kwa sababu ya ile ajali ndogo? Endelea kuota."

Lisa akatoa simu yake kumpigia Joel. Simu iliunganishwa, lakini hakuna aliyejibu.

“Acha kupiga simu. Mzee Ngosha anamsomesha Joel kwa sasa,” Nina alimdhihaki, “Huoni? Mzee Ngosha amekubaliana na wazo la kukufukuza pia, kwa hivyo hakuna kitu Joel anaweza kufanya juu yake.”

“Umesikia? Fanya haraka upotee basi.” Melanie hata alipiga teke nguo zake zilizoanguka chini.

Lisa alipunguza hasira yake na kuingiza vitu vyake kwenye sanduku lake kimoja baada ya kingine. Ni yeye tu aliyejua jinsi alivyokuwa na hasira ndani ya moyo wake. Angewalipa kwa kumdhalilisha mapema au baadaye.

Hata hivyo, kabla Lisa hajaweka vitu vyake vyote, Melanie alichukua maji machafu na kummwagia moja kwa moja. Vitu vyake vyote vikalowa kabisa.

“Lo, samahani. Nilikuwa napanga tu kumwaga maji machafu pembeni bahati mbaya nikakumwagia.”

Melanie alipokuwa akifurahia hali yake, Lisa alidhihaki. "Sasa unajishaua kwa kuridhika kwa sababu tu unaungwa mkono na familia ya Kimaro. Lakini umewahi kufikiria kuwa Alvin anaweza kukuacha siku moja?"

Usemi wa Melanie ulibadilika sana. “Wewe ni bullsh*t nini? Alvin atanioa hivi karibuni.”

"Natumai." Lisa aliuma mdomo kwa kejeli. Kwa kuzingatia kwamba Alvin alikuwa ameeleza wazi nia yake ya kurudiana naye muda si mrefu, alifikiri kwamba hakuwa na hisia na Melanie.

Lisa alipomaliza tu kuongea alibeba vitu vyake na kuondoka bila kuwapa Nina na Melanie nafasi ya kuendelea kumdhihaki. Kwa kuwa hakuwa na mahali pa kukaa Nairobi, hakuwa na budi ila kukaa katika hoteli ya nyota tano iliyokuwa karibu.

Usiku Joel alimpigia simu kwa haraka. "Lisa, kwanini umetoka nyumbani?"

“Baba, hujui kwamba nimefukuzwa?”

"Nini?" Joel alipandwa na hasira. "Damn, Nina ni mtu mbaya sana! Nitashughulika naye. Uko wapi? Ngoja nije nikuchukue sasa hivi.”

"Hakuna haja. Nitakaa nje kwa muda huu,” Lisa alijibu kinyonge, “Sasa kwa kuwa Nina na Melanie wana Alvin Kimaro akiwaunga mkono, ninaogopa hawatakujali. Zaidi ya hayo, Babu anachukua upande wao pia. Nikirudi nyumbani, badala yake niitakuwa vurugu.”

Joel aliendelea kujilaumu. "Ni bure kwangu kukuacha ukiteseka, Lisa."

“Usijali, baba. Hii ni ya muda tu. Ninaamini kila kitu kitakuwa sawa,” Lisa alijibu kwa huzuni huku akitazama nje ya dirisha.

Siku inayofuata, baada ya kuamshwa na simu yake, Lisa alikimbilia kwenye chumba cha mikutano ofisini. Meneja Mkuu Ngololo alisema kwa wasiwasi, "Mwenyekiti Jones, ingawa shamba la Nairobi limeidhinishwa, tuna matatizo na leseni ya kuanzisha biashara huko Kenya."

"Ulijaribu kutumia njia za chinichini?" Lisa akasugua nyusi zake.

“Ndiyo, lakini imeonekana kutozaa matunda.” Meneja Mkuu Ngololo alilazimisha tabasamu. “Hapo awali tulikubaliana. Lakini ghafla walibadilisha mawazo yao. Walisema kuna mzozo juu ya ardhi yetu na kiwanja kilicho jirani yetu.”

Meneja Lomeo kutoka idara ya uhandisi aliuliza, "Je, tumemkosea mtu yeyote huko Nairobi, Mwenyekiti Jones?"

Sura ya:175

Lisa alikumbuka jinsi Alvin alivyozungumza wakati anaondoka jana yake. Alihisi likuwa ni kazi yake.
Meneja Mkuu Ngololo aliongeza, “Vilevile kampuni ya KIM international wameondoa hisa zao zote ghafla kutoka kwenye mtaji wa kampuni. Mtaji wetu sasa unayumba. Ikiwa hatutapata pesa za kunyanyua mtaji haraka iwezekanavyo, mnyororo wetu wa biashara utakatika na kampuni yetu itaachwa juu ya kuti kavu. Ikiwa ni hivyo, kampuni inaweza kufilisika.”

Lisa alishangaa sana lakini hakuwa na haja ya kuilaumu KIM International. “Nitatafuta njia ya kutokea,” Lisa alisita kabla hajajibu.

Baada ya kikao kumalizika, alienda ofisini kumpigia Alvin na kugundua kuwa alikuwa ameifungia namba yake. Alitoa kicheko cha uchungu. Inavyoonekana, alikuwa amemkosea. Hakuwa na la kufanya zaidi ya kumuomba Joel msaada.

Baada ya Joeli kuulizia jambo hilo aliona ni ajabu. “Lisa, umemkosea nani? Hata mimi nimeshindwa kukusaidia wakati huu. Nina hakika hii haihusiki na familia ya Mahewa.”

“Sijui hata ni nani nimemkosea. Ngoja nijaribu kukumbuka.” Lisa alikata simu akiwa ameduwaa. Aliingiwa na wazo la kumwomba Joel kuwekeza mtaji katika kampuni ili kutatua suala la mtaji wa kufanyia kazi, lakini alikumbuka kampuni ya Ngosha haikuwa ya Joel pekee. Kuwekeza zaidi ya makumi ya mabilioni ya shilingi kungehitaji idhini ya Mzee Ngosha. Hata hivyo, Mzee Ngosha bila shaka angekataa ombi hilo.

Kwa bahati nzuri, Chris Maganga aliingia ofisini na kuwasiliana na Lisa mchana ule kwa njia ya video. Alikuwa amesikia mwenendo mbaya wa kampuni. "Lisa, nimesikitishwa na kitendo cha cha KIM International kuondoa hisa zao ghafla na kuathiri mtaji wa kampuni. Hapa kuna shilingi bilioni hamsini naongeza kama hisa zangu kwenye mtaji wa kuendeshea biashara za kampuni. Zinaweza kuwa na uwezo wa kusaidia kampuni kwa wakati huu.”

“Mjomba Chris, asante sana!” Lisa aliguswa. Katika hali kama hiyo, kila mkurugenzi mwingine alikuwa akikosoa tu mambo na kujitetea. Hawakuwa tayari kuchangia pesa yoyote.

"Mama yako aliijenga kampuni hii kwa uchungu. Sitaki kuiona ikifungwa.” Chris akashusha pumzi ndefu. "Hata hivyo, umegundua nini juu ya kifo cha mama yako?"

Baada ya kufikiria kidogo, Lisa alijibu, “Nadhani kifo cha mama yangu hakina uhusiano wowote na familia ya Mahewa. Niligongana na Farres hapo awali na hakuwa na wasiwasi hata kidogo juu ya tukio la kujaribu kuniua kwa ajali ya gari. Lakini nilipotaja kifo cha mama yangu, alionekana kushangaa kana kwamba haelewi chochote.”

“Hiyo ni ajabu. Kabla ya mama yako kufariki, simu yake ya mwisho ilitoka Nairobi.” Chris alihisi kuchanganyikiwa. "Kuna mtu mwingine basi nyuma ya tukio."

Lisa alisugua chake ake. Akili yake ilikuwa imechanganyikiwa.
Chris aliweza kujua kwamba alikuwa amechoka. Baada ya muda, alisema kwa huruma, “Mfadhaiko unaoupata sasa ni mwingi sana kwako katika umri huu mdogo. Ikiwa huwezi kuishughulikia, rudi tu Dar es Salaam. Sawa?”

Lisa alikuwa katika butwaa. Nyakati fulani, alihisi kwamba hakupaswa kwenda Nairobi hata kidogo. Hapo awali, alifikiri kwamba uhusiano wake na baba yake ungeboreka, jambo ambalo lingemwezesha kupata ushindi hatua kwa hatua. Lakini, familia ya Mahewa ilitegemea familia ya Kimaro ambayo waliitegemea kama msaada wao mkubwa. Kweli, alikuwa amechoka!

Alikuwa akishughulikia mgogoro huo siku kadhaa zilizofuata lakini, pande husika zilikataa kukutana naye. Alipotoka nje ya ofisi ya ardhi, alikutana na Jack Kimaro. Jack alipigwa na butwaa kumuona. Alionekana kuwa hakuwa amelala vizuri siku chache zilizopita.

“Unaonekana umechoka, Bi Jones, unakabiliwa na shida yoyote?" Jack aliuliza huku akitabasamu. Muonekano wake ulikuwa tofauti na Alvin. Alvin alikuwa na dharau, kiburi na kujisikia. Kwa kulinganisha, kulikuwa na haiba ya umaridadi juu ya Jack. Jack alikuwa na sifa laini, na alionekana mpole alipotabasamu.

“Ndiyo. Kuna tatizo kuhusu ardhi ya kampuni yangu.” Lisa aliitikia kwa unyonge.

Jack aliinua kichwa chake kwa mshangao. “Ninaelewana na kamishna wa ardhi hapa. Labda naweza kukusaidia?”

Lisa alipigwa na butwaa. Hakuwa amepanga kumuomba msaada. Baada ya yote, alikuwa sehemu ya familia ya Kimaro, kwa hivyo, alionekana kuachwa njia panda.

"Hata hivyo niikikusaidia, basi utaniwia fadhila." Jack alimkonyeza huku akitabasamu.

Lisa alilazimisha tabasamu. "Kwa kuzingatia hali yangu ya chini, huenda nisiweze kurudisha fadhila, Bwana Kimaro."

"Inategemeana. Kwa kuzingatia kwamba uliweza kuweka utulivu wako hata ulipokaribia kufa, nadhani unaweza kuahidi." Jack ghafla alimtazama na kutabasamu. “Ninaelewa jinsi unavyohisi hivi sasa. Hali yetu ni sawa. Katika familia ya Kimaro, watu kila mara huniita mwana haramu ambaye niliharibu familia ya Alvin na baba yake.”


Lisa alipigwa na butwaa. Kwa kweli hakumpenda Jack wakati huo, lakini, wote wawili walikuwa katika hali sawa sasa. “Hupaswi kuhangaika kuhusu hilo, bwana Kimaro. Hatukupata kuchagua asili zetu. Zaidi ya hayo, maisha yako ni ya furaha zaidi kuliko yangu. Wazazi wako wameoana.”

“Ndiyo. Hata hivyo, watu wengine huwa wananilinganisha na kaka yangu. Siku zote ninaishi katika kivuli chake.” Jack alieleza kwa masikitiko. "Njoo, nitakupeleka kwa kamishna."

“… Asante, Bwana Kimaro.”

Lisa alimfuata baada ya kusita kwa muda. Ikizingatiwa kuwa kulikuwa na wafanyikazi zaidi ya 10,000 katika kampuni yake waliotegemea maisha yao kupitia ajira za kampuni hiyo, asingeweza kuachia nafasi hiyo ya kuikomboa kampuni.

Siku tatu baadaye, Alvin alirejea Nairobi baada ya mkutano wake nje ya nchi kumalizika. Mara tu ndege ilipotua kwenye uwanja wa ndege, Hans alimripotia kuhusu hali ya kampuni. Alvin alisikiza kimya kimya. Baada ya kuingia ndani ya gari, Hans alimwambia kwa umbea, "Mgogoro wa leseni ya ardhi ya Mawenzi umetatuliwa."

Alvin akavua tai shingoni. “Nani alimsaidia?”

"Jack Kimaro." Hans alitoboa siri.

Kulikuwa na muda wa ukimya. Hans alihisi woga alipogundua kwamba Alvin alikuwa akikunja mdomo wake maridadi. "Jack anapanga kufanya nini?"

"Labda ni kwa sababu Jack amegundua kuwa una uhusiano na Lisa?" Hans aliuliza kwa mashaka.

“Nadhani amekuwa mvivu sana siku hizi. Mradi wa kiwanda chetu k huko Sudani Kusini unasuasua. Nitampeleka huko ashughulikie,” Alvin alisema kwa huzuni.

Hans aliingiwa na huruma. "Suala la usalama katika Sudan Kusini limekuwa na utata sana hivi karibuni, huko si salama sana. Bibi Kimaro anaweza kukasirishwa na hilo.”

"Atakwenda atake asitake." Kwa kutojali kabisa, Alvin alicheka. "Kwa hiyo, Lisa ana matumaini kwamba Mawenzi iko salama na anaweza kuishi maisha yake bila wasiwasi? Kwa bahati mbaya, ana pointi nyingi dhaifu.”

Akiwa amekunja uso wake, Hans alihisi kwamba Alvin alikuwa akipandisha wazimu. Kwa kumwondoa Jack Kimaro, kungezuka ghasia kubwa ndani ya KIM international wakati palikuwa shwari kabisa kipindi hayupo.

Siku ambayo ujenzi katika ardhi ya Mawenzi huko Nairobi ulipoanza, Lisa alimpigia simu Jack kwa njia ya whatsapp baada kumkos kwenye simu ya kawaida. “Asante kwa msaada wako mapema, Bwana Kimaro. Ningependa kukukirimu kwa chakula kama ishara ya shukrani yangu.”

"Sitaweza kuungana nawe Lisa." Jack alitoa kicheko cha uchungu. “Nimefika Jubah leo. Kaka yangu aliniagiza kuja Sudan Kusini kufuatilia mradi fulani.”

Lisa alishtuka. “Lakini nilisikia Sudan Kusini kwa sasa iko kwenye fujo. Kuna mzozo unaoendelea kati ya maeneo ya kusini na kaskazini mwa nchi. Wageni wengi huwa wanajiingiza kwenye matatizo makubwa huko. Inawezekanaje Alvin akakufanya uende huko?"

Jack alinyamaza kwa dakika moja kisha akajibu, “Hata mimi sina uhakika sana. Ghafla alipandwa na hasira, lakini hata hivyo, hiyo sio kawaida. Nadhani amekuwa akinichukia kwa muda mrefu sana.”

Lisa alihisi kurusha matusi. Alijua kwa hakika kwamba Alvin alikuwa amegundua kwamba Jack alimsaidia.

“Usijali. Mama yangu atapata njia ya kunirudisha haraka iwezekanavyo,” Jack alisema kwa uchungu.

“Sawa. Nitakuandalia chakula ukirudi basi.” Lisa akakata simu.

Usiku, Kelvin alimpeleka kwenye mkahawa wa kichaga ulioko Nairobi kwa chakula cha jioni. Kelvin hakusema neno katika safari yote. Haijalishi Lisa alikuwa mwepesi kiasi gani, aliweza kuhisi kwamba hakuwa na furaha. "Nini tatizo? Nani amekukera?”

“Ulihama nyumbani kwa baba yako na kukaa hotelini peke yako bila kunitaarifu. Hukunifahamisha kuhusu tatizo katika kampuni yako pia.” Kelvin alikunja uso kwa hasira. “Lisa, mimi ni mchumba wako, lakini mbona unanichukulia kama mtu wa pembeni?”

Lisa alisita kwa muda na kusema, “Una mambo mengi ya kushughulikia katika kampuni yako pia. Sikutaka kukusumbua na matatizo yangu—”

"Bila kujali idadi ya mambo yanayoendelea katika kampuni yangu, ninaweza kuyashughulikia. Kwa kuwa wewe ni mpenzi wangu, ni jukumu langu kukusaidia kadri niwezavyo. Je, wanaume hawatakiwi kushiriki mzigo wa wanawake wao?” Kelvin alikuwa na sura ya kuchukiza kuliko Lisa alivyowahi kumuona. “Najua sina nguvu katika sehemu kama Nairobi, lakini nataka ujue kwamba haijalishi nini kitatokea, nitafanya niwezavyo kukusaidia. Lisa, unanifanya nijione sifai sana.”

“Samahani.” Lisa aliomba msamaha. “Sitafanya hivyo tena.”

"Ikiwa kweli umemaanisha kuomba msamaha, hama kwenye hoteli na uje ukae nami." Kelvin alimshika mkono. "Nimenunua jumba la kifahari hapa Nairobi, ambalo ni sawa kwa sisi sote kukaa."

Lisa alipinga wazo hilo bila kujua. Awali alimsababisha apoteze figo kwa sababu alikuwa akimkinga na hatari ya kifo, sasa hakutaka kumsababishia kupoteza kabisa maisha yake.

TUKUTANE KURASA 176-180

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI......... LISA
KURASA..... 176-180

Sura ya:176

Wakati huo huo, simu ya Kelvin ikaita. Baada ya kuipokea simu ile, sura yake ilibadilika sana. “Nakuja sasa hivi.”

“Lisa, nina shughuli za haraka za kushughulikia. Sitaweza kukusindikiza usiku wa leo.” Kwa hayo, Kelvin aliinuka na kuondoka kwa haraka.

Lisa alipigwa na butwaa. Ingawa alikuwa amemfahamu kitambo, hii ilikuwa mara yake ya kwanza kumuona akiwa katika hali ya wasiwasi.

Baada ya kurejea hotelini, alifahamu kupitia televisheni kwamba kulikuwa na tatizo katika dawa zinazozalishwa na Golden Corporation. Kwa sasa, Kelvin alikuwa anazuiliwa.

Habari hizo zilimshangaza sana. Haraka alipeleka wakili kwenye kituo cha polisi. Hata hivyo, wakili alishindwa kumtoa Kelvin nje. Tukio hili lilikuwa linajulikana sana. Ilimkumbusha Lisa wakati alipokamatwa huko Dar es Salaam. Tofauti pekee ilikuwa kwamba mtu huyo alikuwa Kelvin wakati huu.

Wakili alisema, “Bi Jones, Bwana Mushi lazima atakuwa amemkosea mtu mzito sana. Angeweza kuachiliwa bila shida kwa kesi kama hiyo. Kwa vile polisi wanakataa kumwachilia, siwezi kufanya lolote.”

Sasa kulikuwa hakuna kiongozi katika kampuni ya Golden Corporation, na ujenzi ulikuwa umesimama. Ikiwa Kelvin angeendelea kubaki katika kituo hicho, Golden Corporation ingeharibiwa ndani ya wiki moja.

Miguu ya Lisa iligeuka kuwa mlenda. Alikuwa ameelewa kila kitu. Tukio hilo hakika lilihusiana na Alvin. Alifikiri kwamba Mawenzi ilikuwa salama na alikuwa amefanikiwa kuepuka hatari. Badala yake, alikuwa amewaingiza Jack na Kelvin kwenye matatizo.

Hakuwahi kumchukia mwanaume kwa undani kiasi hicho. Alvin alikuwa mnyama kweli. Wakati huo, alijuta sana kumchokoza shetani. Alifahamu vyema nia ya Alvin. Lakini kama angekubaliana naye, angekabiliana vipi na Kelvin wakati alipokuwa nje baadaye?

Lisa alipata shida kupata usingizi usiku mzima. Watu wa familia ya Mushi waliendelea kumpigia simu. Akiwa katika kilio chake, Bibi Mushi alisema, “Lisa, lazima umwokoe Kelvin. Unaweza kumwomba baba yako msaada. Ikiwa ataendelea kuzuiliwa, uzee wetu utaishia pabaya sana.”

“Lisa, Kelvin ana figo moja tu. AAtaweza kufia katika kituo cha kizuizini.” Mzee Mushi naye alilalamika kwa uchungu.

“…Usijali. Nitapata njia ya kutokea.” Lisa aliamuhidi Bi Mushi kwa uchungu.

Kulipopambazuka, alielekea ofisi ya KIM International kwa gari.
Alipomkaribia dada wa mapokezi, mlinzi huyo alimfukuza.

“Unafikiri wewe ni nani? Hakuna takataka yeyote kama wewe inyoruhusiwa kukutana na bosi wetu. Ondoka sasa hivi.” Mlinzi alifunga mlango mara moja.

Lisa hakuwa na la kufanya zaidi ya kusubiri nje. Ni mpaka anga ilipoingia giza tu ndipo hatimaye alimwona Alvin akiendesha gari lake kutoka kwenye maegesho ya magari. Mara moja aliendesha gari lake ili kumfukuzia.

Dereva katika Rolls-Royce alimkumbusha Alvin, “Bwana Kimaro, kuna gari jeupe linalotufuata.” Alvin, ambaye alikuwa akipita hati, alinyamaza kidogo kisha akajibu bila kujali, “Mwache atufuate.”

Nusu saa baadaye, gari lilifika chini ya jumba la klabu. “Simama hapa,” Alvin alisema huku akifunga hati.

Dereva alikuwa ameduwaa. "Lakini huwa unaingia kupitia lifti ya maegesho baada ya kuegesha gari."

Swali la dereva halikupata majibu yoyote. Kwa namna fulani, alianza kuogopa na hatimaye akajua kwamba alikuwa amekwenda mbali sana. Mara moja akaegesha gari. Alvin alifungua mlango moja kwa moja na kutoka nje. Alipoelekea kwenye lango kuu la kuingilia, Lisa alikimbia kama radi na kumzuia.

“Unataka kufanya nini?” Mlinzi alimzuia alipokuwa mbele ya Alvin. Alikuwa katika hali ya tahadhari.

“Alvin, nataka kuwa na neno nawe.” Macho meusi ya Lisa yakatua kwa Alvin ambaye mikono yake iliingizwa mfukoni. Alimtazama Lisa bila huruma kana kwamba alikuwa mgeni.

Kwa sababu mlinzi huyo hakuwahi kumuona Lisa, moja kwa moja alimsogelea na kumsukuma chini kwa fujo huku akijaribu kuteka hisia za Alvin. Kwa sura ya kauzu, Alvin alinyanyua miguu yake mirefu na kuelekea juu.

Lisa huku akiwa amejizuia na maumivu, alisimama na kumfuata. "Alvin, nitakubali madai yako yote hapo awali mradi tu utaacha kufanya mambo kuwa magumu kwa Kelvin na kampuni yake."

Umbo lake refu lilisimama. Hatimaye Alvin aligeuka na kumtazama. Aligeuza mdomo wake kuwa tabasamu la kuudhi. "Sijui hata ni madai gani unayozungumzia."

Lisa alipigwa na butwaa. Muda kidogo, uso wake ulibadilika rangi.
Hakuweza kusema kwa nje kukubali kwake kulala naye. Ukiweka kando ukweli kwamba kwa sasa walikuwa chini ya macho ya umma, hata asingefanya hivyo wakiwa wao wawili tu.

Baada ya kutafakari, aligundua kuwa usiku huo hakudai chochote. Alikuwa amempa chaguzi tu. Aliuma mdomo na kuangusha macho yake. Sauti yake ya chini na ya kishindo ilisikika kwa kiasi. “Bwana Kimaro, nilikuwa bado sijakomaa wakati huo. Wewe ni mtu hodari, kwa hivyo tafadhali usikate tamaa."

“Kwa hiyo…?” Alvin aligeuka na kupiga hatua mbili mbele. Alisimama mbele yake, macho yake yakionyesha kejeli. “Unafikiri kila kitu kitakuwa sawa nikilala na wewe kwa vile umeonyesha majuto na hatia yako?” Kufuatia ulegevu wake, Lisa uso wake ulijawa na aibu na alikuwa akitokwa na machozi.

“Unaonekana mzuri wakati uko kwenye hatihati ya machozi. Inaamsha huruma yangu." Alvin akamshika kidevu chake taratibu. “Nitakupa nafasi nyingine. Twende.”

Mara baada ya kumaliza kuongea, aliingia kwenye jumba la klabu.
Licha ya kutojua mpango wa Alvin, Lisa alimfuata ndani ya jumba hilo kwani alijua kuwa hiyo ndiyo nafasi pekee ya kumuokoa Kelvin. Kisha akapanda lifti.

Mlango wa chumba cha faragha ulipofunguliwa, walionekana wanaume watano hadi sita wakiwa wamekaa ndani. Baadhi walikuwa wanene, wengine wembamba, na wengine walikuwa
Wazee. Wale watu walipogundua ujio wa Alvin, mara wakasimama na kumtazama.

"Bwana Kimaro, hatimaye uko hapa." Mwanaume mwenye tumbo lenye kitambi alishindwa kuacha kumtazama Lisa mara macho yake yalipotua kwake. “Bwana Kimaro, hata ulileta mrembo mzuri pamoja nawe. Unatutia wivu.”

“Bwana Gorman, si lazima uwe na wivu. Kwa kweli, nilikuletea mrembo huyu kimakusudi.” Alvin alitabasamu kwa unyonge.

Hata hivyo, kauli hiyo ilikuja kama pigo kwa Lisa. Alimkodolea macho Alvin ambaye alikuwa akiongea kwa furaha. Angewezaje kumtendea hivi?

“Kweli?” Bwana Gorman alijawa na furaha.

“Ndiyo. Napenda kukushukuru kwa mradi wetu wa Uganda. Kwa wewe kutembelea Nairobi wakati huu, nimeona ni tukio maalum. Hakika imenilazimu kukushukuru.”

Alvin bila kujali alimwonyesha Lisa kwa macho yake. "Nenda na ufuatane na Bwana Gorman sasa."

“Wewe…” Mdomo wa Lisa ulibadilika rangi na kutetemeka. Ni wazi kwamba bado hakuweza kukubaliana na hali hiyo.

Alvin alimsogelea na kusema kando ya sikio lake kwa sauti ya kishetani, "Potea machoni kwangu ikiwa huwezi kukubali."

Pamoja na hayo, alikaa kwenye kiti cha heshima. Kuangalia umbo lake refu, Lisa alihisi kama tundu limekatwa kifuani mwake na lilikuwa likichuruzika damu.

Akiwa njiani kwenda pale, alihisi kuwa anamjali bila kujali tabia yake. Alifikiri kwamba alikuwa akijaribu tu kumlazimisha kuwa naye tena. Ukizingatia kila kitu kilichokuwa kikitokea kwa wakati huo, sasa alikuwa na akili timamu. Ikiwa alikuwa anampenda kweli, asingekuwa akimharibu na kumsukuma shimoni.

Wakati huo, alihisi hamu kubwa ya kumkimbia mwanaume huyo kwa kadri awezavyo. Baada ya kusema hivyo, nini kingetokea kwa Kelvin ikiwa angeondoka? Je, angefungwa milele? Dhamiri yake ingemsumbua sana ikiwa angeondoka sasa.

"Halo, Bwana Gorman." Lisa alijitahidi kutoa tabasamu la kutisha na kukaa kando ya mwanamume yule.

“Haha, asante, Bwana Kimaro.” Bwana Gorman alimkumbatia Lisa moja kwa moja.

Wakati Lisa aliponusa harufu kali ya pombe na sigara juu yake, ilikuwa karibu atapike. Hata hivyo, hakuwa na la kufanya zaidi ya kuguna na kuvumilia huku akisaga meno.

Sura ya:177

Alvin, ambaye alikuwa ameketi mkabala na Lisa, aliyafumba macho yake bila kujua. Alikaribia kuponda glasi ya mvinyo mkononi mwake kama matokeo ya hasira yake.

Jamani! Hapo awali alikusudia kumfundisha tu somo na kumtisha. Alipomwona Gorman akimgusa hata hivyo, kwa namna fulani alihisi kama kukata mikono yake. Lakini, sasa haukuwa wakati wa Alvin kuruka kwa hasira. Kwa kuwa alikuwa akimbembeleza sana Lisa, alipanga kumpa somo. Hakuweza kumuokoa hadi aingie katika hali ya kukata tamaa ili ajifunze somo lake na kunyenyekea kwake.

"Nimefurahi kuwa umependa," Alvin alijibu bila kujali. "Nipe toast Bwana Gorman."

Katika hali ya kukata tamaa, Lisa hakuweza kuhisi hasira wala huzuni machoni pake. Kwa mwonekano wa mambo, asingeweza kuepuka hali hiyo usiku huo.

Lisa bila kupenda alikunywa pombe na kumaliza chupa nzima. Kwa kweli, alikuwa na uvumilivu wa juu wa pombe. Hata hivyo, upesi alipatwa na kizunguzungu, labda kwa sababu alikuwa na jambo fulani akilini mwake usiku huo.

Alifikiri kwamba chakula cha jioni kingedumu kwa muda mrefu. Ajabu ni kwamba Alvin aliinuka na kuvaa suti yake ilipofika saa mbili tu usiku. "Natumai utakuwa na furaha usiku wa leo, Bwana Gorman." Kwa hayo, aliondoka bila kuangalia nyuma.

Lisa aliutazama mgongo wake ukitoweka mbele ya lifti. Hakugeuza kichwa hata mara moja. Wakati huo, hatimaye alielewa hisia ya mshtuko wa moyo na jinsi ilivyohisi kuachwa kwenye shimo la jehanamu. Hata mapenzi kidogo aliyokuwa nayo kwake sasa yalikuwa yametoweka.

"Twende sasa tukaburudike usiku mzima." Gorman alimkumbatia Lisa ambaye alifanana na kikaragosi asiye na roho muda huo kutokana na mawazo.

Hakuwa na uhakika jinsi alivyopanda ghorofani pia. Alipoingia chumbani, aliutazama uso mnene wa Gorman wenye shauku. Alijilazimisha kumkubalia, lakini alijawa na karaha. “Ngoja kwanza, Bwana Gorman Ngoja nioge kwanza.”

“Una harufu nzuri sana. Hakuna haja ya kuoga,” Gorman alijibu kwa kucheka.

"Nataka kujiweka safi zaidi na kukupa usiku mzuri, Bwana Gorman," Lisa alisema bila kupenda.

“Tsk, wewe ni mzungumzaji mtamu sana. Sawa, nitakusubiri." Gorman alibana uso wake.

Baada ya kuingia bafuni, Lisa alioga kwa muda mrefu sana huku akiwaza. Hakujisikia kuondoka bafuni, aliacha maji yaendelee kumwagika kwenye kichwa chake hadi chini ya mwili wake. Kwa mshangao wake, Gorman hakuwa akimpigia hata kelele za kumharakisha kutoka bafuni. Alichukua muda wake mtamu akiwa bafuni na akatoka baada ya dakika 50 baadaye.

Alishtuka kumwona Gorman akiwa anakoroma huku kakumbatia mto kitandani. Kuuona tu mwili wake mnene kulimfanya atake kutapika pombe zote alizokunywa usiku ule.

"Inachukiza, huh?" Ghafla, sauti nzito ya mwanamume ikasikika kutoka kwenye kibaraza.
Aligeuza kichwa chake na kumgundua Alvin akiwa amesimama kwenye kibaraza cha chumba. Umbo lake refu, lililofanana na mti wa msonobari ulio wima, lilionekana nusu gizani. Macho yake meusi yalikuwa kama shimo.

Mwanaume huyo akamsogelea taratibu. Alimtazama nywele zake zilizochafuka, ndefu mabegani mwake ambazo zilikuwa zimekaushwa tu. Uso wake ulikuwa umepauka kiasi kwamba ulikuwa umepoteza rangi. Inavyoonekana, macho yake yalionyesha kwamba alikuwa amepitia mapambano na maumivu mengi na sasa aliongozwa na kukata tamaa. Pamoja na sura kama hiyo, bado alionekana mrembo zaidi.

"Alvin, unapanga kufanya nini?" Lisa alikaribia kupatwa na wazimu kutokana na kuteswa naye kusikoisha. Alikiri kwamba alifanikiwa kumfanya ajute kwa kumkataa hapo awali. Pia alikuwa amemfanya apate hali ya woga isiyo na kifani.

“Lisa, nataka uelewe kuwa ni heshima kwako kwa mimi kuonyesha nia na wewe. Usiwe mtu wa kukosa shukrani tena,” Alvin alionya bila kujali.

Lisa alianguka na kusema kwa sauti kuu, "Wewe ni shetani, Alvin!"

“Ndiyo, kimsingi mimi ni shetani. Sasa, ninakupa nafasi ya mwisho. Ni juu yako kuamua,” Alvin alidhihaki. Akageuka na kuelekea mlangoni.

Lisa alilazimisha tabasamu. Kwa kweli hakuwa na chaguo jingine. Ikilinganishwa na yule jamaa mnene ambaye tayari angeweza kuwa baba yake kulingana na umri wake, angependelea kulala na Alvin.

“Sitaki kulala naye.” Lisa alimfuata Alvin na kumkumbatia kiunoni bila aibu.

Alvin alitazama nyuma bila kujali na kumtupia jicho. Alivuta mikono yake kando na kuamuru, "twende nyumbani kwangu." Lisa alimfuata nyuma yake kimya.

Kufika Oasis, mara Alvin akaingia chumbani na kuketi kitandani. Taa zilizo juu yake zilionyesha sifa zake bora.

“Kwanini umesimama hapo kama mlingoti? Unategemea nikufundishe la kufanya?” Aliinua uso wake na kugeuza mdomo wake kuwa tabasamu baya.

Lisa alimsogelea akiwa amekunja uso. Akitetemeka, akaanza kumbusu midomo yake. Hakuna kitu ambacho Alvin alikuwa akipenda kufanya kama kunyonya mdomo wa Lisa, siku zote aliona kwamba una radha nzuri sana. Mkono wake mmoja ukiwa kwenye kisogo cha Lisa huku mwingine ukiwa kwenye kiuno chake, alimkandamiza taratibu na kuendelea limbusu Lisa aliyekuwa anahema taratibu lakini kwa sauti nzito. Alvin alitumia kama dakika kumi nzima kunyonya tu mdomo na ulimi wa Lisa mpaka kinywa chake kilipokaukiwa mate.

Hakuwa na haraka Alvin, alisafiri kituo baada ya kituo kama daladala na sasa akafika kifuani. Kifuacha Lisa kilikuwa kikipanda na kushuka taratibu na matiti yalikuwa yametuna na kujaa. Alvin hakuwa mchezaji sana hapo, baada ya kuyanyonya tu bila mpangilio kwa muda akahama hapo, ulimi wake ukitereza kama konokono kushuka chini kwenye kupitia kwenye kitovu, akifanya hivyo huku akiendelea kupunguza nguo mwilini mwa Lisa.

Alimtazama Lisa aliyekuwa amefumba macho yake kwa aibu. Hakuonekana kama amechukia au kufurahi, lakini ni wazi kuwa kulikuwa na hisia fulani za raha zikimchukua taratibu. Mara bada ya Lisa kubaki mtupu kabisa, Alvin alishika chuchu zake, kila mkono ukishika ya upande wake na kufanya kuzungusha taratibu kama anafungua nati. Lakini ulimi wake wa moto ulikuwa unamtekenya Lisa kwenye kis*mi chake. Alikuwa akikigonga tu na kukizungukiazungukia kwa ncha ya ulimi na wakati mwingine akawa anakinyonya. Hapo sasa Lisa alipandwa na hisia nyingi mchangnyiko mpaka akaanza kuongea maneno fulani ya mshawasha.

“Alvlisaaa…. aaaahssss….mwenzio sijawahi bwana naogopa….yaaani unavyonifanyia hivi halafu uje uniache kweli…nitaishije mwenzako? Aaah ninyonye hapo hapo…kandamiza kidogo eeheeee…aaaahh…”

Alvin alikuwa kampoteza kabisa Lisa kwenye hisia za utamu ambao hakuwa amewahi kuufikiria kabisa. Lisa alijilegeza na kujiachia kabisa huku akibwajabwaja maneno yaliyomtoka bila kupenda. Baada kama ya dakika kumi hivi za uvumiliu wa Alvin, Lisa alionekana kukakamaa mwili mzima huku akikikandamiza kwa nguvu kichwa cha Alvin pale kwenye pachipachi lake. Alvin alisikia kimiminika fulani kikiujaza mdomo wake, haieleweki ni mkojo a kawaida au mkojo gani ambao Lisa alikuwa amekojoa lakini bila shaka ni mkojo ulioambata na raha sana kwani kwani Lisa aliachia pumzi nzito na ukelele usioeleweka.

Baada ya Lisa kukojoa kama mara tatu hivi alionekana kuchoka kabisa. Hakutaka tena Alvin aendelee kumnyonya. Alvin alimuacha lakini akatawanya miguu yake na kuanza kmnyonya huku akimpuliza tu taratibu kwenye mk*ndu wake. Baada ya kumpuliza kama dakika tano hivi Lisa alijikuta anapitiwa na kausingizi kazito hatari.

Alvin alikuwa amefanikiwa kabisa kuiondoa hofu ya Lisa kwa sababu hakuwa na haraka wala papara. Lisa sasa alikuwa amerelax, mwili wake wote kauachia. Kila Alvin alipomsemesha alifumbua macho kidogo tu, akaongea visivyoeleweka na muda huo huo akapitiwa na usingizi tena.

Hata hivyo Alvin alipotaka tu kumwingilia taratibu, Lisa aliruka kwa hofu. Alvin alisumbuka kidogo kumweka sawa Lisa na mpaka unafikia muda mjeredi wake unapenya na kuingia kwenye chombo cha Lisa Lisa alikuwa kishakizunguka kitanda kama mara kumi hivi.

Kile alichotegemea hakukiona kikitokea kwa Lisa kama kilivyotokea kwa Sara. Kulikuwa na utando kidogo tu wa damu iliyozunguka kwenye mjeredi wake lakini hakuona damu iliyomwagika.


“Lisa Jones, yako wapi? Wewe mwenyewe ulisema kuwa kujawahi, lakini mbona hakuna chochote? Mbona hakuna damu? Ulikuwa unakataa nini kujawahi kulala na Kelvin?”
Badala ya kumwacha apumzike, Kelvin alimwandama Lisa kwa maneno makali yaliyosindikiza maumivu yake. Kwa kweli hakuwa na namna ya kumhakikishia kuwa hajawahi fufanya na hiyo ndiyo ilikuwa mara yake ya kwanza. Kwa masikitiko makubwa, Lisa alichagua kulala kimya bila kuongea chochote.

Baada ya kulala usiku wa manane, Alvin alichukua simu yake na kumpiga picha. Alimtumia Kelvin

Sura ya:178

Siku inayofuata, Lisa aliamka na kumkuta Alvin akiwa amekaa pembeni yake huku akivuta sigara. Alikuwa amevaa nguo za kulalia kwa uvivu. Katika mawazo ya tukio la jana yake usiku, Lisa alionekana kuwa na wasiwasi kidogo.

Alipousogeza mwili wake, Alvin aligeuka na kumtazama. Macho yao yalikutana. Alvin akaweka chini sigara na kuinama ili kugusa nywele zake ndefu nyeusi. “Huwa unaona aibu pia unapokuwa na Kelvin?”

Uso wa Lisa ukapoteza uchangamfu mara moja. Aliinua kichwa chake na kumtazama. Hasira zilimpanda kichwani wakati huo. "Kelvin na mimi hatujawahi kufanya hivyo!"

Alvin alikodoa macho yake. “Kweli? Siamini.” Alipomaliza kuongea tu, alisimama na kuelekea kwenye chumba cha kubadilishia nguo.
Jinsi Lisa alitamani kutumia mto kuvunja kichwa chake. Alikuwa amefanya nini?!

Dakika tano baadaye, Alvin alitoka nje akionekana kuwa mtulivu zaidi. Alimuacha Lisa akihema na kushangaa kana kwamba kilichomtokea usiku wa jana yake kilikuwa ni ndoto tu.

“Kifungua kinywa changu kiko wapi? Nenda ukaniandalie,” Alvin aliamuru kwa namna ya kujihesabia haki.

Lisa alibaki kimya. “Si ukubali kumwachia Kelvin kwanza? Nadhani wewe ni mtu wa neno lako na hutavunja ahadi yako, sivyo?
Alvin alikunja mdomo wake kwa tabasamu mbaya. “Unampenda Kelvin kweli, huh? Kwa kweli unakubali hata kuutoa mwili wako kwa ajili yake.”

"Vyovyote." Lisa alikuwa mvivu sana kueleza zaidi kwani hata hivyo hakuamini alichokisema.

Kumtaja kwake Kelvin kuliharibu hali ya uchangamfu aliyokuwa nayo Alvin tangu jana usiku. Alipiga teke mlango wa chumba hicho na kusema bila huruma, “Usijali, nitafanya kama nilivyokuahidi, lakini huruhusiwi kujumuika naye tena. Unatakiwa kuwa mtiifu na uwe mwanamke wangu kuanzia sasa, la sivyo ataozea jela wakati ujao.” Baada ya hayo, alishuka chini.

Tabasamu la uchungu likatanda usoni mwa Lisa. Hata bila yeye kumuonya, angeaibika sana kuwa na Kelvin tena. Aliacha kuwa na matumaini tena kuhusu mwenzi wake wa baadaye.

Baada ya kunawa, Lisa aliburuta mwili wake uliokuwa unauma chini kwenye ngazi. Alitembea hadi jikoni. Alipofungua jokofu, alishindwa cha kusema. "Hakuna kitu kingine ndani isipokuwa mayai. Unatarajia nikuandalie nini kwa ajili ya kifungua kinywa?"

“Nitakula mayai, basi." Alvin tayari alikuwa na njaa japo kwa kawaida alikuwa hana hamu ya kula.

Lisa alinyamaza kwa dakika moja. Kisha akatayarisha mayai mawili ya kukaanga na mayai manne ya kuchemsha. Wakati anakula mayai, Alvin alishangaa jinsi alivyoyatengeneza. Hata mayai ya kuchemsha yalionekana kuwa matamu.
Baada ya kumaliza mayai yote alihisi kama hajashoba. Kisha akasema, “Ulitayarisha mayai machache sana. Sijatosheka.”

Lisa alikosa la kusema. Lazima alikuwa kichaa. Nani angekula na mayai mengi asubuhi? Kula mayai kunaweza kuchangia cholesterol kubwa. “Sawa. vumilia tu kwa leo. Nitatayarisha chakula kitamu zaidi kesho.”

Alvin aliinuka na kutupa kadi nyeusi kwenye meza. "Utahamia kwenye mtaa mpya mchana huu. Nina ghorofa huko. Melanie na bibi yangu wanajua kuhusu mahali hapa, kwa hiyo haitakuwa rahisi kwako kukaa hapa.”

Kuangalia kadi, Lisa alilazimisha tabasamu. Alikuwa mpenzi wake wa siri sasa? Alidhihaki, “Ni baraka iliyoje kuzungukwa na wanawake, Alvin Kimaro.”

“Usinilaumu. Nilikupa chaguo la kupata mimba ya mtoto wangu na ningemtelekeza Melanie. Wewe ndiye uliyekataa.” Alvin alichukua koti lake na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Lisa alikaa kwenye kiti kwa muda wa nusu saa kabla ya kusimama na kuelekea kituo cha polisi. Akiwa njiani kwenda huko, alinunua kidonge cha kuzuia mimba na kumeza.

Kila kitu kilikwenda sawa wakati huu. Wakili alitumia takriban dakika kumi tu kumtoa Kelvin. Kelvin hakujeruhiwa. Alionekana mnyonge tu kwani alikuwa hajapata mapumziko ya kutosha ndani kutokana na wasiwasi mwingi.

“Samahani, Lisa. Nimekufanya uwe na wasiwasi juu yangu.” Kelvin alimwendea na kumkumbatia kwa nguvu.

“Nimefurahi kuwa hujambo.” Lisa alibaki tuli huku akihisi uchungu ndani kabisa. Kwa kweli hakujua jinsi ya kuanzisha tkuachana naye.

"Lisa usiniache, sawa?" Kelvin ghafla alisema kando ya sikio lake.
Koo la Lisa lilimuuma kidogo. Kwa akili yake, Kelvin alikuwa amegundua kuwa tukio hilo lilikuwa na uhusiano na Alvin.

“Twende nyumbani.” Kelvin alimshika mkono huku akitoka nje.

"Bwana Mushi, mmesahau kuchukua vitu vyako." Afisa wa polisi alimfuata ili kumrudishia vitu vyake. Vitu hivyo ni pamoja na simu, pochi, na saa yake.

Baada ya kuingia kwenye gari, Kelvin aliwasha simu yake. Arifa nyingi za ujumbe na simu ambazo hukujibu zilitokea.
Alizipitia moja baada ya nyingine. Mara tu alipotazama picha maalum, uso wake ukabadilika kuwa mweupe. Akiwa amejifunika kifua chake, ghafla akainama kwa maumivu. Simu pia ilianguka kutoka kwenye kiganja chake.

“Una shida gani, Kelvin?” Lisa alishtuka. Harakaharaka alimnyanyua, akagundua kuwa viungo vyake vinatetemeka. Alionekana kana kwamba atazimia.

Alishika mikono yake huku akishangaa kwanini yuko katika hali hiyo baada ya kuitazama simu yake. Ghafla, aligeuza macho yake chini, na kuiona tu picha kwenye skrini. Katika picha hiyo, alionekana akiwa amelala fofofo mikononi mwa Alvin. Macho yake yalikuwa yamefungwa, na mwili wake uliokuwa mtupu ulionekana kusema yote. Kilichomkasirisha zaidi ni kwamba tarehe ya picha iliyopigwa ilionyeshwa chini. Muhuri wa muda ulikuwa saa tisa usiku wa kuamkia siku hiyo.

Sura ya:179

Lisa aligundua kila kitu ndani ya sekunde chache. Alvin ndiye aliyeichukua ile picha na kumtumia Kelvin kwa makusudi. Kwa hivyo, hakuna njia ambayo angeweza kuficha kile kilichotokea.

"Fanya haraka na umpeleke Bwana Mushi hospitalini," mara moja akamwambia dereva.

Walipofika hospitali, daktari alimfanyia uchunguzi wa kimatibabu haraka na kumwekea Kelvin kanula ya pua. “Wewe ni mpenzi wake, sivyo? Nikukumbushe kuwa amebakiwa na figo moja tu. Jaribu kuzingatia kutomsababishia mfadhaiko wa aina yoyote. Pia anahitaji kula chakula chenye afya ili aweze kuishi muda mrefu zaidi,” daktari akakumbusha, “Tunaweza tu kumruhusu apumzike kwa sasa, ila hatuwezi kutatua tatizo la msingi.”

“Asante, Dokta.” Lisa alitoa shukrani zake kwa daktari kabla ya kuonana naye.

Wodini, Kelvin aliendelea kukohoa huku akijifunika kifua chake. Lisa alimimina glasi ya maji ya joto na kuileta karibu na mdomo wake.
Aliganda kwa muda kabla hajashika glasi. Akamtupia jicho tata ambalo lilijawa na maumivu. “Alikulazimisha kufanya hivyo?”

“Samahani.” Lisa aliona aibu kumtazama Kelvin machoni. "Ikiwa ungeendelea kufungwa kwa siku chache zaidi, ungejisikia vibaya na kampuni yako isingeweza kuishi pia."

Ghafla, Kelvin aliibamiza glasi ya maji kwenye sakafu. Uso wake mzuri ulitoka kwa hasira. "Alvin amekwenda mbali sana na uwezo wake."

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Lisa kumuona Kelvin akiwa amejawa na hasira nyingi. Kuangalia glasi iliyovunjwa, alikuwa mwisho wa akili zake. “Usifanye hivi. Daktari alisema usijitie mfadhaiko, ni hatari kwa afya yako.”

Kelvin alishika mkono wake. Baada ya kuvuta pumzi kwa nguvu, alitulia taratibu. “Najua ulifanya hivyo kwa ajili yangu. Sina haki ya kukulaumu.”
Alimshika kwa nguvu kiasi kwamba alimuumiza.

Lisa alijua kwamba maneno yake hayafanani na mawazo yake. Isingewezekana kwa mwanamume mwingine yeyote ambaye alikuwa katika viatu vyake kukubali.

"Ni sawa, Kelvin." Lisa alilazimisha tabasamu. “Nimeshaharibu. Sistahili kuwa na wewe. Pia, Alvin amekuwa akikuandama sana hata kabla hatujaingia kwenye uhusiano. Utaweza kuvumilia kuona Golden Corporation ikiharibiwa kwa sababu yangu? Fikiria kuhusu wazazi wako. Kwa kuzingatia uzee wao, wanachotaka ni wewe kuishi kwa amani.”

"Kutokana na yote uliyosema, una wazo la kuendelea kuwa na Alvin, sivyo?" Kelvin ghafla akatazama juu na kumtupia macho. Uso wake mpole ukawa wa kuogofya kupita kiasi. “Hujaacha kumfikiria kwa sababu kwa wakati huu, ni yeye pekee anayeweza kukurudisha kwenye familia ya Ngosha na kuwafukuza Nina na Melanie.”

Kwa mshtuko, Lisa alihisi kuchanganyikiwa ndani kabisa. Ikiwa angetaka kuwa na Alvin tena, asingengoja hadi wakati huu. "Kwa hivyo ndivyo umeniona wakati huu wote?"

“Samahani.” Akionekana kupigwa na kitu, Kelvin aliizungushia mikono yake kichwani kwa namna ya aibu. “Lisa, usiniache sawa? Kama hukunipa tumaini wakati huo, nisingefadhaika sana sasa.”

Kuangalia jinsi Kelvin alivyokuwa dhaifu, Lisa alihisi hatia sana. Kwa vile aliujua unyama wa Alvin, hakuwa na la kufanya zaidi ya kusema kwa uwazi, “Nikiendelea kuwa na wewe, mimi ndiye nitakayekuweka kuzimu. Unaweza kupata mwanamke ambaye ni bora kuliko mimi katika siku zijazo."

“Usinimwage kwa haraka. Wacha wakati uamue uhusiano wetu, sawa?" Tabasamu la uchungu likapita usoni mwa Kelvin. Kwa mwonekano wa mambo, Lisa angeweza tu kuchagua kunyamaza.

Baada ya Kelvin kumaliza kuingiziwa dripu, alimwomba dereva amrudishe kwenye nyumba yake ya kifahari. Lisa naye akaanza kuondoka zake.

"Unaenda wapi?" Kelvin alimshika mkono, hakutaka kumwacha aende vile tu. Tena, swali lake lilikutana na ukimya. "Unaenda kukutana na Alvin?" Kelvin alimshika kwa nguvu zaidi bila kuwa na mpango wa kumwachia.

Lisa alishtuka kwa uchungu, huku akiwa hana la kufanya. “Kelvin, nenda ukashughulikie mambo ya kampuni yako. Tutazungumza baadaye.”

“Kampuni…” Kelvin alimtazama Lisa kwa uchungu kwa sekunde kumi kabla ya kumwachia mkono wake aliokuwa kaushika kwa nguvu.

“Chunga…” Lisa aliuma ulimi alipomshauri. Kisha akageuka na kuondoka.

Kelvin aliitazama sura yake inayoondoka kwa baridi kali machoni pake huku akikunja ngumi kwa nguvu. Alipunguza hasira yake na kurudi kwenye kampuni, ambapo mwishowe hakuweza kujizuia zaidi ya kuvunja kila kitu ofisini.

Simu yake ikaita ghafla. Ilikuwa nambari isiyojulikana. Aliikamata kwa hasira na kuiweka karibu na sikio lake. Kicheko cha chini cha mwanaume kilisikika. "Lazima inauma sana kujua kwamba mchumba wako amelala na mwanamume mwingine."

"Wewe ni nani?" macho ya Kelvin yalitetemeka. Hakuweza kuitambua sauti ile.

"Pia najua kuwa haujawahi kupoteza figo yako. Ulighushi kwa makusudi jeraha ili kumdanganya Lisa Jones, na umejua historia yake kwa muda mrefu, kwa hivyo ulifikiri kwamba unaweza kutumia familia ya Ngosha kutimiza malengo yako…”

"Nyamaza!" Kelvin hakuweza kuzuia kishindo chake huku baridi ikishuka kwenye uti wa mgongo wake. Kwa mara ya kwanza, alihisi wazi kabisa. Hisia hiyo ilikuwa ya kutisha sana.

"Mimi ni mtu ambaye anaweza kukusaidia kulipiza kisasi," sauti ya chini ilisema, "naweza pia kusaidia kufanya Golden Corporation kuwa biashara inayoongoza nchini. Ninaweza kukusaidia kumrudisha mwanamke unayempenda mradi tu utanisikiliza katika siku zijazo.”

"Unataka nini?" Kelvin hakuelewa.

"Huna haja ya kujua hilo."

Kelvin alisita kwa sekunde chache tu kabla ya kutikisa kichwa. “Sawa, nakubali.” Asingeweza kukataa ofa hiyo japo hakuwa na uhakika nayo. Alitaka kumfanya Alvin Kimaro kupitia unyonge huo aliopitia siku hiyo.
•••
Saa kumi na moja za jioni, Mtendaji mkuu wa KIM International alikuwa ameketi ofisini akimsumbua Alvin kuhusu hali katika tawi la ng'ambo.
Hans aligonga mlango na akaingia na sura yake ya upole. "Bwana Kimaro, naibu mwenyekiti amerejea na anataka umwone."
Naibu Mwenyekiti? Lea Kimaro?

Lea Kimaro alikuwa amesafiri nje ya nchi na mumewe kwa mwaka mzima, kwa hivyo kila mtu karibu akasahau kwamba alikuwa naibu mwenyekiti wa KIM International. Lakini, kwa nini alirudi ghafla? Ilikuwa ni kwa sababu ya Jack?

Mtendaji mkuu alitazama kwa siri sura ya Alvin lakini aliona tu sura yake ya dharau. “Mwambie kwamba nina shughuli nyingi na sina muda.”
Mtendaji mkuu hakuthubutu kushikilia muda wa Alvin tena na haraka akapata kisingizio cha kuondoka.

Alvin aliinuka na kujiandaa kuondoka ofisini pale mwanamke mmoja mwenye hasira kali alipoingia ghafla.
"Ikiwa huna muda wa kukutana nami, basi nimekuja mwenyewe kwako, Mwenyekiti Kimaro!" Macho makali ya Lea yalitoa mwanga wa hasira. “Naona mbawa zako zimekuwa ngumu kiasi cha kutozingatia maneno yangu tena. Mimi bado ni mama yako.”

“Mama?” Midomo ya Alvin ilipinda kwa kejeli kwa neno hilo. "Basi, mama mpendwa, unafanya nini hapa badala ya kuandamana na mume wako mpendwa?"

"Unajua vizuri kwanini." Sauti ya Lea haikuwa na subira. "Mrudishe Jackson mara moja. Sudan Kusini haina amani sasa. Unajaribu kumuua?”

'”Kuna mamilioni ya watu wanaoishi Sudani Kusini. Wote wanaendelea vizuri, kwa hivyo kwa nini awe uwe na wasiwasi naye?" Alvin aliegemea kiti cha ngozi na kutanua mikono yake. "Kulikuwa na ebola na vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyotokea nilipoenda Kongo kuzungumzia mradi mwaka juzi, lakini sikukuona ukiwa na wasiwasi wowote kunihusu."

Lea aliitazama sura hiyo iliyofanana kwa kiasi fulani na Mike Tikisa, na mtazamo wake ukabadilika ghafla. “Unafanana naye? Wewe ni kombamwiko asiyekufa hata akiuawa kama baba yako.”

"Ndio hivyo?" Alvin aliinamisha kichwa chake, na tabasamu kwenye midomo yake likazidi. “Si unataka ashindane nami kwa KIM inernational? Acha kwanza apate uzoefu wakati yuko huko, basi.”

Sura ya:180

Baada ya Alvin kumaliza kuzungumza, alichukua koti lake la suti na kujiandaa kuondoka.

"Nadhani unataka tu afe huko ili ukose mtu anayeweza kushindana nawe kwa KIM International," Lea alisema kwa sauti kali.

Miguu mirefu ya Alvin ilitulia na akasema kimya kimya, “Fikiria chochote unachotaka.”

"Alvin Kimaro, majuto yangu makubwa ni kukuzaa kwako. Nilipaswa kukutoa ungali uko mimba.” Sauti ya Lea ilisikika kwa nyuma.

Alvin aliingia kwenye lifti moja kwa moja. Hans alitazama uso wake kwa uangalifu. Hakuwa na wasiwasi kwenye uso wake lakini Hans alijua kwamba kwa mtazamo ule, ulikuwa ni utulivu kabla ya dhoruba. Hiyo ilitokea kila mara Alvin na Lea walipokutana. Wawili hao bila shaka wangepigana, kana kwamba mama na mwana walikuwa maadui wa asili. Hans alihema moyoni mwake. Lea Kimaro alikuwa anapendelea sana.

Dereva akaleta gari, na Alvin akafungua mlango na kuingia ndani kabla ya kujiendesha. Nairobi ni kubwa, lakini ilionekana kana kwamba hakuwa na pa kwenda. Aliamua kuendesha gari hadi New Metropolis Park. Alifungua mlango na kuingia ndani. Jumba kubwa la kifahari lilikuwa kimya bila hata sura. Hapo hapo akampigia simu Lisa. Baada ya kuita mara kadhaa, simu ilikatwa na akajaribu tena mara mbili zaidi na ikawa hivyo hivyo tena.

"Vizuri sana." Alvin aliitazama simu ile, macho yake yakiwa yamejawa na mwanga wa damu.

Katika hoteli, Lisa alikata simu na kushtuka ghafla. Kwa tabia ya kijeuri ya Alvin, je, angefanya jambo baadaye? Lakini, baada ya kungoja kwa nusu siku na kutopokea habari yoyote kutoka kwake, mwishowe alipiga simu ya intercom ya hoteli kuagiza chakula cha jioni.

Saa moja jioni akiwa anajiandaa kula chakula cha jioni, ghafla kengele ya mlango ililia na mlango kupigwa teke na mtu. Alvin akasogea kwa hatua pana na kuubamiza mlango kwa kishindo.

“Umeingiaje?” Lisa alishtuka.

"Kampuni yangu inamiliki hoteli hii, na wewe hujui lolote." Alvin akaitupa kadi ya ufunguo pembeni na kumsogelea hatua kwa hatua. "Nilifikiri kwamba ulijifunza somo lako jana usiku, lakini inaonekana kwamba haujafuzu."

Kivuli chake kirefu kilimwangukia, na uso wake mzuri lakini mweusi ulimfanya Lisa kuogopa. “Mimi…nilitaka kuja, lakini wewe ndiye uliyetuma picha hizo jana usiku kwa Kelvin. Umeenda mbali sana.”
“Nilienda mbali sana?” Alvin alitabasamu kwa unyonge. "Nadhani nina huruma sana kwa kutomtumia picha za jinsi ulivyokuwa unafanya jana usiku."

"Nyamaza!" Lisa aligeuka rangi kutokana na unyonge.

“Nimesema kitu kibaya? Wewe ni mchumba wake lakini ulilala na mimi jana.” Maneno ya kikatili yalitoka kwenye mdomo wa Alvin. “Nadhani ulizaliwa tu kudharauliwa. Hujui hata mapungufu yako mwenyewe na bado unataka kuweka mbele…”

“Paah!” Lisa hakuvumilia tena kumsikiliza na kumpiga kofi zuri tu usoni. Alikuwa akilia machozi ya hasira. Macho yake mekundu yalijaa chuki na hasira kali alipokuwa akimwangalia. Ilikuwa ni sura ile ile aliyopewa na Lea Kimaro muda si mrefu kabla ya hapo.

Alvin alihisi tu kama kifua chake kimechomwa visu vikali. “Unathubutu kunipiga Lisa Jones?” Macho yake yaliyofinywa yalionekana kuwa kama ya shetani.

Lisa alichukua hatua mbili nyuma na kusema, "Alvin Kimaro, tafadhari naomba usinidhuru."

"Lisa Jones, sitakuonyesha tena huruma hata kidogo."

Kilichofuata hapo ilikuwa ni kumbukumbu ya pili isiyofutika katika maisha ya Lisa, ukiacha ile ya jana yake usiku. Miaka mingi baadaye, wakati Lisa angekuwa akikumbuka usiku huo, angeweza kutumia neno moja tu kuelezea: KUTISHA! Lisa alihisi kama ameanguka kwenye shimo baya ambalo likawa ndoto yake mbaya zaidi...
•••
Saa nane za usiku, Alvin aliamka kwa hasira na alichokiona kilimshtua.
Mwanamke aliyekuwa kando yake alikuwa amejikunja kama karunguyeye kwa maumivu. Uso wake ulikuwa umepauka sana na midomo yake ilikuwa na damu.

“Lisa!” Moyo wa Alvin ulipiga kelele. Hata hivyo, mwanamke huyo hakuitikia.

Alvin alishtuka. Alimfunga shuka yule mwanamke kwa haraka kabla ya kumchukua na kumkimbiza hospitali.

Usiku sana katika korido la hospitali ya City General. Alvin alisimama karibu na madirisha ya chumba cha dharura na kujaribu kuwasha sigara, lakini aligundua kwamba mkono wake ulikuwa ukitetemeka. Hata baada ya muda mrefu, hakuweza kuwasha sigara.

"No smoking!" Chester Choka, ambaye alikuwa ni daktari katika hospitali hiyo akiwa amevalia koti jeupe, alimsogelea huku akimtazama kwa macho makali. “Umefanya nini Alvin, kwanini unashindwa kudhibiti hasira zako? Nafikiri uraibu wako wa kuvuta sigara pia umezidi kuwa mkubwa zaidi, bila shaka ugonjwa wako wa hasira za hovyo umeanza kupanda tena.”

"Nilikutana na Lea Kimaro leo na akanifanya kupoteza udhibiti wa hisia zangu." Alvin alichanganyikiwa. "Anaendeleaje?"

“Daktari wa kike hospitalini amemchunguza.” Chester alimtazama. “Wewe ni kichaa kweli. Daktari amesema kwamba Lisa ametoka kupoteza usichana wake na bado anamshtuko wa kisaikolojia. Anahitaji angalau siku mbili hadi tatu za kupumzika, lakini ulimfanya nini?

"Umesema nini?" Alvin alitingisha kichwa kumwangalia Chester.

“Hivyo ndivyo daktari Melisa alisema. Unapaswa pia kujua kwamba Daktari Melisa hawezi kusema uwongo. Ameshughulika na wagonjwa wengi na ana uzoefu mwingi.”

Kila neno alilosema Chester lilikuwa kama bomu lililolipuka kwenye kichwa cha Alvin, likivuma. Kwa hivyo… Lisa na Kelvin Mushi hawakuwa na hatia kweli? Alikuwa amemuelewa vibaya?

“Yeye… Kwa hiyo hakufanya chochote na Kelvin Mushi?” Alvin alihisi kwamba ubongo wake ambao siku zote ulikuwa ‘genius’ ghafla ukawa hautoshi. “Lakini hakukuwa na hata na tone la damu lililotoka siku hiyo, inakuweje bikira awe namna hiyo?”

“Umenikumbusha hadithi za magazetini enzi zile nipo shule” Chester alisema huku akicheka, “....mara oooh! nikaanza mnyonya nini na nini kisha nikaingiza...Binti akalia sana kwa maumivu, nilipomaliza nikakuta shuka lote limelowa kwa damu....”

“Kwa hiyo si lazima iwe hivyo?” Alvin alijawa na mshangao mkubwa.

“Hiyo ni fantancy tu!” Chester aliendelea kumwelimisha. “Bikira haloweshi shuka kwa damu unless katikati ya tendo hedhi ikaanza, au wakati wa tendo binti kuvunja ungo. Hii inawatokea mabinti wadogo wanaolazimishwa kuolewa au wanaobakwa au umefanya kwa fujo sana mpaka ukamjeruhi mtoto wa watu”.

“Kwa hiyo inawezekana Lisa hakutoka damu kwa sababu alishavunja ungo siku nyingi?” Alvin aliuliza kwa hamasa.

“Unaweza kuwa ulimwandaa vya kutosha, akatokwa hofu kabisa kwa hiyo akawa amerelax wakati wa tendo.” Dokta Choka alisema. “Enzi zile ndiyo ilijengeka imani hii, kwamba siku ya harusi, usiku binti baada ya tendo anapachikwa kijitambaa cheupe ukeni ili kujua kama bikira imetoka. Kwamba kukiwa na damu, shangwe! Kikiwa kisafi kilio.... Lakini kumbuka enzi zile mabinti wengi waliolewa wakiwa wadogo na bila mapenzi so technically walikuwa wakibakwa na wengine kuvunjishwa ungo kabla ya siku zao hivyo damu ilikuwa ndio ushuhuda pekee!!”

Dokta Choka aliendelea kumpatia Alvin maelezo mengi ya kitaalamu. “Pale ukeni huwa na kijiutandu ambacho kinaweza kutoka kutokana na shughuli za kimaisha au mtindo wa maisha, michezo na kadhalika. Ukweli ni kuwa, Bikira ni kutokufanya tendo la ngono… Kwa hiyo nikijibu swali lako.... Hapana! Sio lazima damu imtoke mwanamke mara yake ya kwanza kufanya mapenzi!

“Siku inayofuata baada ya tendo anaweza kuona uchafu uliochanganyikana na damu kwenye chupi ikiwa aliumia....inategemea ulimuingilia kwa nguvu kiasi gani.nHali hiyo inaweza kuendela kwa siku mbili-tatu kisha akawa poa, again sio lazima kuwe na damu.”

Maelezo yale ya Dokta Choka yalikuwa yamejitosheleza kabisa na kumfanya Alvin aanze kuhisi hatia nzito moyoni mwake.

Je, hakulewa na madawa ya kulevya na kukaa usiku kucha na Kelvin hotelini? Ina maana siku hiyo hawakufanya chochote kweli?

Daktari Melisa asingeweza kusema uwongo. Ilionekana kana kwamba Alvin alikuwa amemuelewa Lisa vibaya. Alipoyafikiria maneno aliyomwambia hapo awali, alijuta na kujipiga makofi mawili ya usoni. Alikuwa amefanya nini? Usiku ule, je, kweli alijizamisha ndani ya maji baridi ili alale, kama vile alivyosema?

Chester akasema. "Nilipoona picha zake akiwa katika urafiki wa karibu na Kelvin Mushi wakati huo, nilifikiri walikuwa tayari… Nani angefikiria hili lingetokea. Hata baada ya kuchumbiwa kwa muda mrefu, usichana wake ulitenguliwa na wewe badala yake. Unafikiri Kelvin hatakufa kwa majuto?”

Alvin alikunja uso kwa nguvu. Hakujua kama Kelvin angekufa kwa majuto, lakini Alvin alikuwa karibu kufa majuto hayo. Alisimama wodini huku akiwa na hisia hizo za majuto. Alipoona sura ya Lisa iliyopauka, akataka kujipiga makofi mengine mawili.

Mambo ambayo alikuwa amemfanyia yalikuwa ya kinyama tu. Alikuwa akimshutumu kwa kulala na Kelvin lakini daktari alidhibitisha kuwa ubikira wa Lisa ulitolewa na yeye. Wakati huo, kope za Lisa aliyelala kitandani zilitetemeka ghafla. Alvin ambaye alikuwa akiwaza jinsi ya kumkabili mwanamke huyo, alikuwa amekata tamaa.

Lisa alifumbua macho taratibu. Alipomuona Alvin amesimama kando ya kitanda chake, tukio lile la kutisha liliibuka ghafla akilini mwake. Alitetemeka kwa woga na uso wake ulikuwa mweupe wa karatasi. “Usije huku!” Lisa aliogopa sana. Alijaribu kujificha pembeni, na macho yake safi yalijawa na hofu juu yake.

Moyo wa Alvin ulipiga kwa maumivu na kujaribu kumtuliza. “Usiogope, sita…”

“Ahhhh, usinishike!” Lisa akaingia kwenye blanketi kwa woga, mwili wake ukitetemeka kama jani.

“Sitathubutu tena. Sikupaswa kukupiga. Unaweza kufanya chochote unachotaka katika siku zijazo. Ninaogopa sana sasa. Nimejifunza somo langu!” Alvin alijitetea bila kueleweka.

TUKUTANE KURASA 181-185

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......181-185

Sura ya:181

"Toka nje…”

“Usijifunike gubigubi utakosa hewa.” Alvin alinyoosha mkono kuvuta blanketi lakini akamwona Lisa akiuma vidole vyake kwa nguvu. Uso wake ulikuwa na michirizi ya machozi.

“Sawa, nitatoka. Nitaomba mtu akuletee chakula kwani usiku kucha haujala.” Alvin alihema na kugeuka kuondoka.

Muda si muda, nesi akaingia. Lisa alipoona Alvin ameondoka, hofu moyoni ikamtoka kidogo, lakini bado mwili ulikuwa ukimuuma sana. Hakuwa na hamu ya kula kabisa na alilala baada ya muda mfupi kidogo.

Alipoamka siku iliyofuata, anga tayari lilikuwa limeangaza. Alvin alisimama mbele ya dirisha na alikuwa kwenye simu, akiongea kwa sauti ya chini. “Sitakuja kwa kampuni leo. Ghairi mkutano huo."

“Lakini Naibu Mwenyekiti Lea Kimaro atahudhuria mkutano wa leo—”

"Nilisema ghairi, kwa hivyo ughairi." Alvin aliamuru.

Alvin akageuka nyuma na kuyaona macho ya Lisa yakiwa yamejaa woga kama ya kulungu. Lisa alikurupuka. Alvin akasogea kitandani na kusema kwa sauti ya upole, “Daktari aliniambia kuwa usichana wako niliutoa mimi kwa mara ya kwanza. Samahani nilikuelewa vibaya hapo awali. Ninaahidi sitatenda kama nilivyofanya jana tena. Unaweza kunisamehe?”

Lisa alipigwa na butwaa. Si ajabu kwamba ghafla alikuwa mpole sana kwake. Alifikiri kwamba hatimaye angemwamni baada ya kuwa ameshuhudia kwa macho yake. Ilibainika kuwa ni kwa sababu daktari alikuwa amemwambia. Alitamani kucheka kwa jinsi ambavyo hakujawa na uaminifu kati ya wawili hao.

“Sawa.” Aliitikia kwa kichwa. “Wewe ni Bwana Alvin Kimaro, nani angethubutu kutokusamehe?”

“Huna lolote lingine la kuniambia?” Alvin alikuwa amepotea kiasi. “Unaweza kunilaumu utakavyo.”

“Kukukaripia? Nani atathubutu kukukemea? Nilikukaripia jana na kuachwa nikiwa hivi. Sitathubutu tena”

Alvin alitabasamu kwa uchungu. Wakati huo, angetumia jitihada zake mwenyewe kuuchochea moyo wake na kumuondoa woga.

Alasiri, Alvin alikamilisha taratibu za kutolewa hoaspitali na kumrudisha Lisa hadi New Metropolis Park. Ilikuwa imepita zaidi ya mwaka mmoja tangu jumba hilo kukarabatiwa, na ilikuwa mara ya kwanza mtu kuishi humo.

Asubuhi, alimwambia Hans kuandaa vifaa vingi vya nyumbani na hata kununua kabati nzima iliyojaa nguo za kike. Gari lilisimama kwenye maegesho, Alvin akainama kumnyanyua. Lisa alimruhusu amsogeze kwa utiifu.

Kilichokuwa muhimu kwake sasa ni kuvumilia. Ni mpaka pale ambapo angejua kuhusu sababu ya kifo cha Sheryl Masawe na kulipiza kisasi, ndipo angeondoka Nairobi. Hakuwa na haja tena na biashara. Alichotaka ni uhuru.

Alvin alimbeba mpaka kwenye sofa na kumfungulia luninga.

“Acha na TV usiku umeingia, kwa hiyo nitaandaa chakula cha jioni.” Lisa alivumilia maumivu na kuinuka.

“Unawezaje kupika namna hii? Usihangaike.” Alvin alimsimamisha na kumshika, hivyo akaketi tena.

"Kukupikia ni jukumu langu." Lisa alikuwa mtiifu kama kijakazi mdogo. "Utakula nini ikiwa sitapika?"
Alvin alikasirika. Zamani hakutaka kitu zaidi ya yeye kuwa mtiifu hivi, lakini sasa Lisa alikuwa mtiifu kwake na bado moyo ulimuuma tena.

"Nitapika." Alvin alivua koti lake na kukunja mikono yake.
Lisa alishangaa. Baada ya kumfahamu kwa muda mrefu, hakuwahi kumuona hata kushika mwiko. Angepikaje?

Alvin kweli hakujua kupika, lakini aliweza kujifunza papo hapo ili tu kumfurahisha Lisa. Kulikuwa na mafunzo mengi kuptia Youtube kwenye simu yake, hivyo aliamni kwamba haiwezi kuwa ngumu kiasi hicho. Baada ya kutumia saa moja kutizama mapishi mbalimbali, hatimaye aliandaa sahani mbili za chips na mayai japo hazikuonekana na sura nzuri. Kulikuwa na samaki pia kwenye friji aliomwagiza Hans awalete akawakatakata na kuwakaanga.

