mireille
JF-Expert Member
- Mar 4, 2020
- 529
- 589
- Thread starter
-
- #41
SIMULIZI........LISA
KURASA.. 136-140
Sura ya 136
Alvin alikaa kwenye siti ya nyuma ya gari lake. Alikuwa ametawaliwa na maamuzi ya hasira mapema asubuhi, lakini sasa ghafla alihisi njaa sana. Tumbo lilianza kumuuma tena. Aliwasha sigara kwa hasira. Ikiwa angejua kwamba hilo lingetokea, angemaliza kula kifungua kinywa chake kwanza kabla ya kupandisha hasira zake za kijinga.
"Bwana Kimaro, ngoja nikununulie chakula." Hans alimtazama kwa wasiwasi.
“Sina njaa. Nenda uniletee Lina Jones hapa,” Alvin alisema kwa upole, “Sikuzote nilitaka Lisa ashughulike naye, lakini haina maana sana. Nitamalizana naye mwenyewe.”
Hans aliitikia kwa kichwa. Ilionekana kana kwamba ingemlazimu kumuombea Lina kwa kile ambacho alihisi kilikuwa kinaenda kumkuta.
•••
Katika kampuni ya Mawenzi Investments. Lina alifukuzwa moja kwa moja na walinzi. Hakutaka kuondoka na kuishia kupiga kelele mlangoni, “Hata kama baba yangu alikamatwa, bado ana hisa kwenye kampuni na mimi bado ni mtoto wake. Nina haki ya kurithi hisa zake na kufurahia gawio langu.”
“Potelea mbali!” Yule mlinzi alimtemea mate isivyostahili. “Kila mtu anajua kuwa wazazi wako walimuua bibi mzee ili wapate hisa za Mawenzi Investments. Walimuua Mzee Madam Masawe. Hawana utu kabisa. Mwenyekiti Jones tayari ameomba mawakili wengi kurejesha hisa za Jones Masawe. Utarithi nini? Endelea kuota!"
"Subiri. Nitakaporudi Mawenzi, nitafanya maisha yako kuwa mabaya zaidi kuliko kifo. Lina alitetemeka kwa hasira.
Hata mlinzi alithubutu kumdhalilisha sasa. Kweli dunia haikuwa ya haki. Ni wazi alikuwa ametuma picha zote za uchafu za Lisa na Kelvin kwa waandishi wa habari jana yake, lakini sio tu kwamba ilishindwa kuharibu sifa ya Lisa, bali watu walianza hata kumuoanisha na Kelvin sasa. Ilikuwa inakasirisha sana na kukatisha tamaa.
Alitembea kando ya barabara wakati gari lisilo na nambari ya leseni lilisimama ghafla mbele yake. Kisha, watu wawili wakamsukuma moja kwa moja kwenye gari.
"Unafanya nini?" Kabla Lina hajajibu, alifunikwa kwenye gunia na kupoteza fahamu. Muda si muda, ndoo ya maji baridi ilimwagiwa juu yake na akapiga kelele kutokana na baridi. Gunia lilipasuliwa.
"Baridi ilikuwa nzuri?" Hans alimtazama kutoka juu.
Lina alitazama juu na kufikiria kuwa anaonekana kuwa mzoefu kidogo. Baada ya muda, alimkumbuka. "Ni wewe. Wewe ni msaidizi wa Alvin Kimaro…”
"Ni vizuri kukumbuka." Hans aliachia tabasamu hafifu. Akageuka pembeni, akamfunua mtu aliyekaa kwenye sofa ambalo halikuwa mbali. Mwanaume huyo alivalia suti nyeusi na kushika sigara mkononi, moshi ukitanda hewani. Macho yake ya wino yaliangaza na mwanga mweusi uliokuwa mkali kama kisu. Mwanamume huyo alitoa sauti ya kutisha.
Lina alimtambua. Hofu isiyoelezeka ikapanda kutoka ndani ya moyo wake. "Bwana. Kimaro, unajishughulisha na kazi ya kisheria. Unataka kunyang'anywa leseni yako kwa kuvunja sheria? Ninakuonya, afadhali uniache mara moja, la sivyo sitakuacha kamwe.”
Hans alicheka kana kwamba amesikia mzaha.
“Unacheka nini? Huwezi kuelewa nilichosema?” Lina alicheka. “Hebu niambie, haufahamu kuwa mimi ni mwanamke wa Willie Kimaro? Unajua Bwana Kimaro ni nani? Unajua kuwa ananipenda sana? Ikiwa huniamini, unaweza kuchukua simu yangu na kuangalia picha zetu pamoja.”
Alvin alimaliza kuvuta sigara na kuitupa kwenye sinia ya majivu kabla ya kuinuka. Mwili wake mrefu ulitembea polepole kuelekea kwake. Lina alifikiri anaogopa na akacheka. “Alvin Kimaro, wewe ni mwanasheria tu. Willie Kimaro si mtu ambaye mtu kama wewe unaweza kudiriki kumuudhi—”
Kabla hajamaliza, Hans alimpiga kofi kwenye shavu na kumng'oa jino mdomoni. Lina alipiga mayowe, “Willie hatakusamehe—”
Smack! Kofi jingine likasikika. Baada ya makofi kadhaa, Lina alipoteza meno machache na hakuthubutu kuongea tena.
"Nyamaza." Hans alitabasamu. “Unafikiri Willie Kimaro ni nani? Hujaelewa kwa nini Willie alibadili mtazamo wake kwako haraka hivyo?”
Lina aliganda. Alimtazama Alvin na ghafla akakumbuka kuwa jina lake la mwisho lilikuwa Kimaro pia. “Hilo haliwezi kuwa. Sijawahi kusikia mtu anaitwa Alvin katika familia ya Kimaro."
“Unawajua watu wangapi katika familia ya Kimaro?" Hans alidhihaki. “Acha nikwambie, Alvin Kimaro ndiye kaka mkubwa katika familia ya Kimaro. Amekuwa akisimamia familia tangu akiwa na umri wa miaka 20.”
Ubongo wa Lina ulivuma kana kwamba anaota. Kila mtu alijua kwamba kaka mkubwa, wa ajabu wa familia ya Kimaro alikuwa mtoto wa Leah Kimaro. Mtu huyo alikuwa mtu wa chinichini sana, lakini mbinu zake za ukatili zilijulikana sana. Aliingia katika kampuni hiyo akiwa na umri wa miaka 20. Mjomba wake wa pili alipokaidi, alimvunja mguu wake mbele ya umati.
Baada ya kuchukua jukumu la kuongoza KIM International, alipanua biashara yake hadi ng'ambo kwa kasi ya radi na hata akaingia katika nyanja za mawasiliano, fedha, na teknolojia kwenye masoko ya nje ya nchi kwa haraka haraka. Kwa wakati huo, alikuwa ameingia kwenye orodha ya watu miamoja tajiri zaidi Afrika, akiachwa kwa karibu sana na kina Dangote, Mo Dewji, Bhakresa na wengineo. Kulingana na uvumi, alikuwa mtu wa tatu tajiri zaidi nchini Tanzania na pia wa kushangaza zaidi.
"Hiyo haiwezekani. Unasema uwongo!” Lina alikuwa akiingiwa na wivu. Lisa alimkamataje mtu kama huyo?
“Kwa nini nikudanganye? Huyo mjinga Willie Kimaro aliogopa sana hivi kwamba alikojoa kwenye suruali yake alipomwona Bwana Kimaro. Hans alifoka. “Lina Jones, Bwana Kimaro hakutaka kushughulika na wewe mara ya kwanza, lakini hukupaswa kumpa Lisa Jones dawa ya kulevya. Na kwa kweli hukupaswa kutoa picha hizo kwenye vyombo vya habari.”
Lina alishtuka. Alipiga magoti mbele ya Alvin na kutetemeka. “Bwana Kimaro, mimi ni mjinga. Nilikuwa mjinga. Tafadhali nisamehe sana.”
Alvin akampiga teke kwa kuchukia. Ujeuri wa macho yake ulidhihirisha kwamba hakutaka chochote zaidi ya kumwangamiza kabisa. “Unadhani nitakuacha ukipumua?”
"Hapana, hapana, hapana. Haikuwa mimi. Sikupiga picha.” Lina akatikisa kichwa kwa hofu. “Nilitumiwa na mtu nisiyemjua. Ni kweli nilimpa Lisa dawa usiku huo, lakini Kelvin Mushi alipokuja, kamera ya video iliyokuwa chumbani iliharibiwa.”
“Hukuwa wewe?” Uso wa Alvin ulikaza zaidi huku alama ya mshangao ikimulika machoni mwake, akiamini hadaa ya Lina.
"Naapa." Lina alikuwa amepoteza meno kadhaa na mdomo wake ulikuwa umejaa damu. “Kama ningekuwa na hizo picha ningezitumia kumtishia Lisa zamani. Ningewezaje kumruhusu kukaa katika nafasi ya mwenyekiti kwa muda mrefu hivyo na kuwaweka wazazi wangu jela?”
“Kiapo chako hakina thamani.” Uso wa Alvin ulizidi kutisha, lakini aliamini maneno ya Lina. Ikiwa hakuwa yeye, basi ni nani?
Alikuwa na wazo, na midomo yake ikachanua katika tabasamu. Usiku huo, mbali na Lisa, ilionekana kana kwamba kulikuwa na Kelvin pekee. Kwa Kelvin Mushi haikuwa rahisi hata kidogo kwa Lisa kumshuku. Lisa alijua kwamba anampenda, lakini bado alikuwa tayari kuendelea kuwa na urafiki naye. Kelvin alikuwa ameenda ng’ambo kufungua ofisi ya tawi alipokuwa kijana, kama yeye tu. Anawajua watu wenye uthubutu wa kuvuka mipaka na kwenda kufanikiwa nje ya nchi huwa wajanja wajanja sana. Alvin hakumwamini Kelvin hata kidogo.
Lina alijua kwamba alimwamini na akasema kwa haraka, “Bwana Kimaro, tafadhali niruhusu niende. Ninaahidi sitomsumbua Lisa tena. Nitaondoka Dar es Salaam.”
“Unadhani nitakuacha uondoke kwa amani?” Alvin alitabasamu kwa giza. “Nimechunguza mambo yako. Ulikulia kijijini baada ya kuibiwa ukiwa mtoto mdogo, ukatolewa usichana wako na mwanakijiji ukiwa na umri wa miaka 15. Baadaye katika shule ya sekondari, ulifumaniwa zaidi ya mara kumi na waume za watu. Uliwekwa kinyumba na tajiri mmoja na hata kutoa mimba zisizo na idadi. Ni aibu iliyoje. Hukuwa na maisha mazuri hata baada ya kurudi kwenye familia ya akina Masawe.”
Uso wa Lina ulikuwa umepauka kwa aibu. Hii ilikuwa historia yake ya giza. Alikuwa ameifunika kwa makini sana, lakini mtu huyu kwa kushangaza aliweza kujua juu yake. Alikuwa anatisha sana.
"Kwa kuwa unapenda wanaume sana, nitakuozesha mume wa kuishi naye." Alvin alisema na kuondoka bila kuangalia nyuma.
Punde, mzee mfupi na mbaya mwenye umri wa miaka 50 aliingia. Alipomwona Lina, alimeza mate ya uchu. "Bwana Kimaro, unaniruhusu nimuoe?"
Lina alimtazama Hans kwa uso wa kutisha. “Usimruhusu anioe. Nitakwenda na wewe. Unaweza kufanya chochote unachotaka. Unaweza kunifanya vile Willie alinifanya pia!”
Hans alikwepa nyuma kwa kuchukizwa. “Usinishike, nachukia mambo machafu. Usimwogope sana. Anaonekana kuwa mzee, lakini ana umri wa miaka 40 tu na amekuwa peke yake kwa miaka kadhaa kwa sababu hakuweza kupata mke. Utamfuata kijijini na kumpatia mtoto.”
Kisha, Hans akaondoka, akimuacha Lina nyuma. Alilia kwa kukata tamaa, lakini hakuna mtu aliyemjali. Wakati huo, alijuta sana. Hakupaswa kumlazimisha Lisa Jones kuondoka nyumbani wakati huo. Hakupaswa kumsukuma Bibi Madam Masawe chini ya ngazi.
Lakini, hakuna na dawa ya majuto katika ulimwengu huu.
Sura ya 137
Katika mlango wa kituo cha polisi, Lisa alikuwa amemaliza tu kurekodi ushahidi wake mara ghafla akasikia mtu akiliita jina lake.
“Lisa.” Aligeuka nyuma na kumuona Kelvin akija kwake huku akiwa na tabasamu usoni mwake. Hali ya hewa ilikuwa ya baridi, na alikuwa amejifunika kitambaa shingoni.
"Ni bahati tu nimekuona. Kwa nini upo hapa?” Lisa alilazimisha tabasamu kumsalimia. Kila alipokuwa akimuona, alizikumbuka picha zile na mgogoro kati ya Alvin na yeye.