Lisa alitazama sehemu ya nyuma ya mkono wake uliokuwa umebadilika na kuwa mwekundu kwa sababu ulikuwa umetapakaa mafuta ya moto. Ikiwa asingepaka asali mara moja, bila shaka angepata malengelenge kesho yake.

"Kula." Alvin akamtengea sahani ya chips na kumsogezea minofu ya samaki. Viazi vya chips vilikuwa vimekatwakatwa hovyohovyo tu, vingine vidogo kama karanga wakati vipande vingine vikubwa kama biskuti, na ilikuwa wazi kuwa alijikatakata kwenye vidole wakati akimenya viazi hivyo. Hata hivyo, viazi hivyo havikuwa na chumvi hata kidogo. Alikumbuka kutia chumvi kwenye mayai lakini nako ilikuwa imepitiliza na kuyafanya mayai yasilike kabisa japo yalinukia vizuri.

Alvin aliyaonja na kugundua dosari hiyo. Akayasukumia pembeni na kumsogezea kipande kikubwa cha minofu ya samaki. "Kula hii."

Lisa, akaguna mara tu ya kumuonja yule samaki. Ilivyoonekana alitolewa kwenye kikaango akiwa hata hajakauka vizuri hivyo minofu mafuta yote yakanyonywa na minofu, lakini, bado alijilazimisha kula samaki huyo kwa utiifu.

Alvin hakuona mwanzoni, lakini baadaye alijaribu kuonja mnofu na akakuta ladha ya samaki ina mafuta kupita kiasi. Kwa kuudhika, alitupa kwenye pipa la taka ile sahani ya minofu ya samaki. “Inatosha, acha kula. Ni wazi ladha yake ni mbaya. Mbona hukusema lolote?” Sauti yake ilipandishwa kwa hasira, na mikono ya Lisa ikatetemeka. Macho yake makubwa yalijawa na wasiwasi na woga.

Moyo wa Alvin ulimuuma. Alimbeba moja kwa moja kwenye mikono yake, sauti yake ikiwa imejaa mamlaka na kutawala,, alisema, “Lisa Jones, nataka uishi na mimi kama tulivyofanya hapo awali huko Dar es Salaam, sawa?”

Lisa alipigwa na butwaa na kumtazama huku akiinamisha kichwa chake. Macho yake yalitetemeka. "Unatakaje, niishi kwa kujinyenyekeza na kujipendekeza?"

Wakati wakiwa huko Dar es Salaam, walikuwa tofauti na jinsi walivyokutana tena Nairobi. Kipindi hicho Lisa alikuwa akimbembeleza akidhani ni mjomba wa Ethan, alimtii hata aseme nini, akajilazimisha kuacha hasira yake na kuacha mambo yote aliyopenda kufanya ili tu kumfurahisha Alvin.

Alvin alijikaza huku moyo wake ukiwa umejaa uchungu. "Kwa hiyo, huko Dar es Salaam ulikuwa ukijinyenyekeza tu na kujipendekeza, madai yako kwamba ulinipenda yalikuwa ya uwongo?"

"Samahani, nilikosea." Lisa aliomba msamaha bila raha. “Usikasirike.”

“Sina hasira. Nilikuwa namaanisha kuwa unaweza kuishi na mimi pasipo kujinyenyekeza tena. Unaweza kudai chochote, unaweza kukasirika au kufurahi, unaweza kupika au usipike ukipenda, unaweza kufanya chochote unachopenda ukiwa huru kabisa. Unaweza kunitendea kama mpenzi wako. Sitakutendea kama jana tena, naapa!” Alvin akamkumbatia kwa nguvu.

Lisa alitabasamu na kuinamisha macho yake, lakini moyo wake ulikuwa umejaa kejeli. Mpenzi? Alikuwa mpenzi wa Melanie, si wake. Alikuwa ni kama hawara tu au mchepuko.

“Kwa hiyo naweza nikwambia kitu na ukanisikiliza?” Lisa aliuliza kwa wasiwasi.

"Ndio, mradi sio kuhusu Kelvin Mushi." Alvin alifikiria kwa muda na kuongeza, “Sitaki uwe na mahusiano naye tena.”

Lisa alitikisa kichwa na kusitasita kwa muda kabla ya kupata ujasiri wa kutosha kuuliza kwa sauti ndogo, "Je, unaweza kumrudisha Jack Kimaro?"

Alipomaliza, aligundua kuwa uso mpole wa Alvin ulikuwa umebadilika na kuwa baridi na giza kwa kasi inayoonekana kwa macho… Kidogo kama vile usiku…Aliingiwa na hofu na kuogopa. "Nilikosea, sikupaswa kukuomba kitu kama hicho. Chukulia kama nilipitiwa tu. Usinidhuru…”

Hasira iliyokuwa ikienda kukimbilia kichwani kwa Alvin ghafla ikatoweka na mara akarudiwa na fahamu zake baada ya kusikia sauti yake ya hofu. Hakuwa na nia ya kukasirika, lakini hakuelewa kuwa Jack alikuwa kivuli moyoni mwake. Jack alikuwa mwiko kwake.

“Sitakuumiza,” Alvin alimshika mkono na kusema kwa sauti ya upole, akitumaini angetulia.

Lisa alimtazama kwa woga. “Nataka kupanda ghorofani nikapumzike.” Kwa kweli hakutaka kukaa naye tena.

Alvin alimpeleka juu na kumuweka kitandani bila ya Lisa kusema neno lolote. “Hukula vya kutosha. Nitapiga simu hotelini kuagiza chakula. Nitakuja kukuchukua baadaye.”

Sura ya 182

Alvin alikuwa amemaliza tu kuongea wakati simu yake ilipoita. Alipoitoa nje ili kuona, Lisa aliona neno 'Bibi' kwenye skrini. Alvin akatoka nje na simu. "Bibi, kuna kitu kilitokea?"

“Siwezi kukupigia kama hakuna kilichotokea? Unashughulika na nini siku nzima? Hujarudi kwenye makazi ya familia kwa siku kadhaa. Mama yako amerudi, kwa hivyo lazima uje kujumuika na familia leo."

Alvin alitazama kwenye mlango wa chumba cha kulala na kukataa. "niko busy."

“Uko busy na mambo gani?" Bibi Kimaro aliuliza kwa hasira, “Lazima uje. Familia nzima itakula pamoja leo.”

Alvin alidhihaki, “Hivi kweli ni mlo tu au kuna ajenda nyingine? Mnataka kunilazimisha nimrudishe Jack?”

Bibi Kimaro alihema. “Alvin, usisahau hii, ni kwa sababu mimi na babu yako tuliendelea kusisitiza kwamba wewe uchukue jukumu la kuongoza kampuni na kumzuia mama yako asisimamie mambo ya kampuni. Tulikuruhusu wewe na Jack kuwa kwenye kampuni licha ya mama yako kuwa hajaridhika na hilo. Kila mtu anajua kwamba Jack ni kipenzi cha mama yako. Ukimchokoza Lea, hata hivyo, haitakuwa rahisi katika siku zijazo atakaporudi kwenye kampuni.”

Alvin alicheka. “Sawa, nitamruhusu arudi.”

"Hiyo ni nzuri." Bibi Kimaro alifurahi sana. "Kwa hiyo utakuja kula chakula cha jioni nami?"

"Bibi, nimekuambia niko busy kwa sasa." Alvin alisisitiza.

Bibi Kimaro alikasirika tena. “Hauko tayari hata kunisindikiza kwa chakula cha jioni? Unafanya nini huko nje, una mwanamke? Usifikiri mimi ni mzee. Nilisikia kwamba ulimpeleka mwanamke Oasis hapa juzijuzi na kulala naye.”

Alvin alicheka. Ni lazima kuwa Melanie ndiye aliyempelekea bibi yake udaku huo. Ni yeye tu aliyeiona siku hiyo, na aliapa angemfunza namna ya kufunga mdomo wake siku nyingine. "Bibi, mimi si mwanamume, kwani kipi cha ajabu?"

“Melanie hakutoshi?” Bibi aliuliza kwa hasira.

“Simpendi na sitaki kumsikia. nakata simu sasa hivi.” Alvin alimjibu kijeuri bibi yake, akakata simu.

Asubuhi iliyofuata Lisa aliposhuka chini, alimuona mtu wa ziada kwenye jumba hilo la kifahari. Alikuwa ni Shangazi Yasmini, ambaye aliwahi kukutana naye huko kwenye makazi ya familia ya Kimaro hapo awali.

Shangazi Yasmini alitabasamu kwa upole. "Bwana Kimaro alinihamisha hapa kutoka kwa makazi ya zamani ili kukutunza."

“Asante, Shangazi Yasmini.” Lisa alikuwa na aibu kidogo. Baada ya yote, Aunty Yasmini alijua utambulisho wake na angeweza kumdharau moyoni mwake.

Shangazi Yasmine aliweza kusoma mawazo yake na akasema kwa kawaida, “Nilimlea Bwana Kimaro. Mimi ndiye mtu ambaye ananiamini zaidi katika makazi ya familia, kwa hiyo lazima awe anakujali sana ikwa kuniomba nikuhudumie.” Lisa alitabasamu kwa huzuni. Alimwonea aibu sana bibi yule.

Punde, Alvin alibadili nguo zake na kutoka nje. Walikaa pamoja kwa kifungua kinywa. Kifungua kinywa cha Shangazi Yasmini kilikuwa kitamu na Lisa alikipenda sana, lakini Alvin hakula sana.

Aunty Yasmini akahema. “Bwana Kimaro, huwezi kula kidogo namna hii. Unapaswa kula zaidi, au mwili wako utachoka."

Lisa akanyamaza. Hakuwa anakula? Kwa chakula alichokuwa akipika yeye angeweza kula sahani mbili au tatu kwa kila mlo. Alionekana kuwa amepoteza uzito mwingi baada ya kurudi Nairobi.

“Shangazi Yasmini, sina njaa.” Alvin alipomaliza kuongea simu yake iliita tena. Wakati huu, alijibu na ghafla akashtuka, sura yake ikibadilika. "Sawa, nitarudi kwenye kampuni mara moja."

“Shangazi Yasmini, mtengeneze Lisa chakula kitamu zaidi saa sita mchana ili kuutunza mwili wake.” Alvin alienda kwa Lisa ili ambusu kichwa kabla ya kugeuka kuondoka.

Lisa hakujua kilichotokea na aliona tu kwamba alikuwa na haraka. Baada ya kifungua kinywa, kipande cha habari kilitokea kwenye simu yake. Jack Kimaro alikumbana na hatari huko Sudan Kusini na kwa sasa hakujulikana alipo.

Habari kuhusu familia ya Kimaro zilikuwa zikizungumzwa zaidi nchini humo. Habari hiyo ya kutoweka kwa Jack Kimaro ilikuwa ni miongoni mwa habari zilizovuma na kutafutwa sana mitandaoni nchini humo. Pia alionekana kujadiliwa kwenye mada mbalimbali za vipindi vya televisheni na redio nchini humo.

Kutoweka kwa Jack Kimaro: [Nilisikia kwamba Jack Kimaro alilazimishwa kwenda Sudani Kusini na kaka yake mwenyewe. Vita mara nyingi huzuka Nchini humo kwa sasa. Ni dhahiri nini kingetokea ikiwa angepelekwa huko kwa wakati huu.]

Kutoweka kwa Jack Kimaro: [Nilisikia kwamba mzozo wa nchi ya Sudan Kusini asubuhi ya leo ulisababisha kurushiana mabomu na kulikuwa na majeruhi wengi. Bwana Jack Kimaro huenda kilipatwa na bahati mbaya.]

Kutoweka kwa Jack Kimaro: [Alvin Kimaro hana huruma kabisa. KIM International tayari ni yake, lakini hatamuacha mdogo wake mwenyewe.]

Habari kuhusu kutoweka kwa Jack Kimaro ilikuwa ni habari ya mjini kwa Kenya nzima. Uso wa Lisa ukazidi kufifia. Jack alipata ajali? Iwapo Jack asingemsaidia, asingepelekwa huko na Alvin. Hii ilimaaanisha kuwa alikuwa na hatia kwenye hilo, lilikuwa kosa lake lote!
•••

Ndani ya KIM International, Alvin alikuwa amefika tu kwenye ghorofa ya juu wakati mama yake, Lea Kimaro, alipomkaribisha kwa kofi la uso. Akamshika mkono. Nywele za Lea zilikuwa zimechafuka huku macho yake mekundu yakiwa yamejawa na hasira. "Alvin, ikiwa chochote kitatokea kwa Jack, hakika utazikwa pamoja naye!" Mwili wake ulitetemeka, na mkono wake chini ya mkono wa Alvin ukatetemeka kidogo.

Kwa upande mwingine, Mason Campos, baba yake na Jack, alifunga mkono wake kwa bega la Lea. “Lea tulia. Jambo muhimu zaidi sasa ni kwenda kumtafuta Jack. Nimemwambia sekretari aandae tiketi. Nitasafiri kwa ndege hadi Jubah baadaye.”

“Wewe?” Lea alionekana kuwa na wasiwasi. “Lakini hali ya huko ni ya machafuko sana sasa. Vita vinaweza kuzuka. Ikiwa chochote kitakupata—”

“Hata kama Jack amekufa, bado ni lazima nitafute mwili wake na kumrudisha.” Mguso wa maumivu makali ulipitia macho ya Mason.

“Hakuna haja ya hilo. Nitakwenda mimi mwenyewe,” Alvin aliongea bila kujali na kugeuka kuondoka.

“Hapana. Nitajuaje ikiwa un mpango wa kwenda kummaliza Jack huko? Nenda na Mason,” Lea akaamuru, “Lazima umrudishe salama.”

Upande wa mdomo wa Alvin ulijivuta kwa ujeuri kabla hajaondoka.
Hans alikasirika sana aliposikia maneno ya Lea. “Bi. mkubwa naye amezidi sana. Hata iweje, wewe pia ulitoka tumboni mwake. Bwana Kimaro, ukiniuliza, hupaswi kwenda kabisa. Acha tu hao wawili baba na mwana wakafie huko.”

“Si unaona jinsi ninavyoshambuliwa kwenye mtandao? Picha yangu kwa sasa imeharibika, kwa hivyo nitaenda huko ili kusafisha jina langu, na… Sidhani kama Jack amekufa. Baada ya yote, habari zimeenea haraka sana. Naamini kwamba kuna mtu aliyeivumisha kimakusudi.” Alvin alidhihaki.

Kabla ya kuingia kwenye ndege, Alvin alimpigia simu Lisa. “Kuwa makini. Lazima niende kwa safari ya kikazi kwa siku chache, kwa hiyo chukua dawa zako na ukae nyumbani kwa utiifu.”

Baada ya kimya cha sekunde chache, Lisa aliuliza kwa sauti ya chini, “Niahidi kwamba hutamdhuru Jack?”

Ilionekana kana kwamba kuna kitu kinapasuka kifuani mwake. Moyo wa Alvin ulikuwa mzito na mchungu ghafla. Wapendwa wote walio karibu naye hawakumwamini, akiwemo yeye. Kila mtu alisema kuwa Sudan Kusini ilikuwa hatari, lakini hakuna aliyejali yeye kwenda huko, kila mtu alimhurumia Jack.

“Sawa.” Alicheka na hakutaka kueleza zaidi. Haijkuwa na maana hata hivyo.

Baada ya kukata simu, alimgeukia Hans. “Umeniletea dawa nilizokuwa nikinywa?”

Hans alipigwa na butwaa. Kisha, akikumbuka jinsi Chester alivyosema kwamba huenda hali ya Alvin ilikuwa imerudi tena, hata hivyo alimkabidhi dawa.

Sura ya 183

Wiki moja baadaye, Pamela aliongozana na Lisa hadi hospitali ili kuondolewa mshono wa nyuzi. Chester binafsi alikwenda kwenye maegesho ya hospitali ili kukutana na watu hao wawili. Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Lisa kukutana naye, na ilibidi aseme kwamba marafiki wa Alvin wote walionekana kama wanamitindo bora.

Chester alivaa koti jeupe la kidaktari na miwani. Umbo lake lilikuwa refu na alionekana mpole. Tabasamu kwenye mdomo wake lilimfanya aonekane mpole na mwenye urafiki, mtu mzuri na asiyejali.

Pamela alishtuka alipomona na kutania kwa sauti kubwa, “unaonekana kama si daktari bali mwanamitindo wa kiume anayepiga picha mbele ya kamera kwa ajili ya filamu."

"Una utani mzuri, Pamela." Chester alitabasamu. “Twendeni. Nimeshaandaa daktari atakayekuhudumia huko.”

“Pole kwa usumbufu. Naweza kwenda peke yangu.” Lisa aliona aibu. Baada ya yote, alikuwa akienda kwenye idara ya magonjwa ya wanawake.

Chester akatikisa kichwa na kutabasamu. “Hapana, hakuna shida kabisa. Alvin mwenyewe alinipigia simu na kunisisitiza nikuhudumie mimi mwenyewe.”

Lisa alishindwa kujizuia kuifikiria ile simu aliyoipokea usiku wa kuamkia jana yake. Kweli Alvin alikumbuka na kumpiga simu kumkumbusha akatoe nyuzi.

Wakati watu hao watatu wanakaribia kupanda lifti, ghafla sauti ya mwanamke aliyemfahamu ilitoka nyuma yao. “Dokta Choka…”

Watu wale watatu wakageuka, na uso wa Lisa ukainuka kidogo. Alikuwa Melanie. Kando yake alisimama mwanamke mwenye hadhi na mrembo aliyejipodoa vilivyo. Alionekana kana kwamba alikuwa na umri wa miaka 50 hivi, na mwili wake mnene kiasi na mrefu ulitoa haiba kama vile alikuwa ameishi katika tabaka la juu kwa muda mrefu. Alimfanya Melanie aonekane kama kijakazi wake tu.

"Anti Lea, ni muda mrefu." Chester alichukua hatua ya kumsalimia kwa heshima. “Umerudi?”

"Ndio, Jack alipata ajali, kwa hivyo ningewezaje kubaki nje ya nchi?" Lea aliwatazama Pamela na Lisa. Wote wawili walikuwa wasichana wachanga katika miaka yao ya mapema ya 20 na walionekana warembo kabisa. Alijua kuwa Chester alikuwa mvulana wa kuchezea mabinti, kwa hivyo alifikiria tu kwamba Lisa na Pamela pia walikuwa wanawake wapuuzi. Hakujishughulisha kuwatazama vizuri.

Melanie ndiye aliyebetua midomo yake na kusema, “Lisa Jones, kwa nini uko hapa? Oh, mimi nimekupata. Lazima uwe ulillala na Dokta Choka ili kurudisha lile shamba."

“Melanie, hadhi ya Dokta Choka si ya kawaida kama unavyodhani, kwa hivyo tafadhali pitia maneno yako kwenye kichungi kabla ya kuongea. Usiwasingizie wengine kiholela,” Lisa alijibu kwa hasira.

Melanie aligeuza macho yake na kumwambia Lea, “ma’mkwe, huyu ni binti wa haramu wa baba yangu.”

Pamela alikasirika. “Unamwita nani binti wa haramu? Wewe ni mdogo kuliko yeye. Ni wazi kwamba mama yako alifanya chochote kilichohitajika ili kuolewa katika familia ya Ngosha."

"Wewe ni nani? Nani alikupa haki ya kuongea?" Melanie akatamba. "Lisa Jones, wewe ni malaya tu kama mama yako. Nakuonya usije ukaaibisha jina la familia ya Ngosha huko nje.”

Lisa alikunja uso, lakini Chester alizungumza kwa kuonya kabla hajaweza, “Binti Ngosha, angalia maneno yako. Lisa ni rafiki wa rafiki yangu. Ukisema maneno ya kashfa kama haya na rafiki yangu akagundua, atakuchanachana usoni.”

Melanie hakutarajia Chester angemsaidia Lisa na alilalamika kwa huzuni. “Dokta Choka mimi ni mpenzi wa Alvin Kimaro. Yeye pia ni rafiki yako mzuri—”

Chester alimtazama kwa upole. "Ndio hivyo? Alvin hakuwahi kunifahamisha kamwe.”

Melanie alikasirika, na Lea akasema bila subira, “Chester, ninaweza kuwa nimekasirika sana siku hizi kwa sababu ya tukio la Jack. Kifua changu kinahisi kuwa kimefungwa na kutokuwa na raha. Nifanyie vipimo.”

Chester alikuwa na wasiwasi. Lea alikuwa mzee, kwa hiyo haingefaa kumkatalia.

Lisa alisema, “Dokta Choka, usijali, we kamhudumie tu mama. Nitapanda juu peke yangu.”

"Sawa, nipigie ikiwa unahitaji chochote." Chester aligeuka ili kuondoka mara simu ya Lea ikaita ghafla. “Nini… Wamerudi? Sawa… Sawa, tutaenda kwenye uwanja wa ndege mara moja.”

Baada ya kukata simu, Lea alitoa tabasamu adimu kwa Melanie. “Jack na Alvin wamefika tu kwenye uwanja wa ndege. Twende, tutaendesha gari na kuwachukua kisha tutarudi kuchunguzwa wakati mwingine.”

“Ndiyo, ma’mkwe. Nimemkumbuka pia Alvin.” Melanie alimtazama Lisa kwa mbwembwe na kuondoka haraka na Lea.

Pamela alimpa Lisa sura ya woga na huruma lakini aliona sura yake imejaa utulivu. “Twende, lifti iko hapa.”

“Inaonekana naweza kukusindikiza tena.” Chester akawafuata ndani na kukohoa taratibu kwenye ngumi yake. "Melanie amezama tu katika mawazo yake mwenyewe. Moyo wa Alvin uko pamoja nawe. Kimsingi sisi ni ndugu zake na tunamuelewa zaidi, hivyo usifikirie kupita kiasi.”

“Sivyo.” Lisa alitabasamu naye. Hakika alifarijika. Ilionekana kuwa Jack alikuwa sawa.

Alipotoka hospitalini, Pamela aliogopa kwamba Lisa angeweza kuruhusu mawazo yake yaende kinyume chake ikiwa angekuwa peke yake, akamwambia, “Twende tukapate chakula. Najua mgahawa wa kitanzania hapa Nairobi wenye chakula kizuri sana.”

“Hakika. Bado sijala kwenye mahakama za chakula za Nairobi.” Lisa aliunga mkono.

Wawili hao waliendesha gari na kuingia kwenye mgahawa mmoja uliokuwa ukipika vyakula vya Kitanzania nakuagiza chakula wakati Alvin alipopiga simu ghafla. “Uko wapi?”

“Ninakula mtori na chapati hapa kwenye mgahawa wa kichaga,” Lisa alijibu kwa woga, akiogopa kukemewa naye. Baada ya yote, alichukia kula vitu kama hivyo.

Alvin alinyamaza kwa muda kabla ya kusema, “Nitumie anuani ya eneo nitakuja kukuchukua.”

Lisa aliganda. Ina maana Melanie hakwenda kumpokea? Kwanini alikuwa anakuja kwake mara baada ya kurudi kutoka Sudan Kusini badala ya kurudi Mlima wa Sherman pamoja na mama yake na mchumba wake?

“Niko katikati ya jiji. Mazingira ya hapa ni mageni sana kwangu…”

“Usinicheleweshe.” Sauti ya Alvin ikakosa subira, Lisa hakuwa na jinsi zaidi ya kumpa anuani ya eneo.

Pamela akawa mwenye huzuni. “Anakuja hapa kwa ajili ya nini? Nitajisikia vibaya kula akiwa hapa.”

“Aling’ang’ania kuja, ningethubutu vipi kumwambia asije? Vinginevyo, anaweza kushuku kuwa niko pamoja na Kelvin tena.” Lisa alitabasamu kwa uchungu.

Dakika 20 baadaye, Alvin alionekana kwenye lango la ukumbi wa chakula. Alikuwa amerudi kutoka Sudan Kusini, na ni wazi alionekana kwamba alikuwa ameteseka kidogo huko. Ngozi yake ilikuwa nyeusi, lakini alionekana kujikaza kiume zaidi. Haiba ya mwili wake ilikuwa kama panga kali, na kuwafanya watu wajisikie kuwa hayuko katika anga za hapa.

Alvin akasogea na kukanyaga kwa bahati mbaya kipande cha tishu kilichotupwa chini. Alikwaruza kiatu chake kwa nguvu lakini hakuweza kukiondoa. Uso wake ukazidi kuwa mweusi zaidi na zaidi.

Lisa aliinama chini ili kuvuta tishu ile kutoka kwenye kiatu chake, lakini Alvin alimvuta mara moja. "Unafanya nini?"

"Nakusaidia kukiondoa." Jibu la Lisa lilikuwa la tahadhari sana.

“Nyanyuka tuondoke.” Alvin hakujali hata kusalimia Pamela.

Lisa akawa mgumu kidogo. “Unamaanisha nini kusema hivyo? Chakula ndo kwanza kimefika tu.”

Pamela naye alikasirika. “Bwana Kimaro, nilitaka kusema hili kwa muda mrefu. Lisa amechumbiwa na Kelvin Mushi, na Kelvin alipoteza figo kwa sababu ya kumwokoa. Sasa bado una shida gani na Lisa? Wewe pia umemchumbia ndugu yake bila hata aibu, na bado hujaridhika, umempiga nusura ya kumuua, lakini hujisikii hatia hata kidogo. Hata kama wewe ni mtu mzito, ndiyo utumie hadhi yako kumnyanyasa binti wa watu asiye na hatia, kwanini?"

"Pamela, acha!" Lisa aliogopa na kutokwa na jasho baridi kwa maneno hayo ya Pamela.

Sura ya 184

“Jitizame mwenyewe. Ulikuwa binti shupavu sana, lakini kakutesa kiasi kwamba umekuwa kama panya mdogo.” Pamela alikuwa akifa kwa hasira. “Nitakuambia ukweli. Nilipokuomba umsaidie katika kesi wakati huo, maneno yote niliyosema yalikuwa ya uongo. Hakuwa na uhusiano wowote nayo. Nilifanya hivyo kwa sababu ikiwa angeenda gerezani, nisingeweza kukutana naye tena. Hajui lolote hata kidogo.”

Lisa alipapasa paji la uso wake na kutazama jinsi sura ya Alvin inavyozidi kuwa nyeusi kama wino. Alisimama mbele yake na kumwambia kwa upole. "Pamela alifanya hivyo ili kuniokoa. Haina uhusiano wowote naye, kwa hiyo usimdhuru.”

Alvin aliona jinsi alivyokuwa akiigiza kama kuku anayemlinda kifaranga wake, moyo wake ukaudhika na kufadhaika. Alimwona kama shetani sasa?

"Sogea kando, nina njaa."

“Heeh?” Lisa alishangaa.

“Hukunisikia? Nimesema nina njaa.” Alvin akamshika mkono na kukaa kwenye benchi.

Meza ilikuwa imejaa vyakula vyenye viungo vikali, vilivyochomwa, na vilivyokaangwa. Alvin akakunja uso. "Mbona hakuna chakula kwangu?"
Alijua kwamba hawezi kula chakula cha viungo vikali.

Lisa aliganda. "Nilidhani hautakula hivi."

“Siwezi kujizuia. Ikiwa unapenda kula hivi, kwa hiyo naweza tu kwenda pamoja nawe.” Alvin alichukua uma na kuchungulia mezani. Angeweza tu kula mishikaki iliyojazwa pilipili ya kutosha. Hakujua ikiwa ni kwa sababu hakuwa na mlo mzuri huko Sudan Kusini, lakini baada ya kujaribu nyama choma, aligundua kwamba ilikuwa limechomwa vizuri na yenye ladha tamu bila kutarajia. "Agiza nyama choma nyingine."

Lisa na Pamela walitazamana kwa kutoamini. Kisha, Lisa aliagiza nyama zisizo na viungo kwa ajili ya Alvin. Yeye alianza kula mishikaki ya pilipili na Pamela.

Mishikaki ilikuwa mitamu sana, lakini pilipili nayo ilikuwa sana mdomoni mwake. Kwa kweli Alvin hakuelewa kwanini alihisi mishikaki ile kuwa mitamu japo hakuwa mpenzi wa vyakula vya migahawani. Hata hivyo, aliona kwamba uso wa Lisa ulikuwa ukionyesha sura ya kuridhika kwa nadra hivyo akanyoosha mkono kumchukua mshikaki kutoka kwenye sahani ake. "Nitakulisha."

“Kohkohhhoooh!” Lisa alipaliwa kwa mshtuko.

Alvin akampa glasi ya maji na kunywa midomo kadhaa kabla ya kutulia. kisha akasema kwa woga, "Hapana, nitakula mwenyewe."

Pamela akachombeza, “Jamani, mwache tu akulishe. Kuna umuhimu gani wa kuwa na wanaume kando yako, basi?.”

Alvin akaguna, hivi kweli mwanamume alitakiwa kufanya hivyo ili kuonyesha upendo wake kwa mwanamke? Alvin Kimaro, ambaye alikuwa ameishi kwa karibu miaka 30, alikuwa akimlisha mwanamke kwa mara ya kwanza hadharani maishani mwake. Alisogeza kijiti kilichochomekwa mishikaki iliyochomwa vizuri mdomoni mwa Lisa, baada ya Lisa kuibana kwa meno yake na kuivuta kutoka kwenye kijiti, alimwacha atafune huku akimtazama kwa mahaba. Lisa alihisi raha iliyochanganyikana na uchungu. Kwa kweli, Alvin wakati mwingine alikuwa romantic sana, na wakati mwingine haeleweki kabisa.

Alvin alimwita mhudumu na kuamuru, "leta mishikaki mingine kumi."
Kisha, akamgeukia Lisa na kusema, “Ukiwa uko pamoja nami, huhitaji kula kwa mikono yako tena.”

Lisa akaguna na kumwangalia Pamela kwa aibu. Hata hivyo, ilipendeza sana kulishwa—hata zaidi wakati mtu aliyemlisha alikuwa ni Alvin, mtu mgumu kabisa kuyateka mapenzi yake.

Kando, Pamela, ambaye alikuwa akila mishikaki yake taratibu, ghafla alihisi kama alikuwa amevamia tu meza ya wapendanao. Shetani alaaniwe, walikuwa wanamrusha roho kwa kuwa yeye alikuwa singo? Baada ya kumaliza mlo wao, Pamela alitoa kisingizio cha dharura na kuondoka haraka. Alvin alimshika Lisa mkono na kuongozana naye hadi kwenye gari. “Ulipanga kwenda wapi tena?” Lisa alichanganyikiwa. "Sinema?"

Alvin aliinua kichwa chake na kumwita Hans. "Kodisha ukumbi wote wa sinema wa Northern Sky Mall. Nitatazama filamu na Lisa baadaye.”

Lisa akapigwa na butwaa. Kukodi ukumbi mzima wa suinema kwa ajili ya filamu ya wao wawili tu? Kulikuwa na filamu maalumu alitaka kutazama naye, au pengine hakutaka tu wengine wamwone kwenye sinema pamoja naye? Nusu saa baadaye, Alvin alimpeleka kwenye jumba la sinema huko Northern Sky Mall. Meneja mkuu wa jumba hilo aliwapokea na kuwapeleka kwenye ukumbi wa wanandoa wa VIP.

Lisa alichagua filamu ya ‘action’ kwa sababu kulikuwa na mtu mwigizaji wa kiume aliyempenda sana, James Bond. Wakati wakitazama sinema, Alvin alimweka Lisa kifuani mwake. Mgongo wa Lisa ulikosa raha baada ya muda mrefu, lakini Alvin hakugundua. Simu yake iliita mara mbili na kugundua kuwa simu ya kwanza ilikuwa ya Melanie huku nyingine ikitoka kwa Bibi Kimaro.

Akainyamazia simu na kuitupa mfukoni. Akainamisha kichwa chake kwa Lisa na kumuuliza, "unapenda aina hizi za sinema?"

"Nadhani." Kwa kweli alipenda hisia za kutazama sinema na watu wengi kwenye sinema.

“Nitafuatana nawe mara nyingi wakati wowote ninapokuwa huru." Vidole vya Alvin vilikiminya kiuno chake taratibu. “Bado kinauma?”

Lisa alifikiri alitaka kumfanya tena usiku hivyo akakaidi. "Bado nahitaji mwezi mwingine mzima, angalau."

Alvin alishusha macho na kumtazama kwa kina. “Si lazima unikumbushe. Daktari tayari aliniambia. Nauliza kwa sababu Daktari Melisa alisema unaumwa leo.”

“Sijambo. Haina uchungu sasa,” Lisa alisema kwa uaminifu.

Alvin alihisi amekasirika na aliweza tu kumvuta kwenye mapaja yake. Alimbusu kwa upole na kusema kwa sauti ya upole, “Nakuahidi, sitafanya hivyo tena.”

“Mmh.” Lisa hakuamini. Haikuwa rahisi kwake kusahau tukio lile.

Baada ya filamu, Alvin alimrudisha kwenye makazi yake mapya ya New Metropolis. Lisa hakuweza kujizuia kuuliza, “Umeondoka kwa zaidi wiki moja. Si urudi kwenye makazi ya familia?"

"Hapana." Alvin alikataa kabisa. Baada ya kuoga alipitiwa na usingizi muda si mrefu akiwa amejilaza kitandani. Ilionekana wazi kutoka kwa uso wake kuwa alikuwa amechoka sana siku hiyo.

Lisa akawasha simu yake. Makala juu ya habari hiyo ilionyesha picha ya Alvin akirudi nyumbani na Jack. Jack alikuwa akishushwa kwenye ndege akiwa juu ya machela na alionekana kuwa hajitambui Uvumi ulienea kwamba alikuwa amejeruhiwa.

Siku mbili baadaye, Lisa aligundua Jack alikuwa hospitalini. Alimtembelea akiwa na zawadi na maua. Baada ya kutomuona kwa muda wa nusu mwezi, Jack alikuwa amebadilika ngozi na kukonda. Paji la uso wake lilikuwa limefungwa kwa chachi, na alikuwa akicheza na simu kitandani ili kujisahaulisha maumivu yake. Alipomwona Lisa akiingia, aliinua mkono wake kumsalimia.

Lisa alikaa chini na kusubiri kwa muda. Alipoweka simu yake chini, hatimaye aliuliza, "Je, unacheza gamme gani?"

“Wallock. Unataka kucheza pia? Niongeze kama rafiki." Jack alitabasamu, akionyesha safu zake mbili za meno meupe.

Lisa alimwambia kitambulisho chake na wawili hao wakaongezana kuwa marafiki. Kisha, alisema kwa shida, "Nilisoma habari na nikasikia kwamba kuna jambo lililokupata huko Sudan Kusini.."

"Ndio, nilinaswa na waasi." Jack alitabasamu kwa uchungu. "Nilikosa chakula kwa siku chache na hata kujeruhiwa."

"Samahani." Lisa alijisikia hatia. Kama Jack asingemsaidia kwa kamishna wa ardhi, asingemkasirisha Alvin.

“Unaomba msamaha wa nini?” Jack alicheka. "Nilikuwa na bahati mbaya tu."

"Jack, uko vizuri leo?" Mlangoni, Lea Kimaro na Mason Campos waliingia pamoja. Lisa hakutarajia kukutana nao akainuka haraka. Macho yake hayakuweza kujizuia kumtazama Mason, baba mzazi wa Jack na baba wa kambo wa Alvin. Alionekana mpole na mstaarabu kabisa.

“Kwa nini uko hapa?” Lea alikunja uso alipomuona Lisa.

“Mama, unamfahamu?” Jack akatabasamu. “Ni yule niliyekuambia hapo awali, ambaye gari lake lilichezewa na nusura afe kwa ajali. Lakini mwishowe, alichukua njia ya ujasiri na utulivu ambayo iliokoa maisha yake. Anaitwa Lisa Jones."

“Oh.” Lea mara chache aliona mwanawe akimsifia mwanamke namna hii. Alikunjua uso wake kwa tabasamu.

Sura ya 185

“Uncle, Aunty, tutaonana tena. nitaondoka sasa hivi.” Lisa hakutaka kubaki. Aliondoka baada ya kuwasalimia.

Lea aliuliza bila kuficha, "Jack, unampenda?" Macho ya Jack yaliangaza huku akiinamisha kichwa chake. "Kidogo, lakini ana mpenzi."

Lea alipigwa na butwaa na kutoridhika. "Yeye ni binti haramu wa familia ya Ngosha na hafai kuwa nawe. Isitoshe, niliona kwamba anafahamiana na Chester Choka pia. Unapaswa kujua vizuri jinsi Chester anavyopenda mabinti kama hawa.”

“Mama, Lisa si mtu wa aina hiyo. Usimwite tu binti wa haramu. Ili kuiweka wazi, nilikuwa pia mtoto haramu zamani,” Jack alijibu kwa kutoridhika.

“Wewe…” Kifua cha Lea kilijaa kwa hasira.

"Sawa, acha kubishana," Mason alisema kwa upole, "si ulisema Jack atafute mtu ambaye anapenda kuwa mpenzi wake ili asifuate nyayo zako?"

Lea akahema. “Naogopa tu utanyanyaswa sana. Alvin atamuoa Melanie. Akikutana na binti wa haramu wa familia ya Ngosha, utakandamizwa na Alvin maisha yako yote, unaelewa?"

Jack aliganda. “Alvin atamuoa Melanie?”

"Inaonekana babu na bibi yako wanataka kumpangia ndoa, haswa kwa sababu ulipata ajali hivi majuzi huko Sudan Kusini na sifa yake kuharibiwa. Joel Ngosha ni mtu mashuhuri nchini, hivyo Alvin anaweza kuokoa sifa yake kwa kuoa binti ya Joel.”

Lea alikuwa amemaliza kuongea ghafla aliposikia Mason akisema, “Bi. Jones, mbona umerudi?”

Waligeuka kutazama mlangoni na kukuta Lisa alikuwa amesimama. Uso wake ulikuwa umepauka kidogo. "Nimesahau simu yangu." Lisa alichukua simu yake na kuondoka mara moja, lakini alichokuwa akikisikia kichwani mwake ni maneno ya Lea tu. Kifua chake kilihisi kama kimepigwa ngumi kali, na kichwa kilikuwa kikipasuka kwa maumivu.

Lisa alijicheka kwa dharau moyoni! Alvin alikuwa akipanga kuoa. Jana yake tu, alikuwa amemlisha mishikaki kwa mahaba kama yote na kutazama naye filamu, na kumpa maneno mazito ya mapenzi.
Hah, kwa hiyo alitaka kuwa nao wote na kumfanya mmoja mke na mwingine mchepuko?

Jack alitazama sura ya Lisa ikipotea na mwanga wa ajabu ukaangaza machoni pake. “Mama, nampenda Lisa. Wakati mwingine, hadhi ya mtu si muhimu. Kwa kukosa maneno bora, Melanie ni mtu asiyefaa kitu, lakini Lisa ni tofauti na alikulia katika shida. Ikiwa binti haramu kama yeye atamwangusha Melanie katika siku zijazo, je, hilo halitapendeza?”

Lea akanyamaza. Hiyo ilikuwa kweli. Alikuwa amekutana na Melanie, naye alikuwa tu binti mjinga mwenye kiburi aliyedekezwa. Kuhusu Lisa
Jones…“Sawa, nitaangalia historia yake.” Lea alimwambia Jack kinyonge.

Alasiri hiyo, rundo la habari kuhusu Lisa liliwasilishwa kwenye dawati la Lea. Kilichomshangaza Lea ni kwamba Lisa alikuwa amechukua udhibiti wa kampuni kubwa ya Mawenzi ndani ya mwezi mmoja hivi. Aliwafunga wanahisa wote kwenye kidole chake. Kilichomshangaza zaidi ni kwamba Alvin alikuwa akiikandamiza Mawenzi kwa siri tangu siku chache zilizopita. Jack alikuwa amemsaidia Lisa mara moja kuhusu Mawenzi na mara akatupwa Sudan Kusini na Alvin.

Mason Campos alikuwa kishaelewa kisa cha Jack kutupwa Sudan Kusini. “Jack alimkasirisha Alvin kwa sababu alikuwa akijaribu kumsaidia Lisa Jones.

"Nafikiri Melanie lazima alimshawishi Alvin amkomeshe Lisa, lakini hakutarajia Jack angeingilia kati, kwa hivyo alikosa furaha." Lea alikasirika zaidi baada ya kugundua ukweli.

Mason akampiga bega. "Achana nayo. Si Alvin tayari amemrudisha Jack? Nadhani Lisa sio mbaya, na Jack anampenda msichana huyu sana. Ni kwamba ataweza kumsaidia sana atakapoonewa na familia ya Ngosha.”

Moyo wa Lea ulitetemeka. "Ingawa yeye si mzuri kama nilivyokuwa zamani, bila shaka atakuwa bora kuliko Melanie katika siku zijazo."

Alifikiria maneno ya Jack. Ikiwa Mawenzi Investiments ingeweza kuinuka haraka na kushamiri huko Kenya, Lisa angeweza hata kuwa jiwe kuu la kukanyagia la Jack. Jambo muhimu zaidi ni kwamba Joel alimpendelea Lisa zaidi kati ya binti zake wawili, kwa hiyo ikiwa wangemsaidia, Joel angekumbuka wema wao na kwa hakika kuchukua upande wa Jack katika siku zijazo.

“Wacha wawasiliane. Tutaona jinsi mambo yanavyokwenda.” Lea alikuwa mfanyabiashara na alikuwa akifikiria kila wakati kwa faida ya kampuni yake.

Ofisini, Lisa alitazama wakati. Ilikuwa saa kumi na mbili jioni hivyo ilibidi ajiandae kurejea nyumbani mapema. Wakati huo Alvin alimtumia ujumbe ghafla. [Sitarudi usiku wa leo. Nenda ulale mapema.]

Ilionekana kana kwamba hakukuwa na haja ya kurudi haraka. Aliwasha tena komyuta yake ili aendelee na kazi lakini hakuwa na mood hata kidogo. Kichwa chake kilivamiwa na maswali ya ajabu ajabu. Je, angekuwa akijivinjari na Melanie usiku huo? Au alikuwa anarudi kwenye makazi ya rasmi ya familia ya Kimaro kuzungumzia harusi yake?

Alikuwa karibu kuoa. Ikiwa angeendelea kumbana Lisa namna ile baada ya ndoa yake, Lisa angejidharau sana maisha yake yote. Ilibidi awe na nguvu ili aweze kuachana naye mapema iwezekanavyo.

Katika makazi ya kifahari ya familia ya Kimaro, Alvin alishuka kwenye gari na kumuona Melanie akiwa amemshika mkono Bibi Kimaro huku wakienda kutembea bustanini. Alikunja uso na bila fahamu alitaka kugeuka, lakini Bibi Kimaro alikuwa amemwona. “Alvin, uko kwa wakati. Melanie nami tunaenda kwenye bustani kuchuma matunda, njoo jiunge pamoja nasi.”

“Bibi, nimechoka. Nataka kurudi chumbani kwangu—” Alvin alihisi kukereka.

“Nataka unisindikize na unasema kwamba umechoka, ina maana hunipendi kiasi hicho?” Uso wa Bibi Kimaro mara moja ukawa haupendezi. Alvin hakuwa na jinsi zaidi ya kuwafuata bustanini.

Bibi yake kwa makusudi alibaki nyuma kwa hatua kadhaa na kuwaacha wawili hao watembee mbele yake. Njiani, Melanie alizungumza na Alvin, lakini kwa kila sentensi kumi Alvin alijibu moja tu. Baada ya kufika kwenye bustani ya strawberry, Melanie alichuma moja na kuonja. Macho yake yalikuwa yakiangaza. “Bwana Kimaro, stroberi ni tamu sana.”

"Hujawahi kula strawberry hapo awali? Unahitaji kuzidisha kiasi hicho?" Alvin alishindwa kujizuia kusema kwa kejeli.

"Unasema nini?" Bibi Kimaro alimpiga na fimbo yake kwa hasira.
"Bibi, usimpige." Melanie alimsimamisha haraka yule bibi na kumtazama Alvin huku akiona haya. “Nimejitia aibu Bwana Kimaro. Stroberi ni laini na nzuri, kwa hivyo wasichana wanazipenda sana.”

Alvin akawaza baada ya kusikia maneno yake. Lisa pia angezipenda, sawa? Alionekana kumuogopa sana siku hizi, lakini bila shaka angefurahi ikiwa angemwonyeshea mapenzi motomoto. Kwa hivyo, aliinua kikapu na kuchuma stroberi kwa bidii, akichagua kubwa zaidi na nyekundu zaidi.

“Mpenzi, tazama hizi, zimeiva vizuri sana.” Wote wawili walikua pamoja kama ua la lotus. Melanie aliweza kuchuma strawberry hizo huku akitabasamu kwa furaha.

Tukio hili lilipigwa picha haraka na Bibi Kimaro ambaye hakuwa mbali. Lo, mbinu yake haikuwa mbaya. Kutoka kwenye picha, walionekana kama wanandoa wenye upendo. Alvin hakuona na akaendelea kuchukua stroberi kutoka mkononi mwa Melanie na kuiweka kwenye kikapu chake. Angemuonyesha Lisa baada ya kuirudi usiku, bila shaka angeipenda.

Melanie akaguna kwa mshangao. Alvin alimaanisha nini kwa kuiondoa bila neno lolote? Je, ilimaanisha kwamba aliipenda sana? Ilikuwa nadra kwamba Alvin alitaka kitu chake. Moyo wa Melanie ulihisi ladha ya utamu.

Baada ya kumaliza kuchuma matunda, Bibi Kimaro alimwambia mpishi, "Chukua stroberi kwenye kikapu cha Alvin na uandae keki ya strawberry."

"Nina matumizi mengine ya stroberi hizi." Alvin alichukua kikapu na kukiweka juu.

Uso wa Melanie ulibadilika kidogo. Ilionekana kana kwamba alikuwa hajafikiria juu yake. Ikiwa Alvin alichukua nyingi kiasi kile, ilikuwa dhahiri alikuwa akimpelekea mtu. Sasa ni nani huyo aliyekuwa akipelekewa hizo strawberry?.

TUKUTANE KURASA 186-190

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.......... LISA
KURASA......186-190

Sura ya 186

Melanie ghafla akakumbuka kwamba kulikuwa na mwanamke amejificha katika jumba lake la kifahari siku moja. Alitafuta mtu wa kuchunguza baadaye lakini hakuweza kupata chochote.

"Oh, nilikumbuka ghafla, nilimwambia amchulie Queen kabla ya hii." Bibi Kimaro alipiga kichwa chake. "Nina kumbukumbu mbaya sana."

"Oh, kumbe!" Melanie alionekana kuridhika kidogo.

Saa moja na nusu usiku, kijakazi mkuu alikuja ghafla na rundo la vitu vya gharama kubwa baada ya chakula cha jioni. Bibi Kimaro alisema, “Unapomrudisha Melanie baadaye, peleka vitu hivi kwa familia ya Ngosha pia. Melanie na wewe mtapata cheti chenu cha ndoa kesho.”

Mara moja Melanie alishusha uso wake kwa haya na kumtazama Alvin kwa matarajio, lakini Alvin alionekana kuwaka na kuuliza, “Nilikubali kufunga ndoa lini?”

"Ikiwa hautaoa sasa, unapanga kusubiri hadi lini?" Bibi Kimaro hakukasirika mara chache, lakini safari hii alipaza sauti. “Ndio hivyo, umemrudisha Jack salama, lakini sasa hivi kuna tetesi huko nje kwamba unataka kumuua ndugu yako mwenyewe. Melanie ni binti ya akina Ngosha, na familia ya Ngosha ni mojawapo ya familia kumi bora nchini.

Wanaheshimiwa na watu, kwa hiyo kwa kuoa binti wa familia na kuonyesha upendo wako, unaweza kurejesha sifa yako.”

“Haya.” Alvin alionekana kama amesikia utani. Cheko la chinichini lilimwagika kooni. "Kwa uwezo wangu na ustadi wangu, bado ninahitaji kufanya maigizo ili kujisafisha machoni pa watu?"

Bibi Kimaro alisema, “Kwa jinsi mtandao ulivyoendelea sasa, utajisafisha vipi bila kick?” Hee, mpaka bibi yule alijua mambo ya kiki, lakini Alvin bado hakumwelewa.

“Sijali.” Alvin akasimama. “Kama unafikiri nina sifa mbaya, basi mwache Jack aketi kwenye kiti cha mwenyekiti. Nina uwezo na mamlaka, hivyo sijali wengine wanasema nini.”

“Unajaribu kunipeleka kwenye kaburi langu?” Bibi Kimaro alipiga meza kwa hasira.

"Mwili wako ni mgumu sana, kwa hivyo hautakufa." Alvin aliifuta midomo yake kwa umaridadi na kwenda juu. Dakika mbili baadaye, alibeba kikapu cha strawberry na kuelekea mlangoni.

Uso wa Melanie ulikuwa mweupe wa karatasi, na Bibi Kimaro akasema kwa hasira, “Subiri. Mrudishe Melanie nyumbani.”

“Sawa.” Kulikuwa na mwanga wa hasira kwenye macho ya Alvin alipokubali. Melanie alikimbia kwa furaha na kuufuata mlango na kuingia kwenye gari lake.

Kabla hajafunga mkanda, gari la Alvin lilifyatuka kama roketi. Alvin alionekana kama anarusha kombeo badala ya kuendesha gari. Gari lililokuwa likiyumba njia nzima. Gari hilo lilifikia mwendo wa karibu kilomita 200 kwa saa, jambo ambalo lilimtisha Melanie hivi kwamba alipiga kelele njia nzima.

Baada ya kuufikia mlango wa makazi ya akina Ngosha, Alvin alifunga breki na Melanie akatapika mara baada ya kushuka kwenye gari. Alvin alitoka nje ya gari kwa umaridadi na kumpa kitambaa. Melanie alishangaa sana na kukipokea, lakini sekunde iliyofuata, alisikia sauti yake ya kupendeza ikipiga masikio yake. "Kama ningekuwa wewe, ningeachana kabisa na uhusiano huu."

"Unamaanisha nini?" Melanie alikuwa na wasiwasi kidogo.

Alvin akawasha sigara na kuing'ata huku akivuta pumzi. Kitendo hicho kilikuwa kizuri, lakini macho yake yalikuwa hayajali. “Huoni? Sivutiwi na wewe hata! Kwanini usiseme tu ukweli kwa kila mtu kuwa mimi na wewe hatuendani ili tuachane tu kwa amani.”

“Sikuamini." Melanie karibu kulia. “Alvin, unanipenda. Vinginevyo, kwa nini ulicheza nami na kuja nyumbani kwetu kwa chakula cha jioni?"

“Wewe ni kipofu.” Alvin alimtemea mate kuyasindikiza maneno hayo matatu moja kwa moja.

Melanie karibu kuvunjika. Angewezaje kumdhalilisha hivi? “Sitaki kuachana na wewe Bwana Kimaro, nimekupenda kwa muda mrefu. Siwezi kuishi bila wewe.”

"Inaonekana hunielewi." Alvin aliinua uso wake.

Melanie alishika mkono wake na kusema kwa huzuni, “Bwana Kimaro, Najua una mwanamke mwingine nje. Naweza kulifumbia macho. Babu na Bibi Kimaro pia wananipenda na watafurahi tukioana. Sifa yako imeharibiwa sasa, kwa hivyo ikiwa habari kuhusu wewe kuwa na mwanamke mwingine itaenea sasa…”

“Unanitisha?” Alvin akamshika kidevu.

Melanie alitetemeka, lakini aliuma meno na kujipa nguvu. “Bwana Kimaro, sitaachana na wewe. Ni wewe uliyechukua hatua ya kunifuata kwanza.”

"Sawa, wacha tucheze mchezo wa kuigiza." Alvin alimuachia na kuingia kwenye gari.

Melanie alilitazama gari lake likiondoka kwa macho yaliyojaa hofu na woga. Nina na yeye walikuwa na nafasi katika familia ya Ngosha kwa sababu walikuwa na familia ya Kimaro kama msaada wao. Hata Mzee Ngosha aliwatendea adabu mama na binti yake kwa sababu tu Melanie alikuwa mkwe wa familia ya Kimaro. Asingeweza kupoteza kizembezembe Bwana Kimaro. Aliamini ni lazima kulikuwa mhalifu nyuma yake aliyekuwa akimchochea. Ikabidi ajue huyo mhalifu ni nani na kumuua.

Akiwa ndani ya gari, Alvin alimpigia simu Lisa. "Unafanya nini? Niko njiani kurudi nyumbani.”

"Ninafanya kazi kwa muda wa ziada ofisini." Lisa alishtuka, si alisema hatarudi?

"Kwa nini unafanya kazi ya ziada wakati tayari usiku umeingia sana?" Sauti ya Alvin haikufurahishwa. “Subiri hapo nitakuchukua.”

Lisa aliitazama simu yake huku akihisi kuchukizwa kidogo. Alichukia sana alipokuja kumtafuta baada ya kuwa amechoka kujiachia na Melanie. Nusu saa baadaye, gari la Alvin lilisimama nje ya jengo la kampuni hiyo na Lisa akaingia kwenye gari. Gari lilijaa harufu ya manukato ya mwanamke. Ilikuwa ni harufu aliyokuwa ameisikia kwa Melanie hapo awali. Alikuwa na hakika kabisa kwamba alikuwa ametoka tu kumrudisha Melanie nyumbani. Je, hakuchoka kushughulika na wanawake wawili kwa wakati mmoja?

“Angalia nilichokuletea.” Alvin alinyanyua kikapu cha stroberry kwenye kiti cha nyuma na kukiweka kwenye mapaja yake. “Nilizichuma mwenyewe kwenye bustani ya Bibi Kimaro. Ni tamu sana.”

Alitazama macho yake kwa kutarajia kwamba angefurahia. Ilikuwa mara yake ya kwanza kujaribu kujipendekeza kwa mwanamke. Lakini, kilichomkatisha tamaa ni kwamba Lisa alizitazama tu na kutabasamu, ila tabasamu hilo lilionekana wazi kuwa la kujilazimisha tu.

"Asante." Lisa alichukua sitroberi moja kutoka kikapuni.

"Hii inaonekana kama sisi." Alvin alimshika mkono kwa nguvu, macho yake ya kupendeza yakizunguka kwa upole huku yakionyesha mwonekano wake. Lisa alisikiliza sauti yake ya upole na ya sumaku. Alipomtazama, alipoteza mawazo kwa muda. Mwanaume huyo alijua kutongoza sana. Hata baada ya kumfanyia mambo hayo mabaya, alipochagua kuwa mpole, ilikuwa vigumu kwake kujiondoa.

Alvin alitabasamu na kuinamia kumbusu kwenye midomo yake.
Midomo yao ilipokaribia kukutana, harufu ya manukato ya Melanie ndani ya gari ilimfanya ageuze uso wake, na busu lake likakwama.

Hewa yenye utata iliibuka mara moja. Muwasho ulimtoka ghafla Alvin kifuani. Alikumbuka jinsi alivyokuwa mpumbavu mapema kuchuma strawberry kwa ajili yake akifikiri kwamba angezipenda. Hata hivyo, alichopata ni majibu ya nusu nusu tu.

Hata hivyo alijua haikuwa sahihi kumlaumu na akashusha pumzi ndefu. Akamgusa kichwa. “Ninavuna nilichopanda. Nilikuumiza, lakini muda utaniruhusu kufungua moyo wako. Usijali, nina muda wa kutosha.”

Lisa alishangaa. Alifikiri kwamba angekasirika tena, badala yake alijutia matendo yake na kuahidi kutomuudhi tena. kwa kweli hakuweza kumudu matokeo.

Kisha, Alvin akawasha gari na kumrudisha Lisa hadi New Metropolis Park. Shangazi Yasmini aliosha yale matunda, na Lisa alikula matunda kwa utii. Kama Alvin alivysema, strawberry zilikuwa tamu sana na nzuri.
Walipoenda kulala usiku, Alvin alimkumbatia na kushika sikio lake, akisema kwa uchungu, “Ikiwa unazipenda, nitakuchumia nyingine wakati ujao.” Lisa alitetemeka kwenye kumbato lake na kuinamisha macho yake kwa kutabasamu.

Sura ya 187

Kesho yake asubuhi Lisa alipoinuka tu kitandani aliwasha simu yake. Alikuwa na mazoea ya kuwasha simu yake kutazama barua pepe alizotumiwa kutoka kwa watendaji wake wa kampuni na kutazama habari zilizovuma. Hoja kubwa iliyovutia watu kwenye mitandao ya kijamii ni picha zilizokuwa zikimwonyesha mwenyekiti wa kampuni kubwa ya KIM International Alvin Kimaro akiongozana na mpenzi wake mpya kuchuma strawberry.

Katika picha hiyo, Melanie alikuwa akiinamisha kichwa chake kumtazama Alvin huku macho yake yakiwa yamekunjamana kwa tabasamu. Walionekana watamu sana. Alikuwa ameshika sitroberi iliyoshikamana na strawberry nyingine, na Alvin alikuwa akimtazama kwa uso wake mzuri. Mwangaza wa machweo ya jua uliangukia kwenye nyuso zao, na kuwafanya waonekane kama jozi ya wapendanao wanaobadilishana mapenzi wao kwa wao.

Ghafla alikumbuka kile Alvin alichosema jana usiku. "Je, stroberi hii haifanani na sisi?" Heh, ni ujinga gani. Alikuwa amechukua stroberi ambayo Melanie aliichuma na kumwambia mwanamke mwingine vile. Je, hakuona aibu hata kidogo?

Naam, kulikuwa na nini cha kuonea aibu? Angeweza hata kuchuma stroberi kwa bibi yake akiwa na mpenzi wake. Ukosefu wake wa aibu ulikuwa wa kushangaza.

"Unaangalia nini?" Alvin, ambaye alikuwa amelala amemkumbatia, aliinama kutazama skrini ya simu yake. Picha iliyokuwemo ilimtia hofu na kusema haraka, “Usielewe vibaya. Bibi yangu alinilazimisha niende naye jana.”

“Mmh, ni sawa.” Lisa alisema kwa utiifu na uso uliotulia.
Uso wa Alvin ulikuwa mgumu na ulijawa na alama za kuuliza juu yake. “Unamaanisha nini kusema hivyo?”

Lisa hakuelewa kwa nini alikosa furaha ghafla na aliweza kusema ukweli tu, “Yeye ni mpenzi wako, kwa hiyo ni kawaida nyinyi wawili kuchuma strawberry pamoja. Sitakuwa na wivu. Najua mahali pangu.”

Alikuwa ni mtu tu ambaye alikuwa akimtumia kwa burudani yake. Alikuwa na utambulisho wa aibu. Alvin alimtazama kwa muda kabla ya kucheka ghafla. Lisa aliumia sana. Wema na unyenyekevu wake viliufanya moyo wake kuishia kwenye machungu. Angeweza walau kumheshimu ingawa hakumjali hata kidogo.

Alvin alikuwa na wasiwasi kwamba angeelewa vibaya na hata akajieleza kwa haraka. "Wow, Lisa Jones, wewe ni mkarimu sana. jana nilitumia nafasi hiyo kumwambia Melanie kuwa simpendi, anajidanganya tu kuwa nitamuoa" Alvin alicheka kwa ujeuri. Ghafla akainua blanketi na kuingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo.

Dakika mbili baadaye, alifunga mlango na kuondoka. Lisa hakumuelewa. Je, alitarajia kumwona akilia na kupata wivu? Ni yeye aliyesema kuwa Melanie atakuwa ameshika wadhifa wa Bi Kimaro, huku yeye akiishia kulala naye tu kwenye kitanda kimoja. Ingekuwa zamani angepata wivu, lakini kilichobaki sasa ni chuki yake kwake. Moyo wake ulikuwa umeganda na haukudunda kabisa kwa ajili ya Alvin.

Alvin alienda kwenye kampuni akiwa na uso uliopooza sana na mara akampigia simu Bibi Kimaro. “Ulipiga hiyo picha?” Ni watu wa familia ya Kimaro pekee ndio wangeweza kumpiga picha akiwa ndani ya nyumba hiyo.

"Ustadi wangu wa upigaji picha wa Bibi ukoje?" Bibi Kimaro alicheka. "Nimewafanya monekane vizuri pamoja, sivyo?"

“Bibi…” Alvin alipaza sauti yake akiwa amejawa na hasira.

“Unapiga kelele nini? Unajaribu kunitisha?” Sauti ya Bibi Kimaro ilikuwa kubwa kuliko yake. "Nini? Wewe ni mjukuu wangu. Siwezi kukupiga picha?”

"Hupaswi kuziposti picha zangu kwenye mitandao ya jamii bila ridhaa yangu." Alvin alijipapasa na kusaga meno.

“Kwa hiyo kama nimeziposti utanifanya nini?” Bibi mzee hakununua maneno yake hata kidogo.

Alvin alikosa la kusema kwa hasira. Bibi Kimaro alifoka kwa hasira. “Umeona kila mtu kwenye mtandao anachosema kuhusu picha yako na Melanie? Wote wanasema kwamba nyinyi wawili ni wanandoa wanaofaa na kwamba ninyi wawili mnapendana sana. Kila mtu anakusifu kwa kuwa mzuri na kumsifia mpenzi wako. Nitaruhusu idara ya PR ikutengenezee mtu anayependa mke kwa ajili yako.”

"Mimi ni mwenyekiti wa kampuni, sio nyota wa filamu anayetafuta kucheza muvi kwa mara ya kwanza." Alvin alikasirika sana akashindwa kuendelea kuongea nae tena akakata simu moja kwa moja.

Alvin aliingia kwenye mtandao na kugundua kwamba watu wengi kweli walikuwa wakimsifu yeye na mke wake mtarajiwa. Kilichomchukiza zaidi ni kwamba kulikuwa na watu wake wa karibu ambao walitoa habari kwamba alikuwa karibu kuoana na Melanie mwezi ujao. Ilikuwa ni fujo kabisa.

Kwa hasira alimpigia simu meneja wa idara ya uhusiano wa umma na kumuamuru aondoe haraka habari hiyo kwenye mitandao.

Meneja alihisi si sawa kuiondoa habari hiyo hasa ukizingatia kuwa watu walianza kusahau sifa mbaya dhidi ya Alvin na kuanza kumpongeza. "Lakini bosi sifa zako zilianza kubadilika.,,"

"Bosi ni mimi au wewe?" Alvin alimkatisha kwa ukali.

"Sawa, nitaondoa habari mara moja." Meneja alitikisa kichwa kwa huzuni.

Ingawa habari hiyo ilifutwa mara moja kwenye mitandao yote ya kijamii, suala hilo lilikuwa tayari likivuma. Kila mtu nchini Kenya alijua kuhusu hilo. Kila mtu alijua kwamba Melanie na Alvin walikuwa wanandoa sasa.
Kwa upande, Lisa hakuwa na presha kwa sababu alikuwa kishajua siku nyingi.

Kelvin alimtumia ujumbe: [Alvin ni mkatili sana kwako. Lisa, ninajitahidi niwezavyo ili kupata nguvu zaidi. Hivi karibuni, nitakuokoa kutoka kwake]

Lisa aliguswa moyo sana na kujali kwake. Jinsi Kelvin alivyokuwa mwema kwake, ndivyo alivyohisi hatia zaidi.

Siku mbili zilizofuata, Alvin hakurudi New Metropolis Park. Lisa hakujua alilala wapi kwa siku zote hizo, wala hakuuliza.

Usiku, Jack alimpigia simu. "Niliruhusiwa jana."

“Hongera sana!” Lisa alijibu kwa upole.

"Niko hapa kukusanya madeni wakati huu." Jack alitabasamu. “Si ulisema unataka kunishukuru? Nitashiriki katika hafla ya hisani kesho, kwa hivyo nitakuomba kufuatana nami." Lisa alisita mwanzoni, lakini aliposikia kwamba lilikuwa tukio la hisani, alikubali.

Siku iliyofuata saa kumi na moja jioni, Jack aliendesha gari lake na kumchukua Lisa kwenye lango la ofisi ya kampuni yake. Lisa haraka akaingia kwenye gari. Jack alitazama nguo zake alizokuwa amevaa na kumshauri. “Umependenza sana Lisa lakini mavazi yako hayafai kwa tukio husika. Nitakupeleka mahali fulani ili ubadilishe.”

Saa moja baadaye, Lisa alitoka kwenye chumba cha kuvaa akiwa amevaa nguo nyekundu ya retro.

“Nzuri!” Jack alipiga vidole vyake.

"Kwa nini nivae hivi kwa hafla ya hisani?" Lisa alichanganyikiwa.

"Hapana, ni chakula cha jioni cha hisani," Jack alisema ghafla.
Lisa alisimama na kukunja uso. “Bwana Kimaro, ulinidanganya? Siendi.”

Ikiwa alikutana na Alvin, angemkaripia kwa kuwa mwanamke rahisi tena. Labda hata angemtesa baada ya kurudi nyumbani usiku. Alimuogopa Alvin sasa.

“Nilidanganya lini? Chakula cha jioni cha hisani bado ni tukio la hisani." Uso wa Jack haukuwa na hatia. “Unanisusia? Nitapata wapi rafiki wa kike wakati huu?”

“Bwana Kimaro, sitaki uvumi uenee…”

“Utakuwa tu mwenzangu wa kike. Usifikirie sana. Mbali na hilo, usifikiri kwamba sijui. Tayari umeachana na Kelvin Mushi.” Jack alimpasulia.

Jack alipoona hajashawishika akapiga makofi kifuani kwa kicheko. “Usijali, hakuna mtu unayemfahamu kwenye chakula cha jioni cha hisani usiku wa leo. Ulipokuja Nairobi kwa mara ya kwanza, ulisema kwamba unapaswa kwenda kwenye hafla ili kukutana na watu wengi zaidi. Unapanga utafanyaje biashara zako bila kutengeneza milango?"

Moyo wa Lisa ukadunda kwa nguvu. Ikiwa alitaka kumtupa Alvin, ilibidi ajipe nguvu kwanza. Hatua muhimu zaidi ilikuwa ni kutengeneza connections.

“Sawa, nitakupa kampani.” Lisa akajitosa.

Katika Hoteli ya ya kimataifa ya Rean, Nairobi. Tukio kubwa la chakula cha jioni cha hisani lilikuwa likifanyika. Jack Kimaro aliingia huku akiwa amemshika mkono Lisa. Alikuwa amevaa suti iliyomtoa kama mheshimiwa fulani alyekuwa akitokea bungeni. Kando yake, Lisa alikuwa kapendeza sana kwenye gauni refu jekundu lililofunika mpaka viatu na nywele ndefu zenye kuvutia zililala mabegani mwake, na mdomo wenye rangi nyekundu ya divai. Alikuwa mzuri na mwenye kung'aa, mrembo asiye na kifani katika kizazi chake.

“Yule binti kando ya Jackson Kimaro ni nani? Yeye ni mrembo sana!” Mara watu wakaanza kuulizana.

"Sijawahi kumuona hapo awali."

Sura ya 188

Mawimbi ya mjadala yalielea hewani, lakini Lisa hakujishughulisha na kusikiliza, alitazama tu skrini kubwa iliyokuwa mbele yake iliyosema 'Kimaro Foundation Charity Night'.

‘Huu ulikuwa ni usiku wa hisani ulioandaliwa na familia ya Kimaro? Je, Alvin atakuwa hapa?’ Lisa alijiuliza akiwa amejawa na hofu.

Alipotazama huku na huko, alihisi kama atazimia. Sio Alvin pekee bali hata Melanie, Bibi Kimaro, Mzee Kimaro, Lea, Valeria na wanafamilia wengine wa Kimaro wote walikuwepo. Hata Nina na Joel walikuwepo pia. Pia walishangaa kuwaona watu hao wawili.

Lisa alihisi tu miguu yake ikitetemeka. Sasa, aliweza kumuona Alvin tu machoni pake. Alikuwa amevalia suti nyeusi. Macho yake meusi na mazito yalikuwa yakimtazama kwa ujumbe ambao yeye pekee ndiye aliuelewa.

"Si ulisema ... hakutakuwa na mtu yeyote ninayemjua?" Alimtazama Jack kwa hasira kidogo.

“Ungekujaje kama sikusema hivyo?” Jack alitabasamu na kumkonyeza. “Huoni kwamba Nina na Melanie wako hapa pia? Nilikuleta hapa makusudi ili uwakoshe.”

“Jackson…” Lisa alitaka kulia. Alikuwa na nia nzuri, lakini mpango wake ulikuwa unaenda kinyume.

“Wacha waone kwamba kuna uhusiano maalumu na mimi. Tutaona ni nani atakayethubutu kukuonea siku zijazo.” Jack alimshika mkono kwa nguvu na kuelekea kwenye umati wa watu.

"Lisa Jones, kwa nini uko hapa?" Melanie alikuwa karibu kulipuka kwa hasira. "Una wivu kwa sababu Alvin yuko nami kwa hivyo ukajipendekeza kwa Jackson Kimaro ili akutungoze?"

"Mimi ni Jack Kimaro ni marafiki." Lisa alishusha pumzi ndefu kabla ya kueleza, akihakikisha Alvin anamsikia.

Alvin akazungusha glasi ya mvinyo mkononi mwake. Uso wake mzuri ulikuwa umekunjamana na haukubadilika, lakini Mzee Kimaro ndiye aliyesema kwa sauti nzito, “Jack ulimkaribia lini? Una miaka mingapi hapa Nairobi? We Jack kwanini unashindwa kuwa macho zaidi?”

Joel akamvuta Lisa pembeni yake. "Mzee Kimaro, Lisa ni binti yangu, sio mgeni."

Nina naye alidhihaki, “Mpenzi, huelewi? Binti haramu ni binti haramu tu. Waheshimiwa na wasomi wote kutoka matabaka mbalimbali wapo hapa usiku wa leo. Uwepo wake utafanya kila mtu acheke. Itaathiri sifa yako."

Jack alinyoosha mikono yake. “Mnafanya nini jamani? Ni mwenza niliyemleta. Usiingiliane ikiwa hujui ni nini kimenikutanisha naye. Utafanya mambo kuwa mabaya zaidi.”

"Inatosha, acha ugomvi," Lea alizungumza ghafla, "Jack alizungumza nami juu ya jambo hili hapo awali. Nilikubali kumruhusu aje naye.”

Kila mtu alishangaa, na macho ya Alvin yalimtoka. “Wewe…”

“Tayari utafunga ndoa na Melanie na Jack si mtoto tena,” Lea akamkatisha.

Nina alikataa kukubali. “Lea, unaweza usijue hili, lakini Lisa ni sawa na mama yake. Tabia yake—”

“Kwa kawaida najua tabia yake ni ya namna gani. Sihitaji wengine kunielekeza.” Lea alikuwa amesimama katika nafasi ya juu kwa muda mrefu. Alipotazama juu, shinikizo lilimfanya Nina ashindwe kusema neno lolote.

“Asante mama,” Jack alisema huku akitabasamu.

Lisa alichanganyikiwa kabisa. Hakuwahi kufikiria kuwa Lea angemtetea. Ilikuwa ni upuuzi.

"Kaa chini, chakula cha jioni kiko karibu kuanza." Bibi Kimaro alimpa jicho la maana Lisa. Kulikuwa na mambo ambayo hayakuhitaji kuharakishwa. Kwa vyovyote vile, asingekubali Jack na Lisa kuwa pamoja. Lisa alikuwa binti haramu na hakustahili kuwa na mjukuu wake.

Kulikuwa na watu mashuhuri wachache waliohudhuria chakula cha jioni cha hisani usiku huo. Baada ya kila mmoja kuketi, Alvin alipanda jukwaani akiwa mwenyekiti wa mfuko na kutoa hotuba. Umbo lake kamili lilikuwa limefungwa kwa suti, na kumfanya aonekane mtukufu na mashuhuri.

Hata alipokuwa akikabiliwa na mikwaju mingi mikubwa chini ya jukwaa, haiba tulivu iliyotoka kwenye mwili wake ilifanya umati kumsifu.
Melanie alimtazama mwanamume huyo jukwaani na kuzidi kupendezwa.
Aliapa ni lazima amshikilie kwa nguvu kabisa mwanamume mrzuri na mtanashati kama Bwana Kimaro.

Nina aliweza kuwaza ni nini binti yake alikuwa akifikiria na kumnong'oneza sikioni, "Ikiwa unataka kumshinda mwanamume kabisa, lazima ushinde kwanza mwili wake."

“Lakini huwa haniruhusu nimguse…” Melanie alikuwa na wasiwasi.

“Chukua fursa hiyo usiku wa leo anapolewa. Nitamwambia bibi yake akuruhusu uende chumbani kumtunza Bwana Kimaro.” Nina alitumbua macho yake kama mchawi.

Wazo lilimjia Melanie. Alipofikiria kuwa mwanamke wa Alvin, uso wake mdogo ulikuwa na aibu, lakini alikuwa akitarajia. “Mama, Lisa hataweza kupatana na Kimaro wa Pili, sivyo…?”

“Anafikiri yeye ni nani? Hastahili. Yeye ni mhalifu kama mama yake." Uso wa Nina ulikuwa umejaa dharau. "Utaona jinsi nitakavyoshughulika naye usiku wa leo."

Baada ya Alvin kushuka jukwaani, waimbaji maarufu walicheza kwa zamu jukwaani. Onyesho lilipokaribia kwisha, Jack aliinama kwenye sikio la Lisa na kusema, “Nitaenda nyuma ya jukwaa kuchukua pesa zilizokusanywa. Nitarudi baadaye.”

“Sawa.” Lisa alitingisha kichwa.

Tukio hilo lilitua machoni mwa Alvin, na kufanya kifua chake kujaa moto wa hasira. Mwanamke aliyelaaniwa! Mara tu alipotazama pembeni, alijibizana na mwanaume mwingine? Wakati huu, alikuwa hata na mdogo wake, Jack. Alikaribia kuivunja glasi ya mvinyo mikononi mwake.
Baada ya kutulia, alitoa simu yake na kumtumia Lisa ujumbe: [Nisubiri kwenye Chumba namba 408.]

Lisa alipokea ujumbe huo. Alimtazama Alvin na kumuona akitazama kwa umakini wasanii waliokuwa wakicheza jukwaani. Alimlaani moyoni. Mnafiki gani!
Kwa kweli hakutaka kwenda kukutana naye. Ilikuwa hatari sana. Aliinamisha kichwa chake na kujibu: [Unaweza kusubiri mpaka turudi?]

Alvin: [Nina hasira sana sasa. Usijaribu kuniudhi zaidi.]

Lisa akawa mpole. Alitabasamu kwa uchungu na aliweza tu kuinuka kimyakimya ili kuondoka. Alipotoka tu kwenye jumba la karamu, mwanamume mlevi wa rika la makamo alimsimamisha ghafla. "Mwanamke mrembo, una wakati wa kuzungumza chumbani kwangu kwa muda?"

“Niko busy.” Lisa hakuhitaji hata kumjua kabisa, akageuka na kuendelea na mwendo wake.

Yule mtu mnene ghafla akamshika kiganja chake na kutabasamu. "Unajua mimi ni nani? Nina pesa nyingi. Ukiwa tayari kuniburudisha kwa usiku mmoja, nitakupa milioni kumi.”

“Kwanini nisikupe hiyo milioni kumi ili upotee mbele yangu badala yake?” Lisa alikwazwa sana na yule jamaa.

"Sawa, usiseme sikukupa chaguo." Yule mwanaume mnene alimsukuma ukutani na kujaribu kumbusu kwa nguvu.

“Niache!” Lisa alimpiga kofi usoni.

“Unathubutu vipi kunipiga, wewe b*tch…” Mwanamume huyo aliinua mkono wake kuuzungusha chini, lakini kiganja kikubwa kikaushika mkono wake hewani. Kisha, mwili wa mtu mnene ulitupwa kando.

“Unathubutuje? Wewe…” Alipomwona mtu mmoja mrefu alimesimama mbele yake, yule mwanamme mnene aliogopa sana hadi miguu yake ikatetemeka. “Bwana Kimaro…”

“Bwana Kimaro, umefika kwa wakati. Alinitongoza.”

"Ndio hivyo? Mkurugenzi Majuto, unathubutu kusababisha vurugu katika moja ya hafla zetu? Inaonekana huhitaji kushiriki katika karamu za jamii ya juu katika siku zijazo.” Alvin alimwambia Hans kwa upole, “Vunja mguu wake mmoja na umtupe nje.”

“Bwana Kimaro, usi…” Mkurugenzi Majuto aliogopa sana akataka kupiga magoti na kuomba msamaha, lakini alikuwa amechelewa. Hans akamtoa nje haraka.

Sura ya 189

“Jack alikuleta hapa, lakini hivi ndivyo anavyokulinda?” Alvin alicheka kwa jeuri. Alipofikiria jinsi midomo ya nguruwe huyo aliyelaaniwa ingemkandamiza usoni ikiwa angechelewa kwa hatua moja tu, alikasirika sana na alitaka kupagawa kwa wazimu.

Lisa alitetemeka huku akisema kwa unyonge, “Hii ni karamu ya chakula cha jioni iliyoandaliwa na KIM International, hivyo Mkurugenzi Majuto asingenisumbua bila sababu. Mtu fulani alimwagiza kufanya hivyo.”

“Oh? Angekuwa nani huyo?” Alvin aliinua uso wake, hakuzungumza kile alichokijua.

Lisa aliuma mdomo. Hakuamini kwamba hakujua ni nani. Alikuwa akifumbia macho tu maana mtu huyo alikuwa mchumba wake. “Sijui…” Aligeuza uso wake sekunde moja baadaye.

Alvin alimtazama kwa makini kwa muda, akadharau na kumvuta juu juu.
Hakuna mtu kati ya wawili hao aliyeona kwamba muda si mrefu baada kuondoka, mtu mmoja alitoka kwenye kona aliyokuwa amejifcha akiwafuatilia. Baada ya kuingia chumbani, Alvin aliufunga mlango kwa nguvu. Akavua suti yake na tai na kuzitupa chini.

“Lisa Jones, mimi sikufai? Kwa nini unaendelea kunilazimisha kukasirika tena na tena?”

Alvin alimsogelea hatua kwa hatua, huku uso wake ukiwa umejawa na hasira. “Kuachana na Kelvin Mushi hukuridhika, kwa hiyo safari hii ni Jack Kimaro. Huwezi kunipa amani?”

“Hapana, sikujua alikuwa akinipeleka kwenye karamu ya chakula cha jioni. Alisema tu kwamba lilikuwa tukio la hisani. Alinisaidia kutatua mzozo wa Mawenzi hapo awali, kwa hivyo nina deni kwake.” Lisa aliingiwa na hofu na hasira iliyokuwa usoni mwake na kukumbuka jinamizi alilolipata usiku ule. Uso wake mdogo mara moja ukageuka mweupe huku machozi yakimdondoka. Alipiga magoti na kumshika mkono, akimsihi, “Hapana, tafadhali usinidhuru. Ninaogopa.

Sitathubutu kufanya hivyo tena…” Mwili wake ulitetemeka kama jani, na macho yake yalijawa na hofu na woga.

Alvin aliganda. Alimtazama na kukunja ngumi kwa maumivu. Alikuwa amepiga magoti mbele yake? Wakati fulani alikuwa mkaidi na mkorofi, lakini sasa, alikuwa akipiga magoti na kumwomba amhurumie? Je! alikuwa anamuogopa kiasi gani?

Alvin alimnyanyua kwa nguvu. “Lisa Jones, huruhusiwi kunipigia magoti. Unanisikia? Wewe ni mwanamke wangu.”

“Sawa, sitapiga magoti. Mimi ni mwanamke wako. Nitasikiliza chochote utakachosema,” Lisa alisema kwa unyenyekevu.

"Hicho sio nilichomaanisha." Alvin alimkumbatia kwa nguvu. “Huna haja ya kuogopa. Nilikuambia sitakuumiza. Nina wivu tu. Umevaa vizuri sana bado umesimama kando ya Jack. Usionane naye tena siku zijazo.”

Lisa aliitikia kwa utii. “Sawa, nilikusudia tu kumlipa fadhila nilizokuwa nazo. Sitakutana naye tena.”

“Vizuri.” Alvin aliinamisha kichwa na kumbusu midomo yake. Hakujua ni aina gani ya lipstick alikuwa amepaka lakini ilikuwa na ladha kama ya stroberi. Akambusu kwa pupa. “Nifanye nini na wewe?”

Lisa alikuwa kimya muda wote na kumruhusu tu ambusu anavyotaka.
Hata hivyo, taratibu alihisi jambo la ajabu juu ya mwanamume huyo na kumsukuma kwa nguvu. “Usifanye hivi. Hafla ya hisani bado haijaisha, na mwili wangu hauwezi…”

“Najua. Sitaenda mbali, lakini acha nikushike tu.” Alvin naye hakujua kinachoendelea. Labda ni kwa sababu alikuwa amekunywa divai nyingi chini ya ghorofa, au labda ni kwa sababu Lisa alikuwa mrembo sana usiku huo. Alitaka tu kumshika mikononi mwake na kumbusu kwa nguvu.
Lisa hakuweza kupinga nguvu za mwanamume huyo na punde si punde alimbusu hadi mwili wote ukaishiwa nguvu na kulegea kabisa.

Ghafla, mlango uliokuwa umefungwa ukafunguliwa kwa nguvu na kundi kubwa la watu wakaingia kutoka nje. “Nilimsikia mhudumu akisema kwamba Mkurugenzi Majuto alimleta Lisa hapa…”

Kabla Melanie hajamaliza, aliona umbo refu na la kupendeza juu ya kitanda. Kichwa chake kilionekana kumlipuka na kuhisi kuwa ana kichaa. “Bwana Kimaro, mbona uko hapa?”

Alvin macho yakamtoka na haraka akavuta blanketi ili kuufunika mwili wa Lisa. Lisa pia alipata hofu. Alipowaona watu walioingia mlangoni, alihisi kama ulimwengu unaelekea mwisho. Alikuwa amekwisha! Wakati huo, alihisi kweli kwamba, pale Kalivari, yote yalikwisha!

Baada ya kuishi kwa zaidi ya miaka 20, hakukuwa na wakati ambapo alihisi aibu kama alivyokuwa smuda huo. Melanie Ngosha, Jack Kimaro, Bibi Kimaro, Lea Kimaro, Joel Ngosha, na Nina Mahewa wote walikuwepo. Wakawatazama watu wawili pale kitandani kwa mshtuko. Nguo zilizokuwa juu ya mwili wa Alvin zilikuwa zimevuliwa, na uso laini wa Lisa ulikuwa umejaa haiba ya mahaba. Hata mpumbavu angeweza kujua kile ambacho wawili hao walikuwa wakifanya.


Bibi Kimaro alikasirika sana hata mkono wake uliokuwa umeshika fimbo ulikuwa unatetemeka.

"Lisa Jones, wewe b*tch!" Melanie alipoteza akili kabisa na kukimbilia kumpiga kama kichaa. “Una aibu kiasi gani? Umemtongoza hata mchumba wangu!”

Hata hivyo, kabla mkono wake haujatua kofi hilo, alishikwa na Alvin na kumtupa pembeni kwa nguvu. Melanie alipoteza usawa wake na akaanguka chini.

Nina alimuunga mkono kwa haraka huku akitetemeka kwa hasira. “Bwana Kimaro, kweli ulimsukuma Melanie kwa sababu ya huyu b*tch? Bibi Kimaro inabidi leo utupe ufafanuzi. Huwezi tu kuwaonea watu namna hii!”

Mwili wa Bibi Kimaro ulikuwa ukitetemeka huku nusura azimie kwa hasira. Hakufikiria kamwe kwamba mjukuu wake mwenye kiburi angefanya jambo hilo la kuumiza na la kipumbavu.

Jack haraka akamuunga mkono na kuwatazama watu wawili pale kitandani huku wakionyesha uchungu. “Kaka kampuni tayari ni yako na haikuwa rahisi kwangu kupata mwanamke ninayempenda. Kwanini umeamua kumpokonya pia?”

Lisa alipigwa na butwaa. Jack alimpenda lini?

“Kukupokonya?” Kicheko cha chini na cha kijeuri cha Alvin kilisikika ghafla masikioni mwake. Aliongea kwa ukali, "Amekuwa mwanamke wangu siku zote, kwa hivyo nilikupokonyaje?"

Kila mtu alipigwa na butwaa, na Lea naye akauliza kwa hasira, “Mmekuwa kwenye uhusiano muda wote huu?”

Mdomo wa Alvin ukafunguka, lakini Lisa aliogopa na kumshika mkono wake kwa kusihi. "Inatosha, usiseme."

Alvin alikasirika. Mwanamke gani mjinga huyu. Hakutaka kufichua uhusiano wao hata wakati kama huo? Je, kweli alitaka kuchukuliwa kama mchepuko wake tu? "Hiyo ni sawa."

Maneno hayo mawili rahisi yaliposemwa, Melanie alihisi kama anga lilikuwa karibu kuanguka. Alilia na kupiga kelele, “Nimeelewa sasa. Nilipokwenda nyumbani kwako hapo awali, alikuwa chumbani kwako, si ndiyo?"

“Melanie Ngosha, nilishawahi kukuambia kuwa haiwezekani kati yetu na hata nilipokupa nafasi ya kuanzisha uchumba, uliwahi kuniuliza kama nina mpenzi? Au ulikuwa unaashumu tu kuwa sina?” Alvin alijibu kinyonge.

“Hata kama wewe ni nyota, unawezaje kukosa chembe ya huruma? Melanie ni mzuri sana, unawezaje kumuumiza hivi?!” Bibi Kimaro alikasirika na kuokota fimbo yake ili ampige.

Alvin hakuikwepa, akatulia tu akapigwa na fimbo. Bibi Kimaro alipoona sura yake ya ukaidi, shinikizo la damu lilipanda juu. Alipoteza fahamu na kuzirai.

“Bibi…” Alvin alishtuka na kumwachia haraka Lisa kumchukua yule kikongwe. "Pigia ambulensi haraka."

Chumba kilikuwa na fujo. Melanie alipofushwa na chuki na akachukua fursa hiyo kumshambulia Lisa, huku akikuna uso wake. “Wewe mhalifu! B*tch! Nitakuua!"

“Melanie, nitakusaidia!” Nina naye aliingilia.

Sura ya 190

Mama na binti walivuta blanketi lakini Lisa alilishikilia kwa nguvu. Hata hivyo, Melanie alifanikiwa kumpiga Lisa makofi kadhaa na kumkwarua usoni na kumfanya apate kizunguzungu kutokana na maumivu hayo.

Alvin alikuwa na wasiwasi na alikuwa karibu kumuweka Bibi Kimaro chini wakati Valeria alipomsihi, “Fanya haraka umpeleke bibi yako hospitalini! Unataka afe kweli?”

“Unathubutu vipi kutongoza wachumba wa watu?! Nitakuharibia uso!” Nina akachukua kisu cha matunda.

Joel alikuwa na wasiwasi na kukimbilia kuwavuta wale wanawake wawili, mama na binti. “Mmeshikwa wazimu?”

“Wewe ndiye mwendawazimu. Joel Ngosha, angalia tu b*tch uliyemzaa. Aliharibu furaha ya Melanie!” Nina alionekana kuwa na kichaa. Tukio hili lilimfanya amkumbuke Sheryl Masawe kutoka zaidi ya miaka 20 iliyopita.

Joel pia hakuweza kujua ni nani alikuwa sahihi na ni nani asiyefaa, lakini kitu pekee alichokuwa na uhakika nacho ni kwamba asingeweza kuruhusu mtu yeyote kumuumiza Lisa.

"Mungu wangu, nini kinatokea hapa?" Ghafla, kundi kubwa la waandishi wa habari nao wakaingia kutoka nje. Ingawa walikuwa wamekosa kipengele muhimu, huku Bibi Kimaro akiwa amepoteza fahamu, nguo za Alvin na Lisa Jones zikiwa zimechanika, na jinsi Melanie Ngosha na Nina Mahewa walivyokuwa wakipigana, wangeweza kukisia kilichotokea.

"Ondoka njiani!" Alvin alinguruma kwa sauti ya juu. Aliwakodolea macho waandishi wa habari alipombeba Bibi Kimaro kumtoa nje ya chumba hicho. “Iwapo yeyote atathubutu kuripoti mambo ya leo, nitamzika pamoja na kampuni yake.”

Baada ya onyo hilo, waandishi wa habari waliogopa sana kiasi cha kumtazama tu Alvin akimtoa bibi mzee yule bila kuchukua picha yoyote. Hata hivyo, haikuwazuia kutazama kipindi hicho kizuri.

Kila mtu wa familia ya Kimaro alikwenda hospitali, na ni watu wa familia ya Ngosha tu ambao walikuwa wanapigana. Kwa bahati nzuri, ilichukua dakika mbili tu kwa Hans kuleta watu na kumsindikiza Lisa kutoka hotelini.

Uso wake ulikuwa umechanwa sehemu nyingi huku akivuja damu sana. Wakati huo, uso wake ambao hapo awali ulikuwa safi ulikuwa wa giza na wa kutisha. Hata hivyo, hakujali. Macho yake yalikuwa mepesi kana kwamba ni kikaragosi asiye na roho. Kwa kweli hakuweza kuelewa jinsi mambo yaliyofikia hatua ile. Kulikuwa na wakati ambapo alitaka sana kuruka nje ya gari na kufa ili kuzima aibu zake.

Hans naye alikasirika na kumkabidhi kitambaa. Lisa hakusogea, na Hans akamfariji. “Bi. Jones, usijali. Teknolojia ya matibabu imeendelezwa sana sasa. Majeraha yako yanaweza kutibiwa bila kuacha kovu. Hutaharibika sura.”

Maneno hayo yalimfanya Lisa acheke kidogo kana kwamba amesikia mzaha. Alikuwa amefanya kosa gani? Je, Mungu alitaka kumwadhibu hivi kwa sababu tu alidhani kwamba Alvin ni mjomba wa Ethan wakati huo? Hans alikuwa amepoteza na alikuwa na maumivu ya kichwa. Hakujua la kumwambia. Kwa kweli, alimwonea huruma sana Lisa.

Baada ya kufika katika hospitali binafsi, daktari wa daraja la kwanza alikuja kumsaidia kutibu majeraha yake. Lisa alimruhusu daktari amzungushe. Wakati fulani, alihisi kwamba itakuwa sawa hata kama angeharibika sura. Hapo awali, alijivunia sura yake nzuri. Pia ni kwa sababu ya sura yake aliweza kumvutia Alvin bila matusi. Hata hivyo, alikuwa ameonja matokeo yake sasa. Ilikuwa bora kuwa na sura mbaya. Ikiwa angekuwa mbaya, labda Alvin angemwacha aende zake. Alijawa na huzuni!

Wakati uso wake ukiwa umefunikwa na chachi, ghafla alimuona Kelvin akiingia kwa kasi kutoka nje. “Lisa, nilisikia kwamba jambo fulani lilikutokea…”

Kelvin alipouona uso mzuri wa Lisa uliofunikwa na chachi, aliumia moyoni. “Hivi ndivyo Alvin Kimaro anavyokutunza? Anawaruhusu wengine kukudhuru hivi? Anafanya nini namna hii, achana naye nimekuambia, njoo kwangu…”

“Bw. Mushi, mmesahau kuhusu onyo hilo?” Hans alimkumbusha Kelvin.

"Nilifikiri kwamba Alvin Kimaro atamtunza vizuri." Kelvin alionekana mwenye hasira. “Kwa kuwa hawezi kumlinda, kwa nini alimchukua? Ilikuwa ni kuthibitisha tu kwamba angeweza kunizuia kuwa na Lisa?”

Lisa akanyamaza. Hiyo ilikuwa kweli. Hadi hapo hakufikiri kwamba kweli Alvin alikuwa naye moyoni. Ikiwa alimpenda, asingemuumiza sana na kumkanyaga.

“Hili ni suala kati ya Bi Jones na Bwana Kimaro. Wewe ni mtu wa nje tu,” Hans alikunja uso na kukumbusha, “Ondoka njiani. Vinginevyo, msinilaumu kwa kukosa adabu.”

“Kelvin, nenda tu,” Lisa alisema kwa upole, “Usisahau ulichoniahidi.”
Kelvin aliganda. Aliwahi kumtumia ujumbe mfupi wa simu akisema kwamba atapata nguvu na kumwokoa.

“Sawa.” Alikunja ngumi na kuvumilia maumivu. "Lazima ujitunze."

“Nitajitahidi.” Lisa aliitikia kwa kichwa huku akikaribia kumwaga machozi.

Jijini Nairobi, ni Kelvin pekee aliyewahi kumjali kwa dhati. Alijuta. Kwa nini alikuwa akimpinga hapo awali? Ni mpaka wakati huo tu ndipo aliweza kuona ni nani aliyemtendea mema.

“Bi. Jones, twende zetu.” Hans alizuia safu ya macho ya wawili hao.
Lisa akasogea mbele, na Kelvin aliendelea kutazama alipokuwa akiondoka.

Mara tu baada ya Lisa kuondoka, Kelvin alipiga namba ya siri kwa huzuni. “Lini hasa utashughulika na Alvin Kimaro? Nataka tu afe sasa!”

“Una haraka gani? Alvin Kimaro tayari yuko kwenye kilele chake. Yeye si rahisi kukabiliana naye.” Mtu wa upande mwingine alicheka. "Lakini kila kitu kimepangwa. Ni lazima tu ufanye kama ninavyosema.”
•••
Katika hospitali nako mambo yalikuwa ni faya. Mzee Kimaro akamshushia kibao Alvin. “Wewe mpuuzi! Nilikulea kwa moyo wote kwa miaka mingi na hivi ndivyo unavyonilipa?”

“Baba, nina hakika Alvin hakukusudia. Ni lazima alitongozwa na yule mwanaharamu.” Valerie alikuja haraka ili kusuluhisha na kumtazama Alvin. “Umemsikia? Fanya haraka uombe msamaha kwa babu yako na uahidi kutowasiliana na Lisa Jones tena.”

“Haiwezekani. Tayari nimeamua kumuoa.” Alvin alisimama pale kimya, macho yake yakiwa yametulia na sauti yake ikiwa thabiti.

Kila mtu alivuta pumzi. Uso wa Mzee Kimaro ulikuwa wa ajabu. "Nadhani umeshikwa na uchawi wake. Ukitaka kumuoa, itabidi utembee juu ya maiti yangu kwanza.”

Lea alikunja uso na kusema, “Tayari umemfanya bibi yako azimie kwa hasira. Je, unajaribu kufanya vivyo hivyo kwa babu yako? Kila mtu anajua kuwa unachumbiana na Melanie, na Lisa alihudhuria hafla hiyo usiku wa kuamkia leo kama rafiki wa kike wa Jack mbele ya kila mtu. Habari kwamba Lisa na wewe sasa mko pamoja zitaenea kesho, familia ya Kimaro itakuwa kituko.”

Ingawa Lea alikuwa na maoni mazuri ya Lisa hapo mwanzo, aliona tabia ya Lisa ya kufanya mambo ya kuzunguka kuwa ya kuchukiza.

“Hiyo ni sawa." Mjomba wa Alvin, Spencer Kimaro, pia alishauri, “Nimepokea habari kwamba tukio zima lilikuwa limeharibika. Ingawa hakuna vyombo vya habari vinavyothubutu kuripoti, habari tayari zimeenea kote. Alvin, hili ni pigo zito kwa sifa yako. Ukisisitiza kufanya hivi, habari mbaya kwenye mtandao kuhusu wewe zitakuwa kali zaidi.”

"Ikiwa bado unataka kuketi katika nafasi ya mwenyekiti wa kampuni ya KIM lazima umuoe Melanie Ngosha mara moja na uzime uvumi huo," Mzee Kimaro alisema kwa hasira.

“Siwezi kumuoa." Alvin alibaki bila wasiwasi.

“Wewe...” Mzee Kimaro alikasirika sana asijue la kusema.

TUKUTANE KURASA 190-195

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......191-195

Sura ya 191

Melanie, ambaye alikuwa akisikiliza kwa upande akiwa na uso uliopauka, alishindwa kujizuia kulia, “Bwana Kimaro, kuna nini kizuri kuhusu Lisa? Ni binti haramu tu. Je, ni kwa sababu anajua kujitongozesha—”

“Melanie Ngosha, afadhali uangalie mdomo wako,” Alvin alionya bila kujieleza.

Uso wa Nina ulikunjamana kwa hasira huku akibishana, “Bwana Kimaro, ulimkaribisha Melanie machoni pa watu wote acheze nawe kwenye ukumbi, na akina Kimaro wakasema kuwa atakuwa mpenzi wako, lakini sasa unasema hapana? Unacheza na akina Ngosha tu? Ataolewa vipi katika siku zijazo?"

Mzee Kimaro naye alijiona wamekosea. "Tutawapa maelezo baadaye, kina Ngosha."

“Vizuri, nakuamini Mzee Kimaro. Jambo hili lisipotatuliwa, ninaamini kwamba habari hizo za aibu za familia ya Kimaro zikienea, hakuna familia yenye ushawishi itakayothubutu kuoa au kuolewa na mtu wa familia ya Kimaro siku zijazo. Na… ikiwa umma utafahamu kuhusu hili, ninaogopa nchi nzima itamwita mhuni.” Nina alimaliza kuongea na kumvuta bintiye waondoke.

“Umesikia walichokisema akina Ngosha?” Mzee Kimaro alikasirika na kutishia, “Kama utaendelea kusisitiza, kesho naikabidhi nafasi ya mwenyekiti wa KIM International kwa Jack. Si wewe pekee katika familia ya Kimaro.”

"Sitaachana naye." Alvin alikunja uso, huku macho yake yakionekana kutojiweza. "Babu, samahani."

“Ondoka nje.” Mzee Kimaro alikasirika sana hakutaka kuongea naye tena.

Wanafamilia ya Kimaro wote walikuwa wakionekana kutafakari. Ilionekana ni kweli kungekuwa na mabadiliko kwa mtu anayesimamia familia ya Kimaro.

Saa tano usiku, Alvin aliingia hospitalini akiwa amevalia shati jembamba.
Alvin hakuwahi kuwa na huzuni vile kwa muda mrefu. Uso wake mzuri uliharibiwa na alama ya kofi. Jack aliingia kutoka nje akiwa na karatasi ya maabara. Alipomuona Alvin, tabasamu changamfu na lisilo na madhara likatokea usoni mwake. “Kaka si utakaa na bibi?”

“Nitakupa nafasi ya kuwafurahisha hawa wazee wawili. Si ndivyo ulivyotaka?” Alvin alimtazama. "Umeridhika na jinsi usiku wa leo ulivyotokea baada ya kupanga kila kitu?"

“Ina uhusiano gani na mimi?” Jack alishtuka. “Alvin, haipendezi kusema hivyo wewe ndiye ulimuiba mwanamke wangu.”

"Jack Kimaro, nimekudharau." Alvin hakuwahi kumtazama Jack kwa makini kama alivyokuwa akifanya muda huo. Labda kaka yake mdogo alikuwa amefanya kazi nzuri sana ya kujificha. "Wakati Lisa alipokuwa nyumbani siku ile ya chakula cha jioni, ulimwona amejificha chumbani kwangu, sivyo?"

Jack aliinua uso wake lakini hakutoa neno. Mguso wa hasira ukamtoka Alvin. "Hukupaswa kumuumiza au kumdanganya."

Midomo nyembamba ya Jack ilinyanyuliwa taratibu na kutabasamu na kusema kikatili, “Alvin, aliyemuumiza si mimi. Ni wewe. Nilimsaidia tu kutembea kutoka gizani hadi kwenye nuru, ambapo anaweza kuonekana na kila mtu.”

"Kulikuwa na njia nyingi za kufanya hivyo, lakini hakika haukupaswa kutumia njia hiyo. Jack, sitakusamehe kwa hili.” Alvin akasogeza miguu yake mirefu na kuondoka bila kuangalia nyuma.

Kurudi nyumbani, Alvin akausukuma mlango wa chumba cha kulala, lakini taa hazikuwa zimewashwa. Harufu hafifu ya dawa ilijaza chumba, na sura ndogo chini ya blanketi ya hariri ilikuwa nyuma ya mlango. Alizunguka kwenye chumba na kusimama mbele ya kitanda. Kwa mwanga wa mbalamwezi, aliweza kuona wazi kwamba uso wake mdogo mrembo sasa ulikuwa umefunikwa na vipande vinne vya shashi, karibu kufunika pande za uso wake na kufunua kidevu chake kilichochongoka tu.

Hapo zamani, alikuwa kama mtoto mchanga aliyenenepa usoni, na alionekana mzuri sana alipomkandamiza. Sasa, alikuwa mwembamba.
Mkono wa Alvin uligusa kwa upole shashi usoni mwake. Kama mwanadamu, hii ilikuwa mara yake ya kwanza kuhisi kushindwa na kukosa nguvu. Usiku huo, aliona watu wengi wakimuumiza, lakini alishindwa kumlinda. Lazima amchukie sana.

Uso wake ghafla ulikwepa mkono wake, na macho yake yaliyofungwa kimya kimya yakafunguka mara moja-yakionyesha ukimya uliokufa ndani.

"Nimekuamsha?" Alvin akamweka chini ya blanketi. “Lala basi, usiku umeenda sana. Tuzungumzie kesho.”

“Bibi yako vipi?” Lisa aliketi moja kwa moja, akifunua vazi lake la kulalia la hariri.

“Hajambo. Ameishiwa na hasira na atakuwa sawa baada ya siku chache za kupumzika." Alvin akazipapasa nywele zake ndefu.

Lisa alishusha kope zake ndefu na kusema kwa sauti dhaifu, “Alvlisa, niache niondoke.”

Alvlisa…?! Hakuwa amemuita hivyo kwa muda mrefu! Wawili hao walipokuwa wakipendana siku za nyuma, kila mara alikuwa akimwita hivyo kwa utamu. Alvin alipoteza mawazo kwa muda.

Lisa akainuka na kupiga magoti chini. Alimtazama huku macho yakimtoka machozi. “Ngoja niende kujisaidia, sawa? Umeona kilichotokea usiku wa leo. Familia yako haitakuruhusu kuwa nami. Kwa kweli siwezi kuvumilia maisha ya aina hii. Watu wengi sana waliingia ndani na kuninyooshea kidole. Alvin, mimi pia ni binadamu. Nimechoka sana!” Alitokwa na machozi wakati akisema.

Tangu utoto wake, ingawa hakuweza kulinganishwa naye, alilelewa na bibi yake. Alikuwa na heshima na kiburi chake. Hawezi kuwa mtu wa tatu katika uhusiano. Hakuweza kustahimili dharau ya wengine. Lakini, kila kitu kiliharibiwa sasa.

Alienda Nairobi, lakini sio tu kwamba alishindwa kulipa kisasi kwa Sheryl, hata alifedhehesha kabisa jina la Sheryl. Alitaka tu kurudi Dar es Salaam. Hakutaka tena kuchunguza kesi ya Sheryl. Alikuwa amechoka sana. Kilichotokea siku hiyo kilikuwa kimevunja safu yake ya mwisho ya utetezi.

Alvin alikuwa katika sintofahamu. Hii ilikuwa mara ya yake ya pili kupiga magoti mbele yake. Mwanamke ambaye hapo awali alimpenda sana alipataje kuwa mnyenyekevu hivyo? Moyo wake ulihisi kama umechomwa na miiba na ulikuwa ukivuja damu.

"Simama." Alinyoosha mkono kumvuta.

"Ikiwa hautakubali, basi sitainuka." Lisa alimtazama, macho yake yakionekana kuwa meusi bila chembe ya mwanga.

"Lisa Jones, umekuwa hivi lini?!" Alvin alimfokea kwa hasira, “Ujasiri wako uko wapi? kiburi chako kiko wapi? Je, hujiheshimu?”

Lisa alicheka vibaya. “Si wewe binafsi ulivunja yote hayo kwa mikono yako mwenyewe? Mbele yako, sina lolote kati ya hayo...”

Mwili wa Alvin uliyumbayumba. Alikuwa mbele yake, lakini wakati huo, walionekana kutengwa kwa umbali mkubwa.

“Sitakuacha uende isipokuwa nife!” Alvin aligeuka na kutoka chumbani.
Alikesha usiku kucha katika maktaba yake akifanya kazi zake.

Saa mbili asubuhi, alitoka nje ya maktaba kwa uchovu. Wakati wa kifungua kinywa, Hans alikuja kuripoti kwake. “Mzee Kimaro na Naibu Mwenyekiti Lea Kimaro walikwenda kwenye kampuni asubuhi ya leo na kusalimiana na bodi ya wakurugenzi pamoja na watendaji wakuu wa kampuni. Jack Kimaro atachukua nafasi ya mwenyekiti wa KIM International kuanzia leo na kuendelea. Sababu ikiwa… hustahili nafasi hiyo.” Alvin alikula kifungua kinywa chake taratibu, na midomo yake ikajikunja kwa kejeli. "Bwana mzee amekasirika sana wakati huu," Hans alisema kwa kusitasita.

Hata Alvin alipokwenda Dar es Salaam mara ya mwisho, Jack alikuwa amesimamia majukumu yake akiwa kama mwenyekiti, lakini sasa ilionekana wazi kuwa Mzee Kimaro alikuwa akimshushia kipigo Alvin.

"Anaweza kufanya apendavyo." Alvin alichukua kitambaa na kuifuta mikono yake.

Sura ya 192

Hans hakuridhika kabisa, akamkumbusha Alvin kwa uchungu. “Kusema kweli, KIM International ilijiendeleza vyema mikononi mwa mama yako miaka minane iliyopita, lakini baada ya kuingia madarakani, ulienda ng’ambo mara nyingi na ukaalika watu wenye vipaji vya hali ya juu, ukaanzisha maabara binafsi, na kupanua uwanja wa sayansi na teknolojia.

Ni wewe uliyeipa umaarufu familia ya Kimaro kama familia tajiri nchini, na ukaiongoza KIM International katika makampuni kumi bora ya Afrika, lakini sasa, yote yanaenda kwa Jack? Jack Kimaro alifanya nini? Ulipokuwa bize kulala saa nane za usiku na kuamka saa kumi alfajiri, alikuwa nje ya nchi akijivinjari na akapata cheo cha juu mara tu aliporudi.”

"Ninaonekana kama mtu ninayeweza kuwapa tu wengine kile nilichofanyia kazi kwa bidii?" Alvin aliinua uso wake ghafla. Hans alinyamaza. Alvin alikitupa kitambaa alichomaliza kujifutia na kubadilisha mada. “Uchunguzi wa tukio la jana usiku ulikwendaje?”

"Mvinyo uliokunywa ulizimwa kwa glasi ya divai ambayo husaidia kusisimua nguvu za kiume." Hans alisema. "Baadaye, mtu alimwambia Melanie Ngosha kwamba Bi Jones aliletwa kwa lazima kwenye chumba ulichokuwamo na Mkurugenzi Amiri."

"Kwa hivyo ndivyo ilivyokuwa?" Alvin aliitikia kwa kichwa. Jana yake usiku, yeye, Melanie, Lisa, na Mkurugenzi Amiri wote walikuwa vibaraka mkononi mwa Jack. ni mchongo uliotengenezwa vizuri sana na Jack ili kumdhalilisha Alvin.

Alvin alitazama chumba cha kulala cha juu na kumgeukia Aunty Yasmini. “Nenda ukamwangalie Lisa.”

Punde, Aunty Yasmini alishuka kutoka ghorofani na kusema kwa wasiwasi, “Bi. Jones amelala bila kujigeuza kitandani na anakataa kula hata kunywa chochote. Nadhani hali yake ni mbaya sana. Anaonekana kama mtu asiye na matumaini wala dhamira ya kuendelea kuishi.” Maneno yale yalikuwa yakitoka kwa uchungu kwenye kinywa cha Aunty Yasmini.

"Anagoma kula?" Macho ya Alvin yalimtoka kwa hasira. Akainuka na kwenda juu.

Kama Shangazi Yasmini alivyosema, macho ya Lisa yalikuwa yamefungwa na uso wake ulikuwa umekakamaa. Hata hivyo, Alvin alijua kwamba alikuwa macho.

“Unamaanisha nini kwa kufanya hivi?” Alvin alidhihaki, “Lisa Jones, lini umekuwa mnyonge kiasi hiki?”

Kope za Lisa zilitetemeka. Ndio, hapo awali, alifikiria kuwa wazazi wake wa kibaolojia walikuwa Jones Masawe na Salome Urassa ama Mama Masawe. Walijaribu kumuua tena na tena, wakamfanyia hata njama aende gerezani na hata kumtesa hadi karibu kufa. Baadaye, alipata habari kwamba bibi yake aliuawa. Alikuwa amekata tamaa, lakini wakati huo, alikuwa tayari amekutana na Alvin kama bahati mbaya tu, na akageuka kuwa msaada wake mkubwa. Ni yeye ambaye alikuwa amempa joto na matumaini. Sasa, alikuwa kama mlima mkubwa. Hakukuwa na jinsi angeweza kupanda juu. Hakuona matumaini hata kidogo!

"Simama." Alvin alinyanyua blanketi na kumvuta kutoka kitandani. “Hutaki kuchunguza chanzo cha kifo cha mama yako?”

“Hapana…” Lisa alijibu kwa sauti ya chini. Alijua ikiwa Alvin angekuwa karibu naye, asingeweza kamwe kulipiza kisasi.

Alvin alipigwa na butwaa na kusema kwa hasira, “Ukiendelea na mawazo yako ya kuachana na mimi, nitaiharibu kabisa kampuni ya Mawenzi na kumpoteza kabisa Kelvin Mushi. Nitahakikisha nawakandamiza Joel Ngosha na hata Pamela Masanja. Maadamu hawa ni watu wa karibu sana kwako, sitamwachilia yeyote kati yao.”

“Alvin Kimaro, kwa nini usiniue tu?” Lisa alikuwa mwisho wa akili zake na kufumbua macho yake. Alichukua mto na kumrushia.

Alvin kumuona hivyo akashusha pumzi. Akamkumbatia kwa nguvu. “Lisa, sitakuua. Nataka ukae upande wangu milele. Nitakuoa na kukutendea mema. Usiniache.”

Macho yake ya mapenzi yalimfanya Lisa kuzama kwenye butwaa kwa muda, lakini muda si mrefu alidhihaki. “Unadhani nitakuamini? Niangalie usoni. Hivi ndivyo unavyomaanisha kunitendea mema?”

"Jana ... ilikuwa ajali," Alvin alielezea kwa huzuni.

“Unadhani nitakuamini?” Macho ya Lisa yalikuwa yamejaa kejeli na karaha.

“Ni kweli. Jana, divai yangu ilitiwa kichocheo. Nilidhani nilikuwa nimekunywa kupita kiasi.” Midomo ya Alvin ilijikunja na kuashiria kujidharau.

Lisa alipigwa na butwaa. Alipofikiria kwa makini jinsi alivyokuwa jana yake usiku, kwa kweli ilionekana kuwa jambo lisilo la kawaida. Hata hivyo, mwishowe, ni kwa sababu wengine walikuwa wakijaribu kupanga njama dhidi yake. Alikuwa tu mwathirika ambaye alilengwa kufanyiwa fedheha.

“Kuwa mwema. Nenda ukanawe na kula chakula. Ngoja nikukamulie dawa ya meno.” Alvin alipoona haongei, alimpapasa kichwani kwa mbwembwe na kuchukua hatua ya kwenda bafuni kumminya dawa ya meno pamoja na kumwagia glasi ya maji ya uvuguvugu kwa ajili ya kusuuza mdomo wake.

“Nitafanya mimi mwenyewe." Lisa hakumzoea Alvin kuwa vile, akachukua mswaki mwingine kabla ya kwenda chooni. Kujitazama alivyokuwa mnyonge kwenye kioo, ghafla alihisi ajabu. Sasa, hakuweza hata kujijua kama alikuwa hai ama mfu. Hakuweza kujua kama alikuwa anaota au ilikuwa ni kweli. Je, angeendelea kujitoa na kuishi maisha duni kama yale mpaka lini? Hapana, asingeweza kufanya hivyo. Kwa kuwa hakuogopa kifo tena, kulikuwa na nini tena cha kuhangaikia? Alimradi bado anapumua, angepigana na mtu huyo!

Alipotoka tena, Alvin alimtazama na kuona amebadilika. “Naweza kukusindikiza kwenda kufanya shopping, au nikupeleke likizo mahali fulani?”

“Naenda ofisini.” Lisa aliingia kwenye chumba cha kubadilishia nguo na kutafuta mavazi ya kikazi.

Alvin alimtazama usoni kwa sura isiyo ya kawaida. "Unaenda ofisini ukiwa namna hii?"

"Kwani namuogopa nani? Au itawatisha wengine?" Macho ya Lisa yalikuwa meusi na tulivu, kana kwamba alikuwa hazungumzi juu yake mwenyewe.

Alvin alikunja uso lakini akasema baada ya muda, “Fanya upendavyo.”

Lisa hakujali. Ilikuwa ni bora kwenda kutafuta kitu cha kufanya huko, kuliko kubaki na kufia nyumbani.

Saa nne asubuhi Lisa aliingia kwenye ofisi ya kampuni ya Mawenzi Investiments jijini Nairobi., Lisa alitoka kwenye lifti akiwa amevalia suti nyepesi ya rangi ya kahawia. Mwili wake ulikuwa umenyooka kama zamani na umbo lake lingeweza kupachikwa kwenye gazeti la mitindo, lakini kwa bahati mbaya, chachi iliyofunika uso wake siku hiyo iliwafanya wafanyakazi kumwangalia kwa sura za kushangaza. Hata hivyo, hakuna aliyethubutu kuuliza. Ni baada ya kupita tu ndipo baadhi ya watu walianza kunong'ona na kujadiliana.

“Ni nini kilitokea kwenye uso wa Mwenyekiti Jones? Je, alifanyiwa upasuaji?"

“Mjinga wewe. Ina maana hujui? Alikamatwa akifanya uzinzi kitandani na kupigwa?”

"Hapana, tayari ni tajiri sana lakini bado anataka kuwa mchepuko?"

“Nilisikia kuwa ni binti wa nje ya ndoa. Wakati huo, mama yake pia aliharibu ndoa ya mtu, na sasa, alimtongoza mchumba wa dada yake mdogo. Hana maadili hata kidogo.”

"Ni kweli, mmejuaje mengi hivi juu yake?" Sauti ya Lisa ilisikika ghafla kutoka nyuma yao, na wanawake wale wakaruka kwa hofu.

“Mwenyekiti- Jones… Kwanini umerudi?”

“Unataka nijieleze kwako kama nani? Jibu swali langu." Lisa alitoa mtazamo wa kimamlaka na wa kuogofya.

“S-Someone alichapisha notisi mlangoni asubuhi. Watu wengi waliiona,” mfanyakazi huyo wa kike alijibu kwa tahadhari, “samahani, Mwenyekiti Jones. Sitathubutu kusema tena.”

“Si ulisema sina maadili? Watu wasio na maadili kama mimi lazima wawe na tabia mbaya, kwa hivyo kuna faida gani ya wewe kufanya kazi kwenye kampuni ya mtu asiye na maadili? Kuna kampuni nyingi sana za watu wenye maadili mema huko mitaani. Kwa hiyo paki vitu vyako uondoke." Lisa akageuka na kurudi ofisini kwake.

Sura ya:193

"Hiyo notisi ya mlango imeondolewa?" Lisa alimuuliza msaidizi wake mara baada ya kuingia ofisini.

'Imeondolewa, lakini habari kuhusu hilo kimsingi imeenea kupitia kampuni," msaidizi wake alisema kwa kigugumizi, "Mwenyekiti Jones, usichukulie kwa uzito uvumi wa watu wengine."

'Sio uvumi. Ni ukweli.” Lisa alimtazama moja kwa moja.

Wakati huo huo, katibu wake ghafla akaingia ndani na kusema, "Mwenyekiti Jones, kuna habari mbaya. Kuna mtu alileta watu kwenye kampuni ili kufanya vurugu. Walipoingia mlangoni walianza kuvunja-vunja vitu na kusema wanataka kukuona.”

“Nitashuka.” Lisa akainuka.

Katibu huyo alishangazwa sana na Lisa. “Mwenyekiti Jones, hilo si wazo zuri. Wamebeba kamera. Lazima watakurekodi na kukuweka mtandaoni.”

“Haijalishi.” Lisa alishuka chini.

Akiwa njiani kuteremka chini ghafla alipokea simu kutoka kwa Alvin. “Usishuke. Tayari nimemjulisha Shani. Atamleta mtu kushughulikia hilo.”

"Hakuna haja. Nitalishughulikia mwenyewe.” Lisa alikuwa mbishi.

“Lisa, usiwe mbishi. Farres Mahewa ni mmoja wa watu waliokuja. Wao si watu unaoweza kujadiliana nao.”

Lisa alicheka kwa dhihaka. “Tangu nilipokufahamu vizuri Alvin, naweza kuchagua tu kujifunza kukabiliana na mambo haya mwenyewe. Baada ya yote…huwezi kunilinda kila wakati.”

Alikata simu na kutoka nje ya lifti. Mara moja, yai lililooza likampiga kwenye paji la uso wake, na papo hapo kuchafua shashi usoni mwake. Ilikuwa ni jambo la kutisha sana.

“B*tch, unaiba mpenzi wa mtu mwingine? Unastahili! Nitakupiga hadi kufa.” Msichana mdogo aliyevalia vizuri alisimama kando ya Melanie, akionekana kuchukizwa na kutapika laana.

“Mwenyekiti Jones…” msaidizi wake alishtuka na kwa haraka akamkimbilia akiwa na kitambaa cha kujifuta usoni.

Lisa aliichana ile chachi na kudhihirisha majeraha mekundu usoni mwake.

“Mbaya kiasi gani! Alvin Kimaro atakapoona sura hii lazima atatapika!” Msichana mwingine aliyevalia mavazi ya kijanja alisema kwa kuchukiza, “Mchafu kama nini, kwanza hustahili kuonekana Nairobi. Fanya haraka upotee.”

“Samahani sana kwa kusema hivyo, lakini Alvin alikuwa bado amelala kitandani kwangu asubuhi ya leo, akinipapasa usoni kwa upole na kuniambia nisimuache.” Lisa alitabasamu kwa upole, na kumfanya Melanie atetemeke kwa hasira.

Melanie alikimbilia kumpiga kofi, akisema, "Lisa Jones, nenda kuzimu!"

Lisa alikuwa akingojea wakati huo kwa hamu. Alimshika Melanie kifundo cha mkono na kumvutia kwake huku akimpiga makofi makali kadhaa. “Hivi ndivyo ulivyonipiga jana. Nakurudishia yote leo!” Melanie alipigwa makofi kadhaa na kuanguka chini.

“Unathubutuje kumwekea mkono mpwa wangu mbele yangu?! Lazima uwe na hamu ya kifo!" Farres aliingilia kati kwa hasira.

Msaidizi wa Lisa aliruka kwa mshangao na angeweza tu kukimbilia mbele kumzuia. Farres akataka kumpiga Lisa teke, na Lisa akatoa kisu cha matunda ili kukikandamiza kwenye uso wa Melanie. Macho yake hayakuwa na huruma. "Ukithubutu kunigusa, nitaharibu uso wake."

“Mjomba, usiondoke. Siwezi kukubari kuharibika sura.” Melanie aliogopa sana hata akakaribia kulia.

"Lisa Jones, ikiwa utathubutu kumgusa Melanie, nitaondoa maisha yako!" Farres alipiga kelele kwa hasira. Alikuwa amefika hapo kumnyoosha, lakini hakutarajia kutishiwa badala yake.

"Maisha yangu? Jisikie huru tu kuyachukua. Kama ningeogopa kifo, usingesimama hapa.” Lisa alidhihaki, “Lakini Melanie ni tofauti. Bado anategemea uso wake kupanda juu ya familia ya Kimaro. Nani atamtaka ikiwa ataharibika?"

"Unataka nini?" Farres alisema kwa hasira.

"Nipatie kamera zote." Lisa akamtazama.

Farres hakuwa na budi ila kupunga mkono wake, na kamera kadhaa zilikabidhiwa kwa wafanyakazi wa kampuni ya Mawenzi. Alipomaliza kukabidhi tu, kundi la askari polisi waliingia kwa kasi kutoka nje.

"Tulipokea taarifa kwamba kuna watu wamefika kwenye kampuni ya Mawenzi kufanya fujo..."

Farres alikuwa karibu kuzungumza wakati Lisa alimsukuma Melanie kando mara moja. Alitembea hadi mbele ya polisi kwa macho mekundu. “Afisa, watu hawa waliingia tu kwenye jengo hili na kuanza kuharibu mali zetu. Hata walinirushia yai viza usoni.”

Melanie alipiga kelele, “Hapana, alijaribu kwa uwazi kuniharibu uso kwa kisu! Fanya haraka ukamkamate!”

Askari polisi alimtazama Lisa ambaye uso wake ulikuwa umejaa majeraha na kupakwa maji maji ya mayai yaliyooza kisha akamtazama Melanie ambaye alikuwa amevalia vizuri na alionekana hana hata upele kabisa. Mara moja polisi alikasirika. "Ni nani aliyejaribu kuharibu uso wa mtu mwingine? Unafikiri mimi ni kipofu?”

"Bwana. Afisa, usipaze sauti yako. Huyu ni binti wa thamani wa familia ya Ngosha na mwanaume huyo ni Farres Mahewa kutoka kwa familia ya Mahewa. Nilisikia kwamba wanafahamiana na watu wazito wengi sana,” Lisa alisema akijifanya kuwa na woga.

Farres alizoea kutenda kwa kiburi na alikoroma kwa baridi alipomsikia yule polisi akiongea. “Unatoka kituo gani? Nitajie mkuu wako.”

Lisa aliangaza macho kwa mshangao na kuchombeza, "sikutarajia mkuu wa polisi kuwa mmoja wa watu wanaowajua. Ni ajabu kiasi gani.”

Macho ya afisa huyo yaliganda alipomfokea Farres kwa haraka, “Mkuu wetu hatajua watu kama wewe. Sijali wewe ni nani. Kamateni kila mtu aliyethubutu kuleta fujo hapa!” Punde, polisi waliwachukua Farres na wengine.

"Bwana. Afisa, asante sana. Tuna shukrani nyingi kwako kwa sababu mmewahi kutusaidia na tuko salama. Ninaahidi kutoa mchango baadaye mchana huu.” Lisa aliguswa na kuwasindikiza polisi mlangoni.

Shani, ambaye alifika tu na kukuta hali hiyo ikiendelea, mara moja alimpigia Alvin bila kuchelewa.

Alvin alitabasamu kwa furaha aliposikia jambo hilo. “Nenda ukamsalimie. Hakikisha watu hao wamefungwa kwa siku kadhaa jela, hasa mwanamke aliyemrushia Lisa yai lililooza.”

Shani alikumbusha, “Bwana Kimaro, mwanamke huyo ni binti wa familia ya Owino…”

“Kwa hiyo iweje?” Baada ya kukemea, Shani alisikia sauti ya simu ikikatika.
•••
Baada ya kutoka kituo cha polisi. Lisa aligundua kuwa uso wake ulikuwa na maumivu zaidi na ikambidi aende tena hospitali. Daktari kutoka idara ya magonjwa ya ngozi alipomsaidia kusafisha majeraha, Dokta Chester Choka aliyevalia nguo nyeupe aliingia ghafla.

“Hakikisha unatumia dawa bora kuponya majeraha usoni mwa Bi Jones haraka iwezekanavyo. Lazima kusiwe na makovu yoyote."

Lisa alikosa la kusema. Je, Dokta Chester alikuwa huru sana? Kwanini siku zote alikuja kumtafuta alipokuja hospitalini? Kusema kweli, sasa alikuwa amechukizwa sana na Alvin na hakuwa na mawazo mazuri ya marafiki zake pia. Ndege wenye manyoya yafananayo huruka pamoja. Aliamini rafiki zake hakika hawakuwa watu wazuri pia.

Baada ya majeraha yake kutibiwa, Lisa alisema kinyonge, “Dokta Choka, rudi kazini. Mimi pia naondoka muda si mrefu.”

“Usiwe na wasiwasi sana. Mimi ni shemeji yako.” Chester alitabasamu. “Isitoshe, utaolewa na Alvin hivi karibuni. Utakuwa shemeji yangu rasmi siku chache zijazo.”

Maneno hayo yalisikika kama dhihaka tu katika masikio ya Lisa. “Mimi si mtu sahihi. Unapaswa kusema hivyo kwa Melanie Ngosha.”

“Melanie Ngosha?” Chester aliitazama sura ya Lisa iliyoonekana kama ngeni kutokana na majeraha. Alvin alikuwa hana maana hata kidogo kumsukumia mbali mwanamke mzuri namna hiyo. Ilikuwa ni juu yake kumsaidia Alvin. “Hujui hili, lakini Alvin hampendi kabisa Melanie Ngosha. Hata alikubali kuondolewa kwenye wadhifa wake kama mwenyekiti wa KIM International ili akuoe.”

Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. Alvin hakuwa tena mwenyekiti wa KIM International? Hiyo inawezaje kuwa?

Sura ya:194

“Ina maana hujaona habari zinazovuma sasa hivi kwenye mitandao?” Chester akamsogelea. “Ni habari za kusisimua zaidi. Watu wote wanazungumza juu yake."

Lisa alipoteza mawazo kwa muda. Alijua kwamba Chester hamdanganyi, lakini hakufikiri kwamba Alvin alifukuzwa kwenye kampuni ya familia kwa sababu alitaka kumuoa. “Hiyo ni kawaida sana. Mwenendo wake haukuwa sahihi. Alikuwa na rafiki wa kike lakini bado alimnyakua kwa nguvu dada mkubwa wa mpenzi wake pia. Hakuweza hata kutawala sehemu ya chini ya mwili wake na kuharibu chakula cha jioni cha hisani kilichokuwa na familia ya Kimaro. Baada ya kufanya vitendo hivyo vya kuchukiza, bila shaka, ataondolewa kwenye nafasi yake.”

Chester aliganda. Muda kidogo, badala ya kukasirika kwa sababu rafiki yake amedhihakiwa, alicheka kwa furaha. "Tathmini yako ni ya moja kwa moja. Alvin kwa kweli ni mtu wa kudharauliwa na ana tabia mbaya."

Lisa alikunja uso, akishangaa kicheko chake. “Hilo ni jambo la kuchekesha?”

"Inasikitisha." Chester alikunja mdomo wake “Lakini baadhi ya ulichosema si sawa. Usiku ule baada ya Alvin kumpeleka Bibi Kimaro hospitali, familia ya Kimaro iligombana. Mzee Kimaro alisema muda wote Alvin amuoe Melanie Ngosha ili kusuluhisha suala hilo, lakini Alvin alikataa na kusema anataka kukuoa wewe tu jambo ambalo lilimkasirisha bwana mzee.”

"Anioe?" Lisa alionyesha kutokuamini.

Chester alimtazama kwa maana. "Nusu ya KIM International ya sasa ilijengwa na Alvin kwa mikono yake mwenyewe. Kucheza na wanawake sio kitu kipya kwa mtu kama Alvin, kwa hivyo bwana mzee asingemwondoa kwa sababu hiyo. Kosa la Alvin lilikuwa ni kuonyesha msimamo wake kwako, kuonyesha kuwa yupo serious na wewe, jambo ambalo lilimkera kabisa bwana mzee.”

Wakati anatoka hospitalini, Lisa alionekana kuwa na mawazo. Siku zote alikuwa akifikiria kwamba Alvin alimuweka kuwa mpenzi ambaye hatawahi kuona mwanga wa siku. Alikuwa kama kikaragosi ambaye hakumpenda na angemtumia tu pale alipomuhitaji. Hata hivyo,alichokisikia kutoka kwa rafiki yake kwamba Alvin alifukuzwa kazi kwa sababu aliweka msimamo wa kumuoa.

Mwenyekiti wa KIM International… Ilikuwa nafasi ambayo ilimweka juu ya wengine 10,000. Ilikuwa ni nafasi ambayo watu kutoka kote nchini waliitazama kwa uchu. Sasa, alikuwa ameanguka kutoka madhabahuni. Je, KIM International iliyompoteza Alvin Kimaro ingekuwa sawa na hapo awali?

Lisa alipoingia tu kwenye gari, Joel alimpigia simu ghafla. “Lisa, uko huru? Tukutane.”

",..sawa." Lisa alijua kwamba mambo fulani hayangeepukika.

Dakika 40 baadaye, baada ya kufika kwenye mgahawa waliokubaliana kukutana, Joel alikuwa tayari ameshamaliza kikombe cha chai. Jozi ya baba na binti wakiwa wameketi pamoja hawakuwa wamewahi kuwa na hali mbaya sana kama hiyo hapo awali. Mwishowe, bado Joel ndiye aliyevunja ukimya. "Uso wako bado unauma?"

Maneno machache ya wasiwasi yalikaribia kumtoa Lisa machozi. Kwa kweli, alikuwa jamaa yake pekee aliyebaki ulimwenguni. “Sijambo.”

“Nina na Melanie walikuwa na hasira sana jana usiku. Usijali, hata mimi nilishtuka…” Joel alitabasamu kwa uchungu. “Lisa, najua kwamba Melanie na wengine walienda kwenye kampuni asubuhi ili kukusababishia matatizo. Unaweza kuzungumza na Alvin Kimaro na kumwacha awaachie?”

Lisa alihisi baridi tu moyoni mwake. “Baba, Melanie alimleta mjomba wake na marafiki kwenye kampuni yangu ili kuvunja mali zetu na kujaribu kunipiga. Ikiwa polisi hawakufika kwa wakati, kuna uwezekano kwamba ningekuwa nimelazwa hospitalini sasa. Sio kama hujui mbinu za Farres Mahewa.”

“Lakini…” Joel alisita. “Kilichotokea kwenye karamu ya chakula cha jioni… Hakika Melanie alikuwa mwathirika. Mtu yeyote atakuwa na hasira."

Lisa alimtazama baba yake ghafla akahisi hasira. “Baba, unafikiri nilimuibia Alvin Kimaro pia?”

“Lisa, sitaki uharibu furaha yako mwenyewe ili ulipize kisasi kwa Nina na Melanie,” Joel alisema kwa uchungu.

Tabasamu la kusikitisha lilipanda usoni mwa Lisa. “Kwa hiyo ndivyo unavyonifikiria mimi. Baba, umewahi kunipenda na kujaribu kunielewa? Kusema ukweli, nimemjua Alvin kwa muda mrefu. Yeye ndiye aliyenilazimisha kuwa naye. Hivi majuzi, amekuwa akikandamiza kampuni yangu na Kelvin. Yote ni matendo yake. Je, unafikiri ninafurahia kuishi maisha yasiyo na heshima? Je, unafikiri ninafurahia kuonyeshwa kidole na kukosolewa kama mtu asiye na adabu?!” Alipoendelea kuongea, hatimaye alikabwa na machozi.

"Nini?” Joel alipigwa na butwaa. “Mbona hukuniambia mapema?"

“Ingekuwa na tofauti yoyote ningekuambia?” Lisa alimtazama kwa dhihaka, “Hukuweza hata kunilinda katika nyumba yako, sembuse mbele ya Alvin?”

Uso wa Joel ulimshuka ghafla, akajiona kama mvulana mdogo na si mtu mzima wa miaka kadhaa. "Sina maana tena kwako. Ni kweli, nilikuleta Nairobi lakini nilikuacha kuonewa na wengine, naenda kumtafuta Alvin sasa hivi. Ameenda mbali sana!”

"Huna haja ya kunitafuta, nipo hapa." Mlango wa chumba hicho cha faragha cha mgahawa ulifunguliwa kwa nguvu, na umbo la Alvin refu na dhabiti likaingia ndani.

"Mbona uko hapa, Alvin?" Lisa alisimama kwa hasira.

"Sijakushika mkia, nmekufuatilia tu ili kuja kukutana na baba." Alvin alivuta kiti kilichokuwa pembeni yake na kuketi, sura yake isiyo na aibu ilimfanya Joel achemke hadi kwenye damu.

“Baba yako ni nani? Umekuwa ukimlazimisha Lisa akusikilize wakati upo kwenye mahusiano na Melanie. Hakika sitakubali binti yangu kuolewa na mtu mbaya kama wewe."

"Nimeweka moyo wangu kwa Lisa. Unapaswa kuwa wazi kuhusu hili tangu usiku wa jana." Alvin aliweka kiganja chake kikubwa nyuma ya mkono wa Lisa na kumtazama kwa macho mazito na ya upole, “Nataka kumuoa.”

Maneno hayo mawili mazito yalimshtua sana Lisa, akageuka nyuma na kumtazama kwa kutokuamini. Ni kweli angemuoa? Ina maana kila alichosema Chester kilikuwa cha kweli? “Haiwezekani!

Joel alipiga meza kwa mshtuko. "Ikiwa unataka kumuoa, kwanini uliingia kwenye uhusiano na Melanie? Kila mtu sasa anajua kwamba Melanie ni mpenzi wako, halafu waje wasikie tena unataka kufunga ndoa na Lisa. Je, umewahi kufikiria jinsi ambavyo watu watakavyomchukulia?”

"Hapo awali, tulikuwa na kutoelewana huko Dar es Salaa ..."

"Sijali." Joel alipunga mkono, “Unapompenda mtu, unapaswa kumheshimu na kumlinda, badala ya kumuumiza…”

Alvin alitoa msisimko kidogo.” “Mjomba Joel, ulikuwa ukimuachilia pia Aunty Sheryl. Muda mfupi tu baada ya kupata ujauzito, ulioa mwanamke mwingine, hata wewe pia ulishindwa katika mahusiano.”

Uso wa Joel ulibadilika rangi. "Ndio. Ndiyo maana ninataka kumlinda Lisa…”

"Alvin alichukua kikombe tupu cha kahawa kutoka mezani, "Ulikuwa wapi Lisa alipofukuzwa nyumbani na Nina na Melanie? Ikiwa ungemlinda jana usiku, angeumizwa na mke wako na binti yako?"

Hapo Joel alipauka sana, Lisa alitazama chini kimya, hakika Joel hakuwahi kumlinda. Hakuwa na ujasiri wa kwenda kinyume na familia ya Mahewa, ambayo pia inaeleza kwa nini alimkosea mama yake, Sheryl enzi hizo.

Macho ya Alvin yalikuwa makali, “Mimi ni tofauti na wewe. Namtaka Lisa, hata nikishindwa kuwa mwenyekiti wa KIM International na kila mtu wa familia ya Kimaro akinipinga, bado nitamuoa.” Alitamka kila neno kwa nguvu sana hadi Joel akashikwa na butwaa, na Lisa pia.

Alvin alimnyanyua Lisa taratibu kwa miguu yake na kusema mbele ya Joel. “Kwa baraka zako tu tunaweza kujumuika kihalali, zaidi ya hapo anaweza kurudi nyumbani kwa Ngosha kihalali baada ya mimi kumuoa, kwa njia hiyo hakuna atakayemdharau tena. Hutaki kuona hilo, mjomba Joel?”

Sentensi ya mwisho ilimwingia Joel. Mwishowe, Lisa alivutwa kwa namna fulani hadi ndani ya gari na Alvin. Lisa alichanganyikiwa. Ilimaanisha kwamba familia ya Kimaro ilimpokonya cheo chake cha mwenyekiti kwa sababu tu alitaka kumuoa?

“Acha kunitazama hivyo.” Alvin alisimamisha gari kwenye njia panda kisha akageuka na kumbusu mdomoni “Twende tukachague pete yako ya ndoa.”

"Sijakubali!" Lisa alikasirika. Kwa kuzingatia tabia yake ya kutisha, alikataa kufungwa naye milele.

"Lisa, nimepoteza kila kitu kwa ajili yako, lakini unakataa kuolewa na mimi?” Macho meusi ya Alvin yalikuwa yamemkazia kana kwamba ni msaliti.

Pembe za mdomo wa Lisa zilimsisimka.“Hata usipokuwa mwenyekiti wa KIM International, bado una mali zisizohesabika kwa jina lako. Naamini wanawake wengi watamiminika. kwako…”

“Sawa. Unaweza kuendelea kuwa mchepuko basi.” Alvin aliinua uso wake. “Nitamuooa Melanie, lakini sitakuacha. Ninyi dada wawili mnaweza kufurahia kuwa nami pamoja wakati huo."

“Alvin, unanichukiza sana!” Kidokezo cha hasira kilitanda machoni pa Lisa.

“Unataka kuwa mchepuko au mke halali? chagua moja.” Alvin alifunga midomo yake myembamba.

Tabia yake ilikuwa mbaya kama kawaida. Lisa ghafla alihisi kubanwa kusikoelezeka kwenye kifua chake. Angeamua kuolewa naye, lakini alikerwa na jinsi alivyomuuliza. Nani asingependa kuolewa? Tena kuolewa kimahaba? Nani angetamani kuwa mchepuko milele? Hasa inapohusisha Melanie kumtawala na kumdharau? La hasha! Kwa ajili ya Sheryl, asingewaruhusu Nina na Melanie wamdharau.

“Sawa, nimekubali.” Kwa hayo aligeuza kichwa chake na kuchungulia dirishani, akalichukulia kuwa ni dili lingine. Hapo mwanzo alikubali kuolewa naye kwa ajili ya kulipiza kisasi kwa Ethan, safari hii alimuoa kwa nia ya kumshinda Nina na Melanie.

Midomo ya Alvin ilijikunja kwa tabasamu kubwa. Akawasha gari lake na punde wakafika kwenye duka la vito. Kauli mbiu iliyokuwa kwenye ubao wa kuingilia dukani hapo iliandikwa, 'The Only Love In Life.’

Hah! ‘Mpenzi Pekee Maishani?’ Ilionekana kuwa ikimdhihaki Alvin na yeye.

Alvin alifungua mlango wa abiria na kumnyooshea mkono, Lisa alidondosha macho yake na kumshika mkono, kwa pamoja wakaingia kwenye duka la vito. Hakujali jinsi sura yake ilivyomletea aibu, kwanini alihangaika na jambo hilo.

“Karibu Bwana Kimaro." Meneja wa kike pale mlangoni alipomuona Alvin akiingia na mwanamke mbaya ambaye uso wake ulikuwa umefungwa bandeji, alishtuka sana hadi akashikwa na kigugumizi kidogo. Mbali na
yule meneja wa kike, sura ya ajabu ikawaka kwenye nyuso za wauzaji pale ndani.
Pia waligundua kitambo kuwa Alvin alikuwa kaingia kwenye mahusiano na Melanie, lakini hakuwahi kumpeleka Melanie kwenye duka la vito vya thamani, na vito vya bei ghali.

Alvin akajibu kwa sauti kubwa yenye nguvu na kujiamini ya kiume, “mchumba wangu yupo hapa kuchagua pete ya harusi, tuleteeni pete za kisasa zaidi, za gharama zaidi na za kuvutia zaidi.”

“Mchumba?” Meneja wa kike alipigwa na bumbuazi. “Bwana Kimaro una ladha ya ajabu!”

“Nini kibaya kwa mchumba wangu?” Alvin alijibu kwa sauti nzito, macho yake yakimeta kwa uhasama.

Sura ya:195

Bibi-mdogo ana umbile la mfano na nywele nene. Mrembo, mrembo afu mrembo tena, anakufaa vizuri.” Kwa mfululizo wa pongezi za meneja huyo wa kike, Lisa alishindwa cha kusema, meneja huyo alidhihirisha ukweli katika tasnia ya uuzaji. Alisifia sura ya Lisa iliyoharibika vibaya na hata nywele zake zilizokuwa hazifai.

Muda mfupi baadaye, vito vya mapambo viliwekwa mbele yao. Mng’aro wa vito uliufanya moyo wa Lisa kwenda mputomputo.

“Umeipenda ipi? Unaweza kuchagua chochote, hata ukitaka tupeleke vito vyote nyumbani, ni sawa tu.” Alvin alisema huku akikumbatia kichwa cha Lisa, akithibitisha nguvu ya utajiri wa mapenzi aliokuwa nao.

Lisa aliamua kuchagua pete ya almasi iliyopendwa zaidi na wadada, lakini kwa sababu ilikuwa ni nyepesi sana, Alvin alimchagulia pete nzito zaidi ya almasi yenye rangi ya waridi badala yake. Baada ya kuiingiza kwenye kidole chake chembamba, kweli alijihisi kama mwanamke mpya na mwenye furaha zaidi duniani.

Meneja wa kike alitabasamu na kusema, "Una ladha nzuri, Bwana Kimaro. Pete hii ya almasi ina uzito wa gramu 13.14."

Lisa bila fahamu aliikataa, “Hii pete ni nzito sana…”

“Ivae na usifikirie kuivua milele” Alvin aliamuru. Alikuwa na ladha nzuri, na alipenda sana rangi ya waridi. Kama jambo hilo lingetukia huko Dar es Salaam, angalifurahi sana.

Alvin akamwambia Lisa, “nichagulie pete ya kiume pia.”

Kwa kuwa alipenda vitu vikubwa, Lisa kimakusudi. akamchagulia pete ya wanaume iliyofunikwa kwa almasi. Pete hiyo inaweza kuonekana kuwa ya kitambo sana, lakini ilionekana kana kwamba ilitoka kwenye kampuni ya mitindo ya kimataifa na mara moja ilipowekwa kwenye kidole chake, ilionekana kustaajabisha bila kujali pembe zake.

Lisa alipigwa na butwaa kumuona Alvin amechanganyikiwa. “Chaguo bora lililoje?” Alvin alipapasa nywele zake kwa kuridhika. Lisa akajshindwa cha kujibu, “Mimi...” Alikuwa kajawa na furaha kupita kiasi.

Wawili hao walipotoka nje ya duka la vito vya thamani, kamera za waandishi ziliangaza. Kulikuwa na waandishi wa habari wakiwapiga picha mfululizo.

Lisa alipotaka kumkumbusha kuhusu jambo hilo kuenea na kuzua taharuki nyingine, Alvin hakumjali. Aliweka tu mkono wake kiunoni mwake na kumuuliza, “unaogopa chochote?”

“Hapana! Umenitesa sana hivi kwamba chochote kitakachotokea si lolote kwangu,” Lisa alidhihaki, “Vipi kuhusu wewe? Kila mtu anafahamu kwamba Melanie ni mpenzi wako.”

“Sidhani kama nimewahi kutangaza hadharani kuwa Melanie ni mpenzi wangu,” Alvin alijibu huku uso wake mzuri ukiwa umetulia.

Lisa alishangazwa sana na Alvin. Familia ya Ngosha na familia ya Kimaro walishafanya hafla kadhaa za chakula, na Alvin na Melanie walikuwa wamehudhuria hafla za aina tofauti wakiwa wawili. Hiyo yote ilikuwa ni sawa na kumtambulisha Melanie kuwa ni mpenzi wake. Ghafla, alihisi huruma kidogo kwa Melanie. Alvin aikuwa ni mbabe sana asiyejali moyo wa mwanamke hata kidogo.

Habari kwamba Alvin alimnunulia Lisa pete ya almasi siku hiyo ilienea kama moto wa nyikani kote Nairobi. Siku iliyofuata, Alvin, aliingia kwenye kilele cha habari zilizovuma kwa mara nyingine tena.

#Ushahidi Usiopingika Wa Alvin Kimaro Kumsaliti Mpenzi Wake Kwa Mwanamke Mwingine! Alvin Kimaro adhihirisha Kiburi chake Hadharani Kwa Kumnunulia Mchepuko wake Pete ya Alamasi!

#Alvin Kimaro atumia mamilioni Kununua Pete Ya Kwa ajili ya Mchepuko Wake. Hii ina Maanisha Kuwa Hana Mpango Tena na Mpenzi Wake wa Kwanza?

#Alvin Kimaro na mwanadada aliyempindua mwenzake kutoka familia ya Ngosha wanaonyesha mapenzi hadharani]

[Kwa mujibu wa mtu wa ndani, Bi Ngosha Alimfumania Alvin na mwanamke huyu wakiwa wamejificha chumbani wakati wa karamu usiku ule.]

#Bi Ngosha anatia huruma sana. Nilisikia alikwenda kumtafuta yule mwanamke mwingine akiwa na rafiki zake, lakini aliishia kutuptwa kituo cha polisi baada ya Alvin Kimaro kuvuta kamba. Bado hajaachiliwa hadi sasa.]
Hakika, Alvin Kimaro ndiye mwanamume mchafu zaidi Nairobi. Anachukiza.]

#Hatimaye naweza kuona ni kwa nini alifukuzwa kutoka wadhifa wa mwenyekiti katika KIM International.]

Katika siku moja tu, Alvin alikuwa adui wa umma katika Nairobi yote.
Lisa hata aligundua kwamba watumiaji wengi wa mtandao walikuwa wakisusia bidhaa za makampuni ambayo Alvin alikuwa amewekeza.
Mwanamume ambaye alikuwa ni milionea nchini Kenya sasa akawa msemwa hovyo mitandaoni nchini Kenya.

Lisa ghafla akajisikiaviabaya sana. Hata akajuta kwanini alichagua kumkubalia jana yake. Alimtupia macho magumu Alvin aliyekuwa anasoma gazeti pembeni yake. Alikuwa amevalia mavazi ya kulalia bado na kwa mwonekano wa mambo siku hiyo hakuwa na mpango wa kwenda kazini. Kiukweli swala hili lisingetokea endapo angekubali kuoana na Melanie na kuachana na Lisa.