"Kuna jamaa wa nyumbani alifanya tukio la ajabu, kwa hivyo nilikuja kumdhamini." Kelvin alionekana hoi. "Nilisikia kwamba Jones Masawe na Mama Masawe walikamatwa hivi majuzi. Je wewe…”
“Ndio, polisi waliniita hapa kuchukua maelezo yangu. Kesi hiyo itafikishwa mahakama wiki ijayo kisha watasomewa hukumu.”
"Hongera, hatimaye umelipiza kisasi kwa bibi yako." Kelvin alifurahi kusikia hivyo.
“Asante.” Tabasamu la Lisa halikumfikia machoni. Alionekana kuchoka kabisa.
Kelvin alitembea pamoja naye kuelekea sehemu ya maegesho, huku akimtazama njiani. “Unaonekana umechoka. Umekuwa ukipumzika vizuri kweli? Na Alvin bado hajakuelewa tu…?!”
"Hatuwezi kuzungumza juu ya hili?" Lisa alimkatisha.
"Ni kosa langu." Kelvin alionekana kuwa na hatia.
“Kosa lako kivipi? Ulinisaidia usiku ule. Kama si wewe, ningefanyiwa ukatili mbaya na pengine ningeweza kujiua muda mrefu uliopita. Jana, hata ulishirikiana nami kufafanua hali ilivyokuwa na kuokoa sifa yangu. Ninapaswa kukushukuru,” Lisa alitikisa kichwa na kusema kweli.
Wawili hao walizungumza huku wakitembea. Lakini kijana mmoja aliibuka kando yao ghafla na hawakumjali, wakidhani ni mpita njia tu. Hata hivyo, ghafla mwanamume huyo alitoa kisu cha matunda kutoka kwenye mfuko wake wa suruali na kukichoma kuelekea kifuani kwa Lisa.
“Lisaaa!” Kelvin aliona Lisa amechelewa sana. Alipoona kile kisu kinataka kumchoma, alinyoosha mkono haraka kukizuia, na kisu hicho kikapenya kwenye mkono wake.
Wakati Lisa anajibu, mtu huyo alikuwa amechomoa kisu haraka ili kumchoma Lisa tena. Kelvin angeweza tu kutumia mwili wake kumkinga, na kisu kikapenya sehemu ndogo ya mgongo wake.
“Msaada!” Lisa alilia. Kwa msukumo aliushika mkono wa mwanaume huyo. "Wewe ni nani?!”
“Hutakiwi kunifahamu. Ni kosa lako kuwa mwanamke wa Alvin Kimaro. Nimekuwa nikikufuatilia kwa muda mrefu sasa.” Mwanaume huyo alifichua uso wake wa kutisha huku akiendelea kudunga kisu kwenye mwili wa Kelvin kana kwamba alikuwa na wazimu.
Kwa bahati nzuri, walikuwa karibu na kituo cha polisi. Polisi mmoja alisikia kilio cha kuomba msaada na haraka akakimbia ili kumshika mhalifu.
Punde, ambulensi ilifika na upesi ikampeleka Kelvin hospitalini. Hata hivyo, tayari alikuwa amepoteza damu nyingi njiani na kupoteza fahamu. Lisa alipiga simu kwa haraka kwa Ethan, ambaye alikimbia mara baada ya Ambulance kufika hospitali.
Mlango wa Emeregence Room ulisukumwa, na daktari akatoka na fomu mkononi. “Kisu kilichomwa kwenye figo ya kushoto ya mgonjwa na inabidi itolewe mara moja ili kuokoa maisha yake. Familia ya mgonjwa iko wapi? Tafadhali saini mara moja.”
Lisa alipigwa na butwaa. Ethan pia aliona ni vigumu kukubali. "Daktari, lazima ni lazima figo iondolewe? Kwani hakuna namna nyingine?"
"Necrosis tayari imeingia kwenye figo ya kushoto, kwa hivyo haina maana sasa," daktari alisema bila msaada, "Kama tungeweza kuiokoa, bila shaka tungeiokoa."
Ethan hakuwa na la kufanya zaidi ya kuvumilia maumivu na kusaini zile karatasi. Lisa alitoa machozi ya uchungu. “Yote ni makosa yangu. Mtu huyo alitaka kuniua. Mjomba wako ndiye aliyetumia mwili wake kunisaidia kuzuia kisu."
Ethan alikuwa na hisia tofauti. Hakutarajia Kelvin angekuwa na hisia za kina namna hiyo kwake. Sasa, pia alikuwa na wasiwasi sana kuhusu usalama wa Kelvin. Angeweza tu kusema, “Usifikirie juu yake. Daktari alisema kuwa kuondoa figo yake kutaokoa maisha yake. Mwili wa mwanadamu bado unaweza kufanya kazi na figo moja tu. Anapaswa kuwa mwangalifu zaidi katika siku zijazo."
Lisa alitabasamu kwa uchungu. Kelvin alikuwa anaenda kupoteza figo. Angewezaje kuwa mzima kama hapo awali? "Umewajulisha babu yako?"
“Hapana, babu na bibi wamezeeka na sitaki kuwapandisha presha. Tusubiri hadi upasuaji wa Mjomba umalizike.” Ethan alimtazama na kuhema moyoni mwake. Aliogopa hasa kwamba babu na bibi yake wangezimia ikiwa wangejua ukweli.
Kwa bahati nzuri, saa tatu baadaye, Kelvin aliokolewa. Operesheni ilikuwa imekwisha, lakini bado hakuweza kufumbua macho.
Muda si muda, polisi walifika hospitalini. Walipomwona Lisa walimwambia. “Bi. Jones, tumemhoji mhalifu. Mtu aliyetaka kukuua anaitwa Zigi Kabwe. Yeye si mwenyeji wa hapa Dar.”
Lisa alikasirika. “Hata simfahamu mtu huyu.”
Afisa huyo alitikisa kichwa. “Kulingana na maelezo yake, alikuwa na dada yake pacha anayeitwa Lily Kabwe. Miaka mitano iliyopita, Lily Kabwe alikuwa na umri wa miaka 17 tu, lakini alivutia macho ya Thomas Njau kutoka kwa familia ya Njau huko Nairobi. Thomas alimbaka Lily kwa nguvu baada ya kukataa kulala naye na akaamua kujirusha hadi kufa kutoka kwenye jengo kutokana na fedheha. Familia ya Kabwe ilimshtaki Thomas. Wakati huo, kulikuwa na karibu ushahidi kamili, lakini familia ya Njau ilimwajiri Alvin Kimaro kutetea kesi yao. Alvin Kimaro alidai kuwa Lily alimtongoza Thomas lakini Thomas alimdharau, hivyo akaamua kujiua kwa sababu ya unyonge wake. Mahakama haikushindwa tu kumwadhibu Thomas, lakini hata ilimfanya Lily aonekane kama mtu duni asiye na maana. Mama yake hakuweza kuvumilia na na akapata presha. Amefariki hivi karibuni…”
Lisa alishtuka. Alijua tu kwamba Alvin hawezi kushindwa mahakamani, lakini hakujua kwamba alikuwa amechukua kesi nyingi zisizo na moyo wa utu. "Kwa hivyo, alitaka kuniua ili kulipiza kisasi kwa Alvin Kimaro?"
“Ndiyo. Alitoweka miaka mitano iliyopita baada ya kesi hiyo, na tuligundua tu kwamba alirudi Dar es salaam mwaka huu. Alitaka Alvin Kimaro ajue uchungu wa kufiwa na mpendwa wake, lakini… Alvin Kimaro amezungukwa na walinzi na ni mwangalifu sana, kwa hivyo Zigi Kabwe ameshindwa kutimiza lengo lake licha ya kujaribu kwa miaka kadhaa.”
Afisa huyo alimwambia, “Amekuwa akikufuata kwa muda, lakini umekuwa ukilindwa na mlinzi siku hizi za karibuni. Ni leo tu ndipo alipata nafasi hiyo kwa sababu hukuwa na mlinzi.”
Ghafla, Lisa alionekana kugundua kitu. Siku chache zilizopita, Alvin alikuwa amepanga ghafla Shani afuatane naye kama mlinzi wake. Haikuwa kumlinda dhidi ya Jones na binti yake bali kumtazama Zigi Kabwe. Hata hivyo, hakumwambia chochote.
Haukuwa ulinzi wake hata kidogo. Kama Kelvin asingetokea siku hiyo, angekufa. Hofu isiyo na kipimo ikaufunika moyo wake. Lisa ghafla alifikiri kwamba hakumfahamu kabisa Alvin kama alivyodhani.
"Kwa nini kulipiza kisasi kwako kwa kile Alvin Kimaro alichofanya kwa mtu mwingine?" Ethan alikasirika. “Lisa, nakushauri ukae mbali na Alvin Kimaro. Nani anajua ni maadui wangapi amewachokoza kwa miaka mingi? Nilisikia huwa anaenda mahakamani kuwatetea matajiri tu, madhalimu na mafisadi, je ni haki za wangapi amedhulumu? Lazima atakuwa amepata pesa nyingi kwa njia isiyo halali."
Lisa alinyamaza, akiinamisha kichwa chini na uso wa huzuni. Moyo wa Ethan uliumia. Ikiwa asingefanya chaguo baya hapo kwanza, Lisa asingeangukia kwa Alvin
Sura ya 138
Saa nne usiku, Alvin aliingia kutoka nje akiwa na uso jeuri na mkali. Alipanda juu ndani ya dakika mbili kabla ya kushuka tena kwa haraka. "Lisa bado hajarudi?"
"Hapana." Shangazi Linda aliogopa kidogo sura yake.
“Mbona bado hajarudi?”
"Sijui. Yeye hapokei simu pia.” Aunty Linda alipomaliza kuongea, hali ya joto ndani ya jumba hilo ilionekana kushuka na kumfanya ashtuke.
Alvin akatabasamu kwa ujeuri. Vizuri. Hata baada ya kumsaliti na Kelvin, bado hakujua jinsi ya kuishi. Ilikuwa tayari saa nne usiku lakini hakuwa amefika nyumbani bado. Hata hakupiga simu nyumbani. Mwanamke huyo hakubadilika kamwe.
“Bwana Kimaro,” wakati huo, Hans alikimbia kutoka nje. “Nimepata habari. Zigi Kabwe alimvamia Miss Jones nje ya kituo cha polisi leo, lakini Kelvin Mushi alimzuia na kuchomwa visu vingi mwilini. Lisa yuko salama, lakini Kelvin amejeruhiwa vibaya na sasa anatibiwa hospitalini.”
Mwili wa Alvin uliganda pale pale huku macho yake meusi yakiwa yamemtoka ghafla. “Shani yuko wapi? Amechoka kazi? Si nilimwambia amlinde Lisa?”
Hans alipumua na kukumbusha kwa upole, “Bwana Kimaro, ulisahau? Ulipoona picha za Lisa na Kelvin kwenye vyombo vya habari siku moja kabla ya jana, ulishindwa na kumwambia Shani aache kumlinda Miss Jones. Ulimwambia Shani amwache Bibi Jones kwa hiari yake mwenyewe.”
'Nilimwambia asimlinde Lisa na kweli aliacha kumlinda Lisa? Ana akili timamu?" Alvin alishindwa kujizuia tena. Hans alikuwa kimya. Shani alifuata tu maneno ya Alvin kwa utii.
“Twende hospitali.” Alvin akatoka nje.
Baada ya kufika hospitalini, alivamia moja kwa moja hadi kwenye wodi ya watu mashuhuri. Kelvin bado alikuwa katika hali ya kukosa fahamu. Mrija wa oksijeni ulikuwa umefungwa kwenye pua yake, na Lisa alikuwa akifuta uso wake kwa kitambaa.
Tukio hilo lilimchoma macho Alvin bila huruma. Hapo zamani alipokuwa amelazwa hospitali, alikuwa amemtunza vile vile. Sasa, alikuwa akimtunza mwanamume mwingine.
"Njoo hapa," alimtazama na kusema polepole, "Tuondoke haraka."
Lisa aliacha harakati zake na kutikisa kichwa. “Bado hajaamka. siwezi kuondoka.”
"Lisa Jones, huelewi nilichosema?" Mwali wa hasira kweny moyo wa Alvin ukawashwa papo hapo. Sauti yake ilikuwa ya kikatili sana. "Ninakupa nafasi ya mwisho."
Sauti yake iliufanya moyo wa Lisa kusinzia. Alikaribia kuchomwa kisu hadi afe siku hiyo. Hakuona kuwa alikuwa ametapakaa damu? Je, aliwahi kumjali? "Alvin Kimaro, kuwa mwenye busara. Kama si Kelvin, ningekuwa maiti kufikia sasa. Alimlinda mpenzi wako. Ni sawa ikiwa huna shukrani yoyote, lakini mtazamo wako unawafanya watu wahisi kwamba wewe ni mnyama mwenye damu baridi.”
“Mimi ni mnyama mwenye damu baridi?” Alvin akapiga hatua kuelekea kwake. Alikuwa amemfanyia mengi, akimlinda mara kwa mara, hata kumpenda. Hata hivyo, alikuwa akimshutumu kwa kuwa na damu baridi? Maneno hayo mawili yaliupiga moyo wake kama kisu, na kusababisha maumivu yasiyovumilika.