Bado Lisa aliona ni ngumu kuamini kuwa Alvin angekata tamaa juu ya utajiri na upendeleo wa familia yake kwa ajili yake. Pia moyoni alihisi badoAlvin hakuwa na mapenzi naye ila alifanya hivyo kwa ajili tu ya kumkomoa Kelvin.

“Mbona asubuhi na mapema unanitazama kwa mvuto?” Alvin aliinua kichwa chake kutoka kwenye gazeti, na midomo yake ikakunja tabasamu.

Lisa alikodoa macho. Je, alikuwa amemtazama kwa muda mrefu? Yeye hakuwa na ufahamu wa hilo.

“Tafadhali. Nilikuwa nikifikiria tu jambo fulani.” Lisa alitazama pembeni kwa aibu.

Alvin alifunga lile gazeti kabla hajainuka na kumfuata nyuma. Akaminya mikono yake kwenye kiti. “Ulikuwa unafikiria nini?”

"Haikuhusu." Lisa alichezea glasi ya maziwa mikononi mwake.

“Hujui kuwa kila kitukinachokuhusu wewe pia kinachohusiana na mimi?” Alvin akainama na kuuegemeza uso wake mzuri kuelekea kwake.

Lisa karibu alegeze nguvu zake kwenye glasi ya maziwa. Mwanaume huyu kwa kweli alikuwa katika hali ya kumdhihaki au? Kweli alikuwa tayari kupoteza kila kitu kwa ajili yake? Hakuamini hata kidogo. Je, alikuwa kichaa?

Lisa aliuma meno kwa nguvu na kusema moja kwa moja, “Alvin, sijui nia yako ni nini kwangu, nina wasiwasi sana, sina hata amani. Naomba uniache tu. Bado unaweza kuokoa kila kitu.”

"Unamaanisha nini kwa kusema naweza kuokoa kila kitu? Sifa? Hali?" Alvin aliuliza huku akitabasamu hafifu.

“Hujui?”

"Ninajua, lakini wewe ndiye haujui." Alvin alifuta maziwa yaliyokuwa pembeni ya mdomo wake kwa kidole chake. "Lisa, huelewi kuwa kila kitu kinafaa kujitolea kwa ajili yako?"

Kila kitu kinafaa kujitolea kwa ajili yake? Sentensi hiyo rahisi ilibomoa ukuta ambao Lisa alitumia muda mrefu kuujenga ili kujikinga naye. Ghafla, moyo wake ulianza kwenda mbio. Hakuelewa!

Alikuwa ameacha kumpenda kwa muda mrefu, sivyo? Hakuhisi chochote ila chuki kwake. Alitamani kuwa angekuwa amekufa. Alitamani kwamba angeweza kukaa mbali naye iwezekanavyo. Kwake, alikuwa shetani wa kutisha. Hata hivyo, kwa nini aliguswa naye, kwanini alikuwa radhi kupoteza kila kitu kwa sababu yake?

“Ha. Usiniambie kuwa unanipenda.” Akiwa amezuia hasira yake, akajikaza kwenye kioo na kutabasamu. “Unaonyesha upendo wako kwangu kwa nguvu. Uliniumiza mwili, ukanitisha, na kunilazimisha nikusikilize. Haya ni mapenzi kweli unayotakiwa kuishi nayo kwangu?"

“Nimeshakuambia sitafanya hivyo tena. Nilofanya vilekwa sababu ya hasira tu. Ningewezaje kukuona na Kelvin?” Alvin alisema kwa kujiona kuwa hana hatia. “Samahani kwa kukuumiza mapema. Sitafanya hivyo tena, na bila shaka nitakusaidia.”

“Utakuwa umenisaidia sana ikiwa utaniacha tu.” Lisa hakutaka amtanie tena. Alikuwa na wasiwasi kwamba angesahau chuki yake kwake na maumivu ambayo alikuwa amemsababishia.

Macho ya Alvin yalitiwa giza. “Unatamani kuwa na Kelvin tena, sivyo?”

“Hapana…” Kwa kuhofia kwamba Alvin angemuumiza tena Kelvin, Lisa alijibu mara moja, “Niliamua kukubali anioe kwa sababu tu nina deni lake..”

Alvin alishtuka sana hadi akamshika bega kwa nguvu. Lisa aligeuza kichwa na kumwangalia, lakini akapata hofu kubwa machoni pake, kama vile ilipotokea siku ile alipompiga sana, ilikuwa ni dalili ileile tena. Aliogopa sana. Angewezaje kuishi naye milele mtu mwenye hasira za ghafla namna hii?

"Hivyo ndivyo ulivyomaanisha kwa kutoniumiza tena." Kwa maumivu, Lisa alitokwa na jasho baridi.

TUKUTANE KURASA 195-200

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI.............. LISA
KURASA..........196-200

Sura ya:196

Alvin alishikwa na butwaa. Alimuachia Lisa na kupiga hatua mbili nyuma. Mikono yake ilikuwa ikitetemeka, na haikuonekana kama ilikuwa karibu kuacha.

Lisa alitazama nyuma na kumtazama kwa woga. “Alvin, unaweza kuwa hujui, lakini siku zote lazima niwe makini ninapokuwa na wewe. Wewe ni mtu wa kiburi, wa kutisha, na mwenye hasira sana. Nina wasiwasi kila wakati kwamba nitaishia kuwamhanga wa hasira zako. Kwangu mimi, wewe ni shetani. Umeona mtu yeyote akiangukia kwa shetani?!”

“Inatosha. Acha!" Kwa macho yenye damu, Alvin alifagia kifungua kinywa chote kilichokuwa mezani hadi sakafuni. Hakuwa na nia ya kumuumiza, lakini kwa nini ilimbidi kumchokoza hivi? Kama binadamu, moyo wake ungeumia pia.

Alipokaribia kushindwa kujizuia, alifungua mlango kwa nguvu na kuondoka. Harakaharaka akaingia ndani ya gari na kuchukua dawa kwenye chupa mara moja. Hata hivyo, hiyo haikutosha kwake. Kwa kuhofu kwamba hasira zake zisingeweza kushuka haraka, alichukua wembe na kujikata mkono. Maumivu yaliyompata yalipunguza hasira zake kwa kiwango fulani.

Katika chumba cha chakula. Lisa alitazama kwa huruma pale sakafuni, na ushanga wa jasho ukamtiririka kwenye paji la uso wake.
Macho ya Alvin yalikuwa ya kutisha sana. Alihisi kana kwamba alikuwa ameonana na shetani mwenyewe.

Kwanini Alvin alikuwa na hasira hivyo? Alikuwa akitaniana naye kwa upole dakika moja, na iliyofuata aligeuka kuwa mbogo. Kwanini hakutambua upande wa kutisha wa Alvin hadi wakati huo?
Hapana, ilimbidi aondoke. Asingeweza kuolewa naye tena kwa uhakika!

Lisa alipogeuka, ghafla alimuona Aunty Yasmini akiwa amesimama kwenye mlango wa jikoni, akitazama tukio hilo kwa wasiwasi.
Alitaka kumfumbia macho lakini ilibidi amwambie ghafla, "Bi Jones, tafadhali usimkasirishe Alvin zaidi."

“Najua. Sitathubutu kufanya tena.” Lisa alilazimisha tabasamu la kujidharau kwenye uso wake uliopauka.

Shangazi Yasmini aliogopa sana. Alitaka kumweleza kwamba Alvin alikuwa na ugonjwa, ugonjwa mbaya sana wa kupoteza udhibiti wa hasira zake. Hata hivyo, kama angemwambia ukweli, Lisa si angemwogopa moja kwa moja Alvin?

•••
Hospitalini. Akiwa anaufunga mkono wa Alvin, Chester aliutazama uso wake uliopauka na mzuri na kusema. "Ni Lisa ndiyo kakusababishia hali hii?"

"Sikutaka kuzidiwa na hasira na kumuumiza tena." Alvin alitazama nje ya dirisha. Alipokumbuka maneno ya kuumiza ambayo Lisa aliyasema, alianza kuchemka kwa hasira tena. Kwa nini mwanamke huyo alidai kuwa hana hisia naye tena baada ya kmnunulia pete ya uchumba na kuonesha nia ya kumuoa?

“Haya, inatosha. Tulia. Nimefunga mkono wako sasa hivi, na damu inavuja tena.” Chester alilazimika kuufungua tena mkono wake.

"Unaweza kuniongezea kipimo cha dawa?" Sura ya kero ikamtoka Alvin.

"Itaharibu tumbo lako zaidi," Chester alijibu kwa mshtuko. "Hata hivyo, ni muda gani haujapata mlo mzuri?"

Alvin aliinua midomo yake na kusema kwa huzuni, "Sitaki kulazwa tena katika hospitali ya magonjwa ya akili."

Akiwa amepigwa na butwaa, Chester akajibu kwa huruma, “Au… unaweza kumjulisha Lisa kuhusu ugonjwa wako na kwamba hukukusudia kumuumiza…”

“Ushauri gani huo, si itamfanya aniogope zaidi?” Kana kwamba Alvin alikasirishwa, aliongeza kwa uchungu, “Umesahau jinsi kila mtu alinichukulia kama mgonjwa wa akili niliposhindwa kujizuia zamani? Wote walitamani nifungwe, na yeye lazima atakuwa hivyo. Hakuna mtu atakayenipenda na ugonjwa wangu.” Kumsikiliza Alvin, Chester alihisi kukosa raha.

Mara baada ya bandeji kufungwa, mlango ukapigwa kwa nguvu. Rodney aliingia ndani. Alipoona majeraha ya Alvin mkononi mwake, alisema kwa uchungu, “Uko sawa, Alvin? Kuishia katika hali hii yote kwa ajili ya mwanamke?”

"Hili ni jambo langu la kibinafsi," Alvin alisema bila kujali.

“Nakuchukulia kama kaka yangu,” Rodney alisema kwa kuudhika. “Angalia Jack amefanya nini. Yeye ndiye aliyeongeza mafuta kwenye moto kwenye Mtandao na kusababisha kila mtu kukuchukia. Hata zile familia zenye ushawishi zilizokuwa zikikustaajabisha na kukuheshimu zinakukwepa kana kwamba wewe ni ukoma. Uko sawa kwa kila mtu kumpendelea Jack sasa?"

Chester alicheka. “Rodney, una hasira kupita kiasi. Unaona Alvin anaonekana kama mtu anayeshindwa kwa urahisi?”

“Lakini…”

“Si rahisi kwa Jack kuchukua kiti cha mwenyekiti wa KIM International.” Chester akahamishia macho yake kwa Alvin.

Alvin alitabasamu. “Wewe ndiye unanifahamu zaidi.”

Rodney akawa mnyonge. “Sawa. Mimi ni mtu mwenye shughuli nyingi. Ulinipiga hata kwenye boti juzijuzi.”

“Uliyataka mwenyewe…” Alvin alijibu bila kujali.

Rodney alishindwa cha kusema. Alikuwa amekasirika sana.

“Sawa. Tujaribu kusahau kuhusu mambo yasiyofurahisha. Rodney alisafiri kwa ndege hapa kutoka Dar es Salaam alipopata habari kwamba jambo baya limekutokea. Tukutane usiku wa leo.”Chester alisema.

Alvin alibaki na uso usio na wasiwasi. “Kuna faida gani ya yeye kuja hapa, kwani atanisaidia nini?”

"Kunywa na wewe." Chester alionyesha tabasamu la meno ya lulu. "Kunywa kunaweza kusaidia kupotezea huzuni za mtu."

•••

Nyumbani kwa familia ya Ngosha. Wakati Nina alipogundua kuwa Alvin alikuwa amemnunulia Lisa kipande cha vito chenye thamani ya shilingi milioni 15 za kenya, ambazo ni sawa na milionizaidi ya mia tatu za Kitanzania, alikasirika sana hadi akavunja mitungi ya maua sebuleni.

“Kuna kitu kibaya sana kwa Alvin. Melanie alimtendea vizuri sana, hata hivyo alichagua kuoa binti asiye halali. Ahhhh. Lisa, unastahili kufa kama mama yako.” Nina alilalamika.

“Inatosha. Maneno yako ni makali sana." Joel hakuweza tena kuvumilia tabia yake.

“Joel, wewe ni takataka zisizo na maana,” Nina alimkosoa huku akionyesha pua yake. “Kuna mtu alimpokonya mpenzi wa binti yako na kumdhulumu, lakini huwezi kufanya lolote kumsaidia. Sasa Melanie na Farres wamefungiwa katika kituo cha polisi, huwezi hata kuwapa dhamana. Wewe ni mwanaume wa aina gani?”

"Angalia mdomo wako, Nina." Joel alikuwa akihema kwa hasira. Ilimjaa chuki kumtazama Nina ambaye alionekana kama mwanamke kichaa wakati huo.

“Nimekosea kusema hivyo? Wewe ni dhaifu, na ndiyo sababu Melanie alidanganywa. Ikiwa hutamuokoa, basi nitatafuta njia ya kutokea.”

Kwa hayo Nina aliendesha gari hadi nyumbani kwa akina Kimaro. Mzee Kimaro aliionea huruma familia ya akina Ngosha, akajaribu kufikiria namna ya kuwaweka dhamana Melanie na Farres kutoka kituo cha polisi.

Siku ambayo Melanie aliachiliwa, alimkumbatia Nina na kulia kwa uchungu. “Mama, Alvin amekwenda mbali sana. Hajawahi kuninunulia hata bangili tu, lakini alitumia pesa nyingi kumnunulia Lisa pete ya uchumba. Nataka kumuua Lisa.”

Nina akasaga meno. “Bila shaka, nitampeleka kuzimu kukutana na Sheryl. Hata hivyo, cha muhimu zaidi kwa sasa ni kukupa kilicho bora zaidi…”

“Mama, napenda tu kuwa na Alvin milele,” Melanie alijibu huku akiwa analia.

“Nyamaza,” Nina alisema kwa hasira. “Mbona bado unamfikiria ingawa alikudhalilisha? Fikiri vizuri. Lakini sitamwacha awe na amani na ndoa yake kwani alitudhalilisha sana safari hii.”

“Mama una mpango gani? Ndiye mrithi wa familia ya Kimaro. Hatuwezi kumudu kumkasirisha…”

Nina alisema kwa upole, “Unafikiria kupita kiasi. Alvin Kimaro hana ushawishi tena kama alivyokuwa hapo awali. Hivi karibuni, atasusiwa na familia zote za kifahari jijini Nairobi, na mustakabali wake utakuwa hatarini.”

Melanie alipigwa na butwaa. “Mama sijui unasema nini. Kwanini familia za watu mashuhuri zinamsusia…?”

“Utajua juu yake muda si mrefu. Familia ya Kimaro inakuonea huruma, kwa hiyo wao binafsi wameahidi kukupangia ndoa. Ni Jerome Campos kutoka familia ya Campos.”

Farres alishangaa na kufurahi. "Jack ndiye mwenyekiti wa KIM International. Zaidi ya hayo, Jerome ni binamu wa Jack na pia mpwa wa Lea, kwa hivyo atakuwa na wakati ujao mzuri. Zaidi ya hayo, hali ya familia ya Campos inalinganishwa na hadhi ya familia ya Ngosha.”

Sura ya:197

“Ni nzuri sana. Jerome ni mtu mwenye heshima hata hivyo.” Nina alimtazama Melanie aliyekuwa ameduwaa. “Achana tu Alvin. Alikufedhehesha mbele ya kila mtu, lakini alijuta baadaye?"

Melanie alirudi kwenye fahamu zake ghafla. Hakika Alvin alikuwa akimdanganya. Hata alimwacha ateseke katika kituo cha polisi. Alimpenda sana, lakini aliishia kuwa kicheko! Ahi! Bila shaka angemfanya ajute na kuomba msamaha! Pia angemuweka Lisa kuzimu!

Mara baada ya Melanie kutoka nje ya kituo cha polisi, kundi la waandishi wa habari lilikuwa tayari likimsubiri nje kumhoji. Wakati huo, alionekana kama mtu mwingine. Machozi yalikuwa yakimlenga lenga usoni mwake.

Waandishi walimkimbilia na kumuuliza, “Bi Jones, kuna tetesi kwamba ulimshika Bwana Alvin Kimaro na yule mchepuko wake wakiwa wamelala pamoja usiku wa tamasha la hisani la KIM International. Je, hii ni kweli?”

“Achana na hizo habari.” Tabasamu la kusikitisha likapita usoni mwa Melanie. “Sitaki kuzungumzia alichokifanya Bwana Kimaro kwa sababu nimempenda kwa muda mrefu sana. Nilifurahi sana hatimaye nilipopata kuwa naye. Ninachoweza kusema ni kwamba niliangukia kwa mtu mbaya, lakini simlaumu. Namtakia maisha marefu yenye furaha.”

“Wewe ni mkarimu kweli Bi Ngosha. Bwana Alvin Kimaro hastahili kuwa na wewe. Je umepanga kumlipiza kisasi?” Mwanahabari mmoja wa kike aliuliza.

“Sina uhakika kama nitafanya hivyo, lakini nimechoka sana kwa sasa. Ushauri kwa kwa mabinti ni kwamba natumai kila mwanamke atajilinda, haswa mioyo ya wengi ipo hatarini."
•••
Ofisini, Lisa alipotazama mahojiano ya Melanie kupitia simu yake, alikunja uso.

Mahojiano ya Melanie yalikuwa yamepata huruma na upendeleo kutoka kwa wafuatiliaji wote. Wanaume walimsifu kwa kuwa na akili nyingi za kihisia na kujizuia, binti anayeishi kulingana na sifa yake kama mwanamke mchanga kutoka familia ya kifahari. Wanawake walimsifu kwa kuwa msamehevu na mkweli. Walimwona kuwa msichana mwenye huruma, asiye na hatia ambaye Alvin hakustahili kuwa naye na alistahili mtu bora zaidi.

Hata hivyo, Lisa alimini kwa kuzingatia kutokuwa na busara kwa Melanie, ilikuwa nje ya uwezo wake kutoa maneno hayo ya busara. Lazima kulikuwa na mtu aliyempanga kusema hivyo na pia kulikuwa na kitu kilikuwa kinaendelea nyuma ya pazia.

Akiwa katikati ya mawazo hayo, Lisa alishtushwa na simu yake ikiita. Pamela alikuwa amempigia simu ili kumsengenya Melanie. “Si Melanie anampenda Alvin? Kwanini kamgeuka na kuongea maneno hayo ya kumsukuma Alvin kwenye shimo?”

“Una wasiwasi naye?” Lisa aliuliza.

“Hapana! Ninaogopa kwamba ungekuwa na wasiwasi juu yake badala yake.”

"Hapana siwezi." Lisa alikanusha bila kujua. "Kadiri anavyozidi kuwa duni, ndivyo uwezekano wa mimi kutoroka makucha yake kama shetani unavyokuwa mkubwa."

“Sawa. Kweli, cha kushangaza, watu wana hamu ya kujua ni nani mpenzi mpya wa Alvin licha ya ugomvi huo. Cha kushangaza ni kwamba vyombo vya habari havikufichua habari zozote kuhusu wewe na Alvin, tangu mlipokuwa Dar es Salaam. Habari zako zimefichwa makusudi ili kumpa nguvu Melanie kukukosoa vikali zaidi.”

Akiwa ananyoosha midomo yake, Lisa alifahamu hilo pia. Kufikia wakati huo, aliamini kuwa ni Jack Kimaro ambaye alipanga kila kitu nyuma ya tukio hilo. Je, hakutaka kumfunua Lisa kwa sababu alimhurumia, au aliogopa kuingizwa katika jambo hilo?
Hata hivyo, Jack asingemsumbua Lisa kwa lolote. Jack alidharaulika zaidi kuliko Alvin. Alvin alikuwa jeuri dhahiri, lakini Jack alificha ubaya wake vizuri sana. Watu kama yeye walikuwa wepesi zaidi kushughulika nao.

Pamela kisha akasema, “Hata hivyo, Alvin anachukuliwa kuwa mwanamume halisi. Kwa kweli, angeweza kufichua utambulisho wako na kudai kwamba ulimtongoza, basi asingekosolewa vibaya hivyo. Lakini alichagua kunyamaza juu yake…”

Lisa alipandwa na hasira. “Wewe ni rafiki yangu au rafiki wa Alvin?”

“Hehe. Nadhani ukweli kwamba mwanamume hajali kupoteza kampuni, hadhi na sifa yake kwa ajili yako inaonyesha kwamba anakupenda kweli. Nilidhani mtu wa aina hii hayupo tena.” Lisa alikosa la kusema. Wimbi la hisia liliishinda akili iliyolegea ya Lisa.

“Kusema ukweli, sidhani kama Patrick ananipenda hata kidogo nikimlinganisha na Alvin sasa…”

“Lazima nifanye kazi. Kwaheri kwa sasa." Lisa alichukizwa sana na maneno ya Pamela.

Lisa alirudi New Metropolis Park baada ya kufanya kazi kwa muda wa ziada hadi saa mbili usiku. Hata hivyo, Alvin hakuwa amerudi bado.
Baada ya kuoga alijilaza kitandani na kuangalia simu yake. Alibofya bila kufahamu kukutana na habari inayovuma kuhusu Alvin. Wakati huu, video ilikuwa imetolewa. Tukio hilo lilionekana kufahamika. Ilikuwa ni usiku ambao aliburutwa hadi kwenye boti ya Rodney.

Katika video hiyo, Alvin alionekana akiwa amembeba wakati Bwana Mdogo Kelly alipouliza, “Bwana Mkubwa, tumekuchokoza vipi?” Rodney alisema, “Mimi ndiye niliyewaita, Alvin. Njoo tu kwangu ikiwa una shida na hilo."

Alvin alijibu, “Kuhusu tukio la usiku wa leo… Ikiwa mtu yeyote atakuwa na ujasiri wa kutosha kueneza neno moja, picha au video, nitahakikisha kwamba familia yake yote inatoweka Kenya. Pia, wale ambao walimgusa hivi sasa hawaruhusiwi kuondoka hadi uvunje mkono wake mmoja. Kunapaswa kuwa na kamera za uchunguzi kwenye yacht."

Baada ya Alvin kumbeba na kuondoka, mkono wa kila bwana mdogo ulivunjika. Wengine walilia kwa uchungu, huku wengine wakipiga magoti wakiomba msamaha. Eneo la tukio lilikuwa la kusikitisha sana. Video hiyo ilikuwa imetazamwa mara milioni mbili tangu ilipotolewa.

[Mwishowe ninatambua kwamba Alvin Kimaro ni fisadi kuliko hapo awali. Ana kiburi sana. Anastahili kuadhibiwa.]

[Alvin Kimaro haziheshimu hata kidogo familia za kifahari jijini Nairobi. Enyi familia za waheshimiwa, jitokezeni mseme jambo.]

[Ni nani aliyetoa video hii? Alvin Kimaro atahukumiwa maisha, na yote ni kazi yake mwenyewe.]

Kufuatia hayo, familia ya Kelly ilitangaza hadharani. [Tutachunguza suala hilo kuhusu kitendo cha Bwana Kimaro kwa Kijana wa Kelly.]
Familia ya Morice ilisambaza ujumbe huo muda mfupi baadaye. [Tutalichunguza pamoja na familia ya the Kelly]

Baadaye, familia tisa zenye ushawishi kutoka Nairobi zilisambaza ujumbe kama huo. Baada ya Lisa kusoma meseji zote, kichwa kilikuwa kikiunguruma. Kifua chake kilikuwa kimembana sana kiasi cha kuhisi anakosa hewa. Watu wengine wanaweza wasielewe kilichotokea, lakini yeye alikuwa anaelewa.

Hakuweza kusahau tukio lile la kufedhehesha kabisa usiku huo.

Alifikiri kwamba Alvin na Rodney walikuwa wameungana kumfundisha somo usiku huo. Ndiyo maana aliweka kinyongo dhidi ya Alvin tangu wakati huo. Lakini, iliibuka kuwa hakuwa na habari juu yake. Ili kuwafundisha wale vijana waliomgusa somo, hata alivunja mikono yo. Pia aliwataka wafute picha na video hizo usiku huohuo.

Kwa kweli alikuwa akimlinda, lakini hakumwambia ukweli. Alijiuliza Alvin ni mtu wa aina gani? Wakati huo maneno ya Pamela yalimshtua. Kwake, hakujali kupoteza kampuni yake, hadhi, na sifa. Hata alienda kinyume na familia zote tajiri jijini Nairobi kwake.

Kenya nzima tayari ilimdharau Alvin. Sasa familia za kitajiri jijini Nairobi zilipokuwa zikienda kulichunguza suala hilo, Lisa hakuthubutu kuwaza kitakachompata Alvin. Je, angeenda jela? Je, maisha yake yangehukumiwa? Lisa alishindwa kuzuia wasiwasi wake, akapiga namba ya Alvin.

Sura ya:198

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa muda mrefu ambapo Lisa alikuwa akimpigia simu Alvin kwa hiari yake mwenyewe. Baada ya muda mrefu, simu hatimaye iliunganishwa. Hata hivyo, ilikuwa ni sauti ya hasira ya Rodney iliyosikika. “Lisa, wewe ni msumbufu sana. Ulimwacha Alvin katika hali mbaya sana.”

“Yuko wapi?” Moyo wa Lisa ulizama.

"Familia tisa za juu zenye ushawishi zinaangalia suala hili. Alvin amekamatwa kwa uchunguzi,” Rodney alisema huku akitabasamu. “Kama si wewe, Alvin asingeishia katika hali hii!”

“Wewe ni nani hata unikosoe?” Lisa alikanusha kwa hasira. “Kama usingeniteka nyara usiku huo, video hiyo isingekuwepo! Yatch ni yako, kwa hivyo sasa video imetolewa, kama si wewe uliyeitoa ni nani? Una jukumu kubwa pia!"

Rodney alikasirika sana hivi kwamba alipoteza maneno kwa muda. "Wale watu wenye ushawishi wanataka kumwacha Alvin juu ya kuti kavu. Mambo si rahisi kama inavyoonekana.”

Lisa alikata simu moja kwa moja na kutaka kumpigia Hans ili kujua hali ya Alvin ilivyokuwa. Ghafla, mfululizo wa hodi za haraka zikasikika kutoka chini. Alivaa nguo zake na kutoka nje. Mlinzi mkuu wa nyumba ya familia ya Kimaro, Mwamba Kisiki, aliingia akiwa na kundi kubwa la walinzi. "Bi Jones, tafadhali fuatana nasi kwenye makazi ya familia ya Kimaro."

Shangazi Yasmini alisema mara moja, “Bw. Kisiki, huwezi kusubiri Bwana Kimaro arudi…”

“Bwana Alvin Kimaro amepelekwa kwenye idara ya mahakama kwa uchunguzi.” Uso wa mlinzi wa nyumba ulikuwa wa baridi. "Tukio hilo linatokana na yeye, kwa hivyo sina budi kumchukua usiku wa leo."

“Ni sawa, Shangazi Yasmini. nitaondoka naye.” Lisa alishuka ngazi. Kwa muda mrefu alitarajia kwamba familia ya Kimaro ingemtafuta. Ilikuwa ni suala la muda tu.
•••
Saa moja baadaye, katika makazi ya familia ya Kimaro kulikuwa na watu wa kutosha. Ilikuwa ni mara ya pili kwa Lisa kutembelea makazi hayo ya kifahari. Alipoingia ndani, kila mtu wa familia ya Kimaro alikuwepo, na wote walikuwa wakimtazama kwa chuki na hasira.

Mbele ya familia hiyo maarufu, macho ya Lisa yalikuwa ya utulivu na yasiyopendeza. Mambo mengi yalikuwa yametokea tangu alipoingia Nairobi, na alikuwa amepitia maisha mengi magumu hadi wakati huo. Tayari alikuwa hana woga.

“Kinyume na matarajio yangu yote, unaonekana mtulivu sana. Si ajabu umeweza kumroga Alvin. Wewe ni mjanja sana, huh?" Macho ya Mzee Kimaro yalikuwa yakimtazama. Ingawa alikuwa na umri wa miaka 70, aliendelea kuwa na nguvu kama vile kichwa cha familia tajiri zaidi.

Lisa hakusema neno. Alipoona jinsi anavyoonekana mtulivu, Mzee Kimaro alidhani ni jeuri, alikasirika sana akachukua kikombe cha kahawa na kumpiga nacho kichwani. Ghafla mtu akajitokeza ghafla kumkinga kutoka upande, na kikombe kilitua kwa Jack.

"Unafanya nini Jack?" Hasira ilimpanda Lea. "Bado unampenda, huh?"
Jack alimtazama kando Lisa ambaye hakuonekana kuwa mnyenyekevu wala mwenye kiburi kando yake na akatabasamu kwa unyonge. “Bibi, tuzungumze mambo. Ukimdhuru, naogopa Kaka atapandwa na hasira akirudi.”

Bibi Kimaro alidhihaki, “Anaweza kufanya hivyo? Kuachiliwa kwake bado hakuna uhakika.”

“Unamjali Kaka zaidi, Bibi. Hakika utamsaidia.” Jack akatabasamu.

“Msaada?” Bibi Kimaro alimtupia jicho Lisa. “Ameniangusha sana muda huu. Niambie ulitumia mbinu gani kumroga Alvin? Wewe ni mjanja kabisa. Ulipokuja hapa mara ya mwisho, nilikuona ukimkonyezakonyeza. Kwa kweli mmetufanya sisi sote kama wapumbavu.”

"Mama, mwanamke huyu ni mjanja," Valeria alisema kwa dharau. “Anamtongoza Jack akiwa kwenye uhusiano na Alvin. Pia nimesikia tayari ana mchumba. Anatufanya sisi ni wajinga tu.”

“Ndio. Si ulisema una mchumba?” Bibi Kimaro alizidi kuchukizwa naye. “Unawezaje kuwa mchepuko wakati una mchumba? Unatamani sana wanaume? Aibu kwako!"

Macho ya Lisa yalitazama sakafuni. Aliendelea kukaa kimya huku akiwa hajui la kusema. Ingekuwa haina maana kukanusha madai yao hata hivyo. Mlinzi mmoja alimpiga Lisa teke la magoti kwa nguvu, akapiga magoti chini kwa maumivu.

Lea alisema bila kujali, “Sema kitu. Kwa kuwa ulikuwa na ujasiri wa kufanya hivyo, kwa nini usithubutu kueleza?”

“Hasa. Hakuna maana kuwa na aibu sasa,” Queen alisema huku mdomo ukimsisimka. "Alvin yuko kwenye shida sana wakati huu kwa sababu yako."

"Kwa kawaida yeye ni mtu mpole, kwanini aliishia hivi?" Spencer Kimaro alisema kwa mawazo. "Baba na mama wameweka bidii nyingi ndani yake."

Mzee Kimaro alipiga meza. "Huwezi kukaa Kenya tena. Ninakupa chaguzi mbili sasa. Nitakupa tiketi ya ndege kuondoka Dar es Salaam na usirudi tena Kenya. Chaguo jingine ni kwamba unaweza kubaki hapa, lakini nitakupeleka kuzimu.”

Lisa aliinua kichwa chake ghafla na kupigwa na butwaa kwa muda.
Kuondoka Nairobi na kupoteza biashara zake alizoanzisha Kenya? Alifikiria kumkimbia Alvin alipomtesa hapo awali. Hata hivyo, kwa kuwa sasa aligundua kwamba Alvin aliziudhi familia zote za kifahari jijini Nairobi kwa ajili yake, hakufikiri angeweza kuondoka akiwa na dhamiri safi.

"Nataka kujua nini kitatokea kwa Alvin." Lisa aliuliza kwa msisitizo akiwa amekunja ngumi. “Mtamwokoa, au mtamwacha afungwe?”

“Inategemeana na yeye. Akiendelea kuwa mkaidi, nitamkana kuwa mjukuu huyu.” Mzee Kimaro alikoroma. “Hata hivyo, sifa yake imechafuliwa tangu alipovunja mikono ya vijana tisa kutoka kwa familia mashuhuri jijini Nairobi. Sasa kila mtu kutoka tabaka la juu anamsusia, na familia hizo zinaishinikiza familia yetu. Kwa kuzingatia kwamba ameharibu sifa ya familia yetu ya miaka mia moja, atakuwa na bahati ikiwa ataokoka.”

Macho ya Lisa yalimtoka kwa wanafamilia wote wa Kimaro. Aligundua kuwa hakuna hata mmoja wao aliyeonyesha wasiwasi na Alvin, pamoja na mama mzazi wa Alvin, Lea.

Mara Lisa alimuonea huruma kidogo Alvin. Ikiwa haya ndiyo mazingira aliyokulia, haikuwa ajabu alikuwa katili sana na wakati mwingine kukosa huruma.

“Alvin ni mjukuu wako. Je, sifa ya familia ya Kimaro au uhusiano wa kifamilia ni muhimu zaidi?” Alishindwa kuvumilia familia ya Kimaro tena, Lisa aliinuka na kusimama. “Nyinyi nyote ni babu yake wa bibi na mama yake wa damu? Mnawezaje kuishi bila kujali? Mlimpendelea wakati alikuwa na uwezo wa kuleta heshima na faida kwa familia. Lakini kwa kuwa sasa yuko chini kabisa, mnamdharau na kumkatia tamaa, badala ya kumpa mkono wa msaada. Hatimaye hii imenifungua macho kuona familia ya Kimaro ilivyo.”

“Unasemaje?” Akiwa amepandwa na hasira, Mzee Kimaro alinyakua kikombe kingine na kukitupa kichwani kwa Lisa. Wakati huu, hakuna mtu aliyemzuia. Ilimuuma sana Lisa hadi akakaribia kuzimia.

Damu zilianza kumchuruzika, na wakati huo, alionekana kuogopa sana.
Hata hivyo, Lisa alikunja ngumi na kujikaza. Macho yake yalikuwa makali zaidi sasa. “Nimekosea? Ikiwa familia inataka kuwa na ushawishi, je, si kila mtu anapaswa kuungana na kuheshimiana? Familia kama hizi pekee ndizo zinazofika mbali.”

Kila mtu alipigwa na butwaa, ama kutoka kwa uso wake wa kutisha au maneno yake. Muda mfupi baadaye, Lea alisema kwa hasira, “Lisa, mwanzoni tulitaka kukupa nafasi ya kuishi kwa kukuruhusu kuondoka Kenya ukiwa hai. Lakini unaonekana huithamini.”

Lisa akamcheka. “Asante kwa kudhani kwamba ningeithamini. Ngoja niwaambie wote ukweli wangu kwamba sitaondoka.”

Jack alikunja uso, na wonyesho wa wasiwasi ukaangaza machoni pake. “Ondoka tu Lisa. Ukikaa hapa, itakuwa kuzimu hai kwako. Familia ya Kimaro haitakuacha. Watakufungia kwenye jela ya familia badala yake, na inatisha sana huko…”

“Loo, haijalishi. Nimetembelea sehemu ambazo zinatisha zaidi.” Lisa alibaki ameduwaa bila dalili yoyote ya hofu usoni mwake.

Jack alipendezwa na tabia yake hata zaidi, lakini alitumaini kwamba asingechagua kubaki. "Itakuwa bure kukaa hapa. Utapoteza uhuru wako milele."

“Angalau… dhamiri yangu haitanisumbua.” Macho ya Lisa yalikuwa yametulia.

“Una dhamiri?” Valeria alitania.

"Hakuna hata mmoja wenu atakayeelewa uhusiano wa chuki na upendo kati yangu na Alvin," Lisa alijibu bila kujali.

"Basi mpelekeni kwenye jela ya familia na mumfungie." Mzee Kimaro alikoroma huku akipunga mkono. Walinzi walimwondoa Lisa kwa kumsukuma.

Sura ya:199

Kila mtu alimtazama Lisa kwa njia tofauti. Baada ya muda kidogo, Bibi Kimaro alisema, “Sikutarajia msichana huyu mdogo angekuwa mkaidi kiasi hiki.

Queen alipiga kelele. “Usimruhusu akudanganye, Bibi. Ikiwa huniamini, jaribu kumnyima uhuru kwa siku chache bila kumpa maji au chakula. Nina hakika ataomba rehema zako.”

"Nyamaza. Atakufa ikiwa hatakula au kunywa kwa siku kadhaa,” Jack alifoka kwa hasira.

“Mbona unanifokea? Hata hakupendi kwanza,” Queen alijibu kwa hasira.

“Sawa. Hakikisha tu kwamba hatakufa.” Bibi Kimaro alisema, “Alvin karibu aingiwe na wazimu Sarah alipofariki wakati huo. Iwapo lolote litampata Lisa, nina wasiwasi kwamba atakuwa mwendawazimu.” Kila mtu alinyamaza.

Baada ya kila mtu kuendelea na mishe zake, Valeria alimpigia Nina simu mara tu aliporudi chumbani kwake.

Nina alifurahi sana aliposikia habari hizo. Upesi akasema, "Mradi utanisaidia kumtesa Lisa hadi kufa katika jela ya familia, nitakupa Ksh. milioni 50 ili kusaidia kampuni yako kufikia lengo lake."

Valerie alitikiswa kwa muda. KIM International ilikuwa na mali nyingi, na kwa muda huo alikuwa akisimamia masuala yanayohusiana na bima katika kampuni hiyo. Hata hivyo, hakuzingatiwa vyema na familia ya Kimaro kwa sababu utendaji wa kila mwaka wa kampuni haukuwa mzuri. Iwapo angefaulu kulenga shabaha kwa robo hii, Mzee Kimaro bila shaka angemwona kwa mtazamo tofauti. Hata hivyo, katika mawazo ya ugonjwa wa Alvin…Alitetemeka kwa hofu. "Siwezi kumtesa hadi kufa."

"Kwa nini isiwe hivyo? Bado unamuogopa Alvin? Amehukumiwa maisha. Hakuna matumaini kwake.”

“Kwa kweli siwezi,” Valeria akajibu. "Naweza kumfanya chochote isipokuwa kumuua."

Baada ya kufikiria kidogo, Nina alitabasamu kifedhuli na kusema. “Sawa basi. Wakati mwingine, ni huzuni zaidi kwa watu kuishi kuliko kufa. Kwa vile anafurahia kutongoza watu, haribu uso wake ili wanaume wamchukie.”

"Hakuna shida."

Katika chumba cha jela ya familia. Lisa alisukumwa kwa nguvu ndani. Muda mfupi baadaye, taa pekee yenye mwanga hafifu karibu na ngazi ilizimwa. Kwa kweli kulikuwa na giza totoro ndani. Hakukuwa na mtandao wa simu pia. Alitumia tochi kwenye simu yake kutazama huku na kule. Hakukuwa na kitu kingine chochote isipokuwa dirisha dogo lenye vyuma na blanketi nyembamba. Hii ilionekana kuwa sawa ikilinganishwa na kufungiwa katika makazi ya zamani ya familia ya Masawe hapo awali. Alipewa blanketi hapa, angalau.

Alijizuia kutumia simu yake kwa kuhofia kwamba betri ingeisha kabla hajapata msaada wowote na kwa hali hiyo, asingejua wakati. Asubuhi iliyofuata, kuna mtu alimletea bakuli la uji. Kwa kweli alifarijika sana kupewa japo kitu cha kula na uji haukuwa umechakaa. Chakula chake cha mchana pia kilikuwa ugali. Katikati ya chakula chake, ghafla alishtuka kusikia mtu akimjia. Mpaka anaingia mlangoni ndipo alipomwona Jack.

Jack aliutazama ugali mgumu mkononi mwa Lisa kwa macho magumu. “Naweza kumsihi babu akuhurumie. Maadamu unaahidi kutorudi Kenya na kuungana tena na Alvin, unaweza kutoka humu.”

Lisa aligeuza macho yake na kuziba sikio kwa maneno yake. Aliendelea kujikita katika kula ugali wake.

“Lisa, hukusikia nilichosema? Hutaweza kustahimili mambo haya milele. Ni giza na baridi sana hapa. Si mahali pa wanadamu,” Jack alisema kwa wasiwasi. "Mtu aliyekaa hapa mara ya mwisho alipatwa na kichaa baada ya nusu mwezi."

“Kweli? Sidhani kama nitakuwa mwendawazimu.” Lisa alitabasamu kwa unyonge. "Nimekaa katika sehemu ambazo ni mbaya zaidi kuliko hizi. Mahali hapa si pabaya sana. Chakula siyo kichungu na maji pia ni mazuri, na kuna blanketi hapa.”

Jack alipigwa na butwaa. "Unamaanisha nini? Umewahi kula chakula kilicohoza na kunywa maji machafu?" Alikuwa amepitia maisha ya aina gani? Kumwangalia mwanamke mtulivu mbele yake, Jack ghafla aligundua kuwa hawezi kuhisi sawa naye kile alichokuwa akipitia.

"Hakuna haja ya kuuliza maswali kama haya, Jackson." Sura ya dhihaka iliosha uso wa Lisa. "Baada ya yote, niko hapa kwa sababu yako."

Jack aliganda. “Hata kama nisingefanya hivyo, uhusiano wako na Alvin ungefichuliwa tu hatimaye.”

"Kwa hivyo ninapaswa kukushukuru?" Lisa alidhihaki, “Asante basi kwa kuweka dawa za kuchochea nguvu za kiume kwenye kinywaji cha Alvin. Asante kwa kuchukua fursa ya Melanie kwa kumleta katika chumba. Kisha, ukafanikiwa kuanika jambo hilo kwa kila mtu katika familia ya Kimaro na kuharibu sifa ya Alvin. Ulisababisha mzozo kati ya Alvin na wazee wake ili uchukue nafasi ya uenyekiti.”

Jack aliona aibu kwa maneno yake. "Ninakubali kwamba mimi ni mtu wa kudharauliwa, lakini ninataka kukusaidia sasa hivi..."

"Inatosha, Jack. Kwa macho yangu, wewe ni mtu wa kudharauliwa zaidi kuliko Alvin. Lazima nimekuwa kipofu wakati huo. Lakini, kwa kuwa uliniokoa mara ya mwisho, wacha tufanye tumelipishana. Sina deni lako tena.”

“Kwanini hujithamini Lisa?” Jack alianza kushindwa kujizuia. "Haina maana kwako kukaa hapa. Hata Alvin hawezi kustahimili mwenyewe kukaa humu.”

"Mimi ni Mtanzania, lakini pia nina haki za kuishi hapa Kenya. Siwezi kuondoka kwa kulazimishwa. Pia… Ninaamini Alvin ataniokoa. Hataweza kushindwa na watu kama wewe."

Nyakati fulani, Lisa hakuelewa kwa nini alichagua kubaki pia. Kwa mawazo tu ya Alvin ambaye kwa muda huo alikuwa kwenye matatizo, hakuweza kutamani kuondoka. Uhusiano wao ulikuwa mchanganyiko wa upendo na chuki. Hata hivyo, asingeweza kusahau kwamba kila alipokuwa katika hali ngumu, Alvin alikuwepo kila mara ili kumwokoa. Aliamini kwamba angefanya vivyo hivyo wakati huo. Ingekuwaje shetani ashindwe kirahisi hivyo?

"Hapana. Kamwe sitamwachia nafasi ya kubadilisha mambo.” Jack alikasirika. "Kwa kuwa huna shukrani kwa kila kitu nilichofanya, jipambanie mwenyewe, basi." Kwa hayo, Jack aliondoka kwa hasira. Hakuonekana tena tangu wakati huo.

Upesi simu ya Lisa iliishiwa na betri, na hakuweza kutofautisha mchana na usiku. Ghafla, uso wake uliokuwa umeumia ulizidi kuwasha huku kidonda kikichubuka taratibu na kumsababishia maumivu makali. Alihisi kuwa uso wake unaweza kuharibika. Alianza kutisha katika hali ile. Alvin angemuona tena angeingiwa na woga. Lakini ingekuwa ni jambo zuri pia. Katika hali hiyo, asingemlazimisha kumpenda tena.

Hakuwa na uhakika ni siku gani yule bibi aliyemletea uji alikuja tena.
Lisa alitazama bakuli la uji na kuuliza bila huruma, "umekumbuka kuniletea uji tena leo?"

Mikono ya bibi huyo ilitetemeka. Hakujisumbua hata kuongea neno lolote. Alitema tu mate na kuliweka bakuli na moja kwa moja akaondoka.

Lisa alitabasamu kwa uchungu. Hata mtumishi wa familia ya Kimaro alikuwa na kiburi sana mbele yake. Ikiwa alitaka kuishi, hakuwa na la kufanya ila kula chakula, hata ikiwa uso wake ungeoza kabisa!

Sura ya:200

Siku tano baadaye. Alvin alitoka nje ya idara ya mahakama huku mikono yake miwili akiwa ameiweka kwenye mifuko ya suruali yake. Baada ya kufungwa kwa siku chache, sasa alikuwa amedhoofu kidogo, lakini haikuharibu mvuto wake. Kinyume chake uso wake wa kuvutia ukawa maarufu zaidi. Ilimfanya aonekane mwenye kiburi zaidi na mwenye kutisha.

"Lazima zimekuwa siku ngumu kwako, Bwana Kimaro." Hans alimwendea kwa furaha.

Rodney alipiga kifua chake. “Mama*cker. Nilifikiri nisingeweza kunywa na wewe tena.”

“Familia zote jijini Nairobi zinajaribu kunitia hatiani. Wamejitahidi sana, lakini si rahisi kunishinda.” Alvin kisha akatazama huku na kule. Kando na walinzi na marafiki zake, sura ambayo alikuwa akitamani kuiona haikuwepo. “Lisa yuko wapi?” Alikunja uso wake, akijiwazia. Je, mwanamke huyo asiye na huruma alichukua fursa hii kukimbia?

Kila mtu alinyamaza kimya huku Hans akiinamisha kichwa chini.

"Niambie." Sauti ya Alvin ilizidi kuwa ngumu, ikajaa hasira.

Baada ya muda, Chester alikohoa na kusema kinyonge, “Wakimaro walimchukua Lisa siku ile ulipokamatwa kwa uchunguzi.”

Alvin alimvuta Hans kuelekea kwake kwa hasira. “Si nilikuomba utafute mtu wa kumwangalia? Na angalia jinsi ilivyotokea. Shani yuko wapi? Kwanini hakumlinda Lisa?"

"Samahani, Bwana Kimaro." Hans aliuma meno na kusema kwa hatia, “Mwamba Kisiki alikusaliti na kumwangusha Shani na kupoteza fahamu. Kisha, mfanyakazi wa nyumba akamchukua Lisa.”

“Mwamba Kisiki?” Alvin alikodoa macho. Hakutarajia hili.

“Ndiyo.”

“Imekuwa siku ngapi?” Alvin aliuliza.

“Siku tano,” Hans alijibu kwa tahadhari. “Lakini nimeomba mtu afuatilie mienendo ya makazi ya familia ya Kimaro. Inaonekana Bi Jones hajapelekwa kwingine.”

"Ikiwa hajapelekwa kwingine, nina uhakika amefungiwa kwenye chumba cha jela ya familia." Alvin alimvuta Hans kwa hasira. “Na wewe unamwacha tu akiwa amefungwa huko? Kwa nini hukutafuta mtu wa kumwokoa?”

Aliposhindwa kuvumilia tena, Rodney aliingilia kati, “Siku hizi, sote tunajaribu kushughulikia familia ulizozikosea huku tukifikiria njia za kukuokoa. Isitoshe, Hans ni msaidizi wako tu. Hana ubavu wa kuingia kwenye nyumba ya familia ya Kimaro. Unajua jinsi Mzee Kimaro alivyo mkorofi, sivyo?”

Chester aliitikia kwa kichwa na kusema vilevile, “Alvin, kama unapanga kumuokoa Lisa, unahitaji kujipanga kwenda kinyume na Mzee Kimaro.”

"Lazima nimuokoe mwanamke wangu." Alvin alipiga hatua kuelekea kwenye gari lake. Ingawa badala ya kuufungua mlango wa gari, alichukua bunduki kutoka chini ya kiti cha dereva.

Kila mtu alishtuka, lakini Chester alikaza na kumkabili. "Alvin, unapanga kuingia kwenye nyumba ya familia yako na bunduki?"

“Wewe ni kichaa. Mwanamke anastahili haya yote?" Rodney alimwambia Alvin kwa hasira, “Umesusiwa na familia zote za kifahari jijini Nairobi. Ukiikera familia ya Kimaro pia, matokeo yake yatakuwa mabaya sana.”

Sam, ambaye alikuwa kimya muda wote, ghafla alisema, "Niko upande wako, Alvin."

"Sam, usikurupuke ili kujifurahisha, sawa?" Hasira zilianza kumpanda Rodney.

“Rodney, nina uhakika usingesema hivyo ikiwa angekuwa Sarah,” Sam alisema kwa ukali.

Uso wa Rodney uliganda. "Sarah ni tofauti. Alikua nasi, lakini Alvin na Lisa wamefahamiana kwa muda mfupi tu.”

“Nyie si lazima mseme chochote kingine. Sikufanikiwa kumlinda Lisa mara ya mwisho, kwa hiyo sina budi kumuokoa wakati huu.” Alvin aligeuza kichwa chake na kumwamuru Hans, “Wachukue wana ONA wote waelekee kwenye nyumba ya familia ya Kimaro. Nataka eneo hilo lizungukwe.” Kisha akaingia kwenye gari na kuanza kuondoka.

Chester alimtazama Alvin akiondoka huku akiwa na macho magumu. Kisha akatoa simu yake kumpigia msaidizi wake. "Waombe walinzi wa Choka wote waelekee kwa nyumba ya familia ya Kimaro sasa hivi ili kumuunga mkono Alvin."

"Chester, umepandwa wazimu pia?" Rodney alikasirika.

"Rodney, inafaa kutumia silaha zote kumsaidia rafiki yetu." Chester alishtuka. "Sio jambo kubwa kama hutaki kumsaidia."

Rodney alijibu kwa huzuni, “Kwa kuwa unamsaidia, je, mimi ni rafiki yake nisipomsaidia?” Akiwa ameachwa bila chaguo, Rodney alifahamisha watu wake ili kumuunga mkono Alvin mara moja.

Gari la rangi nyeusi lilisafiri hadi kwenye nyumba ya familia ya Kimaro kama upepo. Kisha, ikaegeshwa kwa haraka kwenye lango la jengo kuu. Alvin akaingia ndani. Familia kubwa ya Kimaro ilikuwa ikipata chakula cha mchana kwenye chumba cha kulia chakula.

Mara tu walipoona uwepo wake, hali ya chumba cha kulia ikawa mbaya. Bibi Kimaro alipigwa na butwaa hadi akasimama. “Ni vizuri kujua kwamba umeachiliwa. Tafadhali usifanye mambo ya kipumbavu hivyo tena. Unawezaje kuvunja mikono ya vijana wa familia nzuri kwa ajili ya mwanamke?”

“Lisa yuko wapi?” Alvin alimkatisha huku akimwangalia kwa ukali. “Mlete kwangu.”

“Ebboh!” Mzee Kimaro akiwa amefura kwa hasira, akapiga bakuli mezani ambayo ilitoa sauti kubwa. “Nadhani umepatwa na wazimu. Umefungwa kwa siku kadhaa, lakini hata hukujifunza somo lako. Vipi bado unamtamani huyo mwanamke? Nimejitahidi sana kukulea. Ungewezaje kunifanyia hivi?”

“Umefanya nini kunilea?” Alvin alicheka. “Kabla sijafikisha umri wa miaka minane, ni yaya ndiye aliyenitunza. Kisha nilipokuwa mkubwa, nilipelekwa kwenye hospitali ya magonjwa ya akili. Baada ya kuachiliwa, ulinidharau na kunichukulia kama kichaa. Ilikuwa ni kwa juhudi zangu bila kuchoka kwamba nilivutia umakini wako na ulinipa nafasi. Kuanzia hapo, nilianzisha KIM International na kupata mali yenye thamani ya mamia ya mabilioni ya shilingi. Ni familia ya Kimaro yenye deni langu.”

“Sawa. Sikujua ndivyo unavyoona.” Akiwa amewaka kwa hasira, Mzee Kimaro aliinua mkono wake na kumpiga kofi la uso Alvin. “Kama isingekuwa kwangu, usingepata nafasi ya kuingia KIM International. Huna shukrani kabisa!”

“Inatosha. Acha mabishano.” Bibi Kimaro alimsimamisha Mzee Kimaro. "Hamaanishi alichosema."

“Sitaki kubishana juu ya hili sasa. Mleteni tu Lisa kwangu.” Alvin akaonekana kutojali.

"Hapana." Mzee Kimaro alimkataa Alvin. “Acha kumfikiria huyu mwanamke. Tayari nimempeleka nje ya nchi.”

“Usidanganye. Yeye yuko moja kwa moja kwenye makazi ya familia hii, amefungwa kwenye jela ya familia, sivyo? Nitakwenda kumtafuta.” Alvin alitembea moja kwa moja hadi nyuma ya nyumba.

“Mzuie.” Mzee Kimaro alipunga mkono. Nje ya bluu, walinzi zaidi ya 20 walitokea kwenye sebule kubwa na kumzuia Alvin asipite. Mzee wa makamo ambaye alikuwa amesimama mbele alikuwa Mwamba Kisiki, mlinzi bora zaidi wa ONA. ONA kilikuwa ni kikundi cha siri cha ulinzi cha familia ya Kimaro.

"Umenisaliti, Kisiki." Macho ya Alvin yalikuwa baridi.

“Bwana Kimaro, ONA siku zote imekuwa mali ya familia ya Kimaro, ambao nimekuwa mwaminifu kwao. Kwa hiyo ni nini kinakufanya useme kwamba nilikusaliti?” Kisiki akajibu kwa urahisi.

Mzee Kimaro alikoroma, “Niliweka ONA kando yako tu kwa sababu nilitaka uchukue mambo ya familia. Ulidhani kimakosa kwamba jamaa alichukua upande wako.”

Naona…” Alvin aliitikia kwa mawazo. Ghafla, alichomoa bastola yake na kuifyatua kwenye sehemu zote mbili za magoti ya Mwamba Kisiki na kisha akampiga teke kwa nguvu. Licki alilia huku akianguka chini. Magoti yake yalikuwa yametapakaa damu.

Wanawake wa familia ya Kimaro walipiga kelele kwa mshtuko. Mzee Kimaro naye alilipuka kwa hasira. Bwana ambaye alikuwa ametumia mafunzo ya miaka kumi kupata ujuzi wa ulinzi aliharibiwa.

"Unathubutu vipi kunikoromea katika nyumba ya familia ya Kimaro, b*stard." Alvin aliishika bunduki bila hisia kwenye paji la uso Kisiki. "Kwa kuwa hauko upande wangu, unaweza kuwa takataka isiyo na maana kwa maisha yako yote."

Mwamba Kisiki alionekana kuogopa. Hapo ndipo hatimaye akagundua kuwa alikuwa amemchokoza mtu kichaa. Sasa kwa kuwa magoti yake yalikuwa yameharibiwa, maisha yake yote yalikuwa yamechoka.

“Njoo umkamate.” Mzee Kimaro alipoteza utulivu. "Nitakwenda kumlemaza."

“Hapana, Mzee. Wanachama wa ONA wameyazunguka makazi ya familia. Wanachama wa Chester kutoka kwa familia ya Choka na mabaunsa kutoka familia ya Shangwe wapo nje pia." Mlinzi wa nyumba aliingia ndani ya nyumba akiwa na woga.

Kila mtu katika familia ya Kimaro alishangaa. Lea alimkazia macho Alvin kana kwamba ni mgonjwa wa akili. "Kwa Lisa, umeungana na watu wa nje kutushambulia?"

Bibi Kimaro alisikitika. “Alvin, umeniangusha sana.”

“Unasisitiza kunizuia njia yangu?” Alvin hakuwa na tabia ya kufoka nao kama hivyo.

Mzee Kimaro alikaribia kukohoa damu, lakini hakuweza kufanya lolote kumzuia. Wakati huo, alichoweza kufanya ni kumruhusu kupita.

Alvin aliufungua kwa nguvu mlango wa sebule. Baada ya hapo, akawasha tochi kwenye simu yake na kuteremka. Harufu chafu na ya kutisha ikitoka alipoingia kwenye chumba cha jela ya familia. Alvin akawasha taa pande zote. Akiwa amepofushwa na mwanga huo, mwanamke mmoja aliyejilaza kitandani alifunika macho yake kwa mikono yake bila kujijua.

Ilikuwa ni mzigo kwenye akili yake kujua kwamba alikuwa hai. Hata hivyo, alipomkaribia, alishtuka sana hadi simu yake ikakaribia kuanguka chini. Huyu alikuwa Lisa? Je, alikuwa mwanamke ambaye uzuri wake ulivutia macho yake alipokutana naye kwa mara ya kwanza? Hakuweza kumtambua sasa.

Ilikuwa ni siku tano tu tangu alipomwona mara ya mwisho, na hakuwa chochote ila ngozi na mifupa. Kando na hayo, uso wake… ulikuwa ukioza vibaya sana. Alvin alishusha pumzi kana kwamba anakabwa!


Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..........LISA
KURASA.....201-205

LISA KITABU CHA TANO

Sura ya:201

“Umekuja, Alvin!” Lisa alikuwa gizani kwa muda mrefu na macho yake yaliyokuwa yamezama gizani hatimaye yakaona mwanga. Moyo wake pia ambao ulikuwa umeanza kukata tamaa ukaona mwanga wa matumaini. Alihangaika sana, akafumbua macho kidogo tu. Ingawa mtu aliyewasha tochi alisimama gizani, aliweza kuhisi kuwa ni Alvin kutokana na harufu yake aliyoizoea. Mdomo wake ulijikunja kwa tabasamu tulivu. Alijua Alvin angepata tu njia ya kumwokoa. Alikuwa shetani, na mashetani hawashindwi kirahisi.

Lisa hakuwa na wasiwasi wala hofu tena, lakini alikuwa hana hisia zozote. Alvin alimtazama kwa uchungu machoni mwake. Ingawa alikuwa amesimama mbele yake, alihisi kama yuko mbali zaidi naye. Alikuwa amefika, lakini alikuwa amechelewa. Moyoni mwake alipandwa na hasira, lakini alijitahidi sana kuizuia.

"Nini kimetokea kwenye uso wako?" Alvin alimuuliza kwa masikitiko.

“Uso wangu ulikuwa tayari umejeruhiwa, lakini nahisi kuna mtu kaniwekea dawa kwenye chakula changu, jambo ambalo limezidisha makali ya jeraha langu.” Lisa alijigusa usoni na kuuliza kwa huruma "Ninatisha, huh?"

Macho ya Alvin yalimtoka kwa hasira. Nani alikuwa na roho mbaya kiasi cha kuharibu uso wa msichana yule mdogo asiye na hatia? Kadiri alivyokuwa mtulivu, ndivyo hasira zilivyozidi kuchemka zaidi ndani yake. Alikuwa kama volkano ambayo ilikuwa tayari kulipuka wakati wowote.

“Ngoja nikutoe humu kuzimu kwanza.” Alvin alimbeba Lisa huku mikono yake ikitetemeka kupita kiasi. Lisa alikuwa mwepesi sana mikononi mwake hivi kwamba hakuweza kuhisi uzito wowote. Lisa kwa utii alifunga macho yake. Alvin alitoka nje ya chumba cha jela hiyo ya familia akiwa amemkumbatia juu juu kwenye mikono yake.

Hans, Shani na watu wengine waliwafuata. Walipoitazama kwa makini sura ya Lisa aliyekuwa mikononi mwa Alvin, wote walishangaa kwa huruma. “Bi Jones…”

“Tafuta mtu ambaye amekuwa akimpelekea chakula kila siku.” Alvin alitamka maagizo yake.

Hans akashusha pumzi ndefu na kwenda kutekelezamaagizo hayo. Aunty Kollo, ambaye alikuwa na jukumu la kumpelekea Lisa chakula, haraka akaletwa mbele ya Alvin. Alvin alimtaka Shani amwangalie Lisa, ambaye alishindwa kusimama kwa kujitegemea, ili yeye akadili na hao watu waliomdhuru.

Alvin kisha akamtazama Aunty Kollo kwa hasira. Aunty Kollo aliogopa sana. “Bwana Mkubwa Kimaro, huwezi kunilaumu kwa hili. Kunywa uji kila siku inachukuliwa kuwa anasa kwa mtu aliyefungiwa ndani ya jela…”

“Kata ujinga. Nani alikuagiza kufanya hivyo?” Alvin akachomoa bunduki yake na kuigandamiza kwenye paji la uso wa Aunty Kollo. Macho yake yalikuwa na huzuni. "Moja, mbili..."

"Alikuwa ni Binti wa Tatu." Shangazi Kollo alianguka papo hapo. “Binti wa Tatu alinipa dawa na kuniambia niiweke kwenye uji wake. Aliniambia hatakufa baada ya kula, lakini kidonda kitaongezeka kuharibika zaidi na zaidi hadi abaki mifupa tu...”

Hans alishtuka. Wanawake wa familia ya Kimaro walikuwa na roho mbaya sana, na kwa uficho alimtazama Lisa. Lisa ghafla alitabasamu na kuuliza, “Kwani mimi nimewakosea nini hadi muamue kunifanyaia hivi?”

Shangazi Kollo alimtazama usoni na kutetemeka, hakuthubutu kumtazama tena. Alvin alimpiga teke la kifua Aunty Kollo kisha akapiga hatua kuelekea kwenye ukumbi mkuu.

Hans alipotazama mwonekano wake, alijua kwamba dhoruba kali ilikuwa imeanza. Akauma meno na kupiga magoti mbele ya Lisa. “Bi Jones, nakuomba tafadhali msihi Alvin. Ili kukuokoa leo, ameleta kundi la watu kuzunguka eneo lote la makazi, na imemkasirisha sana Mzee Kimaro. Ikitokea lolote kwa Valeria Kimaro, familia ya Kimaro haitamsamehe kamwe. Na kama familia ya Kimaro itaungana pamoja na familia nyingine zenye ushawishi katika mji mkuu, Alvin atakuwa amekwisha.”

Lisa alipigwa na butwaa kwa sekunde kadhaa. Alvin alikuwa ameleta watu kuzunguka makazi ya familia ya Kimaro ili kumuokoa? Kusema kweli, hakutarajia kama Alvin angeenda kinyume na familia yake kwa ajili yake.

"Kwanini ni muhimu kwangu ikiwa atakwisha?" Lisa alimtazama Hans kwa chuki machoni mwake. “Nilikosea nini? Ninaweza kupuuza ukweli kwamba wengine huniita mchepuko wake na kunitukana kwa kuharibu mapenzi ya dada yangu wa kambo, lakini sasa uso wangu umeharibiwa. Isingekuwa Alvin Kimaro, nisingeishia hivi.”

Shani alisema kwa unyonge, “Ikitokea kitu kwa Valeria, Alvin Kimaro atakuwa amekwisha. Lakini familia ya Kimaro pia haitakuacha wewe salama, pamoja na marafiki na kampuni yako.”

Lisa aliuma meno. Alimchukia Alvin, lakini ilimbidi amhurumie.

Hans alisema kwa haraka, “Bi Jones, unaweza kulipiza kisasi baadaye, lakini sasa si wakati wake. Umezungukwa na maadui. Ni Alvin pekee ndiye aliye upande wako. Yeye na wewe mko kwenye boti moja sasa.”

“Sawa, nitaenda.” Hatimaye Lisa alikubali.

Katika ukumbi uliofungwa, Alvin aliingia kwa nguvu. Lea alipomwona alisema kwa hasira, “Sasa kwa kuwa umemuokoa Lisa Jones, unaweza kupotea? Usiwahi kuonyesha uso wako kwenye familia hii tena. Familia ya Kimaro haina mtoto asiye na shukrani kama wewe. Nitajifanya kuwa hukuzaliwa na mimi kamwe.”

Macho meusi ya Alvin hayakuwa juu yake bali kwa Valeria ambaye alikuwa amejificha kwa nyuma bila kujua. Kwa kuhisi macho yake yalivyokuwa meusi kwahasira, Valerie aligeukia mlango kwa woga.

"Mam’dogo wa tatu, nakuomba upite hapa mbele." Alvin alimnyooshea bunduki mgongoni.

Valerie aliogopa sana hivi kwamba miguu yake ilidhoofika. Haraka akakimbilia kujificha nyuma ya Bibi Mzee.

“Alvin Kimaro, si umetosha?” Bibi Kimaro alikuwa haamini. Maumivu ya moyo yalionekana machoni pake. “Umepandwa wazimu tena? Unawezaje kuthubutu kumnyooshea mam’dogo wako bunduki?”

“Alvin, unaumwa kweli. Mama yangu hakukufanyia chochote.” Queen Kimaro alisema kwa hasira.

"Basi muulizeni alifanya nini." Alvin alitembea kuelekea kwa Valeria. “Ngoja nikuulize. Kwanini ulimwambia Shangazi Kollo atie dawa kwenye uji wa Lisa ambayo imeharibu uso wake?”

Kila mtu alipigwa na butwaa, na Jack alishindwa kuamini. "Hiyo haiwezekani."

Sura ya:202

“Nilimuuliza Shangazi Kollo mimi mwenyewe, na pia nikaona uso wa Lisa. Yeye ni mwanamke wangu. Unajua jinsi sura ilivyo muhimu kwa mwanamke?" Mikono ya Alvin ilikuwa ikitetemeka kutokana na hasira yake. “Amekukosea nini hasa? Una kinyongo gani dhidi yake?”

“Sijui unazungumza nini, mimi sikufanya lolote.” Valeria alijificha nyuma ya Bibi Mzee na kutetemeka.

“Usifikiri sijui. Ni Nina Mahewa na bintiye walikuambia ufanye hivyo, sivyo? Uko karibu nao sana. Walikuahidi faida gani?” Macho ya Alvin yalichomwa na hasira, kana kwamba angeweza kupoteza busara wakati wowote..

Valeria akijua kwamba hawezi kuficha ukweli, aliuma meno yake na kusema. "Sawa, ikiwa ningefanya hivyo? Alvin, mimi ni mam’dogo wako. Je, utaniua kwa sababu ya mtu wa nje?”

“Yeye si mtu wa nje. Yeye ni mwanamke wangu. Sitakuua, lakini nataka umlipe kwa uso wako.” Alvin alitembea kuelekea kwa Valeria hatua kwa hatua.

“Huwezi kufanya hivyo.” Bibi Kimaro alimtetea Valeria na kusema kwa hasira, “Alvin, shangazi yako ni binti yangu. Ukimdhuru, sitakusamehe kamwe.”

Spencer Kimaro naye aliongea. “Alvin, tulia. Teknolojia ya matibabu imeendelea sana sasa. Tunaweza tu kumpeleka Lisa nje ya nchi na kumpa sura mpya.”

Lea naye alikasirika. “Ukithubutu kumdhuru mam’dogo wako, nitavunja uhusiano wetu wa mama na mtoto.”

“Unafikiri kweli kwamba ninajali uhusiano wetu wa mama na mtoto?” Alvin akamsogeza Bibi yake pembeni na kumsukumia Valeria pale mezani. Akachukua kisu cha matunda.

Valerie aliogopa sana hivi kwamba alitetemeka kama jani linalosukumwa na upepo. “Alvin, usifanye hivyo. Nilikosea. Sitathubutu kufanya tena. Nitaomba msamaha kwa Lisa, sawa?"

“Kama kuomba msamaha kutarudisha sura yake, wacha niuchonge uso wako kisha nikuombe msamaha…” Alvin alitabasamu kwa hasira.

Valeria karibu alowe maji. "Wewe chizi. Bibi na Babu yako hawatakusamehe ukifanya hivyo.”

“Vizuri, mam’dogo Valeria. Hakika nitauchonga uso wako vizuri.” Macho ya Alvin yalimtoka kwa mng'ao wa kichaa, akakizungusha kisu usoni mwake.

“Alvin, acha.” Sauti ya Lisa ilisikika kutoka mlangoni na kumfanya Alvin asitishe zoezi lake. Kila mtu alimtazama na kushtuka alipoona sura yake waziwazi.

Mzee Kimaro akaamuru mara moja, “Lisa, umefika kwa wakati. Mzuie kichaa huyo.”

Lisa alikunja uso kwa kuchukia, lakini bado alienda kumshika mkono.

"Ondoka," Alvin aliamuru, hakutaka kuona upande wake wa kikatili.

“Sihitaji ulipize kisasi,” Lisa alisema kwa sauti ya chini. "Mbali na hilo, sio yeye ambaye anataka kuniumiza."

“Ndiyo ndiyo, nilikuwa nimepagawa kwa muda tu.” Valeria alidakia kwa haraka.

"Ninajua. Haijalishi ni nani, nitawalipa mmoja mmoja, nikianza na wewe." Alvin alibaki bila wasiwasi.

“Yeye ni familia yako. Sitaki… sitaki upoteze familia yako kwa sababu yangu. Mimi sina thamani.” Lisa alimkazia macho.

Alvin alishikwa na butwaa. Ingawa sura ya mwanamke huyo iliharibiwa, maneno yake bado yangeweza kugusa moyo wake kama hapo awali.

"Hapana, unastahili." Alisema kwa sauti ya chini.

Lisa alinyamaza kwa muda kabla hajashusha macho yake. “Fikiria bibi yako. Akimwona mjukuu wake akimdhuru bintiye, unafikiri ataweza kuvumilia? Yeye tayari ni mzee sana."

Alvin aliduwaa na kugeuka nyuma kumtazama Bibi Kimaro aliyekuwa akimwangalia kwa macho ya kusihi. Kisu mkononi mwake kikalegea, na Valeria akatoroka haraka kana kwamba ameokolewa.

“Njoo, twende nyumbani.” Lisa alimshika mkono.

‘Nyumbani?’ Sehemu ya maumivu ilitanda kwenye uso mzuri wa Alvin.
Hapo zamani za kale, hiyo ilikuwa nyumba yake, lakini, mahali pekee palipoonekana kama nyumbani kwake sasa ni pale alipokuwa pamoja na Lisa.

“Sawa.” Baada ya muda mrefu, Alvin alitikisa kichwa. Alimshika na kuwaacha akina Kimaro bila kuangalia nyuma.

Valeria alipoona umbo la Alvin lkitoweka, alitetemeka na kusema, “Mama, Baba, nadhani ni lazima Alvin atakuwa mgonjwa tena. Alikuwa anatisha sana sasa hivi. Ilikuwa kama kipindi kile alipokuwa akiwaumiza wengine…”

“Imetosha.” Bibi Kimaro alimpiga kofi usoni kwa kukata tamaa. “Vipi una ujasiri wa kusema hivyo? Hutosheki kwa familia ya Kimaro? Unawezaje kuhongwa na watu wa nje kufanya mambo ya ajabu namna hii?”

Jack kwa hasira alimshutumu pia. "Mam’dogo Valeria, wewe ni mkatili sana."

Kwa aibu, Valeria alikunja ngumi kwa huzuni. Alimchukia sana Alvin mpaka meno yalimuuma. Alipanga kulipiza kisasi naye.
•••

Gari lilipanda kwenye miinuko ya Mlima wa Sherman. Hans aliendesha gari huku Alvin akiendelea kutazama mwili wa Lisa uliochoka. Lisa alijua jinsi uso wake ulivyokuwa wa kutisha na alikasirishwa na kutazamwa kwake. “Si lazima uchukue nilichosema mapema kwa uzito. Sikutaka tu umdhuru Valeria na kugombana na familia ya Kimaro. Ikiwa jambo fulani litatokea kwako, ninaweza kufungwa kwenye jela ya familia yenu tena au sehemu mbaya zaidi.”

“Najua." Alvin alipandwa na hasira, lakini alirudi katika hali yake ya kawaida haraka. Hakuwahi kufikiria kwamba Lisa angemsamehe kirahisi hivyo baada ya tukio hilo lenye kuumiza. Alijihisi hatia kubwa kwamba alikuwa hana maana kabisa kwa Lisa. Alidai kwamba angemlinda, lakini mwishowe, hakuweza kufanya hivyo. Maumivu makali ya moyo yalishika moyo wake. Mkono wake ukatetemeka kwa nguvu tena kana kwamba anakaribia kushindwa kujizuia.

“Simamisha gari.” ALvin alitoa amri ghafla. Hans akasogea mara moja.

“Mpeleke hospitali. Nitaenda kwenye gari la nyuma kwa ajili ya kuvuta sigara.” Alvin alishuka haraka kwenye gari.

Hans alimtazama kabla hajaondoa gari na Lisa akamtazama kwenye kioo cha nyuma na kumwona akiingia kwenye gari la nyuma yao. Kisha akacheka na kusema, “Hans, ninanuka! Ni lazima iwe vigumu kwake kuvumilia.”