"Unapaswa kuwa tayari umejua kwa nini Zigi Kabwe alitaka kuniua," Lisa alidhihaki, "Hivi kweli familia maarufu ya Kimaro ina ukata wa pesa kiasi kwamba unalazimika kupigania kesi isiyo ya haki kwa pesa hizo kidogo? Au ilikuwa kwa ajili ya umaarufu? Ulifika kileleni na kupata sifa uliyonayo sasa katika ulimwengu wa wanasheria kwa kuwakanyaga watu wengine?”
Alvin alikunja ngumi. Mishipa ya nyuma ya mkono wake ilitoka nje. "Lisa Jones, elewa hili. Mimi ni mwanasheria. Wanasheria hushinda au kushindwa tu. Mimi si mjumbe fulani wa haki.”
"Lakini mtu hawezi kuishi bila dhamiri." Lisa akatikisa kichwa. Ghafla aligundua kuwa yeye na Alvin walionekana kutoka dunia mbili tofauti kabisa.
“Nimekufanyia mambo mengi, lakini leo hii unasema sina dhamiri?”
Alvin alimtazama kwa hasira. Hajawahi kumtendea mwanamke kinyume sana hapo awali, lakini alipinga kila kitu katika sentensi moja. “Kwa sababu Kelvin alitoa maisha yake ili kukuokoa, kwa hiyo unataka kuwa pamoja naye? Ni kweli, siku zote amekuwa akikufuata.”
"Acha kuongea ujinga." Lisa alikasirika. "Amepoteza figo kwa sababu yangu. Siwezi hata kukaa na kumtunza? Hiki ndicho kitu kidogo zaidi ninachoweza kumfanyia baada ya kuokoa maisha yangu.”
“Sijali. Njoo tuondoke mara moja. Kelvin Mushi sio mtu mzuri kama unavyofikiria wewe. Kelvin ndiye aliyetuma picha hizo kwa siri kwa Lina. Alijifanya kama mtu mzuri juu ya uso lakini alicheza hila za siri gizani. Alikuwa ni mnafiki tu.” Alvin hakujali hata kidogo kuhusu hali ya Kelvin.
"Nadhani wewe ndiye ambaye sio mzuri." Lisa alikasirika.
Muda huo Ethan aliingia kutoka nje akiwa na nguo. “Lisa, nimekuletea nguo. Unapaswa kubadilisha haraka…” Kabla hajamaliza, akamuona Alvin na uso wake ukiwa mweusi mara moja. “Nani alikuruhusu kuingia humu? Ondoka haraka..."
Alvin alimtazama kisha akamtazama Lisa kabla ya kucheka ghafla. “Si ajabu hutaki kuondoka. Mpenzi wako wa zamani yuko pamoja nawe, na mpenzi wako mpya amelala kitandani. Una jozi hii ya mjomba na mpwa wake iliyozunguka moyoni mwako. Lazima uwe na furaha tele.”
"Nimekuozea, siku zote nimekuwa mtu kama huyo moyoni mwako." Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku mwili ukimtetemeka bila kuvumilika.
“Alvin Kimaro, umeenda mbali sana. Je, hilo ni jambo ambalo mwanadamu anaweza kusema?” Ethan hakuweza kuvumilia. Akatupa zile nguo pembeni na kumpiga ngumi Alvin. Alvin aliinua mkono wake kwa urahisi ili kuizuia, na Ethan akanguruma kwa hasira. “Hapana, wewe si binadamu hata kidogo. Lisa na mjomba wangu wamebeba tu matokeo ya matendo yako maovu. Walikaribia kupoteza maisha kwa sababu yako, lakini huna ubinadamu. Ondoka mbele yangu!”
"Nitaondoka, lakini sitaondoka peke yangu, lazima nimchukue mwanamke wangu." Alvin alinyoosha mkono kumnyanyua Lisa begani. Ethan alikimbia kumzuia, lakini Hans alimzuia haraka.
“Alvin Kimaro, niache! Usifanye hivi! nitakuchukia.” Lisa alianza kumpiga mgongoni, lakini Alvin alipuuza.
“Huchukii kuwa mimi ni mchafu? Je, huogopi kwamba nitakuchafua?” Lisa alipiga kelele.
Alvin akamshusha na kumtupa kwenye gari. Hans akawasha gari na kufunga milango. Lisa alijua kwamba asingeweza kushinda dhidi yake na akachagua kukaa mbali naye iwezekanavyo, bila kumwangalia hata kidogo.
Moyo wa Alvin uliudhika sana, akawasha sigara ili avute katika safari nzima. Lisa alikohoa mfululizo. Alijua kuwa hapendi kuvuta sigara hata kidogo kabla ya hii, lakini sasa, alikuwa akivuta sigara mara kwa mara. Hakupenda wanaume wanaovuta sigara, na hakupenda wanaume wasio na akili kama yeye hata kidogo.
Baada ya kufika nyumbani, Alvin alimbeba tena na kumtupa kitandani. Lisa alipanda na kusema kwa ujeuri, “Utanifunga tena? Alvin Kimaro, mimi ni mwenyekiti wa kampuni sasa. Kuna watu wengi nyuma yangu wananitegemea. Siamini kwamba utaweza kunifunga maisha yangu yote.”
“Kila saa ni ampuni, kampunii! kampuni, ni upuuzi tu kwangu.” Alvin alimuigiza kwa kubana pua. “Je, utaniamini nikisema nitaifunga kesho?” Alvin alifoka na kumpa jicho la pembeni. "Si tayari kabisa unajua utambulisho wa jina langu?"
Macho meusi ya Lisa yalitetemeka. Ilibadilika kuwa tayari alijua. Je, Willie Kimaro alimwambia? Yule mwongo aliyelaaniwa. Yeye ndiye alisema atamficha Alvin. Ingawa hakuwa wazi kuhusu utambulisho halisi wa Alvin katika familia ya Kimaro, pamoja na ujuzi wake, angeweza kweli kufanya hivyo. Familia ya Kimaro ilimiliki 25% ya hisa za kampuni hiyo, ukichanganya na ujuzi wake wa sheria, kufumba na kufumbua tu alikuwa anaukosa uenyekiti wake!
"Alvin Kimaro, ungekuwa na furaha zaidi ikiwa ningeuawa na Zigi Kabwe leo?" Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku machozi yakimtoka. "Ninamtunza Kelvin si kwa sababu ninampenda, lakini kwa sababu ninamshukuru."
“Sitakuruhusu umkaribie tena.” Macho ya Alvin yalikuwa yamepoa sana. Alikuwa na hisia kwamba ikiwa angemruhusu Lisa abaki na Kelvin kwa muda mrefu, angempoteza milele. Japo alikuwa amepoa kwake, bado hakutaka kutengana naye baada ya kujua kuwa alikuwa amenyweshwa dawa na Lina. Hata hivyo, hakuweza kuondoa fundo lililokuwa moyoni mwake. Bado alihitaji muda.
Sura ya 139
“Lisa Jones, kama kweli unanipenda, usiende kwa Kelvin Mushi tena. Hii ni nafasi ya mwisho ninayokupa.” Alvin alimtazama kwa kina, sauti yake ikisikika kwa ukali na kishindo.
Lisa alipigwa na butwaa. Ingawa alimchukia na kumkasirikia, bado moyo wake ulimpenda. "Na wewe je? Unanipenda?" Ikiwa alimpenda, kwa nini aliita jina la mwanamke mwingine wakati alikuwa amelewa?
"Naweza kukupenda, na ninaweza kuacha kukupenda wakati wowote." Alvin alisema bila kujali kabla ya kugeuka kuondoka.
Lisa alikaa kitandani huku akishangaa kidogo. Alvinaliweka wazi kuwa upendo wake unaweza kubadilika wakati wowote. Je, ni kwa sababu hakumpenda vya kutosha?
Katika chumba chake cha maktaba, Alvin alisimama mbele ya dirisha akiwa na glasi ya divai nyekundu, akitazama nje ya dirisha matone ya mvua yakishuka chini taratibu. Alitumaini kwamba Lisa alimuelewa. Ndio, ingawa alimpenda, ikiwa angetaka kuendelea kujihusisha na Kelvin Mushi, basi angeweza tu kuachana na upendo huo. Ingawa Kelvin alikuwa ameokoa maisha yake, Alvin alikuwa ameokoa maisha yake mara nyingi zaidi. Asingeweza kuvumilia kumuona mwanamke wake akimlipa fadhila kwa kumhudumia hospitali. Alvin alikunywa divai nyekundu kwa machungu.
Hans alisimama nyuma yake kimya. “Bwana Kimaro, kwa nini hukumwambia Bi Jones kuhusu picha hizo?”
“Kuna faida gani kumwambia? Je, angeniamini? Kelvin Mushi ndiye mwokozi wake sasa. Atafikiri kwamba ninamsingizia kwa makusudi kwa sababu simpendi,” Alvin alidhihaki.
Hans alikuwa kimya. Ilibidi akubali kwamba Kelvin Mushi alikuwa amedhamiria sana. Ili kumlinda Lisa, hata alitoa sadaka maisha yake. Ikiwa hata yeye angelikuwa mwanamke, angeliguswa pia.
Usiku sana, Lisa alioga na kukaa kitandani huku akiwa ameduwaa. Mwishowe, alichukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Pamela, akimwomba aende hospitali kumuona Kelvin kwa niaba yake.
Pamela : [[emoji2297]Usiniambie! Kelvin Mushi alipoteza figo kwa ajili yako? [emoji24][emoji22]Nini unadhani; unafikiria nini? Usichanganyikiwe tu, sawa?]
Lisa: [[emoji26]Sikuwahi kufikiria kwamba angefanya hivyo. Nina deni kubwa kwake. Sitaweza kumlipa maisha yangu yote.]
Pamela : [[emoji22]Hapana, usifikirie sana juu yake. Chukulia tu ni ajali ya kawaida. Ninapanga kumleta Patrick nyumbani kwa Krismasi. Kisha nitaandamana naye hadi kwa familia ya Jackson katika Mkesha wa Mwaka Mpya.]
Lisa: [[emoji39]Nyinyi watu mmesuluhisha matatizo yenu?]
Pamela : [Nilimchunia kwa nusu mwezi, na aliniahidi kukutana na Linda haraka iwezekanavyo katika siku zijazo. Nitamtambulisha mpenzi kwa Linda pia. Nataka kumpa Patrick nafasi moja zaidi. Ninampenda kupita kiasi.[emoji849][emoji849][emoji849]]
Lisa: [[emoji122][emoji122]Hongera kwa kumpata tena Bwana wako.]
Alipotuma tu ujumbe huo, mlango wa chumba cha kulala ulifunguliwa. Mkono wake ulitetemeka, na akazima skrini bila fahamu kabla ya kuweka simu chini.
“Unachat na nani?” Alvin alitoa harufu ya mvinyo mwekundu, na uso wake wote uliwaka kwa hasira. “Nionyeshe simu yako.”
Lisa hakuamini. Alvin hakuwahi kuangalia simu yake hapo awali, lakini alikataa kumpa kabisa. "Alvin, usiende mbali sana."
"Mbali sana? Nitajuaje kama unawasiliana na Ethan Lowe au Kelvin Mushi nyuma yangu?” Alvin hakuwahi kuwapenda wanaume ambao walisisitiza kuangalia simu za wanamke wao, lakini alipoona tabasamu kwenye midomo ya Lisa mapema, moyo wake ulikosa raha ghafla. Alipaswa kuwa na uhakika Lisa alikuwa anachat na nani!
Lisa hakuwahi kufikiria kwamba uaminifu kati yao ulikuwa umeshuka sana. Hata hivyo, huenda asingemuelewa tena ikiwa angeona yaliyomo kwenye simu yake, kwa hiyo alisema tu waziwazi, “Nilikuwa niachat na Pamela . Alikuwa akizungumza kuhusu mpenzi wake. Pia… ataenda hospitali kumwona Kelvin. Siwezi kwenda mwenyewe, lakini marafiki zangu wanaweza kwenda kwa niaba yangu.” Alitazama kinyonge jinsi sura nzuri ya Alvin ikibadilika na kuwa mbaya kwa hasira iliyoonekana waziwazi kwa macho. Moyo wake ulihisi kuchoka ghafla.
“Lisa Jones, wewe ndiye uliyekuwa unachat na Kelvin Mushi? Ni kitanda changu unacholala sasa ujue.” Alvin alichukua simu yake na kuivunjavunja ukutani. Kelele kubwa ilimfanya Lisa kuziba masikio yake kwa hofu.
Alvin aliinua mikono yake na kumkandamiza kitandani, akimbusu kwa nguvu kwenye mdomo. "Niambie, busu langu linakupendeza zaidi, au busu la Kelvin Mushi ndilo tamu zaidi?" Akambusu kana kwamba ana wazimu. Lisa alikuwa akiumia tu kutokana na busu hilo na kumsukumia mbali, lakini hakuweza kumzuia hata kidogo.
Alvin alikuwa amekunywa nusu chupa ya divai nyekundu katika chumba chake cha maktaba. Ubabe wake ulionekana kuongezeka mara moja. Alipokumbuka busu lake na Kelvin, macho yake yakawa mekundu huku akimbusu zaidi.
"Alvin unaniumiza bwana." Lisa alikwepa kwa maumivu.
“Kwanini unakwepa busu langu? Unatamani ningekuwa Kelvin badala yake?” Alvin alikuwa tayari amezidiwa na moto wa wivu. Akararua nguo yake ya kulalia kwa nguvu. "Au aliufanya usiku huo kuwa usiosahaulika sana, ndio maana umeenda naye kituo cha polisi leo? Huwezi kumwacha kabisa?”
Lisa aliogopa sana. Haraka haraka akamshika mkono na kutikisa kichwa bila msaada. “Hapana, nimechoka. Ninaogopa leo sitaki…”
“Hutaki kwa sababu ni mimi, sivyo?” Alvin alicheka ghafla. “Akili yako imejaa Kelvin Mushi sasa. Ungekuwa tayari kama angekuwa yeye, si ndiyo?"
“Mbona unaendelea mbali sana Alvin, hutaki kunielewa kwanini?” Lisa alijisikia kuchoka sana na kukata tamaa. Alikaribia kufa siku hiyo, lakini hakumjali hata kidogo. Alijua tu jinsi ya kumtilia shaka.
Alitabasamu kwa huzuni na hakuhangaika tena, akamwacha afanye anavyotaka. “Sawa, fanya tu kama unataka. Fanya chochote unachotaka.” Machozi yake yalimtoka kwenye pembe za macho yake na kutiririka kwenye nywele zake. Macho yake yalikuwa hafifu.
Siku zote alikuwa akitiliwa shaka, kukanyagwa, na kudhalilishwa naye, lakini bado alikuwa binadamu.
Mwili wa Alvin ukakakamaa kana kwamba alipigwa ghafla kichwani.
Kwanini amekuwa hivi? Ilikuwa ni kama amekuwa pepo. Hakuweza kujizuia kwa mwanamke? Kweli alipoteza busara kwa sababu ya mwanamke? Aligeuka na kukimbilia bafuni. Maji baridi yakamwagika juu ya mwili wake, na ghafla akajichukia. Alipotoka kuoga, Lisa alikuwa amelala chali pembeni ya kitanda, mtupu kabisa hana chochote baada ya nguo zake kularuliwa na Alvin. Kama kware mdogo, alijikunyata, hana msaada wowote, tayari kukwakupaliwa na mwenye mwenye njaa kali!
Alvin hakufanya chochote tena, alilala upande wa pili wa kitanda kimya! Wawili hao walitenganishwa kwa umbali, lakini hakuna aliyemkaribia mwenzake. Hakujua kuwa Lisa ambaye alikuwa amemrudisha nyuma kimawazo machozi yalikuwa yakimtoka. Hakupata usingizi mpaka ilipofika usiku sana.
Kulipopambazuka, Alvin aliamka, lakini Lisa hakuwapo tena kitandani. Haraka akainuka na kushuka chini. Lisa alikuwa amekaa kwenye meza ya chakula akinywa uji wake wa ulezi. Macho ya Alvin yalilegea kidogo, na akashuka haraka. Aliketi kando yake na kuuliza kwa ukali, "Kiamsha kinywa changu kiko wapi?"
Sura ya 140
“Bwana Kimaro, kifungua kinywa chako kimefika.” Shangazi Linda alitoka na kifungua kinywa alichotengeneza.
Alvin akakitazama, na uso wake ukachukizwa mara moja. "Lisa Jones, kwanini hukuniandalia kiamsha kinywa?"
"Wewe ndio ulisema chakula changu ni kichafu kama mimi." Lisa alimtazama kwa utulivu. Siku zote alikuwa hivi. Alipomuelewa vibaya, alimdhalilisha kwa kumwambia chakula chake ni kichafu na asimpikie tena, lakini sasa alitaka apike tena. Je, hakuchoka kumnyanyasa?
"Nitengenezee sasa hivi." Uso wa Alvin ulikuwa mbaya kwa hasira.
"Hapana. Mimi siyo yaya wako.” Lisa alisimama baada ya kumaliza uji wake. "Naenda kazini."
Alvin aligeuka na kuongea na Shani aliyekuwa amesimama mlangoni. “Mfuate kwa karibu. Akithubutu kwenda hospitali, mpige na umrudishe hapa.”
"Mimi sio mtumwa wako." Macho ya Lisa yalikua mekundu kwa hasira. Tayari alikuwa ameamua kutokwenda hospitali, lakini bado alisisitiza kumlazimisha kumwekea mlinzi wa kumchunga. "Alvin Kimaro, usiende mbali sana."
“Kwa kuwa ulinichanganya, unapaswa kuwa tayari kuwa mtumwa wangu. Hakuna anayeweza kwenda kinyume na mimi.” Alvin hakujieleza sana, lakini maneno yake yalitosha kudhihirisha hasira zake.
Lisa alichukua mkoba wake na kuondoka huku Shani akimfuata.
Njiani kuelekea ofisini kwake, haijalishi Lisa aliendesha gari kwa haraka vipi, Shani alikuwa makini naye muda wote. Kwenye maegesho, Lisa alishuka kwenye gari na Shani akamfuata kwa nyuma kwa kasi.
“Shani, unaweza kuacha kunifuata? Sitaenda hospitalini.” Lisa alitmwambia Shani kwa upole. Kwa kweli, hakuwa na shida yoyote na mlinzi yule.
"Samahani, hili ni agizo la Bwana Kimaro, bosi wangu."
“Agizo ni la Alvin, lakini usalama ni wa kwangu. Najua namna ya kujilinda mwenyewe!” Lisa mwishowe alikasirika. “ Sawa, Alvin alikuajiri? Anakulipa kiasi gani? Mimi nitakupa mara mbili." Lisa akatoa kadi kwenye begi lake.
Shani hakujali. “Bi Jones, haijalishi unanipa kiasi gani. Nilifunzwa na familia ya Kimaro. Ninafanya kazi kwa ajili yao tu.” Lisa alipigwa na butwaa. Je, familia ya Kimaro ilikuwa na watu wengi kama Shani? Familia ya Kimaro ilionekana kuwa na mambo mengi zaidi kuliko vile alivyofikiria. “Kwa hiyo lazima umekuwa na Alvin kwa muda mrefu. Kwa maana hiyo unamjua mtu anayeitwa Sarah?”
Hali ya wasiwasi ikaangaza kwenye macho tulivu ya Shani. Ingawa lilitoweka hapo hapo, Lisa bado aliliona vizuri. “Nilimsikia Alvin akimzungumzia siku moja akiwa amelewa. Lazima awe mpenzi wake wa zamani. Walikuwa wanapendana sana?"
“Bi Jones, hayo yote ni ya zamani. Bwana Kimaro ana wewe tu moyoni mwake sasa,” Shani alisema haraka.
"Ndio hivyo?" Lisa alitabasamu kwa kujidharau. Alikuwa akimpima tu Shani, lakini jibu la Shani lilimhakikishia kwamba kweli Alvin alikuwa na mpenzi wa zamani anayeitwa Sarah. Alimwita jina lake wakati alikuwa amelewa. Je, iliwezekanaje kuwa Lisa ndiye pekee moyoni mwake sasa?
“Shani, asante kwa kuniambia hivi.” Aligeuka na kwenda juu ofisini.
Shani alimfuata kinyonge.
•••
Siku iliyofuata, saa kumi na nusu jioni, Pamela alitoka hospitali baada ya kumtembelea Kelvin, akihisi huruma moyoni mwake.
Kama asingekuwa amekosea na kumchanganya Alvin na Kelvin hapo mwanzo, huenda Lisa na Kelvin wangekuwa tayari wameoana. Hapo Kelvin asingepoteza figo pia. Hata hivyo, haikufaa kujutia juu ya maziwa yaliyokwishamwagika sasa.
Akatoa simu yake na kumpigia Patrick. “Patrick, unakwenda kuwachukua wazazi wangu, au unaenda moja kwa moja kwenye Mgahawa tuliokubaliana kukutana?”
“Niko na mkutano ofisini ambao unaweza kuendelea hadi saa kumi na moja na nusu. Nitaenda huko moja kwa moja baadaye. Nisaidie kuomba radhi kwa wazazi wako kwa ajili yangu,” Patrick alisema kwa sauti ya upole.
“Ni sawa, lakini usichelewe. Baba yangu anachukia watu ambao hawatimizi ahadi zao.” Pamela alimuonya kwa upole.
“Usijali, ni suala la maisha yangu. Hakika sitachelewa. Tayari nimekuandalia zawadi ambayo wazazi wako watapenda. Tutafunga ndoa mapema, nami nitakuwa mumeo.” Patrick akatabasamu kwa dhati. Moyo wa Pamela ulikuwa mtamu alipokuwa akimsikiliza.
Baada ya kukata simu, Pamela aliendesha gari kuwachukua wazazi wake kisha akaenda Mambo Garden Restaurant. Ilikuwa saakumi na moja kamili jioni alipofika. Baada ya kuagiza chakula, kaka yake Forrest alifika. Saa kumi na mbili jioni bado Patrick alikuwa hajafika. Babake Pamela alikosa subira, akasema, “Kwa nini bado hajafika? Si sawa kutufanya wazee tungojee.”
Pamela alisema, “Baba, ni saa za jioni sasa. Pengine kuna msongamano mkubwa wa magari barabarani.”
Mama yake aliitikia kwa kichwa na kukubali. “Wafanyabiashara wana mambo mengi ya kushughulikiwa mwishoni mwa mwaka, hiyo inaeleweka. Kuwa na subira zaidi.”
Pamela alimpigia simu Patrick, lakini hakupokea, akajifariji. "Lazima asipokee kwa sababu yuko barabarani, atakuwa karibu tu hapa."
Baada ya nusu saa nyingine, Patrick hakutokea tu. Baba yake alikasirika. “Ni mara yake ya kwanza kukutana nasi lakini anatuletea dharau namna hii. Hata ukimpigia simu ni bure. Sidhani kama yeye ni mkweli hata kidogo. Sitakubali kukuruhusu uolewe naye.”
Wakati huu, mama yake hakusema chochote, na Forrest pia alikuwa na uso wa kukata tamaa. “Achana naye. Sio kama hakuna wanaume wengine ulimwenguni."
Pamela alihudhunika. Mbele ya shutuma za familia yake, alijilazimisha kutotoa machozi. Yeye tu alijisikia kukata tamaa sana kwa aibu. Zamani, alimuahidi mara nyingi, lakini sasa, hata alikosa mkutano wa kwanza pamoja na wazazi wake. Je, alimpenda kweli?
Mama yake akasema. “Pamela, jambo la muhimu zaidi katika maisha ya mwanamke ni kupata mwanaume ambaye ni mzuri kwako kwa moyo wote. Bado wewe ni mdogo, kwa hivyo usikimbilie kuolewa. Sasa, tule. Chakula kinakuwa baridi.” Wakati wote wa chakula, ilikuwa kama anatafuna nta. Mpaka mwisho, Patrick hakutokea, wala hakupiga simu hata mara moja kuelezea shida ni nini.
Baada ya kuachana na familia yake, Pamela aliendesha gari hadi ofisini kwa Patrick. Ofisi yake ilikuwa tayari imefungwa. Alianza kuhisi wasiwasi kidogo. Alikuwa na wasiwasi kwamba huenda Patrick alikuwa amepata ajali ya gari au kitu kibaya. Hata hivyo, hakujua namba za wazazi wa Patrick. Baada ya kusita kwa muda, alimpigia simu Linda. Hakutarajia kuwa mtu aliyemjibu angekuwa ni mwanamume ambaye sauti yake aliifahamu vizuri. “Habari, Pamela…”
Pamela alitazama sura yake iliyokuwa na ukungu kwenye dirisha la kioo mbele yake na ghafla akacheka peke yake. Je, alionekana kama mjinga? “Kwa nini hukupokea nilipokupigia simu? Na mbona unapokea simu ya Linda?”
“Pamela, samahani. Linda alipata ajali ya gari jioni. Niko hospitalini sasa. Nilisahau kabisa hata kuchukua simu yangu ofisini,” Patrick alisema kwa hatia, “Oh, nimechelewa sana? Mmemaliza kula? Tafadhali mwambie baba na mama smahani kwa kushindwa kuja.
Nitawaalika kwenye chakula cha jioni wakati mwingine.”
"Hakuna haja tena," Pamela alisema kwa sauti isiyo na maana.
"Pamela, ilikuwa ni dharura wakati huu ..."
“Ndiyo, kila kitu kuhusu Linda ni dharura. Kwani amekufa? Kilema? Kwani hana wazazi tena, ana wewe tu?"
Moyo wa Patrick ukasisimka. "Pamela, unawezaje kusema maneno kama haya? Kwani Linda alitaka kupata ajali? Hata kama humpendi, unapaswa angalau umuonee huruma.”
Pamela alidhihaki. “Sawa, nimekuuliza swali. Kwani amekufa? Amepooza? Mlemavu?”