Lisa alicheka. Mazingira ya jela yalikuwa ya kuchukiza sana, lakini alikula, kunywa, na kulala katika chumba kila kila siku. Zaidi ya hayo, hakuweza kuoga wala kupiga mswaki. Hata yeye hakuweza kustahimili uvundo uliokuwa umeenea kwenye gari.

Hans alieleza kwa haraka, “Bi Jones, haukuelewa. Bwana Mkubwa Kimaro…” Alisita ghafla baada ya kukosa maneno sahihi. Asingeweza kumwambia kwamba Alvin alikuwa mgonjwa na alihitaji kwenda kwenye gari lingine kuchukua dawa yake au labda ... kujidhuru tena ili kupunguza hasira yake!

“Si lazima unifafanulie. Najua.” Lisa aliona jinsi Hans alivyokuwa akijaribu kutafuta kisingizio cha kumtetea Alvin lakini hakuweza. Hans alikuwa hoi. Alijua Lisa hakuelewa ni kwa kiasi gani Alvin alimjali.

Sura ya:203

Baada ya kufika City General Hospital, Chester alipanga madaktari bingwa hospitalini wamfanyie Lisa uchunguzi wa kina wa kimwili. Matokeo yalitoka haraka sana.

Chester alimtazama Lisa aliyedhoofika pale kitandani akihema kwa huruma. “Viashiria vyote haviko kwenye kiwango. Hypoglycemia, upungufu wa damu, upungufu wa maji mwilini, utapiamlo, na kidonda cha peptic.”

Lisa aliitikia kwa kichwa. Mwili wake ulikuwa wake mwenyewe. Nyakati hizo mara nyingi alikuwa akitapika na kusumbuliwa kwa maumivu ya tumbo, kwa hiyo alijua yote hayo.

Alvin alikunja ngumi kwa hasira iliyochanganyikana na huzuni. Alijua kwamba Lisa hakuwa na afya nzuri, lakini sasa hali yake alikuwa imezidi mbaya zaidi.

“Pole sana Lisa, unapaswa kupumzika kwanza.” Chester ghafla akamwambia Alvin, “Njoo uchukue dawa…”

“Dokta Choka, unaweza kusema lolote mbele yangu, hata kama linahusiana na uso wangu…” Lisa alitabasamu kumtazama. "Huna haja ya kunificha."
Chester alimtazama kwa huruma. "Sawa, kusema ukweli, majeraha usoni kwako yamekuathiri sana. Nimewasiliana na wataalamu kadhaa wakubwa wa ngozi, na watafanya kadiri wawezavyo kukurekebisha, lakini… si rahisi kwa sura yako kurudi kama hapo awali.”

"Dokta Choka, unaweza kueleza kwa undani zaidi?" Lisa alimtazama.

Kadri Alvin alivyoona jinsi alivyokuwa mnyonge na mwenye wasiwasi ndivyo moyo wake ulivyozidi kumuuma. “Hakuna haja ya kumuuliza. Ikiwa teknolojia ya hapa haitoshi na huwezi kurekebishwa ndani ya nchi, tutaenda ng'ambo. Teknolojia ya urembo hapa nchini sio ya kiwango cha kimataifa.”

"Sitaki kufanyiwa upasuaji wa plastiki kwa ajili ya uso mpya." Lisa akamkatisha.

Alvin aliifuta miwani yake na kumwamngalia kwa udadisi. "Kutakuwa na makovu yanayotofautiana."

"Naelewa." Lisa aliitikia kwa kichwa na kuegemea mto. "Asante kwa kujali lakini nitaridhika na matokeo."

"Usijali. Teknolojia inakua kwa kasi sana sasa, kwa hivyo hupaswi kukata tamaa.” Chester alimfariji.

'Ni sawa. Lakini haina haja." Lisa alikuwa na tabasamu hafifu usoni mwake tangu mwanzo, lakini mtu yeyote mwenye jicho la utambuzi angeweza kusema kwamba hakuwa na matumaini tena. Alikuwa amekata tamaa na kujisalimisha kwa hatima yake. Hakujali tena.

Macho ya Alvin yakafifia, akamwambia Chester, “Kwanini usitoke kwanza?”

“Sawa.” Chester alitoka na kufunga mlango.

Alvin akasogea karibu na kitanda chake na kumshika Lisa mkono kwa nguvu. Macho yake meusi yalikuwa mazito. “Haijalishi unaonekanaje, sijali. Ninakupenda wewe, sio uso wako."

"Ni kweli?" Lisa alitazama mavazi yake mapya. “Usijidanganye. Ulinikumbatia mwanzoni, lakini tayari umebadilisha nguo zako. Na kwenye gari ulinikimbia kwa sababu niilikuwa nanuka. Alvin, wewe kweli ni mwigizaji mashuhuri, unalijua hilo?”

“Hapana… sivyo…” Kwa mara ya kwanza, Alvin alijihisi kama mtoto. Alikuwa katika hali ya kutojielewa. Asingeweza kumwambia kwamba alikuwa amejiumiza na kulowesha nguo zake kwa damu kwa sababu ugonjwa wake ulimchukua tena. Ilimbidi abadili nguo safi kwa sababu nguo zake zilikuwa zimetapakaa damu. Ikiwa angejua kwamba alikuwa mgonjwa, angemwogopa hata zaidi.

“Huwezi hata kujieleza vizuri,” Lisa alisema kwa mzaha. “Alvin, kwa kweli sina huzuni kwamba sura yangu imeharibika. Kwa kweli, nina furaha. Ni jambo jema. Sasa kwa kuwa mimi ni kituko na mwenye kuchukiza kiasi cha kuwafanya watu wacheke, bado unaweza kulala kando yangu? Tunapaswa tu kuachana kwa nia njema sasa. Angalau nipe hadhi hii ya mwisho."

Alvin alikasirika. "Lisa, mimi sio mtu wa juu juu kama unavyofikiria. Nitakuthibitishia sasa hivi.”

Alvin alimvuta Lisa kwa nguvu mikononi mwake na kuifunga midomo yake na ile ya Lisa iliyokuwa imepasuka kwa vidonda. Vidonda bado vilikuwa vikitema majimaji ya usaha, na uso wake bado ulinuka vibaya kutokana na majeraha. Kusema kweli, hata Lisa mwenyewe alijionea kinyaa. Lakini, mwanamume huyu alimshika kama vile alikuwa ameshika tunda tamu lenye harufu nzuri. Busu lake lilikuwa la upole na la huzuni. Alvin alimbusu Lisa mpaka akajihisi kama anakata roho.

Busu lilipoisha, midomo yake ilianguka kwa upole kwenye jeraha kwenye shavu lake kama manyoya. Mabusu ya upole yalimpa Lisa hisia kali.
Ni kana kwamba alimpenda sana kiasi cha kutojali sura yake. Hata hivyo… Lisa bado alijiuliza. Hiyo inawezaje kuwa kweli? Ni wangapi kati ya wanaume kama hao walikuwepo katika ulimwengu huu? Hasa mwanaume mzuri kama Alvin alivyokuwa? Hata kama hakuwa yeye tena aliyesimama juu ya ufahari wa familia yao, wanawake wengi bado walikuwa tayari kujirusha kwake.

"Inatosha." Lisa aligeuka na kufunika macho yake. “Alvin, usijilazimieshekufanya hivi. Utaishia kukimbilia kutapika chooni baadaye.”

“Haijalishi. Nitaishi maisha yangu yote kukuthibitishia hilo.” Alvin akambusu paji la uso wake. “Chester alisema huwezi kula chakula kigumu kwa sasa kwa sababu tumbo lako haliwezi kumeng’enya. Nitakuletea chupa ya maziwa ya moto.” Akainuka na kwenda jikoni.

Mlango wa wodi ulisukumwa, na Pamela mara moja akaingia ndani kwa kasi. Alipomwona tu swali likamtoka moja kwa moja. "Kwa nini uso wako ..."

"Pamela, nimeharibika?" Lisa alitabasamu.

“Kumetokea nini?” Pamela alizidi kuhoji kwa mshangao. “Sikuweza kukupata kwenye simu siku hizi zote. Hata nilipiga simu polisi.” Pamela alianza kulia ghafla. “Kwanini Mungu anakutendea hivi? Ulikuwa mzuri sana, mrembo zaidi tulipokuwa shuleni. Wavulana walikutazama bila kujali ulienda…”

“Inatosha. Sikukuita hapa kuzungumza mambo ambayo yangemhuzunisha.” Alvin alimkabidhi Lisa maziwa na kumkatisha Pamela kwa ukali.

Pamela alipandwa na hasira baada ya kumuona Alvin. Moto machoni mwake ukawaka. “Sihitaji hata kukisia. Lazima utakuwa unahusika kwenye madhara yaliyomfanya awe hivi. Kufikiri kuwa wewe ndiye mtu tajiri zaidi nchini Kenya kuna kupa jeuri sana Alvin. Ukiniuliza, wewe ni kipande cha takataka ambacho huwezi hata kumlinda mwanamke. Kuna faida gani ya wewe kuwa naye? Unapaswa kuishi maisha yako yote peke yako."

“Pamela…” Lisa alikuwa na wasiwasi kidogo. Ingawa aliona maneno ya Pamela yakimfurahisha, aliogopa kwamba Pamela angemkera Alvin.

“Wewe...” Ilikuwa ni mara ya kwanza Alvin kukaripiwa vikali hivyo na mwanamke tofauti na Lisa. Hasira ilimpanda tumboni mwake, lakini hakuweza kuiruhusu imtawale kichwani.

"Nini? Nimesema chochote kibaya?" Pamela aliendelea kumlaani huku macho yake yakiwa mekundu. “Lisa wangu bila shaka ni mrembo sana, angeweza kuolewa na mwanaume anayempenda na kumlinda, lakini sasa ameharibika kabisa. ”

“Hajaharibika nitamuoa,” Alvin alisema.

“Hah unataka kumuoa kisha umtupe tena baada ya siku chache, huoni talaka uliompa mara moja tayari inatosha? Ulishindwa kumpenda alipokuwa na sura yake, utampenda sasa akiwa hivi?" Pamela hakumuamini hata kidogo, machoni mwake Alvin alikuwa akiigiza tu kutokana na dhamiri yake mbaya,

“Pamela Masanja, unathubutuje kumkemea Alvin hivyo?” Kutokea mlangoni mara sauti ya mtu mwenye hasira kali ilisikika.

Pamela alitazama nyuma na kuona kuna vijana wawili wakiingia mlangoni, mmoja alikuwa Sam Harrison na mwingine alivaa shati la rangi ya pinki, kijana mzuri lakini macho yake yalikuwa yamejaa moto wa hasira. Ni yeye ndiye aliyesema maneno hayo.

"Oh, ni wewe." Pamela alimkumbuka. Aliwahi kumuona pale alipoenda hotelini kukutana na Alvin. Alikuwa akicheza karata na Alvin enzi hizo, lakini hakukumbuka kuwa alikuwa msumbufu namna hio. Aliwahi kumuona pia wakiwa na Lisa mgahawani siku moja. Anaitwa Rodney Shangwe.

Rodney alidhihaki kwa ujeuri na alikuwa anakaribia kuongea lakini Pamela ghafla akapaza sauti akamwambia, “Ziba mdomo wako. Nyote ni kundi la mbwa mwitu. Ndege wa aina moja huruka pamoja.”

"Umesema nini?" Rodney alikasirika. "Wewe mwanamke mjinga. Unajua mimi ni nani?"

"Mjinga? Nadhani wewe ndiye mjinga. Sina hata haja ya kujua wewe ni nani. wewe ni kipande cha takataka tu ... " Kwa kuwa Pamela hakumpenda Alvin, pia hakuwapenda marafiki zake.

Lisa alikuwa na wasiwasi sana kwa sababu alimjua Rodney ni nani.

Sura ya: 204

“Pamela…” Lisa alitaka kumzuia lakini Pamela aliwahi kumkatisha.

“Lisa nyamaza, wala usiseme chochote. Najua anaweza kuwa mtoto mwingine wa kishua kutoka kwenye familia tajiri, ila siogopi hata kidogo. Kama ni kuniharibu acha waniharibu tu hata nifanane na wewe, nina deni kubwa kwako. Kama nisingemchanganya Alvin Kimaro kwa mtu mwingine, usingejihusisha nae na haya yote yasingekukuta. ” Pamela nusura alie kwa majuto.

"Oh, kwa hiyo yote yalianza kwa sababu yako. Nilijua wasichana wajinga kama wewe wanajua kuongea tu, kumbe huna maana hata kidogo?" Rodney alisema kwa ukali.

"Funga mdomo wako, wewe mwanamke,” Pamela alimfokea.

“Unasema nini?” Uso mzuri wa Rodney ulikuwa karibu kugeuka kuwa kama zimwi.

“Nimesema chochote kibaya, wewe ni mwanaume uliyevaa shati la pinki, unaonekana mrembo kuliko wanawake na unaongea zaidi ya mwanamke, wewe ni mwanaume au mwanamke?” Pamela alikuwa kachanganyikiwa.

"Wewe mwanamke mjinga. Nisipokuua..." Rodney alikuwa karibu kumrukia kwa hasira, lakini Sam alimzuia kwa haraka. "Bro, tulia."

“Si umemsikia mwenyewe akinitukana, nitulie vipi? Rodney alikasirika.

Pamela akaongeza kwa jeuri, "hata ukikasirika, wewe bado ni mrembo tu, kwa hivyo unaonekana mzuri hata ukiwa na hasira."

Lisa aliumwa na kichwa na ikabidi amwambie ukweli, “Pamela, inatosha. Yeye ni bosi wako. Ni Rodney Shangwe, mwenyekiti wa Osher Corporation.”

Pamela alokosa la kusema, eti nani? Hakuwahi kukutana na mwenyekiti wa kampuni yake, hata siku ile alipomuaga Lisa kuwa anaenda kukutana na mwenyekiti kwa kikao cha dharura hakuonana naye kwani alileweshwa pombe kabla hajafika. Ila kama mfanyakazi wa kampuni alifahamu kuwa mwenyekiti wa kampuni ni Rodney Shangwe. Kulingana na fununu alizozisikia, Rodwy alikuwa mtu mwenye nidhamu na mcheshi, lakini mbona aliyemwona alikuwa tofauti kabisa?

Pamela Masanja, umekwisha." Rodney alimdhihaki.

“Sawa, nimeelewa, najua madhara ya kumkosea heshima bosi wangu, lakini ulistahili. Nitaacha kazi tu, nitarudi kufungasha vitu vyangu.” Pamela hakujali hata kidogo.

“Usisahau mkataba uliosaini na kampuni.” Rodney alimkumbusha. “Mkataba wako ni tofauti na wafanyakazi wa kawaida. Ulisaini mkataba wa usiri. Ukithubutu kuacha kazi yako bila kibali nataka kuona ni nani atathubutu kukuajiri katika siku zijazo." Rodney alitisha.

"Bwana Rodney, rafiki yangu alikasirika tu kwa sababu ya kile kilichonipata. Natumai hutachukulia hili jambo kibinafsi." Ilimbidi Lisa amgeukie Alvin. "Pamela anaongea kwa mihemko, lakini fikiria juu yake. Kama ni wewe uliyeharibika sura, marafiki zako wasingekasirika vile vile? Kama vile mara ya mwisho Bwana Rodney aliponifundisha somo…"

"Nini ?Alikufundisha somo gani?” Pamela alimkazia macho Rodney, "Wewe bado ni mwanaume kwa kumnyanyasa mwanamke?"

"Ukisema neno lingine, nitakuthibitishia kuwa mimi ni mwanaume." Rodney alionya,

"Inatosha, acheni kulumbana. Hii ni wodi ya hospitali na sio uwanja wa malumbano. Mgonjwa anahitaji kupumzika." Alvin aliingilia kati kwa ukali, na watu wote wakanyamaza mara moja. Macho ya Alvin yalizunguka chumba kile na kutua kwa Rodney, “Rodney wewe ni mwanaume, uwe mkarimu, Pamela ni rafiki wa Lisa, achana naye.”

Rodney alimuangalia Pamela ambaye alimtumbulia macho tu, “Alvin huna shukrani kweli, niliongea kwa ajili yako tu kwa sababu alikuwa anakukaripia.”

Sam akamvuta na kusema kwa sauti ya chini “Rodney inatosha namuelewa Pamela, kusema kweli kumuona Lisa hivi imeniuma sana hata ninajilaumu kumpigia simu Alvin kumuita Dar es Salaam wakati huo.”

Sam alifikiri kwamba Alvin na Lisa walikuwa ni pea iliyotengenezwa mbinguni, lakini ikageuka kuwa ni hadithi mbaya ya mapenzi.

Rodney alitazama sura ya Lisa na ghafla akanyamaza, hakumpenda sana hapo awali, lakini alimhuzunikia ghafla muda ule.

"Ikiwa unanifikiria kama kaka, basi fikiria zawadi kwa ajili ya harusi yangu. Ninapanga kufanya naye harusi ya kusisimua baada ya mwezi mmoja." Macho meusi ya Alvin yalimtazama Lisa huku akisema kwa umakini, “Huniamini, lakini nataka kuuambia ulimwengu wote kwamba haijalishi sura yake, haitabadilisha upendo wangu kwake.”

Lisa aliinua macho yake ghafla na kukutana na macho yake kwa mshtuko.
Kwa kweli hakuweza kuamini kile Alvin alimaliza kusema. Alikuwa tayari ulimwengu mzima kuona anaoa mwanamke mwenye uso ulioharibika?"

Lisa alisema kila neno kwa sauti na wazi, "Nilichokuwa nataka ni ulimwengu usijue kama unanipenda kwa sababu yote hayo ni ya juu juu. Unaelewa?"

Maneno yake yalikuwa kama kisu kikali kinachomchoma Alvin moyoni. Alvin hakuelewa lolote. Alichojua ni kwamba alikuwa na deni kubwa sana. Katika maisha haya alitaka kumuweka pembeni yake daima na kumtunza.
•••
Lisa aliendelea kulazwa hospitalini kuuguza afya yake kwa siku kadhaa. Alvin alilala naye hospitalini kila siku.

Maneno juu ya Alvin kuleta watu kuzunguka makazi ya kifahari ya familia ya Kimaro ili kumuokoa Lisa yalikuwa yameenea Nairobi kote. Nyakati hizo, Nairobi ilijaa fujo na dhoruba nyingi za chini kwa chini.

Katikati ya dhoruba hizo, tukio la furaha lilishtua ghafla jiji. Binti wa familia ya Ngosha, Melanie Ngosha, na Jerome Campos kutoka familia ya Campos walikuwa wachumba waliotarajia kuchumbiana Jumamosi iliyofuata, na mshenga wao alikuwa Bibi Kimaro kutoka familia ya Kimaro.

Lisa alikuwa amepumzika wodini alipoona habari hizo. Alipigwa na butwaa. Aliwahi kusikia kuhusu familia ya Campos hapo awali. Familia ya Campos ilionekana ilikuwa familia ya kawaida sana jijini Nairobi zaidi ya miaka ishirini iliyopita. Hata hivyo, baada ya Mason Campos kumuoa Lea Kimaro, familia ya Campos haraka ikanyanyuka na kuwa mojawapo ya familia nne kuu za Nairobi kwa usaidizi wa familia ya Kimaro.

Kwa kuwa Jack alikuwa mrithi wa KIM International, ilimaanisha kuwa familia ya Kimaro ingeongozwa na Jack hapo baadaye. Kwa vile wazazi wa Jack pia walikuwa wanafamilia wa Campos, familia ya Campos bila shaka ingekuwa ya pili baada ya familia ya Kimaro hapo baadaye. Haishangazi Melanie alibadilika ghafla na kuacha kumsumbua Alvin. Kwa hivyo hiyo ndiyo ilikuwa sababu. Melanie alikuwa akisaka fursa za hadhi ya juu.

Hata hivyo, Melanie hakuwa na akili hiyo. Inaelekea ni Nina, mama yake, ndiye alikuwa injinia wa mipango yote. Nina Mahewa hakuwa mtu rahisi.

Usiku huo, Melanie alipakia video fupi mtandaoni. “Ndiyo, naingia kwenye uchumba. Najua kila mtu anashangaa kwanini nataka kuolewa ghafla baada ya kuachana na Alvin. Sababu ni rahisi. Nimechoka sana, na ni ngumu sana kumpenda mtu. Katika siku zijazo, ninataka kupata mtu anayenipenda, anayesamehe, kunithamini, kunijali na kunitendea kama binti wa kifalme, na si kama mtumwa.”

Videohiyo ilipokea maoni mengi sana kutoka kwa mashabiki zake;

[Moyo wangu unauma kwako binti wa kifalme Melanie. Lazima ujipende mwenyewe kuanzia sasa. Mwambie huyo mchafu Alvin aende kuzimu.]

[Alvin amekwisha. Yeye hastahili kuwa na wewe.]

[Nilisikia aliyemtongoza Alvin Kimaro ni dada wako wa kambo. Yeye ni binti wa haramu wa Joel Ngosha.]

[Hapana, Joel Ngosha ni mmoja wa watu kumi bora nchini. Ni mtu mzuri anayejali familia yake na kumpenda mke wake. Haya ni maneno ya uwongo]

[Nina hakika sana. Mtu huyo aliitwa Sheryl Masawe, na binti yake ni mwenyekiti wa Mawenzi Invenstments. Hata nina picha yake.]

Hapo picha za Sherly Masawe zikaanza kusambaa mtandaoni zikiambatana na maneno ya ajabu ya kumdhihaki.

Sura ya: 205

Kisha, picha za Sheryl na Lisa zilienea kwenye mtandao. Lisa alipokea simu kutoka kwa kampuni yake ikisema kwamba Facebook ya Mawenzi ilikumbwa na shutuma nyingi. Bodi ya wakurugenzi ya kampuni hiyo ilikuwa ikipigia kelele kuitisha mkutano tena.

“Nitakuja kwa kampuni mara moja." Lisa aliposema hivyo, Alvin akaichukua simu yake. Kisha akatoa amri kwa upande mwingine, “Mimi ni Alvin Kimaro. Nitashughulikia mambo yote huko Mawenzi. Usimpigie simu na kumsumbua mke wangu kwa muda huu.” Baada ya hapo, akaitupa simu pembeni.

“Alvin, unafanya nini?” Lisa alikasirika sana hadi tumbo lilimuuma. “Hata huwezi kujilinda sasa hivi, unawezaje kujali mambo yangu?”

"Huwezi kuondoka hospitali katika hali hii." Macho ya Alvin yalikuwa ya upole, lakini sauti yake bado ilikuwa kubwa kama zamani.

“Lakini siwezi kusimama tu kutazama picha ya mama yangu inapoenea kwenye mtandao. Amekufa kwa zaidi ya miaka ishirini, lakini bado anasingiziwa mambo ya fedheha.” Machozi yalimjaa Lisa. Kisha, machozi yalishuka chini ya mashavu yake. Alijilaumu. “Yote ni makosa yangu. Sina maana. Sikuweza kulipiza kisasi, na siwezi hata kumwacha mama yangu apumzike kwa amani.”

“Hayo yote hayajatokea kwa bahati mbaya. Yamepangwa na Melanie Ngosha na mama yake.” Alvin alimbembeleza. “Lisa, usilie. Niamini. Nitatafuta mtu wa kuzima mada hii mara moja. Tayari nimefanya maandalizi. Kadiri wanavyoruka ndivyo wanavyozidi kujitengenezea mazingira ya kuanguka kesho.” Alvin akauzungusha mkono wake kiunoni na kuinamisha kichwa chake ili kumbusu kwenye machozi yake. Sauti yake ilikuwa laini.

Akiwa hana raha kutokana na busu lake, Lisa aligeuza uso wake pembeni, na machozi yakakoma. Alikuwa kachanganyikiwa. “Unapanga kufanya nini?”

“Sitakuambia sasa. Ni siri, lakini utajua kesho.” Alvin alikuwa akizipapasa nywele za Lisa kwa kuzirudisha nyuma. “Ngoja nikulishe kwanza.”

Baada ya hapo, alimpa bakuli la supu ambayo Shangazi Yasmini alichemsha. Akapuliza juu yake ili kuipoza taratibu na kumlisha kijiko kwa kijiko. Kila mara alibaki akimwangalia kana kwamba hakuchoka kumuona usoni, lakini, Lisa hakuweza kuvumilia. Alijitazama kwenye kioo akajua ni mbaya, hivyo hakuelewa ni kwa jinsi gani mwanaume huyu hakuwa na kinyongo hata kidogo baada ya kumtazama kwa siku kadhaa.

“Nitakunywa mwenyewe…” Lisa alisema kwa aibu.

“Hapana. Chester alisema kuwa tumbo lako haliko vizuri sasa, na huwezi kunywa chochote kikiwa cha moto sana au baridi, lakini wewe huwa hauzingatii kamwe hivyo ni wajibu wangu kukusimamia." Alvin alisisitiza na kuendelea kumlisha.

Lisa hakuwa na chaguo. Alihisi kuwa Alvin sasa alikuwa akiigiza kama tafsiri ya kitabu cha mtu mwema. Hata hivyo, alihisi kwamba baada ya muda Alvin asingeweza kuukubali uso wake.
•••
Siku iliyofuata, Alvin alikuwa tayari ameondoka wakati Lisa alipoamka. Ilikuwa saa tatu asubuhi, na Aunty Yasmini alikuwa amewasha TV. Mara Lisa alipoinua macho, alimuona Alvin kwenye akihojiwa na mwandishi wa runinga. Hii ilikuwa mara yake ya kwanza kuonekana rasmi kwenye TV.

Kwa nyuma kulikuwa na chumba cha kupumzika, na Alvin alikuwa amekaa kwenye sofa. Alikuwa amevalia suti ya rangi ya kijivu ya gharama iliyoukumbatia mwili wake uliokamilika. Uso wake mzuri, mashuhuri, macho makini yenye haiba ya kujiamini, pua iliyonyooka, na mikono na miguu vyote vilikuwa vya kifahari na vya kupendeza. Aliwakabili watazamaji, na macho yake ya kina yaling'aa kama yamejaa maelfu ya nyota.

Lisa alitazama skrini kwa mshtuko. Wakati huo Alvin alikuwa mtanashati kiasi kwamba hakuweza kumtoa kasoro yoyote. Kando yake, watangazaji mbele ya TV pia walionekana kumshangaa muda wote. Ingawa kila mtu alijua kuwa Alvin Kimaro alikuwa ni mzuri, hawakuwahi kufikiria kuwa mwanaume huyo angekuwa na mvuto wa pekee namna ile kuwa naye karibu.

Mwandishi alisema, “Ni nadra kwa Bwana Alvin Kimaro kukubali mahojiano yetu. Nimejaribu kufanya miadi na wewe mara kadhaa huko nyuma, lakini ulikataa kila wakati. Unaonekana ni mtu ambaye hupendi kuonekana hadharani, kwa hiyo ni sababu gani iliyokufanya kukubali wakati huu?”

Alvin alipishanisha miguu, na sura yake ilikuwa shwari. “Watu wengi wamekuwa wakinikosoa kwenye mitandao siku za karibuni. Kusema kweli, hainisumbui, na sijali jinsi wengine wanavyoniona. Lakini jana walianza kumtusi mke wangu mtandaoni. Hili ni jambo ambalo siwezi kuvumilia…”

Mwandishi alishtuka. "Mke?"

"Kama ulivyosikia." Alvin alitazamana na kamera, na midomo yake ya kichawi ikajikunja na kutabasamu. "Mwenyekiti wa Mawenzi Investments, Lisa Jones. Yeye ni mke wangu.”

Mwandishi alipigwa na butwaa. “Una ushahidi gani? Mna cheti cha ndoa?”

"Kusema ukweli, tuliffunga ndoa zaidi ya miezi minne iliyopita." Alvin alisema kwa kujiamini.

Mwandishi huyo alishangaa. "Hiyo ni ... haiwezekani."

“Ni nini kisichowezekana kuhusu hilo? Cheti hiki hapa nimekuja nacho” Alvin akatoa cheti kwenye faili. Sio tu kilikuwa na picha zao, lakini saiani zao na tarehe ya ndoa pia iliandikwa kwa uwazi. Mpiga picha aliki’zoom kwenye kamera na cheti kikaonekana vizuri kwenye skrini.

Katika wodi, Aunty Yasmini alishangaa sana hata akadondosha machungwa mkononi mwake. “Bi Jones… Hapana… Bibi mdogo, kumbe mmefunga ndoa kabisa?”

Lisa alikosa la kusema. Ndiyo, walikuwa wameoana, lakini pia walikuwa wametalikiana. Alikuwaje bado ana cheti cha ndoa? Kichwa cha Lisa kilianza kudunda. Hakuweza kujua maana ya kitu chochote.

Kwenye runinga, mwandishi pia alichanganyikiwa. “Lakini si ulikuwa bado unachumbiana na Melanie Ngosha kutoka familia ya Ngosha nusu mwezi uliopita…?”
"Kuhusu suala hilo, pia nina hamu sana ya kuzungumza juu yake." Mdomo wa Alvin ukavutwa kwa tabasamu la kejeli. “Melanie Ngosha. Bi Ngosha, kama unatazama habari sasa, nataka kukuuliza tu. Tangu lini nimeanza kukuchumbia? Je, nilianza kukuchumbia kwa sababu tu nilicheza nawe kwenye karamu ya chakula cha jioni huko kwenye makazi ya familia ya Kimaro? Sijawahi kukutongoza au kutangaza wazi kuwa wewe ni mchumba wangu, na nimekuwa wazi kwako tangu mwanzo. Ninaamini mtu yeyote angeweza kusema kwamba sikupendezwa nawe.”

Mwandishi alipigwa na butwaa. "Lakini hapo awali, kuna mtu alikupiga picha mbili ukichuma naye matunda ya strawberry bustanini kwenu. Nyinyi wawili mlionekana kuwa karibu sana…”

“Oh, wakati huo? Niligundua tu kwamba alikuwa pale niliporudi kwenye makazi ya familia. Bibi yangu alinivuta pamoja naye hadi kwenye bustani ili kuchuma matunda na akapiga picha hiyo kwa makusudi ili kupotosha umma. Nilimpelekea mke wangu zile strawberry ili ale. Nilipoondoka siku hiyo nilimweka wazi Bi Ngosha na kumwambia asinisumbue.”

Alvin alitazamana na kamera, macho yake yakiwa yamepoa. “Bi Ngosha, kutokana na maneno yako, Kenya yote inaniona kama mpuuzi. Unapaswa kujua vizuri kwamba sijawahi kuwa mchumba wako hata kidogo.”

Mwandishi alishtuka. "Bwana Mkubwa, familia ya Kimaro inafahamu kuhusu ndoa yako na Bibi Lisa Jones?"

Alvin akatikisa kichwa. “Wanafikiri tu kuwa nachumbiana na Lisa, lakini familia yangu inapinga hilo. Wanafikiri hadhi yake ni ya chini sana kuolewa na mimi, na hanistahili kwa sababu hawezi kuniletea manufaa katika siku zijazo, lakini sijali. Nilikutana naye Dar es Salaam, na hakujua hata hali yangu wakati huo, lakini alinipenda kwa jinsi nilivyokuwa. Siwezi kuvumilia dharau ya familia yangu kwake tena. Nimeamua kuwa nitafanya naye harusi baada ya mwezi mmoja na kila mtu ajue kuwa nina yeye tu moyoni mwangu.”

“Pia…” Alvin alinyanyuka ghafla kwenye sofa. "Ni kweli mimi ndiye niliyevunja mikono ya wale vijana kwenye boti ya kifahari. Sitazungumza kile walichokifanya, lakini hawakupaswa kamwe kumdhalilisha mke wangu. Lisa ni mstari ambao hakuna mtu anayeweza kuvuka. Maadam ninaishi, nipo radhi kweenda kinyume na ulimwengu wote kwa ajili yake.” Wakati akiongea, macho ya Alvin yalikuwa kana kwamba yanamtazama Lisa moja kwa moja mbele ya TV.

Moyo wa Lisa ulikuwa ukidunda kwa nguvu. Ilibidi akubali kwamba hawa na nguvu za kuweza kupinga jambo hilo wakati uso mzuri na mkamilifu wa mwanamume ampendae uliposema maneno yenye kutawala na yenye kusisimua ya upendo. Hata hivyo bado alikuwa na wasiwasi. Alifikiri kuwa labda alikuwa akisafisha sura yake ya kifisadi hadharani. Lisa alibaki akiwa na hisia mchanganyiko baada ya tukio hilo.


Pembeni, Aunty Yasmini alitokwa na machozi. “Bibi mdogo, nilijua Bwana Kimaro alikuwa na wewe tu moyoni mwake, lakini sikutarajia kama angeweza kuwa jasiri na kuutangazia ulimwengu waziwazi namna hii. Inashangaza sana. Jitahidi mapema na umzalie mapacha. Nitakusaidia kuwalea.”

Lisa alikosa la kusema.

Lisa aliongea na tabasamu la hasira usoni mwake. ‘'Anti Yasmine, umesahau kuwa mimi ni mbaya sasa?'’

TUKUTANE KURASA 206-210

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..........LISA
KURASA.....206-210

Sura ya: 206

Kwa upande mwingine, mahojiano ya Alvin yaliibua taharuki kwenye Mtandao. Hisia za watu kwenye mtandao pia zilibadilika haraka sana.

[Sh*t! Kwa hivyo kama Bwana Kimaro amefunga ndoa na Lisa Jones zamani sana, ina maana yeye si mchepuko hata kidogo. Ni kawaida kabisa kwa mume na mke kulala pamoja. Melanie Ngosha ndiye alikuwa mchepuko badala yake.]

[Hebu fikiria hilo, zaidi ya ile picha alipokuwa akichuma strawberries na Melanie Ngosha, sijawahi kumuona akiwa na Melanie Ngosha hata siku moja. Kinyume chake, Alvin Kimaro amemkumbatia Lisa Jones na kumnunulia pete ya uchumba. Yeyote mwenye jicho kali anaweza kuona hayo ni mapenzi ya kweli.]

[Sasa nadhani Lisa Jones hana raha. Familia ya Kimaro haimkubali, na sote tulikuwa tukimsema hovyo pia. ]

[Bwana Kimaro, tulikosea. Wewe ni mwanamume kweli, wewe si fisadi hata kidogo, Ulipigana na familia za kitajiri Nairobi kwa ajili ya mke wako. Uko poa sana!]

[Mwishowe wa siku ile familia ya Kimaro iliondoa nafasi yake ya uenyekiti kwa sababu Alvin Kimaro alitaka kuwa na Lisa Jones. Walikunea sana!]

[Ee Mungu wangu, Alvin Kimaro aliachia kiti chake kwa ajili ya Lisa Jones? Siamini kama watu wema kama yeye bado wapo katika huu ulimwengu.]

Sikupaswa kugomea bidhaa za Alvin Kimaro. Kuanzia leo nitaunga mkono bidhaa zote anazowekeza.]

[Hakika Alvin Kimaro, wewe ni mwanamume wa ndoto zangu.]
•••

Katika familia ya Ngosha.

Melanie Ngosha na Nina Mahewa walipandwa na hasira kwa kuona taarifa hiyo. Joel alikuwa amezoea kutazama mama na bintiye wakivunja vitu karibu na nyumba kama vile wagonjwa wa akili.

"Hiyo haiwezekani. Ahh, inawezekana vipi Alvin na Lisa Jones kufunga ndoa miezi minne iliyopita?” Uso mzima wa Melanie ulikuwa umepinda. “Anasema hajawahi kuchumbiana nami kabisa. Kwanini anafanya hivyo? Alipofika nyumbani kwetu kwa chakula cha jioni hata alinishika mkono. Mama, kila mtu huko nje ananiita mchepuko sasa. Wote wanasema sina aibu…”

“Huyo Alvin Kimaro ni mshenzi sana. Sikuwahi kufikiria angeweza kufanya hivi.” Nina pia alipigwa na butwaa.

Tukio hilo lilitokea wakati ambapo Nina alikuwa amezama katika furaha ya uchumba kati ya bintiye na familia ya Campos. Alidhani Alvin Kimaro alikuwa amekwisha na asingeweza kuinuka tena. Hata alimtaka Melanie ajenge picha ya hali ya juu ya mtu ambaye alikuwa amekomaa katika mahusiano, kwamba angeweza kumpenda mtu au kumwacha ikiwa angehitaji kufanya hivyo. Hata hivyo, hakutarajia mashua yao kuzama siku iliyofuata. Alvin alikuwa na cheti cha ndoa mkononi mwake. Ulikuwa ukweli mgumu usioweza kupingika.

Kwa jazba, Nina aligeuza hasira yake kwa Joel. “Ulijua hili tangu mwanzo? Ukatuzuga kwamba Kelvin Mushi ndiye mchumba wa Lisa. Unatuchukuliaje kwa mfano?” Joel alimpuuza tu.

Melanie alihuzunika sana hivi kwamba alishindwa kujizuia pia. “Baba mbona hukuniambia? Mimi hunipendi hata kidogo. Unachowaza kichwani mwako ni kumsaidia Lisa tu."

“Nyie ni wagonjwa kweli. Siwezi kuishi na nyie tena. Siitaki nyumba hii. Baada ya ndoa ya Melanie katika familia ya Campos, tutapeana talaka.” Joel alishindwa kuvumilia, hapohapo alifungasha vitu vyake na kuondoka katika jumba la familia yake.

“Utachumbiwa na familia ya Campos hivi karibuni. Usijali sana mwanangu wengine wanasema nini kuhusu wewe.” Nina alimshika mkono Melanie. "Kwa kuwa familia ya Campos inatuunga mkono, ni suala la muda kabla ya Alvin Kimaro na Lisa Jones kushughulikiwa."

Melanie aliitikia kwa kichwa. Bila shaka angerudisha matusi kwa Alvin mara elfu. “Mama, ni kweli baba atakutaliki?”

"Babu yako hataweza kukubali." Nina alijigamba.

•••
Katika makazi ya kifahari ya familia ya Kimaro.

Asubuhi na mapema Mzee Kimaro nusura afe kwa hasira kwa sababu ya mahojiano ya Alvin kwenye runinga, hasa alipoonesha cheti cha ndoa. "Huyu kijana ni mshenzi, sikufikiria kuwa alimuoa Lisa Jones zamani sana."

Bibi Kimaro akajipapasa paji la uso. Bado alikuwa hajapata fahamu zake vizuri kutokana na mshtuko. “Naam, sasa ni mtu mzima, na ametudanganya sote. Hata nilihangaikia ndoa yake kama mpumbavu.”

Valeria alisema kwa hasira, “Mama, yale ambayo Alvin alisema kwenye TV yalikuwa mengi sana. Familia yetu ilimlea na kumkuza, lakini mwishowe, ameifanya familia yetu ionekane kama wapuuzi.”

“Unazungumza kana kwamba sisi si wapuuzi kweli,” Willie Kimaro hakuweza kujizuia.

“Willie, unatutukana?!” Spencer alimwangalia.

“Kama si upuuzi ni nini?” Willie alikazia, “tunamzungumzia tu Alvin ambaye amejua kucheza karata zake vizuri, kwanini tusiangazie familia badala yake? Sasa, sifa ya Alvin inabadilika. Ikiwa kutakuwa na tatizo na maendeleo ya siku za usoni katika KIM International, bila shaka tutageuka kuwa kituko.”

Kila mtu mara moja akamgeukia Jack. Mzee Kimaro alimtazama na kusema. “Jack, bora usiniangushe. Nimesikitishwa sana na Alvin.”

Jack akatabasamu. “Babu, usijali. KIM International ndio biashara kuu Afrika Mashariki. Ingawa baadhi ya watu wanasema ni Alvin aliyeifanya KIM International jinsi ilivyo leo, nadhani ni miunganisho ambayo familia yetu ilipata kutoka kwa vizazi na uwezo wetu wa kifedha ambao ulimsaidia. KIM International ina vipaji vingi, hivyo kutokuwepo kwake hakutakuwa na athari kubwa.”

“Uko sawa.” Mzee Kimaro aliridhika sana. “Alvin ana kiburi sana. Atajuta mapema au baadaye. Kwa kuwa sasa ameondoka KIM International, yeye si lolote.”

Range Rover nyeusi iliondoka kwenye jumba la kifahari la familia ya Kimaro. Lea, ambaye alikuwa ameketi kwenye kiti cha nyuma, aliuliza kwa kawaida, “Jack, vipi maendeleo ya utafiti na uendelezaji wa teknolojia mpya ya cement? Mkutano na waandishi wa habari utafanyika mwezi ujao."

"Mama, mhandisi mkuu wa utafiti, Simon Mbugui, aliongoza kikundi cha wafanyakazi wenzake kuwasilisha barua zao za kujiuzulu." Jack alishika usukani kwa nguvu. Uso wake mzuri ghafla ukageuka kwa huzuni. "Sikuidhinisha, lakini hawajafika kiwandani kwa siku kadhaa."

"Nini?" Lea alitazama juu kwa mshangao na mara moja akagundua. “Nakumbuka sasa. Simon Mbugui ni kipaji ambacho Alvin Kimaro alikisomesha nje ya nchi miaka mitano iliyopita. Karibu watu wote katika kiwanda waliajiriwa na Mbugui.

"Ndio, kuna uwezekano mkubwa kwamba Alvin ndiye mpangaji mkuu wa njama hizi." Jack hakuonekana vizuri. “Nilikuwa nikitafuta mtu wa kuchukua nafasi ya Simon Mbugui, lakini hatuna muda. Watu kama Mbugui hawawezi kupatikana kwa mwezi mmoja au miwili tu.”

Mason ghafla alisema, "Si ajabu, nilikuwa najiuliza kwanini Alvin aliondoka kwa urahisi sana. Amekaa KIM International kwa miaka mingi sana, lakini hakufanya fujo hata kidogo alipofukuzwa. Kumbe bado alikuwa na kadi ya kucheza."

"Utafiti huu wa simenti ni muhimu sana. Ikiwa uzalishaji utacheleweshwa, kampuni zinazoshindana nasi zitachukua fursa hiyo kuinuka, hasa hii kampuni ya Alvinarah.” Lea alikunja uso na kukemea, “Hali si nzuri, bado ulijigamba mbele ya babu yako kwamba utaweza.”

“Mama, haikuwa rahisi kwangu kutwaa KIM International. Siwezi kumruhusu babu afikiri kwamba mimi ni dhaifu kwa Alvin baada tu ya kushika wadhifa huo.” Jack alipiga kelele.

"Nitaenda kwa Alvin mchana kufanya uchunguzi…” Lea alisema.

“Kwa ajili ya nini? Nyinyi wawili mmekuwa mkitofautiana kila mara.” Mason alimpigapiga nyuma ya mkono wake. “Mshaurini tu arudi kwenye kampuni. Ndugu wawili wanaweza kufanya kazi pamoja. Kuna haja gani ya kupigana hadi kufa?”

“Baba, wewe ni mtu wa kufikiria sana. Nisipopigana, atanifukuza nje ya kampuni mara Bibi na Babu watakapokuwa hawapo. Kunatakiwa kuwa na mtu mmoja tu katika KIM International, na mtu huyo ni mimi,” Jack alisema kwa dhihaka.

"Ni kweli, hata mimi nataka pia Jack kuchukua jukumu la KIM International. Alvin anataka kumuoa Lisa Jones, lakini hana utulivu kihisia na karibu kumuumiza Valeria wakati huo. Simpendi zaidi sasa hivi.” Lea akatikisa kichwa. Ikiwa angeweza kurudi zamani, bila shaka asingemzaa Alvin.

Sura ya: 207

Baada ya chakula cha mchana.

Upepo wa utulivu na wa kustarehesha ulivuma kutoka dirishani, ukimpulizia Lisa kwa unyonge. Alifumba macho kwa kuduwaa, alitaka kulala, lakini ghafla akahisi mtu akimbusu usoni. Alikuwa ni nani?

Harufu nzuri ya kiume iliyopeperushwa kutoka kwa upande mwingine haikumchukiza hata kidogo. Macho ya usingizi ya Lisa yalifunguliwa polepole, na aliona sura ya kupendeza na kuvutia. Alionekana mtu ambaye hapo awali alikuwa kivutio cha wengi kwenye TV.

“Umeamka, nguruwe mvivu? Umelala kwa zaidi ya saa mbili.” Alvin alibana pua yake kama mtu aliyepagawa na upendo na kusema kwa sauti ya kuvuta.

Lisa alikuwa akihema kwa muda akafikiri yuko Dar es Salaam. Hata hivyo, hata huko Dar es Salaam, ni mara chache sana Alvin alikuwa mpole na mwenye kujali namna hii.

“Ulikuja saa ngapi?” Alikaa haraka. Alvin alifika kwa wakati kwani Lisa alikuwa na maswali mengi ambayo alitaka kumuuliza.

“Si muda mrefu, kama saa moja iliyopita. Nimekuja kukuona ukikoroma.” Alvin alitazama saa yake na kutania.

“Sikoromagi mimi.” Lisa alimtazama Alvin na kujibu kwa aibu.

"Utajuaje ikiwa unakoroma wakati tayari umelala?" Alvin alikuwa hajamuona hivyo kwa muda mrefu, hivyo alimtania makusudi.

“…Sawa, ni vizuri hata hivyo nikoromee. Angalau hakuna mtu atakayetamani kulala nami katika siku zijazo." Lisa alimkazia macho.

“Wewe ni mke wangu. Nitalala na nani kama si wewe?" Alvin alitabasamu na kumkazia macho.

“Inatosha, Alvin.” Lisa akabadili mada ghafla. “Tuliachana muda mrefu uliopita. Hicho cheti feki cha ndoa sijui umekipata wapi…”

“Nani kasema kuwa tuliachana? Hiki siyo cheti feki. Jionee mwenyewe.” Alvin alichukua baadhi ya nyaraka, moja ambayo alipewa aliposaini hati za talaka.

Lisa aliinyakua ili kuangalia. Ilikuwa sawa kabisa na ile ya awali. "Sisi ... hukunipa talaka?"

"Kusema ukweli, tulitia saini tu makubaliano ya talaka. Bado hatujakamilisha taratibu za kutalikiana.” Alvin alimtazama kwa tabasamu. "Tuliposaini karatasi, tayari ilikuwa mwishoni mwa mwaka, na ofisi za Jiji pia zilifungwa kwa likizo. Nani alijua kwamba tungegongana mara tu baada ya kufika Nairobi. Heh? Hata ukapata na mchumba mwingine siku kumi tu baadaye."

Lisa aliona aibu. Kwa maneno mengine, yeye ndiye alisaliti katika ndoa?

“Wewe pia ulikuwa msaliti. Ulitafuta rafiki wa kike,” Lisa alijibu kwa haraka. "Halafu, ulikana moja kwa moja kuwa una uhusiano wowote naye. Niliona kwa macho yangu jinsi ulivyomshika mkono kwa upendo ulipokutana na wazazi wake, karibu nikuite shemeji.”

“Una wivu?” Alvin alizungusha ncha ya pua yake. Alikuwa mchangamfu haswa alipoona sura yake mbaya isiyo ya kawaida.

“Unawaza kupita kiasi, sina wivu.” Lisa akatazama pembeni. Alivyojichukulia mwenyewe kwa sura yake, hakustahili hata kuwa na wivu.

“Sawa, nitakuwa mkweli kwako.” Alvin alimshika mkono na kuuweka chini ya kidevu chake. “Kila nilipowasiliana na Melanie Ngosha, ni kwa sababu anafanana kidogo na wewe. Kwa hivyo hapo mwanzo nilitamani kuwa naye kwa sababu tu alifanana na wewe.”
“Sijawahi kukuelewa…” Yalikuwa maneno mawili tu, lakini Lisa alihisi ghafla kuwa ndiyo sentensi pekee ambayo alikuwa amesema hadi muda huo ambayo ilimtoka kwa kawaida na kumgusa tangu aje Nairobi.

Moyo wake ulipiga kwa kasi. Alipokutana na Melanie kwa mara ya kwanza, alihisi pia kwamba Melanie na yeye walikuwa wanafanana kidogo. Hata hivyo, hakuamini kuwa hiyo ndiyo sababu ya Alvin kumwendea Melanie. Baada ya yote, alikuwa na uamuzi wa kuachana naye wakati anaondoka Dar es Salaam. Kutokuamini kwake pia kulimuumiza sana.

“Mwanzoni, nilifikiri kwamba kwa vile hukuwahi kunipenda na ulinikaribia tu ili kunidanganya, ningeoa mwanamke anayefanana na wewe na kusahau hilo. Lakini sikutarajia angekuwa dada yako wa kambo.” Macho ya Alvin yalikua magumu. “Tangu nilipokutana nawe kwenye makazi ya Ngosha, sikuwahi kufikiria kutaka kuwa na Melanie tena.”

“Lakini ulikuwa unaongozana naye hadi kwenye makazi ya Ngosha. Pia, umesahau jinsi ulivyokuwa na kiburi kwa kumlinda wakati wa sherehe ya kuzaliwa kwa babu yangu?” Lisa aliuma meno kwa chuki na kumbukumbu. “Sikuhisi kama unanijali sana. Hata umenifedhehesha mara nyingi sana.”

Alvin alimtazama kwa ajabu. “Kama si kwa sababu nilitaka kukuona, unafikiri kwanini ningehudhuria sherehe ya kijinga kama ya siku ya kuzaliwa? Kwa upande mwingine ulimleta Kelvin Mushi ili akutane na wazazi wako ukiwa bado kwenye ndoa. Umewahi kufikiria hisia zangu? Ulitaka nikae naye meza moja na kuangalia jinsi wewe na Kelvin mnavyopendana?”

Lisa alimsikiliza akitoa mashtaka ya uwongo huku uso wake ukiwa wa haki. Hakuwa na furaha. "Kwani wewe hukuonyesha upendo wako na Melanie mbele yangu pia?"

Alvin alikoroma kwa ujeuri na kumuuliza. "Ilikukuuma nilipofanya?"

"…Hapana." Lisa aligeuza uso wake mbali.

Alvin alikasirika, lakini ilimbidi akubali tu pale Lisa alipoonesha tabia kama hiyo. Alichoweza kufanya ni kumshika mikononi mwake na kumkumbatia kwa nguvu. “Hata kama haujali, mimi najali. Lisa, najua unanichukia, lakini nifanye nini? Nadhani unacheza nami, lakini siwezi kukuacha uende. Ninasumbuliwa na sumu inayojulikana kwa jina la Lisa Jones.”

Kadiri alivyozidi kuongea ndivyo alivyozidi kusononeka. Akainamisha kichwa chini na kuuma mdomo wake. Akampa busu lililojaa huzuni, upendo na huruma.

Lisa alikuwa amemkataa hapo awali. Kwa namna fulani, kila mara alionekana kuwa na mkanganyiko wa hisia moyoni mwake. Alijawa na chuki dhidi yake. Lakini, kwa kuwa sasa alikuwa amemwaga moyo wake kwake, moyo wake ulilainishwa kwa busu lake bila kupenda. Hakuweza kumpinga. Alijua kwamba bila kujali kuta alizojenga, Alvin angezibomoa kidogo kidogo.

Hiyo ni kwa sababu alikumbuka jinsi Alvin alivyopigana na familia nzima ya Kimaro kwa ajili yake. Alipigana dhidi ya familia tajiri jijini Nairobi kwa ajili yake, na akaachana na nafasi ya mwenyekiti wa KIM International kwa ajili yake. Hayo yote yalikuwa ukweli. Vinginevyo, Mzee Kimaro alipompa chaguo, kama angekuwa hampendi angechagua kubaki. Lakini, aliondoka kwa sababu yake.

Alipoona kwamba kulikuwa na mabadiliko kidogo ndani yake, Alvin alifurahi sana. Alizidisha busu kabla ya kumkandamiza mwili wake taratibu. Lisa alimfikiria Shangazi Yasmini jikoni na kumshika mkono wake bila fahamu, akisema kwa upole, “Usifanye hivyo, Shangazi Yasmini yuko hapa…”

Kilichomjibu ni mkono wa mwanamume huyo unaotetemeka ghafla. Kisha, aliona mwanga wa ghafla wa maumivu katika macho yake ya kina, lakini ni kwa muda mfupi sana.

“Wewe…”

“Sawa. Ni sawa kama hutaki.” Alvin aliinua mwili wake kwa mkono mmoja.

“Naenda uani…”

Sura ya: 208

“Subiri…” Lisa alimvuta nyuma ghafla.

"Nini?" Hakuwa amechukua hatua ya kumzuia kwa muda mrefu. Uso mzuri wa Alvin ulichanua tabasamu la kejeli. “Huwezi kuvumilia kuniona nikiondoka?”

Lisa aliuma midomo yake na kuinua mkono wake wa kushoto, na kuona mkono wake umefungwa kwa bandeji. “Umejeruhiwa na nini?”

"Ni jeraha dogo tu." Sura isiyo ya kawaida iliangaza machoni mwa Alvin, na mara moja akatoa mkono wake.

“Umeumia vipi?” Lisa alimkazia macho. “Ikiwa ni jeraha dogo tu, kwa nini utetemeke kwa maumivu kwa kuguswa kidogo tu?”

“Una wasiwasi na mimi?” Alvin alikunja midomo yake kwa tabasamu. Sauti yake nzito ilijawa na furaha. "Moyo wako unaumia kwa ajili yangu?"

",.. Toka nje." Lisa alikasirika kutokana na aibu. Alifikiri kwamba anamjali, lakini ... ilikuwa ni kwa sababu bado alikuwa mume wake kwenye karatasi.

Alvin alitabasamu kwa upendo na kwenda uani. Ndani, uso wake mzuri ulibadilishwa na wimbi la maumivu. Alifunua safu ya bendeji kwa safu. Ndani, jeraha kali lilikuwa limeunda mapele mekundu, na mistari minene ya hasira usoni kwake ilionekana kuwa ya kutisha. Alikaa hapo kwa dakika sita au saba. Kisha, simu yake ya mkononi iliita nje.

Lisa aliitazama simu iliyokuwa kitandani na kusema. "Mama yako anapiga simu."

Alvin aliifuata simu iliyokuwa kitandani, na sauti jeuri ya Lea ikasikika. "Una muda? Nataka tule chakula pamoja kama mama na mwana.”

"Si tulikuwa tayari kukata mahusiano yetu kama mama na mwana? Ulisema wewe mwenyewe.” Alvin alimkumbusha.

Lea akafoka, “Alvin Kimaro, usiende mbali sana. Mimi ndiye niliyekuzaa.”

“Ndiyo ulinizaa, lakini hukuchukua jukumu la kunilea. Wewe ni mama mzuri sana lakini si mlezi bora." Alvin alidhihaki. “Najua unataka nifanye nini. Sitakuja.”

“Wewe…” Lea alivuta pumzi kwa jazba. “Sawa, kama hukubaliani, basi usinilaumu kwa kwenda kwa mkeo Lisa Jones. Unafikiri atakuonaje nikimwambia kuhusu ugonjwa wako?” Uso wa Alvin ulibadilika ghafla. "Alvin, kila mtu anaogopa udhaifu wake zaidi, na wewe umeonyesha udhaifu wako sasa," Lea alisema kila neno wazi wazi.

"Utajuta kwa hili." Alvin akakata simu.

Lisa alimtazama. Machale yake yalimwambia kwamba kuna kitu kilikuwa hakiko sawa kati yake na mama yake. Macho yake yalikuwa yakimeta kwa damu kana kwamba yangetoka wakati wowote. Kusema kweli, aliogopa kumuona vile. Hata hivyo, alijua lazima mama yake alisema jambo lisilopendeza sana. Akiwa kama mtazamaji tu, aliona Lea Kimaro ni mkatili kweli. Ni mama gani ambaye angekosa huruma kwa mwanawe?

"Nini tatizo?" Alinyoosha mkono kumshika Alvin. Alikuwa na huzuni kali sana kiasi cha kumfanya aumie kidogo moyoni.

“Si kitu. Natoka mara moja.” Alvin alitikisa kichwa na kugeuka kuondoka.
•••
Saa 4:00 usiku, Chester alifika kumtembelea. "Vipi hali hali kwa sasa?"

"Siwezi kula sana, vinginevyo tumbo litauma," Lisa alimjibu kwa umakini.

"Kula polepole. Kula kidogo lakini mara nyingi. Unapaswa kuondoka hospitali kesho kutwa. Kuhusu uso wako… njoo kila baada ya siku mbili upate matibabu…”

“Dokta Choka, unajua jinsi Alvin alivyoumia mkono wake?” Lisa alimtazama ghafla.

Chester alisimama kwa muda huku akiifuta miwani yake. “Alvin alikuambia nini?”

"Hakuniambia chochote."
“Kwa vile hakuzungumza nawe kuhusu hilo, basi si wajibu wangu kusema lolote pia.” Chester alitabasamu kwa heshima. “Si lazima ufikiri kupita kiasi. Ujue tu kwamba Alvin anakupenda.”

Kwa hivyo kila mtu alijua kwamba anampenda? Lisa aliinamisha macho yake taratibu. Hata hivyo, kwa namna fulani, kulikuwa na hisia mbaya moyoni mwake ambayo haikuweza kufutika kwa maneno mepesi tu ya Dokta Chester.

“Lakini nataka kujua ni nani aliyemuumiza. Nina wasiwasi aliikasirisha familia ya Kimaro kwa sababu yangu…”

“Alvin si mtu wa kawaida, hivyo familia ya Kimaro haiwezi kumfanya chochote. Usijali. Sasa hivi ni wewe tu unayeweza kumdhuru.” Chester alipouendea mlango, aligeuka na kutabasamu. “Umeanza pia kumjali Alvin. Ina maana uko tayari kumsamehe?”

Lisa alipigwa na butwaa kwa sekunde chache, na uso wake ukalegea kidogo. Chester akacheka. “Naomba ukae naye. Alvin ana hasira kidogo, lakini inahusiana na malezi yake. Kama unavyoona, watu wengi katika familia tajiri ni wabinafsi na wanafikiria tu masilahi yao wenyewe. Alvin kwa kweli anasikitisha sana.”

Baada ya kuondoka, msemo 'Alvin anasikitisha sana' ulijirudia akilini mwa Lisa kwa muda mrefu. Nani angefikiri kwamba mtu tajiri zaidi katika Nairobi nzima angefafanuliwa kuwa mwenye kuhuzunisha? Hata hivyo, alipofikiria jinsi alivyotengwa na kuachwa na kila mtu wa familia ya Kimaro, moyo wake haukuweza kujizuia kumuonea huruma.

Wakati huo, Shangazi Yasmini aliingia na kumuuliza, “Bibi mdogo, naweza kukuandalia uji kwa chakula cha jioni leo?”

Lisa alitikisa kichwa na kuongeza muda mfupi baadaye, “Tengeneza supu ya kuku pia, na uchemshe pamoja na ndizi.”

Shangazi Yasmine alikuwa na shaka. "Lakini daktari alisema tumbo lako halitaweza kuyeyusha vyakula vigumu kwa wakati huu..."

"...Hapana, ni kwa ajili yako na Alvin." Lisa aliitazama simu yake haraka haraka ili kuficha aibu yake.

Shangazi Yasmine aliingiza midomo yake kwenye tabasamu. Alikuwa ameona kwa muda mrefu mapenzi ya watu hawa wawili kwa kila mmoja. Sasa kwa vile bibiye huyo alikuwa tayari kumjali bwana mkubwa, alitarajia siku zao ziendelee kuwa bora.

“Ni kweli nitatengeneza, lakini Bibi mdogo nitamwambia bwana mdogo kuwa wewe ndiye uliyeniomba nifanye, vinginevyo, hatakula. Kama unavyoona, kwa kawaida hayuko tayari kula chakula changu.”

Lisa aliuma mdomo. Alijua kwamba Alvin angefurahi sana kujua kwamba alimjali tena. Hakutaka kuona sura yake ya kihuni.

Aunty Yasmine akasema. “Hutakiwi kuwa na aibu. Afya ya Bwana Kimaro ni muhimu zaidi. Hajapata chakula cha kueleweka kwa muda mrefu, na huwa anahangaika sana linapokuja suala la chakula.” Lisa alifikiria juu ya jeraha lake na kutikisa kichwa kwa huruma.

Jioni, Alvin alifika na kukuta chakula cha jioni kimeandaliwa. Shangazi Yasmini alitenga chakula huku akitabasamu kwa unyonge. "Hii ndio supu ya kuku ambayo Bibi mdogo aliniomba nikuandalie."

Macho ya Alvin yaliangaza na kumgeukia Lisa, lakini aliinamisha kichwa kwa haraka ili ale na kukwepa kukutana na macho yake.

“Kwa kuwa kilipangwa maalum na mke wangu, lazima nile.” Alvin akaachia tabasamu la kufoka. Alikunywa bakuli kubwa la supu mpaka hakuna kilichosalia. Alimaliza hata ndizi zote na kutamani kulamba kabisa hadi bakuli.

Shangazi Yasmine alishangaa sana. "Bibi mdogo lazima utoe neno ndipo mumeo ale? Sijawahi kumuona Bwana Mkubwa akila chakula kingi hivi.”

Lisa alikosa la kusema. Alikuwa mlaji mzuri tu alipokuwa Dar es Salaam, lakini aligeuka kuwa na tabia nyingi mbaya aliporudi Nairobi.

“Siwezi kujizuia. Kwa kuwa Mm’wagilia roho yangu amezungumza, ni lazima nisikilize kwa utiifu, la sivyo hataniruhusu nilale karibu naye usiku.” Tabasamu la furaha lilienea usoni mwa Alvin.

Lisa alishindwa kuvumilia kumsikiliza kwa aibu na kumpiga teke kali.

"Teke la mpenzi haliumi." Alvin aliinua uso wake mzuri. Alionekana kana yuko tayari kupokea mateke zaidi. Lisa alikuwa hoi kabisa dhidi yake na aliweza tu kula chakula chake kimyakimya.

Saa tatu na nusu usiku, Lisa alikuwa tayari kuzima taa ili alale, lakini Alvin alivua nguo ghafla na kuingia ndani haraka.

“Alvin Kimaro, ondoka...” Walikuwa wamelala katika vitanda tofauti tangu Lisa alazwe hospitalini, hivyo alimfukuza kwa vile hakuzoea.

"Oh, teke lako limeanza kuniuma." Alvin alijieleza kwa uchungu.

“Acha kuigiza. Mguu wangu hauwezi kukujeruhi.” Lisa alimfokea.

“UNaumia sana, labda nikilala karibu na wewe ndiyo nitapona…” Alvin alimtazama kwa uchungu.

Sura ya: 209

Wakati huo huo, Lisa alishukuru kwamba alikuwa amezima taa mapema. Vinginevyo, Alvin angeona kinyaa kumtizama kwenye mashavu yake. Uso wake ulioharibika bila shaka ungekuwa na kidonda.

“Sikuwa…”

“Hakika ulikuwa unajaribu kunilemaza. Kwanini usiniangalie na kuona kama nimejeruhiwa?” Akacheka vibaya masikioni mwake.

"Hakika, nitaangalia baada ya kukupa teke lingine." Hatimaye, akainua mguu wake kwa mara nyingine. Alvin aliitikia haraka na kumshika mguu wake uliokuwa ukining'inia hewani.

"Msichana wangu mzuri, unataka kunitia ulemavu?"

Lisa alihisi kutetemeka kwa mgongo wake baada ya kusikia neno hilo la kupendeza. Kwa kweli alishindwa kuelewa ni kwanini mwanaume huyo hakujali kabisa kuhusu sura yake mbaya. “Alvin, unaweza kuacha masihara yako? Nataka kwenda kulala.”

"Mume na mke wanalala kitanda kimoja." Baada ya kusema hivyo, aliweka hata cheti chao cha ndoa karibu na mito, kana kwamba alikuwa na wasiwasi kwamba huenda amesahau kuhusu ndoa yao.

Lisa hakuwa na la kusema huku hisia ngumu ikitokea moyoni mwake. “Huogopi kuota ndoto mbaya kutokana na kuona sura yangu mbaya katikati ya usiku?”

"Hakuna kitu cha kuogopa. Ilimradi bado uko vile vile katika maeneo mengine.” Uso wake ulidhihirisha kuwa hakujali hata kidogo.

Kwa mara nyingine tena, uso wake ukalainika ndani ya sekunde chache. "Umekosea ikiwa hufikirii kuwa sina nguvu za kukutia kilema."

“Lisa, ninajaribu tu kukuambia kwamba hakuna kitakachobadilisha jinsi ninavyohisi kuhusu wewe. Haijalishi unaonekanaje.” Akaenda chini ya shuka ili kumkumbatia kwa nguvu. Hakuwa na hakika jinsi ya kuitikia ukweli wa sauti yake. Mtu huyu alikuwa kweli… Sigh, hakuwa na neno kwa hilo. Ina maana kweli hakujali kuhusu uso wake ulioharibika? Ilimshangaza sana.

“Unaniamini sasa? Nitathibitisha kwa matendo yangu.” Alvin alimtazama machoni kwa nguvu bila kuzuia hisia zozote.

Hilo lilimshangaza Lisa na haraka akaitikia kwa kichwa. “Sawa, acha kuongea. Nakuamini."

"Naweza kupata busu?" Akasogea karibu zaidi kutaka busu.

Lisa alisikia mapigo ya moyo yake yakidunda kwa kasi chini ya ngozi. Mwanaume huyu… kweli hakujali sura yake? Aliweza kuamini kwamba hakuwa anajifanya. Jinsi alivyombusu ilikuwa kama jinsi ile ile alivyombusu awali kabla hajajeruhiwa. Hakuna kilichobadilika. Ilikuwa ni kana kwamba hatawahi kuchoka kumbusu hata kidogo.

Siku ya tatu, Lisa alielekea moja kwa moja hadi Mawenzi Corporations baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini. Hakuwa amejitokeza kwenye kampuni hiyo kwa takriban nusu mwezi. Jambo la kwanza alilofanya aliporudi ni kuandaa mkutano wa dharura na watendaji. Hata hivyo, watendaji wote walipigwa na butwaa baada ya kumuona sura yake. Alijua alikuwa anaonekana vibaya sasa lakini daktari alikuwa amemwambia ni muhimu kuacha majeraha yapumue. Kwa hivyo, aliamua kutofunika uso wake siku hiyo.

“Samahani. Mambo mengi yametokea hivi karibuni na uso wangu… huenda usipone. Natumai nyote hamjashtushwa sana na hili.” Aliukabili umati kwa utulivu.

Watendaji walivutiwa kuwa mwanamke huyu mchanga katika miaka yake ya mapema ya 20 aliweza kukabiliana na hali mbaya kama ile kwa utulivu kama huo. “Mwenyekiti Jones, usikate tamaa. Kwa teknolojia ya kisasa ya matibabu, muonekano wako hakika utatengenezwa. Ni suala la muda tu,” Meneja Mkuu alisema kumfariji.

“Siyo ishu kubwa kihivyo, kwa kweli. Sisimamii kampuni kwa sura yangu bali kwa uwezo wangu,” Lisa alijibu kwa mzaha nusunusu. “Sawa, wacha tuendelee kujadili maendeleo ya miradi inayoendelea katika maeneo mbalimbali…”

Mkutano uliisha saa moja baadaye.

Lisa alirudi ofisini kwake na kukutana na kadi ya mwaliko kutoka kwa Melanie na Jerome kwenye meza. Walikuwa wakifanya sherehe yao ya uchumba huko Mombasa katika Hoteli ya Pavilion Intercontinental kesho yake.

Melanie alikuwa akijaribu kusema nini na mwaliko huo? Akiwa anawaza hayo tu, akapokea simu kutoka kwa namba asiyoifahamu. “Dada mkubwa, umeiona kadi yangu ya mwaliko?”

“Usiniite hivyo. Sina dada mdogo ambaye alijaribu kumuiba mume wangu.” Lisa aliongea maneno hayo akiwa na uhakika wa kulindwa na cheti cha ndoa upande wake.

“Una jeuri kweli. Nani kakuibia mume?" Melanie nusura apige kelele kwa hasira lakini akavuta pumzi ndefu badala yake. “Sawa. Hatimaye nimepata furaha yangu. Wewe ni binti wa baba hata iweje na hakuna kinachoweza kubadilisha ukweli kwamba tunashiriki damu moja. Nina hakika hutakosa sherehe ya uchumba ya dada yako mdogo sawa?”

“Bila shaka nitakuwepo kwa vile umenialika kwa fadhili." Lisa alijibu kwa upole.

Melanie alishtushwa na jibu chanya ambalo hakulitarajia. “Unakaribishwa sana. Enhee kabla sijasahau, nilisikia juu ya ulemavu wako wa uso. Usisahau kuvaa barakoa kesho. Sitaki uwaogopeshe wageni wangu. Natarajia kukuona.” Alikata simu baada ya kucheka.

Hatimaye Lisa alielewa nia ya Melanie. Walitarajia nafasi ya kumdhihaki. Lakini, hakuwa na wasiwasi sana juu ya kile watu hao wasio na maana walifikiria juu ya sura yake. Labda wangekuwa wao ndio wanaojisikia kuchukizwa kesho yake.

Shani alikuja kumchukua baada ya kazi badala ya Alvin. "Bwana Kimaro anafanya kazi ya ziada usiku wa leo, kwa hivyo hakuweza kupata muda wa kuja kukuchukua." Shani alieleza baada ya Lisa kujiweka kwenye siti ya nyuma.

Hili lilimshangaza Lisa. Alijua Alvin mwanasheria na angeweza kuwa busy muda wowote. Lakini pia alifahamu Alvin alikuwa na vitega uchumi vingine hata baada ya kufukuzwa kazi kama mwenyekiti wa KIM International. Lakini, alionekana kutojua chochote kuhusu mambo yake.

"Alvin kafukuzwa KIM International. Anafanya kazi katika kampuni gani kwa sasa?" Lisa aliuliza kwa mshangao.

Macho ya Shani yalimtoka baada ya kusikia swali hilo na kunyamaza.

"Ni sawa ikiwa hutaki kujibu." Lisa alitingisha kichwa na kuangalia pembeni. "Nauliza tu kwa kawaida."



Shani alikunja uso, akiwa amechanganyikiwa kidogo. “Bwana Kimaro hakufichii mambo kimakusudi. Ninaogopa kwamba unaweza kufikiria kupita kiasi baada ya kusikia jina la kampuni hiyo.”

Lisa alitazama juu kana kwamba alikuwa amekumbuka kitu ghafla. “Je, inawezekana… kwamba jina hilo linahusiana na yule mwanamke anayeitwa Sarah?”


“Inaitwa Alvinarah,” Shani alieleza, “Lakini kampuni hiyo ilianzishwa miaka mitano iliyopita, kabla ya Bwana Kimaro kukutana nawe. Nina hakika asingetumia jina hili kama angeanzisha kampuni mpya leo.”

“Sawa.” Lisa aligeuka pembeni kutazama dirishani.

Alvinarah… Ni dhahiri lilikuwa jina lililotokana na mchezo wa maneno wa majina ya Alvin na Sarah. Jina zuri kama nini! Kama ilivyokuwa yeye, Alvin na Lisa, Alvlisa.

Lisa alifikiri kwamba labda asingekuwa katika hali hiyo ikiwa mwanamke huyo anayeitwa Sara angalikuwa hai.

Sura ya: 210

Lisa alioga baada ya kurejea nyumbani na kukimbilia kwenye maktaba na kukagua kompyuta ndogo ya Alvin.

Kila idara ya kampuni yake ilikuwa imemtuma barua pepe yenye data za mauzo za bidhaa katika mikoa mbalimbali. Alichanganyikiwa haraka baada ya kukagua ripoti kwa ufupi. Asingeweza kupinga kuitafuta kampuni ya Alvinarah mtandaoni. Matokeo yalimshangaza sana!

Kampuni ya Alvinarah lilianzishwa chini ya miaka mitano iliyopita, lakini, thamani yake ya soko tayari ilikuwa imepita Shilingi za Kenya bilioni 200.
Kando na hilo, biashara kubwa yenye faida katika Alvinarah Corporation na KIM International ilikuwa katika miradi ya marighafi za ujenzi, kama vile simenti, jipsamu, chokaa na vitu kama hivyo. Bila shaka, nafasi ya KIM International katika sekta hiyo haikutetereka. Licha ya hayo, kampuni ya Alvinarah iliweza kujitokeza kutoka kwa ushindani na kudhibiti zaidi ya robo ya faida katika sekta iliyotajwa hapo juu.

Kwa maneno mengine, Alvin alikuwa ameanza mpango huu kwa siri yapata miaka mitano iliyopita. Je, alitarajia kwa muda mrefu kwamba angeachwa na familia ya Kimaro? Papo hapo, Lisa alihisi kutetemeka kupita ndani yake.

"Unapeleleza kampuni ya Alvinarah?" Sauti ya Alvin ilisikika nyuma yake ghafla.