TUKUTANE KURASA 141-145
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
KURASA.. 136-140
Sura ya 136
Alvin alikaa kwenye siti ya nyuma ya gari lake. Alikuwa ametawaliwa na maamuzi ya hasira mapema asubuhi, lakini sasa ghafla alihisi njaa sana. Tumbo lilianza kumuuma tena. Aliwasha sigara kwa hasira. Ikiwa angejua kwamba hilo lingetokea, angemaliza kula kifungua kinywa chake kwanza kabla ya kupandisha hasira zake za kijinga.
"Bwana Kimaro, ngoja nikununulie chakula." Hans alimtazama kwa wasiwasi.
“Sina njaa. Nenda uniletee Lina Jones hapa,” Alvin alisema kwa upole, “Sikuzote nilitaka Lisa ashughulike naye, lakini haina maana sana. Nitamalizana naye mwenyewe.”
Hans aliitikia kwa kichwa. Ilionekana kana kwamba ingemlazimu kumuombea Lina kwa kile ambacho alihisi kilikuwa kinaenda kumkuta.
•••
Katika kampuni ya Mawenzi Investments. Lina alifukuzwa moja kwa moja na walinzi. Hakutaka kuondoka na kuishia kupiga kelele mlangoni, “Hata kama baba yangu alikamatwa, bado ana hisa kwenye kampuni na mimi bado ni mtoto wake. Nina haki ya kurithi hisa zake na kufurahia gawio langu.”
“Potelea mbali!” Yule mlinzi alimtemea mate isivyostahili. “Kila mtu anajua kuwa wazazi wako walimuua bibi mzee ili wapate hisa za Mawenzi Investments. Walimuua Mzee Madam Masawe. Hawana utu kabisa. Mwenyekiti Jones tayari ameomba mawakili wengi kurejesha hisa za Jones Masawe. Utarithi nini? Endelea kuota!"
"Subiri. Nitakaporudi Mawenzi, nitafanya maisha yako kuwa mabaya zaidi kuliko kifo. Lina alitetemeka kwa hasira.
Hata mlinzi alithubutu kumdhalilisha sasa. Kweli dunia haikuwa ya haki. Ni wazi alikuwa ametuma picha zote za uchafu za Lisa na Kelvin kwa waandishi wa habari jana yake, lakini sio tu kwamba ilishindwa kuharibu sifa ya Lisa, bali watu walianza hata kumuoanisha na Kelvin sasa. Ilikuwa inakasirisha sana na kukatisha tamaa.
Alitembea kando ya barabara wakati gari lisilo na nambari ya leseni lilisimama ghafla mbele yake. Kisha, watu wawili wakamsukuma moja kwa moja kwenye gari.
"Unafanya nini?" Kabla Lina hajajibu, alifunikwa kwenye gunia na kupoteza fahamu. Muda si muda, ndoo ya maji baridi ilimwagiwa juu yake na akapiga kelele kutokana na baridi. Gunia lilipasuliwa.
"Baridi ilikuwa nzuri?" Hans alimtazama kutoka juu.
Lina alitazama juu na kufikiria kuwa anaonekana kuwa mzoefu kidogo. Baada ya muda, alimkumbuka. "Ni wewe. Wewe ni msaidizi wa Alvin Kimaro…”
"Ni vizuri kukumbuka." Hans aliachia tabasamu hafifu. Akageuka pembeni, akamfunua mtu aliyekaa kwenye sofa ambalo halikuwa mbali. Mwanaume huyo alivalia suti nyeusi na kushika sigara mkononi, moshi ukitanda hewani. Macho yake ya wino yaliangaza na mwanga mweusi uliokuwa mkali kama kisu. Mwanamume huyo alitoa sauti ya kutisha.
Lina alimtambua. Hofu isiyoelezeka ikapanda kutoka ndani ya moyo wake. "Bwana. Kimaro, unajishughulisha na kazi ya kisheria. Unataka kunyang'anywa leseni yako kwa kuvunja sheria? Ninakuonya, afadhali uniache mara moja, la sivyo sitakuacha kamwe.”
Hans alicheka kana kwamba amesikia mzaha.
“Unacheka nini? Huwezi kuelewa nilichosema?” Lina alicheka. “Hebu niambie, haufahamu kuwa mimi ni mwanamke wa Willie Kimaro? Unajua Bwana Kimaro ni nani? Unajua kuwa ananipenda sana? Ikiwa huniamini, unaweza kuchukua simu yangu na kuangalia picha zetu pamoja.”
Alvin alimaliza kuvuta sigara na kuitupa kwenye sinia ya majivu kabla ya kuinuka. Mwili wake mrefu ulitembea polepole kuelekea kwake. Lina alifikiri anaogopa na akacheka. “Alvin Kimaro, wewe ni mwanasheria tu. Willie Kimaro si mtu ambaye mtu kama wewe unaweza kudiriki kumuudhi—”
Kabla hajamaliza, Hans alimpiga kofi kwenye shavu na kumng'oa jino mdomoni. Lina alipiga mayowe, “Willie hatakusamehe—”
Smack! Kofi jingine likasikika. Baada ya makofi kadhaa, Lina alipoteza meno machache na hakuthubutu kuongea tena.
"Nyamaza." Hans alitabasamu. “Unafikiri Willie Kimaro ni nani? Hujaelewa kwa nini Willie alibadili mtazamo wake kwako haraka hivyo?”
Lina aliganda. Alimtazama Alvin na ghafla akakumbuka kuwa jina lake la mwisho lilikuwa Kimaro pia. “Hilo haliwezi kuwa. Sijawahi kusikia mtu anaitwa Alvin katika familia ya Kimaro."
“Unawajua watu wangapi katika familia ya Kimaro?" Hans alidhihaki. “Acha nikwambie, Alvin Kimaro ndiye kaka mkubwa katika familia ya Kimaro. Amekuwa akisimamia familia tangu akiwa na umri wa miaka 20.”
Ubongo wa Lina ulivuma kana kwamba anaota. Kila mtu alijua kwamba kaka mkubwa, wa ajabu wa familia ya Kimaro alikuwa mtoto wa Leah Kimaro. Mtu huyo alikuwa mtu wa chinichini sana, lakini mbinu zake za ukatili zilijulikana sana. Aliingia katika kampuni hiyo akiwa na umri wa miaka 20. Mjomba wake wa pili alipokaidi, alimvunja mguu wake mbele ya umati.
Baada ya kuchukua jukumu la kuongoza KIM International, alipanua biashara yake hadi ng'ambo kwa kasi ya radi na hata akaingia katika nyanja za mawasiliano, fedha, na teknolojia kwenye masoko ya nje ya nchi kwa haraka haraka. Kwa wakati huo, alikuwa ameingia kwenye orodha ya watu miamoja tajiri zaidi Afrika, akiachwa kwa karibu sana na kina Dangote, Mo Dewji, Bhakresa na wengineo. Kulingana na uvumi, alikuwa mtu wa tatu tajiri zaidi nchini Tanzania na pia wa kushangaza zaidi.
"Hiyo haiwezekani. Unasema uwongo!” Lina alikuwa akiingiwa na wivu. Lisa alimkamataje mtu kama huyo?
“Kwa nini nikudanganye? Huyo mjinga Willie Kimaro aliogopa sana hivi kwamba alikojoa kwenye suruali yake alipomwona Bwana Kimaro. Hans alifoka. “Lina Jones, Bwana Kimaro hakutaka kushughulika na wewe mara ya kwanza, lakini hukupaswa kumpa Lisa Jones dawa ya kulevya. Na kwa kweli hukupaswa kutoa picha hizo kwenye vyombo vya habari.”
Lina alishtuka. Alipiga magoti mbele ya Alvin na kutetemeka. “Bwana Kimaro, mimi ni mjinga. Nilikuwa mjinga. Tafadhali nisamehe sana.”
Alvin akampiga teke kwa kuchukia. Ujeuri wa macho yake ulidhihirisha kwamba hakutaka chochote zaidi ya kumwangamiza kabisa. “Unadhani nitakuacha ukipumua?”
"Hapana, hapana, hapana. Haikuwa mimi. Sikupiga picha.” Lina akatikisa kichwa kwa hofu. “Nilitumiwa na mtu nisiyemjua. Ni kweli nilimpa Lisa dawa usiku huo, lakini Kelvin Mushi alipokuja, kamera ya video iliyokuwa chumbani iliharibiwa.”
“Hukuwa wewe?” Uso wa Alvin ulikaza zaidi huku alama ya mshangao ikimulika machoni mwake, akiamini hadaa ya Lina.
"Naapa." Lina alikuwa amepoteza meno kadhaa na mdomo wake ulikuwa umejaa damu. “Kama ningekuwa na hizo picha ningezitumia kumtishia Lisa zamani. Ningewezaje kumruhusu kukaa katika nafasi ya mwenyekiti kwa muda mrefu hivyo na kuwaweka wazazi wangu jela?”
“Kiapo chako hakina thamani.” Uso wa Alvin ulizidi kutisha, lakini aliamini maneno ya Lina. Ikiwa hakuwa yeye, basi ni nani?
Alikuwa na wazo, na midomo yake ikachanua katika tabasamu. Usiku huo, mbali na Lisa, ilionekana kana kwamba kulikuwa na Kelvin pekee. Kwa Kelvin Mushi haikuwa rahisi hata kidogo kwa Lisa kumshuku. Lisa alijua kwamba anampenda, lakini bado alikuwa tayari kuendelea kuwa na urafiki naye. Kelvin alikuwa ameenda ng’ambo kufungua ofisi ya tawi alipokuwa kijana, kama yeye tu. Anawajua watu wenye uthubutu wa kuvuka mipaka na kwenda kufanikiwa nje ya nchi huwa wajanja wajanja sana. Alvin hakumwamini Kelvin hata kidogo.
Lina alijua kwamba alimwamini na akasema kwa haraka, “Bwana Kimaro, tafadhali niruhusu niende. Ninaahidi sitomsumbua Lisa tena. Nitaondoka Dar es Salaam.”
“Unadhani nitakuacha uondoke kwa amani?” Alvin alitabasamu kwa giza. “Nimechunguza mambo yako. Ulikulia kijijini baada ya kuibiwa ukiwa mtoto mdogo, ukatolewa usichana wako na mwanakijiji ukiwa na umri wa miaka 15. Baadaye katika shule ya sekondari, ulifumaniwa zaidi ya mara kumi na waume za watu. Uliwekwa kinyumba na tajiri mmoja na hata kutoa mimba zisizo na idadi. Ni aibu iliyoje. Hukuwa na maisha mazuri hata baada ya kurudi kwenye familia ya akina Masawe.”
Uso wa Lina ulikuwa umepauka kwa aibu. Hii ilikuwa historia yake ya giza. Alikuwa ameifunika kwa makini sana, lakini mtu huyu kwa kushangaza aliweza kujua juu yake. Alikuwa anatisha sana.
"Kwa kuwa unapenda wanaume sana, nitakuozesha mume wa kuishi naye." Alvin alisema na kuondoka bila kuangalia nyuma.
Punde, mzee mfupi na mbaya mwenye umri wa miaka 50 aliingia. Alipomwona Lina, alimeza mate ya uchu. "Bwana Kimaro, unaniruhusu nimuoe?"
Lina alimtazama Hans kwa uso wa kutisha. “Usimruhusu anioe. Nitakwenda na wewe. Unaweza kufanya chochote unachotaka. Unaweza kunifanya vile Willie alinifanya pia!”
Hans alikwepa nyuma kwa kuchukizwa. “Usinishike, nachukia mambo machafu. Usimwogope sana. Anaonekana kuwa mzee, lakini ana umri wa miaka 40 tu na amekuwa peke yake kwa miaka kadhaa kwa sababu hakuweza kupata mke. Utamfuata kijijini na kumpatia mtoto.”
Kisha, Hans akaondoka, akimuacha Lina nyuma. Alilia kwa kukata tamaa, lakini hakuna mtu aliyemjali. Wakati huo, alijuta sana. Hakupaswa kumlazimisha Lisa Jones kuondoka nyumbani wakati huo. Hakupaswa kumsukuma Bibi Madam Masawe chini ya ngazi.
Lakini, hakuna na dawa ya majuto katika ulimwengu huu.
Sura ya 137
Katika mlango wa kituo cha polisi, Lisa alikuwa amemaliza tu kurekodi ushahidi wake mara ghafla akasikia mtu akiliita jina lake.
“Lisa.” Aligeuka nyuma na kumuona Kelvin akija kwake huku akiwa na tabasamu usoni mwake. Hali ya hewa ilikuwa ya baridi, na alikuwa amejifunika kitambaa shingoni.
"Ni bahati tu nimekuona. Kwa nini upo hapa?” Lisa alilazimisha tabasamu kumsalimia. Kila alipokuwa akimuona, alizikumbuka picha zile na mgogoro kati ya Alvin na yeye.
"Kuna jamaa wa nyumbani alifanya tukio la ajabu, kwa hivyo nilikuja kumdhamini." Kelvin alionekana hoi. "Nilisikia kwamba Jones Masawe na Mama Masawe walikamatwa hivi majuzi. Je wewe…”
“Ndio, polisi waliniita hapa kuchukua maelezo yangu. Kesi hiyo itafikishwa mahakama wiki ijayo kisha watasomewa hukumu.”