Lisa alishtuka, akafunga laptop haraka. Hisia ngumu ilijidhihirisha moyoni mwake baada ya kumuona mtu nyuma yake ambaye alijitokeza bila kutarajia.

“Tayari nimeona skrini. Shani alikuambia kuhusu hilo?” Aliegemea meza kwa umaridadi.

"Ndio. Lakini kwa sababu nilimuuliza kuhusu hilo, "Lisa alisema mara moja kwa kuogopa kwamba Alvin angemlaumu mlinzi wake.

"Sio mbaya kwamba unaonyesha kujali kuhusu mume wako." Akainama huku akitabasamu usoni. "Lakini unaweza kuniuliza chochote ambacho unatamani kujua badala ya kukitafuta mtandaoni."

“Aaahmm..” Lisa aliinua midomo yake, lakini hakujua la kuongea.

Akampigapiga kichwani. "Unafikiri ninaogopa kwa kuanzisha kampuni ya Alvinarah kwa siri miaka mitano iliyopita kwenda kinyume na KIM International?"

“Si kweli? Ninaelewa umuhimu wa kujiandaa kwa siku za dhiki.” Lisa alijibu.

"Wewe ni mgeni, kwa hivyo labda hujui kuwa KIM haikutumaiwa kuwa biashara yenye faida zaidi ya makampuni yote. Ilianza kwa kujikongoja na ilifanya vibaya katika tasnia ya ujenzi. Mgogoro wa kifedha ulitokea baada ya mimi kuchukua kampuni, kwa hivyo sikuwa na chaguo ila kuimarisha nafasi yake katika tasnia ya ujenzi. Lakini mimi nilikuwa mwenyekiti tu. Kwa maneno mengine, mimi ni kama mfanyakazi mwingine tu. Ilinibidi nitengeneze mpango mbadala…Nilianzisha Alvinarah ili kuua ushindani wa nje na kuipa kampuni KIM nafasi ya kuongoza soko”

Aliendelea kusema, “Kama ningefanikiwa kurithi KIM International, Alvinarah angeendelea kuwepo katika nafasi ya pili milele na hakuna ambaye angemjua bosi halisi nyuma ya kampuni hiyo.”

“Lakini wewe si mwenyekiti tena wa KIM International. Je, unapanga kuiongoza Alvinarah kuiangusha biashara ya familia yako?" Lisa aliuliza.

“Timu nzima iliyokuwa inafanya kazi katika mradi wa utafiti wa teknolojia mpya ya cement na jipsam katika KIM International tayari imejiuzulu na hivi karibuni watakuja kunifanyia kazi Alvinarah. KIM International itaondolewa hivi karibuni bila kuwa na wahandisi wasomi na wenye uzoefu. Sekta ya ujenzi inabadilika haraka kila siku inayopita.”

Lisa ghafla alijiona mjinga sana. Alidhani Alvin ameachana na KIM International kwa ajili yake. Hata hivyo, yeye pia alishangazwa na hatua hiyo ya ujasiri. Kweli, kama ilivyotokea, tayari alikuwa na mpango mbadala mahali. Asingeweza kamwe kuondolewa kutoka juu ya ufahari wake. Labda angeweza kuwa na nguvu zaidi baadaye. Hilo lingetokea, kweli angekuwa tajiri mkubwa nchi nzima bila kuzuiwa na mtu mwingine yeyote.

“Mbona unaniambia haya? Je, huogopi kwamba ninaweza kufichua siri hiyo?” Lisa aliuliza kwa wasiwasi.

"Hapana, hauwezi, kwa sababu wewe ni mke wangu." Alimnyanyua kutoka kwenye kiti, akaketi mwenyewe, na kumweka kwenye mapaja yake.

Lisa alishusha macho yake chini ili kuficha kejeli machoni mwake. “Mke?'
Sahau. Jina la Alvinarah ni lako na la mwanamke mwingine.”

“Alikuwa mke zamani, sasa mke wangu ni wewe.”

"Alvin, hujisikii kuwa na hatia kidogo unaponiambia maneno haya?” Aliuliza ghafla kwa sauti ya kawaida. “Kama ilikuwa zamani kwanini sasa usibadilishe?’

Lisa aliona hisia zisizofaa ambazo zilijitokeza kwenye uso wa Alvin kabla ya kutabasamu kawaida. "Itaamuliwa baada ya majadiliano ya ndani ya mimi na wewe."

“Tusilizungumzie hilo tena. Hii ni nini?" Alipunga kadi ya mwaliko mkononi mwake.

ALvin alikumbuka kuiacha kwenye meza baada ya kurudi nyumbani. "Melanie alinialika."

"Alinialika na mimi pia." Alvin alicheka kabla ya kusema, "Anafikiria anaweza kuturusha roho kwa kuolewa na Jerome Campos."

Lisa alikosa la kusema. Mwanamke huyo hata alimwalika mpenzi wake wa zamani. Ilionekana kana kwamba siku hiyo ingekuwa ni siku ya kuvutia.

“Vema… Si lazima uende. Ipuuze tu.” Alvin akaitupa kadi ya mwaliko.

"Na wewe je?" Alimtazama machoni.

"Nitaitembelea familia ya Campos." Alvin alijibu kifupi.

Mwanga wa mshangao uliangazia katika macho ya Lisa. "Unafikiri familia ya Campos inahusika katika matukio ya hivi majuzi?"

"Ndio, haswa video hiyo kutoka kwenye Yatch. Jack hana uwezo wa kufanya hivyo peke yake. Nadhani familia ya Campos ilimsaidia,” Alvin alisema huku akipapasa vidole vyake. Alifurahi kumuona akiwa amevaa pete yao ya ndoa. "Zingatia kazi yako na acha nishughulikie hili."

“Hapana, tayari nilimuahidi Melanie kwamba nitakuwepo.” Aliinua kichwa chake juu kwa kumaanisha.

“Usiende…” Alvin alikunja uso.

Lisa aliruka kutoka mapajani mwake. “Unaogopa nitakudhalilisha kwa sababu ya sura yangu si ndiyo? Au labda una wasiwasi kwamba kwenda kwenye hafla za umma na mwanamke mbaya kama mimi kunaweza kukufanya kuwa kituko?”

"Lisa Jones ..." Sauti ya Alvin ilidhihirisha kutofurahishwa kwake. “Hivyo ndivyo unavyonifikiria mimi? Sitaki uende kwa sababu ninataka kukulinda dhidi ya Melanie. Nina hakika unajua nia yake mbaya.”

"Lakini ulemavu wangu ndo umeshatokea. Ina maana ni lazima niepuke matukio ya hadhara maisha yangu yote?” Alibembeleza uso wake kwa ufupi. "Hadhi yako ya heshima inamaanisha kutakuwa na hafla nyingi za kijamii zinazokungoja katika siku zijazo. Nini kinatokea watu wanapouliza kuhusu mke wako? Una mpango wa kunificha chumbani milele? Kwa upande mwingine, je, natakiwa kubaki nyumbani na kutazama unapojitokeza kwenye hafla na wanawake warembo tofauti kila wakati? Ikiwa ndivyo, basi unapaswa kunitaliki sasa hivi, sitaweza kuvumilia.” Baada ya kusema hivyo aligeuka na kuondoka.

Wimbi la kufadhaika lilimpitia Alvin. Amfanyeje mwanamke huyu ili ajue kwamba anampenda?

Lisa alipanda kitandani mara baada ya kukanyaga chumbani. Hakuwahi kukosa utaratibu wake wa kutunza ngozi wakati wa usiku hapo awali lakini kwa muda huo aliona haikuwa lazima tena.

Muda mfupi baadaye, Alvin alipanda kitandani na kumkumbatia kwa nyuma. Sauti yake ilijawa na unyonge. “Tafadhali usiwe na wazimu.
nitahudhuria tukio hilo pamoja nawe kesho. Ni wakati mzuri wa kutangaza kwa jamii ya watu matajiri wa Nairobi kwamba wewe ni mke wangu.”

Lisa aligeuka kumtazama na kuona mapenzi yakimiminika kutoka kwenye macho yake gizani. “Lakini… naonekana mbaya. Watu wanaweza wakakucheka.”

ALvin alibana pua yake kwa kuichezeachezea. "Ulikuwa ukinifokea tu kwa kukuzuia kwenda, lakini sasa unajidharau tena, maana yake nini?"

Lisa aliuma mdomo kwa kuchanganyikiwa. Alijua kweli alikuwa anajipinga mwenyewe. Hakuwa na wasiwasi kuhusu maoni ya wengine lakini maoni yake… bado yaliathiri hisia zake.

“Msichana mpumbavu, ni lazima nikuambie mara ngapi kwamba haijalishi sura yako bali nakupenda wewe kama Lisa?” Alvin alinong’ona kwa upole, “Sikutaka uende kwa sababu naogopa unaweza kukosa furaha. Sijali kuhusu wengine wanafikiri nini. Kitu pekee ambacho ni muhimu kwangu ni kile unachofikiria."

TUKUTANE KURASA 211-215

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI..........LISA
KURASA......211-215

Sura ya: 211

“Lakini… ikiwa uko tayari kukabiliana na watu pamoja nami, basi nitahudhuria mikusanyiko yote ya baadaye pamoja nawe huku nikikuweka kwa karibu."

Alvin alisisitiza kila neno kwa uzito kana kwamba alikuwa akisema nadhiri zake kanisani. Lisa alihisi kitu kikimsonga. Alikuwa mwanamke wa kawaida tu. Hakuweza kupinga kuguswa hasa wakati maneno matamu yalipotoka kinywani mwake, licha ya kuhisi kuwa Alvin alikuwa anaigiza tu kumpenda. Alihisi kutomwamini lakini wakati huohuo mvuto wa kutatanisha aliouonyesha Alvin ulipita kwenye hisia zake.

“Inaonekana kama itabidi nithibitishe upendo wangu kwako kwa vitendo."
Midomo ya Alvin ilijikunyata na kuwa tabasamu la kutatanisha kabla ya kumbusu midomo yake.

“Hapana…” Lisa alifadhaika alipotambua alichokuwa anataka kufanya. Alikuwa amepatwa na kiwewe tangu usiku ule wa kwanza.

"Msichana mzuri, wewe kwangu ni tunu ya thamani, kwa hivyo lazima nikupe hali ya usalama." Akamshika kiuno chake chembamba na kumvuta karibu. Aliachia tabasamu kali na kutamka katika hali ya kujiamini, “Nakuahidi sitakuumiza tena.” Lisa alijikuta akizama kwa sauti yake ya upole.

Siku iliyofuata, Alvin alitoka bafuni baada ya kuvaa na kumkuta Lisa bado amejilaza kitandani. Midomo yake ilionekana laini na nyororo. Alibaki amefumba macho huku akisitasita kumtazama.

"Nguruwe mvivu, jua limetoka na ni wakati wa kuamka. Mbunifu wa mitindo atakuwa hapa baadaye kidogo kukuletea vazi utakalo vaa jioni.” Kwa upole akampa busu kwenye paji la uso wake.

Hapo awali Alvin alikuwa ameajiri mwanamitindo mashuhuri kutoka Afrika Kusini kwa ajili ya kubuni gauni la Melanie la kuvaa siku ya harusi hiyo. Sasa kwa kuwa hakuwa tena na Melanie, alipindua tu oda hiyo na kumpa Lisa badala yake kwa sababu Lisana Melanie waliendana kwa umbo na kimo.

“Wewe ndiye nguruwe mvivu,” Lisa alifumbua macho yake na kumkemea.
Hata hivyo, macho yake yalikuwa yamejawa na mapenzi. Akacheka. Ingawa sura yake ilikuwa tofauti, macho yake bado yalikuwa yanavutia kama hapo awali.

"Mpenzi, ngoja nikusaidie kutafuta nguo ya kuvaa." Alvin alitembea kuelekea kwenye kabati la nguo.

“Sitaki msaada wako. Naweza kufanya mwenyewe.” Lisa alimsukuma.

Akiwa kwenye chumba cha kubadilishia nguo, Lisa alichanganyikiwa baada ya kuona uso wake kwenye kioo. Alvin alikuwa amethibitisha kwa matendo yake jana yake usiku kwamba hakujali kuharibika kwake usoni, lakini hakuweza kuamini kwa sababu hata yeye wakati mwingine ilikuwa ngumu kujikubali. Ilibidi akubali kwamba alipata hali mpya ya amani baada ya kusikia maneno ya kutia moyo ya Alvin jana yake usiku.


Mbunifu mitindo alifika mida ya saa nne asubuhi akiwa na gauni la jioni la rangi ya samawati lisilo na bega. Lilionekana la kawaida lakini lilimbadilisha kabisa Lisa. Nguo hiyo ilifunikwa na almasi ndogo ndogo zilizofanana na nyota zinazoanguka kutoka angani. Alitoka nje ya chumba cha kubadilishia nguo kama binti wa kifalme kutoka kwenye jumba la ufalme, kila hatua yake ilikuwa ya kuvutia na yenye mvuto wa ajabu.

Mbunifu mitindo huyo pia alimtengeneza nywele zake katika mikunjo mikubwa ya mawimbi na nywele ndefu za mbele zikifunika nusu ya uso wake. Macho yake ya pande zote yalionekana ya kupendeza sana chini ya mikunjo hiyo. Mabega yake yalifunuliwa na vazi lile lisilo na mabega, yakionekana kuwa safi.

"Bibiye, nataka uonekana wa ajabu leo. Gauni hili la jioni limebuniwa na Bonny King, mbunifu bora kutoka Afrika Kusini. Sio tu kwamba linagharimu zaidi ya milioni 5 za Kenya, bali pia ni la pekee duniani kote.” Mbunifu mitindo yule alimwambia Lisa kwa husuda. Lisa alishangaa kidogo. Hakutarajia gauni hilo kuwa la asili na gharama kama hivyo.

"Nilisikia Miss Ngosha alikuwa akipanga kuvaa hii kwa sherehe ya uchumba wake lakini sio kitu ambacho unaweza kununua kama mboga mboga hata kama una pesa," mbunifu huyo alisema huku akitabasamu. "Bila shaka utakuwa kitovu cha umakini wa watu katika sherehe usiku wa leo."

Kusema kweli, Lisa alifurahishwa sana na jitihada za Alvin.

Saa tano kamili asubuhi Alvin alifika nyumbani kutoka kazini kumchukua Lisa. Akasogea mbele kumshika mkono, na macho yake yakang'aa kama nyota za anga la usiku. "Nimelipenda sana vazi hili la jioni."

"Asante kwa kunijali mume." Lisa alisema huku akiinua macho.

Wakiwa njiani kuelekea Mombasa ambako sherehe za uchumba zingefanyika, gari lilisimama kwenye makutano ya barabara, likisubiri taa ya kijan iwaruhusu kupitai. Lisa ghafla aligundua kitu nje ya dirisha na akahisi moyo wake ukipiga. “Paki pembeni ya barabara. Ninataka kununua kitu kutoka kwenye duka la dawa."

"Unahitaji nini? Nitakwenda kukununulia.” Alvin alimtazama machoni.

“Um… dawa za kupanga uzazi,” alijibu bila wasiwasi.

"Hakuna haja, tunaweza kufikiria kuwa na watoto," Alvin alisema kwa sura ya umakini, "nakuahidi nitakuwa baba mzuri."

“Aaah Bwanaa..Muda bado Alvin…” Lisa alihisi uhusiano wao haukuwa thabiti kwa kupata watoto. Isitoshe, bado alilazimika kushughulikia matatizo mengi. “Sitaki watoto sasa. Mimi bado ni mtoto katika umri huu,” alisema huku akigeuza uso wake pembeni. Sauti yake ilisisitiza maamuzi yake.

“Sawa. nitakuletea dawa.” Gari lilisimama kando ya barabara. Alvin aliingia kwenye duka la dawa peke yake. "Nipatie vidonge vya Vitamini C na vidonge vya kudhibiti uzazi."

Muuzaji kwenye duka la dawa alimletea alichoomba. Hapo hapo, Alvin alibadilisha vilivyo ndani ya chupa mbele ya muuzaji. Muuzaji alikosa la kusema.

Baada ya kuingia ndani ya gari, Alvin alimkabidhi Lisa vidonge na chupa ya maji. "Nitakuacha utumie wakati huu lakini dawa kama hizi sio nzuri kwa afya yako. Nitatumia kinga wakati ujao.”

“Next time…?!” Lisa alimtazama kwa aibu Alvin baada ya kumtazama Hans aliyekuwa amekaa mbele. Alvin hata hakuhisi aibu.

“Mpenzi wangu, si jambo la kuonea aibu. Sisi si mume na mke?” Alvin alitabasamu kwa kujiachia. Lisa alikataa kujibu akihofia mazungumzo yangekuwa mabaya zaidi.

Sura ya: 212

•••
Hotel Pavilion Intercontinental. Mombasa!

Hoteli hii ya nyota tano karibu na bahari ilijengwa katika miaka ya hivi karibuni huko Mombasa. Ilikuwa na ufukwe wa kibinafsi na mikahawa saba ambayo ilihudumia vyakula vya kila aina kutoka kote ulimwenguni. Watu wengi matajiri na watu mashuhuri walipenda kufanya harusi zao za kifahari katika eneo hilo maarufu.

Sherehe ya uchumba ilifanyika kwenye ufukwe wa kibinafsi wenye bustani ya kifahari. Melanie alikuwa akifurahia pongezi kutoka kwa wageni wake.

"Jerome ni mkarimu sana hata amekutengea hoteli nzima," Aunty Irene alisema huku akitabasamu.

“Hiyo ni kweli, Melanie. Nina wivu sana,” Yvonne Ngosha, binamu wa Melanie, aliunga mkono.

“Nyie wawili mnatia chumvi. Ama kwa hakika, Jerome ndiye mwekezaji mkubwa wa hoteli hii la sivyo isingekuwa rahisi sana kwake kuhifadhi eneo lote hili,” Melanie alijigamba kana kwamba anazungumzia Jumba la White House.

“Oh, kwa hiyo hoteli hii ni mali ya Jerome! Nilisikia kwamba mauzo ya hoteli hii kwa mwaka ni sawa na mauzo ya hoteli tatu bora nchini Kenya. Hiyo inavutia.”

"Hiyo ni sawa." Melanie alielekeza macho yake kwa Jerome ambaye alikuwa amezungukwa na umati wa watu. Mwanaume huyo alipendeza sana, ingawa hakuwa mtanashati sana wala hakuwa sawa na Alvin Kimaro. Mbali na hilo, mustakabali wake ulikuwa umejaa fursa na uwezo.

Kila mtu kutoka familia ya Kimaro alikuwepo siku hiyo, bila kusahau majina mengine makubwa yenye ushawishi katika uwanja ya siasa na biashara.
Alijiona kuwa anajulikana kwa kuwa na wageni kama hao kwenye sherehe ya uchumba wake. Hiyo ndio harusi ambayo alikuwa akiiota. Alimini Alvin angejutia chaguo lake baada ya kufika pale baadaye. Lilikuwa kosa lake kukataa kumuoa. Kwa kuongezea, Lisa pia angekuwepo. Kwa kufikiria hivyo, Melanie alihisi huyo mwanamke aliyeharibika sura lazima angemuonea wivu sana.

“Tazama, Bwana Kimaro anaingia! Ameongozana na Lisa Jones.”
Aunty Irene alipiga kelele ghafla.

Kila mtu aliyekuwepo kwenye ufukwe wa hoteli hiyo aligeuza kichwa chake kwenye lango kuu. Alvin aliingia huku akiwa amevalia suti nyeupe. Ni mara chache sana alionekana katika hafla za umma akiwa amevaa nguo nyeupe lakini kwa wakati huo, alifanana na Prince Charming kutoka kwenye zile muvi za katuni za Disney. Wageni wengine wa kiume waliokuwepo hawakuweza kufananishwa naye.

Kando na hilo, Jerome, bwana harusi mtarajiwa pia alikuwa amevalia suti nyeupe siku hiyo. Alionekana wa wastani sana ukilinganisha na mwonekano wa kupendeza wa Alvin. Kwa hasira, Jerome akaivunja glasi ya mvinyo mkononi mwake baada ya kumuona Alvin amempiku kwa mvuto.

Kwa upande mwingine, Melanie pia alikuwa ameshindwa kuzuia hisia zake za wivu. Hii ilikuwa ni kwa sababu aliona gauni la jioni la rangi ya samawati ambalo Lisa alikuwa amevaa wakati huo, likiwa kali kuliko lake. Alikuwa akitaka kuvaa kipande hicho cha kazi ya ustadi kutoka kwa mbunifu mtaalamu Bonny King kwa sherehe yake ya uchumba lakini alishindwa kupata walau mkono wake tu licha ya kutoa pesa nyingi. Hata hivyo, Lisa sasa alijitokeza kwenye sherehe hiyo akiwa amevalia mavazi hayo!

Yvonne alifunika mdomo wake kwa mshangao kabla ya kunong'ona, "Hilo ndilo gauni lako la jioni uliloshindwa kulipata kutoka kwa Bonny King?..."

Melanie alimtazama kwa jicho la kumtoboa mara moja.

“Ni sawa. Uso wa Lisa ni wa kutisha hata hivyo. Ni sawa na bure tu hata kama gauni hilo la jioni lilianguka mikononi mwake,” Yvonne alisema sekunde chache baadaye.

“Uko sawa.” Zamani, Melanie alikuwa akimwonea wivu Lisa kwa kuwa mrembo kuliko yeye, na sasa alikuwa na furaha zaidi kuhusu ulemavu wa uso wake uliomfanya aonekane kama kinyago.

Baada ya kufurahi kidogo, Melanie alitembea kuelekea kwa wanandoa hao wapya waliowasili akiwa na Jerome. “Bwana Kimaro, uwepo wako kwenye sherehe ya uchumba wangu unaleta mwanga wa unyenyekevu katika sherehe yetu ya leo.” Jerome akasogea mbele huku akitabasamu. Licha ya salamu hiyo ya heshima, hakutoa mkono wake kwa Alvin.

Hii ilikuwa mara ya kwanza kwa Lisa kukutana na Jerome. Kusema kweli, mwanamume huyo alikuwa mzuri na pengine alisimama kwa urefu wa futi 5'7. Hata hivyo, alionekana mlegevu alipotabasamu. Hakuonyesha umaridadi wa heshima kama Alvin alivyofanya.

Bwana Thompson, rafiki wa Jerome ambaye alikuwa amesimama karibu, alicheka kufuatia maneno ya Jerome. "Ameleta nuru ya unyenyekevu kwenye sherehe yako? Bwana Campos, una mustakabali mzuri mbele yako. Bwana Jack Kimaro hata alitia saini mkataba mpya wa mkakati wa ushirikiano na kampuni yako baada ya kuchukua kiti cha uongozi wa biashara ya familia. Una uwezo mkubwa zaidi kuliko mtu fulani."

Melanie alikuwa juu ya mwezi baada ya kusikia hivyo. Aliunganisha mikono yake na ya Jerome kabla ya kuachia tabasamu la maana. “Bwana Thompson, hukupaswa kusema hivyo. Bwana Kimaro ndiye mfanyabiashara anayeheshimika zaidi jijini Nairobi, bila kusahau mtu tajiri zaidi nchini Kenya.

"Mtu tajiri zaidi?" Thompson alitoa mkoromo wa dharau. “Alifanikiwa kufanya hivyo kwa sababu ya msaada kutoka kwa familia ya Kimaro. Yeye si lolote sasa bila msaada wa familia yake.” Thompson alinyamaza kwa muda ili maneno yake yamwingie haswa Alvin kabla ya kumuuliza Mzee Kimaro aliyekuwa amesimama si mbali kutoka kwao, “ niko sawa, Mzee Kimaro?”

Mzee Kimaro alifoka huku akimtupia jicho la pembeni Alvin. "Ni aibu mtu mwenyewe haonekani kulitambua hilo."

Bwana Thompson hakujaribu hata kuficha dharau machoni mwake alipomtazama Alvin. “Bwana Kimaro, una bahati. Unatakiwa kufurahia karamu yako ya mwisho na watu wa hali ya juu usiku wa leo na mke wako. Labda hakuna mtu mwingine ambaye atakualika tena kwenye hafla za kipekee kama hizi katika siku zijazo.”

"Sawa, basi ninakushukuru Bwana Thompson kwa ushauri wako." Alvin alitabasamu kwa kushangaza. Hakuonekana kukasirika au kufadhaika bali alionekana zaidi kana kwamba alikuwa akitazama onyesho la vikaragosi la kipuuzi.

“Bwana Kimaro, tafadhali usifadhaike.” Melanie ghafla akatumia mkono kuziba mdomo wake kana kwamba ndo kwanza alikuwa anamwona Lisa. "Oh, nini kilitokea kwenye uso wako? Unatisha! Utadhani umeshushwa kutoka kuzimu?"

Kitu kama mwanga mkali wa moto kiliangaza machoni mwa Alvin. Alipasua midomo yake, akikusudia kulipiza kisasi lakini Lisa akaushika mkono wake na kutabasamu kwa utulivu. “Inatisha sana. Wakati mwingine, hata mimi hujichukia katikati ya usiku. Lakini kwa bahati nzuri, Alvin yupo karibu nami akinipa ujasiri ninaohitaji. Ananipenda, kunitia moyo, na kunijali. Hawapigi hata kope wanawake wengine wanaoendelea kujigongagonga kwake.”

Utulivu wa sauti yake ulifanya tusi la Melanie lionekane lisilo na maana.
Kinyume chake kabisa, maneno ya Lisa yalidokeza kwamba Melanie aliwahi kumsumbua Alvin lakini bado angependelea kuwa na mwanamke aliyeharibika sura kuliko yeye.

Melanie alikasirishwa na fedheha hiyo, lakini tabasamu la fumbo likaangaza usoni mwa Jerome. "Bi. Kimaro, wanaume huwa hawasemi ukweli. Baada ya yote, kile kilichotokea kwenye uso wako kinatia huruma sana."

Sura ya: 213

“Hiyo ni kweli, ninajisikia vibaya kwa ajili yako pia," Melanie aliunga mkono, "Mbali na hilo, wakati mwingine wanaume husema kile wanachosema kwa ajili ya heshima."

Lisa akajibu kwa kutabasamu. "Kwa kweli, ni muhimu kwa mwanamume kulinda sifa yake. Ah, Bwana Campos, nilipowasili Nairobi kwa mara ya kwanza na kusikia uvumi mbaya kuhusu wewe kujihusisha kimapenzi na mwanafunzi wa kike wa shule ya sekondari, nilifikiri kwamba msichana yeyote kutoka familia yenye hadhi asingetamani kuolewa na wewe. Kama ilivyotokea, nilikosea."

Baada ya kutulia kwa sekunde chache, Lisa alimwambia Melanie kwa uzito, “Dada yangu mdogo, kwa kuwa ni sherehe ya uchumba wako leo, ningependa kukupa neno la kweli la ushauri. Kila mwanamke atakuwa mzee au mbaya siku moja. Wanawake wazuri wapo kila mahali lakini uzuri wa ndani haufifii wala kuzeeka. Hii ndiyo siri ya kweli ya kudumisha ndoa yenye kudumu.”

“Uko sahihi mke wangu.” Alvin alisema kabla ya kugeuka kumwangalia Bwana Thompson. "Nadhani unaelewa hili vizuri. Baada ya yote, Bwana Thompson, wewe huwafuata wasichana wadogo wenye umri wa miaka 18. Nilisikia kwamba umejipatia kigori mwingine mdogo hivi majuzi. Bibi Thompson kwa kuwa anajijua kwamba yeye ni mzee, anafumbia macho yote hayo.”

Mara Lisa alijifanya kuwa na hasira na kumkodolea macho Jerome. “Bwana Campos, wewe ni rafiki mzuri wa Bwana Thompson lakini natumai hutafuata mtindo wake wa maisha. Hupaswi kumuumiza moyo dada yangu Melanie, sawa? ”

Uso wa Jerome ulikuwa umetanda kwa hasira baada ya kufedheheshwa hivyo kwenye sherehe yake ya uchumba. Melanie, ambaye alikuwa jeuri mapema, pia aliona aibu sasa. Hapo awali alifikiri kwamba Jerome alikuwa mwanamume mzuri lakini hakutarajia kusikia kuwa aliwahi kutoka kimapenzi na mwanafunzi mdogo wa shule ya sekondari, na pia rafiki yake mkubwa Bwana Thompson hakuwa mwaminifu pia. Mawazo hayo yalimtia kichefuchefu.

"Hapana. Tumeunganishwa na upendo wa mara ya kwanza kati yetu. Nitampenda na kumlinda Melanie milele.” Jerome alitabasamu kwa kujilazimisha.

“Vema, Bwana Campos, itakuwa vigumu sana kwako kujaribu kudumisha upendo huu wa upande mmoja. Mbaya zaidi unamuoa binti ambaye mawazo na mapenzi yake yote yapo kwa mwanaume mwingine, na wewe anakutumia tu kama kiboko cha kumchapia huyo mwanamume…” Lisa alifunika mdomo wake haraka kwa mkono wake. “Ah, jifanye hujasikia nilichokisema, samahani...”

"Lisa, unafanya hivi makusudi?" Melanie alikasirika. "Nilikuwa na uamuzi mbaya siku za nyuma. Jerome ni bora zaidi kuliko Alvin kwa kila njia.”

“Naelewa." Lisa aliitikia kwa kichwa. "Hasa kwa sababu sasa Jack amechukua biashara ya familia. Vinginevyo, sidhani kama ungemtazama Campos kwa mara ya pili.”

“Acha upuuzi…” Melanie alijuta kumualika Lisa baada ya kuona furaha ikitoweka taratibu kwenye ngozi ya Jerome. Alikuwa amefikiria kumwalika Lisa ili amdhihaki lakini hakika hakutarajia kama Lisa angekuwa na ulimi mkali namna hiyo. Angewezaje kuwa na kiburi hata akiwa na ulemavu wa uso?

“Ni sawa, Melanie. Twende zetu. Tuna wageni muhimu zaidi wa kuwasalimia. Watu wa hadhi za chini kama wao hawastahili wakati wetu mwingi.” Jerome hakuweza kuvumilia kuendelea kusikiliza kejeli za Lisa tena.

“Uko sawa.” Melanie aliunganisha mikono wake na Jerome na kuelekea kwa familia ya Kimaro. Hata hivyo, wawili hao walionekana kupooza sana baada ya yale waliyoyasikia.

Alipotazama maumbo yao yakitoweka, Alvin alibana ncha ya pua ya Lisa kwa kuichezeachezea. “Si mbaya hata kidogo. Uligundua hata maisha ya zamani ya Jerome kuwahi kutoka kimapenzi na mwanafunzi wa sekondari. Ulijuaje kuhusu hilo?”

“Pamela aliniambia. Amekuwa akifahamiana na mabinti na wanawake kadhaa wa jamii za kitajiri za hapa Nairobi na kusikia porojo nyingi kutoka kwao,” alijibu huku akitabasamu. "Na wewe umewezaje kujua kuhusu masuala ya mapenzi ya Bwana Thompson? Wewe si mtu wa kufuatilia mambo ya watu."

"Najua tabia za mabosi uchwara kama hao vizuri sana." Wawili hao walitembea kuelekea kwenye umati wa watu wakiwa wameshikana mikono.

Ingelikuwa ni zamani kabla hajavuliwa cheo cha uenyekiti, Alvin bila shaka angekuwa kazungukwa na kundi kubwa la watu ndani ya sekunde chache, lakini alichopokea siku hiyo ni dhihaka na dharau. Wengi wao hata walimsengenya Lisa hadharani.

“Usiichukulie hli personal. Hivi karibuni… watu hawa wote watakuja kujipendekeza kwako,” Alvin alinong’ona.

“Haijalishi hata hivyo. Ninachojali ni kuishi kwa amani na furaha na wewe tu basi.” Lisa alijibu na kumuona Joel akielekea kwake.

Joel alimtazama Lisa usoni kwa huruma. “Lisa, kwa nini hukuniambia kuhusu sura yako? Ni nini hasa kilitokea? Alvin Kimaro, ulijigamba kwa kusema unataka kumuoa binti yangu lakini hivi ndivyo unavyomlinda?”

Alvin alikunja uso huku akionekana kutofurahishwa. Joel aliendelea kupiga kelele kwa hasira, “Sikupaswa kusikiliza ahadi zako tamu. Ningejua ningeondoka naye tu…”

“Baba, Nina alihusika na ulemavu wangu wa sura,” Lisa alimkatiza. “Si muda mrefu uliopita, nilifungiwa na familia ya Kimaro kwenye shimo lao. Nina alishirikiana na Valerie na kuwaagiza wafanyakazi kuniwekea sumu kwenye uji wangu ili vidonda kwenye uso wangu vioze.”

"Nini?" Joel alishtuka. “Nitaenda kumtafuta huyu mwanamke kichaa…”

“Baba, wageni wengi wanaotambulika wako hapa kushuhudia sherehe ya uchumba kati ya akina Ngosha na familia ya Campos. Sio wakati wa kutengeneza tukio. Isitoshe Mzee Kimaro na wanafamilia yake wengine wapo pia. Nina hakika hawatakuelewa hata kidogo.” Lisa alijaribu kubadilisha mawazo yake.

Joel alikunja mikono yake kuwa ngumi na kuongea akiwa na hasira. “Lakini uso wako…”

“Ancle Joel, mambo mengine huchukua muda,” Alvin alisema kwa sauti ya chini, “Nitahakikisha wale waliomuumiza Lisa watalipa kwa matendo yao.”

Joel alihisi kutwishwa kitu kizito kifuani mwake. Alikuwa amefurahia umaarufu na mafanikio kwa sehemu kubwa ya maisha yake. Hata hivyo, alitambua kwamba alikuwa na deni kubwa sana kwaa binti yake huyo hivi kwamba asingeweza kumfidia kamwe. “Lisa, nimeamua kumtaliki Nina baada ya harusi ya Melanie. Sitabadili mawazo yangu hata kama kila mtu katika familia ya Ngosha angejaribu kunizuia.”

Lisa alimtazama baba yake kwa mshangao. Kusema kweli, alifikiri alikuwa mwenye moyo mpole sana kuelekea Nina na Melanie…

“Msiniangalie hivyo. Nasema ukweli.” joel aliwahakikishia. “Nina asilimia 40 ya hisa kwenye kampuni ya Ngosha Corporation. Nimeamua kukupa 35% na 5% iliyobaki kwa Melanie. Nitaiandika kwenye wosia mbele ya wakili haraka iwezekanavyo.”

“Baba…”

“Hilo linatosha. Keti tu na kupumzika huku utajiri ukianguka kwenye paja lako. Ninataka kuhakikisha kuwa unaweza kuishi bila wasiwasi kwa maisha yako yote. Kwa njia hiyo, unaweza kumudu kujinunulia kijana hata kama mumeo atakuzingua siku zijazo.” Alimtazama Alvin machoni baada ya kusema hivyo.

Lisa nusura apaliwe na mate. Hakutarajia baba yake angetamka maneno kama hayo waziwazi.

“Baba, sitamkatisha tamaa,” Alvin alijibu huku akitabasamu.

"Ha! Nitaaminije? Wanaume wamejaa uwongo." Sauti ya Joel ilisikika kwa kutoamini.

Alvin alishindwa cha kusema. Lisa alicheka bila ya kupenda. Ucheshi wa baba yake ulikuwa zaidi ya matarajio yake.

Nina, ambaye alikuwa akitazama kila kitu kwa mbali kidogo, aliuma meno yake kwa hasira. Joel alionekana kuwa na wakati mzuri na binti yake wa nje kwenye sherehe ya uchumba wa Melanie?

“Anti Nina, usijali. Nitawafundisha somo moja baadaye.” Jerome alifuata uelekeo wa macho yake huku kona za midomo yake zikibadilika na kuwa tabasamu baya. Kwa hakika aliapa kutowasamehe wawili hao kwa udhalilishaji wao hapo awali.

Nina alionekana kusitasita. “Lakini watu wengine wa familia ya Kimaro wako hapa pia…”

“Labda kuna kitu hujui. Familia nzima ya Kimaro haitaki kabisa kumsikia Alvin hivi sasa. Hakuna aliye na shauku zaidi yao kumuona Alvin akianguka.”

"Jerome, Melanie ndiye mwenye bahati ya kukupata." Nina alifurahi sana hakuweza kuacha kutabasamu.

Sherehe ilikuwa karibu kuanza. Msimamizi wa hoteli aliwaongoza Alvin na Lisa kwenye meza iliyokuwa mwisho wa ukumbi. "Samahani, hivi ni viti vyenu kwani ni watu mashuhuri tu ndio wanaoruhusiwa kwenye meza za mbele."

Nuru ilimulika machoni mwa Lisa alipotazama mbele ya ukumbi. Familia ya Kimaro na wengine walikuwa wamekaa kwenye meza ya katikati iliyokuwa mbele ya ukumbi. Valeria hata alikuwa akiwatazama kwa dharau walipopelekwa kwenye viti vya nyuma.

Sura ya: 214

“Lisa…” sauti ya upole ya Kelvin ilisikika ghafla masikioni mwake. Aliinua macho yake kutazama chanzo cha sauti hiyo. Alikuwa ni Kelvin Mushi. Alionekana kupendeza sana katika suti yake ya bluu. Macho yake yalitiririka kwa mshtuko na huruma alipomtazama. Akapiga hatua mbele na kuunyanyua mkono wake na kuubembeleza usoni mwake. Mkono mwingine ukamshika begani.

Alvin aliinuka na kumkumbatia Lisa karibu yake. "Kuna nini? Mbona unakosa adabu, yaani unamshika mke wangu hadharani mbele yangu?”

“Alvin Kimaro, wewe si yule uliyekuwa hapo awali, na ninakuhakikishia kuwa nitamchukua Lisa muda si mrefu. Hustahili kuwa naye.” Baada ya onyo hilo, alimgeukia Lisa na kusema kwa upole. “Nipe muda kidogo.”

“Kelvin, sikutarajia kukuona hapa leo.” Lisa, ambaye alikuwa amekwama katikati ya wanaume wale wawili, alijaribu kuongoza mada ya mazungumzo.

"Nimekuwa nikifanya kazi pamoja na Campos Ltd. hivi karibuni." Kelvin alisema, akimaanisha kuwa alikuwa mshirika wa Jerome Campos.

Sauti yake ilipopungua, katibu wa Jerome alikuja na kumsalimia kwa shauku, “Bwana Mushi, tumekuandalia kiti huko mbele. Ni watu wa hadhi ya chini tu ndio wanaopata viti vya nyuma.

"Ndio hivyo? Lakini huyu ni Alvin Kimaro..." Kelvin, ambaye kila mara alikuwa akimhofia Alvin, hatimaye akapata nafasi ya kumdhihaki.

“Alvin Kimaro ndiyo nani? Hastahili hata kukaa meza moja na Bwana Campos.” Sekretari wa Jerome alikoroma kabla ya kumuongoza Kelvin.

“Lisa unataka kujiunga na mimi?” Kelvin alimnyooshea mkono Lisa ghafla.

Kila mtu aligeuka na kuwatazama kwa ajabu. Wanawake walikuwa na wivu kuwa wanaume wawili wa sura zao walikuwa wakimgombania mwanamke aliyeharibika sura. Hali ya aibu ikamtanda Lisa.

“Kelvin Mushi, mara ngapi ninahitaji kukukumbusha kwamba yeye ni mke wangu?” Sura ya kupendeza ya Alvin sasa ilikuwa imekunjamana, na sauti yake ilisikika kwa vitisho.

“Unataka Lisa akae na wewe huku kwenye mkia wa ukumbi?” Kelvin aliuliza kwa upole ingawa macho yake yalionyesha nia ya dhihaka. “Hujamsikia katibu alivyosema? Ni watu wenye hadhi ya chini tu ndiyo wanastahili kukaa huku. Lisa ana hadhi ya juu kuliko wewe hivi sasa”

Kelvin hakujizuia kwa maneno yale ya kihuni. Wengine waliokaa meza hizo za nyuma hawakuthubutu hata kusema neno lolote kwani wengi wao walikuwa wamezamia tu na wengine hata kuhonga pesa ili kuingia kwenye sherehe hiyo ya uchumba ya kitajiri waweze kufahamiana na watu wengi zaidi kutoka familia zenye uwezo. Walishukuru kupata nafasi za kuketi ambazo wengine walisema ni za watu wa chini kama Alvin na Lisa.

Alvin alitabasamu.“Kelvin ulikerwa sana nilivyokudhalilisha kwenye sherehe ya kuzaliwa ya Mzee Ngosha mara ya mwisho kwa hiyo unalipiza kisasi?”

Kelvin aligoma kujibu. Hata hivyo, ni yeye pekee aliyefahamu jinsi alivyokuwa akifurahia wakati huo.

Alvin akalegeza midomo yake kwa tabasamu.“Unajionyesha kuwa ni mtu mstaarabu na mwenye adabu lakini inavyoonekana umejaa udhaifu mtupu na kutojiamini ndani yako. Kama mimi nipo wa hadhi ya chini, unawezaje kupambana na mtu ambaye tayari ameanguka?"

lilimshangaza sana Lisa. Alielewa kuwa Kelvin alikuwa anamchukia Alvin, lakini hakuwahi kumdhihaki hata siku moja. Lakini baada ya kusikia hivyo alimdharau sana Kelvin. Kweli Kelvin alionekana kuwa mtu tofauti siku hiyo. Hata aliuona unafiki uliomo ndani yake.

Alvin aligeuka na kumpigapiga Lisa kwenye uso wake. "Wanaume wengine ni wanafiki wazuri sana, tazama, mimi sijaribu kuficha kuwa ni mtu mbaya, tofauti na wengine wanaojionyesha kuwa watu wazuri lakini wana roho mbaya sana kwa ndani."

"Inatosha, Alvin Kimaro! Unadhani ninaweza kuzungumza nawe kwa utulivu baada ya kuiba mchumba wangu?" Kelvin aliripuka. Uso wake sasa ulikuwa umetanda kwa hasira. “Lisa njoo twende mama, nina uwezo wa kukuhudumia sasa hivi.”

“Pole, Kelvin, nadhani nitakaa hapa.” Lisa alimtazama huku uso wake ukiwa na huzuni, “Tafadhali nenda, siendani na wewe na sura yangu ya kutisha.”

“Umesikia hayo?” Alvin alimkumbatia Lisa kwa mahaba na kumwambia kwa upole, “keti mpenzi, tafadhari, nitaendelea kukunywesha wine taratibu.”

Kuna kitu kilipita machoni mwa Kelvin huku akimwangalia Lisa aliyekuwa ameegemeza kichwa chake kwenye kifua cha Alvin. Kelvin alizuia hasira zake za ndani na kugeuka ili kuondoka. Lisa alihema kwa ndani huku akiinua macho yake kumtazama akiondoka. Alitamani sana Kelvin aondoke haraka. Kwa kuwa alikuwa ameamua kurejea upande wa Alvin, alijua kwamba haiwezekani wawe pamoja tena.
Ilikuwa ni vigumu zaidi kwa kuwa bado alikuwa ameolewa na Alvin.

"Kula snacks zako na uache kuwafikiria wanaume wengine." Alvin alimgutusha ghafla kutoka kwenye fikra zake.

Lisa akageuza uso wake na kusema. “Kelvin huyu si kama yule niliyekuwa namjua…”

“Si kila mtu anaweza kuhudhuria sherehe hii ya uchumba. Yeye si mwenyeji wa Nairobi na hana watu wengi anaofahamiana nao hapa, hata hivyo alifanikiwa kufika hapa leo. Isitoshe amewekewa kiti kwenye meza nne za mbele. Unafikiri haya yote yametokea kwa bahati tu?” Alvin alimuuliza.

Lisa hakuwa na neno la kusema. Hakika, alihisi kama Kelvin alikuwa na mwenendo usio wa kawaida siku hiyo.


Baada ya sherehe. Familia ya Campos iliwaalika wageni wao kwenye bustani kwa ajili ya picha na burudani nyingine. Kundi la watu likaanza kutembea kuelekea mlangoni. Lisa alikuwa ananyanyuka tu pale alipohisi mtu akimpiga kwa nguvu. Mara, mwanamume mnene akageuza kichwa chake ili kumnyooshea kidole. "Kwanini unanigusa makalio yangu?!"

Lisa alimtambua mtu huyo papo hapo. Alikuwa ni Mkurugenzi Majuto ambaye alikuwa amejaribu kumsumbua kwenye chakula cha jioni cha hisani cha KIM International.

"Nini? Unathubutuje kumshika makalio mume wangu?! Mwanamke mwenye sura ya kutisha namna hii unataka kumtongoza mume wangu? Amini nikisema nitakupiga hadi ufe." Mwanamke mnene karibu na Mkurugenzi Majuto akasogea mbele haraka kwa nia ya kumpiga Lisa makofi,

"Bi Majuto, unataka kupoteza mkono?" Macho ya Alvin yalimtoka kwa hofu huku akishika mkono wa mwanamke huyo.

“Msaada, Bwana Kimaro anataka kunivunja mkono!” Bi Majuto alipiga kelele za kishindo ghafla.

Wageni waliokuwa wakielekea bustanini waligeuza vichwa vyao kuelekea chanzo cha zogo hilo. “Mkurugenzi Majuto na Bi Majuto, kuna nini?” Jerome akawasogelea huku akionekana kuwa na wasiwasi,

“Asante sana kwa kuwahi kufika hapa, nilikuwa napita tu pale mwanamke huyu aliponishika vibaya, mke wangu ana hasira na alipokuwa anamkaripia ghafla Bwana Kimaro alitishia kumvunja mkono mke wangu. ” Majuto alisema akifanya ana hasira.

"Haya, Lisa, haujaridhika kwamba Alvin si mwenyekiti tena wa KIM International, kwa hivyo unatarajia kutafuta bosi mwingine kwa nguvu?" Valeria aliziba mdomo wake kwa mkono ghafla.

"Unachukiza sana. Mwanamke usiye na haya!"

“Fanya haraka muombe msamaha Mkurugenzi Majuto na mkewe.” Wageni waliomzunguka wakaanza kumkemea Lisa.

Papo hapo, Bi Majuto alifumba macho ghafla na kuanza kulia kwa kwikwi. "Bwana Kimaro pia alivunja mkono wa mume wangu..."

"Tazama, mkono wangu bado unauma..." Mkurugenzi Majuto alizuga kukasirika.

Uso wa Mzee Kimaro ulikuwa umetanda hasira, “Unavuka kikomo, Alvin muombe msamaha Mkurugenzi Majuto haraka.”

Jack alipumua na kusema kwa majonzi. "Ndugu, Mkurugenzi Majuto ni mshirika muhimu wa biashara wa KIM International. Yeye pekee ana uwezo wa kununua tani milioni mia moja za simenti kwa mwaka. Umevuka mipaka kwa kweli wakati huu."

"Ndio hivyo?" Alvin alilegeza tie ya shingo huku akiwa na tabasamu lisilojali usoni mwake.“Basi Mkurugenzi Majuto nikuombeje msamaha ili unisamehe?”

Sura ya: 215

Mkurugenzi Majuto alikagua kwa macho yake eneo zima ili kuhakikisha hakuna mtu kutoka kwa familia ya Kimaro ambaye alikuwa na nia ya kumsaidia Alvin.
“Mimi si mtu asiye na akili. Kwa kuwa uliniumiza mkono wangu siku ile, basi leo nitarudisha kisasi kwa kukuvunja mkono wako. Isitoshe mke wangu amedhalilishwa na mkeo kwa kunishika makalio yangu. Lakini tunaweza kusawazisha hili ikiwa utamruhusu mke wangu kumpiga mke wako kofi usoni.”
Lisa alicheka baada ya kusikia hivyo. “Una uthibitisho kwamba ni kweli nilikushika makalio yako? Nina hakika kuna kamera za usalama kila mahali. Hebu tuangalie picha tuone kama kweli nilikuwekea mkono wangu...”
Mkurugenzi Majuto akaruka kwa hamaki. "Unamaanisha nini? Kwanini nimsingizie mwanamke mbaya kama wewe?"
"Mkurugenzi mashuhuri Majuto hawezi kukusingizia. Mambo yamefikia pabaya sana lakini bado unakataa kukiri kosa lako. Nadhani kofi moja usoni haitoshi hata kidogo.” Bwana Thompson alionekana kujaribu kufanya mambo kuwa mabaya zaidi.
Melanie alipendekeza zaidi, “Lisa, omba msamaha haraka kwa mwanamume huyo na umuahidi hutarudia tena.”
Lisa alitabasamu tu kwa kejeli na kusema, “Naona mmedhamiria haswa kwa kila njia kutudhalilisha sisi wawili siku ya leo. Ukweli hata haujalishi, kwanini tusichunguze kwanza kama ni kweli ndipo niombe msamaha?"
"Hatuna muda wa kupoteza, Bi Jones, mtu mzima na hadhi yake kama Mkurugenzi Majuto hawezi kamwe kukusingizia uwongo." Jerome alisema kwa sauti ya chini. "Hata hivyo, mtu anapaswa kuvuna matokeo ya matendo yake. Unasemaje, Bwana Alvin Kimaro?"
Kila mtu akahamishia macho yake kwenye sura ya Alvin iliyokuwa imefura kwa hasira. Si muda mrefu uliopita, mtu huyu alikuwa juu ya uongozi. Sasa akiwa ameanguka kutoka juu, kila mtu alishindwa kujizuia kutaka kumuona akiteseka.
Chini ya macho ya umma, macho ya Alvin yaligeuka kuwatazama watu wa familia ya Kimaro. “Babu, Bibi, Mama, mnakubali pendekezo lao? Mko tayari kweli Mkurugenzi Majuto anivunje mkono na kumchapa kibao cha uso mke wangu?” Kwa maoni ya wanafamilia, alikuwa akitafuta msaada.
Bibi Kimaro alitingisha midomo yake. “Nafikiri—”
“Nadhani ni wakati wa nyie wawili kupata adhabu,” Mzee Kimaro alimshika mke wake kwa bega huku akimkatiza. "Tulishindwa kukuelimisha, lakini kwa bahati mbaya tukakugeuza kuwa mtu mwenye kiburi na dhalimu."
Valeria alikuwa akitabasamu kutoka sikio hadi sikio. “Alvin, naamini hukuliona hili likija. Hivi umesahau jinsi ulivyonifanyia mara ya mwisho? Lakini sasa unaona umuhimu wetu? Endelea kuota."
"Mama, unaonaje?" Alvin alimkazia macho Lea. Mwanamke yule akakwepesha macho yake.
Alvin akainamisha macho yake kwa masikitiko. Lisa hakuweza kujizuia kumuonea huruma mwanaume wake, akamshika mkono wake kwa nguvu. Alielewa uchungu wa kuachwa na familia yake mwenyewe. Alitazama juu ya bega lake kukutana na macho yake.
Mkurugenzi Majuto akafurahi sana kusikia familia nzima ya Kimaro ilimuunga mkono. “Umesikia hivyo? Nyoosha mkono wako sasa hivi. Hmm, nadhani tunapaswa kwenda na mkono wako wa kulia."
Alvin alipoinua kichwa chake tena kutazama chumba chote, midomo yake maridadi ilijikunja na kuwa tabasamu hafifu. "Kwa kweli, ghafla nilikumbuka kitu. Kwa kuwa karibu familia zote tajiri za Nairobi ziko hapa leo, naomba mniruhusu nijitambulishe tena.”
Alichukua kadi ya jina la dhahabu kutoka mfukoni mwake na kuionyesha huku akiongea kwa madaha. "Mimi ndiye mwanzilishi, mkurugenzi, na mwenyekiti wa kampuni ya Alvinarah, Alvinarah Corporation…”

Kila mtu aliifahamu kampuni hiyo, lakini hawakumjua mmiliki wake hadi alipojitambulisha. Ilikuwa ni kampuni kubwa, haswa ikiwa imejikita katika kuzalisha na kusambaza vifaa vya ujenzi katika nchi za Kenya, Uganda Somalia na Sudani Kusini. Ilikuwa na sehemu ndogo ya soko lake nchi Tanzania pia. Ingawa ilianzishwa chini ya miaka mitano iliyopita, kampuni hiyo ilikuwa imekua kwa kiasi kikubwa. Huko Kenya, sasa ilikuwa kampuni ya pili katika kuzalisha vifaa vya ujenzi baada ya KIM International. Anvinarah pia ilimiliki kundi la vyombo kadhaa vya habari nchini Kenya na Tanzania kwa mwavuli wa Alinarah Media Network ama kwa kifupi AMEN Group.
Wanafamilia ya Kimaro, haswa, walikuwa wakimtazama Alvin kwa macho ya kutokuamini. "Nini? Wewe ndiye mwanzilishi wa Kampuni ya Alvinarah?" Mzee Kimaro alikasirika.
"Alvin, unawaza nini?" Lea aliona ni vigumu kuamini pia. "Wewe ulikuwa mwenyekiti wa KIM International lakini ulikuwa unajenga kampuni ya Alvinarah kwa siri pia? Unawezaje kusaliti familia ya Kimaro?!"
"Mwanaharamu wewe, kosa langu kubwa maishani ni kukuruhusu uchukue KIM International!" Mzee Kimaro alitamani angeweza kushusha nyundo kwenye kichwa cha mjukuu wake muda huo.
“Baba usiwe na wazimu. Sio jambo kubwa. Kampuni ndogo kama Alvinarah haiwezi kushindana na biashara ya familia yetu,” Valeria alisema kwa huzuni.
"Hiyo ni sawa. Kimaro Cement ndio chapa bora zaidi ya simenti Afrika Mashariki. Kampuni ya Alvinarah ni takataka ukilinganisha na sisi,” Queenie aliunga mkono huku akitabasamu.
Vipengele vya wasiwasi kwenye uso wa Mzee Kimaro hatimaye vilipungua kidogo. “Alvin, wewe si sehemu ya familia ya Kimaro kuanzia leo. KIM International itafanya kila kitu kuifilisi Alvinarah. Jack, nakuamuru uiharibu kampuni ya Alvinarah katika muda wa miezi mitatu na itoweke kabisa Kenya.”
"Babu, nitafanya." Jack alijaribu kuzuia wasiwasi wake.
Alvin alitabasamu baada ya kuona sura zao zikitapatapa. “Jack, hujawaambia kuwa timu ya uhandisi ya Simon Mbugui iliyokuwa KIM International imejiuzulu? Sawa, nilisahau kutaja kwamba Timu ya Simon tayari imejiunga na Alvinarah. Tunafanya mkutano wa kimataifa ili kutangaza kutolewa kwa brand mpya ya Oceanic Cement saa 11:00 asubuhi Ijumaa ijayo.”
Kila mtu hakuamini masikio yake. KIM International ndiyo ilitakiwa kutangaza kuachiwa kwa brand mpya ya Oceanic Cement. Sasa iliangukiaje mikononi mwa Alvinarah?
Jack alicheka kwa kejeli. “Alvin, bado unaota? KIM International ilitumia miaka mitatu kufanya kazi na timu ya uhandisi ya Simon Mbugui kuvumbua Oceanic Cement. Kwanini Simon ajiunge Alvinarah na data zote muhimu? Kwa hakika ninaweza kurejesha umiliki wa uvumbuzi huo. Wakati huo huo, nitawashtaki pia Simon na Alvinarah kwa wizi wa hatimiliki.”
“Jack, wewe ni kituko sana, na sijui utawezaje kuiongoza KIM International kwa akili za matope kama hizi” Alvin alijibu huku akitabasamu, “Umewahi kusoma mkataba wa kazi wa Simon? Tangu mwanzo, hajawahi kusaini mkataba na KIM International bali alisaini na mimi binafsi. Mtaji wote uliowekezwa katika maendeleo ya mradi huo wa Oceanic Cement pia ulitoka kwangu peke yangu. Nyaraka zote za hakimiliki zimeandikwa kwa jina langu, si la kampuni. Kwa hali hiyo una haki gani kumshtaki Simon?”
Hakika chezea mtu mwingine lakini si mwanasheria, hasa mwanasheria mwenyewe akiwa ni msomi na mahiri kama Alvin. Jack aliufyata mkia, Alvin akazidi kutamba.
"Kinyume chake ..." Alvin alikaza macho yake. "Mimi na Simon tuna haki ya kurejesha umiliki wa bidhaa zote tulizozivumbua tukiwa na KIM International hapo awali. Jack, kaa tu na usubiri barua yangu ya kisheria.”
Rangi zote zilitoka kwenye uso wa kila mtu wa familia ya Kimaro waliposikia hivyo. Uso wa Jack ulikuwa umepauka kama karatasi huku Mzee Kimaro akitetemeka kwa hasira.
"Alvin, utalaaniwa kwa kifo kibaya!" Mzee Kimaro alimnyooshea mjukuu wake kwa kidole kinachotetemeka. "Familia ya Kimaro ilikulea miaka hii yote na hivi ndivyo unavyotulipa?"
“Alvin, huwezi kufanya hivyo. Uamuzi wako utatuharibia.” Moyo wa Bibi Kimaro ulikuwa kwenye maumivu makali sana.

“Babu, Bibi, nimewapa nafasi. Dakika chache zilizopita, niliuliza kuhusu maoni yenu lakini nyote mlinidhalilisha zaidi. Je, kuna mtu yeyote kutoka kwa familia ya Kimaro aliyenionyesha heshima yoyote?” Uso wa Alvin ulikuwa umetulia kama maji. Lisa pekee ndiye aliyejua jinsi mkono wake ulivyokuwa ukitetemeka. Mwanamume huyo hakukata tamaa tu bali alikasirika.
“Jack amechangia nini kwenye KIM International?” Alvin aliendelea. “Kampuni zingine zote chini ya KIM International hazijafanya vizuri katika miaka ya hivi karibuni. Ni mimi niliyeleta Kimaro Cement kwenye nafasi yake ya juu ili kuwa biashara yenye faida zaidi ya kampuni. Nilianzisha kampuni ya Alvinarah kama njia ya kupunguza ushindani wa nje. Ikiwa ningefanikiwa kurithi hisa kwa KIM International, bila shaka ningeunganisha makampuni yote mawili kuwa kampuni moja kubwa sana. Lakini, kwa kuwa familia imekata tamaa juu yangu, basi nitaendelea kuiongoza Alvinarah kama mpinazani wa KIM International.”
Hakujaribu kuficha dhamira na tamaa machoni pake. "Siwezi kamwe kujitolea kwa ajili ya wengine bila kupata manufaa yoyote."
"Kuiangusha KIM International? Unaweza kuendelea na ndoto yako nzuri!” Jack alimfokea kwa sauti kubwa.
“Tusubiri tuone basi. Lakini utawaelezaje washirika wakati huwezi kukabidhi mradi wa uzinduzi wa chapa mpya ya Cement kama ulivyoahidi?" Alvin alihoji kabla ya kuelekeza macho yake kwa Mkurugenzi Majuto na Bwana Thompson. “Na nyie mabosi, mmoja wenu ni mkandarasi wa barabara huku mwingine ni mkandarasi wa majengo. Ikiwa hamtoweza kupata Cement yenye teknolojia mpya na ya kipekee kama Oceanic Cement, ni suala la muda tu kabla hamjatupwa na kampuni zingine kwenye sekta yenu.”

TUKUTANE KURASA 216-220

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......216-220

Sura ya: 216

Mkurugenzi Majuto na Bwana Thompson walihisi magoti yao yakigongana walipokumbuka kwamba wote wawili walikuwa wamemfedhehesha Alvin hapo awali. Hakukuwa na maana ya wao kulia juu ya maziwa yaliyomwagika sasa.
“Bwana Mkubwa… Bwana Kimaro, nilikosea kwa kutoona mbali. Kwanini usivunje tu mkono wangu?” Mkurugenzi Majuto alikuwa kwenye hatihati ya kulia sasa. "Au labda ungependa kunipiga kofi usoni?"
Alvin alinyoosha mkono kulibana shavu lililokuwa na mafuta ya mwanaume huyo. "Ulionekana kuwa na kiburi hapo awali, huh? Ulisema mke wangu alikugusa?"
"Bwana kimaro, samahani sana." Mtu huyo alipiga magoti chini.
"Nenda kumsihi Jack badala yake. Angalia kama anaweza kutengeneza Cement ya teknolojia mpya ndani ya wiki moja ili kukusaidia. Hakuna mtu anayekwenda na wakati ambaye atataka jengo lake litengenezwe na simenti ya teknolojia ya zamani.” Alvin aligeuza midomo yake kwa tabasamu kabla ya kutembea akiwa ameshikana mkono na Lisa kuelekea mlangoni. Kwa wakati huo, hakuna mtu aliyethubutu kuwazuia. Hata Jerome na Melanie hawakutulia na walikuwa na wasiwasi.
Alipokaribia tu kuufikia mlango, ghafla aligeuka na kuutazama umati huo kwa ujeuri kabla ya kumwambia Jerome. "Bwana Campos, nitakumbuka kila wakati tukio hili ulilonipangia."
Midomo ya Jerome ilitetemeka. Matokeo yalikuwa nje ya matarajio yake.
“Mbali na hilo, hakuna mtu anayeruhusiwa kumdhalilisha mke wangu, Lisa Jones. Yeyote anayethubutu kusema kwamba yeye si mrembo ananiudhi waziwazi.” Kisha, akaweka mkono wake kiunoni mwa mkewe na kuondoka eneo hilo kwa madaha.
Melanie nusura apoteze akili alipotazama umbile la mwanamume huyo lililokuwa likipungua taratibu machoni mwake. Alikuwa amemchagua Jerome tu kwa sababu alifikiri Alvin asingepanda tena juu ya ngazi. Bila kutarajia, utukufu bado ulikuwa uking'aa sana kwa Alvin. Mbali na hilo, bila kuzuiliwa na KIM International, bila shaka angepanua himaya yake zaidi.
“Babu… Babu, kuna nini…” Mtu mmoja ghafla alipiga kelele nyuma. Sherehe ya uchumba iligeuka kuwa machafuko tu.
Mzee Kimaro alihisi moyo wake ukikaza kwa sababu ya hasira kali. Wanafamilia ya Kimaro mara moja walimpeleka mzee huyo kwenye chumba cha mapumziko.
"Jack, njoo hapa." Mzee Kimaro alimuashiria mjukuu wake mdogo.
“Babu…” Jack akasogea mbele, akihisi kukosa raha.
Mzee Kimaro alishika fimbo yake na kuitupa kwenye chumba kwenye mabega ya kijana huyo. "Kwanini hukutuambia kuhusu timu ya Simon kuacha kazi kwenye kampuni?"
“Baba tulia. Alvin hana lolote.” Mara Lea akasogea mbele kumkinga mwanae.
"Ulijua kuhusu hili kabla ya leo?" Mzee Kimaro alikohoa. "Ni wazi, Alvin amepanga hili kama mpango mbadala. Nisingekuwa na ugomvi naye kama ningejua mapema.”
“Baba, huoni? Alvin ana matamanio makubwa na anapanga kuchukua udhibiti kamili juu ya KIM International,” Valeria alisema kwa wasiwasi, “Anataka mamlaka uliyonayo mikononi mwako. Nini kitatupata ikiwa familia itakuwa chini ya udhibiti wake?”
Bibi Kimaro akadakia. "KIM International itafanya nini mara tu Alvinarah itakapofanya mkutano wa kuzindua simenti yao ya teknolojia mpya wiki ijayo? Jack, unaweza kupata timu nyingine ya kufanya kazi kwenye mradi wa Cement? Hata hivyo, Alvinarah labda atakuwa ametoa toleo la pili la Cement wakati tutakapofaulu.”
Jack alikunja mikono yake kuwa ngumi. Sura ya aibu ilitanda usoni mwake lakini hakuna neno lililotoka kinywani mwake.
Mzee Kimaro alitingisha kichwa chake katika hali ya kukata tamaa mbele yake. Alvin alidharauliwa, lakini aliweza kujua ni yupi kati ya wajukuu zake alikuwa na uwezo wa kweli.
Macho ya Valeria yalitiririka kwa uzuri. "Baba, tunaweza kumtaka Alvin kukabidhi data za mradi Cement au tutatangaza ugonjwa wake wa akili na kuonyesha jinsi ambavyo alijaribu kumuua mtu. Hakuna mtu ambaye angethubutu kushirikiana na mfanyabiashara mwenye ugonjwa wa akili.”
“Unawezaje kusema hivyo?” Bibi Kimaro alipaza sauti, "Yeye bado ni mpwa wako!"

"Mama, karibu aniharibu sura, umesahau? Hata mara moja hajanichukulia kama mam’dogo wake.” Alikoroma kabla ya kumgeukia dada yake. “Lea, una maoni gani kuhusu wazo langu? Kwa kuwa anamjali sana Lisa, tutamjulisha kuhusu ugonjwa wake na nina uhakika hatathubutu kuwa naye tena baada ya hapo.”
Hisia ngumu iliyotokea katika moyo wa Lea. Ingawa alikuwa amemtisha Alvin kuhusu hilo hapo awali, bado hakuwa tayari kuafiki. Aligeuka kutazama upande mwingine. "Alvin ni damu ya familia ya Kimaro, baada ya yote. Hatuwezi kuvuka mstari. Isitoshe, sote tunawajibika kwa ugonjwa wake.”
“Anataka kuangusha biashara ya familia tuliyoijenga kwa miaka mingi halafu bado mnamkingia kifua?—” Valerie alipiga kelele, akionekana kukasirika.
“Nyamaza!” Mzee Kimaro hatimaye akaruka kwa hasira. “Wazo gani la kijinga kama hilo? Rudini ofisini mara moja mkajadiliane kupata suluhu.” Mzee Kimaro alishusha pumzi ndefu baada ya wengine kuondoka.
Bibi Kimaro akammiminia glasi ya maji. "Kweli, katika umri huu, unaweza pia kuachia nguvu zote? Kusema kweli, hakuna hata mmoja wa wajukuu zetu aliye na uwezo zaidi kuliko Alvin. Haifai kupoteza cheo chetu kama familia tajiri zaidi kwa hili.”
"Inanikera sana kwamba kijana huyo ni muasi sasa." Mzee Kimaro akapiga kifua chake kizito. “Lakini hana huruma, hilo ni la uhakika. Hakuna mtu mwingine katika familia anayeweza kulinganishwa naye. Lea ana uwezo lakini yeye si kitu ukilinganisha na Alvin.”
"Anapaswa kuwa mkatili ili kudumisha nafasi yake katika familia tajiri zaidi nchini.” Bibi Kimaro alimkumbusha.
•••
Sehemu ya maegesho ya hoteli.
Baada ya kuingia ndani ya gari, Lisa alishindwa kujizuia kumuangalia Alvin aliyekuwa amekaa karibu yake huku akifunga mkanda wa usalama. Kiti cha dereva cha hali ya juu kilifunika umbo lake dhabiti. Ilibidi akubali kwamba mwanamume huyo alikuwa anavutia sana, hasa jinsi alivyozungumza kwenye sherehe ya uchumba mapema… Ilipendeza sana!
Aliuona uso huu kila siku lakini uzuri wake usio na kifani bado ulimfanya moyo wake kwenda mbio.
“Niangalie unavyotaka. Hakuna ubaya kuthamini sura nzuri ya mumeo. Sitasema lolote.” Alvin akageuka pembeni na kumshika macho yake ya wizi kwa mara nyingine tena.
Lisa akatabasamu kwa aibu. “Sikuwa nakutazama. Nilikuwa nikinyoosha shingo yangu tu. Inahisi kuwa ngumu zaidi." Alichungulia dirishani baada ya kusema hivyo.
Alvin alikibana kiganja chake kwa kukichezea huku kicheko cha furaha kikitoka kinywani mwake. "Au ulirogwa na haiba ya mumeo sasa hivi?"
“Si kweli, ila umemchanganya kila mtu…” Kabla sauti yake haijakatika, alimshika kidevu na kufunga kinywa chake kwa midomo yake.
Lisa akapepesa macho. Alitaka kumsukumia Alvin pembeni lakini alipokumbuka namna alivyomkosha kwenye sherehe hiyo hakika nguvu zilimuishia. Lisa hakuweza kujizuia katika hilo. Hakutaka kujisalimisha, lakini hakuweza kumshinda tena na tena. Ilibidi akubali kwamba Alvin angeweza kumshinda mwanamke yoyote kwa urahisi kwa sababu alikuwa na haiba yenye nguvu sana.
Gari jeusi la kifahari lilipita taratibu na kulipita gari la kina Lisa. Kelvin, ambaye alikuwa ameketi kwenye kiti cha nyuma, aliona watu wawili walioketi ndani. Dirisha la gari la kina Alvin lilikuwa nusu limevingirishwa chini. Alvin alikuwa ameegemea kiti cha abiria huku Lisa akiwa amezungusha mikono yake yote shingoni. Walionekana wamezama sana katika busu hilo kiasi kwamba hawakujua kilichokuwa kikiendelea karibu nao.
Kelvin alikunja ngumi pamoja. Nia ya hatari ikamjaa machoni. 'Lisa Jones, hivi ndivyo ulimaanisha uliposema huna chaguo ila kurudi kwa Alvin?' Kelvin hakuweza kuvumilia alipojiwazia hayo. Hakuwahi hata kupewa busu lolote na Lisa, achilia mbali busu la midomo kama jinsi alivyokuwa akifurahia tendo hilo la karibu na Alvin. Kwa kifupi, alihisi kudanganywa na Lisa. Hakukusudia kumwacha Alvin! Ikiwa ndivyo ilivyokuwa, kwa nini alimpa tumaini tangu mwanzo? Moyo wa Kelvin ulijaa chuki!
Taratibu akainua dirisha na kufumba macho, akamwambia dereva wake. “Twende zetu.”

Sura ya: 217

Hatimaye, Alvin akajiondoa kwenye midomo ya Lisa bila kupenda. Kwa aibu, aliinua macho yake na kushangaa kuona kwamba dirisha lilikuwa limefunguliwa nusu. “Nafikiri… nilisikia gari likipita mapema…”
Lisa alihisi kutaka kujiua sekunde hiyo hiyo. Inawezekana kuna mtu yeyote aliyewaona mapema?
“Hmm.” Macho ya Alvin yalimetameta kabla hajatoa tabasamu. "Hakuna kitu kibaya kuhusu mume na mke kubusiana." Aliuma mdomo. “Hii haina uhusiano wowote na kuolewa au la. Mimi sina aibu kama wewe,” alimwambia.
“Muda ule… Kwanini ulinishika mkono?” Alvin akamtazama kwa makini.
Aibu ilibadilisha hali ya kuchanganyikiwa usoni mwake sekunde chache baadaye.
“Sijui unamaanisha nini.” Lisa alitazama upande.
"Namaanisha wakati familia yangu ilipomuunga mkono Mkurugenzi Majuto kuvunja mkono wangu, kwanini ulishika mkono?" Akainama mbele kumcheki masikioni. "Ulijisikia vibaya juu yangu?"
'Sikuwa na wazo lolote. Acha kujifikiria sana.” Akiwa amechanganyikiwa, alibadili mada ya mazungumzo ghafla. "Bado utashirikiana na Mkurugenzi Majuto na wengine?"
“Hapana.”
"Lakini wanaongoza makampuni makubwa katika nchi hii..."
"Teknolojia ya hali ya juu inakua haraka kwa wakati huu. Biashara haiwezi kuendelea kwa kutegemea bidhaa zilizotengenezwa kwa teknolojia ya zamani,” Alvin alieleza kwa kumaanisha. “Nimejifunza kitu kutokana na tukio hili. Ninapanga kusaidia kampuni mpya kukua kwa kuwekeza kwao kama mmiliki wa hisa. Ni wakati wa makampuni ya kizamani ambayo yanayojiendesha kimazoea kwa kuchukua fursa ya mazingira yanayowazunguka kuachia ngazi.”
Lisa alielewa karibu mara moja. “Unataka kujenga himaya ya biashara ambayo ni yako peke yako, ambapo umesimama juu ya uongozi?”
“Unaweza kuiweka hivyo. Sitaki kuendelea kufanya biashara ili kumfurahisha mtu mwingine.” Macho yake yalidhihirisha dhamira huku sauti yake ikiakisi ubabe.
Lisa akavuta pumzi kwa kasi. Tamaa ya Alvin ilikuwa mbaya kuliko alivyofikiria. Ilionekana kana kwamba alikuwa anaenda kubadilisha jiji la Nairobi.
Hata hivyo… angeweza kweli kumudu mwanaume kama Alvin? Bila shaka, wanawake wengi zaidi wangekuwa wakijitupa mikononi mwake dakika ambayo angerudisha nafsi yake nyuma. Je, bado angeweza kulinda hadhi yake kama Bibi Kimaro katika siku zijazo?
•••
Siku mbili baadaye. Pambano kubwa lilikuwa likiendelea katika familia ya Ngosha.
“Joel, nitakufa kabla ya kunitaliki,” Nina alifoka kwa hasira.
“Acha kunitisha. Nitakutaliki hata ukifa.” Sauti ya Joel ilidhihirisha azimio lake lisiloyumbayumba. “Wewe ni msaliti. Ungewezaje kumshawishi Valeria aharibu sura ya Lisa? Bila kusahau jinsi ulivyomshawishi Mkurugenzi Majuto kumnyanyasa Lisa kwenye sherehe ya uchumba! Usifikiri kuwa sijui chochote.”
"Lazima ni Lisa amekujaza maneno ya uwongo tena, huh? Unaamini kila kitu anachosema kwa sababu tu ni binti wa Sheryl. Unamjali huyo mwanamke tu!” Nina aling’aka.
“Ni kweli, Sheryl ndiye mwanamke pekee ambaye nimempenda katika maisha yangu yote. Majuto yangu makubwa ni kuoa mwanamke mwenye roho mbaya kama wewe.” Joel alikuwa amechachamaa. "Una siku tatu za kusaini karatasi. Vinginevyo nitakwenda mahakamani kukata rufaa ya talaka.” Joel akasimama na kuondoka chumbani.
“Joel, mwana haramu wewe!” Nina alipiga magoti chini na kuanza kulia kwa sauti.
Simu ya Nina ilianza kuita muda si mrefu. Aliona jina la mpigaji na kupiga kelele kwenye simu, "Unataka nini sasa?"
"Joel Ngosha amezungumza na wakili kuhusu mgawanyo wa hisa zake. Lisa anapata 35% huku Melanie akipata 5%.”
"Nini?" Nina alikuwa karibu kupoteza akili. “Anamjali sana binti huyo wa nje ya ndoa halafu anataka kunitaliki mimi? Joel ni mkatili. Hakumbuki kama nilitumia miaka 20 iliyopita kujenga familia pamoja naye!”
"Kwa kweli ameamua wakati huu. Matokeo yatakuwa mabaya ikiwa makubaliano haya yatahalalishwa."
“Tufanyeje sasa?” Nina likuwa amechanganyikiwa kweli.
"Chaguo pekee tulilo nalo kwa sasa ni kumfanya Joel Ngosha afariki."
Hilo lilimshangaza Nina. “Itawezekanaje…”
"Fikiria kile alichokufanyia wewe na binti yako."
“Lakini…”
“Usijali, nitashughulikia hili. Unakumbuka jinsi Sheryl alivyokufa?"

“Sawa.” Macho ya Nina yalimtoka kwa hasira. "Hawezi kunilaumu kwa kuwa mkatili ikiwa yeye pia hana huruma."
“Sawa.”
•••
Asubuhi, Lisa alikuwa akienda kazini baada ya kifungua kinywa. Mara tu alipotoka nje ya mlango, alimwona Alvin akimfuata. Alvin alikuwa amevalia nguo zake za mapumziko na mikono yote miwili mfukoni mwake kama kawaida.
“Mbona bado unanifuata? Huendi kazini leo?” Lisa alimuuliza kwa mshangao.
Alvin akamjibu, “nitakupeleka ofisini kwako." Moyo wa Lisa ulirukaruka baada ya kusikia sauti yake ya chini iliyojaa mahaba.
Alvin aliongozana naye hadi kwenye gari na kumwendesha hadi katikati ya jiji kwenye jengo ambalo Mawezi Investments ilikuwa imepanga ofisi zake.
Lifti ya private iliyokuwa inaelekea kwenye ghorofa za juu ilikuwa chini ya uchunguzi wa usalama siku hiyo, kwa hivyo iliwabidi kutumia lifti ya umma.
Ulikuwa ni muda wa asubuhi na watu walikuwa na haraka sana kuwahi makazini, hivyo kulikuwa na harakati nyingi ndani ya lifti. Mabinti na vijana ndiyo walikuwa wengi. Lisa aligundua kuwa karibu kila binti aliyeingia kwenye lifti angeibia macho kumtazama Alvin aliyesimama karibu naye. Baadhi ya wale wenye ujasiri hata waliegemea kwa Alvin kwa hila wakati watu walipobanana kwenye nafasi ndogo ya lifti.
"Mke, mikono yangu ni ya baridi." Ghafla Alvin alimkumbatia Lisa kwa nyuma na kuweka mikono yake mbele ya kifua chake. Mwonekano huo wa kimapenzi usoni mwake uliwafanya wanawake wengine wote kuyeyuka kwa wivu.
Hata hivyo, walishangaa wakati huo huo. Ilikuwa ngumu kuamini jinsi mwanamke aliyeharibika sura anavyoweza kuwa na mwanamume mwenye sura nzuri kama huyo.
Hatimaye wapendanao hao waliiacha lifti ilipofika ghorofa waliyokuwa wakienda. Waliwaacha mabinti ndani ya lifti kwenye mjadala mkali baada ya kupiga hatua chache, baadhi ya maneno yao waliweza kuyanasa kwa mbali kabla lifti haijaondoka.
“Unamfahamu huyu mkaka? Jamani huyu kaka anajua kupenda nyie acheni! Alikodisha kipindi kizima cha TV ili tu kumtetea mke wake. Nilisikia kwamba ni tajiri mkubwa Nairobi nzima. Na hata mke wake usimuone hivyo, ni bosy lady na pesa zake za kutosha…”
Uso wa Alvin ukaanguka papo hapo. Kwa upande mwingine, Lisa alicheka bila hiari. "Mvulana wangu mzuri, unaweza kurudi nyumbani sasa. Jisikie huru tu.”
Hasira iliyokuwa ndani yake ilimwacha baada ya kuona tabasamu lile la furaha. Midomo yake ikaachia tabasamu. "Msichana wangu sukari, nipe busu na nitarudi nyumbani." Kisha, akainua midomo yake maridadi.
Lisa aliona haiaminiki kushuhudia haya. Ni nini kilimtokea Alvin yule mwenye kiburi na jeuri?
Alvin aliondoka na Lisa akaingia ofisini kuendelea na kazi. Aliporudi nyumbani baada ya kazi, alikutana na suprise nyingine kutoka kwa Alvin
“Mpenzi wangu sukari, nina zawadi kwa ajili yako.” Alvin akazungusha kichwa chake na kuashiria kulia.
Lisa alitazama upande ule na kugundua gari jeupe ‘sports car’ jipya kabisa limeegeshwa pembeni. Ilikuwa na muundo mzuri wa nje.
Hakuwahi kuona aina hiyo ya gari huko Kenya hapo awali lakini alikuwa ameona kitu kama hicho alipokuwa akisoma nje ya nchi. Kulingana na utafiti wake, gari la bei rahisi zaidi kutoka kwa brand hiyo lingegharimu angalau shilingi za Kitanzania milioni 250. Mbali na hilo, plate namba ya gari hilo ilikuwa ‘4EVA.’ Yaani ‘Daima na Milele.’
Lisa aliona aibu lakini alifurahi kwa siri kuona sahani ya gari aliyotengenezewa na Alvin. Hakuwa amewahi kufikiria kuwa Alvin alikuwa mwanamume romantiki kiasi hicho hapo awali, lakini kwa hakika alikuwa na mbinu kadhaa ambazo tayari zilikuwa zikiubomoa kabisa moyo wa Lisa na kumfanya awe nyang’anyang’a kwake!

Sura ya: 218

"Vipi, unaipenda?" Alvin alitabasamu kwa upole kabla ya kuinamisha kichwa chake upande mmoja kutazama majibu ya Lisa.
“Kwa nini umeninunulia gari ghafla wakati nina magari mengi tu?” Alijaribu kila awezalo kujiondoa katika mshtuko wake.
“Hayo magari hayana kile ninachokitaka kwa mke wangu. Nataka uwe na kilicho bora zaidi." Alibonyeza kitufe cha ufunguo na milango ikatanda kama mbawa za mwewe, ikionyesha mambo ya ndani ya kifahari na ya kuvutia.
“Naipenda. Asante." Lisa alitikisa kichwa kwa dhati. Huenda angeikataa zawadi hiyo hapo awali, lakini, kwa vile alikuwa mke wake sasa, aliona inafaa.
“Umeipenda kweli?” Alvin aliinua macho yake kumwangalia, akionekana kutoridhika. "Unataka nini kingine?"
Mwonekano huo wa uso wake ulimfanya Lisa aone haya mara moja. “Nitake nini tena? Mimi ni mke wako, hivyo kilicho chako ni changu.”
“Hiyo ni sawa. Hata mwili wangu ni wako.” Akasogea karibu na kumkandamiza mlangoni. Baada ya busu refu na la mapenzi, alijiondoa kwa kusita. “Mtoto mzuri, unazidi kuwa mrembo kila kukicha.”
“Asante mume. Niache nikapumzike sasa.” Hakuweza kumudu tena mahaba ya Alvin, mtu yule aliyekuwa na kiburi hapo awali ambaye muda huo alikuwa romantiki kupita kiasi. Hiyo ilimpa hisia fulani za usalama. Alvin hakujali sura yake mbaya; bado alimjali kama hapo awali.
•••
Kesho yake Lisa aliendesha gari lake jipya barabarani asubuhi na mapema akielekea kazini.
Gari hillo la kifahari lililokuwa na plate namba ya kipekee lilivutia macho mengi kutoka kwa wapita njia. Alikuwa amekwama kwenye njia panda akisubiri taa ya kijani imruhusu kupita wakati Pamela alipomrushia video fulani kutoka whatsapp ikiwa na maelezo yafuatayo:
[Lisa, nimeona video hii kwenye group la whatsapp ikanivutia sana. Limelipenda sana hili gari.]
[Kwa hiyo?] Lisa aliuliza kwa mshangao. hakuwa ameelewa point ya Pamela.
[Nasikia ndiyo mara ya kwanza kuonekana nchi nzima. Wadau mtandaoni wanasema gari hilo lina thamani ya takriban dola laki mbili na ni toleo maalum. Hata hivyo, plate namba yake imenikosha sana, 4EVA, ina maana ya milele, Inamaanisha mengi zaidi ya kusema tu nakupenda.]
[Kwa hiyo una maanisha nini?] Lisa alizidi kumzingua Pamela ambaye alionekana hajui kama gari hilo ni lake.
[Namaanisha mwambie Alvin akununulie pia. Yeye ni tajiri na atamudu. Ningekuwa na bwana tajiri kwa kweli nisingemwelewa hadi aninunulie kitu kama hicho.]
[Pole wee! Ina maana hujui?... Hiyo gari ni mali yangu.] Lisa alimwambia ukweli.
[Nini?] Pamela alikuwa haamini bado.
[Alvin alinizawadia jana. Nimeanza kuliendesha nusu saa tu iliyopita, sasa nashangaa imesambaaje haraka hivyo mtandaoni?] Lisa hakujua kuwa wakati anatoka tu nyumbani kuna mtu alichukua video ya gari hilo na kuiposti kwenye group la whatsapp.
Kulikuwa na ukimya wa muda mfupi upande wa pili wa whatsapp kabla ya Pamela kuanza kulalamika, [[emoji21]Unataka kuwafanya watu wasioolewa kama mimi tuwe na wivu? Alvin alikuwa mtu jeuri asiyejua jinsi ya kuonyesha mapenzi. Tangu lini amekuwa romantiki hivi?]
[Sijui.[emoji1787][emoji1787][emoji1787]] Lisa aliweka emoji za kucheka kwa furaha. [Tafuta mwanaume kama yeye ikiwa una wivu. Ni muda mrefu umepita tangu uhamie Nairobi. Bado hakuna mtu anayekumezea mate?[emoji12]]
[[emoji2086][emoji2086]Sihitaji uhusiano kwa sasa…]
[Huhitaji uhusiano kwa sababu bado haujamuacha Patrick?] Lisa akashusha pumzi.
[Usitaje jina lake. Inanifanya niwe mgonjwa.]
[Sawa, basi. Endelea kuwa na wivu juu ya gari langu la 4EVA.]
[Kipi cha ajabu kuhusu hilo? Nitamwomba kaka yangu aninunulie pia.[emoji849][emoji849][emoji849]] Pamela akakata simu.
Lisa akatikisa kichwa, akitabasamu. Alipata pongezi nyingine tena baada ya kufika ofisini.
Harvey Ngugi, msaidizi wake, aliingia na tabasamu. “Mwenyekiti Jones, unaonekana mzuri sana siku hizi na baraka tele zinazidi kukumiminikia. Kila mtu hapa Nairobi anajua jinsi Bwana Kimaro anavyokudekeza kama mtoto mdogo. Sawa, huu ni mwaliko wa chakula cha jioni cha biashara kutoka kwa kampuni ya Holt... Na huu ni mwaliko kutoka kwa mwanadada wa Heaven Fashions kwa hafla ya onyesho la mitindo ya mavazi yake…”
Lisa hakuwa na la kusema alipotazama rundo nene la mialiko.

"Kampuni ya Alvinarah inakaribia kuzindua brand ya Cement yao mpya, kwa hivyo kila biashara inajaribu kujenga mahusiano mazuri na Alvin Kimaro. Kwa hiyo watu wanajaribu kunitumia mimi waweze kujenga uhusiano na mume wangu. wafanyabiashara ni wajanja sana. Ilikuwa vigumu sana kupata hata mwaliko mmoja kama huu hapo awali.” Alitabasamu kwa kejeli. "Kwa kweli, kujipendekeza kunamaanisha kila kitu huku Nairobi."
“Ni kwa sababu Bwana Alvin Kimaro ana uwezo. Mwenyekiti Jones, una bahati sana naye." Harvey alidokeza.
Lisa alikosa la kusema. “Peleka mialiko hii kwa wajumbe wengine wa bodi. Wanaweza kushiriki kwa niaba yangu.”
“Hakuna tatizo bosi, ikiwezekana na mimi nipatie moja wapo.” Harvey alijipigia debe wakati akiondoka.
Baada ya Harvey kuonndoka, Lisa alipokea simu kutoka kwa namba isiyojulikana. “Lisa, muda umepita. Nimefika Nairobi. Tunaweza kuonana kwa chakula cha mchana?" Sauti ya Patrick ilisikika kupitia kwenye spika.
•••
Lisa alikutana na Patrick kwa mara nyingine tena. Ni wazi kwamba mwanamume huyo hakuonekana yuko sawa wakati huo. Alionekana amekonda sana kuliko mara ya mwisho walipokutana. Alionekana kuchoka kimwili na kiakili, kama mtu aliyepoteza matumaini kabisa.
"Muda mrefu ... sijaona." Mshtuko ulimtoka Patrick baada ya kuona sura ya Lisa.
“Unaweza kuokoa wakati kwa kuzungumza ulichoniitia hapa na kuacha kushangaa sura yangu,” Lisa alisema kwa uthabiti.
"Ok, samahani. Najua hali yako ni tofauti sasa. Kila mtu anajua kuwa mwenyekiti wa Mawenzi Inventments ni mke wa Bwana Alvin Kimaro. Inaonekana kwamba siku zote nilikudharau zamani.” Sauti ya Patrick ilidhihirisha ishara ya majuto.
Lisa bado alimuona kama anatapatapa tu. “Nenda kwenye point.”
“Nataka kujua Pamela yuko wapi. Amebadilisha namba yake ya simu,” alieleza kwa unyonge, “sijaweza kuwasiliana naye tangu aondoke Tanzania.”
“Muda wote huo?” Lisa alicheka kwa kejeli. "Pamela amebadilisha namba zake zote za simu na whatsapp hata akaacha kuwasiliana na marafiki zake wa zamani baada ya kuhamia Nairobi. Lakini namba yangu ya whatsapp ni ileile. Ungeweza kunipigia simu wakati wowote lakini hukunipigia. Miezi mitatu ameondoka mpaka leo hujamtafuta, kweli?”
Lisa alitoa kicheko kingine cha dhihaka, akasema, “Ulikuwa ukimdharau na kumfanyia unavyotaka, ulifikiri kwamba Pamela hawezi kukuacha kamwe? Ulifikiri angeanza yeye kukutafuta lakini baada ya kukaa kimya kwa miezi michache, sasa tu ndipo unapogundua kuwa anaweza kuwa serious, sivyo?” Patrick aliaibishwa na madongo ya moja kwa moja.
"Lisa, nimekuwa na Pamela kwa miaka michache tayari na tulizungumza juu ya kufunga ndoa mwaka huu. Huu sio mzaha. Tulicho nacho kati yetu ni cha kweli.” Patrick alijitetea.
"Samahani, lakini sidhani." Lisa aliruka kwa hasira. “Unakimbilia kwa Linda kila anapokuhitaji. Ulifanya hivyo siku ambayo ulitakiwa kukutana na wazazi wa Pamela kwa mara ya kwanza na nadhani ungefanya hivyo tena siku ya uchumba wako au hata siku ya harusi yako. Pamela naye ni mtu, ana moyo na anaumia. Lakini wewe hukumjali hata kidogo.”
“Lisa nisikilize kidogo…”
Patrick hakupewa hata sekunde ya kujitetea. “Pamela yuko sawa, unastahili kuwa na Linda kwani nyinyi wawili mnaendana zaidi. Acha kujaribu kuharibu maisha ya Pamela tena.”
“Kwa kweli mimi ninamwona Linda kama dada yangu tu…” Patrick alipata nafasi ya kuongea.
“Samahani kwa kusema ukweli, lakini hakuna mtu anayeweza kumvumilia mwanamume ambaye kila mara anamtanguliza dada yake asiyehusiana naye kwa damu badala ya mpenzi au mke wake.” Lisa alisimama baada ya kusema hivyo. “Ulikuwa unasema ninaharibu uhusiano wako na Pamela kwa makusudi. Uko sawa, sitakuacha umdhuru tena na hakika sitakuambia aliko.”

Sura ya: 219

“Lisa, usivuke mipaka. Hii ni kati yangu na Pamela.” Patrick alikasirika sasa. "Usifikiri kwamba unaweza kufanya kiburi kwa sababu wewe sasa ni mke wa Alvin Kimaro."
"Hivyo ndivyo unavyowaona marafiki wa Pamela… Hujawahi kumheshimu na hakika humstahili." Lisa alichukua mkoba wake na kuondoka baada ya kusema hivyo.
“Nitakaa Nairobi na sitaondoka hadi nionane na Pamela." Sauti ya Patrick ya hasira ilisikika nyuma yake lakini aliziba sikio lake kusikia maneno yake.
Akiwa ofisini, Alvin alimpigia simu Lisa ghafla. "Nimesikia ulienda kwenye mgahawa na mwanaume mwingine, kwanini hukunijulisha?"
"Pfff!" Lisa alitema kahawa kinywani mwake akiwa amekasirika. "Ni Shani ndiye aliyekuwambia?"
“Si yeye.” Alvin alikanusha. “Wewe ni mke wangu, na cheo hicho kinakufanya karibu kuwa mtu maarufu. Mapaparazi wanakutazama kila mahali lakini nilifanikiwa kudhibiti kabla picha hazijavuja.” Alvin alisikika akigonga vidole vyake kwenye meza iliyokuwa upande wa pili wa simu. “Unamfahamu vipi? Hata miguu yangu inaonekana bora kuliko uso wake mbaya."
Lisa akajibu kwa hasira kidogo. “Ni mpenzi wa zamani wa Pamela. Anataka kujua alipo Pamela lakini sikumwambia chochote.”
"Mhm, usitoke tena na wanaume wasiojulikana, watakupotezea heshima." Alvin alimuonya.
“Si upo bize na uzinduzi wa Cement ijumaa? Hakika unaonekana kama una muda mwingi wa bure mkononi." Lisa alichanganyikiwa baada ya kusikia sauti yake ya kibabe.
"Ninafanya kazi lakini pia nahitaji kumtazama mke wangu kwa ukaribu zaidi," Alvin alijibu kwa uthabiti, "Wanaume wengi hapa mjini wanavutiwa na wanawake walioolewa siku hizi."
“Unawaza mambo kupita kiasi. Hakuna mtu atakayevutiwa na sura yangu ya kutisha."
“Sijui unamaanisha nini. Wewe ni mrembo kabisa machoni pangu.”
Lisa hakuweza kuvumilia maneno hayo ya huba ambayo hakuyatarajia, na moyo wake ulidunda bila mpangilio. "Kwa nini umekuwa ukiniambia maneno mengi ya asali hivi karibuni?"
“Nitayafanya masikio yako yasikie maneno matamu zaidi nikipata kula nyama ya nguruwe iliyochomwa utakayotengeneza.” Kicheko cha upole cha Alvin kilisikika kuvutia zaidi ya muziki kutoka kwa kinanda.
Maneno hayo ya mahaba yaliuosha na kuusafisha kabisa moyo wa Lisa. “Sawa, lakini unamjua mwanamume yeyote mzuri unayeweza kumpendekeza kwa Pamela? Anahitaji uhusiano mpya ili kusahau kuhusu mpenzi wake wa zamani...”
“Hapana…” Alvin alijibu baada ya kutafakari kwa ufupi. "Rodney ni mkali, Chester si mwaminifu, na tabia ya Sam haina shaka."
“Kwa hiyo wewe huna marafiki wazuri?” Lisa alijiwazia. Hata hivyo, ilimbidi akubaliane na maoni yake kuhusu Rodney na Chester. Wasingemfaa Pamela. "Nafikiri Sam Harrison si mbaya," alisema, "Yeye ni mwadilifu, mpole, mcheshi, mwonekano mzuri..."
"Sikujua kuwa unamfikiria sana." Alvin alitabasamu kiwivu-wivu. “Vipi kuhusu mimi?”
"Tunazungumza juu yako tukiwa chumbani ..." Lisa alifunika kiganja chake kwenye uso wake kwa aibu.
"Niambie sasa hivi." Sauti ya Alvin ilisisitiza maamuzi.
Lisa alifikiri juu ya hilo kwa uzito kwa muda mfupi na kusema. “Um, wewe ni handsome, genius… una moyo mzuri… tajiri… unafaa…”
Lisa hakuweza kufikiria kitu kingine chochote. Kwa upande mwingine, angeweza kuandika orodha ndefu ikiwa Alvin angemuuliza kuhusu sifa zake mbaya.
“Hata wageni wangeweza kusema mambo hayo. Unaweza kusema kitu kingine cha kipekee?" Alvin aicheka kwa mbwembwe. “Lisa, hatimaye najua ni uwongo kiasi gani ulioniambia ulipokuwa unajaribu kunitongoza huko Dar es Salaam. Hakika nimekatishwa tamaa na wewe. Hujawahi kunijali jinsi ninaivyokujali.” Alikata simu ghafla baada ya hapo.
Baada ya kutoka kazini, Lisa aliendesha gari lake kuelekea kwenye duka la nyama na kununua nyama ya nguruwe. Alifungua redio wakati akiendesha gari.

Kipande cha habari kilichomvutia kilisikika baada ya dakika kama kumi hivi nbaada ya kuwasha redio. “Tunakuletea habari zilizotufikia hivi punde. Mkurugenzi wa Ngosha Corporation, Joel Ngosha, amepata ajali baada ya gari lake kugongana na lori nusu saa iliyopita. Dereva huyo alifariki dunia eneo la tukio huku Joel Ngosha akipelekwa hospitali kwa matibabu ya dharura, lakini hali yake bado haijafahamika. Kulingana na baadhi ya habari kutoka eneo la tukio, hali ilikuwa yake ilikuwa ya kutatanisha sana…”
Maneno yaliyokuja baadaye yalipenya masikioni mwa Lisa kwa ukungu. Alikuwa katika mshtuko. Ingawa muda aliokaa na Joel ulikuwa mfupi, bado alikuwa familia yake pekee iliyobaki. Alikuwa amepata ajali? Aligeuza gari kwa haraka na kukimbilia hospitali.
Korido ya chumba cha dharura ilikuwa imejaa watu wa familia ya Ngosha.
Nina, ambaye alikuwa akipiga kelele, alipomwona Lisa, alimshtaki kwa hasira na kumpiga. “Wewe ni jini! Joel almepata ajali mara tu ulipokuja kwenye familia yetu. Yote ni kwa sababu ya mikosi yako."
Lisa aliupiga mkono wake kwa hasira. Alimkaripia kwa macho yaliyojaa damu, “Baba yangu yuko ndani, na bado haijulikani ikiwa ataishi au atakufa. Badala ya kuwa na wasiwasi juu ya mumeo, wewe, kama mke wake, unapandisha hasira yako juu yangu kwa makusudi. Unawazimu?"
“Nani kasema nakutolea hasira zangu? Bila shaka ni kosa lako.” Nina alilegea kwa sekunde moja chini ya macho makali ya Lisa. “Ni kweli, nina wasiwasi na Joel. Nina wasiwasi naye kuliko mtu mwingine yeyote.”
“Basi ushikilie hasira yako. Kila mtu ana wakati mgumu, kwa hivyo acha ugomvi. Hatimaye nilimpata baba yangu na tuliungana tena kwa muda mfupi tu. Sitaki kumpoteza.”
Lisa alijaa maombi na uchungu. Jinsi alivyomtazama Nina ni kana kwamba alikuwa mtu asiye na akili, na hilo lilimfanya Nina kuwa na hasira.
“Unamaanisha nini kusema hivyo? Ilikuwa ni wewe—”
“Inatosha, funga mdomo wako.” Bibi Ngosha aliingiwa na majonzi, lakini baada ya kusikia maneno ya uchungu ya Lisa, alifikiri pia tabia ya Nina haikubaliki. “Lisa yuko sawa. Joel bado anapambania maisha yke huko ndani. Huwezi kuwa mtulivu?”
Nina aliona aibu kwa kuambiwa hivyo. Alifunika tu uso wake kwa mikono yake na kuanza kupiga kelele kwenye korido.
Saa moja baadaye. Daktari alitoka nje na kusema kwa masikitiko, “Samahani. Tumefanikiwa kuokoa maisha ya Bwana Ngosha kwa sasa, lakini kuna uwezekano mkubwa atashindwa kuamka.”
Nina alikuwa na wasiwasi. "Unamaanisha kuwa atakuwa katika hali ya kupooza?"
“Ndiyo.” Daktari aliitikia kwa kichwa. "Lakini bado kuna matumaini. Wagonjwa wengine huamka hata baada ya kukaa kitandani kwa miaka michache au zaidi ya miaka kumi.”
“Loo, maskini Joel wangu!” Bibi Ngosha alilia kwa huzuni. “Hii imetokeaje? Mbona alikuwa sawa tu, Alipataje ajali?”
“Bibi, usiwe na huzuni. Ninaamini Baba hakika ataamka.” Melanie naye alilia. Ijapokuwa Joel alikuwa na upendeleo kwa Lisa siku za karibuni, angalau huko nyuma alimjali sana.
“Usilie mwanangu, nitafanya kila liwezekanalo ili baba yako aamke.” Nina alilia huku akifikicha macho yake. “Mama, baba, msijali. Nitamtunza Joel vizuri.”
Mzee Ngosha aliitikia kwa huzuni. Alipokuwa karibu kuzungumza, Lisa alisema kwa sauti ya chini, “Babu, ningependa kumtunza Baba mimi mwenyewe. Kwanza, muda niliokaa na Baba ulikuwa mfupi sana. Ninataka kutimiza wajibu wangu kama binti yake. Haijalishi hata kama upo katika hali ya kupooza. Angalau naweza kuutazama uso wake zaidi.”
“Asante mjukuu wangu…” Bibi Ngosha aliguswa.
“Pili, Alvin ana uhusiano wa karibu na Dokta Choka. Ujuzi wa matibabu wa Dokta Choka ni wa kipekee. Hospitali kuu za binafsi nchini Kenya zinamilikiwa zaidi na Dokta Choka pia. Hata kama Dokta hawezi kuwa na msaada wowote, Alvin ana uhusiano mpana, kwa hivyo labda anaweza kupata madaktari mashuhuri kutoka ng'ambo…”

Sura ya: 220

“Hapana,” Nina. akasema, “Joel ni mume wangu. Ninawezaje kukuacha umtunze? Nikizungumza kuhusu madaktari mashuhuri, ninawafahamu wengi pia.”
“Hiyo ni kweli,” Melanie alitikisa kichwa na kusema kwa chuki, “Hata kama mtu mwingine angelazimika kumtunza Baba, angekuwa mimi. Hutaweza kuwa na nafasi. Usisahau kwamba hata hujaorodheshwa kwenye daftari la ukoo wa Ngosha.”
"Ikilinganishwa na familia ya Choka, unafikiri unawajua madaktari bingwa zaidi kuliko wao?" Lisa aliuliza.
Nina alikosa la kusema kwa muda lakini akasisitiza na kusema, “Hata hivyo, sitawahi kukupa haki za kumtunza Joel. Sikuweza kushindana dhidi ya mama yako hapo awali. Sasa Joel amepoteza fahamu, usiniambie kwamba siwezi hata kushindana na binti wa Sheryl.” Akiwa na huzuni, alianza kulia tena.
Maneno ya Lisa yalikuwa yamewagusa wote wawili Mzee Ngosha na Bibi Ngosha, waliona wazi kuwa haikuwa haki kwa Nina kumtunza mumewe.
Lisa alimpuuza Nina na kumkazia macho tu Mzee Ngosha. "Babu, unajua vizuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote kwamba Baba amekuwa akisisitiza kuhusu talaka na Nina hivi karibuni. Sasa, kwa kuwa sasa Baba amepata ajali, atawezaje kumhudumia kwa upendo? Kwa hivyo, ugawaji wa mali ya baba yangu utaenda kwa mwanaye na wazazi wake.”
Mzee Ngosha alishikwa na butwaa. Hapohapo Nina alijitupa kwa Lisa na kumsukuma kwa hasira. “Unajaribu kumaanisha nini? Unataka kusema kwamba nimepanga kumuua Joel? Lisa, wewe ni mwanamke katili, lakini usiwafikirie wengine kuwa katili kama wewe. Nampenda Joel. Ninampenda kuliko mtu mwingine yeyote.”
“Sikusema umepanga kumuua baba. Nawakumbusha tu Babu na Bibi nini kitatokea ikiwa baba hataamka.” Sauti yake ilikuwa kali. “Bila shaka, sina shaka kwamba una nia potofu. Nafikiri ni afadhali kuwa macho kwani familia tajiri si kama familia za kawaida.”
Bibi Ngosha aliamini. “Sawa, nimekubali kukuacha umtunze Joel.”
“Mama, unaamini maneno yake kwamba nitamuumiza Joel?” Nina alilia kwa mfadhaiko, “Ikiwa watu wa nje wangesikia haya, wangefikiriaje?”
"Anti, ninafanya hivi kwa faida yako mwenyewe." Lisa alikuwa na uso wa dhati. “Kwa kuwa baba yangu amepata ajali, kampuni ya Ngosha lazima iingie kwenye hali mbaya sasa. Je, wewe na Melanie hamhitaji kuendesha kampuni? Mtawezaje mambo ya kampuni huku mkimhudumia baba? Kwa kawaida, Melanie anajua tu jinsi ya kujipamba na kwenda kufanya shopping. Ni wakati wa kuanza kuchukua majukumu sasa. Unapaswa kumsaidia kama wewe ni mama yake."
Melanie alishangazwa na maneno yake. Nina alifungua kinywa chake ili kujibu, lakini Damien, mdogo wake na Joel, ambaye muda wote alikuwa ameketi kimya kwenye kiti cha magurudumu, alisema hivi ghafula, “Lisa aliyosema ni maneno ya busara. Kama mke, unapaswa kuchunguza chanzo cha ajali ya gari pia."
",..sawa." Nina alimkazia macho Lisa. “Lazima umtunze Joel ipasavyo. Ikiwa chochote kitampata, sitakuacha salama.”
Lisa alitabasamu kwa uchungu. "Bila shaka nitafanya. Hakuna faida kwangu ikiwa baba ataaga dunia. Ikiwa nahitaji uwepo kwake, siwezi kumuona kama akifa. Hata kama ninahitaji utajiri wake, sitapata hata senti moja ikiwa atakufa. Ikilinganishwa na mimi, Melanie ana bahati zaidi ikiwa baba atakufa…”
Alisikika kama mtu asiyejali, lakini Mzee Ngosha na Bibi Ngosha walikuwa na akili za haraka. Mara moja walielewa ni nani angepata manufaa zaidi ikiwa Joel angekufa. Kwa kawaida, ingekuwa ni Nina na binti yake. Kila kitu kilikuwa sawa wakati wote, lakini ajali ya gari ilitokea ghafla. Hilo liliwafanya wawe na mashaka.
“Baba, mtendaji mkuu wa kampuni alipiga simu na kusema kwamba waandishi wengi wanakusanyika mbele ya jengo la kampuni. Hali si shwari sasa,” Damien alisema.
“Ndugu yako atakuwa amepoteza fahamu kwa muda mrefu. Utasimamia kampuni kwa muda sasa. Kuhusu Melanie, anahitaji kwenda kwa kampuni mara moja pia. Unapaswa kumsaidia vyema.”
Damien alitabasamu kwa huzuni. "Lakini mimi si mzuri katika kushughulikia masuala ya kampuni..."
"Lazima uifanye hata kama huwezi." Mzee Ngosha alikuwa na sura ya ukali. "Familia ya Ngosha haiwezi kuanguka."
“Sawa, nitafanya niwezavyo.” Damien aliitikia kwa kichwa.

Baada ya kumkalisha Joel, Mzee Ngosha na wengine walitoka wodini. Walikutana na Alvin ambaye alikuwa akija kwa kukimbia.
“Bwana Mkubwa Kimaro…” Akifikiria maendeleo ya baadaye ya Alvin, Mzee Ngosha alipanda haraka na kumpa mikono.
“Habari babu Ngosha. Nilisikia kuhusu hali ya Baba kutoka kwa Chester. Hakika nitatafuta daktari bora zaidi kwa matibabu yake.” Sauti ya Alvin ilibeba heshima ambayo mdogo anapaswa kuwa nayo kwa mkuu wake. Mtazamo wake ulikuwa tofauti kabisa na pale alipoongozana na Melanie kwenye karamu ya siku ya kuzaliwa ya Mzee Ngosha.
"Asante." Mzee Ngosha alimkazia macho Lisa. Ilionekana wazi kuwa Alvin alimjali sana huyu mjukuu wake.
Ilionekana kwamba wangetakiwa kumjali sana Lisa na kumtendea vizuri zaidi katika siku zijazo. Kwani akina Ngosha walipoteza tegemeo baada ya Joel kupata ajali. Bado walilazimika kuwategemea waume wa wajukuu zao.
Mzee Ngosha alifikiria kwa muda kisha akamgeukia Lisa na kusema, “Usiwe na huzuni kupita kiasi. Bado wewe ni mchanga na unapaswa kuendelea kutembea kwenye njia yako. Unaweza kufika nyumbani mara kwa mara ili kututembelea. Ukitaka kuingia Ngosha Corporation, tuambie wakati wowote.”
Lisa alishangaa, lakini alielewa haraka. Watu wa familia ya Ngosha walikuwa wapuuzi kwelikweli waliojua kujipendekeza haswa.
“Babu, unawezaje kukubali kumruhusu Lisa aingie kwenye Kampuni ya Ngosha?” Melanie alipiga kelele. Hakuweza kukubali hata kidogo.
“Inatosha. Lisa bado ni dada yako, na anaweza kukusaidia katika siku zijazo pia.” Mzee Ngosha aliondoka na Bibi Ngosha baada ya kumaliza kuzungumza.
Melanie alikanyaga miguu yake kwa kutoridhika. Aligeuka na kumwangalia Lisa, lakini sura ya Alvin yenye mvuto mkali ilikutana na macho yake badala yake. Moyo wake ulipiga bila mpangilio. “Bwana Kimaro…”
Alvin hakumtazama hata kidogo. Akasogea na kuizungusha mikono yake kiunoni mwa Lisa, akimfariji kwa upole. “Usiwe na huzuni. Uko nami kuanzia siku zote.”
Melanie alikuwa anakaribia kuwa wazimu kutokana na wivu alipotazama tukio hilo. Alvin hakuwahi kumfanyia mahaba kama hayo hapo awali. Japokuwa Jerome alijitahidi kumwonyesha mapenzi, bado alikosa hekima ukilinganisha na Alvin. Isitoshe, Jerome hakuwa na umbo zuri kama Alvin pia.
Melanie aliuma mdomo wake kwa chuki na kusema, “Usijidai sana Lisa. Babu alifanya hivyo tu kwa heshima ya Bwana Mkubwa Kimaro. Kama sivyo, huwezi kuwa sehemu ya familia ya Ngosha.”
Lisa alishindwa kabisa kuyaelewa mawazo ya Melanie. “Melanie, nimevutiwa sana na wewe. Baba amepoteza fahamu sasa, lakini wewe, kama binti yake, bado unapata wivu juu ya mambo kama hayo.”
“Hiyo haikuhusu” Melanie alidhihaki, "Ngoja nikuambie. Kuna mtu ambaye Bwana Kimaro anamthamini. Huyo ni mtu ambaye huwezi kamwe—”
“Melanie Ngosha.” Alvin alimkatisha kwa nguvu huku macho yake yakionyesha onyo kali. "Ukithubutu kusema neno lingine, nitakufanya ujute kuwa na ulimi."
“Bwana Mkubwa Kimaro, Melanie yuko katika hali mbaya. Anaongea ujinga tu.” Nina alihisi kwamba Alvin alikuwa amekasirika, hivyo mara moja akamshika Melanie na kuondoka zao.
“Alvin Kimaro, hata kama huniruhusu nizungumze, kila mtu katika familia tajiri jijini Nairobi anajua. Lisa atajua mapema au baadaye…” Sauti isiyo na kikomo ya Melanie ilisafiri kwenye korido kutoka mbali.
Wodi ilikuwa kimya isipokuwa sauti ya mashine ya electrocardiograph.
Alvin alimtazama mwanamke aliyekuwa pembeni yake kwa woga. Hata hivyo alimuona tu Lisa akiwa ametulia akichota maji ya moto ili kumfuta Joel usoni. Ni kana kwamba maneno ambayo Melanie alisema haykuyasikia kabisa.
“Babe, kuhusu yale Melanie alisema, usi…”

TUKUTANE KURASA 221-225

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI...............LISA
KURASA..........221-225

Sura ya: 221

“Usijali, sitafikiria sana. Siko katika hali ya kufikiria kitu kingine chochote isipokuwa baba yangu sasa,” Lisa alimkatisha tamaa.
Alvin hakujua kwamba Lisa alikuwa anajua tangu muda mrefu kuhusu kuwepo kwa Sarah maishani mwake. Pia alielewa kwamba Sara alikuwa amechongwa sana moyoni mwake. Hiyo ndiyo sababu asingeweza kujisikia vibaya. Alikuwa kaishazoea tayari. Hakukuwa na sababu ya kumfanya ajisikie kuchukizwa na jambo hilo pia. Wafu hawawezi kupigana na walio hai hata hivyo.
“Sawa, ni vizuri basi.” Pamoja na kusema hivyo, bado moyo wa Alvin ulizidi kudunda pasipo kujua.
Alihofia kwamba Lisa angeelewa vibaya au kufikiria mambo kupita kiasi. Hata hivyo, alijisikia vibaya kumuona akionyesha kupuuza kabisa jambo hilo. Baada ya yote, alihisi kwamba sababu ya Lisa kupuuzia jambo hilo inaweza kuwa ni kwa sababu hakumpenda vya kutosha. Akamkazia macho. Kero ndani ya moyo wake ilikuwa ikimrudia tena. Akatoka na kwenda kuvuta sigara mbili nje.
Alirudi nusu saa baadaye. Lisa alikuwa akimnywesha maji Joel aliposikia mlango unafunguliwa. Alimtazama kisha akakwepa macho yake.
Alvin alihisi kutokuwa na raha moyoni mwake. Alitoka wodini kwa muda mrefu, lakini hata aliporudi Lisa hakuuliza kwanini alikuwa ametoka. Ina maana aliamua kumpuuza kabisa? Hata hivyo, alipotazama hali ya Joel, alihisi kwamba moyo wa Lisa haukuwa na nafasi ya kufikiria juu ya upuuzi huo.
Alvin alikohoa kidogo na kusema, “Nilimjulisha Chester sasa hivi na kumwomba aandae muuguzi bora wa kumtunza baba yako. Pia atawasiliana na madktari bingwa wa ng'ambo ili kujadili hali ya baba…”
“Asante,” Lisa alisema kwa dhati.
“Hakuna haja ya wewe kunishukuru. Wewe ni mke wangu. Ninafanya sehemu ya wajibu wangu tu.” Alvin hakuridhika na tabia yake ya kuwa na adabu kupitiliza. "Halafu pia, ulipigania kumtunza baba yako kwa sababu ulishuku Nina anahusika na ajali yake?"
“Ndiyo, ninashuku huenda aligundua kuwa baba yangu alitaka kunihamishia asilimia 35 ya hisa. Mwanamke mwenye ubinafsi kama Nina, na Farres nyuma yake, angeweza kufanya chochote kulinda faida zake.”
“Kweli.” Alvin aliitikia kwa kichwa. "Tayari nimeweka mtu wa kuchunguza chanzo cha ajali."
Lisa alizama kwa muda katika mawazo yake. "Lakini ... Kuna mtu mwingine ambaye ananipa hisia isiyo ya kawaida."
"Nani?"
“Damien.” Lisa alitamka waziwazi na kuendelea. “Nilipoomba kumtunza baba yangu hapo awali, Nina aliendelea kugoma na kufanya fujo. Lakini Damien alipomshawishi, Nina alikubali ghafla. Pia nadhani aliendelea kubadilisha mada ili kumsaidia Nina, iwe kwa makusudi au la. Mara ya kwanza nilipoenda nyumbani kwa akina Ngosha, aliongoza mada ili kunilenga mimi na kila alichoongea Nina alisapoti na yeye akasapoti kile Nina alisema. Ingawa yeye ni mtu wa maneno machache, nadhani yeye sio mtu rahisi kama anavyoonekana.”
Baada ya Lisa kumaliza kuongea, aligundua kuwa Alvin alikuwa akimwangalia kwa kina. "Nini? Kuna kitu usoni mwangu?" Lisa alijishtukia na kujigusa usoni.
"Hapana, nadhani hisia za mwanamke wangu zinazidi kuwa kali." Alvin alibana uso wake mdogo. "Kama nilivyotarajia kwa mwanamke ambaye nimempenda."
Lisa alikosa la kusema. Hakuwa katika hali ya kubebishana naye muda huo.
“Sawa, sikuweza kujizuia kukusifu.” Alvin aliutoa mkono wake kwa unyonge na kuweka uso ulionyooka. “Nisingeona kama usingetaja. Damien huyu hakuwa wa kuvutia macho hata kidogo. Nilisikia kwamba ana ulemavu wa kuzaliwa. Alikuwa mlemavu wakati wa kuzaliwa, hivyo kila mtu katika familia ya Ngosha ni mzuri kwake. Hata baada ya kukua, bado anaishi chini ya ulinzi wa baba yako na familia ya Ngosha. Bado hajaoa.”
“Kwanini? Una maanisha hawezi kufanya ngono?” Maneno ya Lisa yalikuwa ya kushangaza.
Alvin alitafakari maneno yake kwa muda. Kisha, akasema kwa ukali, “Tumia tafsida basi. Unafikiri inafaa wewe kama mke wa mtu kuzungumzia mambo kama hayo moja kwa moja?”
“Nina hamu ya kutaka kujua. Inawezekanaje kwa mwanamume kuhimili tamaa za mwili tangu ujana hadi uzee bila kuoa?”

Alvin aliinua uso wake na kumtupia Lisa jicho lisiloeleweka. “Bila shaka, inawezekana. Siku zote nilikuwa peke yangu kabla ya kukutana na wewe, miaka karibu mitano nimeweza kuvumilia.”
“Kwa mwanamume si rahisi, lazima ulikuwa unapoza sehemu!” Lisa alikataa kuamini.
“Mimi—” Alvin alitaka kuongea lakini Lisa akamkatisha haraka.
“Sijasema kwamba haiwezekani, inawezekana lakini inategemeana.” Lisa aliendelea kusema. “Ikiwa mwanamume hataki kuoa, ni aidha hana uwezo wa kufanya ngono, au ana mtu moyoni mwake. Nadhani Damien anaweza kuwa anampenda Nina.”
Alvin alibisha, “…Hapana.”
“Huniamini?” Lisa alikunja uso. "Silika ya mwanamke ni sahihi sana. Nilisoma vitabu vya kisaikolojia hapo awali na kuligundua hilo. Kwa wale ambao wamekuwa walemavu tangu kuzaliwa, baadhi yao wana fikra chanya na wenye furaha, huku baadhi yao wakiwa na fikra potofu na waliojikatia tamaa.”
"Haijalishi, hii ni dhana yako tu. Lazima kuwe na ushahidi.” Alvin alisema. “Lakini mtu aliyemuumiza baba yako lazima aogope kwamba atarudiwa na fahamu. Mtu huyo anaweza hata kuja kummalizia mwenyewe…”
“Nafikiri hivyo pia.” Lisa aliunga mkono hoja. “Sasa tutasubiri. Maadam atajitokeza, ni hapo tu ndipo tunaweza kumshika injinia wa ajali hii.”
Lisa alibadilishana macho na Alvin na akaelewa mara moja. Kama alivyotarajia kwa mwanamke wake. Hapo awali alihofia kwamba Lisa asingeweza kukabiliana na utata na mikimikiki ya jiji la Nairobi. Alikuwa akifanya maendeleo haraka kuliko vile alivyofikiria.
Siku iliyofuata, kama vile anga lilivyoangaza, Hans alileta matokeo ya uchunguzi. “Hakuna tatizo kwa dereva wa lori lililohusika katika ajali hiyo. Sedan ya Mkurugenzi Ngosha ndiyo ilishindwa kujizuia na kuligonga lori hilo kwa mbele. Polisi walimfanyia uchunguzi dereva wa Mkurugenzi Ngosha na kubaini kuwa tumbo lake lilikuwa na kiasi kikubwa cha dawa za kulevya.”
"Dereva alipoteza udhibiti wa gari kutokana na kutumia dawa za kulevya?" Lisa alishangaa.
"Hii inapaswa kuwa sababu kuu ya ajali hiyo. Hata hivyo, kwa mujibu wa wataalamu waliomchunguza, dereva huyo hakuwa ametumia dawa za kulevya tangu azaliwe, hivyo huenda alizitumia kimakosa. Lakini dereva amekufa, hivyo hakuna anayejua alikuwa akiwasiliana na nani alipokuwa hai na ni nani aliyempa dawa hizo. Watu waliokufa hawaongei.” Hans aliweka kituo kifupi na kumalizia, “Farres pia alichunguzwa, na inaonekana hana uhusiano wowote na kesi hii."
Lisa alikata tamaa kidogo, lakini alitarajia kwamba kwa vile kuna wahalifu waliothubutu kumuumiza Joel, wangekuwa wamejitayarisha vya kutosha.
“Tufanye taratibu. Mradi tu tukifuatilia kwa karibu, mtu huyo hakika atafahamika.” Alvin alimtuliza.
Lisa aliitikia kwa kichwa. Alijua hakukuwa na faida ya kuwa na papara.
"Mume, kampuni yako inafanya mkutano na waandishi wa habari kesho kutwa. Kila kitu kiko tayari?" Lisa alimkumbusha Alvin ghafla.
"Tunahitaji kujiandaa na nini?" Alvin alimshangaa.
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda. "Kwanini unaniuliza hivi? Mimi sijui chochote kuhusu makampuni ya saruji. Kila mtu nchini Kenya kaandaa macho yake kwenye mkutano huo na waandishi wa habari kesho kutwa.”
“Usijali. Nahitaji tu kula nyama choma ya nguruwe iliyotengenezwa na mke wangu na sitakuwa na shida kabisa.” Alvin alijieleza kwa utulivu, lakini macho yake yalijawa na matarajio.
Lisa alinyamaza. Alihisi Alvin lazima ali’miss sana nyama ya nguruwe choma. Hans, ambaye alikuwa amesimama pembeni, alishindwa kujizuia na kuangua kicheko.
“Unacheka nini? Toka nje.” Alvin alimfurusha bila huruma.
“Mbona unakuwa mkali sana kwake?” Lisa aliutazama mgongo wa Hans kwa huruma wakati anaondoka. Hans ni mtu pekee ambaye alikuwa na uwezo mkubwa wa kustahimili hasira za Alvin.
“Yeye si mke wangu hata hivyo. Unasema kwamba ni lazima niwe mpole kwake?” Alvin alimshika mkono. "Nina uwezo wa kuwa mpole kwako tu."
Lisa aliishiwa na akili kwa muda, lakini alipata fahamu haraka. Tayari alikuwa amefunikwa na majeraha, na moyoni mwa Alvin alibaki kuwa mtu asiyeweza kufutika.

"Ninajaribu kuwa na wewe kimapenzi, lakini kila nikikuweka karibu unarukaruka tu kwanini?" Akiwa amehuzunika, Alvin alimvuta kwenye kumbatio lake na kumng’ata mdomoni kana kwamba ni adhabu. “Unanipenda au hunipendi?”

Sura ya: 222

Lisa alishangaa sana. Maongezi yao yaliruka kutoka mada moja hadi nyingine haraka sana. Kama ingekuwa kipindi wako Dar es Salaam, Lisa angejibu kwamba anampenda bila kusita. Hata hivyo, kwa muda huo hakuwa na uhakika na hisia zake…
Kusita-sita kwake kuliufanya moyo wa Alvin kuzama. "Je! ni ngumu sana kwako kujibu swali hili?"
"Hubby, unapaswa kwenda kazini sasa." Lisa alimsukuma na kuanza kuondoka. Alvin alitazama jinsi anavyoondoka na macho yake yakawa na huzuni.
•••
Baada ya kufika kwenye kampuni, Alvin alifungua kompyuta na kuuliza kwenye Google swali hili kwa hasira:
[Kwanini mwanamke hamuonei wivu mume wake?]
Jibu 1: [Mwanamke huyu anajitegemea kihisia. Anajiamini na anajizuia kujionyesha hata kama anampenda sana mumewe.]
Jibu 2: [Mwanamke huyu ana moyo dhabiti. Ana imani thabiti na mume wake na ana uelewa kamili kwake.]
Jibu 3: [Hampendi vya kutosha.]
Cha kushangaza, jibu la tatu ndilo lililomkaa zaidi kichwani Alvin. Kwa hasira akaitupa huko laptop yake na kukivunjavunja kikombe cha kahawa alichokuwa amekishika palepale.
Hans aliyesikia mshindo huo akaingia na kumtazama kwa wasiwasi. Ni yeye pekee ndiye aliyeshuhudia jinsi hasira za Alvin zilivyozidi kuwa mbaya siku hadi siku. Hakuweza kuelewa. Alvin alikuwa akipendana na Lisa, lakini nini kilikuwa kikimkasirisha papo hapo? Hans alikuwa na wasiwasi. Ugonjwa wa Alvin ulionekana kuzidi kuwa mbaya zaidi.
Kwa upande mwingine, Lisa akiwa hospitali, alipokea simu kutoka kwa Pamela “Otea niko wapi?”
"Siwezi kuotea." Sauti ya Lisa haikuwa na furaha hata kidogo.
“Sawa. Nimefika nje ya ofisi za kampuni yako. Nilihisi utakuwa katika hali mbaya tangu baba yako alipopata ajali. Kama rafiki yako, nilinunua chakula kitamu na kukuletea hapa kukupa pole.” Pamela alicheka. “Siamini kwamba Alvin yuko makini kivile na kukumbuka kukuletea chakula. Hmph.”
Lisa alipigwa na butwaa kwa muda kisha akasema kwa haraka, “Usiingie ofisini. Geuka, ingia ndani ya gari na uondoke."
“Lisa, unamaanisha nini?” Pamela alishangaa kufuatia jibu la Lisa. “Nimepoteza muda wangu kuendesha gari kutoka mbali ili kuja kukufariji. Nilikwama hata kwenye msongamano wa magari kwa muda wa saa moja, na hivi ndivyo unavyonijibu?…”
Pamela alipokuwa akipandwa na hasira, mara aliona umbo la mtu aliyemfahamu likijongea kwake kwa hatua ndefu. Macho yake yakawa yamemtoka! Mtu huyo katika kumbukumbu zake ambaye alijaribu sana kumsahau ghafla alionekana mbele ya macho yake. Alihisi kukosa pumzi. Ni kana kwamba kuna kitu kilimlipuka ndani ya kichwa chake. Alikuwa na wasiwasi, fadhaa, na katika hali ya mfadhaiko.
“Pamela…” Patrick akaenda moja kwa moja mbele yake.
Pamela alikuwa bado katika hali ya mshangao. Baada ya kutengana na Patrick kwa miezi zaidi ya mitatu, hakutarajia kumuona mapema au baadaye, achilia mbali ndani ya jiji la Nairobi.
Pamela alikuwa kapendeza kiasi chake japo si sana. Alikuwa na nywele zilizojipinda zenye rangi ya asali zilizolegea. Alikuwa amevalia suruali ya jeans brand ya ‘cardigan’ nyekundu chini ya fulana ndefu nyeupe na jozi ya viatu vya ‘Dk. Martens’. Alikuwa amejipodoa kidogo lakini alivutia.
Hapo awali, Pamela angekonda kidogo kila walipotengana baada ya kuachana na Patrick. Lakini, kwa wakati huo alionekana kung'aa na kunawiri kana kwamba alikuwa amezaliwa upya. Kwa mara ya kwanza, Patrick alikuwa na hisia kwamba asingeweza kumpata tena.
Pamela aliduwaa mpaka akasahau kwamba simu ya Lisa ilikuwa hewani. “Sawa, inaonekana umeshakutana na Patrick.” Upande wa pili wa simu, Lisa alicheka kwa uchungu. “Alikuja na kunitafuta jana. Hebu kaeni chini mzungumzie tofauti zenu.”
",..sawa." Pamela akatulia taratibu. Aliinua kichwa na kumtazama mpenzi wake wa zamani.
“Pamela, kwanini hukuniambia kuwa unakuja Nairobi kufanya kazi?” Patrick alitabasamu kwa uchungu. “Ulizuia simu zangu zote na jumbe zangu za WhatsApp. Bado una hasira tu hata baada ya kunichunia kwa muda mrefu hivyo?”
“Kukuchunia?” Moyo wa Pamela ukaduwaa. Baada ya muda wote huo, bado alifikiri kwamba alikuwa akimpenda tu kama kawaida na kwamba yote yangepita mradi tu ambembeleze?

“Sawa, ninakubali kwamba nilikuwa na makosa wakati huo. Nimetafakari makosa yangu, naomba unisamehe. Tukirudi Dar, nitakutana na wazazi wako nyumbani kwenu ili kuwaomba msamaha. Tunaweza kufunga ndoa mara moja.” Patrick alimshika mkono.

Patrick alikiri kwamba hakuwahi kumthamini ipasavyo siku za nyuma na alimchukulia kawaida sana, akifikiri kwamba angebaki karibu naye siku zote. Kwa hivyo, aliishia kumpuuza sana. Aliapa asingefanya hivyo tena.
"Sitarudi nyuma." Pamela alibaki na msimamo wake. "Ninafanya kazi katika kampuni ya vipodozi ya Osher kwa sasa, na maendeleo yangu ya baadaye ya kazi ni mazuri hapa. Nilishasahau kero zako zote ulizokuwa ukinifanyia."
Patrick alishikwa na butwaa. "Kwa hiyo, kazi yako ya awali huko Dar es Salaam haikuenda vizuri?"
"Patrick Jackson, nilikaa Dar es Salaam kwa ajili yako tu, hata nikaghairi karibu mara tatu kuja kufanya kazi Nairobi nikisubiri ahadi yako ya kunioa. Lakini ulifanya nini? Uliniabisha mimi na wazazi wangu na kaka yangu pia kwa kutuweka mgahawani tukikusubiri masaa mawili, hukutokea wala kutoa taarifa, matokeo yake ukakimbilia kwa Linda. Nimeelewa kila kitu sasa. Bado mimi ni binti mdogo na mrembo, kwa hivyo ninataka kutembea na kujionea mengi ya ulimwengu huu. Sitaki kuolewa tena kwa sasa. Kwanini niingie kwenye kaburi la ndoa mapema hii?”
“Acha kujipoteza akili.” Patrick alimwambia kwa dharau. “Si wewe uliyekuwa ukililia kuolewa nami zamani?—”
Pamela akamkatisha. “Ilikuwa zamani, kwa hiyo ulidhani zamani ingebaki milele hata kama hukuithamini? Sitaki sasa. Patrick, nilishakuambia wazi kabisa tulipoachana mwaka jana. Tumemalizana. Sifanyi mzaha, usije kunitafuta tena.” Aligeuka ili kuondoka.
Patrick alipigwa na butwaa. Alimfuata na kumshika mkono. “Pamela, siamini. Tumekuwa pamoja kwa muda mrefu sana na tuliachana na kurudiana mara nyingi. Unawezaje kusema tu kwamba tumemalizana kirahisi rahisi hivi? Ninaapa, simpendi kabisa Linda—
“Basi unaweza kuniahidi kutowasiliana naye milele zaidi ya kwenda kwenye mazishi yake atakapokufa? Kama upo tayari mpigie simu sasa hivi na umwambie. Ninakupa nafasi ya mwisho.” Pamela alimkazia macho.
Patrick alikuwa haamini. “Tusiende mbali kiasi hicho. Kwa uchache zaidi, ninakuahidi kupunguza mahusiano yangu na Linda. Pia nitamwambia atafute mpenzi haraka iwezekanavyo—”
“Inatosha. Unasemaga hivi kila mara. Sitaki tena kusikiliza upuuzi wako.” Pamela alikasirika sana. "Kwanini unilazimishe?"
Patrick aliendelea kumshika na kukataa kumuachia. “Pamela, inatosha sasa. Unajua nimeacha kazi ngapi katika kampuni yangu kwa siku hizi mbili ili kukusubiri nje ya ofisi za Lisa?"
“Nyamaza kama hujui kuongea.” Pamela alikasirika baada ya kusikia maneno yake ya kijinga. “Unanibembeleza au unaniamrisha?”
“Hukuwa hivi hapo awali. Unapumbazwa na Lisa, huh? Kwanini huwa unamsikiliza? Alikuja Nairobi na wewe ukamfuata. Mwenzio sasa ameolewa, utaendelea kumfuata milele?” Patrick alifoka kwa jazba.
Pamela nusura afe kutokana na hasira. Ikiwa wasingekuwa hadharani, angevua viatu vyake na kumpiga navyo.
Kwa bahati mbaya au nzuri, Rodney alikuwa akitshuka kutoka ghorofani alipokwenda kwenye ofisi za Mawenzi kumtafuta Lisa akiwa na nia ya kumpendekezea vipodozi kadhaa kwa ajili ya uso wake ambavyo vilitengenezwa mahususi na kampuni yake. Alishangaa kumuona Pamela akibishana na mwanamume hadharani.
Tangu alipofokeana naye kwenye wodi ya Lisa kule hospitali, Rodney alikuwa na fikra kwamba Pamela hakuwa msichana aliyetulia. Sasa, hata alikuwa akirumbana na mwanamume mwingine hadharani, na ni wazi kwamba mwanamume huyo alikuwa mpenzi wake.
Alipokumbuka jinsi alivyomdhalilisha hapo awali, alipata hamu ya kulipiza kisasi. Alitaka kumharibia kabisa Pamela kwa mpenzi wake huyo. Alitabasamu kwa dharau na kuwasogelea kwa hatua ndefu. "Hey, babe, ni nani huyo?"

Sura ya: 223

Pamela akiwa katikati ya hasira yake alishtuka aliposikia sauti ya mwanaume aliyemfahamu. Aligeuka nyuma na kumwona Rodney, yule kijana wa kujionyesha, akimsogelea huku akimuwashia tabasamu la upendo.
“Babe, ni jana tu ulisema unanipenda mimi peke yangu, na leo nakufumania na jamaa mwingine. Unacheza na moyo wangu eti eeh?" Maneno ya utata ya Rodney yalikaribia kumfanya Pamela alowe na jasho mwili mzima.
“Huyu ni nani? Una uhusiano gani naye?" Uso mzuri wa Patrick ulitiwa giza baada ya kumuona yule jamaa ambaye alitokea ghafla.
Ikiwa Rodney asingekuwa bora kuliko Patrick katika kila nyanja, Pamela angehisi kufedheheshwa kidogo. Hata hivyo, Rodney alikuwa mzuri, mtanashati na mwenye mwonekano wa kitajiri zaidi kuliko Patrick. Mwili wake wote ulitoa haiba isiyozuilika, ya kutisha na kuvutia kwa wakati mmoja. Hakika hakuwa mtu wa kawaida.
Pamela akalegeza macho yake ghafla na kuachia tabasamu kana kwamba moyo wake umefunguka kwa Rodney. Alikutanisha kiganja chake cha mkono wa kulia na kiganja cha mkono wa kushoto wa Rodney na kusema, “Nilisahau kukuambia. Tayari nina mpenzi mpya, anaitwa Rodney.”
Mwili wa Rodney ukasisimka ghafla. Kwanini hali ilikuwa tofauti na alivyotarajia? Kwa hiyo walikuwa wameshaachana? Yeye alienda tu kuwachokoza ili waachane, lakini kwa kutokujua kumbe alikuwa akimsaidia Pamela badala yake.
“Haiwezekani.” Uso wa Patrick ulikunjamana kwa kutokuamini na kumpungia mkono Pamela. “Unatumia njia hii kunizuga? Pamela, nakubali kwamba unajua kuigiza. Twende nyumbani.”
“Unataka nikwambie mara ngapi kuwa sikutaki? Tulishaachana zamani.” Pamela aligeuza uso kwa Rodney kumuonyesha Patrick. “Angalia jinsi alivyo mzuri. Anaonekana kama Tony Montana wa kutoka kwenye muvi ya Scarface. Ana uwezo wa kutimiza ndoto yangu kwani ana sura nzuri, umbo maridadi, pesa na ushawishi. Patrick, ulimwengu wangu ulikuwa wewe tu hapo awali, kwa hivyo sikugundua mtu mwingine yeyote. Lakini baada ya kuja Nairobi, niligundua kuwa kuna watu wengine bora kuliko wewe. Hufai tena kuishi kwenye moyo wangu.”
Rodney hakujua kilichokuwa kikiendelea. Alivamia vita isiyomhusu na yeye akaishia kuwa mateka, mateka wa huba!
Ghafla akakumbuka kejeli zote ambazo Pamela alimtupia kule hospitali. Nii nani aliyesema kule hospitali kwamba alikuwa kipande cha takataka? Ni nani aliyesema kuwa yeye ni mrembo tu? Ni nani aliyesema kuwa hafanani na mwanaume?
“Unadhani kusema hivyo kutanifanya nikuamini?” Patrick akatikisa kichwa kwa huzuni. Hakutaka kuamini hata kidogo. “Bado una hasira na mimi na Linda. Unataka tu kunitia wivu…”
“Sisemi uwongo. Nampenda sana. Ngoja nikuthibitishie kama huniamini.” Bila neno lingine, Pamela aliikamata shingo ya Rodney na kuishusha chini. Kisha kukutanisha vichwa vyao, akapenyeza ulimi wake kwenye mdomo wa Rodney na kumpiga denda kwa nguvu.
Kadiri Rodney asiyejua lolote alivyozidi kupinga, ndivyo Pamela alivyozidi kumwongezea manjonjo. Alijisahau hata akanogewa kabisa. Rodney alibusuwa kwa lazima na mwanamke kwa mara ya kwanza katika maisha yake yote. Alitaka kumsukuma, lakini Pamela alimkandamiza kisogoni na kusema kwa sauti ambayo ni wao wawili tu ndio walikuwa wakisikia, “Si ulikataa kuwa wewe si mwanamke? Sasa ni wakati wa kuthibitisha hilo.”

Hiyo ilimaanisha kwamba asingeweza kujithibitisha kuwa mwanamume ikiwa angemsukuma Pamela. Rodney alikiri kwamba alikuwa amechanganyikiwa. Rodney alimkumbatia mgongoni na kurudisha busu lake kwa nguvu.
Patrick aliweza kuwatazama wawili hao akiwa hoi. Macho yake yalikuwa mekundu kutokana na mshtuko. Je, huo ulikuwa ni 'upendo' ambao alikuwa ameungama kwake siku za nyuma?
Alimtongoza kwa muda mrefu, lakini alipotaka sana kumtendea mema, alichagua kumuumiza hivyo.
“Pamela, nimekatishwa tamaa kabisa na wewe. Sitakutafuta tena.” Patrick alishindwa kuendelea kutazama tamthilia ile ya mahaba, akaondoka zake kwa hasira na kwa jazba.

Hakuona muda huohuo alipogeuka, tone la chozi lilidondoka kwenye jicho la Pamela. Matone ya machozi yakatua kwenye midomo ya Pamela na Rodney na Rodney akaonja kitu cha chumvi. Alipigwa na butwaa kwa muda, muda uliofuata akajikuta anasukumwa na Pamela.
Yule mwanamke aliyembusu hapo awali alikuwa akijifuta uso na mdomo kwa nguvu kana kwamba alikuwa ameramba kitu kichafu.
“Pamela Masanja…” Rodney alikasirika sana.
"Je, unahitaji tishu?" Pamela alichukua kipande cha tishu na kumpa. Macho yake mazito bado yalikuwa yakimeta kwa machozi, kama paka asiye na hatia.
Rodney alichukua kipande cha tishu kwa hasira na kuufuta mdomo wake kwa nguvu. “Mhh! Nahisi kichefuchefu hadi natamani kutapika!” Rodney akatema mate mfululizo.
“Nahisi hivyohivyo pia.” Pamela aliitikia kwa kichwa huku akifanya hivyohivyo. "Kumbusu mtu ambaye simpendi ni kinyaa sana."
Rodney alihisi kwamba kejeli yake ilikuwa ikipuuzwa, na moyo wake ulikuwa karibu na maumivu kutokana na hasira. “Unalia nini? Unajilazimisha kumuacha jamaa wakati bado unampenda, lhuku kwa ndani inakuuma. Je, huoni kwamba wewe ni mnafiki?”
“Hakika huna rafiki wa kike,” Pamela alicheka ghafla, “hukuwa na ujuzi katika busu hilo sasa hivi. Inawezekana kuwa busu lako la kwanza, sivyo?
“Bullsh*t...Ujuzi upi katika kujilazimisha kumbusu mwanamke nisiyempenda?” Rodney alikuwa na aibu sana kwamba Pamela alikuwa amemgundua ukweli. Hakuweza kujizuia kutema maneno machafu.
"Inaonekana nimepatia eeh?" Kuangalia sura yake ambayo ilikuwa karibu kulipuka kutokana na hasira, Pamela alipunguza jazba na kuongea kwa utulivu. “Si unajua kuwa wanawake wanapenda kujishaua? Wanaume wanaodharau mashauzi ya wanawake hawatapata wapenzi kamwe. Jifunze kitu.”
Rodney aliuma meno. "Pamela, nilikusaidia sasa hivi, kwa hiyo hivi ndivyo unavyonilipa fadhili zangu?”
“Nilikuomba unisaidie?” Pamela alimshushua. “Si ni wewe ndiye uliyekimbia hapa kwa hiari na kuniita 'babe'. Umesema hata mambo ya kutuchonganisha? Usifikiri kuwa nilikuwa sijui nia yako.” Pamela alicheka na kuondoka zake. Rodney alitoa sauti kubwa ya kusonya na kuondoka akionekana kuchukizwa.
Pamela akamuona Lisa ambaye alikuwa anakuja kwake. Lisa alisimama baada ya kumuona Rodney aliyekuwa nyuma ya Pamela. “Nyinyi wawili…” Lisa alikosa la kusema. Alipikicha macho yake kuona kama yalikuwa na ukungu uliomzuia kuona vizuri. Kwanini Rodney alionekana kuwa mpole sana wakati huo?
“Kwanini yuko hapa? Mmegombana tena? Patrick yuko wapi?” Maswali dabodabo yalimtoka Lisa.
"Patrick ameondoka. Tumeachana rasmi safari hii. Alisema hatanitafuta tena.” Pamela alitazama juu na kutabasamu, lakini macho yake yalikuwa na machozi.
"Usifikirie sana, ni hatua nzuri. Tunahitaji kuangalia mbele. Kuna wanaume wengi wazuri jijini Nairobi.” Lisa alimshika mkono na kuelekea ndani ya kampuni pamoja.
“Sijali. Nina huzuni leo. Inabidi unitowe usiku wa leo ukaniweke sawa.” Pamela alijidekeza.
“Siwezi kutoka usiku wa leo. Niliahidi kwenda nyumbani kumpikia Alvin.” Lisa akamkaribisha, akisema, “Kwanini usije kula nyumbani kwangu?”
“Usijali, sina hamu ya kuiona sura ya Alvin,” Pamela alisema kwa hasira, “Kwa kuwa sasa umeolewa, huna muda wa kutoka na mimi, ghafla najihisi mpweke sana.”
"Ndiyo sababu unapaswa kutafuta mpenzi wa kukuriwadha." Lisa akashusha pumzi ndefu na kusema. "Niangalie. Baada ya kuolewa, siwezi hata kwenda kula chakula na watu wa jinsia tofauti. Hata nikitoka na wasichana wenzangu, bado nahitaji kuripoti kwake. Nahitaji kurudi nyumbani mara baada ya kazi kwani Alvin atakuwa hana furaha nikichelewa kurudi nyumbani.”
"Kama ndo hivyo basi nadhani sitaweza kuolewa." Pamela aliingiwa na hofu baada ya kumsikiliza Lisa.

Sura ya: 224

Jioni, Alvin alikuwa bado hajarudi Lisa alipofika nyumbani. Shangazi Yasmini alikuwa tayari ametayarisha mboga. Lisa alitazama mboga kwenye ubao na kusema, “Hukukata nyama ya kutosha, na mboga pia hazitoshi.”
"Lakini hii tayari ni nyingi." Shangazi Yasmine alishangaa. "tukiongeza itakosa walaji na kuharibika..."
"Mimi nilikuwa nikimchomea kilo mbili za nyama, na Alvin anamaliza yote." Lisa akatoa nyama nyingine kutoka kwenye friji.
Shangazi Yasmine alikuwa na hamu ya kujua. "Je, hii inaweza kuwa nguvu ya upendo? Nimemuona Alvin akikua tangu akiwa mdogo. Hajawahi kuwa mlaji mzuri. Ni kana kwamba hapendi kula chochote na alishiba hata kama alikula sahani ndogo tu ya wali.”
Kusema kweli, kama Lisa asingekuwa na muda na Alvin jijini Nairobi, asingeweza kuamini maneno ya Aunty Yasmine. Alvin alikuwa akipenda sana mapishi ya Lisa walipokuwa Dar es Salaam. Ilikuwa tu ni vile kwamba Alvin hakuwahi kusema mawazo yake waziwazi kwamba mapishi yake yalimvutia. Kwa kuwa kulikuwa na mtu ambaye alipenda chakula alichotengeneza. Hilo lilimfanya Lisa awe na shauku zaidi ya kupika.
"Baadaye, utagundua jinsi Alvin alivyo mlaji mzuri." Lisa alianza kukata nyama ya nguruwe.
Kuandaa nyama ya nguruwe choma kulihitaji muda mwingi. Wakati anasubiri, alianza kupitia habari za mitandaoni kwenye simu yake.
Hata hivyo, alipoona habari iliyoshika hatamu kwenye mitandao kadhaa, Lisa alishikwa na bumbuwazi. Mtandao wa Niambie.co.ke ukaandika: [Bwana Alvin Kimaro Ni chizi. Aliwahi kuua Mtu Hapo Zamani.]
Mtandao wa Ghafla.co.ke ukaandika: [Rangi za Kweli za Tajiri mkubwa nchini Kenya; Bwana Alvin Kimaro ana historia ya ugonjwa mbaya wa akili. Alipelekwa katika hospitali ya magonjwa ya akili baada ya kujaribu kumuua yaya wake. Inatisha. Kuna picha kama ushahidi.]
Moyo wa Lisa ulitetemeka. Aligonga kwenye picha.
Kulikuwa na picha chache za kijana mdogo. Sifa na sura ya mvulana huyo ndivyo Alvin alivyoonekana alipokuwa mdogo. Picha moja ilimuonyesha akiwa ameshika kisu chenye damu mikononi mwake. Macho yake yalikuwa na mng'aro mkali, na uso wake mchanga ulionekana kukunjamana na kutisha. Kulikuwa na picha nyingine mbili. Moja alimwonyesha akikamatwa na polisi huku nyingine akiwa amevalia shati jeupe baada ya kulazwa katika hospitali ya magonjwa ya akili.
Maoni ya watu yakaanza kutiririka: [Nilisikia juu ya ugonjwa huu hapo awali. Katika mtaa wetu, kulikuwa na mgonjwa wa akili ambaye aliua mtu. Watu wa aina hii wanatisha kweli kweli.]
[Ee bwana wangu, hiyo inatisha sana. Hata alitaka kumuua yaya wake aliyemtunza? Huyu ni kichaa kamili! Mbona aliruhusiwa kutoka hospitali ya magonjwa ya akili? Je, ikiwa ataumiza mtu? Nilisikia ugonjwa huu unahitaji dawa za muda mrefu. Kama sivyo, utajirudia.]
[Nilisikia kwamba yeye ndiye mwanzilishi wa Alvinarah Company. Je, mtu mwenye ugonjwa kama huu bado anaweza kuendesha kampuni?]
Kulikuwa na maoni zaidi ya 10,000 mtandaoni. Kichwa cha Lisa kilikaribia kumlipuka. Alikumbuka tukio ambalo Alvin alimpiga na kumuumiza mara ya mwisho. Baada ya hapo, wakati mwingine alipomkasirisha, macho yake yalikuwa yanatisha sana. Kuna wakati mkono wake pia ulikuwa umeumia kwa njia ya ajabu.
Alifikiria jinsi Alvin alivyokuwa na hasira na mkali kila wakati, alijua ni tabia yake ya kawaida. Hakuwahi hata siku moja kufikiria kwamba angekuwa mgonjwa wa akili. Baada ya yote, alionekana kawaida sana.
Lisa alikimbia ghorofani na kugundua chupa chache za dawa kutoka kwenye droo kwenye meza yake ya maktaba. Alitafuta majina ya dawa hizo kwenye simu, na dawa mbili kati ya hizo zilikuwa za kutuliza hasira na dawa nyingine ni za kuzuia magonjwa ya akili.