"Hongera, hatimaye umelipiza kisasi kwa bibi yako." Kelvin alifurahi kusikia hivyo.
“Asante.” Tabasamu la Lisa halikumfikia machoni. Alionekana kuchoka kabisa.
Kelvin alitembea pamoja naye kuelekea sehemu ya maegesho, huku akimtazama njiani. “Unaonekana umechoka. Umekuwa ukipumzika vizuri kweli? Na Alvin bado hajakuelewa tu…?!”
"Hatuwezi kuzungumza juu ya hili?" Lisa alimkatisha.
"Ni kosa langu." Kelvin alionekana kuwa na hatia.
“Kosa lako kivipi? Ulinisaidia usiku ule. Kama si wewe, ningefanyiwa ukatili mbaya na pengine ningeweza kujiua muda mrefu uliopita. Jana, hata ulishirikiana nami kufafanua hali ilivyokuwa na kuokoa sifa yangu. Ninapaswa kukushukuru,” Lisa alitikisa kichwa na kusema kweli.
Wawili hao walizungumza huku wakitembea. Lakini kijana mmoja aliibuka kando yao ghafla na hawakumjali, wakidhani ni mpita njia tu. Hata hivyo, ghafla mwanamume huyo alitoa kisu cha matunda kutoka kwenye mfuko wake wa suruali na kukichoma kuelekea kifuani kwa Lisa.
“Lisaaa!” Kelvin aliona Lisa amechelewa sana. Alipoona kile kisu kinataka kumchoma, alinyoosha mkono haraka kukizuia, na kisu hicho kikapenya kwenye mkono wake.
Wakati Lisa anajibu, mtu huyo alikuwa amechomoa kisu haraka ili kumchoma Lisa tena. Kelvin angeweza tu kutumia mwili wake kumkinga, na kisu kikapenya sehemu ndogo ya mgongo wake.
“Msaada!” Lisa alilia. Kwa msukumo aliushika mkono wa mwanaume huyo. "Wewe ni nani?!”
“Hutakiwi kunifahamu. Ni kosa lako kuwa mwanamke wa Alvin Kimaro. Nimekuwa nikikufuatilia kwa muda mrefu sasa.” Mwanaume huyo alifichua uso wake wa kutisha huku akiendelea kudunga kisu kwenye mwili wa Kelvin kana kwamba alikuwa na wazimu.
Kwa bahati nzuri, walikuwa karibu na kituo cha polisi. Polisi mmoja alisikia kilio cha kuomba msaada na haraka akakimbia ili kumshika mhalifu.
Punde, ambulensi ilifika na upesi ikampeleka Kelvin hospitalini. Hata hivyo, tayari alikuwa amepoteza damu nyingi njiani na kupoteza fahamu. Lisa alipiga simu kwa haraka kwa Ethan, ambaye alikimbia mara baada ya Ambulance kufika hospitali.
Mlango wa Emeregence Room ulisukumwa, na daktari akatoka na fomu mkononi. “Kisu kilichomwa kwenye figo ya kushoto ya mgonjwa na inabidi itolewe mara moja ili kuokoa maisha yake. Familia ya mgonjwa iko wapi? Tafadhali saini mara moja.”
Lisa alipigwa na butwaa. Ethan pia aliona ni vigumu kukubali. "Daktari, lazima ni lazima figo iondolewe? Kwani hakuna namna nyingine?"
"Necrosis tayari imeingia kwenye figo ya kushoto, kwa hivyo haina maana sasa," daktari alisema bila msaada, "Kama tungeweza kuiokoa, bila shaka tungeiokoa."
Ethan hakuwa na la kufanya zaidi ya kuvumilia maumivu na kusaini zile karatasi. Lisa alitoa machozi ya uchungu. “Yote ni makosa yangu. Mtu huyo alitaka kuniua. Mjomba wako ndiye aliyetumia mwili wake kunisaidia kuzuia kisu."
Ethan alikuwa na hisia tofauti. Hakutarajia Kelvin angekuwa na hisia za kina namna hiyo kwake. Sasa, pia alikuwa na wasiwasi sana kuhusu usalama wa Kelvin. Angeweza tu kusema, “Usifikirie juu yake. Daktari alisema kuwa kuondoa figo yake kutaokoa maisha yake. Mwili wa mwanadamu bado unaweza kufanya kazi na figo moja tu. Anapaswa kuwa mwangalifu zaidi katika siku zijazo."
Lisa alitabasamu kwa uchungu. Kelvin alikuwa anaenda kupoteza figo. Angewezaje kuwa mzima kama hapo awali? "Umewajulisha babu yako?"
“Hapana, babu na bibi wamezeeka na sitaki kuwapandisha presha. Tusubiri hadi upasuaji wa Mjomba umalizike.” Ethan alimtazama na kuhema moyoni mwake. Aliogopa hasa kwamba babu na bibi yake wangezimia ikiwa wangejua ukweli.
Kwa bahati nzuri, saa tatu baadaye, Kelvin aliokolewa. Operesheni ilikuwa imekwisha, lakini bado hakuweza kufumbua macho.
Muda si muda, polisi walifika hospitalini. Walipomwona Lisa walimwambia. “Bi. Jones, tumemhoji mhalifu. Mtu aliyetaka kukuua anaitwa Zigi Kabwe. Yeye si mwenyeji wa hapa Dar.”
Lisa alikasirika. “Hata simfahamu mtu huyu.”
Afisa huyo alitikisa kichwa. “Kulingana na maelezo yake, alikuwa na dada yake pacha anayeitwa Lily Kabwe. Miaka mitano iliyopita, Lily Kabwe alikuwa na umri wa miaka 17 tu, lakini alivutia macho ya Thomas Njau kutoka kwa familia ya Njau huko Nairobi. Thomas alimbaka Lily kwa nguvu baada ya kukataa kulala naye na akaamua kujirusha hadi kufa kutoka kwenye jengo kutokana na fedheha. Familia ya Kabwe ilimshtaki Thomas. Wakati huo, kulikuwa na karibu ushahidi kamili, lakini familia ya Njau ilimwajiri Alvin Kimaro kutetea kesi yao. Alvin Kimaro alidai kuwa Lily alimtongoza Thomas lakini Thomas alimdharau, hivyo akaamua kujiua kwa sababu ya unyonge wake. Mahakama haikushindwa tu kumwadhibu Thomas, lakini hata ilimfanya Lily aonekane kama mtu duni asiye na maana. Mama yake hakuweza kuvumilia na na akapata presha. Amefariki hivi karibuni…”
Lisa alishtuka. Alijua tu kwamba Alvin hawezi kushindwa mahakamani, lakini hakujua kwamba alikuwa amechukua kesi nyingi zisizo na moyo wa utu. "Kwa hivyo, alitaka kuniua ili kulipiza kisasi kwa Alvin Kimaro?"
“Ndiyo. Alitoweka miaka mitano iliyopita baada ya kesi hiyo, na tuligundua tu kwamba alirudi Dar es salaam mwaka huu. Alitaka Alvin Kimaro ajue uchungu wa kufiwa na mpendwa wake, lakini… Alvin Kimaro amezungukwa na walinzi na ni mwangalifu sana, kwa hivyo Zigi Kabwe ameshindwa kutimiza lengo lake licha ya kujaribu kwa miaka kadhaa.”
Afisa huyo alimwambia, “Amekuwa akikufuata kwa muda, lakini umekuwa ukilindwa na mlinzi siku hizi za karibuni. Ni leo tu ndipo alipata nafasi hiyo kwa sababu hukuwa na mlinzi.”
Ghafla, Lisa alionekana kugundua kitu. Siku chache zilizopita, Alvin alikuwa amepanga ghafla Shani afuatane naye kama mlinzi wake. Haikuwa kumlinda dhidi ya Jones na binti yake bali kumtazama Zigi Kabwe. Hata hivyo, hakumwambia chochote.
Haukuwa ulinzi wake hata kidogo. Kama Kelvin asingetokea siku hiyo, angekufa. Hofu isiyo na kipimo ikaufunika moyo wake. Lisa ghafla alifikiri kwamba hakumfahamu kabisa Alvin kama alivyodhani.
"Kwa nini kulipiza kisasi kwako kwa kile Alvin Kimaro alichofanya kwa mtu mwingine?" Ethan alikasirika. “Lisa, nakushauri ukae mbali na Alvin Kimaro. Nani anajua ni maadui wangapi amewachokoza kwa miaka mingi? Nilisikia huwa anaenda mahakamani kuwatetea matajiri tu, madhalimu na mafisadi, je ni haki za wangapi amedhulumu? Lazima atakuwa amepata pesa nyingi kwa njia isiyo halali."
Lisa alinyamaza, akiinamisha kichwa chini na uso wa huzuni. Moyo wa Ethan uliumia. Ikiwa asingefanya chaguo baya hapo kwanza, Lisa asingeangukia kwa Alvin
Sura ya 138
Saa nne usiku, Alvin aliingia kutoka nje akiwa na uso jeuri na mkali. Alipanda juu ndani ya dakika mbili kabla ya kushuka tena kwa haraka. "Lisa bado hajarudi?"
"Hapana." Shangazi Linda aliogopa kidogo sura yake.
“Mbona bado hajarudi?”
"Sijui. Yeye hapokei simu pia.” Aunty Linda alipomaliza kuongea, hali ya joto ndani ya jumba hilo ilionekana kushuka na kumfanya ashtuke.
Alvin akatabasamu kwa ujeuri. Vizuri. Hata baada ya kumsaliti na Kelvin, bado hakujua jinsi ya kuishi. Ilikuwa tayari saa nne usiku lakini hakuwa amefika nyumbani bado. Hata hakupiga simu nyumbani. Mwanamke huyo hakubadilika kamwe.
“Bwana Kimaro,” wakati huo, Hans alikimbia kutoka nje. “Nimepata habari. Zigi Kabwe alimvamia Miss Jones nje ya kituo cha polisi leo, lakini Kelvin Mushi alimzuia na kuchomwa visu vingi mwilini. Lisa yuko salama, lakini Kelvin amejeruhiwa vibaya na sasa anatibiwa hospitalini.”
Mwili wa Alvin uliganda pale pale huku macho yake meusi yakiwa yamemtoka ghafla. “Shani yuko wapi? Amechoka kazi? Si nilimwambia amlinde Lisa?”
Hans alipumua na kukumbusha kwa upole, “Bwana Kimaro, ulisahau? Ulipoona picha za Lisa na Kelvin kwenye vyombo vya habari siku moja kabla ya jana, ulishindwa na kumwambia Shani aache kumlinda Miss Jones. Ulimwambia Shani amwache Bibi Jones kwa hiari yake mwenyewe.”
'Nilimwambia asimlinde Lisa na kweli aliacha kumlinda Lisa? Ana akili timamu?" Alvin alishindwa kujizuia tena. Hans alikuwa kimya. Shani alifuata tu maneno ya Alvin kwa utii.
“Twende hospitali.” Alvin akatoka nje.
Baada ya kufika hospitalini, alivamia moja kwa moja hadi kwenye wodi ya watu mashuhuri. Kelvin bado alikuwa katika hali ya kukosa fahamu. Mrija wa oksijeni ulikuwa umefungwa kwenye pua yake, na Lisa alikuwa akifuta uso wake kwa kitambaa.
Tukio hilo lilimchoma macho Alvin bila huruma. Hapo zamani alipokuwa amelazwa hospitali, alikuwa amemtunza vile vile. Sasa, alikuwa akimtunza mwanamume mwingine.
"Njoo hapa," alimtazama na kusema polepole, "Tuondoke haraka."
Lisa aliacha harakati zake na kutikisa kichwa. “Bado hajaamka. siwezi kuondoka.”
"Lisa Jones, huelewi nilichosema?" Mwali wa hasira kweny moyo wa Alvin ukawashwa papo hapo. Sauti yake ilikuwa ya kikatili sana. "Ninakupa nafasi ya mwisho."
Sauti yake iliufanya moyo wa Lisa kusinzia. Alikaribia kuchomwa kisu hadi afe siku hiyo. Hakuona kuwa alikuwa ametapakaa damu? Je, aliwahi kumjali? "Alvin Kimaro, kuwa mwenye busara. Kama si Kelvin, ningekuwa maiti kufikia sasa. Alimlinda mpenzi wako. Ni sawa ikiwa huna shukrani yoyote, lakini mtazamo wako unawafanya watu wahisi kwamba wewe ni mnyama mwenye damu baridi.”
“Mimi ni mnyama mwenye damu baridi?” Alvin akapiga hatua kuelekea kwake. Alikuwa amemfanyia mengi, akimlinda mara kwa mara, hata kumpenda. Hata hivyo, alikuwa akimshutumu kwa kuwa na damu baridi? Maneno hayo mawili yaliupiga moyo wake kama kisu, na kusababisha maumivu yasiyovumilika.