Kwa hiyo habari hiyo ilikuwa ni kweli? Hapo awali alitaka kumuua yaya aliyemtunza, na sasa, alikuwa amemdhuru. Baadaye ingekuwaje? Akafikiria…Alihisi ubaridi ukishuka chini ya uti wa mgongo wake na hakuthubutu kushuka chini.

“Bibi Mdogo, Bwana Kimaro hajarudi. Unataka kumpigia simu?” Shangazi Yasmine alitokea mlangoni. Alipoziona dawa alizokuwa ameshika Lisa, sura yake ikasisimka. “Dawa hizi…”

“Shangazi Yasmine, ulisema umemwona Alvin akikua tangu mdogo. Kwa hiyo unapaswa kujua ... kwamba yeye ni mgonjwa wa akili, sivyo?" Uso wa Lisa ulikuwa umepauka, na midomo yake ilikuwa ikitetemeka.

Shangazi Yasmine alishindwa aseme nini. Aliifuta mikono yake kwenye apron yake na kuuliza. “Ulisikia wapi? Hili haliwezekani…

“Habari Ipo kwenye mtandao.” Lisa alimuonyesha picha hizo. “Shangazi Yasmine, yote haya ni kweli?”

Aunty Yasmine alishtuka baada ya kuziona zile picha. “Nani alichapisha mambo hayo? Hizi ni picha za siku nyingi sana… Bibi mdogo, lazima umwamini Bwana Kimaro. Ni mtu mzuri.”

"Lakini tabia yake ya kawaida kwa kweli ni mtu mkali mkali tu na ana hasira zilizokithiri. Dawa hizi pia ni uthibitisho wa hilo.” Lisa alishikilia chupa za dawa kwa nguvu na kunung'unika, "Shangazi Yasmine, mimi huwa namuogopa pia. Aliwahi kunipiga vibaya sana na kuniumiza hapo awali, na lilikuwa tukio la kutisha. Nataka tu kujua ukweli.”

“Sawa, nitakuambia. Natumai hutamuelewa vibaya kama watu wa nje.”
Shangazi Yasmine akashusha pumzi ndefu. “Bwana Kimaro alianza kuonyesha dalili za ugonjwa huu alipokuwa na umri wa miaka minane. Wakati huo, wazazi wake walikuwa tayari wameachana na mama yake hakumjali hata kidogo. Katika familia ya Kimaro, Mzee Kimaro alikuwa mtu busy aliyejikita tu kwenye kazi zake. Bibi Kimaro alimpenda Alvin, lakini alikuwa na watoto na wajukuu wengi. Alihitaji kujumuika nao pia, kwa hiyo hakuwa na wakati wa kumtunza. Hakuna mtu aliyegundua kwamba yaya wake alikuwa akimnyanyasa Alvin kwa sababu hawakumjali.”

“Kumnyanyasa?” Lisa alishtuka.

“Ndiyo. Wakati Alvin alipokuwa mdogo, alijihisi kutojiamini na kulia mara kwa mara. Bila shaka, hiyo ilikuwa mbinu tu ya mtoto ili kupata upendo wa wazazi wake. Lakini yaya wake alifikiri kwamba alikuwa akideka, hivyo mara nyingi alimfungia kwa siri ndani ya chumba na kumshindisha njaa. Wakati wa majira ya baridi kali, alimvua nguo zake na kumwacha akipigwa na baridi na njaa.”

Lisa alihisi kifua kinamuuma kwa uchungu. Alikuwa amepitia hisia hiyo ya baridi na njaa hapo awali, lakini Alvin alikuwa mtoto tu wakati huo. Mtu anawezaje kuwa mkatili kiasi hicho kwa mtoto?

“Alvin alilalamika kuhusu hilo hapo awali, lakini hakuwa ameumia sehemu yoyote mwilini. Kwa hiyo, kila mtu alifikiri alikuwa akimsingizia tu yaya kimakusudi.”

Aunty Yasmine aliendelea kusema, “Babake hakumjali pia. Alikuja amelewa kila siku. Kisha, Alvin alipokuwa na umri wa miaka minane, baba yake alienda ng'ambo na mwanamke mwingine. Alipotoka alikata mahusiano yote na Alvin na kumwambia asimtafute tena kwani kumwangalia kulimkumbusha siku za nyuma zisizo na furaha. Kuondoka kwake ndio lilikuwa jiwe la mwisho ambalo lilimponda Alvin…”

Lisa aliona vigumu kuongea. “Kwa hiyo…?!”

“Ndipo Alvin alipoingia kwenye mfadhaiko. Hakuzungumza wala kula. Hata alimchoma kisu yaya wake aliposhindwa kustahimili kunyanyaswa tena. Bibi Kimaro alipokagua kamera za ulinzi, tuligundua kuwa ni kweli yule yaya alimnyanyasa sana Alvin, lakini alikuwa amechelewa. Alvin alikuwa tayari kapelekwa hospitali ya wagonjwa wa akili ambapo alipata matibabu kwa miaka mitatu. Baada ya kurejea, alirejesha usikivu wa familia ya Kimaro kupitia bidii yake na kuwa hivi alivyo leo.”

Macho ya shangazi Yasmine yalikuwa mekundu. “Bibi mdogo, ni kawaida kumuogopa Bwana Kimaro. Lakini natumai hutamdharau wala kumuacha. Anatia huruma kweli. Akikupoteza, atapoteza kila kitu na hata tumaini la kuishi tena.”

“Sawa, sitathubutu.” Lisa akaitikia kwa kichwa. Moyo wake bado ulihisi dalili za maumivu.

Ni nani angeweza kufikiria kwamba mwanamume mwenye kiburi na mashuhuri kama yeye alikuwa akificha maisha ya utotoni yenye huzuni na maumivu? Ghafla alijisikia kumkumbatia kwa nguvu. Alitaka kumwambia kwamba angempa furaha ya familia ambayo alikuwa ameipoteza maisha yake yote.

Hata kama watu wengine wangemwogopa, yeye asingemugopa tena.

Alikumbuka kitu ghafla. Alihisi Alvin angejisikia vibaya baada ya kuona hizo picha. Alimpigia simu, lakini hakuna aliyepokea. Aliweza tu kumpata Hans kwenye simu. “Hans, Alvin yuko wapi? Niliona habari fulani kuhusu yeye. Yuko wapi sasa hivi?”

Sura ya: 225

“Bibi Mdogo, Bwana Kimaro…” Hans alisikika akiwa na wasiwasi, lakini hakujua aanzie wapi.

“Nimesikia kila kitu kutoka kwa Shangazi Yasmine. Sijali ugonjwa wake, we niambie tu alipo.” Lisa alijua anachofikiria.

“Baada ya Bwana Kimaro kuona habari hiyo, aliendesha gari peke yake. Hatujui alikokwenda na tunamtafuta kila mahali. Nadhani kuna kitu hakiko sawa na hisia zake. Ugonjwa wake unaweza kujirudia, na ninashuku kwamba ataenda kumtafuta Mama yake.

“Lea?”

“Ndiyo. Alipoona habari hiyo sasa hivi, nilimsikia akinong'ona kuwa hiyo lazima iwe kazi ya Lea. Kama Lea anahusika, atapoteza udhibiti wa hisia zake na ninahisi atamfanyia kitu kibaya." Hans alisema kwa wasiwasi, "niko njiani kumtafuta Lea sasa hivi."

“Nitumie anwani ya sehemu ulipo pia. Nitakupitia sasa hivi.” Lisa alichukua funguo ya gari na kutoka nje haraka.
•••
Katika jumba lake binafsi, Lea alipoona habari kuhusu ugonjwa wa akili wa Alvin kwenye mtandao, alimpigia simu Valerie mara moja. “Wewe ndiye uliyevujisha hizo picha?”

"Kwanini unanishuku mimi?" Valeria aliuliza kwa wasiwasi.

"Watu wa familia ya Kimaro pekee ndio wenye picha hizi. Kando na wewe, ni nani katika familia ya Kimaro…” Lea alikuwa bado hajamaliza kuzungumza wakati sauti za mapigano ziliposikika kutoka nje. Alifungua mlango na walinzi wote walikuwa wamelala chini. Alvin alisimama mlangoni akiwa na sura mbaya.

“Wewe…”

“Nifuate.” Alvin alimpiga mama yake kwa nguvu na kumvuta kuelekea juu ya paa. lilikuwa ni paa la flati la ghorofa. Simu yake ilidondoka chini. Sauti ya Valerie yenye wasiwasi ilitoka kwenye simu, lakini hakuna aliyejali kuhusu hilo.

Akiwa juu ya paa, Lea alionekana kufadhaika huku akiburutwa huku na kule. “Alvin, unajaribu kufanya nini…. Ah!” Nusu ya mwili wake ilisukumwa kutoka kwenye ukingo wa paa, akikaribia kuangushwa chini kutokea juu.

“Nilikuonya hapo awali usijaribu kutumia ugonjwa wangu wa zamani kunidhalilisha, lakini ulifanya nini? Kwanini nina mama kama wewe?" Alvin alimshika shingo kwa nguvu huku akipiga kelele. Alikuwa amevunjika moyo kabisa.

Lea alitoa macho kwa mshtuko huku uso wake ukiwa umekunjamana. “Siyo mimi…”

“Ni nani mwingine zaidi yako?” Macho ya Alvin yalikuwa yakiwaka kwa hasira. "Unajali tu kuhusu Jack tangu akiwa mtoto. Ulinizaa wa nini? Wakati huu wote, umekuwa ukimsaidia Jack kwa sababu ulitaka kunitoa kwenye nafasi yangu ya uenyekiti katika kampuni. Unanidharau tangu uliponizaa. Mimi sikujali hayo, lakini kwanini uliamua kueneza picha zangu? Nilikuambia kwamba nitakufanya ulipe kwa hili."

Tangu utotoni, Alvin hakuwahi kuhisi upendo wa kifamilia na uchangamfu kutoka kwa familia ya Kimaro. Sasa, hatimaye alipata tena mwanamke ambaye alimpenda, alitaka tu kuwa na maisha ya furaha, ya kawaida pamoja naye. Lakini, watu wa karibu wa familia yake walikuwa wametumia njia ya kikatili kufunua maisha yake ya aibu.

Mtandao ulikuwa umejaa maoni makali na mabaya kuhusu yeye. Kila mtu alimuogopa na hakuna aliyekuwa na hamu ya kumsogelea. Aliamini Lisa angeweza pia kuwa na hofu. Tayari alikuwa akimuogopa hapo awali. Joto na furaha yake iliyobaki ilikuwa imetoweka kama mapovu.

“Alvin, tulia. Mimi ni mama yako,” Lea alisema kwa sauti ya kutetemeka, “Unachofanya sasa ni kitendo cha jinai. Utatupwa jela utengwe na ulimwengu wote.”

“Ha! Kwani hivi sasa sijatengwa na kila mtu? Kwanini umenizaa? Wewe ndiye mwanamke mbaya zaidi ulimwenguni. Unanichukiza!” Alvin alipiga kelele kwa nguvu zake zote. Nusu ya mwili wa Lea ulining'inia hewani, na alikuwa karibu kuanguka.

“Utaniua kweli mwendawazimu wewe!” Lea alilalamika kwa hofu.
“Mimi ni mwendawazimu kweli, na wewe ndiye uliyenipeleka hadi kwenye ukichaa." Alvin alikasirishwa naye zaidi.

Alipokaribia kushindwa kudhibiti akili yake, alisikia kelele za Lisa nyuma yake. "Alvin, hapana!"

Mwili wa Alvin ulitetemeka, na uso wake mzuri ukabadilika kuwa wa kutisha zaidi. Hakuthubutu kugeuka na kumwangalia. Aliogopa kwamba angeona uso wake uliojaa hasira na ukatili. Alihisi kwamba ugonjwa wake ulikuwa mbaya zaidi kila mara tangu ulipojirudia. Kifua chake kilijawa na uadui. Hapo awali, angeweza kujizuia asimdhuru Lea. Lakini siku hiyo, hakuweza kujizuia tena. Hakutaka mtu yoyote kumsogelea kwa sababu hakuwa tayari kufungiwa tena katika hospitali ya watu wenye matatizo ya kiakili. Kulikuwa na pande nne tu za kuta huko. Hakuna mtu ambaye angemjali au kuwa na wasiwasi juu yake.

"Alvlisa, njoo hapa." Lisa alishusha pumzi na kumsogelea hatua kwa hatua.

“Imetosha, usisogee tena!” Alvin alimfokea kwa hasira. Uso wake mzuri ulijaa uchungu. "Mimi ni mgonjwa. Nitakuumiza. Unajua hilo?"

Lisa aliona upande huo wa Alvin uliojificha kwa miaka mingi. Moyo ulimuuma huku machozi yakimtoka. "Siogopi. Hakuna aliyezaliwa kuwa hivi. Huna hatia. Waliokudhulumu ni wale walio katika udhalimu.”

“Acha kuongea, sikuamini.” Alvin alitikisa kichwa bila kusita. "Mama yangu alinidanganya vivyo hivyo siku za nyuma, na alinipeleka kwenye hospitali ya magonjwa ya akili mara tu nilipogeuka."

Lea alidakia na kusema. “Kwa hali yako wakati huo, kama singekupeleka kwa matibabu—”

“Nyamaza!” Alvin alimkatisha ghafla. “Wewe ndiwe uliyesababisha ugonjwa wangu. Ulikuwa wapi nilipofungiwa chumbani kwa siku tatu mchana na usiku? Ulikuwa wapi nilipovuliwa nguo wakati wa baridi kali na karibu kufa kutokana na njaa na baridi?” Alizidi kuhamaki huku akiendelea kuongea, akawa anaelekea kushindwa kujizuia tena.

Lisa alishindwa kabisa afanye nini. Wakati huo Chester alikuja pembeni yake akiwa na sindano mkononi. “Ninaogopa kuwa wewe ndiye mtu pekee ambaye unaweza kumkaribia sasa. Mchome sindano hii mkononi na atazimia.”

"Lakini sijawahi kudunga sindano hapo awali ..." Lisa aliogopa.

"Unaweza kufanya hivi." Chester alimtazama bila kuyumbayumba na kumuelekeza. "Jitahidi. Usiruhusu Alvin kupita hatua ambayo tutashindwa kumrudisha."

"Sawa." Lisa akashusha pumzi ndefu na kuificha ile sindano kwa siri. Alimsogelea Alvin taratibu.

“Nilikuambia usije. Hunielewi?” Alvin aligundua kuwa Lisa alikuwa karibu naye na akamfokea.

"Siwezi kusimama karibu na kukuona ukiingia kwenye matatizo!" Lisa alizidi kumfokea Alvin kwa macho mekundu. “Alvin, huwezi kuwa mbinafsi kiasi hicho. Uso wangu uliharibika kwa sababu yako. Popote ninapoenda, watu hunidhihaki kwa kuwa na sura mbaya. Ulisema kwamba hutanionea aibu. Uliahidi kunipa furaha na kwamba ungetumia maisha yote kunithibitishia. Je! hivi ndivyo unavyothibitisha?”

Alvin aliutazama uso wake mdogo wenye michirizi ya machozi. Ghafla, alikuwa amepotea kama mtoto. “Mimi…”

“Bado huelewi? Siku zote nimekupenda. Bado nitakupenda haijalishi utakuwaje. Sitakuogopa kwa sababu ya maisha yako ya nyuma. Ni kinyume kabisa. Nitasikia maumivu tu kwa ajili yako, na ninataka kukupa joto kwa maisha yako yote. Wewe ni mgonjwa, na mimi ni mgonjwa pia, tutariwadhana. Hiyo ni sawa. Naweza kuwa kando yako. Ikiwa huwezi kupona, bado nitakuwa nawe maisha yote.”

Lisa akamsogelea hatua kwa hatua, na koo lake likamkaba. "Vivyo hivyo, ikiwa mimi ndiye mgonjwa, hutaniacha, sivyo?" Alvin alishikwa na mshangao, na macho yake makali yakaanza kupoa na ule moto wa hasira ukaanza kuzima taratibu.

Lisa alichukua nafasi hiyo na kumchoma mkono. Alvin akageuza kichwa chake na kumtazama. Hakuweka upinzani wowote, na macho yake polepole yakapoteza mwelekeo. Mkono wake uliomshika Lea ukalegea, akaanguka chini taratibu!.

TUKUTANE KURASA 226-230

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
SIMULIZI............LISA
KURASA.......226-230

Sura ya: 226

Lisa alimkumbatia mara moja na kumnong'oneza sikioni, “Ninakuahidi kwamba sitaondoka. Ukiamka nitakuandalia nyama choma ya nguruwe.”

Macho ya Alvin yakalegea taratibu. Alianguka na kupoteza fahamu na kuonekana kama mtoto ambaye alikuwa amelala fofofo. Hakuna mtu ambaye angeweza kufikiria kwamba alikuwa mgonjwa ambaye alipandisha wazimu muda mfupi uliopita.

Lea alikaa chini baada ya kuokolewa. Hata baada ya muda mrefu kupita, amani haikurudi usoni mwake.

Jack alimkimbilia na kumsaidia kuinuka. "Mama, tayari nimewasiliana na hospitali ya magonjwa ya akili. Watatuma gari kumchukua Alvin.” Lea alipigwa na butwaa.

Lisa alimkazia macho. “Nani alikuambia upige simu hiyo?”

Jack alisema kwa ukali, “Kama hatutampeleka kwa matibabu, kwa hali yake ya sasa, je, unatfikiri ataishije na watu?”

“Yuko sahihi. Alvin alikuwa katika hali ya kutisha sana sasa hivi.” Mason alishika mikono ya Lea na kusema kwa woga, “Niliogopa sana. Bado kidogo tu angekusukuma chini. Ni Lea wakati huu, lakini ugonjwa wake utakapomrudia, nani atafuata?”

Aliongea kwa kusitasita, lakini Lea alimwelewa na kumuunga mkono. “Ni bora kumpeleka hospitali kwa matibabu. Siyo jambo geni, hata zamani aliwahi kutibiwa pia…”

Lisa hakutaka kusikia tena. “Si umesikia alichosema Alvin sasa hivi? Ukweli kwamba ulimdanganya na kumpeleka hospitali ya magonjwa ya akili siku za nyuma tayari umeacha kovu juu yake. Kama mama, unajua kipi kingine cha kumsaidia zaidi ya kumsukumia hospitali? Hustahili kuwa mama hata kidogo.” Aibu na haya vilitanda kwenye uso wa Lea.

Jack alikunja uso na kuongea kwa hasira. "Unajua nini? Ikiwa hatutamfunga, ataumiza mtu mwingine tena. Anaweza hata kukuumiza wewe mwenyewe.”

“Hiyo ni juu yangu.” Lisa alihisi hasira kali kwa ajili ya Alvin. “Jack, ni rahisi kwako kusema hivi kwa sababu si wewe uliyekuwa umefungwa hospitalini. Tangu utotoni, umekuwa na upendo wa wazazi wako. Hata baada ya kukua, mama yako bado anafikiria njia nyingi za kukusaidia, na sasa anapanga kukukabidhi biashara na familia ya Kimaro mikononi mwako. Lakini vipi kuhusu Alvin? Kwanini alikua mgonjwa wa akili? Ni kwa sababu alikuwa amefungiwa kwenye chumba peke yake wakati nyinyi watatu mkiwa na familia yenye furaha. Wazazi wako walipokupeleka kusafiri kote ulimwenguni, Alvin alinyimwa chakula na joto kwa sababu ya unyanyasaji wa yaya wake. Ni sawa ikiwa mnahisi hamna hatia na hamna makosa hata kidogo, lakini je, mnaweza kumhurumia japo kwa muda mfupi tu?”

Jack alijihisi vibaya kutokana na kukemewa, na rangi zote zikatoka usoni mwa Lea.

Lisa alidhihaki, "Hata uliniambia mwanzo kwamba mimi na Alvin tuna hatima sawa. Inafurahisha sasa ninapofikiria juu yake. Wewe ni mroho usiyetosheka. Una kila kitu lakini bado ulitaka kunyakua KIM International ambayo ilikuwa kitu pekee ambacho Alvin alikuwa nacho. Alipata tu mapenzi kutoka kwa familia ya Kimaro kupitia msaada wa KIM International. Anawajali ninyi, lakini ninyi ni kundi la watu mnaomuumiza kila mara.”

“Umemaliza kututukana?” Jack aliuma meno na kukunja ngumi kwa hasira.

Lisa akawatupia jicho la chuki. “Kuhusu ugonjwa wa akili wa Alvin kufichuliwa, hakuna mtu mwingine anayeweza kuwa nyuma ya hili isipokuwa nyie familia ya Kimaro. Tutawafanya mlipe deni hili."

Alimtazama Chester baada ya kumaliza kuongea. “Hebu mchukue Alvin tuondoke.”

Chester alimtazama Lisa kwa kumshangaa na kutikisa kichwa. Akambeba Alvin na kushuka chini.

“Nyie…” Jack alitaka kuwafuata, lakini Lea akamvuta nyuma. Akatikisa kichwa chake na kumwambia. “Achana nao…”

Mason alikuwa na hali ya wasiwasi. “Lakini…”

“Ninapaswa kuwajibika kwa ugonjwa wa Alvin.” Lea alikuwa na hisia tofauti. Alikuwa hajapenda kuwepo kwa Alvin muda wote. Ilikuwa ni kwa sababu yake ilimbidi aolewe na mtu ambaye hakumpenda. Mara ya mwisho alipohisi hatia kwa Alvin ni wakati ugonjwa wake ulipomshika alipokuwa na umri wa miaka minane.Lakini, wakati huo, Lea alikuwa na kazi yake, familia yake, na Jack wa kumlea, akampeleka Alvin akalelewe hospitali ya vichaa. Hatimaye Alvin alirudi baada ya kukaa katika hospitali ya wagonjwa wa akili kwa miaka michache na tayari alipata nafuu. Aligeuka kuwa mwenye hasira na mkatili baada ya kupona, na kumfanya azidi kumdharau.

Tukio lililotokea siku hiyo lilimfanya Lea akumbuke baadhi ya mambo ya muda mrefu uliopita. Alikuwa amemwachia Alvin majeraha mengi. Hakika alidharau uwepo wa Alvin, lakini Alvin alimchukia kwa kumzaa pia.

“Jack, ngoja nikuulize hivi, Wewe ndiye uliyesambaza picha hizo?” Lea alikunja uso na kuuliza, “Mkutano wa wanahabari na kampuni ya Alvinarah kuhusu cement yao mpya unafanyika kesho. Bila shaka picha hizi zimetolewa makusudi ili kuvuruga tukio hilo. Mtu anayeshukiwa zaidi katika familia ya Kimaro ni mam’dogo wako, na anayefuata ni wewe."

"Mama, mimi sikufanya." Jack alikasirika. "Hata iweje, bado nina uhusiano naye wa damu. Alikuwa mgonjwa tangu mwanzo, na hata iweje nisingefikia hatua ya kumdhalilisha kwa kutumia ugonjwa wake.”

Lea alipapasa paji la uso wake. Alikuwa anaumwa na kichwa. Alijua mtoto wake alikuwa na utu gani. Je, ni kweli Valerie ndiye aliyefanya hivyo?

"Mama, baada ya hili la Alvin, katika hali hii, mkutano wa waandishi wa habari wa kesho bado unaweza kufanywa?" Jack aliuliza kwa kusitasita.

Lea alimkazia macho na kuondoka zake. Alikuwa anaenda kumfuata Valerie.
•••
Chester alimpeleka Alvin moja kwa moja hadi kwenye hospitali binafsi kwa ajili ya kumfanyia uchunguzi na kumtwisha dripu iliyokuwa na dawa za kutuliza. Wakiwa wodini, Lisa alimshika mkono Alvin kimyakimya.

Aliona tu upande wake wa kiburi, jeuri, na ukatili katika siku za nyuma. Siku hiyo, alikuwa ameona upande wake dhaifu. Moyo wake bado ulimuuma.

"Kusema kweli, nilipojua kwa mara ya kwanza kwamba wewe na Alvin mmekutana, nilifikiri kuwa haukuwa mzuri kwake." Chester alitabasamu. “Lakini sasa, ninaona aibu kuwa na mawazo hayo. Unastahili kuthaminiwa na Alvin.”

Lisa hakushangaa. Alvin na marafiki zake walikuwa ni watu ambao walikuwa wamesimama juu ya ufahari wa Kenya, kwa hiyo ilikuwa kawaida kwamba wangemdharau. Aliachana na mada hiyo na kumuuliza swali tofauti. "Dokta Choka, unaweza kuniambia jinsi Alvin alivyopata jeraha kwenye mkono wake sasa?"

Chester alitabasamu kwa uchungu. "Unaweza kuwa umekisia tayari, lakini ndio, wakati wowote Alvin anapokaribia kushindwa kuthibiti hasira zake, huwa anajikata kwa kisu. Ilitokea mara mbili, na mara zote mbili zilihusiana na wewe." Lisa alishtuka. Aliinua kichwa na kumtazama.

"Mara ya kwanza uligombana naye asubuhi. Baada ya kuondoka alijiumiza ndani ya gari. Mara ya pili ilikuwa njiani kuja hospitali baada ya kukuokoa kutoka kwenye jela ya familia ya Kimaro.”

Lisa alikumbuka hili. Asubuhi hiyo, alisema kuwa hampendi na kisha akaondoka kwa hasira. Kwa mara ya pili, ghafla alisema kwamba anataka kutoka kwenye gari. Alidhani alichukizwa na harufu ya uvundo kwenye mwili wake. Kumbe aliondoka kwenda kujiumiza mwenyewe. Alijuta sana.

"Wewe na Lea ndio watu pekee mnaoweza kumfanya ashindwe kujidhibiti kwa sababu anawajali ninyi wawili." Chester alimtazama na kumwambia moja kwa moja.

Moyo wa Lisa ulitetemeka. “Nitamsaidiaje?”

"Kaa naye," Chester alisema, "Hawezi kufanya kazi katika hali hii sasa. Alvin ana jumba lake Mombasa kando ya bahari. Napendekeza nyie mngeenda huko. Fuatana naye ili kupata hewa safi na kumpa joto na upendo.”

“Sawa.” Lisa aliitikia bila kuchelewa.

“Naamini hutamchukua tena baada ya kuujua ukweli wake.” Chester aliinua macho yake kwa udadisi. “Si uliendelea kumlaumu kwa kutumia mbinu za siri kuwatenganisha wewe na Kelvin? Na Alvin alichangia pia kwa wewe kuharibika sura?"

Sura ya: 227

Lisa alihisi uchungu. "Ndio, ilikuwa ni lazima nimchukie. Nilipaswa kumchukia kwa kutoniamini huko Dar es Salaam, kwa kunidhalilisha tena na tena, na kwa kuniumiza. Baada ya kusema hivyo, sikuweza kujizuia kuwa na wasiwasi juu yake nilipogundua kwamba kuna jambo lililompata. Niliumia sana kufahamu kuhusu maisha yake magumu ya utotoni. Nilijidanganya kwa kuamini kwamba nimeacha kuwa na hisia naye, lakini siwezi kuudanganya moyo wangu. Kadiri ninavyoelewana naye, ndivyo ninavyozidi kumpenda.”

Alimtazama kwa upendo yule mtu aliyekuwa amepoteza fahamu pale kitandani. Aliamua kuacha yaliyopita yawe yamepita. Kuanzia siku hiyo na kuendelea, alitaka kuwa mzuri kwake. Sasa Joel alikuwa hajitambui kitandani, Alvin ndiye alikuwa mwanafamilia pekee aliyebaki kwake, ilibidi amthamini kwa kila hali.

Chester alifurahishwa na hali hiyo, lakini Hans aliyekuwa kando yake alionekana kuwa na wasiwasi. "Ikiwa Bwana Kimaro hawezi kufanya kazi, mkutano wa waandishi wa habari kuhusu uzinduzi wa cement mpya utafanyika vipi? Zaidi ya hayo, habari kuhusu hali ya akili ya Bwana Kimaro inaenea kama moto wa nyika. Ni lazima tupunguze zogo.”

Lisa alipigwa na butwaa. "Je, hakuna mtu mwingine yeyote anayeweza kuchukua jukumu la kampuni ya Alvinarah wakati kama huu?"

"Kunao, lakini tayari imetangazwa kuwa Bwana Alvin Kimaro ndiye atakayehudhuria mkutano huo. Ninahofia kwamba kutokuwepo kwake kwa dharura kutasababisha ghasia na kuathiri vibaya maendeleo ya Alvinarah ya siku za usoni.”

Lisa alikunja uso na kufikiria kwa nusu dakika kabla ya kusimama ghafla. “Nitahudhuria kwa niaba yake. Kama mke wake, nitawajibika kwa hilo.”

Hans na Chester wote walishangaa. "Lakini hakika kutakuwa na wanahabari wengi watakaokuuliza maswali kuhusu hali ya Bwana Mkubwa Kimaro wakati wa mkutano huo..."

'”Nitajibu maswali ya waandishi." Lisa alielekeza macho yake makali kwa Hans. “Nisaidie kukusanya taarifa. Nataka umma ujue kuwa Alvin si kichaa.”

Hans aliyekuwa anatetemeka ghafla aliguswa na ujasiri wake. Angalau kulikuwa na mtu ambaye alimjali bosi wake katika maisha yake.

Siku iliyofuata, Jumba la Alvin lililokuwa huko Mombasa likitazamana na Bahari ya Hindi, lilivamiwa na wageni wa ghafla. Vuli ilikuwa imefika na maua yalikuwa yamechanua kabisa.

Baada ya kupoteza fahamu kwa usiku mmoja, Alvin aliyekuwa kitandani alifumbua macho na kuketi. Kwa kasi alikimbilia mlangoni bila kuvaa nguo zake. Hapo hapo mlango ukasukumwa. Hans aliingia ndani huku akionekana kushangaa. “Umeamka, bosi…”

Alvin alimsukuma na kuelekea chini. Baada ya kuangaza-angaza, alimvuta Hans kwenye shati lake kwa macho yenye muwako wa damu. "Yuko wapi? Ameenda wapi?”

Hans akapata fahamu. "Bi Jones -"

"Aliondoka, sivyo?" Alvin akamkatisha sentensi yake na kuunguruma, “Amenidanganya! Aliahidi kukaa karibu nami wakati wa matibabu yangu na kuniandalia nyama choma ya nguruwe. Wote ni uongo.”

"Bwana Mkubwa, umemwelewa vibaya." Akihofia kwamba Alvin angeshindwa kujidhibiti tena, Hans mara moja alisema, "Bi Mdogo ameenda kuhudhuria mkutano wa waandishi wa habari na Alvinarah kwa niaba yako."

"Nini?" Alvin alikodoa macho.

"Dokta Choka alisema kuwa hautoweza kutoka nje, lakini kashfa nyingi zaidi kuhusu wewe zinaenea huko na ni ngumu kuzizuia. Waandishi hao tayari wamejazana kwenye ukumbi wa mkutano tangu jana usiku. Kwa sababu hiyo, Bi Jones aliamua kuhudhuria mkutano huo badala yako na kwenda kufafanua kuhusu hali yako pia.”

Alvin alimtazama Hans kwa hasira. "Je, viongozi wa juu wa kampuni wamekufa? Pia, unawezaje kumruhusu ashughulike na wanahabari hao wakatili? Hapana, hawezi kushughulikia. Lazima niharakishe huko…”

“Bwana Mkubwa, huwezi kwenda huko.” Hans akamzuia.

"Niondokee. Wewe ni msaidizi wangu tu. Unathubutuje kunizuia?!" Alvin alipandwa na hasira.

"Hans anakuzuia kwa faida yako mwenyewe." Chester aliingia ghafla. Hakuwahi kuwa mkali hivi hapo awali. “Jiangalie. Unajua wazi kwamba waandishi watakuuliza maswali ya kutisha, una uhakika 100% kwamba hutaathiriwa na maswali yao na hutapoteza udhibiti?"

Koo la Alvin likakaza, na vidole vyake vitano vilijikunja na kuwa ngumi.
Chester aliendelea kusema, "Ugonjwa wako ukitokea mbele ya kamera, Alvinarah itakuwa imetupwa majini na maisha yako yatakwisha."

"Acha kunitisha!" Macho ya Alvin yalimtoka kwa huzuni.

“Uwe na imani na Lisa. Yeye si dhaifu kiasi hicho.” Chester akatoa simu yake na kubofya programu iliyokuwa ikitangaza mkutano huo moja kwa moja. "Sasa, wacha tuone jinsi anavyofanya."

Mtiririko wa moja kwa moja wa matukio ya mkutano wa kampuni ya Alvinarah na waandishi wa habari uliofanyika usiku huo ulipata watazamaji zaidi ya milioni moja kutoka ndani na nje ya Kenya. Lisa akiwa amevalia gauni jeusi alikuwa akitoa hotuba jukwaani.

Ilikuwa ni mara ya kwanza kuonekana hadharani kama mke wa Alvin.
Wale ambao hawakuwahi kumuona walikuwa wakidhani kwamba alikuwa mrembo mkubwa, ikizingatiwa kwamba Alvin Kimaro, tajiri mkubwa zaidi nchini Kenya alimpenda sana. Lakini, dakika ambayo alionekana hadharani, kila mtu alipigwa na butwaa.

Alvin hata aligundua kuwa watazamaji wengi waliendelea kujaza ukurasa wa maoni.

[Inawezaje kuwa yeye? She's so ugly.]

[Damn! Nini kilitokea kwa uso wake? Ni mbaya sana.]

[Je, inawezekana kwamba kuna kitu kilienda vibaya kwa macho ya Bwana Kimaro tangu alipokuwa na ugonjwa wa akili?]

Akiwa ameshtuka, Chester alifunga mara moja ukurasa wa maoni.
Hata hivyo, Alvin tayari alishaona maoni hayo na kulipuka kwa hasira.

“Hawa watu wamerukwa na akili nini? Je, wana nia ya kutazama mkutano au wanawake warembo?”

Kwa kujisikia vibaya, Hans alibadilisha mada haraka. “Bwana Kimaro, tazama. Bi. Jones ameanza kuongea. Ana sauti ya mamlaka na ushawishi.”

Alvin alimkazia macho. Hakuhitaji Hans kumkumbusha kwani aliweza kuona kwa macho yake. Ilikuwa ni mara yake ya kwanza kumuona Lisa akiwa amesimama mbele ya waandishi wa habari. Mkutano wa usiku huo ulikuwa umevuta hisia za makampuni mengi ya ndani na nje ya Kenya.

Wakati wa mkutano huo kuanza, Lisa aliinua kipaza sauti kwa utulivu. Aligonga kipaza sauti ili kukijaribu kabla ya kuanza kuzungumza, “Habarini nyote. Mimi ni mke wa Alvin Kimaro, Lisa Jones. Niko hapa kukaribisha mkutano na waandishi wa habari kuhusu Alvinarah's Oceanic Cement. Hii ni brand ya kwanza ya cement bora zaidi zinazozalishwa nchini Kenya. Mwanzilishi wa cement hiyo, Alvin Kimaro, alipaswa kutambulisha bidhaa hiyo ana kwa ana, lakini Bw. Kimaro hakuweza kuja kwa sababu za kibinafsi—”

Kabla hajamaliza kuzungumza, ripota kutoka Nairobi Financial Times alikatiza hotuba yake, “Je! ni kwa sababu ugonjwa wake wa akili umemshika tena? Ni kweli alimuua yaya aliyekuwa akimtunza tangu akiwa mdogo? Si lazima aende jela baada ya kumuua kwa sababu ya kosa la jinai, sivyo? Au ni kwa sababu ya hadhi yake ya juu ndiyo maana hajafungwa?”

Mara baada ya ripota huyo kuanzisha somo, waandishi wengine wengi walianza kumuuliza maswali mfululizo juu ya Alvin.

"Tulisikia kwamba ambulensi kutoka hospitali ya wagonjwa wa akili ilikwenda nyumbani kwa mama yake jana. Ugonjwa wake ulianza tena?"

“Mbona bado hajapelekwa hospitali ya magonjwa ya akili? Je, kama ataumiza wengine wakati ujao?”

"Je, watu wenye matatizo ya akili kama yeye wanaweza kuiongoza vizuri Alvinarah? Je, kunaweza kuwa na tatizo na cement?"

“Sasa unaishi na Alvin huogopi? Amewahi kukuumiza?”

"Sio tu kwamba kuna tatizo kwenye akili ya Alvin, lakini pia ana matatizo ya macho pia . Vinginevyo, kwanini alikuchagua wewe kuwa mke wake?”

Lisa aliulizwa maswali mengi mabaya kutoka kwa waandishi wa habari waliokuwa chini ya jukwaa. Mimuliko ya mara kwa mara ya kamera iliumiza macho yake pia. Hata hivyo, aliendelea kuvaa tabasamu la upole na la adabu. Dakika tano baadaye, waandishi walikuwa wamechoka kuuliza maswali. Walipoanza kunyamaza, Lisa alifungua mdomo wake. “Mmemaliza kuuliza maswali?”

Sura ya: 228

Swali la Lisa lilipita kimya.

“Naam, hatimaye naweza kuzungumza sasa.” Lisa akaanza. “Kuhusu ugonjwa wa Alvin, ni kweli, lakini nashangaa hakuna hata mwandishi mmoja aliyeuliza chanzo cha ugonjwa wake, wote mmeishia kumtuhumu na kumjaji kana kwamba ni mhalifu mkubwa. Kila mtu ana matatizo. Kama ilivyo kwa binadamu wengine, Alvin naye ana matatizo yake. Hakumuumiza yaya wake kwa kupenda wala bila sababu. Hii hapa ni ripoti ya matibabu kuhusu matibabu ya Alvin alipokuwa na umri wa miaka minane. Aligundulika kuwa na msongo wa mawazo na kiwewe baada ya mfadhaiko kwa sababu alikuwa akiteseka kutokana na unyanyasaji kwa muda mrefu. Ni ukweli kwamba alikuwa amenyanyaswa kwa muda mrefu na yaya wake.”

Lisa alitazama nyuma ya jukwaa, na video ya zamani ilionyeshwa kwenye skrini kubwa. Katika video hiyo, afisa wa polisi alionekana akimhoji mwanamke wa makamo mwenye nywele chafu na mikunjo usoni.

"Ulimfanya nini huyu mtoto wakati analia?"

“Nilimvua nguo zake na kumfungia chumbani."

“Ulimfungia kwa muda gani?”

"Kwa kawaida siku moja hadi mbili. Familia ya Kimaro haikuwa ikimjali, kwa hivyo hakuna mtu aliyejua. Asingekufa baada ya kutokula kwa siku mbili hata hivyo, siku ya tatu ndipo nilimfungulia na kumpa chakula kidogo.”

Afisa wa polisi alikasirika. "Je, ulifanya hivyo wakati wa baridi pia?"

“Ndiyo. Nilipoona kwamba angezimia nyakati fulani kutokana na baridi kali, mara moja nilimtoa nje na kuiambia familia ya Kimaro kwamba alikuwa na homa. Familia ya Kimaro iliniamini. Zaidi ya hayo, ukizingatia jinsi Alvin alikuwa mbali na kila mtu, wote walimchukia.”

Baada ya video ya dakika tano kumalizika, kimya kilitanda kwenye ukumbi huo. Waandishi wengi wa kike walikasirika. Lisa akashusha pumzi ndefu, na macho yake yalikuwa mekundu kidogo. “Ninachojaribu kusema ni kwamba hakumuua yaya. Alimchoma kisu tu kwa sababu alishindwa kujizuia na akajitetea dhidi yake baada ya kufungwa kwa siku tatu ngumu. Baadaye, alikaa katika hospitali ya magonjwa ya akili kwa miaka mitatu. Daktari alisema kwamba mara chache angerudia tena hali hii, kwa hivyo almiruhusu Alvin kurudi nyumbani.

“Hata hivyo, habari kuhusu hali yake na picha zake za zamani zilianza kusambaa jana. Hakika, ilipangwa kwa makusudi siku moja kabla ya mkutano huu wa waandishi wa habari ili kuvuruga tukio hili. Nilipotoka nyumbani leo, bado alikuwa amepoteza fahamu. Mkutano wa waandishi wa habari ulikaribia kusitishwa hivyo nikaamua nije mimi."

Ghafla macho ya Lisa yalizidi kuwa makali. "Ni wazi kwamba mtu ambaye alisambaza picha hizo kwa nia mbaya alikuwa anajaribu kuongeza jeraha kwenye moyo wa Alvin ambao tayari unavidonda. Tunaweza kushindana kama biashara, lakini hatuwezi kuvuka msingi wa maadili. Katika miaka hii yote, Alvin ametoa shilingi bilioni 200 kwa hisani, ameunda nafasi nyingi za kazi, na kusaidia familia nyingi. Amefanya kosa gani? Amewahi kuwaumiza nyie?"

Kila mtu aliyekuwepo kwenye mkutano huo alinyamaza. Mwanahabari aliyeanzisha mjadala huo hatimaye aliomba msamaha, “Ninaomba msamaha kwa Bwana Kimaro kwa kuuliza swali hili, sikuwa na nia mbaya ila nilitaka tu kujua. Samahani sana. Swali langu linaweza kuwa limekwenda mbali sana."

“Ni sawa.” Lisa aliinua midomo yake na kutabasamu kwa unyonge. Macho yake yakatua kwa mwandishi huyo wa Nairobi Financial Times. "Ikiwa nakumbuka vizuri, lilikuwa ni gazeti lako ambalo ilichapisha habari kuhusu hali ya Alvin na picha zake. Wewe pia ulikuwa wa kwanza kuanzisha mada hiyo hapa leo. Alvin amewakosea?”

Ripota kutoka Nairobi Financial Times alishuka. "Ninatimiza tu majukumu ya mwandishi."

“Kweli? Kama ripota wa habari za fedha, unaonekana kutaka kuchimba mambo ya kibinafsi badala ya kuniuliza maswali yanayohusiana na maendeleo ya kampuni na masuala ya kifedha,” Lisa alimdhihaki huku akicheka, “Familia ya Campos ilikulipa kiasi gani kutimiza jukumu hili?”

“Familia ya Campos?” Zogo lilizuka ukumbini hapo. “Familia ya Campos inahusikaje?"

“Chukueni hii kwa faida yenu.” Lisa alijiweka sawa. “Familia ya Campos ni familia ya baba wa Jack, na Jack ni mwenyekiti wa KIM International ambayo kwa sasa ina ushirikiano wa kibiashara na familia ya Campos. Familia ya Campos wanamdidimiza Alvin ili kudumisha nafasi ya Jack kama mwenyekiti wa KIM International na kulinda maslahi yao kwenye kampuni. Ni wazi, tukio hili linahusiana na familia ya Kimaro na familia ya Campos. Msisahau kwamba Alvinarah Company na KIM International sasa ni washindani wa biashara.”

“Jamani. Alvin ni wa familia ya Kimaro pia. Hawana aibu?"

"Kama wangekuwa na aibu yoyote, Alvin angenyanyaswa na yaya katika umri mdogo?"

"Kuna nini?! Wanafamilia ya Kimaro ni watu wa aina gani?"

Katikati ya mjadala mkali, ripota yule kutoka Nairobi Financial Times alijibu kwa haraka, “Familia ya Campos? Sielewi hata kidogo unachokisema.”

“Ni sawa. Utaelewa baada ya muda mfupi. Ukiwa mwakilishi wa chombo cha habari, ulieneza harakaharaka picha za faragha za Alvin mtandaoni na kumsababishia madhara kiakili. Nimeripoti suala hilo kwa polisi, kwa hivyo unaweza kwenda kujieleza huko hizo picha ulizipata wapi.” Lisa alisema kwa moyo mwepesi, “Tafadhali mchukueni, walinzi. Polisi wanasubiri nje.” Maneno yake yalimtia hofu mwandishi huyo. Wanausalama walimchukua bila kumpa nafasi ya kuongea.

Kwa jinsi Lisa alivyokuwa akishughulikia suala hilo bila huruma, waandishi wote waliokuwa pale ukumbini hawakuwa na ujasiri wa kuongea kizembe tena. Kila mtu alimtazama yule mwanamke aliyevalia mavazi meusi kama hakimu jukwaani. Aliweka uso usio na wasiwasi na alionyesha haiba ya kipekee na ya kiburi, ambayo ilimwacha kila mtu katika hofu.

Lakini, Lisa bado alitabasamu wakati huo. "Suala la kibinafsi limetatuliwa, kwa hivyo turudi kwenye japo husika lililotukutanisha hapa, Oceanic Cement. Baadhi ya watu wanashangaa kama teknolojia ya cement hii ilivumbuliwa na KIM International. Kwa kweli, haikuwa hivyo. Ilikuwa Team Simon iliyovumbua cement hii, na Alvin anamiliki hakimiliki yake. Kwa kuwa sasa Alvin ameondoka KIM International, ataomba kurejeshewa hakimiliki kwenye prototype ya bidhaa zote ambazo Team Simon ilivumbua ikiwa kwenye kampuni hiyo.”

Hili lilikuja kama pigo jingine kwa KIM International. Ikiwa hii ingetokea kweli, hakuna kampuni yoyote ambayo ingekuwa na ujasiri wa kufanya kazi na KIM International, ikizingatiwa kuwa kampuni hiyo isingekuwa na bidhaa yake yenyewe ambayo ni halisi.

Waandishi waliuliza kwa mshtuko, “Ina maana kwamba Bwana Kimaro anaingia kwenye vita na KIM International?”

"Hakutakuwa na vita vya aina yoyote. Kampuni ya Alvinarah inataka tu kurudisha mali zake.” Lisa alijibu kwa kujiamini. Hakukuwa na swali tena kutoka kwa waandishi, na zogo likatulia.

Tabasamu likatanda usoni mwa Lisa. "Acha niwajulishe nyote kuhusu undani wa Oceanic cement."
•••
Katika jumba la kifahari lililo kando ya bahari, Alvin alikuwa akimtazama yule mwanamke mrembo, aliyejiamini, akizungumza kupitia mtiririko wa moja kwa moja. Hakuweza kujizuia kuachia mshangao wake kwa kiburi. Hakika huyu ndiye mwanamke ambaye alikuwa amemtamani sana. Alijiuliza ni lini yule mwanamke mnyonge na mwenye aibu ameanza kukua na kuwa jasiri vile. Alikuwa na ujasiri na busara zaidi. Hapo zamani, Alvin alilazimika kumuokoa na kumlinda kila wakati kutokana na uzembe wake.
Sasa, alikuwa bora kama yeye!

Kutazama video hiyo, Chester alihisi utulivu. “Lisa ananiumiza vichwa vya watu. Nina kiwango kipya kabisa cha heshima kwake. Yeye ni mzuri. Anazungumza kitaalamu zaidi kuliko wataalamu.”

“Usiongee kama hujui huyo mwanamke ni wa nani.” Midomo ya Alvin haikuweza kuficha kiburi chake.

Chester alikosa la kusema. Je, ni kweli huyu ndiye mtu ambaye alikataa katakata kumwamini Lisa kabla ya hapo?

Hans alicheka na kusema, "Bi. Jones alitumia usiku mzima kukariri data. Alikuwa na wasiwasi kwamba waandishi wangemuuliza kuhusu maswala kuhusu teknolojia yake, kwa hivyo alipitia habari zote muhimu.

Sura ya huzuni ilivuka kwenye uso wa Alvin. Kwanini alilazimika kuhangaika sana? Alvin alimtazama Hans. "Mwanamke wangu alifanya karibu kila kitu. Kuna faida gani mimi kuwaweka nyie kwenye kampuni na kuwalipa pesa nyingi sana?”

Aliposikia shutuma hizo, uso wa Hans ukageuka kuwa jivu. Akiwa hana msaada, Chester alimtetea, "Jana usiku, Hans alikuwa na shughuli nyingi akitafuta video ya kukiri kwa yaya baada ya kukamatwa wakati huo."

"Lilikuwa wazo lako kupata video kuhusu kuhojiwa?" Alvin aliuliza huku akiwa ameinua kichwa chake.

Hans alijibu kwa kusitasita, “…Lilikuwa wazo la Lisa.”

"Ha, nilijua tu." Alvin hakuweza kuficha kejeli katika sauti yake. Hans hakuwa mjinga. Alijua kabisa kuwa kejeli ile ilikuwa inaelekezwa kwake.
Chester alikosa la kuongea. “Kusema kweli video ilirekodiwa miaka mingi iliyopita. Haikuwa rahisi kwa Hans kuipata.”

Sura ya: 229

Alvin alitoa sura ya kutoridhika. “Umenifanyia kazi kwa muda mrefu. Lakini kwanini hukuweza kushughulikia hili? Hupaswi hata kuitwa msaidizi wangu.”

Hans na Chester walibaki midomo wazi. Ilionekana kuwa mchango wao haukuthaminika na ni mke wake tu ndiye aliyeonekana kuwa mpambanaji zaidi. Aliupiga mwingi kiasi kwamba hakuna mtu angeweza kulinganishwa naye.

Mkutano na waandishi wa habari uliendelea kwa saa tatu. Baada ya kumalizika, Lisa alirudi kwenye jumba lao la ufukweni.

Dereva alipofungua mlango wa gari, Lisa alitoka na kumuona Alvin akiwa amesimama kwenye kingo kandokando ya bwawa la kuogelea. Alivaa suruali laini ya kitambaa na shati ambalo halikuchokewa ndani ya suruali yake kama kawaida. Alionekana akiwa amepumzika na kujisahau kabisa.

Upepo wa baharini ulipita nyuma ya shati lake na kulipeperusha taratibu.
Kwa mtazamo wa haraka haraka, alionekana kuwa mdogo kwa miaka kumi kuliko alivyokuwa. Alionekana kama mwanafunzi wa chuo kikuu, akionekana mpole na mtulivu. Hata hivyo, ngozi yake ilikuwa imepauka sana.

Lisa alitembea taratibu kuelekea kwa Alvin na kudhibiti mapigo yake ya moyo kabla ya kusema kwa tahadhari. “Nisamehe kwa kukiri ugonjwa wako hadharani. Utanilaumu kwa hilo?”

Alvin alipitisha mkono wake kwenye nywele zake na kumkumbatia. "Umefanya vizuri zaidi ya nilivyotegemea mke wangu."

"Hujachukia?" Lisa alishikwa na butwaa. “Nilifikiri ungekasirika kwa kukubali hadharani kuhusu ugonjwa wako?”

"Sitajali endapo utakuwa karibu nami." Alvin aliukunjua uso wake kwa tabasamu na kumkazia macho yake meusi. "Uko tayari kuwa karibu nami wakati wa matibabu yangu?"

“Ndiyo.” Lisa alikubali kwa kichwa na sauti.

“Lakini sina uhakika ni lini nitapona ugonjwa wangu. Pengine nisiweze kupona kamwe. Zaidi ya hayo, nimekuumiza mara nyingi. Ninahofia kwamba huenda nikapoteza tena udhibiti wakati fulani.” Macho ya Alvin yalidhihirisha wasiwasi na taabu.

"Alvlisa, mradi uko tayari kutibiwa ugonjwa wako, sitakuacha." Lisa aliuma mdomo kana kwamba amedhamiria. "Wacha tupate mtoto pamoja."

Alvin alishtuka. "Lakini hukutaka kuwa na mtoto hapo awali."

“Nimejadili hali yako na Dokta Choka, Alvlisa. Moyoni mwako unatamani kuwa na familia. Familia yetu sisi wawili itakuwa kamili tukiwa na mtoto." Lisa aliinua macho ya upole. "Ninaamini utaweza kusahau polepole kumbukumbu hizo chungu za utoto wako baada ya kupata mtoto pamoja."

“Asante, babe.” Alvin alimkumbatia Lisa kwa nguvu, macho yake yakamtoka. "Kwa hivyo ... twende tukatafute mtoto sasa?"

Kwa aibu, Lisa alimkandamiza kiunoni. “Ni mchana sasa. Huna aibu kwenda kujifungia chumbani na jua lote hili? Sijapata hata chakula changu cha mchana. Tutafanya baadaye, sawa?”

"Tutafanya baada ya chakula cha mchana, basi?"

“Alvlisa, hunihurumii? Nimekesha usiku wote wa jana kukariri data za mradi wako. Nimechoka eti!” Lisa alijifanya kuwa na hasira na kumkodolea macho.

“Nashukuru kwa bidii yako mpenzi,” Alvin alijibu kwa huruma.

“Hakuna maana kusema tu. Utanikanda mabega yangu baada ya kumaliza chakula changu cha mchana,” Lisa alimuamuru kabla hajaingia kwenye jumba hilo.

“Umesema nini?” Alvin alitilia shaka sana ikiwa alisikia vibaya.
‘Huyu mwanamke anathubutu vipi kuniamuru nimfanyie masaji?!’

“Hutanifanyia?” Lisa alimuuliza kwa sura iliyoshuka. “Kwa sababu yako, sikulala usiku kucha. Data nyingi nilizokariri bado zinaniumiza kichwa.”

Alvin alipoona sura yake ikiwa imepooza, alinyamaza kwa muda.

Baada ya kubadilisha slippers za nyumbani, Lisa aliingia kwenye chumba cha chakula. Shangazi Yasmine alimtengea chakua baada ya kukipasha moto.

Lisa aligeuza kichwa chake na kumtazama Alvin. "Nipakulie wali."

Alvin alimtazama kwa macho meusi. "Mimi ni mgonjwa sasa, sitakiwi kusumbuliwa."

"Kwani mikono na miguu yako imelemaa?" Lisa alipepesa macho na kumtazama juu chini.

"Hapana." Alvin alitilia shaka sana iwapo Lisa alikuwa akijaribu kumlipa kwa yale aliyomfanyia hapo awali.

"Ngoja nikupakulie, Bibi mdogo." Shangazi Yasmine hakujua ni nini kilikuwa kinaendelea kati yao. Aligeuka kuchukua hotpot la wali.

“Hapana, Shangazi Yasmine. Huu ni utani wa kimapenzi kati yetu.” Lisa alimnong’oneza Aunty Yasmine na kuegemeza kidevu chake kwenye mikono yake. Macho yake makubwa yenye kung'aa yalitua kwa Alvin kwa fujo. Macho yake yaliyeyusha moyo wa Alvin mara moja.

“Sawa, nitafanya hivyo.” Alvin alifungua hotpot na kuanza kupakua wali.

Kwa tabasamu, Lisa alimvuta pembeni Aunty Yasmine na kumnong’oneza kwa sauti ambayo Alvin hakusikia, “Ninajua kuhusu hali yake, lakini nadhani ni bora kumchukulia kama mtu wa kawaida katika maisha yetu ya kila siku. Kadiri tunavyokuwa wachangamfu kwake, ndivyo atakavyohisi hisia za kupendwa zaidi.”

Aunty Yasmine hatimaye alielewa. "Wewe ni mzuri, Bibi mdogo. Unajua Bwana Kimaro hajala. Lazima umshawishi ale baadaye."

Punde, Alvin alijaza sahani ya wali. “Mbona hujipakulii chakula?” Lisa alimuuliza.

“Nimekula kidogo. Sihisi njaa." Alvin aliweka sahani ya wali mbele yake.
“Unadanganya. Shangazi Yasmine aliniambia kuwa hujala chochote, kwa hivyo unahitaji kula kitu. Lisa akamlazimisha kuketi. "Lazima ule kidogo."

“Sijisikii kula…”

“Ngoja nikulishe.” Lisa alichota kijiko cha wali uliomwagiwa njegere na kumwekea mdomoni. Alipotafuna akamlisha na kipande cha nyama ya kuku. Alikuwa akiona ladha ya wali kuwa mbaya sana hapo awali, lakini kwanini ladha hiyo ilipendeza ghafla alipolishwa na Lisa?

“Nilishe zaidi,” Alvin aliendelea kumwagiza baada ya kunogewa.

"Jaribu na kula peke yako." Lisa alimwekea kijiko mkononi mwake.

"Hapana. Sijisikii kula.” Alvin alitazama pembeni, akionyesha uso wa kukaidi.

Lisa alikuwa hoi. Hakuonekana hivyo alipomlisha mara ya kwanza. Je, ni kwa sababu chakula alichomlisha kilikuwa na ladha tofauti? Alihisi ni madeko tu ya Alvin. Hata hivyo, asingeweza kumwacha na njaa. Bila kuwa na chaguo lingine, Lisa alimlisha na kula chakula chake kwa wakati mmoja. Bila yeye kutambua, Alvin alikuwa amekula sahani mbili za wali wakati yeye alikuwa na sahani moja tu.

Sura ya mshangao iliosha uso wa Aunty Yasmine. “Ni muda umepita tangu Bwana Kimaro kula wali mwingi kiasi hiki. Inaonekana anahitaji wewe umlishe, Bibi Mdogo.”

Lisa alikosa maneno, alijiuliza kwanini hakutambua upande huu wa kitoto wa Alvin enzi hizo.

Ghafla, alihisi kubanwa mabegani mwake. Aligeuza kichwa chake na kukutana na macho machachari ya Alvin. "Uliniambia nikufanyie masaji baada ya chakula cha mchana, sivyo?"

“Ndio.” Lisa alifarijika kidogo. Angalau jitihada zake za kumlisha hazikuwa bure. Muda mfupi baadaye, alipiga kelele kwa uchungu, “Fanya taratibu basi! Unaniumiza!"

"Mbona nafanya taratibu sana?"

“Hapana, tafadhali usinikande mabega yangu tena. We unafanya utadhani ukanda unga wa chapati? Inauma sana.” Lisa aliikwepa upesi mikono yake kama shetani. “Nifanyie kitu kingine badala yake. Nisaidie kufua nguo zangu kwa mikono baada ya kuoga."

"Nini?" Alvin aliuma meno. “Lisa, unajaribu kunilipiza kwa ajili ya kazi nilizokufanyisha wakati huo? Kama vile kufua nguo na kusafisha nyumba?”

“Uko sahihi. Hiyo ni kwa sababu ulinitesa hivyohivyo hapo awali.” Lisa alitoa ulimi wake nje kwa namna ya kucheza. "Nataka upate machungu ya mambo uliyonifanyia hapo awali."

Kwa kicheko kibaya, Alvin alimbeba na kuelekea juu. “Sawa, ngoja nikakuogeshe.”

"Hapana. Niache mara moja, wewe mpuuzi!” Kicheko kitamu cha wanandoa hao wachanga kilisikika kutoka juu.

Kwa hayo, ahueni ikamshinda Aunty Yasmine. Ilikuwa ni busara sana kwa Lisa kukabiliana na hali ya Alvin kwa njia hiyo. Aunty Yasmine hakutarajia kuwa Alvin angeweza kupata furaha nyingi kiasi hicho.

Dakika 40 baadaye, Lisa alitoka bafuni baada ya kuoga vizuri. Alikaa mbele ya dressing table akikausha nywele zake. Baada ya kukausha nywele, alirudi bafuni.

Alvin alikuwa amekaa bafuni, akimsaidia kusugua… chupi yake.

“Lisa ulikuwa umelowa ndani ya sekunde chache tu?” Alvin alimtania huku akipekecha chupi yake sehemu ya katikati. Lisa hakuwa na tabia ya kufua chupi. mara zote alivaa chupi na sidiria zake mara moja tu kama pedi. Hata hivyo siku hiyo aliamua tu kumfanya Alvin afue kama utani wa kimapenzi tu.

Katika muda usiozidi nusu siku, Hans alirudi na baadhi ya matokeo. “Maurine Langa hakika ni binamu wa Sarah Nelson Langa. Alikuwa akisoma nje ya nchi na hivi karibuni alirudi nyumbani. Tangu kifo cha mama yake, familia ya Langa imekuwa haifanyi vyema chini ya unyanyasi wa familia ya Nelson. Maurine anabaguliwa hospitalini pia na kila mara hupewa jukumu la kuwaangalia wagonjwa wenye jeuri na fujo. Lakini, utendaji wake hospitalini umekuwa mzuri sana. Sio tu kwamba yeye ni mvumilivu bali pia ana mawazo yenye nguvu ya kuvumilia magumu.”

Sura ya 230

Hata hivyo, Lisa hakuwa na haya kama alivyokuwa wakati huo. “Acha. Nitafua mwenyewe.” Alimsogelea na kumfukuza.

"Hapana. Nataka nipate mateso ambayo mke wangu alipitia hapo awali,” Alvin alijibu kwa mzaha baada ya kuona uso wake ukiwa umekunjamana.

"Hujui jinsi ya kufua." Lisa aliingiwa na aibu na kero. “Huwezi kuisugua hivi. Usiiharibu.”

“Basi, nifundishe.” Alvin aliinua uso wake na kujifanya kama mtoto mzuri ambaye alikuwa tayari kujifunza.

Kwa mara ya kwanza, Lisa alijua maana ya kujipalia makaa yeye mwenyewe. Aliuanzisha mchezo lakini Alvin akawa mchezaji mzuri kuliko yeye.

"Harakisha." Alvin alimhimiza.

Akiwa hoi, Lisa aliketi kando yake na kumuongoza. “Isugue ndani nje…”
Baada ya Lisa kumwangalia mwanamume huyo akiosha chupi yake kwa uangalifu chini ya uongozi wake, kila aina ya hisia zilimjaa akilini.

Baada ya kuanika chupi hiyo, Alvin aligeuka nyuma na kuyaona macho ya mwanamke huyo ambayo yalitoa hisia kali za huba. Ilikuwa ya kufurahisha na kuudhi kwa wakati mmoja. “Umefurahi?”

“Bila shaka. Ni kwa sababu kuna mtu alinifulia nguo kwa mara ya kwanza.” Mdomo wa Lisa ulitetemeka. Ingawa alikuwa katika uhusiano na Ethan kwa miaka kadhaa nyuma, wawili hao hawakuwa wamewahi kuwa wa karibu namna hiyo.

Kabla ya hili, Lisa alikuwa amesikia tu wanawake kwenye mtandao wakijisifu kuhusu wapenzi wao wanaofua chupi zao. Alipokutana na Alvin, hakutarajia kabisa kwamba mwanaume mwenye kiburi kama yeye siku moja angefua nguo zake za ndani.

"Umewahi kupata wanaume wangapi wa kufua nguo zako za ndani?" Alvin alimbeba juu juu na kumuweka kitandani. Kisha akamuonya, “Unatakiwa kujisikia mwenye bahati kwamba hukuruhusu Ethan na Kelvin kufua nguo zako za ndani. Vinginevyo, ningeikata mikono yao.”

“Hakika nisingewaruhusu wanifulie nguo yangu ya ndani. Ninakupenda wewe tu.” Lisa akauzungusha mkono wake shingoni na kuchukua hatua ya kumbusu kwenye midomo. "Nakupenda, Alvilisa."

Akiwa amekabiliana na utani wake, wimbi la hisia lilimkumba Alvin ndani kabisa. Akaunyoosha mkono wake na kumbana pua yake. "Una uhakika?"

“Ni lini sikuwa serious?” Lisa aligeuka kuwa mnyonge. Kwa kweli, alikuwa akikiri mapenzi yake kwake.

"Zamani?" Macho ya Alvin yalitiwa giza. "Uliniambia kila wakati jinsi ulivyokuwa unanipenda kabla ya hii. Lakini kumbe yote yalikuwa uwongo." Lisa alijisikia vibaya. "Bado siwezi kujua wakati unasema ukweli na wakati unasema uongo. Afadhali kuwa mkweli na mimi. Ulianza kunipenda lini?” Alvin alimtazama kwa hasira. "Afadhali uniambie ukweli."

Lisa aligusa pua yake kwa aibu. "Huwezi kuwa na hasira baada ya kukuambia, sawa?"

“Ndio. Nimejipanga kiakili.” Alvin alionekana kutojali.

“Pengine… muda ulioniokoa nilipokuwa karibu kujeruhiwa kwenye eneo la ujenzi…”

“Kwa hiyo mambo yote uliyoniambia kabla ya hapo yalikuwa ya uwongo?” Alvin alishindwa kujizuia. Kwa kweli alikuwa amemdanganya kwa muda mrefu sana na kumchukulia kama mpumbavu.

“Lo… Hapana. Acha nifikirie tena. Pengine ilikuwa wakati uliniokoa kutoka kwenye jumba letu la ukoo…” Lisa aliingiwa na hofu kuuona uso wake uliopauka. “Oh, hapana. Labda ilikuwa wakati ulipoingia hotelini ili kuniokoa baada ya kunyweshwa dawa…”

“Ilikuwa lini hasa, mbona unanichanganya?” Alvin alishindwa kumvumilia sasa. Alianza kujisikia hasira. "Afadhali usianzishe ugonjwa wangu."

Lisa akaizungushia mikono yake mwilini mara mwake moja. “Hata mimi sina uhakika. Labda upendo wangu kwako ni kama nukuu hii kutoka kwenye kipande cha muvi ya ‘WHEN HARRY MET SALLY’--‘Unapogundua kuwa unataka kutumia maisha yako yote na mtu, unataka maisha yako yote yaliyobaki yaanze haraka iwezekanavyo'.”

Alvin alitabasamu. "Kazi nzuri. Umejifunza nukuu nyingi kutoka kwenye sinema za mapenzi, huh? Tulipokutana kwa mara ya kwanza, ulinichezea kimapenzi kwa nukuu tamutamu, 'Siwezi kujizuia kujisikia furaha kwa kuwa nimekutana na mpenzi wa maisha yangu'. Niambie nini kingine unajua. Jaribu na uniambie sasa hivi.” Kumbukumbu yake kali ilimwacha Lisa hoi. Yeye mwenyewe alikuwa kisha sahau kama aliwahi kumwambia Alvin maneno hayo.

Hatimaye, alijihisi mnyonge na akaizungushia mikono yake shingoni mwake kwa shauku. “Samahani, mume. Hata hivyo, sisemi uwongo kwa sasa. Sasa kwa kuwa unataka nikuambie nilipoanza kukupenda, siwezi kubainisha kwa wakati maalum. Pengine ilikuwa katika moja ya siku hizo tulipokaa pamoja. Inaweza pia kuwa wakati uliniokoa kishujaa tena na tena. Kufikia wakati nilipopata fahamu, tayari nilishaanza kukupenda.”

Maneno yake yaliyeyusha moyo wa Alvin. “Kweli?”

“Ndio. Kwa kweli, nilipokutana na wewe kwa mara ya kwanza, nilifikiri kwamba wewe ndiye mwanamume mzuri zaidi ambaye sijawahi kukutana naye katika maisha yangu, lakini hukuwa na moyo wa kimapenzi. Siku zote ulinitendea kwa dharau na hata kunifanya nilie kwa hasira mara kadhaa. Vinginevyo, ningekuangukia mapema zaidi. Kwa kweli, ilikuwa rahisi kwako." Lisa alishika mashavu yake yenye kupendeza. Uso wake ulionekana katika macho yake.

Alvin alimbusu kwa mahaba kwenye midomo. “Unajivunia sana kutaniana na wanaume. Ulishawahi kuwachezea wanaume wangapi hapo awali?"

"Wewe tu. Utakuwa peke yako pia." Lisa alimkumbatia kwa nguvu.
Koo la Alvin likasogea, na sauti yake ikageuka kuwa ya kishindo. “Vizuri. Unanifanya nijisikie kuwa na mtoto na wewe.”

Uso wa Lisa ulikuwa unawayawaya. Akiwa anasitasita kuitikia kwa kichwa, simu ya Alvin ikaita ghafla. Baada ya kuitazama simu yake, alikunja uso na kuiweka pembeni ya sikio. Sauti ya hasira ya Mzee Kimaro ilisikika.

“Wewe mwanaharamu, endelea kumtazama mwanamke wako! Kwa hakika anaomba kurejeshewa hakimiliki za bidhaa za KIM International. Inaonekana anajiamini kupita kiasi kuliko uwezo wake.”

Lisa aliinua kichwa chake. Alvin alimtazama huku akitabasamu, lakini sauti yake ilikuwa na jeuri. “Nakubaliana na mke wangu.”

"Alvin, unajaribu kuifanya damu yangu ichemke?" Sauti ya Mzee Kimaro ilitetemeka.

“Babu, mwanzoni sikupanga kufanya unyama kama huu, lakini nyie ni wakatili sana,” Alvin alijibu bila huruma.

“Alvin, sijawahi kufikiria kukushambulia kwa hizo picha. Kwani wewe ni mjukuu wa familia ya Kimaro.” Sauti ya Mzee Kimaro ilijaa unyonge. “Unajua vizuri njia zangu. Hata kama ningepanga kukufanyia ubaya, nisingetumia mbinu za siri kama hizi.”

“Hiyo haimaanishi kwamba watoto na wajukuu zako wengine hawatafanya hivyo,” Alvin alijibu kwa upole, “Kama unavyojua, mimi ndiye wakili mahiri zaidi hapa nchini na sijawahi kupoteza kesi yoyote. KIM International pia haiwezi kunishinda hata kama mtaenda mahakamani.”

Kulikuwa na muda wa kimya kimya upande wa pili wa simu. Mzee Kimaro aliuliza kwa unyonge, “Unataka nifanyeje ili uachane na harakati hizi? Niambie masharti yako.”

“Ni rahisi. Nataka tu mamlaka na hisa zako. Ninataka kuiongoza KIM International katika siku zijazo. Pia, msinisumbue kuhusu ndoa yangu na mke wangu.” Alvin alisema kwa upole, "Ninaamini tayari unafahamu kwamba cement ya Alvinarah Corporation imezalisha mauzo ya zaidi ya shilingi bilioni moja nchini kote ndani ya masaa matatu tu baada ya kuzinduliwa. Zaidi ya hayo, tumetia saini makubaliano na makampuni mengi ya kigeni kufanya kazi pamoja. Bila hakimiliki ya Oceanic Cement, KIM International italazimika kukoma kuendesha biashara yake ya saruji nchini kote. Nyinyi watu mnahitaji kuajiri timu nyingine ili kuvumbua cement mpya, ambayo itachukua angalau miaka miwili ya utafiti. Miaka miwili baadaye, je KIM International bado itashikilia nafasi ya kwanza?"

Kwa muda mrefu, Mzee Kimaro hakutoa neno lolote.

KIM International ilihusika katika nyanja mbalimbali, ikiwa ni pamoja na fedha, bima, mawasiliano na ujenzi. Kwa sababu ya ushindani mkali, hata hivyo, ilichukua asilimia 20 tu ya soko. Zaidi ya hayo, watu kama Spencer na Valerie walikuwa na uwezo mdogo wa kuendesha biashara. Familia zingine zingeweza kuipiku familia ya Kimaro kwa urahisi katika nusu mwaka, chini ya miaka miwili.

'Kama unamtarajia mama yangu…” Alvin alicheka ghafla na kusema, “babu, kwa kusema kweli, huoni kwamba Jack na mama yake wanapendelea familia ya Campos kupita kiasi? Miaka 20 iliyopita, mali ya familia ya Campos ilikuwa na thamani ya dola milioni kumi pekee.

Sasa, wameweza kuingia katika familia tatu tajiri zaidi nchini Kenya. Hata mama yangu hakuenda mbali katika kukuza kampuni yake.”

TUKUTANE KURASA 231-135

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…