"Unapaswa kuwa tayari umejua kwa nini Zigi Kabwe alitaka kuniua," Lisa alidhihaki, "Hivi kweli familia maarufu ya Kimaro ina ukata wa pesa kiasi kwamba unalazimika kupigania kesi isiyo ya haki kwa pesa hizo kidogo? Au ilikuwa kwa ajili ya umaarufu? Ulifika kileleni na kupata sifa uliyonayo sasa katika ulimwengu wa wanasheria kwa kuwakanyaga watu wengine?”
Alvin alikunja ngumi. Mishipa ya nyuma ya mkono wake ilitoka nje. "Lisa Jones, elewa hili. Mimi ni mwanasheria. Wanasheria hushinda au kushindwa tu. Mimi si mjumbe fulani wa haki.”
"Lakini mtu hawezi kuishi bila dhamiri." Lisa akatikisa kichwa. Ghafla aligundua kuwa yeye na Alvin walionekana kutoka dunia mbili tofauti kabisa.
“Nimekufanyia mambo mengi, lakini leo hii unasema sina dhamiri?”
Alvin alimtazama kwa hasira. Hajawahi kumtendea mwanamke kinyume sana hapo awali, lakini alipinga kila kitu katika sentensi moja. “Kwa sababu Kelvin alitoa maisha yake ili kukuokoa, kwa hiyo unataka kuwa pamoja naye? Ni kweli, siku zote amekuwa akikufuata.”
"Acha kuongea ujinga." Lisa alikasirika. "Amepoteza figo kwa sababu yangu. Siwezi hata kukaa na kumtunza? Hiki ndicho kitu kidogo zaidi ninachoweza kumfanyia baada ya kuokoa maisha yangu.”
“Sijali. Njoo tuondoke mara moja. Kelvin Mushi sio mtu mzuri kama unavyofikiria wewe. Kelvin ndiye aliyetuma picha hizo kwa siri kwa Lina. Alijifanya kama mtu mzuri juu ya uso lakini alicheza hila za siri gizani. Alikuwa ni mnafiki tu.” Alvin hakujali hata kidogo kuhusu hali ya Kelvin.
"Nadhani wewe ndiye ambaye sio mzuri." Lisa alikasirika.
Muda huo Ethan aliingia kutoka nje akiwa na nguo. “Lisa, nimekuletea nguo. Unapaswa kubadilisha haraka…” Kabla hajamaliza, akamuona Alvin na uso wake ukiwa mweusi mara moja. “Nani alikuruhusu kuingia humu? Ondoka haraka..."
Alvin alimtazama kisha akamtazama Lisa kabla ya kucheka ghafla. “Si ajabu hutaki kuondoka. Mpenzi wako wa zamani yuko pamoja nawe, na mpenzi wako mpya amelala kitandani. Una jozi hii ya mjomba na mpwa wake iliyozunguka moyoni mwako. Lazima uwe na furaha tele.”
"Nimekuozea, siku zote nimekuwa mtu kama huyo moyoni mwako." Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku mwili ukimtetemeka bila kuvumilika.
“Alvin Kimaro, umeenda mbali sana. Je, hilo ni jambo ambalo mwanadamu anaweza kusema?” Ethan hakuweza kuvumilia. Akatupa zile nguo pembeni na kumpiga ngumi Alvin. Alvin aliinua mkono wake kwa urahisi ili kuizuia, na Ethan akanguruma kwa hasira. “Hapana, wewe si binadamu hata kidogo. Lisa na mjomba wangu wamebeba tu matokeo ya matendo yako maovu. Walikaribia kupoteza maisha kwa sababu yako, lakini huna ubinadamu. Ondoka mbele yangu!”
"Nitaondoka, lakini sitaondoka peke yangu, lazima nimchukue mwanamke wangu." Alvin alinyoosha mkono kumnyanyua Lisa begani. Ethan alikimbia kumzuia, lakini Hans alimzuia haraka.
“Alvin Kimaro, niache! Usifanye hivi! nitakuchukia.” Lisa alianza kumpiga mgongoni, lakini Alvin alipuuza.
“Huchukii kuwa mimi ni mchafu? Je, huogopi kwamba nitakuchafua?” Lisa alipiga kelele.
Alvin akamshusha na kumtupa kwenye gari. Hans akawasha gari na kufunga milango. Lisa alijua kwamba asingeweza kushinda dhidi yake na akachagua kukaa mbali naye iwezekanavyo, bila kumwangalia hata kidogo.
Moyo wa Alvin uliudhika sana, akawasha sigara ili avute katika safari nzima. Lisa alikohoa mfululizo. Alijua kuwa hapendi kuvuta sigara hata kidogo kabla ya hii, lakini sasa, alikuwa akivuta sigara mara kwa mara. Hakupenda wanaume wanaovuta sigara, na hakupenda wanaume wasio na akili kama yeye hata kidogo.
Baada ya kufika nyumbani, Alvin alimbeba tena na kumtupa kitandani. Lisa alipanda na kusema kwa ujeuri, “Utanifunga tena? Alvin Kimaro, mimi ni mwenyekiti wa kampuni sasa. Kuna watu wengi nyuma yangu wananitegemea. Siamini kwamba utaweza kunifunga maisha yangu yote.”
“Kila saa ni ampuni, kampunii! kampuni, ni upuuzi tu kwangu.” Alvin alimuigiza kwa kubana pua. “Je, utaniamini nikisema nitaifunga kesho?” Alvin alifoka na kumpa jicho la pembeni. "Si tayari kabisa unajua utambulisho wa jina langu?"
Macho meusi ya Lisa yalitetemeka. Ilibadilika kuwa tayari alijua. Je, Willie Kimaro alimwambia? Yule mwongo aliyelaaniwa. Yeye ndiye alisema atamficha Alvin. Ingawa hakuwa wazi kuhusu utambulisho halisi wa Alvin katika familia ya Kimaro, pamoja na ujuzi wake, angeweza kweli kufanya hivyo. Familia ya Kimaro ilimiliki 25% ya hisa za kampuni hiyo, ukichanganya na ujuzi wake wa sheria, kufumba na kufumbua tu alikuwa anaukosa uenyekiti wake!
"Alvin Kimaro, ungekuwa na furaha zaidi ikiwa ningeuawa na Zigi Kabwe leo?" Macho ya Lisa yalikuwa mekundu huku machozi yakimtoka. "Ninamtunza Kelvin si kwa sababu ninampenda, lakini kwa sababu ninamshukuru."
“Sitakuruhusu umkaribie tena.” Macho ya Alvin yalikuwa yamepoa sana. Alikuwa na hisia kwamba ikiwa angemruhusu Lisa abaki na Kelvin kwa muda mrefu, angempoteza milele. Japo alikuwa amepoa kwake, bado hakutaka kutengana naye baada ya kujua kuwa alikuwa amenyweshwa dawa na Lina. Hata hivyo, hakuweza kuondoa fundo lililokuwa moyoni mwake. Bado alihitaji muda.
Sura ya 139
“Lisa Jones, kama kweli unanipenda, usiende kwa Kelvin Mushi tena. Hii ni nafasi ya mwisho ninayokupa.” Alvin alimtazama kwa kina, sauti yake ikisikika kwa ukali na kishindo.
Lisa alipigwa na butwaa. Ingawa alimchukia na kumkasirikia, bado moyo wake ulimpenda. "Na wewe je? Unanipenda?" Ikiwa alimpenda, kwa nini aliita jina la mwanamke mwingine wakati alikuwa amelewa?
"Naweza kukupenda, na ninaweza kuacha kukupenda wakati wowote." Alvin alisema bila kujali kabla ya kugeuka kuondoka.
Lisa alikaa kitandani huku akishangaa kidogo. Alvinaliweka wazi kuwa upendo wake unaweza kubadilika wakati wowote. Je, ni kwa sababu hakumpenda vya kutosha?
Katika chumba chake cha maktaba, Alvin alisimama mbele ya dirisha akiwa na glasi ya divai nyekundu, akitazama nje ya dirisha matone ya mvua yakishuka chini taratibu. Alitumaini kwamba Lisa alimuelewa. Ndio, ingawa alimpenda, ikiwa angetaka kuendelea kujihusisha na Kelvin Mushi, basi angeweza tu kuachana na upendo huo. Ingawa Kelvin alikuwa ameokoa maisha yake, Alvin alikuwa ameokoa maisha yake mara nyingi zaidi. Asingeweza kuvumilia kumuona mwanamke wake akimlipa fadhila kwa kumhudumia hospitali. Alvin alikunywa divai nyekundu kwa machungu.
Hans alisimama nyuma yake kimya. “Bwana Kimaro, kwa nini hukumwambia Bi Jones kuhusu picha hizo?”
“Kuna faida gani kumwambia? Je, angeniamini? Kelvin Mushi ndiye mwokozi wake sasa. Atafikiri kwamba ninamsingizia kwa makusudi kwa sababu simpendi,” Alvin alidhihaki.
Hans alikuwa kimya. Ilibidi akubali kwamba Kelvin Mushi alikuwa amedhamiria sana. Ili kumlinda Lisa, hata alitoa sadaka maisha yake. Ikiwa hata yeye angelikuwa mwanamke, angeliguswa pia.
Usiku sana, Lisa alioga na kukaa kitandani huku akiwa ameduwaa. Mwishowe, alichukua simu yake na kutuma ujumbe kwa Pamela, akimwomba aende hospitali kumuona Kelvin kwa niaba yake.
Pamela : [[emoji2297]Usiniambie! Kelvin Mushi alipoteza figo kwa ajili yako? [emoji24][emoji22]Nini unadhani; unafikiria nini? Usichanganyikiwe tu, sawa?]
Lisa: [[emoji26]Sikuwahi kufikiria kwamba angefanya hivyo. Nina deni kubwa kwake. Sitaweza kumlipa maisha yangu yote.]
Pamela : [[emoji22]Hapana, usifikirie sana juu yake. Chukulia tu ni ajali ya kawaida. Ninapanga kumleta Patrick nyumbani kwa Krismasi. Kisha nitaandamana naye hadi kwa familia ya Jackson katika Mkesha wa Mwaka Mpya.]
Lisa: [[emoji39]Nyinyi watu mmesuluhisha matatizo yenu?]
Pamela : [Nilimchunia kwa nusu mwezi, na aliniahidi kukutana na Linda haraka iwezekanavyo katika siku zijazo. Nitamtambulisha mpenzi kwa Linda pia. Nataka kumpa Patrick nafasi moja zaidi. Ninampenda kupita kiasi.[emoji849][emoji849][emoji849]]
Lisa: [[emoji122][emoji122]Hongera kwa kumpata tena Bwana wako.]
Alipotuma tu ujumbe huo, mlango wa chumba cha kulala ulifunguliwa. Mkono wake ulitetemeka, na akazima skrini bila fahamu kabla ya kuweka simu chini.
“Unachat na nani?” Alvin alitoa harufu ya mvinyo mwekundu, na uso wake wote uliwaka kwa hasira. “Nionyeshe simu yako.”
Lisa hakuamini. Alvin hakuwahi kuangalia simu yake hapo awali, lakini alikataa kumpa kabisa. "Alvin, usiende mbali sana."
"Mbali sana? Nitajuaje kama unawasiliana na Ethan Lowe au Kelvin Mushi nyuma yangu?” Alvin hakuwahi kuwapenda wanaume ambao walisisitiza kuangalia simu za wanamke wao, lakini alipoona tabasamu kwenye midomo ya Lisa mapema, moyo wake ulikosa raha ghafla. Alipaswa kuwa na uhakika Lisa alikuwa anachat na nani!
Lisa hakuwahi kufikiria kwamba uaminifu kati yao ulikuwa umeshuka sana. Hata hivyo, huenda asingemuelewa tena ikiwa angeona yaliyomo kwenye simu yake, kwa hiyo alisema tu waziwazi, “Nilikuwa niachat na Pamela . Alikuwa akizungumza kuhusu mpenzi wake. Pia… ataenda hospitali kumwona Kelvin. Siwezi kwenda mwenyewe, lakini marafiki zangu wanaweza kwenda kwa niaba yangu.” Alitazama kinyonge jinsi sura nzuri ya Alvin ikibadilika na kuwa mbaya kwa hasira iliyoonekana waziwazi kwa macho. Moyo wake ulihisi kuchoka ghafla.
“Lisa Jones, wewe ndiye uliyekuwa unachat na Kelvin Mushi? Ni kitanda changu unacholala sasa ujue.” Alvin alichukua simu yake na kuivunjavunja ukutani. Kelele kubwa ilimfanya Lisa kuziba masikio yake kwa hofu.
Alvin aliinua mikono yake na kumkandamiza kitandani, akimbusu kwa nguvu kwenye mdomo. "Niambie, busu langu linakupendeza zaidi, au busu la Kelvin Mushi ndilo tamu zaidi?" Akambusu kana kwamba ana wazimu. Lisa alikuwa akiumia tu kutokana na busu hilo na kumsukumia mbali, lakini hakuweza kumzuia hata kidogo.
Alvin alikuwa amekunywa nusu chupa ya divai nyekundu katika chumba chake cha maktaba. Ubabe wake ulionekana kuongezeka mara moja. Alipokumbuka busu lake na Kelvin, macho yake yakawa mekundu huku akimbusu zaidi.
"Alvin unaniumiza bwana." Lisa alikwepa kwa maumivu.
“Kwanini unakwepa busu langu? Unatamani ningekuwa Kelvin badala yake?” Alvin alikuwa tayari amezidiwa na moto wa wivu. Akararua nguo yake ya kulalia kwa nguvu. "Au aliufanya usiku huo kuwa usiosahaulika sana, ndio maana umeenda naye kituo cha polisi leo? Huwezi kumwacha kabisa?”
Lisa aliogopa sana. Haraka haraka akamshika mkono na kutikisa kichwa bila msaada. “Hapana, nimechoka. Ninaogopa leo sitaki…”
“Hutaki kwa sababu ni mimi, sivyo?” Alvin alicheka ghafla. “Akili yako imejaa Kelvin Mushi sasa. Ungekuwa tayari kama angekuwa yeye, si ndiyo?"
“Mbona unaendelea mbali sana Alvin, hutaki kunielewa kwanini?” Lisa alijisikia kuchoka sana na kukata tamaa. Alikaribia kufa siku hiyo, lakini hakumjali hata kidogo. Alijua tu jinsi ya kumtilia shaka.
Alitabasamu kwa huzuni na hakuhangaika tena, akamwacha afanye anavyotaka. “Sawa, fanya tu kama unataka. Fanya chochote unachotaka.” Machozi yake yalimtoka kwenye pembe za macho yake na kutiririka kwenye nywele zake. Macho yake yalikuwa hafifu.
Siku zote alikuwa akitiliwa shaka, kukanyagwa, na kudhalilishwa naye, lakini bado alikuwa binadamu.
Mwili wa Alvin ukakakamaa kana kwamba alipigwa ghafla kichwani.
Kwanini amekuwa hivi? Ilikuwa ni kama amekuwa pepo. Hakuweza kujizuia kwa mwanamke? Kweli alipoteza busara kwa sababu ya mwanamke? Aligeuka na kukimbilia bafuni. Maji baridi yakamwagika juu ya mwili wake, na ghafla akajichukia. Alipotoka kuoga, Lisa alikuwa amelala chali pembeni ya kitanda, mtupu kabisa hana chochote baada ya nguo zake kularuliwa na Alvin. Kama kware mdogo, alijikunyata, hana msaada wowote, tayari kukwakupaliwa na mwenye mwenye njaa kali!
Alvin hakufanya chochote tena, alilala upande wa pili wa kitanda kimya! Wawili hao walitenganishwa kwa umbali, lakini hakuna aliyemkaribia mwenzake. Hakujua kuwa Lisa ambaye alikuwa amemrudisha nyuma kimawazo machozi yalikuwa yakimtoka. Hakupata usingizi mpaka ilipofika usiku sana.
Kulipopambazuka, Alvin aliamka, lakini Lisa hakuwapo tena kitandani. Haraka akainuka na kushuka chini. Lisa alikuwa amekaa kwenye meza ya chakula akinywa uji wake wa ulezi. Macho ya Alvin yalilegea kidogo, na akashuka haraka. Aliketi kando yake na kuuliza kwa ukali, "Kiamsha kinywa changu kiko wapi?"
Sura ya 140
“Bwana Kimaro, kifungua kinywa chako kimefika.” Shangazi Linda alitoka na kifungua kinywa alichotengeneza.
Alvin akakitazama, na uso wake ukachukizwa mara moja. "Lisa Jones, kwanini hukuniandalia kiamsha kinywa?"
"Wewe ndio ulisema chakula changu ni kichafu kama mimi." Lisa alimtazama kwa utulivu. Siku zote alikuwa hivi. Alipomuelewa vibaya, alimdhalilisha kwa kumwambia chakula chake ni kichafu na asimpikie tena, lakini sasa alitaka apike tena. Je, hakuchoka kumnyanyasa?
"Nitengenezee sasa hivi." Uso wa Alvin ulikuwa mbaya kwa hasira.
"Hapana. Mimi siyo yaya wako.” Lisa alisimama baada ya kumaliza uji wake. "Naenda kazini."
Alvin aligeuka na kuongea na Shani aliyekuwa amesimama mlangoni. “Mfuate kwa karibu. Akithubutu kwenda hospitali, mpige na umrudishe hapa.”
"Mimi sio mtumwa wako." Macho ya Lisa yalikua mekundu kwa hasira. Tayari alikuwa ameamua kutokwenda hospitali, lakini bado alisisitiza kumlazimisha kumwekea mlinzi wa kumchunga. "Alvin Kimaro, usiende mbali sana."
“Kwa kuwa ulinichanganya, unapaswa kuwa tayari kuwa mtumwa wangu. Hakuna anayeweza kwenda kinyume na mimi.” Alvin hakujieleza sana, lakini maneno yake yalitosha kudhihirisha hasira zake.
Lisa alichukua mkoba wake na kuondoka huku Shani akimfuata.
Njiani kuelekea ofisini kwake, haijalishi Lisa aliendesha gari kwa haraka vipi, Shani alikuwa makini naye muda wote. Kwenye maegesho, Lisa alishuka kwenye gari na Shani akamfuata kwa nyuma kwa kasi.
“Shani, unaweza kuacha kunifuata? Sitaenda hospitalini.” Lisa alitmwambia Shani kwa upole. Kwa kweli, hakuwa na shida yoyote na mlinzi yule.
"Samahani, hili ni agizo la Bwana Kimaro, bosi wangu."
“Agizo ni la Alvin, lakini usalama ni wa kwangu. Najua namna ya kujilinda mwenyewe!” Lisa mwishowe alikasirika. “ Sawa, Alvin alikuajiri? Anakulipa kiasi gani? Mimi nitakupa mara mbili." Lisa akatoa kadi kwenye begi lake.
Shani hakujali. “Bi Jones, haijalishi unanipa kiasi gani. Nilifunzwa na familia ya Kimaro. Ninafanya kazi kwa ajili yao tu.” Lisa alipigwa na butwaa. Je, familia ya Kimaro ilikuwa na watu wengi kama Shani? Familia ya Kimaro ilionekana kuwa na mambo mengi zaidi kuliko vile alivyofikiria. “Kwa hiyo lazima umekuwa na Alvin kwa muda mrefu. Kwa maana hiyo unamjua mtu anayeitwa Sarah?”
Hali ya wasiwasi ikaangaza kwenye macho tulivu ya Shani. Ingawa lilitoweka hapo hapo, Lisa bado aliliona vizuri. “Nilimsikia Alvin akimzungumzia siku moja akiwa amelewa. Lazima awe mpenzi wake wa zamani. Walikuwa wanapendana sana?"
“Bi Jones, hayo yote ni ya zamani. Bwana Kimaro ana wewe tu moyoni mwake sasa,” Shani alisema haraka.
"Ndio hivyo?" Lisa alitabasamu kwa kujidharau. Alikuwa akimpima tu Shani, lakini jibu la Shani lilimhakikishia kwamba kweli Alvin alikuwa na mpenzi wa zamani anayeitwa Sarah. Alimwita jina lake wakati alikuwa amelewa. Je, iliwezekanaje kuwa Lisa ndiye pekee moyoni mwake sasa?
“Shani, asante kwa kuniambia hivi.” Aligeuka na kwenda juu ofisini.
Shani alimfuata kinyonge.
•••
Siku iliyofuata, saa kumi na nusu jioni, Pamela alitoka hospitali baada ya kumtembelea Kelvin, akihisi huruma moyoni mwake.
Kama asingekuwa amekosea na kumchanganya Alvin na Kelvin hapo mwanzo, huenda Lisa na Kelvin wangekuwa tayari wameoana. Hapo Kelvin asingepoteza figo pia. Hata hivyo, haikufaa kujutia juu ya maziwa yaliyokwishamwagika sasa.
Akatoa simu yake na kumpigia Patrick. “Patrick, unakwenda kuwachukua wazazi wangu, au unaenda moja kwa moja kwenye Mgahawa tuliokubaliana kukutana?”
“Niko na mkutano ofisini ambao unaweza kuendelea hadi saa kumi na moja na nusu. Nitaenda huko moja kwa moja baadaye. Nisaidie kuomba radhi kwa wazazi wako kwa ajili yangu,” Patrick alisema kwa sauti ya upole.
“Ni sawa, lakini usichelewe. Baba yangu anachukia watu ambao hawatimizi ahadi zao.” Pamela alimuonya kwa upole.
“Usijali, ni suala la maisha yangu. Hakika sitachelewa. Tayari nimekuandalia zawadi ambayo wazazi wako watapenda. Tutafunga ndoa mapema, nami nitakuwa mumeo.” Patrick akatabasamu kwa dhati. Moyo wa Pamela ulikuwa mtamu alipokuwa akimsikiliza.
Baada ya kukata simu, Pamela aliendesha gari kuwachukua wazazi wake kisha akaenda Mambo Garden Restaurant. Ilikuwa saakumi na moja kamili jioni alipofika. Baada ya kuagiza chakula, kaka yake Forrest alifika. Saa kumi na mbili jioni bado Patrick alikuwa hajafika. Babake Pamela alikosa subira, akasema, “Kwa nini bado hajafika? Si sawa kutufanya wazee tungojee.”
Pamela alisema, “Baba, ni saa za jioni sasa. Pengine kuna msongamano mkubwa wa magari barabarani.”
Mama yake aliitikia kwa kichwa na kukubali. “Wafanyabiashara wana mambo mengi ya kushughulikiwa mwishoni mwa mwaka, hiyo inaeleweka. Kuwa na subira zaidi.”
Pamela alimpigia simu Patrick, lakini hakupokea, akajifariji. "Lazima asipokee kwa sababu yuko barabarani, atakuwa karibu tu hapa."
Baada ya nusu saa nyingine, Patrick hakutokea tu. Baba yake alikasirika. “Ni mara yake ya kwanza kukutana nasi lakini anatuletea dharau namna hii. Hata ukimpigia simu ni bure. Sidhani kama yeye ni mkweli hata kidogo. Sitakubali kukuruhusu uolewe naye.”
Wakati huu, mama yake hakusema chochote, na Forrest pia alikuwa na uso wa kukata tamaa. “Achana naye. Sio kama hakuna wanaume wengine ulimwenguni."
Pamela alihudhunika. Mbele ya shutuma za familia yake, alijilazimisha kutotoa machozi. Yeye tu alijisikia kukata tamaa sana kwa aibu. Zamani, alimuahidi mara nyingi, lakini sasa, hata alikosa mkutano wa kwanza pamoja na wazazi wake. Je, alimpenda kweli?
Mama yake akasema. “Pamela, jambo la muhimu zaidi katika maisha ya mwanamke ni kupata mwanaume ambaye ni mzuri kwako kwa moyo wote. Bado wewe ni mdogo, kwa hivyo usikimbilie kuolewa. Sasa, tule. Chakula kinakuwa baridi.” Wakati wote wa chakula, ilikuwa kama anatafuna nta. Mpaka mwisho, Patrick hakutokea, wala hakupiga simu hata mara moja kuelezea shida ni nini.
Baada ya kuachana na familia yake, Pamela aliendesha gari hadi ofisini kwa Patrick. Ofisi yake ilikuwa tayari imefungwa. Alianza kuhisi wasiwasi kidogo. Alikuwa na wasiwasi kwamba huenda Patrick alikuwa amepata ajali ya gari au kitu kibaya. Hata hivyo, hakujua namba za wazazi wa Patrick. Baada ya kusita kwa muda, alimpigia simu Linda. Hakutarajia kuwa mtu aliyemjibu angekuwa ni mwanamume ambaye sauti yake aliifahamu vizuri. “Habari, Pamela…”
Pamela alitazama sura yake iliyokuwa na ukungu kwenye dirisha la kioo mbele yake na ghafla akacheka peke yake. Je, alionekana kama mjinga? “Kwa nini hukupokea nilipokupigia simu? Na mbona unapokea simu ya Linda?”
“Pamela, samahani. Linda alipata ajali ya gari jioni. Niko hospitalini sasa. Nilisahau kabisa hata kuchukua simu yangu ofisini,” Patrick alisema kwa hatia, “Oh, nimechelewa sana? Mmemaliza kula? Tafadhali mwambie baba na mama smahani kwa kushindwa kuja.
Nitawaalika kwenye chakula cha jioni wakati mwingine.”
"Hakuna haja tena," Pamela alisema kwa sauti isiyo na maana.
"Pamela, ilikuwa ni dharura wakati huu ..."
“Ndiyo, kila kitu kuhusu Linda ni dharura. Kwani amekufa? Kilema? Kwani hana wazazi tena, ana wewe tu?"
Moyo wa Patrick ukasisimka. "Pamela, unawezaje kusema maneno kama haya? Kwani Linda alitaka kupata ajali? Hata kama humpendi, unapaswa angalau umuonee huruma.”
Pamela alidhihaki. “Sawa, nimekuuliza swali. Kwani amekufa? Amepooza? Mlemavu?”
TUKUTANE KURASA 141-145
Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app